Hamari Media TZ

Hamari Media TZ Nice

🚨_|| AMEANDIKA FARHAN JRMimi siwezi kujadili HISIA bali HOJA, najadili KITU na sio MTU, we attack MATTER not the SUBJECT...
11/11/2025

🚨_|| AMEANDIKA FARHAN JR

Mimi siwezi kujadili HISIA bali HOJA, najadili KITU na sio MTU, we attack MATTER not the SUBJECT na uhalisia ni kwamba nitakuwa Mjinga kukasirishwa na Watu ambao wamewahi kunipost sana kunisifia hivyo wana haki zao pia Kikatiba kunipost wakichukia ila Mimi nasimamia misingi ya kazi yangu ama taaluma yangu, nimewachukulia k**a Watoto ambao Kibiblia hawapaswi kunyimwa mapigo japo wanapambana kupingana na maandiko.

Nitakapoona hapa Young Africans ni haki yao na nikapima nikaona ni haki basi bila kujali ni dhidi ya nani Mimi nitasimama nao na nionapo hapa sio haki siwezi kusimama nao, nikiona hapa Yanga wanastahili sifa zao nitawapa bila haya na nitakapoona hapa wanastahili kukosolewa basi nitawakosoa vikali bila kujali nani kapenda ama hajapenda, mifano ya Vita zao nzito ambazo mikono yangu iliandika bila hofu ipo na Mimi ni yule yule ambaye kwasasa nawaandika wao bila hofu yoyote ile.

Ushauri tu kidogo japo sio lazima hiyo Klabu ni kubwa saana tangu 1935 ina miaka 90 wakati Mkulima nimezaliwa 1997 na nina miaka 28 tu, Kalamu yangu haitishi k**a mnavyojaribu kupambana nayo, hakuna Mkubwa zaidi ya timu yenu hivyo tambueni thamani ya Logo yenu maana Kalamu ya Mwandishi haiwapi Yanga alama tatu, haiwakoseshi alama tatu wala haifanyi icheze vibaya, kuiweka Yanga, ninyi na Mkulima sehemu moja ni kuitukana taasisi hiyo Kongwe ipeni heshima yake, its Young Africans sio Kosovo ya Ifakara.

Kuna mengine siwezi kujadili kwasababu sio Utamaduni wangu, Mimi ni MNGINDO nimeingia Jandoni na nimetairiwa kwa Kisu cha Madafu bila uwepo wa Nesi wala sindano za Ganzi, mengine nayaweka kifuani na kuacha Uanaume ufanye kazi, hayo siyapi nafasi naona kwasasa zinajadiliwa zaidi HISIA kuliko UHALISIA, ukiona Watu wanataka tu kusifiwa basi kuna kitu hakipo sawa sehemu, naisubiri ikirejea International break k**a itakuwa vile vile basi hatutoacha.

Naona napostiwa postiwa sana nimeweka na picha nyingine hapo slide namba mbili inafaa kuitumia kwenye Makala zenu, unaweza kuzoom ukipenda.

🚨_|| AMEANDIKA PRIVALDINHOHuna sababu za kupanic kijana. Huko kwenye kutahiriwa tutajadili wakati mwingine, kwa sasa wac...
11/11/2025

🚨_|| AMEANDIKA PRIVALDINHO

Huna sababu za kupanic kijana. Huko kwenye kutahiriwa tutajadili wakati mwingine, kwa sasa wacha tukupige msasa wa kitaaluma.

Hoja ya msingi ni kwamba umefanya kosa la kitaaluma. Kitendo cha mwandishi wa habari kujitanabaisha upande uliopo bila sababu za msingi basi unakosa weledi wa kuwa neutral.

Kesi ya mbuzi huwezi kumpelekea fisi.

Naongelea taaluma yako ya uandishi wa habari. Mwandishi wa habari kuchagua upande ni kosa kubwa la kimkakati ambalo linakunyima uhalali wa kufanya kazi yako kwa weledi na kuaminika.

Unawapa watu wakati mgumu wa kutambua kuwa ni wakati gani unaongea kishabiki na wakati gani unaongea k**a mwandishi. Tunashindwa kujua kuwa upo kwenye majukumu ya KPI za kuwapigania makolo au majukumu ya kazi ya uandishi

Umesema tumewahi kukusifia, ndio. Kusifiwa jana haimaanishi leo ukipotosha tukae kimya. Unapigwa tu. Unasema unaisifia Yanga? Sawa kwani nani kakutuma? Je kuisifia Yanga ina maanisha ukipotosha wakae kimya? Kwani sifa ni sadaka?

Kubali kwanza umepotoka kimaadili kujiweka wazi kuwa shabiki. Kaka yetu Dauda ambaye ametulea hakuwahi kutufundisha kuweka wazi hisia zetu.

Taalum ya uandishi wa habari sio kazi ya kuonesha hisia zako ni wajibu unafanya kazi kwa uhalisia wake.

Achana na haya mambo ya kutahiriwa kiimeili, wacha tukutahiri kitaalum kwanza.

FUNGUA COMMENT ALICHO ANDIKA FARHAN JR

TANZIA
11/11/2025

TANZIA


11/11/2025

Kipaji cha Morice Abraham kinazidi kuwafurahisha wana Msimbazi.

UPDATESKutokana kuwa free agent mpaka kurejea timu ya taifa ya Guinea sio ishu ndogo kabisa, Simba Sc imefanya Naby Cama...
11/11/2025

UPDATES

Kutokana kuwa free agent mpaka kurejea timu ya taifa ya Guinea sio ishu ndogo kabisa, Simba Sc imefanya Naby Camara kurejesha makali yake, alichokifanya Naby Camara ni kucheza vizuri kila alipopewa nafasi na performance nzuri ndio imefanya aitwe timu ya taifa.

Kuna namna wachezaji wengi wakija Tanzania hususani kwenye timu hizi mbili kubwa Simba Sc na Yanga Sc hufanya kuonekana wapya kwasababu ya kiwango wanachoonyesha.

Tumeona kwa kiasi kikubwa ligi ya Tanzania inavyozidi kutoa fursa kwa wachezaji wengi wa kigeni kuitwa kwenye mataifa yao.

Uzuri mwingine kutoka kwa Naby Camara ni mchezaji kiraka hivyo Kocha anaweza kumtumia kwenye eneo zaidi ya moja.

11/11/2025

Bodi ya ligi kuu Tanzania NBC yatoa Tathmini yake

11/11/2025

mwaka huu tutapiga wote

hii simba unakumbuka ilikua mwaka gani
11/11/2025

hii simba unakumbuka ilikua mwaka gani

11/11/2025
11/11/2025

Kocha wa mpya wa yanga hana utofauti na Romain Folz

11/11/2025

Miguel Ángel Gamondi ni kocha mpya tuliemzoea

11/11/2025

Hakuna timu itakayoishinda Simba msimu huu

Address

Bagamoyo
Dar Es Salaam
BAGAMOYO

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hamari Media TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share