Ananias Edgar Tv

Ananias Edgar Tv Ananias Edgar TV - Is the YouTube channel owned by FOMA ENTERTAINMENT MEDIA COMPANY LIMITED

Katika msimu wa baridi kali ikiambatana na theluji ikiwa imefunika kila kitu … ndani ya misitu ya Finland, alikuwepo mtu...
17/05/2025

Katika msimu wa baridi kali ikiambatana na theluji ikiwa imefunika kila kitu … ndani ya misitu ya Finland, alikuwepo mtu mmoja – mwenye utulivu wa ajabu, macho makali k**a tai, na uwezo wa kulenga na kuua kimya kimya.

Jina lake ni Simo Häyhä (Simo Heiha) – aliyetajwa baadaye na maadui wake k**a “The White Death”.

Simo alizaliwa tarehe 17 Desemba 1905, huko Rautjärvi (Rautijaavi), kijiji kidogo kilichopo mpakani na Urusi. Alikuwa mkulima na mwindaji, mtu wa maisha ya kawaida, mpole, asiyeongea sana.

Akiishi maisha ya upweke, akitumia muda wake mwingi kwenye uwindaji na kilimo.

Lakini mbali na kuwa sura yake ya unyenyekevu, alikuwa na jicho kali lisilokosea shabaha, na roho ya ujasiri isiyoyumba hata mbele ya kifo.

Mnamo Novemba 30, mwaka 1939 – Jeshi la Sovyeti liliivamia Finland. Likiwa na silaha nyingi, magari ya kivita na wanajeshi maelfu, walidhani wataisambaratisha Finland mapema tu. Lakini hawakujua kwamba, walikuwa wamemkanyaga simba mkali.

Simo Häyhä (Simo Heiha), akiwa na umri wa miaka 34, aliitikia wito wa nchi yake kuipigania. Aliingia vitani akiwa na bunduki yake ndogo ya zamani aina ya M/28-30, iliyokuwa haina hata darubini (scope). Hakuipenda darubini kwa sababu mbili kuu:

Mng’ao wa darubini kwenye mwanga wa jua ungeweza kumuonyesha kwa adui.

Darubini ilimlazimisha kuinua kichwa chake juu zaidi ya mwinuko wa theluji – na hilo lingeweza kumgharimu maisha.

Akiwa amevalia mavazi meupe ya theluji, akijificha kwenye kingo za barafu, Simo huketi masaa kadhaa bila hata kusogea, wala kupepesa macho. Aliweka theluji mdomoni wakati akipiga risasi ili moshi wa pumzi yake usionekane kwenye baridi.

Kwa ustadi wa hali ya juu wa kupiga shabaha, aliua wanajeshi zaidi ya 500 wa Soviet kwa kipindi cha chini ya miezi mitatu!

Hawakujua ni nani anayewaua. Hawakumuona muuaji wala kumsikia. Waliona tu wenzao wakianguka tu ghafla, kimya kimya.

Kwa majeshi ya Soviet, aligeuka kuwa jinamizi la kila siku – wakaanza kumwita “The White Death” – Mauti Nyeupe.

Soviet hawakukaa kimya. Kujibu mapigo walituma ma-sniper wao bora kabisa kumtafuta mtu huyu mmoja. Hakuna hata mmoja aliyerudi. Wakatuma vikosi vya kijeshi eneo la tukio – hakuna kilichosaidia. Simo hakuwa tu snipa – alikuwa ni k**a kivuli kisichoonekana.
Baadhi ya siku, aliua hadi wanajeshi 25 kwa siku moja. Wakati mwingine hakurudi kambini kwa masaa 24 – akijificha chini ya theluji kwa kujichimbia handaki dogo lililomficha huku akiwatazama maadui kwa utulivu, kana kwamba tai wa mwituni.

Lakini hatimaye, Machi 6 mwaka 1940, Simo alipigwa risasi ya usoni – mdomo na taya yake vilivunjika vibaya. Hata hivyo, alinusurika kifo.
Alitibiwa kwa siku nyingi, na hata aliporudi katika hali ya kawaida, shape ya uso wake ulikuwa umeharibika vibaya.

