Manara Tv

Manara Tv For your Sports, Business, Politics, and Entertainment, with Breaking News in-depth analysis and Exclusive Interviews

01/12/2025

Vijana nchini Tanzania wametakiwa kuendelea kuilinda na kuidumisha amani ambayo imeifanya nchi hiyo kutambulika duniani k**a moja ya mataifa yenye utulivu na mshik**ano mkubwa.

Wito huo umetolewa na Mbunge wa Jimbo la Madaba, Mhe. Omary Msigwa, alipokuwa akizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Feo Girls, iliyopo wilayani Songea mkoa wa Ruvuma, wakati wa mahafali ya kidato cha nne shuleni hapo.

Mhe. Msigwa amesema Tanzania imekuwa ikiheshimiwa kwa amani yake kwa miaka mingi, kiasi cha kuwa kimbilio kwa nchi ambazo zilipoteza utulivu. Hata hivyo, alionya kuwa matukio ya hivi karibuni yanaashiria dalili za kupungua kwa misingi hiyo, na hivyo ni jukumu la vijana kuhakikisha kuwa hali hiyo haijitokezi.

Kwa upande wao, wanafunzi wa Feo Girls wamesema amani ndiyo nguzo ya maendeleo ya taifa lolote, hivyo vijana hawana budi kuendelea kushirikiana na serikali na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha misingi hiyo inasimama imara.

Wamesema bila amani hakuna elimu bora, maendeleo ya kiuchumi wala fursa za ajira, hivyo ni wajibu wa kila kijana kuhakikisha matendo na kauli zao hazitetereshi utulivu wa nchi.


01/12/2025

Tamasha la Magari ya Zamani msimu wa kwanza limezinduliwa rasmi mkoani Kilimanjaro, likiwa na lengo la kuwakutanisha wakazi wa mkoa huo na wale wanaoishi mikoani, hasa kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka,Tamasha hilo limeandaliwa na Kampuni ya African Sports Agency.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Yusufu Nzowa, amesema tamasha hilo lina manufaa makubwa kwa mkoa huo, ikiwemo kuchochea ukuaji wa uchumi na kutangaza utalii wa Kilimanjaro kimataifa.

“Kuwepo kwa tamasha hili moja ni fursa ya kuutangaza mkoa ndani na nje ya nchi. Tuna uhakika watu mbalimbali watajitokeza kuja kushuhudia magari haya ya miaka ya nyuma, yaliyohifadhiwa tangu miaka ya 1990 kurudi nyuma,” amesema Nzowa.

Ameongeza kuwa ujio wa wageni kutoka nje ya nchi na mikoa mingine ni msukumo mkubwa kwa uchumi wa mkoa huo, kwani watatumia huduma mbalimbali ikiwemo hoteli, usafiri k**a bodaboda na bajaji, pamoja na kununua bidhaa za ndani hatua inayoongeza kipato kwa wananchi mmoja mmoja.

Mkurugenzi wa African Sports Agency Company Ltd, Joseph Mselle, ambaye ni mratibu wa tamasha amesema dhamira kuu ya tamasha mbali na burudani na historia ya magari hayo ya miaka ya nyuma, tamasha hilo pia linahamasisha matumizi ya nishati safi na salama ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, sambamba na kutengeneza mtandao wa mahusiano (connections) kati ya washiriki kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

Aidha, kupitia tamasha hilo kutakuwa na safari maalum za kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini, hatua itakayoongeza uelewa na kuvutia wageni wengi zaidi kutembelea Tanzania.

Kwa upande wake, Afisa Utalii wa Hifadhi ya Makuyuni Wildlife Park chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mustapher Yusuph, amesema tamasha hilo ni aina ya kipekee ya utalii inayopanua upeo wa vivutio vya kanda ya Kaskazini na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki.

“Huu ni utalii k**a utalii mwingine. Tunawakaribisha wakazi wa Kanda ya Kaskazini wafike kwa wingi. Tumeandaa pia safari maalum za utalii wa ndani kwa washiriki wa tamasha hili ili kuendelea kutangaza vivutio vyetu,” amesema Yusuph.


