Wasafi FM

Wasafi FM The leading radio station in Tanzania specializing in the latest music & entertainment news.
(1)

09/09/2025

Wananchi wa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, wamepokea habari njema kuhusu maendeleo ya miundombinu baada ya Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Abdallah Ulega, kutangaza kuwa serikali imeridhia rasmi upanuzi wa Barabara Kuu ya Kilwa Road kuwa ya njia nne.

Mradi huo mkubwa unatarajiwa kuanzia Kongowe, kupitia Vikindu, hadi kufika Mkuranga, na umeingizwa katika Bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa ajili ya utekelezaji.

Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Vikindu mnamo Septemba 9, Ulega ambaye pia ni Waziri wa Ujenzi, alisema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ameridhia ujenzi huo, na bajeti yake imepitishwa katika Bunge la Bajeti lililomalizika hivi karibuni.

Katika hotuba yake, Ulega aliwaomba wananchi waendelee kuiamini CCM na kumpa ridhaa ya kuwatumikia kwa awamu nyingine, akisisitiza kuwa dhamira yake ni kuhakikisha Mkuranga inasonga mbele kimaendeleo.

Aidha, Diwani wa Kata ya Vikindu, Mohammed Maundu, alieleza kuwa tayari shilingi milioni 40 zimetolewa kwa ajili ya kuboresha huduma za jamii, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya maji na jengo la wazazi katika Kituo cha Afya cha Vikindu.

WAFUGAJI WAENDELEA KUFURIKA MIKUTANO YA DKT. SAMIAKatika kumuunga mkono mgombea wa nafasi ya Rais kupitia Chama Cha Mapi...
08/09/2025

WAFUGAJI WAENDELEA KUFURIKA MIKUTANO YA DKT. SAMIA

Katika kumuunga mkono mgombea wa nafasi ya Rais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wafugaji wengi wameendelea kujitokeza katika mikutano ya kampeni ya chama hiko na kuonesha wazi namna wanavyomuunga mkono Dkt. Samia katika uchaguzi wa mwaka huu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Akizungumza leo mbele ya kundi hilo kubwa la Wafugaji lililojitokeza Katika Uwanja wa Samora Mkoani Iringa wakati Dkt. Samia akihitimisha Kampeni zake mkoani Iringa mapema leo, Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Taifa, Ndg. Mathayo Daniel amesema kwamba k**a walivyoahidi wakiwa Morogoro, Dodoma na Mbeya Wafugaji wataendelea Kujitokeza kwa wingi Kumuunga mkono Dkt. Samia kwani aliyoyafanya katika kuboresha na kuimarisha sekta ya mifugo ni mengi na ya kihistoria.

05/09/2025

BANDARI YA DAR ES SALAAM YASHIKA KASI, YAANZA KUPOKEA MELI KUBWA KUTOKANA NA MABORESHO"

Malengo ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa kituo kikuu (hub) cha kuhudumia shehena ya mizigo inayokwenda nchi jirani, yameanza kuzaa matunda, baada ya bandari hiyo kuanza kupokea meli kubwa zenye urefu wa hadi mita 300.

Mafanikio haya yametokana na maboresho makubwa ya miundombinu yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia mradi wa maboresho wa Dar es Salaam Maritime Gateway Project (DMGP).

Kwa mara nyingine katika historia yake, Bandari ya Dar es Salaam imefanikiwa kuhudumia meli kubwa ya Mv. MYNY aina ya Post Panamax, yenye urefu wa mita 300, uwezo wa kubeba tani 75,201 ikiwa imebeba shehena ya makasha 6,840.

Akizungumza mara baada ya meli hiyo kufunga gatini, Mkurugenzi wa Marini na Shughuli za Kibandari, Kapteni Abdallah Y. Mwingamno, amesema hatua hiyo ni ushahidi wa uwezo mpya wa Bandari ya Dar es Salaam kuhudumia meli kubwa za kizazi cha sasa.

“Mafanikio haya ni matokeo ya maboresho makubwa ya miundombinu yaliyofanywa na Serikali kupitia TPA. Tunapenda kuwahakikishia wateja na wadau wetu kwamba sasa Bandari ya Dar es Salaam ina uwezo wa kuhudumia meli kubwa na za kisasa kwa ufanisi zaidi,” alisema Kapteni Mwingamno.

Ameeleza pia kuwa mbali na maboresho ya miundombinu, Serikali kupitia TPA imewekeza kwenye ununuzi wa mitambo ya kisasa ikiwemo Ship to Shore Gantry Cranes (STS), Rubber Tyred Gantry Cranes (RTG), Reach Stackers na Forklifts za kisasa, ambayo itapunguza muda wa meli kukaa bandarini kwa kuongeza kasi ya upakuaji na upakiaji mizigo.