Lakini hata hivyo, siku hiyo hiyo aliyopigwa risasi, mkataba wa amani ulisainiwa kati ya Finland na umoja wa soviet – ni kana kwamba kazi ya Simo ilikuwa imekamilika.

Basi bwana, Simo hakupenda mambo mengi. Baada ya vita, alirudi kijijini kwake akaendelea na maisha ya kawaida. Alikataa ofa nyingi zakuingia kwenye siasa za nchi yake. Aliendelea kuwinda, kukaa kimya na kufurahia mandhari ya msituni.. Alikufa mwaka 2002 akiwa na umri wa miaka 96.
Wachambuzi wa kijeshi duniani kote waliendelea kumtazama k**a snipa bora zaidi kuwahi kutokea. Hakuwahi kujigamba. Hakuwahi kuomba sifa aina yeyote. Lakini dunia ikamwandika kwenye vitabu vya historia kwa herufi kubwa.

Simo Häyhä (Simo Heiha)hakuwa shujaa wa kelele nyingi au majigambo – alikuwa mshindi wa kimya kimya. Katika hali ya kawaida, hakuwa na umbile la kutisha, wala sauti ya mamlaka – lakini alibeba sifa ya mauti nyeupe, na alilinda nchi yake dhidi ya nguvu kubwa kwa ustadi, subira, na akili ya vita isiyo na mfano.

Kwa wale waliobaki kusema walimuona:

“Hakuna aliyepiga risasi kwa utulivu k**a Simo. Alikuwa kivuli, baridi k**a theluji, lakini makali kuliko risasi yenyewe.

K**a wewe ni mpenzi sana wa kusoma soma, ninakitabu changu kizuri sana cha Jicho la GENGHIS KHAN.

Kitabu cha Jicho la Genghis Khan kinaangazia:

Mbinu za kiintelijensia zilizotumiwa na Wamongolia kabla na wakati wa uvamizi. Jinsi mak**anda wake hususani wa ngazi za Noyan walivyotisha kwa mauaji na kuvaa ngozi na damu za binadamu.

Mafuvu ya maadui wao kuyaning'iniza kwenye kambi zao za kijeshi.

Ulinganisho wa kiufundi kati ya ujasusi wa Wamongolia na ule wa Dola zingine k**a Warumi, Wachina, na Wapersia.

Urithi wa mbinu hizi kwa mataifa ya sasa na funzo kwa taasisi za kiusalama leo.
Kwa yeyote anayetaka kufahamu mizizi ya ujasusi wa kale na namna ambavyo maarifa haya yanaweza kutumika leo, kitabu hiki kinaelezea mambo yote hayo.

Kwa sasa kipo softcopy, unalipia TZS 9,999 kwa M-PESA +255755448591 ANANIAS KITAGE.

Kabla ya vita, Salomon Sorowitsch alikuwa mtaalamu wa kuchapisha fedha bandia huko Vienna, Austria. Alikuwa maarufu kwen...
16/05/2025

Kabla ya vita, Salomon Sorowitsch alikuwa mtaalamu wa kuchapisha fedha bandia huko Vienna, Austria. Alikuwa maarufu kwenye ulimwengu wa uhalifu wa kifedha – akili nyingi, mikono mizuri, na macho yaliyoweza kuiga sahihi yoyote.

Lakini ujanja wake ulimfikisha gerezani. Huko ndiko alipopatikana na Wajerumani, wakati walipovamia Austria mnamo 1938. Na kwa kuwa alikuwa Myahudi, alipelekwa moja kwa moja kwenye kambi ya mateso ya Sachsenhausen.

Mnamo mwaka 1942, mawazo ya kichaa yaliingia katika kichwa cha Adolf Hi**er na Himmler:

“Tuchapishe mamilioni ya pauni bandia – tuingize sokoni Uingereza – tuuharibu uchumi wao kabisa.”

Huo ukawa mwanzo wa Operation Bernhard – mpango mkubwa wa kivita wa kiuchumi, wa kihistoria kuwahi kutekelezwa.

