Manara Tv

Manara Tv For your Sports, Business, Politics, and Entertainment, with Breaking News in-depth analysis and Exclusive Interviews
(4)

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu, ameupongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa...
24/07/2025

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu, ameupongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa jinsi unavyotekeleza majukumu yake ya kuhakikisha wastaafu wanapatiwa mafao yao kwa wakati.

Ameyasema hayo alipotembelea banda la watoa huduma wa PSSSF kwenye mkutano mkuu wa kwanza wa Maafisa Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala (TAPA-HR) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC jijini Arusha, Julai 24, 2025.

“ Katika kipindi cha hivi karibuni ukwasi wa mfuko umeendelea kukua na namna ambavyo mnavyowekeza kimkakati inasaidia Mfuko kuwa himilivu.” Alibainisha.

Pia, amesisitiza PSSSF kuendelea kutoa elimu kwa watumishi wanaokaribia kustaafu ili wanapostaafu mafao wanayopatiwa yaweze kuwa na tija kwao.

Akitoa maelezo kwa Mhe. Sangu, Afisa Mkuu wa Matekelezo PSSSF, Bw. Venance Mwaijibe, alisema tangu kuanza kwa mkutano huo Julai 22, maafisa wa Mfuko wamekuwa wakitoa elimu kwa Maafisa Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala kuhakikisha kuwa wanawaandaa watumishi (wanachama ) wawe tayari kustaafu.

“Lakini pia tunawaeleza kuwa huduma zetu kwa sasa zinapatikana kwa njia ya mtandao kupitia PSSSF Kidijitali, k**a vile kusajili wanachama, kuwasilisha madai mbalimbali ya mafao, wastaafu kujihakiki kupitia simu janja lakini pia wanaweza kuuliza maswali yoyote yanayohusiana na uanachama.” Alisema Bw. Mwaijibe.

Mkutano huo ambaoi umewaleta pamoja maafisa haom kutoka bara na visiwani, unafikia kilele Julai 25, 2025 ukiwa umebeba kaulimbiu isemayo 'Mwelekeo mpya wa nafasi ya wataalamu wa usimamizi wa rasilimali watu na utawala kusukuma mabadiliko kuendana na mageuzi ya teknolojia'.
Mwisaho.

Msanii maarufu wa Bongo Fleva,  , pamoja na mkewe .priscy wametangaza rasmi kuwa wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza....
24/07/2025

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, , pamoja na mkewe .priscy wametangaza rasmi kuwa wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza. Wapenzi hao wamewashangaza mashabiki wao baada ya kuchapisha picha kwenye kurasa zao za Instagram, ikimuonesha Priscilla akiwa mjamzito.

Katika picha hiyo Jux na Priscilla waliambatanisha ujumbe mfupi uliosomeka kuwa

"MOM & DAD
BLESSED. GRATEFUL. THANKFUL
less swaggdaddyyoungray
THANK YOU LORD"

Ujumbe huo unaashiria furaha yao kubwa na shukrani kwa Mungu kwa baraka ya ujauzito.

✍️|


Kwa mujibu wa tafiti za kisaikolojia na za neva, binadamu huzaliwa akiwa na hofu mbili tu za kiasili:1. Hofu ya sauti ku...
24/07/2025

Kwa mujibu wa tafiti za kisaikolojia na za neva, binadamu huzaliwa akiwa na hofu mbili tu za kiasili:

1. Hofu ya sauti kubwa

2. Hofu ya kuanguka kutoka juu

Hofu hizi ni za kiasili na zinahusiana moja kwa moja na silika ya kujilinda na kuishi. Zinamsaidia mtoto mchanga kujiweka salama hata kabla ya kuelewa mazingira yake.

Hata hivyo, tafiti zinaonyesha kuwa hofu nyingine zote k**a hofu ya kushindwa, kukataliwa, giza, kuongea mbele ya watu, au hata buibui ni matokeo ya uzoefu binafsi, malezi ya kifamilia, na athari za kitamaduni. Kwa maneno mengine, hofu hizi hujifunzwa kadri mtu anavyokua na kuishi.

