Wasafi FM

Wasafi FM The leading radio station in Tanzania specializing in the latest music & entertainment news.
(1)

Mchezaji wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Ureno, Diogo Jota, amefariki dunia kwa ajali ya gari nchini Hispania ...
03/07/2025

Mchezaji wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Ureno, Diogo Jota, amefariki dunia kwa ajali ya gari nchini Hispania akiwa na umri wa miaka 28.

Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari pamoja na taarifa rasmi kutoka mamlaka za Hispania, ajali hiyo ilitokea mapema alfajiri ya Alhamisi, Julai 3, 2025 katika mkoa wa Zamora, kaskazini-magharibi mwa Hispania. Gari walilokuwa wakisafiria lilipoteza mwelekeo na kugonga kingo za barabara kabla ya kuwaka moto.

Katika ajali hiyo ya kusikitisha, ndugu yake Diogo Jota aitwaye André Silva, pia alifariki dunia papo hapo. Wote wawili walikuwa wamesafiri kwenda kusherehekea mafanikio ya familia na walikuwa wametoka katika hafla binafsi.

Diogo Jota alijiunga na Liverpool mwaka 2020 kutoka Wolverhampton Wanderers, na amekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya klabu hiyo. Alifunga jumla ya mabao 65 katika mechi 182 alizochezea Liverpool, na kusaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England msimu wa 2024/25, pamoja na makombe mengine ya ndani.

Katika timu ya taifa ya Ureno, Jota alicheza mechi 49 na kufunga mabao muhimu, ikiwa ni pamoja na kuchangia ushindi wa Ureno kwenye michuano ya UEFA Nations League mwaka 2025.

Taarifa hii imepokelewa kwa mshtuko mkubwa na huzuni katika ulimwengu wa soka.
Klabu ya Liverpool, Shirikisho la Soka la Ureno (FPF), wachezaji wenzake, mashabiki na viongozi mbalimbali duniani wameendelea kutuma salamu za rambirambi kwa familia ya Jota na watu wote walioguswa na msiba huu.

Diogo Jota aliacha mjane na watoto watatu, siku chache tu baada ya kufunga ndoa rasmi na mke wake mnamo Juni 22, 2025.

Pumzika kwa amani Diogo Jota – shujaa wa Ureno na Liverpool. 🕊️

✍🏽

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Uongozi wake wakiongozwa na Mwe...
03/07/2025

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Uongozi wake wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bw. M***a Uledi na Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda wamesimama na kupiga Makofi kwa Dakika Moja mfululizo ili kuonyesha Shukrani kwa Walipakodi waliowawezesha kuandika historia ya kuvuka malengo ya makusanyo kwa miezi 12 mfululizo ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Tukio hilo la aina yake limefanyika Julai 01.2025 kwa nchi nzima baada ya Kamishna Mkuu Mwenda kuwasilisha taarifa ya makusanyo iliyoonyesha kuwa katika mwaka wa fedha 2024/2025, TRA imekusanya jumla ya Sh. Trilioni 32.26, sawa na ufanisi wa asilimia 103 ya lengo la Sh. Trilioni 31.5, na ukuaji wa asilimia 16.7 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Kamishna Mkuu Mwenda, amesema TRA inawathamini na kuwajali Walipakodi wote nchini ndiyo maana wameamua kuwaonyesha heshima maalum ya kusimama na kuwapigia makofi kwa Dakika Moja mfululizo na kuahidi kuwa TRA itaendelea kuwahudumia na kutatua changamoto zinazowakabili.

“Nguzo yetu kubwa ni Wafanyabiashara, ndiyo maana tumekuwa tukiweka mazingira mazuri ya ulipaji Kodi kwa hiari kwa lengo la kuwezesha biashara nchini, na hii ni sehemu ya kutekeleza maagizo ya Rais wetu Dk. Samia Suluhu Hassan aliyetuelekeza kuweka mazingira rafiki ya kukusanya Kodi “ amesema Bw. Mwenda.

Bw. Mwenda amesema kwa miezi yote 12 ya mwaka wa fedha 2024/2025, TRA ilivuka malengo ya makusanyo jambo ambalo halijawahi kutokea tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo na ni matunda ya mahusiano mazuri na Walipakodi.

