Manara Tv

Manara Tv For your Sports, Business, Politics, and Entertainment, with Breaking News in-depth analysis and Exclusive Interviews

Habari zilizojiri kupitia kurasa za mbele za Magazeti leo Jumapili ya tarehe 07/09/2025
07/09/2025

Habari zilizojiri kupitia kurasa za mbele za Magazeti leo Jumapili ya tarehe 07/09/2025


06/09/2025

Maelfu ya watu wamejitokeza Kigoma Mjini kwenye ufunguzi wa kampeni za chama cha ACT Wazalendo.


06/09/2025

Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya kimezindua rasmi kampeni zake za kusaka kura za Rais, Ubunge na Udiwani, kikiwa na dhamira ya kushinda viti vyote kwa kura za kishindo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Akizungumza na wananchi katika uzinduzi huo uliofanyika Itumbi, kata ya Matundasi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lupa kwa tiketi ya CCM Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, amewahakikishia wananchi kuwa chama hicho kitaendelea kuwa mstari wa mbele kusimamia maendeleo ya jamii kwa vitendo na si kwa maneno.

ameeleza kuwa tangu mwaka 2020 alipopewa ridhaa ya kuwatumikia wananchi, ametekeleza kwa vitendo ajenda alizoahidi, na sasa anaomba nafasi ya kuendeleza kazi iliyokwisha kuanzishwa kupitia chama hicho.

“Tumefanya mengi kwa ushirikiano na wananchi, bado yapo makubwa mbele yetu. Ndiyo maana tunaomba ridhaa ya awamu nyingine ili tukamilishe tulipoishia,” alisema Masache.

Aidha Masache ameainisha vipaumbele vyake kuwa sekta ya madini itaendelea kupewa kipaumbele maalumu kutokana na fursa zilizopo wilayani Chunya, sambamba na maboresho makubwa kwenye sekta ya elimu, ujenzi wa barabara, na upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.

Aidha, amesisitiza mshik**ano wa wananchi katika kuunga mkono juhudi za CCM, akibainisha kuwa maendeleo ya kweli yatapatikana endapo kila mmoja ataendelea kushirikiana na kuamini sera na mikakati ya chama hicho kikongwe nchini.

✍🏼


06/09/2025

Katika tukio la kusikitisha wazazi wa mtoto Bright Joel Malila (15), wakazi wa mtaa wa Igodima, kata ya Iganzo jijini Mbeya wanadaiwa kumuua mtoto wao kwa kipigo wakimtuhumu kuiba televisheni ya nyumbani, kisha kutokomea kusikojulikana baada ya tukio hilo.

Majirani na wananchi wa mtaa huo wamesema siku ya tukio walisikia kelele za mtoto huyo wakati akiadhibiwa na wazazi wake, lakini zilisikika kwa muda mfupi na wao kudhani kuwa ni hali ya kawaida ya mzazi kumuadhibu mtoto.

Baadaye, majirani hao walishangazwa walipoitwa na kushuhudia hali ya kusikitisha baada ya kubaini kuwa adhabu hiyo iligeuka kuwa kipigo cha kikatili kilichosababisha kifo cha mtoto huyo.

Tukio hili limeacha simanzi kubwa kwa wakazi wa eneo hilo, huku wengi wakilaani kitendo hicho na kuwataka wazazi kuepuka kutumia nguvu kupita kiasi katika malezi ya watoto wao.
tanzania

✍🏼


06/09/2025

Mbunge mteule wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Moshi Mjini, mkoani Kilimanjaro, Ibrahim Mohammed Shayo maarufu k**a *Ibraline*, amevunja rasmi makundi yote yaliyokuwa ndani ya chama hicho wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea wa ubunge.

Akizungumza Septemba 6, 2025, katika hafla maalum ya kuvunja makundi hayo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Ibraline alisema kuwa hatua ya uteuzi ndani ya chama sasa imekamilika, na kinachotakiwa kwa sasa ni mshik**ano wa pamoja kuelekea ushindi wa wagombea wote wa CCM.

“Kwa sasa tunatakiwa tuwe na kundi moja tu kundi la CCM. Umoja wetu ndio silaha ya ushindi kwa wagombea wetu wa Udiwani, Ubunge na Urais,” amesema Ibraline.