Na kwa hili, walihitaji watu wasio wa kawaida – walihitaji wajanja walioko gerezani. Salomon Sorowitsch, akiwa tayari gerezani, aliona fursa ya kuishi.

Wajerumani waliwachagua wafungwa wachache kutoka kambi mbalimbali –wakiwemo wachapishaji, wasanii, wahandisi, wahasibu – wote wakiwa Wayahudi.

Wakawakusanya katika sehemu maalum ndani ya kambi ya Sachsenhausen, ambapo walipewa vyumba safi, vitanda vizuri, chakula kizuri, na hata burudani.

Lakini walipewa masharti:

“Mkiweza kuiga noti za Uingereza (Pauni), mtaendelea kuishi. Mkishindwa – gesi ya sumu inawasubiri kuwaangamiza.”

Salomon na wenzake hawakuwa na jinsi, walianza kuifanya kazi hii ngumu.

Kwanza kwa;

Kujifunza karatasi halisi ya pauni

Kuiga watermark, mikunjo ya karatasi, na hata namba za mabenki

Na zaidi: walipaswa kuchapisha kiasi kikubwa cha pesa kwa haraka – zaidi ya pauni milioni 130 walizalisha.

Lengo la Hi**er lilikuwa kupeleka pesa hizi kwenye soko la kimataifa, kuharibu thamani ya sarafu ya Uingereza, na kufeli kwa uchumi wao. Baadhi ya fedha hizi bandia ziliingizwa hata katika akaunti za Uswisi kupitia mawakala wa N**i.

Hili lilifanikiwa kwasababu; serikali ya Ujerumani haikuridhika tu kuzitupa mitaani — walitaka kuzigeuza kuwa halali na kuzitumia kwenye miamala ya kimataifa.
Hivyo waliwatumia Wapelelezi na Mawakala wao waliokuwa huko Uswisi

Kipindi hicho Ujerumani ilikuwa na mtandao mpana wa majasusi kwenye mashirika mbalimbali ya kifedha, mashirika bandia, au hata matajiri wa Kijerumani kwenye nchi za kigeni.

Watu hawa walipewa fedha hizo bandia, kisha:

Walizibadilisha kwa franc za Uswisi katika ofisi za ubadilishaji wa fedha (ambapo ilikuwa vigumu kugundua uhalali wa noti hizo).

Walizitumia kufungulia akaunti kwenye benki za Uswisi, benki ambazo zilijulikana kwa kutotoa taarifa za wateja wao (siri ya kifedha ilikuwa sheria madhubuti sana Uswisi wakati huo).

Baadhi ya pesa hizo zilihifadhiwa, nyingine zilitumika kununua bidhaa kutoka nchi zisizo na upande (neutral) – k**a vile Uswisi yenyewe, Sweden, au hata baadhi ya nchi za Amerika Kusini.

Lakini pia zilitumika kwenye;

Ununuzi wa silaha au vifaa kutoka kwa wafanyabiashara wa kimataifa waliotaka pesa bila kuuliza maswali mengi.

Malipo kwa wapelelezi, wanaharakati, au hata wanasiasa waliokuwa wakifanya kazi kwa siri kwa niaba ya serikali ya Ujerumani.

Lakini pia benki nyingi za Uswisi, kwa wakati huo:

Hazikuwa zikichunguza sana asili ya fedha

Hazikuwajibika kutoa taarifa kwa mataifa ya nje

Pia hazikuwa na vifaa vya kisasa vya kugundua noti bandia zilizotengenezwa kwa umahiri wa hali ya juu

Basi bwana, Wafungwa hawa hawakutaka kuendelea tena na mpango huo.

Salomon, kwa ujanja, alianza kuchelewesha kazi kimakusudi. Aliharibu baadhi ya matoleo ya noti. Alifanya makosa ya kudhamiria. Hakutaka kuwa mshiriki wa kuharibu dunia. Lakini pia hakutaka afe.