Habari njema ni kwamba ubongo wa mwanadamu una uwezo wa kubadilika (neuroplasticity), hali inayomaanisha kuwa mtu anaweza kuufundisha tena ubongo wake na kuondokana na hofu nyingi alizojifunza baadaye maishani.

Kwa hivyo, ikiwa unakabiliwa na hofu inayokuzuia kufanikisha malengo yako, kumbuka haukuzaliwa nayo na unaweza kuikabili na kuishinda.

Je, Hofu gani huwa inakutatiza?

✍️|


Rapa maarufu kutoka Memphis, GloRilla, amejikuta tena matatani kwenye mkono wa sheria katika jimbo la Georgia  kufuatia ...
24/07/2025

Rapa maarufu kutoka Memphis, GloRilla, amejikuta tena matatani kwenye mkono wa sheria katika jimbo la Georgia kufuatia tuhuma nzito zinazohusiana na madawa ya kulevya. Kwa mujibu wa taarifa kutoka TMZ, alik**atwa siku ya Jumanne katika Kaunti ya Forsyth na kufikishwa rumande kwa makosa mawili ya jinai, moja ikiwa ni kumiliki dawa za kulevya za ratiba maalum (scheduled controlled substance) na kumiliki bangi zaidi ya kiasi kilichoruhusiwa kisheria (zaidi ya ounce moja).

Makosa yote mawili yanachukuliwa k**a makosa makubwa chini ya sheria za jimbo hilo. Kulingana na rekodi za gereza zilizopatikana na TMZ, msanii huyo alik**atwa na baadaye kuachiwa huru siku hiyo hiyo baada ya kuwekewa dhamana ya dola 22,000 sawa na zaidi ya Tsh Milioni 57.

Hii inakuwa mara ya pili kwa Msanii huyo kutiwa mbaroni huko Georgia ndani ya kipindi kisichozidi mwaka mmoja. Mnamo Aprili 2024, alik**atwa katika Kaunti ya Gwinnett kwa tuhuma za kuendesha gari akiwa amelewa (DUI).

✍️|


Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Juma Mwenda, ametoa wito kwa wafanyabiashara wa mitandaoni ...
24/07/2025

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Juma Mwenda, ametoa wito kwa wafanyabiashara wa mitandaoni ambao hawajajisajili na TRA kujisajili mara moja ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.

Ameyasema hayo wakati akizindua rasmi utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano (MoU) kati ya TRA na Shirika la Kimataifa linashughulika na masuala ya Kodi (IBFD) ambao umefanyika katika Chuo cha Kodi (ITA) jijini Dar es Salaam Leo tarehe 24.07.2025.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema wametoa mwezi mmoja kuanzia Agosti Mosi mpaka Agosti 31.2025 wafanyabiashara wote wanaoendesha shughuli zao mtandaoni wajisajili TRA ili waanze kuchangia katika kulipa Kodi wakiwemo wenye nyumba wanaopangisha nyumba zao kutumia Air BNB na hawalipi kodi.

Amesema watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo la kujisajili ndani ya kipindi cha mwezi mmoja watachukuliwa hatua ikiwemo kutozwa faini maana hawajasamehewa kulipa kodi hiyo wakiwemo wale wanaouza vitu mbalimbali mtandaoni bila kulipa kodi kwani wanavunja sheria kwa kutokulipa kodi hiyo.

“Kuanzia Agosti Mosi tutakuwa na kampeni kubwa ya kuhakikisha kila anayefanya biashara ya kupangisha nyumba kupitia mtandao anasajiliwa na kulipa Kodi pamoja na watu wanaofanya biashara mtandaoni ambao kipato chao kinazidi Sh. 4,000,000 kwa mwaka nao watatakiwa kulipa Kodi na kila mmoja atalipa kutokana na kipato chake” amesema Mwenda.

Kamishna Mkuu Mwenda ametoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za watu wanaofanya biashara mtandaoni kuziwasilisha TRA na kuwa zipo njia nyingi za kuwabaini watu ambao hawalipi kodi hata k**a wanafanya biashara mtandaoni na risiti zitatolewa kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa VFD.