Habari zilizojiri kupitia kurasa za mbele za Magazeti leo Jumatatu ya tarehe 01/12/2025
01/12/2025

Habari zilizojiri kupitia kurasa za mbele za Magazeti leo Jumatatu ya tarehe 01/12/2025


30/11/2025

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ametoa maelekezo kwa Mameneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) nchi nzima kuhakikisha hakuna foleni zisizo na sababu zitakazokwamisha na kuzorotesha shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

Ulega ametoa agizo hilo jijini Dar es Salaam jana wakati akikagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya Mbagala Rangi Tatu - Kongowe (km 3.8) ambapo alizungumza na wananchi wa eneo hilo na kuwaeleza kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameidhinisha zaidi ya Shilingi Bilioni 54 kutumika kwa ajili ya kutatua kero ya foleni kwa wakazi wa Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

"Wakurugenzi kutoka TANROADS, ninaagiza kwa Mameneja wote nchi nzima nikisikia habari za foleni zinalalamikiwa na wananchi na hakuna suluhu ya muda mfupi na ya muda mrefu hufai kuwa Meneja," alisema Waziri Ulega.

Aidha, Ulega ametoa angalizo kwa Mameneja hao katika kipindi hiki cha mvua zinazotarajiwa kunyesha kuhakikisha barabara hazileti athari kwa wananchi na kusababisha kushindwa kufanya shughuli zao kutokana na kukosa suluhu ya jambo hilo mapema.

"Mameneja fanyeni kazi, msikae kimazoea na kuona jambo hilo ni la kawaida, kukatika kwa barabara tafsiri yake Meneja hukagui barabara yako na kuona hapa kuna udhaifu ambao lolote likitokea pataharibika," amesisitiza Ulega.

Vilevile, Ulega amemuagiza Meneja wa TANROADS mkoa wa Pwani kuhakikisha anaitengeneza barabara ya zamani ya Morogoro haraka iwezekanavyo ili iweze kuwa njia mbadala ya kutatua changamoto za magari kukwama katika barabara kuu ya Dar es Salaam hadi Chalinze.

Naye, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Lazeck Alinanuswe ameeleza kuwa upanuzi wa barabara hiyo unatekelezwa na Mkandarasi STECOL Corporation kutoka China na kusimamiwa na Kitengo cha TECU kutoka TANROADS kwa muda wa miezi 15 na hivyo mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba 2026.


Msanii  wa Bongo Flava,  , ameendelea kuweka rekodi na kuthibitisha ukubwa wake kimataifa baada ya wimbo wake “Oh Mama T...
30/11/2025

Msanii wa Bongo Flava, , ameendelea kuweka rekodi na kuthibitisha ukubwa wake kimataifa baada ya wimbo wake “Oh Mama Tetema” kupata tuzo ya 8× Gold nchini India, ikiwa ni mauzo ya muziki na streams.

Tuzo ya Gold kawaida inahesabiwa kulingana na mchanganyiko wa mauzo ya muziki na streams. Hi ikimaanisha wimbo wa umepata mafanikio makubwa ya wimbo katika mauzo na usikilizwaji.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, amejivunia mafanikio hayo akisema:

“Hakuna kenge wala mjusi wa kugusa hizi mambo nchi hii. Naweka rekodi ambazo nakuja kuzivunja tena mimi mwenyewe. Tetema ya Colombia ilipiga Gold moja, hii imepiga mara nane.”

Wimbo “Oh Mama Tetema” ni kolabo ya kimataifa inayowakutanisha Rayvanny, Nora Fatehi, Shreya Ghoshal, Vishal Mishra, Sanjoy na Bhushan K, na umeendelea kupaa katika majukwaa ya kimataifa kutokana na ushirikiano huo wa Afrika na India.

Mafanikio haya yanaifanya “Oh Mama Tetema” kuwa moja ya nyimbo za Rayvanny zilizofanya vizuri zaidi duniani, ikivunja rekodi ya awali ya “Tetema” iliyopata Gold moja nchini Colombia.

Rayvanny ameahidi kuendelea kusukuma muziki wake mbele akisema atavunja rekodi zake mwenyewe siku zijazo.