Lakini jambo kubwa na la kufurahisha zaidi ni baada ya;

Mpango huo kugunduliwa mwishoni mwa vita hivyo. Wanajeshi wa jeshi la Muungano walipofika Sachsenhausen, waliwakuta wafungwa wakitupa pesa bandia kwenye tanuru – wakiharibu ushahidi.

Kwahiyo, Operation Bernhard haikufanikiwa k**a Hi**er alivyotamani. Uchumi wa Uingereza haukuanguka, lakini baadhi ya fedha bandia zilibaki katika mzunguko hadi miaka ya 1950.

Salomon Sorowitsch aliokolewa na alipotoka alichagua kutotumia uwezo wake wa kutengeneza pesa bandia tena.

Na hakusema chochote kuhusu mpango huo hadi miaka ya baadaye sana.

Muvi ya The Counterfeiters (2007), iliyoongozwa na Stefan Ruzowitzky, ilitengenezwa kwa kuzingatia kisa chake halisi – na hata kuja kushinda Tuzo ya Oscar k**a Filamu Bora ya Kigeni.

Kumbe basi kwa kumalizia, Wakati wengine walikuwa mstari wa mbele na bunduki, wengine walikuwa kwenye vita ya kiuchumi, wakipambana na sarafu, karatasi, na maamuzi ya uhai na kifo ndani ya kambi za mateso.

K**a wewe ni mpenzi sana wa kusoma soma, ninakitabu changu kizuri sana cha Jicho la GENGHIS KHAN.

Kitabu cha Jicho la Genghis Khan kinaangazia:

Mbinu za kiintelijensia zilizotumiwa na Wamongolia kabla na wakati wa uvamizi. Jinsi mak**anda wake hususani wa ngazi za Noyan walivyotisha kwa mauaji na kuvaa ngozi na damu za binadamu.

Mafuvu ya maadui wao kuyaning'iniza kwenye kambi zao za kijeshi.

Ulinganisho wa kiufundi kati ya ujasusi wa Wamongolia na ule wa Dola zingine k**a Warumi, Wachina, na Wapersia.

Urithi wa mbinu hizi kwa mataifa ya sasa na funzo kwa taasisi za kiusalama leo.

Kwa yeyote anayetaka kufahamu mizizi ya ujasusi wa kale na namna ambavyo maarifa haya yanaweza kutumika leo, kitabu hiki kinaelezea mambo yote hayo.

Kwa sasa kipo softcopy, unalipia TZS 9,999 kwa M-PESA +255755448591 ANANIAS KITAGE.

Vasily Grigoryevich Zaytsev alizaliwa tarehe 23 Machi 1915 katika kijiji kidogo kiitwacho Yeleninskoye, kilichopo huko m...
15/05/2025

Vasily Grigoryevich Zaytsev alizaliwa tarehe 23 Machi 1915 katika kijiji kidogo kiitwacho Yeleninskoye, kilichopo huko milimani mwa Urusi ya Kusini (sasa linaitwa eneo la Bashkortostan).

Akiwa mtoto wa wakulima wa kawaida, Vasily alilelewa katika mazingira ya msituni na porini au bush – sehemu ambazo baadaye zilichangia kumkuza kuwa mlenga shabaha sniper mashuhuri zaidi katika historia ya Urusi.

Tangu akiwa na umri wa miaka 7, babu yake alimfundisha jinsi ya kutumia bunduki, si kwa ajili ya mapambano vitani, bali kwa kuwinda wanyamapori k**a vile swala na sungura.

Lakini mafundisho hayo yaliambatana na nidhamu ya hali ya juu – babu yake alimsisitizia kupiga risasi moja tu kwa kila mnyama mmoja na kamwe asirudie kupiga risasi ya pili kwa shabaha moja ya mnyama.

Hii ilimfundisha uvumilivu, umakini, na usahihi wa kufocus wa hali ya juu.

