29/05/2026
KUTOKA KUSHIKANA MASHATI SLIPWAY HADI AFRIKA KUSINI: HIVI NDIVYO ADAM MCHOMVU NA FID Q WALIVYOKUTANA KWA MARA YA KWANZA! 🥊🎙️
Kazi ya utangazaji wa burudani (U-Presenter) ina faida zake, lakini ina “risks” zake pia, hasa unapogusa heshima ya ma-Legend wa Hip Hop! Adam Mchomvu amefunguka stori ya kusisimua kupitia kwenye kuhusu siku aliyoshtukizwa na ngumi ya Fid Q kwa sababu ya dongo la redioni. 🤫💥
Enzi hizo kipindi cha mchana cha Clouds FM kikijulikana k**a Dr. Beat (kabla ya kuwa XXL), msanii Rado alitoa ngoma yake ya “Diss” ya ‘Usiulize’ na kumchana Fid Q. Adam Mchomvu, kwa “vibe” la utangazaji, akatoa comment redioni: “Sasa hivi Fid Q inabidi ajipange, amekuja mkali mwingine kutoka Mwanza anaitwa Rado!” 🤯📻
Siku hiyo Adam akaenda zake kujirusha viwanja vya Slipway. Akakutana na “Heavyweights” wa game: P-Funk Majani, Gardner G Habash, Lady Jaydee, na Fid Q. Fid hakupoteza muda, akamuanzia noma Adam hapo hapo kisa kauli yake ya kumpandisha Rado. Purukushani ikawa kubwa hadi wakashikana mashati! 🥶🥊
Kesho yake, Adam alienda “kush*taki” kwa mkurugenzi Ruge Mutahaba. Chini ya usimamizi wa Ruge, Fid Q na P-Funk walikuja ofisini, wakaomba msamaha, yakaisha na urafiki ukaanza. 🤝✨
Urafiki huo ukawa mkubwa kiasi kwamba Fid Q alipopata shoo ya kihistoria ya kutumbuiza kwenye Big Brother Africa, alimchagua mtu aliyeshikana naye mashati Adam Mchomvu kwenda naye Afrika Kusini kumpigia backing vocals jukwaani! 🇿🇦🎤
Hii inathibitisha kuwa “Real Hip Hop Culture” ya zamani ilikuwa na hisia za ukweli, lakini mwisho wa siku “Maturity” ilishinda. Unadhani watangazaji wa sasa wana ujasiri wa kutoa maoni makali redioni k**a alivyofanya Adam kwa Fid Q bila kuogopa kuharibu uhusiano wao? 👇🏾🍿
insideoutz