Mbunge huyo mteule amesema uwepo wa makundi hayo uliathiri watu wengi, si yeye pekee, bali pia baadhi ya viongozi wa chama, wanachama na hata wananchi wa kawaida.

“Wapo walioathirika kibiashara, kiuchumi, kijamii, na wakati mwingine makundi haya yalifika hadi hatua ya kubeza utu wa binadamu. Kwa kifupi, asilimia 70 ya tuliyopo hapa kwa namna moja au nyingine tumeguswa na makundi haya,”ameongeza Ibraline.


Msanii wa R&B, Chris Brown, ameibuka na ujumbe mzito kwa mashabiki wake na wadau wa muziki wanaopenda kulinganisha wasan...
06/09/2025

Msanii wa R&B, Chris Brown, ameibuka na ujumbe mzito kwa mashabiki wake na wadau wa muziki wanaopenda kulinganisha wasanii juu ya Msanii gani nii bora zaidi.

Akiwa kwenye mapumziko mafupi ya Breezy Tour, Breezy aliposti ujumbe kupitia Instagram Story yake leo Jumamosi asubuhi akisema,

"Kwa maoni yangu ya dhati Beyonce, Michael Jackson na Usher wote ni Superstars wakubwa katika nafasi zao za kipekee. Enzi hizo muziki ulikuwa na ubunifu wa hali ya juu, na tulivutiwa na kila msanii kwa sababu walikuwa matoleo bora ya ubunifu wao, bila mijadala ya nani bora zaidi."

Kupitia kauli hiyo, Chris Brown amesisitiza kuwa kila msanii ana upekee wake na anatakiwa kuthaminiwa kwa mchango wake, badala ya kuendelea na mabishano ya nani anastahili taji la Msanii bora zaidi.

✍️|


06/09/2025

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jackson Kiswaga  amempongeza kwa dhati Mgombea Urais wa CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya kuleta maendeleo ndani ya Jimbo la Kalenga na mkoa wa Iringa kwa ujumla.

Akizungumza mbele ya Rais Samia, Viongozi wa CCM na wana CCM Kiswaga amesema maendeleo yaliyofanyika Kalenga ni ushahidi wa wazi kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia imefanya kazi kubwa na yenye kugusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Ameeleza namna barabara kuu na barabara za vijijini zilivyoimarishwa ikiwa ni pamoja na miradi mikubwa ya elimu, afya, kilimo, umeme na maji inayotekelezwa kwa kasi kubwa na kwa viwango vya juu.


Klabu ya Trabzonspor ya Uturuki imefikia makubaliano na Manchester United kwa ajili ya kumsaini kwa mkopo golikipa wa ti...
06/09/2025

Klabu ya Trabzonspor ya Uturuki imefikia makubaliano na Manchester United kwa ajili ya kumsaini kwa mkopo golikipa wa timu hiyo, André Onana.

Hatua pekee iliyosalia ni makubaliano binafsi kati ya mchezaji huyo raia wa Cameroon na Trabzonspor kabla ya dili hilo kukamilika rasmi.

Onana, ambaye alijiunga na Manchester United akitokea Inter Milan, amekuwa chini ya presha kubwa kutokana na makosa kadhaa tangu kuwasili kwake Old Trafford, hali iliyochangia mjadala mkubwa kuhusu nafasi yake katika kikosi cha kwanza.

Iwapo makubaliano hayo yatakamilika, Onana atajiunga na Trabzonspor kwa msimu wa 2025/26 kwa lengo la kupata nafasi zaidi ya kucheza na kurejesha kiwango chake.


Mafundi wa pikipiki katika Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kuacha tabia ya kufungia wateja wao taa zenye mwanga mkali, ...
06/09/2025

Mafundi wa pikipiki katika Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kuacha tabia ya kufungia wateja wao taa zenye mwanga mkali, hatua inayotajwa kusababisha ajali na kuhatarisha maisha ya watumiaji wengine wa barabara.

Elimu hiyo imetolewa na Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, alipowatembelea mafundi hao katika maeneo yao ya kazi.