Kwa mujibu wa Bw. Mwenda, wastani wa makusanyo ya kila mwezi umefikia Shilingi Trilioni 2.69 – kiwango cha juu zaidi kuwahi kufikiwa, kikiwa ni ongezeko kutoka Shilingi Trilioni 2.30 ya mwaka uliopita. Rekodi ya juu zaidi ya makusanyo kwa mwezi ni ya Desemba 2024 ambapo zilikusanywa Shilingi Trilioni 3.58, ikifuatiwa na Juni 2025 (Shilingi Trilioni 3.42) na Septemba 2024 (Shilingi Trilioni 3.02).

✍🏽

SHAMIRA ARUDISHA FOMU YA VITI MAALUM VIJANA BARA.Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Viti Vitatu Bara Ndg. Shamira Mshangama amec...
02/07/2025

SHAMIRA ARUDISHA FOMU YA VITI MAALUM VIJANA BARA.

Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Viti Vitatu Bara Ndg. Shamira Mshangama amechukua na kurudisha fomu ya kutia nia ya kugombea Ubunge wa Viti Maalum Vijana Tanzania Bara kutoka Mkoa wa Tanga.

25/06/2025

MIRADI YA TACTIC IMELETA MAPINDUZI YA KIUCHUMI MAJIMBONI KWETU- WABUNGE

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameeleza mageuzi makubwa ya kiuchumi na Kijamii yaliyojitokeza ikiwemo fursa za kiuchumi inayotokana na kuboreshwa kwa mazingira ya ufanyaji wa biashara katika Majimbo yao tangu kuanza kutekelezwa kwa Mradi wa Uboreshaji wa miundombinu ya Miji Tanzania TACTIC kwa awamu ya kwanza na ya pili ya mradi huo.

Leo Jumatano Juni 25, 2025 kwenye Mji wa Serikali, Mtumba Mjini Dodoma wakati wa utiaji saini utekelezaji wa miradi hiyo kwa Miji 11 ya Tanzania bara, ambayo ni Morogoro na Songea kwa awamu ya kwanza pamoja na Miji ya Tanga, Korogwe, Babati, Shinyanga, Bukoba, Bariadi, Lindi, Iringa na Njombe, Wabunge wanufaika wa miradi hiyo wameeleza kuwa TACTIC imesaidia katika kuboresha usimamizi na ukuaji wa Miji sambamba na Kuboresha utoaji wa huduma zinazotolewa na Halmashauri zao kwa wananchi.

Mbunge wa Tanga Mjini Mhe. Ummy Mwalimu, miongoni mwa Viongozi wanufaika wa Ujenzi wa mifereji ya maji, taa za barabarani na barabara za lami, amebainisha pia kuwa ujenzi wa Soko la Makorora na Soko la Samaki la Deep Sea Mjini Tanga ilikuwa ni ndoto na kilio cha muda mrefu na kubainisha kuwa kukamilika kwake kutabadilisha hadhi na muonekano wa Mji wa Tanga na kuongeza kipato kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wa Mji huo kutokana na mazingira yao ya biashara kuwa ya kisasa na yenye kuvutia.

Kwa upande wake Mbunge wa Iringa Mjini Mhe. Jesca Msambatavangu amebainisha kuwa kujengwa kwa soko la Kihesa kwenye mradi wa TACTIC awamu ya pili kutaondoa adha ya Wajasiriamali kufukuzwa na Mgambo wa Mji kutokana na kufanya biashara maeneo yasiyokuwa rasmi katikati ya Mji pamoja na kukuza mzunguko wa fedha na uchumi wa Iringa Mjini.

Aidha mbele ya Mgeni rasmi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mhe. Msambatavangu pia ameeleza kuwa ujenzi wa barabara ya Mkimbizi – Bima, Mtwivila, Viziwi na barababara ya Bontank kutainufaisha zaidi Iringa kiuchumi na Kiutalii, na hivyo kupendezesha mandhari ya Mji wa Iringa pamoja na kuimarisha shughuli za kiutalii katika Mji huo ulio kitovu cha Utalii kwa kanda ya Kusini.

Kwa upende wake Mbunge wa Bukoba Mjini Steven Byabato na Mhe. Patrobas Katambi wa Shinyanga Mjini, nao wameshukuru kwa ujio wa miradi ya TACTIC katika Miji yao wakimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuongoza mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kustawisha Jamii kupitia Miradi ya TACTIC, wenye lengo la kuboresha miundombinu ya Miji 45 ya Tanzania pamoja na kujenga uwezo wa Halmashauri ili ziweze kujiimarisha na kutoa huduma zenye ubora kwa wananchi wanaowahudumia.