Katika umri wake wa ujana, aliingia jeshini. Lakini kabla ya kuingia jeshini, Vasily alisomea kazi ya uhasibu na kufanya kazi k**a mhasibu wa jeshi la wanamaji (Navy) wa Umoja wa Kisovyeti.
Lakini baada ya kuibuka kwa vita vya pili vya dunia.
Mwaka 1941, alijitolea kujiunga na Jeshi la Ardhini la Usovyeti (lililoitwa Red Army) akiwa na umri wa miaka 26 tu.
Na wakati wa vita hivyo vya ulmwengu, alipopelekwa kwenye mapigano huko Stalingrad mwaka 1942, awali alipewa kazi ya kawaida k**a askari.

Lakini siku moja alipata nafasi ya kutumia bunduki ya sniper ambayo aliiokota kwa bahati mbaya kutoka kwa askari aliyekufa – na hapo ndipo kipaji chake kilipoonekana waziwazi.

Kwasababu katika muda mfupi tu, Vasily aliweza kuwaua wanajeshi zaidi ya 30 wa jeshi la N**i kwa risasi moja moja tu, kwa umbali wa hadi mita 1,000.

Jina lake lilisambaa kwa kasi ya kimbunga ndani ya Jeshi la Usovyeti, wakubwa wake wakapendezwa naye sana na akateuliwa rasmi kuwa sniper wa kikosi maalum.

Basi bwana, Mapigano ya Stalingrad yalikuwa miongoni mwa mapigano makubwa na vya kikatili zaidi kuwahi kutokea katika vita vya pili vya dunia . Jiji zima liligeuka kuwa magofu, lakini kilichoendelea humo kilikuwa ni vita vya mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba, na hata dirisha kwa dirisha yani ilikuwa balaa.

Zaytsev aliyatumia mazingira haya kwa ustadi. Akijificha ndani ya vifusi, kwenye dari za nyumba zilizobomoka, au ndani ya mahandaki ya zamani.

Jamaa alijifunza kutotumia sehemu moja mara mbili, na mara zote alikuwa anabadilisha sehemu baada ya kurusha kila risasi.

Akiwa na bunduki aina ya Mosin-Nagant yenye darubini kali kipindi hicho, alitengeneza rekodi ya kuua zaidi ya wanajeshi 225 wa N**i kwa mkono wake mwenyewe.

Idadi hiyo ni pamoja na maofisa, snipers wengine, waongozaji wa ndege, wapiga mizinga, na wapiganaji wa kawaida.

Umaarufu wa Vasily ulipofika hadi makao makuu ya kijeshi ya Ujerumani, Wajerumani waliingiwa na hofu. Walihisi kuwa huyu mtu mmoja alikuwa akiathiri morali ya majeshi yao zaidi ya hata kikosi kizima.
Wakampeleka sniper wao bora kutoka Berlin – Major Erwin König, ambaye inasemekana alikuwa mkufunzi (mwalimu) mkuu wa shule ya mafunzo ya snipers wa jeshi la N**i.
Basi bwana, kwa siku tatu nzima, Vasily na König walikuwa kwenye duwa ya kivita yani wakiwindana k**a ule mchezo wa paka na panya.

Kila mmoja alikuwa na lengo moja tu – kumuua mwenzake.

Walikuwa kimya, kila mmoja akimvizia mwenzake. Mvua, baridi, njaa, na usingizi havikuweza kuwatenganisha.

Hatimaye, Vasily alitambua sehemu ambayo König alikuwa amejificha baada ya kumuona kwenye mng’ao mdogo wa mwanga wa Darubini yake ya kulengea.

Akavuta pumzi, akapumua polepole… na akaminya trigger. Risasi ilimlenga moja kwa moja kichwani. König akaanguka chini na kupoteza maisha.

Kwa ushindi huo, Zaytsev hakuwa tu ameua mtu mmoja – alikuwa ameua matumaini ya askari wa jeshi zima la N**i kwenye uwanja wa mapambano.

Baada ya Vita ya Pili ya Dunia, Vasily Zaytsev hakubaki jeshini. Alirudi kwenye maisha ya kawaida, akaendelea na kazi za kiraia k**a mhandisi kwenye kiwanda cha nguo huko Kiev, Ukraine.

Alikuwa mtu wa kawaida sana machoni mwa watu – aliishi kwa unyenyekevu hadi alipofariki dunia mnamo tarehe 15 Desemba 1991.

