Bongo Boxing Safari

Bongo Boxing Safari We are informative, reliable platform for all boxing (Professional and Amateur) news and funny boxing contents across East Africa especially TANZANIA.

Kwa taarifa za uhakika za mchezo wa masumbwi Tanzania

Bondia Ismail Galiatano amefanikiwa kumchapa kwa pointi mpinzani wake Muskini Swalehe 'Alkasusu' katika mchezo uliopigwa...
26/02/2023

Bondia Ismail Galiatano amefanikiwa kumchapa kwa pointi mpinzani wake Muskini Swalehe 'Alkasusu' katika mchezo uliopigwa kwenye Ukumbi wa YMCA Moshi hapa Kilimanjaro.

Katika pambano hilo ambalo lilikuwa ni pambano kuu, Galiatano ameshinda kwa ushindi wa majaji wote wa tatu katika pambano hilo la Kili Boxing Tours ambalo ndiyo lilikuwa main card.

🥊

Bondia Karim Mandonga 'Mtu Kazi' ameendelea kuweka sawa rekodi yake ya ushindi baada ya kumchapa kwa TKO ya raundi ya pi...
26/02/2023

Bondia Karim Mandonga 'Mtu Kazi' ameendelea kuweka sawa rekodi yake ya ushindi baada ya kumchapa kwa TKO ya raundi ya pili Ali Boznia kutoka Tanga katika pambano la utangulizi la raundi sita.

🥊

Bondia Shaban Ndaro ameendeleza ubabe wake kwa mabondia wa ndani baada ya kumchapa kwa TKO ya raundi nne Musa Dragon ali...
26/02/2023

Bondia Shaban Ndaro ameendeleza ubabe wake kwa mabondia wa ndani baada ya kumchapa kwa TKO ya raundi nne Musa Dragon aliyeshindwa kuendelea na pambano kwa kuacha mwenyewe.

🥊

Bondia Amani Bariki 'Man Chuga amemwaga machozi na kugomea kutoka ndani  ya ulingoni kwa muda kufutia madai yake ya  kud...
25/02/2023

Bondia Amani Bariki 'Man Chuga amemwaga machozi na kugomea kutoka ndani ya ulingoni kwa muda kufutia madai yake ya kudhulumiwa ushindi wake dhidi ya Mudy Pesa katika pambano la utangulizi la Kili Boxing Tours.

Mabondia hao ambao wamecheza pambano la raundi nane lakini kwenye matokeo yamempa ushindi Mudy Pesa kwa majaji wawili kwa mmoja hali iliopeleka Man Chuga kuishiwa nguvu na kugoma kutoka nje ya ulingoni kutokana na kuongoza kwa raundi nyingi licha ya kuzidiwa nguvu.

BADO TUPO LIVE YOUTUBE YA BONGO BOXING SAFARI

🥊

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Sara Alex amefanikiwa kulipa kisasi kwa kumchapa kwa pointi mpinzani wake Samira Kasi...
25/02/2023

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Sara Alex amefanikiwa kulipa kisasi kwa kumchapa kwa pointi mpinzani wake Samira Kasim katika pambano la utanguli la Kili Boxing Tours ambalo limepigwa kwa raundi nne.

TUPO LIVE NDANI YA YOUTUBE CHANNEL YA BONGO BOXING SAFARI

🥊

Bondia Kasim Hamad amefanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi kufuatia kumchakaza Gabriel Chola katika pambano la  utangul...
25/02/2023

Bondia Kasim Hamad amefanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi kufuatia kumchakaza Gabriel Chola katika pambano la utangulizi ambalo limepigwa kwa raundi nane.

TUP LIVE BONGO BOXING SAFARI NDANI YA YOUTUBE
🥊

Girbert Machupa amefanikiwa kumtandika kwa pointi Roja Mjeshi katika pambano la utangulizi la Kili Boxing Tours ambalo l...
25/02/2023

Girbert Machupa amefanikiwa kumtandika kwa pointi Roja Mjeshi katika pambano la utangulizi la Kili Boxing Tours ambalo limepigwa kwa raundi sita, hapa YMCA bado moto unawaka.

🥊

Bondia  Waziri Magombana kulia amefanikiwa kumchapa kwa pointi Haruna Ndaro katika pambano la utangulizi ambalo limepigw...
25/02/2023

Bondia Waziri Magombana kulia amefanikiwa kumchapa kwa pointi Haruna Ndaro katika pambano la utangulizi ambalo limepigwa kwa raundi sita.

Usisahau TUPO LIVE YOUTUBE

🥊

Bondia Zuberi Kwedi amefanikiwa kumchapa kwa TKO ya raundi ya nne Simon Mrema hapa YMCA Moshi katika pambano la Kili Box...
25/02/2023

Bondia Zuberi Kwedi amefanikiwa kumchapa kwa TKO ya raundi ya nne Simon Mrema hapa YMCA Moshi katika pambano la Kili Boxing Tours.

🥊

25/02/2023

Masikini bondia Tony Rashid amevuliwa ubingwa kufuatia rais wa Umoja wa Shirikisho la Ngumi Afrika, Houcine Houichi kugomea ushindi wa Mtanzania kwa mujibu wa kadi ya matokeo iliotumwa kwao na kupelekea Sabelo Ngebinya kupewa mkanda huo wa ubingwa akiwa Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kurejea kwao Afrika Kusini.

Houcine amekiri kumvua ubingwa Mtanzania huyo baada ya kutokana na matokeo yaliotumwa kwake tofauti na ambayo yalitangazwa baada ya pambano hilo.

Rais huyo wa ABU alisema kuwa: "Ndiyo, ni kweli, msimamizi alifanya hesabu isiyo sahihi kwa jaji wa tatu, matokeo yalipswa kuwa 113-115 lakini badala yake msimmizi aliandika 115-113 ambayo ni makosa kabisa kulingana na 'mastercard' aliyotuma. Lilikuwa pambano zuri sana lakini Tony Rashid alishindwa kwa Split Decision".

Sabelo amekabidhiwa mkanda huo leo akiwa katika uwanja wa ndege kabla kuondoka baada ya kuchukuliwa kwa Tony Rashid aliyetangazwa jana k**a mshindi.

🥊

Usikose Kutazama 'LIVE' Usiku wa Kili Boxing Jumamosi ya Februari 25, kupitia YouTube Channel ya BONGO BOXING SAFARI na ...
25/02/2023

Usikose Kutazama 'LIVE' Usiku wa Kili Boxing Jumamosi ya Februari 25, kupitia YouTube Channel ya BONGO BOXING SAFARI na JEMEDARI TV, Ushuhudie Mapambano Makali kati ya Mandonga Mtu Kazi, Ismail Galiatano na Mengine mengi...

K**a Bado Hauja 'SUBSCRIBE' Kwenye YouTube Channel ya JEMEDARI na BONGO BOXING SAFARI Basi Fanya Hivyo Mapema, Moshi Kumekucha.....

Address

79905
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongo Boxing Safari posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share