Wasafi FM

Wasafi FM The leading radio station in Tanzania specializing in the latest music & entertainment news.
(2)

29/10/2025

UCHAGUZI PWANI WAANZA KWA AMANI; VIONGOZI WAHIMIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI

Zoezi la upigaji kura mkoani Pwani limeanza mapema leo saa moja asubuhi k**a ilivyopangwa, likiendelea kwa utulivu na amani katika vituo mbalimbali vya kupigia kura.

Wakati wa ziara ya asubuhi hii, WASAFI MEDIA imetembelea baadhi ya vituo na kushuhudia hali ya upigaji kura ikiwa shwari, huku wananchi wakijitokeza kutimiza haki yao ya kikatiba.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani SALIM Morcase amethibitisha kuwa hali ya usalama iko vizuri, na doria zinaendelea katika mitaa yote kuhakikisha wananchi wote wanashiriki katika mchakato huu bila wasiwasi wowote.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ameongoza wananchi mapema leo katika zoezi hilo na kuwataka wote kujitokeza kwa wingi kupiga kura, akisisitiza umuhimu wa kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa amani na utulivu.

denongara
Digital

29/10/2025

WAGOMBEA CHAUMA NA CCM UYOLE KULINDIANA KURA.

Wagombea ubunge wa ubunge jimbo la Uyole, Bwana Ipyana Samson Njiku kupitia Chama cha Ukombozi waumma (CHAUMMA) na Dkt Tulia Ackson kupitia chama cha mapinduzi (CCM) wamekutaka kwenye kituo cha kupigia kura Itezi Magharibi na kuomba kulindiana kura kwenye vituo wanavyotembelea.

Cc

29/10/2025

CHAMWINO NI SALAMA,WATU WANAPIGA KURA-DC CHAMWINO

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Janeth Mayanja amesema kuwa Hali ya usalama imeimarika katika vituo 961 vya kupiga kura ambavyo vinapatika katika vijiji 107 vilivyomo Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma

Mhe. Mayanja ameyasema hayo Leo Oct 29,2025 katika kituo Cha kupiga kura Cha Ofisi ya Kijiji chamwino Ikulu Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma

Mhe. Mayanja amesema kuwa katika kila kituo Kuna muamko wa Watu kujitokeza kupiga kura

Cc:

29/10/2025

HUKI NDICHO KITUO ATAKACHOPIGIA KURA DKT. SAMIA

Muda huu katika kituo Cha kupiga kura Cha ofisi ya Kijiji chamwino Ikulu Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma Leo Oct 29,2025 watu wanaendelea na mchakato wa kupiga kura ya kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani

Katika kituo hiki Cha Ofisi ya Kijiji chamwino Ikulu ndipo Mgombea wa kiti Cha Urais Kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)Dkt. Samia Suluhu Hassan atapiga kura

Cc:

29/10/2025

HAKUNA TUKIO LOLOTE LA UVUNJIFU WA AMANI MBEYA - SACP KUZAGA.

Kamanda wapolisi mkoa wa Mbeya Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Benjamini Kuzaga amesema hadi sasa mkoa wa Mbeya hali ni shwari na hakuna tukio lolote la uvunjifu wa amani lililo ripotiwa kwenye mkoa wa Mbeya.

SACP Kuzaga amesema hali hiyo ni ishara kwamba huu ni ustaarabu wa hali ya juu kwa wananchi wa mkoani humo na kwamba waendeleze ustaarabu huo ili kuhakikisha mkoa wa mbeya unaendelea kua salama wakati huu wa kupiga kura na wakati wa kutoa matokeo.

Cc

29/10/2025

DKT. NDUMBARO APIGA KURA, APONGEZA UTULIVU NA UHAMASISHAJI WA WANANCHI SONGEA

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, ameambatana na familia yake kupiga kura katika kituo namba moja cha Mjimwema A, eneo ambalo amekuwa akipigia kura kwa miaka mingi.

Akizungumza mara baada ya kupiga kura, Dkt. Ndumbaro amesema amefika kutimiza haki yake ya kikatiba ya kuwachagua viongozi, na amepongeza muitikio mzuri wa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo muhimu la kidemokrasia.

Ameeleza kuwa katika eneo la Mjimwema A kuna jumla ya vituo tisa vya kupigia kura na wananchi wamejitokeza kwa wingi, huku mchakato ukiendelea kwa amani na utulivu.

Dkt. Ndumbaro ameongeza kuwa mji wa Songea una jumla ya vituo 500 vya kupigia kura, na baada ya kupiga kura wananchi wanaendelea na shughuli zao za kila siku za kujiletea maendeleo katika hali ya usalama na utulivu.

Aidha, Dkt. Ndumbaro amewahimiza wananchi ambao bado hawajapiga kura kujitokeza kutimiza wajibu wao wa kikatiba, huku akiwataka waliomaliza kupiga kura kuendelea na shughuli zao kwa amani.

Kwa upande wake, Zakaria Ngonyani, mkazi wa Mtaa wa Mjimwema A, amesema ameridhishwa na maandalizi na mwenendo mzima wa zoezi la upigaji kura, na amepongeza hatua ya kuongeza vituo vingi vya kupigia kura, jambo lililorahisisha ushiriki wa wananchi wengi zaidi.