25/06/2025

SPIKA WA BUNGE AMPONGEZA KAMISHNA MKUU WA TRA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dk. Tulia Ackson amempongeza Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) CPA Yusuph Juma Mwenda kwa kazi nzuri anayoifanya ya kukusanya mapato kwa wingi.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha mjadala wa bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2025/26 bungeni Juni 24.2025 Mhe. Tulia ametoa pongezi hizo kwa Kamishna Mkuu Mwenda na Uongozi wa TRA kwa kukusanya Kodi kwa wingi.

"Kipekee kabisa nitumie fursa hii kumshukuru na kumpongeza Kamishna Mkuu wa TRA kwa kazi nzuri anayoifanya na tunaamini kwa hatua ambazo zinaendelea kupigwa basi makusanyo yataendelea kuongezeka kwa kadiri yanavyopiga hatua sasa tunaona yanakimbia na tunaamini yataendelea kukimbia na yeye tunamtakia kila lakheri katika kuhakikisha makusanyo yanaendelea kukua" amesema Mhe. Tulia.

Amewataka Waheshimiwa Wabunge k**a wawakilishi wa wananchi wawe mfano mzuri katika kulipa kodi ili nchi iweze kupata maendeleo zaidi.

21/06/2025

Kutoka Chimbo amewakilisha k**a hivyo

Cc.

🖥

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepew...
21/06/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepewa heshima na hadhi ya kuwa Mtemi wa Sungusungu, jeshi la jadi, kwa mikoa mitano ya Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Geita na Tabora.

Mhe. Rais Dkt. Samia ambaye pia ni Mkuu wa Machifu nchini, akijulikana kwa jina la Chifu Hangaya, ametangazwa rasmi kuwa Mtemi wa Sungusungu kupitia risala ya utii wao kwake, wakati wa hafla ya kumpongeza kwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati, iliyofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, mkoani Mwanza, jana Ijumaa, tarehe 20 Juni 2025.

“Mheshimiwa Rais (Dkt. Samia) kwa kuwa wewe ni Amiri Jeshi Mkuu, na sisi ni walinzi wako, watiifu kabisa, tunaomba upokee hadhi ya kuwa Mtemi wa Sungusungu. Nakukabidhi vifaa vya ulinzi wa jadi, ambavyo vitatolewa maelezo. Aidha, tunaomba tukutambulishe watemi na mak**anda wa Sungusungu, ambao tumekuwa tukishirikiana katika mikoa hii mitano,” alisema Ndugu Richard Bundala, kiongozi wa Sungusungu hao.

Mtemi wa Sungusungu Kanda ya Ziwa, Sumbe Martine Mogani alimkabidhi Dkt. Samia silaha za kijadi, ambazo ni upinde na mishale, pamoja na mavazi ya kaniki na kofia, ikiwa ni ishara ya kumpatia heshima na hadhi hiyo ya kuwa mtemi wa Sungusungu katika mikoa hiyo mitano.

Kwa upande wake, Mhe. Rais Samia aliwapongeza Sungusungu kwa kutimiza miaka 42 tangu jeshi hilo la ulinzi wa jadi lilipoanzishwa kwa nia ya kuitikia wito wa kisera wa ulinzi na usalama, uliomtaka kila Mtanzania kuwa mlinzi ndani ya nchi yake, huku akiwataka kuendelea kushirikiana na mamlaka za kisheria, hasa Jeshi la Polisi, kupitia polisi jamii, katika kulinda amani na utulivu wa nchi katika maeneo yao.

Rais Dkt. Samia pia aliwapongeza walinzi hao wa jadi kwa mchango mkubwa ndani ya muda huo wote tangu kuanzishwa kwao, huku akiwataka kuendelea kuwa sehemu ya ulinzi na usalama wa mali na miradi ya maendeleo ambayo nchi imeanzishwa na kukamilishwa kwa gharama kubwa kote nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 16.06.2025 amezindua jengo la Mamlaka ya ...
16/06/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 16.06.2025 amezindua jengo la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Simiyu na kuwataka Watanzania kujenga utamaduni wa kulipa Kodi kwa hiari ili kuiwezesha Nchi kujitegemea kiuchumi.

Rais Samia amesema kujitegemea kiuchumi kunaletwa na Wananchi kupitia Kodi wanazolipa na kuitaka TRA kuendelea kukusanya Kodi kwa njia rafiki kwa wananchi na kuwapatia elimu ya Kodi wananchi ambao hawana uelewa wa masuala ya Kodi.

