11/04/2026
Kwa muda mrefu mashabiki walitamani kuona Usher na Chris Brown wakichuana kwenye jukwaa la Verzuz, lakini sasa wamekuja na mshangao mwingine mkubwa—ziara ya pamoja ya muziki.
Kupitia kurasa zao za Instagram, mastaa hao wawili walitangaza rasmi ziara hiyo mpya iitwayo “Raymond & Brown Tour”, wakisindikiza na ujumbe mfupi uliosomeka “ITS TIME! &Brown”. Tangazo hilo liliambatana na video inayowaonyesha wakiendesha pikipiki usiku huku wakifuatwa na mashabiki waliokuwa na shangwe kubwa.
Ziara hiyo inatarajiwa kuwa moja ya matukio makubwa ya R&B, ikiwakutanisha wakali wa vizazi tofauti—Usher wa miaka ya 2000 na Chris Brown wa miaka ya 2010. Hata hivyo, ratiba kamili na maeneo ya ziara hiyo bado hayajawekwa wazi.
Tangazo hili pia limekuja muda mfupi baada ya Chris Brown kuachia wimbo wake mpya “Obvious”, kutoka kwenye albamu yake inayotarajiwa kutolewa Mei 8.