Fursa Digital

Fursa Digital Nakusaidia kuongeza mauzo mitandaoni bila kutumia gharama kubwa ya matangazo. https://beacons.ai/fursadigital

Sikiliza..Hivi unajua unaweza kubadili kipaji au hobbie yako ikawa ni ajira ya kudumu.K**a unapenda kuangalia movies ten...
02/12/2024

Sikiliza..

Hivi unajua unaweza kubadili kipaji au hobbie yako ikawa ni ajira ya kudumu.

K**a unapenda kuangalia movies tengeneza account mtandaoni halafu unakuwa unafanya movie recap.

Yaani elezea story nzima ya movie kwa sababu sio watu wote wanaangalia muvi wanaelewa.

Sasa wewe wasaidie kuelewa.

Hii itakusaidia kuanza kuwauzia n.k

Umenipata ?

Haya sasa niambie wewe unakipaji gani lakini hujawahi kukitumia kabisa.

#2025

Njia rahisi ya kubadilisha changamoto kuwa Fursa unafanya hivi.Kabla sijaendelea fahamu kwamba mawazo mengi yanakufa kab...
09/11/2024

Njia rahisi ya kubadilisha changamoto kuwa Fursa unafanya hivi.

Kabla sijaendelea fahamu kwamba mawazo mengi yanakufa kabla ya kuanza kutekelezwa.

Moja ya sababu kubwa ni kutengeneza hoja (logic) kwenye changamoto hasa zinazokuzunguka.

Na kuwaza visivyowezekana kabla ya vinavyowezekana.

Sasa mbinu nzuri ni kuwaza kwa njia ya SAIKOLOJIA, kwa sababu mwanadamu anafanya maamuzi mengi kwa saikolojia kabla ya logic.

Mfano Rolls Royce & Lamborghini magari yao badala ya kuuza kwenye yards wao wanauzia kwenye viwanja vya ndege.

Mteja akienda kununua gari huku pembeni imepaki ndege za kifahari, atahusishanisha bei ya gari na ndege.

Wateja wananunua mitazamo na sio bei.

Hebu niambie kwenye comments wazo lako lipi umeshindwa kulifanya kisa mtazamo ?



Ndungu mjasiriamali.K**a unaweka bidhaa zako Facebook Marketplace basi epuka makosa haya.1. Kutopost Mara kwa Mara: unap...
07/11/2024

Ndungu mjasiriamali.

K**a unaweka bidhaa zako Facebook Marketplace basi epuka makosa haya.

1. Kutopost Mara kwa Mara: unapoteza wateja wengi kwa kutopost bidhaa mara kwa mara kwenye Facebook Marketplace.

Usipost mara moja halafu basi ukaacha.

Hakikisha unarepost bidhaa kila baada ya siku 7 kupita ili algorithms ipushi zaidi k**a bidhaa mpya.

2. Kushindwa Kutumia Picha Bora: Bidhaa zinazovutia huuzwa zaidi, lakini wengi wanatumia picha zisizo na ubora, na kufanya wateja kupuuza.

3. Kutojibu Haraka DM (messanger): mteja anauliza bidhaa na utaratibu wa kupata wewe unamjibu baada ya siku 3 na kupelekea mteja kutafuta bidhaa kwingine.

4. Kutokuweka Maelezo: Watu wanapenda kujua undani wa bidhaa, lakini wengi hawatoi maelezo ya kina kwenye posti zao.

Mfano, k**a ni nguo size, je used au mpya. Hakikisha unaweka maelezo ya kutosha

5. Bei zisizo Wazi, usipoweka bei maana yake mteja anajua hapa kila mtu anabei yake. So anahisi kupigwa.

Uzuri wa marketplace unaweza kuweka bei mbili moja ya offa na nyingine anzia.

Hebu niambie kwenye comments umewahi kutumia Facebook Marketplace ??


Hebu fikiria Ac, pasi au bomba lako la maji limeharibika na umechoka kuita mafundi ambao sio uhakika.Umeshawatumia mafun...
02/11/2024

Hebu fikiria Ac, pasi au bomba lako la maji limeharibika na umechoka kuita mafundi ambao sio uhakika.

Umeshawatumia mafundi wengi ila tatizo liko pale pale.

Habari nzuri ni kwamba kuna APP ya kibongo bongo inakukutanisha na Fundi moja moja

Kizuri zaidi ni bei iko kwenye App unachofanya ni ku request na kumpangia muda gani aje nyumbani au ofisini kwako.

Itakurahisishia hii ? Fundi anafika popote ulipo..

Hebu niambie kwenye comment unaijua hii App. ?

💧🛠️

Hivi itakuwaje biashara yangu ikafa ?Hivi itakuwaje ni kifeli mitihani yangu ya chuo? Vp k**a nitakosa kazi baada ya kum...
12/10/2024

Hivi itakuwaje biashara yangu ikafa ?

Hivi itakuwaje ni kifeli mitihani yangu ya chuo?

Vp k**a nitakosa kazi baada ya kumaliza chuo ?

Hivi itakuwaje ndoa yangu ikafa ?

Vp nikifukuzwa kazi ?

Usichokijua ni kwamba wasiwasi unazalisha magonjwa mengi sana.

K**a Heart attack.

Usipoweza kushinda UWOGA ulionao utakufa Mapema.

Badala yake jifunze kujikubali halafu jipige kifua sema.

Kila kitu kinachonikuta ni kwa sababu mungu kataka. Anza kuishi sasa achana na UWOGA.

Hebu niambie kwenye comments WASIWASI wako ni mkubwa ni upi ?

25/09/2024
Jenga ujuzi wako ukupe ajira ya uhakika..
05/08/2024

Jenga ujuzi wako ukupe ajira ya uhakika..

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fursa Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share