Amesema kutegemea msaada ni utumwa hivyo TRA kupitia Kodi zinazokusanywa zimekuwa zikitekeleza miradi ya kijamii k**a vile kupeleka Maji, Umeme na Huduma za Afya nchi nzima na katika miradi mikubwa ndiyo nchi imekuwa ikikopa au kupata msaada wa kutekeleza.

"Tunataka TRA ikusanye zaidi ndiyo maana tumewaongezea nguvu Kazi na majengo ya kisasa, nendeni mkakusanye kodi kwa njia rafiki, lakini kwa wale masugu na viburi lazima nao wafanywe walipe Kodi k**a ilivyo kwa wengine" amesema Rais Samia.

Aidha Rais Samia ameagiza kuongezwa kwa kasi ya ujenzi wa majengo ya TRA ambayo bado hayajakamilika ili yaanze kutoa huduma katika mazingira rafiki.

Kwa upande wake Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda amesema jengo hilo limegharimu kiasi cha Sh. Bilioni 9.83 na ni miongoni mwa majengo mengine yanayojengwa nchi nzima kwa gharama ya Sh. Bilioni 116.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema jengo hilo na mengine yanayoendelea kujengwa nchini yataongeza utoaji huduma bora kwa Mlipakodi, yataongeza hamasa kwa Watumishi pia yataongeza makusanyo ya Kodi kwa ujumla.

"Mhe. Rais tunashukuru kwa kutupatia fedha za ujenzi wa majengo yote yaliyokamilika na yanayoendelea kujengwa hii itasaidia tuendelee kukusanya Kodi na kuvuka malengo k**a ilivyokuwa kwa miezi 11 mfululizo tangu kuanza mwaka wa fedha 2024/2025 pia tunashukuru umetuongezea nguvu Kazi ya Watumishi wapya 1896" Kamishna Mkuu Mwenda amesema.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema katika kipindi cha miezi 11 TRA ilitakiwa kukusanya Sh. Trilioni 27.841 lakini imekusanya Sh. Trilioni 28.861 sawa na ufanisi wa asilimia 105 na anatarajia mwezi uliosalia wa June watavuka malengo.

Serikali imeendelea kupongezwa kila kona kwa uwekezaji mkubwa uliofanya katika bandari mbalimbali hapa nchini hususani b...
15/06/2025

Serikali imeendelea kupongezwa kila kona kwa uwekezaji mkubwa uliofanya katika bandari mbalimbali hapa nchini hususani bandari ya Dar es Salaam ambayo sasa imekuwa na ufanisi mkubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara ya kikazi bandarini jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dkt Joseph Mhagama amesema upanuzi na uboreshaji wa bandari hiyo imekuwa lulu kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.

“Leo tumekuja kwenye ziara yetu ya kawaida ya kikazi iliyo na lengo la kujionea utekelezaji wa miradi ya uboreshaji na upanuzi wa bandari hii ya Dar es Salaam”, alisema Dkt Mhagama.

Dkt Mhagama aliongeza kuwa taarifa ya uwekezaji huo haipo kwenye makaratasi tu bali ipo kwa vitendo, ndio maana mapato ya bandari yameongezeka na idadi ya wateja imeongezeka pia.

“Kwa hakika uwekezaji wa bandari hii umeifanya Bandari hii kuwa ni kitovu cha Utalii nchini, kwani mpaka hivi sasa kwenye mapato ya TRA yanaonesha bandari hii imechangia kwa asilimia 30”, alisisitiza Dkt Mhagama.

Aidha, Dkt Mhagama alisema kuwa wao k**a k**ati inayohusiana na masuala ya sheria mbalimbali, watashirikiana na TPA pamoja na Wizara ili kuhakikisha changamoto za kisheria zinatatuliwa ili kuongeza ufanisi kwa mamlaka hiyo kwani wameambiwa muingiliano wa kisheria ni mojawapo ya changamoto wanayokumbana nayo.

“Pamoja na hayo yote, kwa niaba ya Kamati hii ambayo mimi ninaiongoza tunampongeza Rais Samia kwa uthubutu na uwekezaji mkubwa anaoufanya kwenye miradi mbalimbali ya kimkakati sio tu hapa bali miradi yote hapa nchini”, alihitimisha Dkt Mhagama.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Bw. David Kihenzile akimuwakilisha Waziri wa Wizara hiyo Profesa Makame Mbarawa alisema kuwa wamepokea taarifa hiyo ya Kamati ya Bunge na kuahidi kuifanyia kazi.