Rayvanny sasa anazidi kukita mizizi k**a mmoja wa Wasanii wakubwa barani Afrika na duniani, huku mchango wake katika kuutangaza muziki wa Bongo Flava ukizidi kutambulika kimataifa.


30/11/2025

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri kuelekeza Mfuko wa Taifa wa Maji kutoka shilingi Milioni 500 na kuzielekeza Kivule, Ilala Jijini Dar Es Salaam ili kuchimba visima katika eneo hilo na kuondoa adha ya maji kwa wananchi wa maeneo hayo.

Waziri Aweso amebainisha hayo mbele ya Mamia ya wananchi wa Kivule, wakati wa muendelezo wa Ziara yake ya kikazi Mkoani humo, akisisitiza kuwa dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kuwa hakuna mwananchi anayeteseka na changamoto ya maji katika maeneo yote nchini Tanzania.

"Mradi huu ufanyike haraka na nitakuja kuuzindua mimi mwenyewe na hiyo ndio ahsante yangu na niombe muendelee kumuombea sana Rais Samia Suluhu Hassan." Amesema Waziri Aweso.

Katika maelezo yake mengine kwa wananchi hao, Waziri Aweso amesema ni mpango wa Rais Samia kuunganisha mradi wa maji wa Bangulo na wananchi wa Kivule, akisema kukamilika kwa miradi hiyo kutaondoa changamoto kubwa ya maji kwa wananchi wa eneo hilo.


Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Ado Shaibu Ado amesema kuwa kuwa katika utumishi katika nafasi hiyo kipaumbel...
30/11/2025

Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Ado Shaibu Ado amesema kuwa kuwa katika utumishi katika nafasi hiyo kipaumbele chake namba moja kitakuwa ni elimu. Ndugu Ado ametoa kauli hiyo katika mahafali ya Shule ya Awali ya Kawetu Day Care Center iliyopo Wilayani Tunduru yaliyofanyika leo tarehe 30 Novemba 2025.

Akizungumza na wazazi, walimu na wanafunzi wa shule hiyo Ado amesema kuwa jamii ikikombolewa kwenye elimu ni rahisi kupata ukombozi wa kiuchumi na kijamii. Ndugu Ado ametoa ahadi ya kukutana na wamiliki na waendeshaji wa shule za Awali kwa ajili ya kusikiliza changamoto zao na kuzishughulikia.

Akijibu changamoto za Shule ya Awali ya Kawetu Day Care zilizowasilishwa na Mkurugenzi wa Shule hiyo amesema kuwa changamoto zote mbili zilizowasilishwa atazifanyia kazi. Amesema kwa upande wa changamoto ya magodoro kwa ajili ya kulalia watoto ataitatua ndani ya siku moja akitoa agizo kwa Katibu wake kupeleka magodoro hayo leo. Kwa upande wa ujenzi wa uzio wa shule hiyo kwa ajili ya usalama wa watoto amesema ataketi chini na uongozi wa shule hiyo kwa ajili ya kufanya tathmini ya kina na kuahidi kutoa mchango wake baada ya tathmini hiyo.
Katika hatua nyingine Ndugu Ado ameomba wazazi kupeleka watoto wao katika shule za Awali na pia kwa wale waliofikisha miaka sita wapelekwe shule ya msingi.
“Ipo tabia ya baadhi ya wazazi kutotilia mkazo suala la kupeleka watoto shule. Tunduru tunapaswa kuipenda, kuikumbatia na kuijali elimu kwa nguvu zote kwani ndio itayoikomboa jamii yetu” alisisitiza Ndugu Ado.




30/11/2025

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera, Ndugu Faris Buruhani, ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika kuimarisha elimu ya ufundi stadi nchini kupitia mpango wa ujenzi na upanuzi wa vyuo vya VETA nchini kote.

Akizungumza katika Mahafali ya Pili ya wahitimu wa ngazi ya pili ya mwaka 2025 yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma VETA Kagera, Faris alisema kuwa uwekezaji unaofanywa na serikali ni ushahidi wa dhamira ya dhati ya kuboresha elimu ya ufundi kwa vijana.