Amesema ufuatiliaji wa biashara mtandao utawezeshwa na mafunzo ambayo watumishi wa TRA wamepatiwa kwa ushirikiano na IBFD kwa udhamini wa Serikali ya Uholanzi na kubainisha kuwa makampuni yaliyowekeza nchini na kujihusisha na ukwepaji wa kodi yatafikiwa.

Mwenda amesema Serikali ya Tanzania imefungua milango ya uwekezaji ambapo makampuni mengi yanakuja kuwekeza hivyo yanao wajibu wa kulipa Kodi kwa Mujibu wa sheria.


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kulia), akimkabidhi tuzo ya shukrani Mkur...
24/07/2025

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kulia), akimkabidhi tuzo ya shukrani Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu na Utawala, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Paul Kijazi kufuatia PSSSF kuwa miongoni mwa taasisi wezeshi za mkutano mkuu wa kwanza wa Maafisa Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala (TAPA-HR) katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC jijini Arusha, Julai 24, 2025.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imefanikiwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2024/25 kwa asilimia ...
24/07/2025

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imefanikiwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2024/25 kwa asilimia 125.19 baada ya kukusanya jumla ya Shilingi bilioni 10.4 dhidi ya bajeti ya awali ya Shilingi bilioni 8.3. Hii ni zaidi ya Shilingi bilioni 2.1 kutoka makadirio ya awali.

‎Hatua hiyo imechangiwa na usimamizi madhubuti wa mapato ya ndani pamoja na udhibiti wa mianya ya upotevu, ambapo watendaji wa halmashauri waliweka msukumo mkubwa katika uadilifu na ubunifu wa vyanzo vya mapato.

‎Kupitia mafanikio ya ukusanyaji wa mapato, Halmashauri iliweza kutenga Shilingi bilioni 3.1 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta za elimu, afya, miundombinu na utawala.

‎Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa shule mpya, zahanati, vituo vya afya, nyumba za watumishi pamoja na ofisi za kata.

‎Aidha, kwa kutekeleza agizo la Serikali la kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo, Halmashauri ilitoa mikopo yenye thamani ya Shilingi bilioni 1.8 kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu waliokidhi vigezo, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuwawezesha kiuchumi.

‎Katika kuimarisha mapato ya siku zijazo, Halmashauri imeendelea kutwaa maeneo ya kimkakati kwa ajili ya uwekezaji.

‎Mnamo Julai 24, 2025, Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ilifanya ziara katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro kukagua maeneo yanayotarajiwa kutwaliwa kwa uwekezaji.

‎Miongoni mwa maeneo hayo ni eneo lenye ukubwa wa hekari 14 litakalotumika kwa ujenzi wa kituo cha mabasi (Katoro Bus Stand) pamoja na soko la Kariakoo Katoro, hatua ambayo inalenga kuboresha mazingira ya biashara na kuongeza mapato.

‎Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kutekeleza mikakati ya kuongeza mapato ya ndani ili kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi, huku ikiishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuipatia rasilimali na fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo.


Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amekabidhi Leseni ya Utafiti na Uchimbaji Mkubwa wa Madini Adimu na Muhimu ambayo...
24/07/2025

Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amekabidhi Leseni ya Utafiti na Uchimbaji Mkubwa wa Madini Adimu na Muhimu ambayo ni ya kimkakati ya Rare Earth Elements (REE) kwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), ikiwa ni hatua muhimu ya kuliwezesha shirika kuingia kwenye shughuli za uchimbaji mkubwa kwa lengo la kuwanufaisha wananchi wote wa Tanzania.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Julai 24, 2025 katika viwanja vya Shule ya Msingi Sesenga kijiji cha Sesenga Kata ya Mgazi Wilaya ya Morogoro, kufuatia uamuzi wa Serikali wa kuirejesha leseni hiyo kutoka kwa kampuni ya Wigu Hill Mining Company Limited baada ya kumalizika kwa shauri la madai kwenye Baraza la Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji(ICSID).

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara kwenye hafla ya makabidhiano ya leseni hiyo, Waziri Mavunde amesema kuwa madini ya Rare Earth Elements ni miongoni mwa madini ya kimkakati ambayo kwa sasa yanahitajika kwa kiwango kikubwa duniani kutokana na umuhimu wake katika sekta ya teknolojia ya kisasa.