“Nipende kuipongeza k**ati hii, kwani mara zote imekuwa na maono k**a aliyonayo Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan ya kutaka bandari zetu ziwe zinachangia pato kubwa katika nchi”, alisema Bw Kihenzile.

Aidha, Kihenzile alisema kuwa mipango ya Serikali ni mikubwa na ni endelevu ndiyo maana k**ati imefurahi na kuipongeza Serikali kwa uwekezaji huo uliofanywa kwa bandari mbalimbali hasa ya Dar es Salaam, Tanga, Mtwara na nyinginezo za maziwa.

“Licha ya hayo Serikali inaendelea na ujenzi wa meli katika ziwa Tanganyika na ziwa Viktoria, ambapo moja ya ziwa Viktoria ipo kwenye majaribio na muda siyo mrefu itaanza kazi”, alielezea Bw. Kihenzile.

Pamoja na hayo waziri Kihenzile alisema miradi hiyo yote inayojengwa imelenga kurahisa biashara na kutoa huduma bora kwa wananchi na kuwapunguzia ugumu wa maisha wananchi hasa kwa kuwasogezea karibu huduma zote muhimu.

Naye Mbunge wa viti maalumu kutoka mkoa wa Dar es Salaam wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bi Agnesta Kaizer alisema kuwa hana budi kumpongeza Rais Samia pamoja TPA kwa uwekezaji uliofanyika bandarini hapo na kufanya mazingira ya biashara yawe rahisi zaidi.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kuja huku bandarini mara baada ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali pamoja na wawekezaji, nilikua nasikia taaarifa za maboresho ya bandari hii kwenye vyombo vya habari pekee, lakini leo nimeamini” alisema Bi Kaizer.

15/06/2025

KAMISHNA WA UMEME NA NISHATI JADIDIFU AKAGUA MIRADI YA UMEME JIJINI DAR ES SALAAM

Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Innocent Luoga amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme ya Gridi Imara inayoendelea katika Jiji la Dar es Salaam, na kutoa maelekezo muhimu kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) pamoja na wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo.

Miradi hiyo inalenga kuimarisha upatikanaji wa umeme kwa kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuhakikisha huduma bora na ya uhakika kwa wananchi.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Kamishna amesema ameridhishwa na hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, licha ya changamoto mbalimbali za kimazingira, na kusisitiza umuhimu wa kuendelea na jitihada za kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

“Nimeridhishwa na hatua zilizofikiwa, lakini nimeagiza wakandarasi waharakishe kazi, vifaa vipatikane kwa wakati, na viwango vya kazi vizingatiwe ili miradi hii itoe matokeo yaliyokusudiwa kwa wananchi,” amesisitiza Mhandisi Luoga.

Akifafanua amebainisha kuwa miradi hiyo ya kimkakati, inayotekelezwa na TANESCO kwa ufadhili wa Serikali, inalenga kuboresha huduma ya umeme kwa wakazi wa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini. Aidha, ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuidhinisha rasilimali fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo muhimu.

Katika maagizo yake, ameitaka TANESCO kuongeza usimamizi kwa wakandarasi katika kuhakikisha upatikanaji wa vifaa kwa wakati, na kusimamia ubora wa kazi ili kuepuka ongezeko la gharama zitokanazo na ucheleweshaji.

Kwa upande wake, Mhandisi Abdallah Chikoyo, Meneja wa Miradi ya Kuzalisha Umeme TANESCO aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji , ameahidi kuongeza juhudi katika usimamizi wa miradi na kuweka mipango kazi inayotekelezeka kwa wakati.


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akifuatilia Hotuba ya Mapendekezo ya Serika...
12/06/2025

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akifuatilia Hotuba ya Mapendekezo ya Serikali kuhusu Bajeti Kuu ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 akiwa ofisini kwake, katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma, leo Alhamisi, tarehe 12 Juni 2025. Pamoja naye ni maofisa waandamizi wa CCM Makao Makuu.

11/06/2025

NILITEGEMEA YANGA WALALAMIKE TANGU MSIMU WA KWANZA SIO LEO -

Nasri amewaza kwa sauti! Inakuwaje Yanga Sc waanze kulalamike leo kuhusu hela ya Ubingwa wa misimu mitatu mfululizo? Nini kipo nyuma ya Pazia?
9

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wasafi FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category