Sajenti Ndimila aliwaasa mafundi hao kuacha tabia hiyo kwa kuwa imekuwa kero na hatari kubwa kwa watumiaji wa vyombo vya moto, hasa nyakati za usiku. Alibainisha kuwa mwanga mkali unaweza kumsababisha dereva wa chombo kingine kupoteza uelekeo na hatimaye kusababisha ajali.

Aidha, aliwataka mafundi wa pikipiki kujitambua na kujisimamia katika majukumu yao kwa kuhakikisha hawachangii katika kusababisha ajali barabarani, bali wawe walimu na washauri bora kwa wateja wao wanapokuja kupata huduma za matengenezo.
tanzania


Mafundi wa pikipiki katika Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kuacha tabia ya kufungia wateja wao taa zenye mwanga mkali, ...
06/09/2025

Mafundi wa pikipiki katika Manispaa ya Shinyanga wametakiwa kuacha tabia ya kufungia wateja wao taa zenye mwanga mkali, hatua inayotajwa kusababisha ajali na kuhatarisha maisha ya watumiaji wengine wa barabara.

Elimu hiyo imetolewa na Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, alipowatembelea mafundi hao katika maeneo yao ya kazi.

Sajenti Ndimila aliwaasa mafundi hao kuacha tabia hiyo kwa kuwa imekuwa kero na hatari kubwa kwa watumiaji wa vyombo vya moto, hasa nyakati za usiku. Alibainisha kuwa mwanga mkali unaweza kumsababisha dereva wa chombo kingine kupoteza uelekeo na hatimaye kusababisha ajali.

Aidha, aliwataka mafundi wa pikipiki kujitambua na kujisimamia katika majukumu yao kwa kuhakikisha hawachangii katika kusababisha ajali barabarani, bali wawe walimu na washauri bora kwa wateja wao wanapokuja kupata huduma za matengenezo.
tanzania


06/09/2025

Kikosi cha wagosi wa kaya kimerejea jijini Tanga baada ya kuondoshwa katika michuano ya Tanzanite Tornament yanayoendelea mkoani Babati katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa.

Msemaji Hussein Mchomvu maarufu k**a Diego amesema wanaendelea kujiweka sawa kuelekea tamasha la Coastal Union Festival Day litakalofanyik Sept 14, likinogeshwa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Fc Bomet ya Nchini Kenya.

Ameongeza kuwa mbali na mchezo huo pia kikosi kipo tayari kwa msimu mpya wa ligikuu 2025/2025 ambapo mchezo wa kwanza watacheza na Tanzania Prison kutoka jijini Mbeya.

✍️


06/09/2025

Mteule wa kugombea ubunge kwa nafasi ya vijana kutokea Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Jasmine Ng'umbi ameonyesha shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambaye ni mgombea wa urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan kwa kuwaamini vijana na kuwapa nafasi katika uongozi wa kitaifa na ndani ya CCM.

‎Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Mafinga mkoani Iringa Leo Septemba 6, 2025 Jasmine amesema uteuzi wake ni ushahidi wa namna Rais Samia anavyowajali vijana na kufafanua kuwa awali alikuwa namba saba kwenye orodha ya wagombea lakini alipandishwa hadi nafasi ya sita, jambo alilolieleza kuwa ni heshima kubwa kwake na kwa vijana wa Mufindi.

‎Katika mkutano huo wa hadhara, Jasmine alipiga goti hadharani kumshukuru mgombea urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini, na kuahidi kuwa atahakikisha ifikapo Oktoba 29, Wananchi wanampigia kura mgombea huyo kwa kishindo.

‎Aliwataja viongozi wengine vijana walioteuliwa na Rais Samia k**a ushahidi wa dhamira yake ya kweli, akimtaja Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa, Kenani Kihongosi k**a mfano wa kuigwa.

‎Mkutano huo ulivuta umati mkubwa wa wanachama wa CCM waliokuwa wakishangilia kwa nguvu huku wakitamka jina la chama chao mara kwa mara, kuonesha kuunga mkono nafasi aliyopewa Jasmine Ng'umbi..


Address

Salamanda Tower
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manara Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share