29/10/2025

RAIS MWINYI ALIVYOPANGA FOLENI NA KUPIGA KURA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye pia ni mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), leo amejitokeza kupiga kura katika Kituo cha Kariakoo kilichopo Jimbo la Kwahani, Unguja.

Akiwasili kituoni hapo saa za asubuhi, Dkt. Mwinyi alipanga foleni pamoja na wananchi wengine na kutimiza haki yake ya msingi ya kikatiba kwa utulivu na nidhamu.

Akizungumza mara baada ya kupiga kura, Dkt. Mwinyi amesema kuwa ameridhishwa na namna zoezi la upigaji kura linavyotekelezwa na Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar (ZEC), akibainisha kuwa maandalizi yamekuwa mazuri na taratibu zimezingatiwa ipasavyo.

Amesema kuwa hadi sasa uchaguzi unaendelea katika mazingira ya amani, usalama na utulivu huku wananchi wakiendelea kujitokeza kwa wingi katika vituo mbalimbali.

"Zoezi linaenda vizuri, nimefurahishwa kuona wananchi wengi wamejitokeza mapema. Hii inaonyesha uwazi wa demokrasia na mwamko wa wananchi kushiriki katika maamuzi ya nchi yao," alisema Dkt. Mwinyi.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi wote wa Zanzibar ambao hawajapiga kura kuhakikisha wanajitokeza katika muda uliopangwa ili kutumia haki yao ya kidemokrasia bila hofu wala kushawishiwa na kauli za kuchochea uvunjifu wa amani.

"Tuendelee kulinda amani tuliyonayo. Uchaguzi ni tukio la siku moja, lakini Zanzibar ni yetu daima. Tushiriki kwa utulivu, tukubali matokeo halali na tuweke mbele maslahi ya taifa," amesisitiza.

cc:

29/10/2025

ZOEZI UPIGAJI KURA BABATI, HALI NI SHWARI – DC KAGANDA

Mkuu wa Wilaya ya Babati, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, ameongoza wananchi wa Wilaya hiyo katika zoezi la kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaofanyika leo, ambapo mapema asubuhi alitimiza haki yake ya msingi kwa kupiga kura katika kituo chake cha kupigia kura.

Akizungumza baada ya kupiga kura, Mhe. Kaganda ameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa maandalizi mazuri na kuweka vituo vya kutosha pamoja na vyumba vingi vya kupigia kura katika maeneo mbalimbali.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kuwa hali ya ulinzi na usalama katika Wilaya ya Babati ni shwari, huku wananchi wakiendelea kujitokeza kwa wingi na kwa amani kutekeleza haki yao ya kikatiba. Ameongeza kuwa vyombo vya usalama vimeimarishwa kuhakikisha zoezi hilo linaendelea kwa utulivu hadi mwisho.

29/10/2025

HALI NI SHWALI TUJITOKEZE KUPIGA KURA - DKT TULIA.

Spika wa Bunge la Tanzania na Mgombea Ubunge Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Mapinduzi Dkt.Tulia Ackson amejitokeza kupiga kura kwenye kituocha cha Shule ya Msingi Tambukareli Kata ya Itezi jijini Mbeya ikiwa ni sehemu aliyojiandikisha ili kutumia haki yake ya kikatiba.

Baada ya kupiga kura Dkt. Tulia amesema muitikik umekua mkubwa kwa wananchi kujitokeza kupiga kuda huku akitoawito kwa wananchi wa jimbo la Uyole na watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua Viongozi wanaowataka kwakua hali ni shwali jimboni humo.

Cc

29/10/2025

Zoezi la kupiga kura linaendelea kwa utulivu katika kituo cha Buyuni, kilichopo Changanyikeni, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, likianza mapema saa 1.00 asubuhi. Wananchi wameendelea kujitokeza kwa utaratibu kutekeleza haki yao ya kikatiba katika mazingira ya amani na usalama.

Maafisa wa tume ya uchaguzi wanaendelea kusimamia mchakato huo kwa weledi, wakitoa huduma kwa wapiga kura kwa namna inayoonesha maandalizi mazuri ya uchaguzi huu.

Wananchi wametakiwa kuendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani, wakizingatia maelekezo yanayotolewa na wasimamizi wa vituo, ili zoezi hilo muhimu kwa demokrasia ya nchi liwe na mafanikio makubwa.

28/10/2025

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Ahmed Makarani, amesema maandalizi ya kiusalama kuelekea Uchaguzi Mkuu wa kesho yako vizuri na hakuna tishio lolote lililoripotiwa. Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Manyara, Kamanda Makarani ameeleza kwamba kwa maeneo yote yaliyowahi kuonesha viashiria vya vurugu, askari wameshapelekwa na wako tayari kukabiliana na tukio lolote litakalojitokeza.

Ameongeza kwamba wananchi wanapaswa kujitokeza kupiga kura bila wasiwasi, na mara watakapomaliza zoezi hilo waendelee na shughuli zao za kila siku ikiwemo biashara, kwa kuwa uchaguzi haupaswi kuwa kikwazo cha maendeleo yao.

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wasafi FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category