Lakini jina lake halikuwahi kusahaulika. Mnamo mwaka 2001, sinema ya “Enemy at the Gates” ilieleza hadithi ya mapambano yake na Major König, ikimpa Zaytsev hadhi ya kimataifa k**a shujaa wa kivita aliyeua si kwa manufaa yake binafsi, bali kwa usalama wa taifa lake.

Mpaka leo, jina la Vasily Zaytsev linakumbukwa k**a allegory (mfano hai) wa ujasiri, ustadi, na utulivu hata katikati ya ghasia kubwa. Alifundisha askari wengine zaidi ya 30 kuwa snipers, ambao nao waliua maelfu ya wanajeshi wa N**i.
Hivyo, athari yake haikuwa tu kwenye bunduki yake – bali pia kwenye kizazi kizima cha wapiganaji waliofuata njia yake.
“Mpiga risasi mzuri huua kwa risasi moja tu. Mpiga risasi bora huua kwa kusubiri wakati sahihi.” – Vasily Zaytsev

Hadithi ya Vasily Zaytsev si tu hadithi ya mwanajeshi, bali ni hadithi ya mtu wa kawaida aliyekubali kuweka maisha yake mbele kwa ajili ya taifa lake.

Alikuwa na risasi, lakini akawa na lengo kubwa zaidi – uhuru, usalama, na historia.

K**a wewe ni mpenzi sana wa kusoma soma, ninakitabu changu kizuri sana cha Jicho la GENGHIS KHAN.

Kitabu cha Jicho la Genghis Khan kinaangazia:

Mbinu za kiintelijensia zilizotumiwa na Wamongolia kabla na wakati wa uvamizi. Jinsi mak**anda wake hususani wa ngazi za Noyan walivyotisha kwa mauaji na kuvaa ngozi na damu za binadamu.

Mafuvu ya maadui wao kuyaning'iniza kwenye kambi zao za kijeshi.

Ulinganisho wa kiufundi kati ya ujasusi wa Wamongolia na ule wa Dola zingine k**a Warumi, Wachina, na Wapersia.

Urithi wa mbinu hizi kwa mataifa ya sasa na funzo kwa taasisi za kiusalama leo.

Kwa yeyote anayetaka kufahamu mizizi ya ujasusi wa kale na namna ambavyo maarifa haya yanaweza kutumika leo, kitabu hiki kinaelezea mambo yote hayo.

Kwa sasa kipo softcopy, unalipia TZS 9,999 kwa M-PESA +255755448591 ANANIAS KITAGE.

Maafa ya Uwanja wa Heysel yalitokea Mei 29, 1985, ambayo ilikuwa siku ya Fainali za Kombe la Ulaya 1985 kati ya Juventus...
06/02/2025

Maafa ya Uwanja wa Heysel yalitokea Mei 29, 1985, ambayo ilikuwa siku ya Fainali za Kombe la Ulaya 1985 kati ya Juventus na Liverpool.

Katika siku hiyo mchezo ulitarajiwa kuwa mzuri, lakini uligeuka na kuwa ndoto. Uwanja wenyewe ulikuwa katika hali mbaya hata kabla ya mechi kuanza.

Ghasia zilizuka, wakati mashabiki wa Liverpool walipoanza kuwarushia miamba wafuasi wa Juventus. Hii ilisababisha Waitaliano kuhama, kujaribu kupanda juu ya ukuta ili kuepuka kupambana na mashabiki wa Liverpool pamoja na miamba ya kuruka, na ndipo maafa yakatokea.

Ukuta wa uwanja huo ulianguka chini ya uzito wa mashabiki wa Juventus, na kusababisha vifo vya watu 39 na zaidi ya majeruhi 600.

Uzembe wa mashabiki wa Liverpool ulisababisha vilabu vyote vya Uingereza kufungiwa kushiriki mashindano ya Uropa kwa miaka 5, huku Liverpool ikipigwa marufuku ya miaka 6. Aidha, mashabiki 14 wa Liverpool walipatikana na hatia ya kuua bila kukusudia.