"Madini haya yanatumika katika vifaa vya kivita, kutengeneza simu janja, kompyuta, betri za magari ya umeme, vifaa vya matibabu na mashine mbalimbali. Hii ni fursa adhimu kwa kijiji cha Sesenga, Wilaya ya Morogoro, Mkoa na Taifa kwa ujumla kunufaika na rasilimali hii muhimu," amesisitiza Waziri Mavunde.

Pia, Waziri Mavunde amebainisha kuwa mradi huo utafungua fursa nyingi za ajira kwa wakazi wa maeneo ya jirani na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kupewa kipaumbele kwa wananchi wanaozunguka mgodi kuuza bidhaa zao mgodini (Local content) na kupitia uwajibikaji wa kampuni kwa jamii (CSR).

Vilevile, ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro itaongeza mapato yake kupita tozo za huduma ambazo hutozwa kwenye shughuli za madini.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde ameitaka STAMICO kuanza mara moja mchakato wa uendelezaji wa leseni hiyo ili shughuli za uzalishaji madini hayo ziweze kuanza kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro M***a Kilakala amempongeza Waziri Mavunde kwa kuisimamia vizuri Sekta ya Madini na kumuahidi Waziri huyo kuendelea kusimamia sekta hiyo kwa karibu kwa ajili ya masilahi ya taifa.

Ulimwengu wa mieleka umempoteza mmoja wa magwiji wake, Hulk Hogan, ambaye ameripotiwa kufariki dunia akiwa na miaka 71 k...
24/07/2025

Ulimwengu wa mieleka umempoteza mmoja wa magwiji wake, Hulk Hogan, ambaye ameripotiwa kufariki dunia akiwa na miaka 71 kufuatia mshtuko wa moyo uliompata mapema siku ya leo Alhamisi July 24,2025 nyumbani kwake huko Florida.

Kwa mujibu wa taarifa za TMZ Sports, madaktari wa dharura walikimbilia nyumbani kwa Hogan katika mji wa Clearwater, ambapo walimtoa kwa machela na kumkimbiza hospitalini.

Kifo chake kinatokea wiki chache tu baada ya mke wake, Sky Hogan, kuwakanusha vikali waliokuwa wakidai kuwa nyota huyo alikuwa katika hali ya koma, akisisitiza kuwa alikuwa mwenye nguvu baada ya kufanyiwa upasuaji. Mwezi uliopita, vyanzo vya karibu vilieleza kuwa Hogan alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya shingo, yaliyotokana na majeraha ya zamani aliyopata wakati wa taaluma yake ndefu ya mieleka.

Hulk Hogan, ambaye jina lake halisi ni Terry Gene Bollea, alikuwa mmoja wa wacheza mieleka maarufu zaidi katika historia ya mieleka duniani, akiwahi kushinda mataji lukuki na kuvuma sana miaka ya 80 na 90 kupitia WWE. Alijulikana kwa maneno yake maarufu k**a "Whatcha gonna do when Hulk**ania runs wild on you?" na alikuwa kipenzi cha mashabiki kote duniani.

✍️|


Msanii wa Bongo Fleva Tanzania  amemjibu  baada ya msanii Billnass kuulizwa swali "ni kitu gani kilifanya yeye kutokuwa ...
24/07/2025

Msanii wa Bongo Fleva Tanzania amemjibu baada ya msanii Billnass kuulizwa swali "ni kitu gani kilifanya yeye kutokuwa na ukaribu na Nay, ambapo Billnass amejibu kwa kudai kuwa kuna tukio lilitokea Nay akawa anashinikiza kwa mamlaka husika ili yeye aende kufungwa jela 👉 3

Kupitia Video hiyo msanii Nay amekuja kwenye section na kutoa ujumbe unaosomeka hivi 👇 👉 2

"Msanii mjinga ambae amekua Anapenda trending kwa style yoyote ile aya Acha nikupe unachotaka Wewe ni mwizi ungeenda jela kwa tabia yako ya wizi. Nina kazi nyingi za kufanya nianze kukukandamiza wewe kwenda jela how yani.?! Mgande Nandy ivyo ivyo ili usije ukaendelea na udokozi.!!"

✍️

📹 Video Credit by


Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manara Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share