Amebainisha kuwa serikali imewekeza katika miundombinu ya kisasa, vifaa vya kufundishia na teknolojia mpya, hatua inayolenga kuongeza ubora wa mafunzo na kuwajengea vijana ujuzi utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa viwanda.


Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askof...
30/11/2025

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askofu Dkt. Josephat Gwajima k**a walivyokuwa wametangaza awali ili aweze kuendelea shughuli zake.

Amesema baada ya kutoa msamaha kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, waumini wanahitaji wamuone kiongozi wao, hivyo anatakiwa ajitokeze hadharani aendelee na kazi yake. “Mwacheni ajitokekeze tujenge umoja wa kitaifa, tushik**ane kurudisha umoja wa kitaifa. Tumekutana na TEC, viongozi wa dini, wa mila na viongozi mbalimbali; twendeni sote kwenye jambo hili, tujitokeze tuhamasishe Tanzania yenye amani, huu ndio wito wa kiongozi wetu wa nchi”

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Novemba 30, 2025) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Arumeru katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Magufuli Leganga, kata ya Usa River, wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Waziri Mkuu amewataka Watanzania wakatae kushawishiwa na wanaharakati wanaochochea vurugu kwani zinarudisha nyuma maendeleo ya nchi. “Nimekuja kuwapa pole wananchi wenzangu, kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Anatambua mambo yanayoendelea. Anatambua kazi kubwa ya kujenga Taifa mnayoifanya,” amesema.

Kabla ya mkutano huo, Waziri Mkuu alikagua uharibifu uliofanywa wakati wa vurugu za Oktoba 29, mwaka huu kwenye kituo cha polisi cha Kikatiti (mita 500 kutoka barabara kuu ya Arusha - Moshi); Mahak**a ya Mwanzo ya Maji ya Chai (km. 3 kutoka barabara hiyo kuu); kituo cha mafuta Total Energies kilichopo Maji ya Chai (kipo barabarani) ambavyo vyote vilichomwa moto ikiwemo kuiba mali kwenye supermarket na kubomoa sefu ya kutunzia fedha.

Klabu ya Mbeya City FC imetangaza kusitisha mkataba na aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo Malale Hamsini, kuanzia tarehe ...
30/11/2025

Klabu ya Mbeya City FC imetangaza kusitisha mkataba na aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo Malale Hamsini, kuanzia tarehe 30 Novemba 2025. Uamuzi huo pia umehusisha kusitishwa kwa mikataba ya kocha msaidizi M***a Rashid, kocha wa magolikipa Wilbert Mweta, pamoja na daktari wa timu Hashraf Mapunda.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari ya klabu hiyo, hatua hiyo imefikiwa kufuatia kutoridhishwa na mwenendo wa timu katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara (NBC Premier League), ambapo matokeo ya hivi karibuni hayakutimia matarajio ya uongozi.

Klabu imewapongeza waliokuwa makocha hao kwa mchango wao ndani ya Mbeya City na imewatakia mafanikio mema katika majukumu na safari zao mpya.

✍🏼


FULL TIME |  Singida BS 1️⃣ 🆚 1️⃣ Stellenbosch FC🏟️New Amaan Complex🏆 ⚽Langelihle Phili Dk 52'⚽Marouf Tchakei (P) Dk 90+...
30/11/2025

FULL TIME |

Singida BS 1️⃣ 🆚 1️⃣ Stellenbosch FC
🏟️New Amaan Complex
🏆

⚽Langelihle Phili Dk 52'

⚽Marouf Tchakei (P) Dk 90+


Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Ado Shaibu Ado amepokelewa kwa kishindo Jimboni kwake Tunduru Kaskazini kwake...
30/11/2025

Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Ado Shaibu Ado amepokelewa kwa kishindo Jimboni kwake Tunduru Kaskazini kwake katika ziara yake ya kwanza baada ya kuapishwa kuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Ndugu Ado ameanza ziara yake ya kuwashukuru wananchi wa Tunduru Kaskazini kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo hilo kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Baraza la Idd Tunduru Mjini leo tarehe 30 Novemba 2025.




Address

Salamanda Tower
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manara Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share