29/10/2025
UCHAGUZI PWANI WAANZA KWA AMANI; VIONGOZI WAHIMIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI
Zoezi la upigaji kura mkoani Pwani limeanza mapema leo saa moja asubuhi k**a ilivyopangwa, likiendelea kwa utulivu na amani katika vituo mbalimbali vya kupigia kura.
Wakati wa ziara ya asubuhi hii, WASAFI MEDIA imetembelea baadhi ya vituo na kushuhudia hali ya upigaji kura ikiwa shwari, huku wananchi wakijitokeza kutimiza haki yao ya kikatiba.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani SALIM Morcase amethibitisha kuwa hali ya usalama iko vizuri, na doria zinaendelea katika mitaa yote kuhakikisha wananchi wote wanashiriki katika mchakato huu bila wasiwasi wowote.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ameongoza wananchi mapema leo katika zoezi hilo na kuwataka wote kujitokeza kwa wingi kupiga kura, akisisitiza umuhimu wa kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa amani na utulivu.
denongara
Digital