Talent We Trust

Utafiti umeonyesha kuwa kunguru wana uwezo wa kutambua watu kwa sura na hata kutofautisha kati ya watu tofauti. Pia, wan...
04/02/2025

Utafiti umeonyesha kuwa kunguru wana uwezo wa kutambua watu kwa sura na hata kutofautisha kati ya watu tofauti.

Pia, wanajua jinsi ya kujibu kulingana na uzoefu wao na watu hao. Hii inamaanisha kuwa k**a mtu aliwahi kuwa na mwingiliano mzuri au mbaya na kunguru, anaweza kuwa na athari kwa jinsi kunguru wanavyomwona mtu huyo tena.

Huu ni mfano wa uwezo wa wanyama hawa wa kuonyesha ufanisi katika kumbukumbu na kutambua sura.

talent We Trust

Mbuzi hawa, hasa mbuzi wa Aoudad (au Barbary), wanapenda kupanda miti ya argan, ambayo ni mti maarufu nchini Morocco. Hi...
04/02/2025

Mbuzi hawa, hasa mbuzi wa Aoudad (au Barbary), wanapenda kupanda miti ya argan, ambayo ni mti maarufu nchini Morocco. Hii ni tabia ya ajabu ambayo inawafanya mbuzi hawa kuwa maarufu miongoni mwa watalii wanaotembelea katika nchi hiyo.

Mbuzi hao hupanda miti ili kupata majani na matunda, na hii ni njia ya kujilinda kutokana na majanga ya mazingira k**a vile upungufu wa malisho kwenye ardhi kavu. Vilevile, mbuzi hawa wana uwezo wa kupanda kwa ustadi mkubwa, na hii inachukuliwa k**a sehemu ya tabia zao za kipekee.

Talent We Trust

Tukio hili lilitokea mnamo Septemba 10, 1945, katika mji wa Fruita, Colorado, Marekani.Mmiliki wake, Lloyd Olsen, alipan...
01/02/2025

Tukio hili lilitokea mnamo Septemba 10, 1945, katika mji wa Fruita, Colorado, Marekani.

Mmiliki wake, Lloyd Olsen, alipanga kumchinja Mike kwa ajili ya chakula.

Hata hivyo, baada ya kukata kichwa chake, sehemu kubwa ya shingo na ubongo wake wa nyuma (brain stem) ilibaki intact. Kwa mshangao, Mike aliendelea kuonyesha ishara za uhai akijaribu kutembea na hata "kujipanga manyoya" kwa mdomo wake usiokuwepo.

Baada ya hayo Mike aliendelea kuishi kwa kumwagiwa chakula na maji moja kwa moja kupitia koo lake lililobaki
wazi.

Kuku huyo aliendelea kukua, akifikia uzito wa 3.6 kg na akawa kivutio kikubwa na kuonyeshwa kwenye maonesho mbalimbali ya wanyama wa ajabu kote Marekani.

Mnamo Machi 1947, baada ya miezi 18, Mike alifariki. Inasemekana aliziba koo lake na Olsen hakufanikiwa kumsafisha kwa wakati.

Talent We Trust

Paul Deschanel alikuwa Rais wa Ufaransa kwa muda mfupi mwaka 1920, na moja ya matukio ya kushangaza yaliyomhusisha ni ji...
30/01/2025

Paul Deschanel alikuwa Rais wa Ufaransa kwa muda mfupi mwaka 1920, na moja ya matukio ya kushangaza yaliyomhusisha ni jinsi alivyoanguka kutoka kwenye treni usiku wa manane!

Mnamo Mei 24, 1920, Paul Deschanel alikuwa akisafiri kwa treni ya kifahari kutoka Paris kuelekea Montbrison. Usiku huo, akiwa amechoka, alifungua dirisha la chumba chake kwa bahati mbaya na akaanguka nje ya treni wakati ikiwa inatembea kwa kasi.