Katika maboresho hayo, kupitia Mradi wa DMGP, Serikali imeimarisha gati namba 1–7 kwa kuongeza kina kutoka mita 8 hadi mita 14.5, sambamba na kuongeza eneo la kuhudumia mizigo. Aidha, eneo la kugeuzia meli (turning basin) limeongezwa kina hadi mita 15 ili kuruhusu meli kubwa zaidi kuhudumiwa kwa ufanisi.

Vilevile, lango la kuingilia meli limepanuliwa na kuongeza kina chake ili kuruhusu meli zenye upana mkubwa kuingia bila changamoto.

Mradi wa maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam (DMGP) unagharimu Shilingi trilioni 1.118, ambazo zinatokana na mkopo wa Benki ya Dunia, misaada ya wafadhili na mapato ya ndani ya TPA. Mradi huu umehusisha pia ujenzi wa gati maalumu la kuhudumia meli za magari (RoRo Berth), kuimarisha gati za 8–11 kwa kuongeza kina kutoka mita 12 hadi mita 14.5, kuboresha mtandao wa reli ndani ya bandari na usimikaji wa mfumo wa umeme bandarini.

Kwa maboresho haya, Bandari ya Dar es Salaam sasa imejiweka kwenye nafasi ya ushindani mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, na kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na usafirishaji mizigo.

02/09/2025

‘MTOTO WA ULEGA’ MWENYE KIPAJI APATA SHULE

Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega, ametimiza ahadi yake ya kumsomesha mtoto Ridhiwani Martin Asheri mwenye umri wa miaka 13 kutoka Kibaigwa, Dodoma, ambaye ana kipaji cha kipekee cha kujenga barabara na madaraja.

Ridhiwani amepokelewa rasmi katika Shule ya Trust St. Patrick Schools iliyoko jijini Arusha, ambapo ataanza masomo yake ili kuendeleza kipaji chake na kufikia ndoto zake za kuwa mhandisi mashuhuri siku za usoni.

Mzazi wa Ridhiwani amemshukuru kwa dhati Waziri Ulega kwa kutekeleza ahadi hiyo muhimu. "Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Abdallah Ulega kwa kutimiza yale aliyoyaahidi kwa mwanangu, alikuwa anaongea k**a utani lakini leo hii yametimia"

Hatua hii ya Waziri Ulega inatajwa k**a mfano bora wa kuunga mkono vipaji vya vijana wadogo nchini na kuhakikisha wanapewa fursa ya kuendeleza vipaji vyao kwa manufaa yao binafsi na taifa kwa ujumla.

Ridhiwani alikutana na Waziri Ulega kwa mara ya kwanza mwezi Julai 2025, ambapo Waziri Ulega alivutiwa na kipaji chake na kuahidi kumsaidia ambapo baada ya kufikishwa shule hapo kwaajili ya Masomo pia ametoa shukrani kwa Waziri Ulega na kumuahidi kusoma kwa Bidii.

02/09/2025

WAZIRI ULEGA ATEKELEZA AHADI YA KUMSOMESHA MTOTO RIDHIWANI
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega, ametimiza ahadi yake ya kumsomesha mtoto Ridhiwani Martin Asheri mwenye umri wa miaka 13 kutoka Kibaigwa, Dodoma, ambaye ana kipaji cha kipekee cha kujenga barabara na madaraja.

Ridhiwani amepokelewa rasmi katika Shule ya Trust St. Patrick Schools iliyoko jijini Arusha, ambapo ataanza masomo yake ili kuendeleza kipaji chake na kufikia ndoto zake za kuwa mhandisi mashuhuri siku za usoni.

Mzazi wa Ridhiwani amemshukuru kwa dhati Waziri Ulega kwa kutekeleza ahadi hiyo muhimu. "Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Abdallah Ulega kwa kutimiza yale aliyoyaahidi kwa mwanangu, alikuwa anaongea k**a utani lakini leo hii yametimia"

Hatua hii ya Waziri Ulega inatajwa k**a mfano bora wa kuunga mkono vipaji vya vijana wadogo nchini na kuhakikisha wanapewa fursa ya kuendeleza vipaji vyao kwa manufaa yao binafsi na taifa kwa ujumla.

Ridhiwani alikutana na Waziri Ulega kwa mara ya kwanza mwezi Julai 2025, ambapo Waziri Ulega alivutiwa na kipaji chake na kuahidi kumsaidia ambapo baada ya kufikishwa shule hapo kwaajili ya Masomo pia ametoa shukrani kwa Waziri Ulega na kumuahidi kusoma kwa Bidii.


02/09/2025

Fuatilia LIVE WASAFI FM

02/09/2025

Fuatilia LIVE WASAFI FM

02/09/2025
02/09/2025

Fuatilia LIVE Vipindi vya WASAFI FM

01/09/2025
01/09/2025

Fuatilia LIVE Vipindi vya WASAFI FM

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wasafi FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category