Watu wa kwanza kumuona walikuwa wafanyakazi wa reli waliompata akizurura vichakani akiwa hana viatu na akiwa hana fahamu kabisa kuhusu kilichotokea. Alijitambulisha kwao kuwa yeye ni Rais wa Ufaransa, lakini hawakumwamini! Walidhani alikuwa mlevi au mgonjwa wa akili.

Tukio hili lilimfanya aonekane k**a mtu asiye na uthabiti wa akili, na upinzani wake wa kisiasa ukalitumia kumchafua.

Afya yake ilizidi kudhoofika, na baadaye mwaka huo alilazimika kujiuzulu k**a rais baada ya kuhudumu kwa miezi sita pekee.

Talent We Trust

Saparmurat Niyazov (1940–2006) alikuwa rais wa kwanza wa Turkmenistan baada ya kuvunjika kwa Umoja wa Kisovyeti mnamo 19...
30/01/2025

Saparmurat Niyazov (1940–2006) alikuwa rais wa kwanza wa Turkmenistan baada ya kuvunjika kwa Umoja wa Kisovyeti mnamo 1991.

Alitawala nchi hiyo kwa mkono wa chuma hadi kifo chake mwaka 2006, akijulikana kwa maamuzi ya ajabu na ya kushangaza yaliyovutia dunia.

Maamuzi yake yalikuwa k**a vile;
- Aliamua kubadilisha majina ya miezi ya mwaka, ambapo:

*Januari ilipewa jina lake(Turkmenbashi).

*Aprili ilipewa jina la mama yake(Gurbansoltan).

- Aliandika Kitabu Kilicholazimishwa Kusomwa na Wote.

-Aliamuru majengo na magari yote yawe meupe. Na mengineyo mengi.

Talent We Trust

Jambo lingine la ajabu kuhusu Kim Jong-il alikuwa na uwezo wa kufanya mambo yasiyo ya kawaida, k**a vile kucheza gofu kw...
30/01/2025

Jambo lingine la ajabu kuhusu Kim Jong-il alikuwa na uwezo wa kufanya mambo yasiyo ya kawaida, k**a vile kucheza gofu kwa mara ya kwanza na kupata hole-in-one mara 11.

Talent We Trust

Sanamu la The Knife Angel lina urefu wa futi 27, limetengenezwa kwa visu 100,000. Sanamu hilo liliundwa na msanii Alfie ...
29/01/2025

Sanamu la The Knife Angel lina urefu wa futi 27, limetengenezwa kwa visu 100,000.

Sanamu hilo liliundwa na msanii Alfie Bradley na British Ironworks Center mwaka 2018. Sanamu hiyo ni Mnara wa Kitaifa Dhidi ya Vurugu na Uchokozi.

Visu vya kwenye sanamu hilo vilikusanywa kutoka kwa kampeni ya kitaifa ya kukusanya visu nchini Uingereza.

Sanamu hii iliundwa ili kuongeza uelewa kuhusu vurugu za visu na athari zake katika jamii. Ilionyeshwa katika maeneo mbalimbali nchini Uingereza, ikiwa ni pamoja na London, k**a sehemu ya kampeni ya kuhamasisha amani na usalama.

Talent We Trust

Kituo hiki ni nyumbani kwa meli nyingi za Jeshi la Wanamaji la Marekani (U.S. Navy) na ni sehemu muhimu kwa operesheni z...
28/01/2025

Kituo hiki ni nyumbani kwa meli nyingi za Jeshi la Wanamaji la Marekani (U.S. Navy) na ni sehemu muhimu kwa operesheni za majini za Marekani na washirika wake.

Kilianzishwa mwaka 1917 , wakati wa Vita vya Kwanza vya Dunia
kituo hicho Kinaweza kuhifadhi meli zaidi ya 75, ikiwa ni pamoja na aircraft carriers, submarines, na destroyers.

Katika eneo hilo kuna zaidi ya wanajeshi na wafanyakazi 80,000
pia kuna uwanja wa ndege wa kijeshi unaotumiwa na ndege za Jeshi la Wanamaji na Jeshi la Anga.

Talent We Trust

Address

Dar Es Salam

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 17:00

Telephone

+255222701398

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ananias Edgar Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share