Manara Tv

Manara Tv For your Sports, Business, Politics, and Entertainment, with Breaking News in-depth analysis and Exclusive Interviews

11/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ameendelea na ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Kigamboni, ambapo leo alifika Kata ya Vijibweni kujionea changamoto ya ubovu wa barabara inayowakabili wakazi wa eneo hilo.

Akizungumza katika ziara hiyo, Chalamila alisema Serikali inatambua adha wanayopata wananchi na inaendelea kutafuta suluhisho la kudumu. Alieleza kuwa zaidi ya nyumba 300 zinatarajiwa kupisha ujenzi wa Barabara ya Soweto, huku akisisitiza kuwa zoezi hilo litafanyika kwa kuzingatia sheria, taratibu na maslahi ya wananchi.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa alimpa tahadhari mkandarasi wa mradi huo kuwa tayari kuanza utekelezaji mara baada ya mvua kupungua jijini Dar es Salaam. Alisema wananchi wamechoshwa na kuchelewa kwa mradi huo na hawatakuwa tayari kuvumilia ucheleweshaji zaidi.

Chalamila aliwataka wananchi kuwa na subira na kuendelea kuiamini Serikali, akiahidi kuwa maeneo yote yenye changamoto yatapatiwa ufumbuzi baada ya msimu wa mvua ili kuboresha huduma za usafiri na kuchochea maendeleo.

Kwa upande wao, wananchi wa eneo la Soweto walisema ubovu wa barabara hiyo umekuwa kero ya muda mrefu. Walidai kuwa mara nyingi matengenezo hufanyika kwa muda mfupi wakati wa ziara za viongozi, lakini husimama punde baada ya ziara hizo kumalizika.

11/06/2026

Mtengeneza maudhui maarufu Nchini Tanzania amefunguka kuwa siku zote alizokaa Nchini humo hakuna siku hata moja aliyosikia wimbo wa msanii wa Tanzania Nchini humo.

Full Video tumekuwekea YouTube Manara Tv


11/06/2026

Mipango yetu ilikua ni kumaliza mchezo kipindi cha kwanza wapinzani walibadilika baada ya sisi kufanya makosa lakini tumepita kwa mikwaju ya penati amesema Yohana Cipriano wa chuo cha Kampala

Shabani Mdoe kwa upande wa chuo cha IAA amesema mpango wako mwalimu aliwaambia wamsome mpinzani wakasawazisha lakini kwenye penati wametolewa

Amemshukuru mdhamini wa mashindano hayo Vunjabei kwa kuthamini na kuwekeza ili kuibua na kukuza vipaji


11/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ameagiza Jeshi la Polisi Wilaya ya Kigamboni kumk**ata kwa kumshikilia Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lingato, Kata ya Kisarawe II, Cosma Kulwa maarufu k**a Kalimanzira, kwa tuhuma za kuuza viwanja mara mbili na kusababisha migogoro ya ardhi kwa wakazi wa eneo hilo.

Chalamila alitoa agizo hilo leo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo, kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Wilaya ya Kigamboni.

Akiwa katika Mtaa wa Kichangani akitatua mgogoro wa ardhi unaohusisha zaidi ya familia 23 na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la Hassan alijitokeza na kutoa malalamiko dhidi ya mwenyekiti huyo, akimtuhumu kumuuzia eneo la ekari moja ambalo baadaye lilidaiwa kuuzwa kwa mtu mwingine.

Kwa mujibu wa madai yaliyotolewa na wananchi, mwenyekiti huyo amekuwa akihusishwa na uuzaji wa viwanja vyenye migogoro pamoja na viwanja ambavyo tayari vilikuwa vimeuzwa kwa wanunuzi wengine, hali inayodaiwa kuchangia kuongezeka kwa migogoro ya ardhi katika eneo hilo.

Baada ya kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusu nyaraka za mauziano zinazodaiwa kuhusika katika sakata hilo, Chalamila aliamuru ak**atwe mara moja na kuwekwa mahabusu.

"Ak**atwe na akawekwe mahabusu mpaka kesho. Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, kesho itisha mkutano wa hadhara wa wananchi. Huyu mwenyekiti kesho atoke mahabusu akiwa na pingu ahudhurie mkutano huo. Amesema Chalamila.

11/06/2026

"Kwa umri huu siwezi kukaa darasani eti najifunza kengereza hilo haliwezekani "Alisema Kiredio

🎤 | .Full interview tumekuwekea YouTube Manara Tv


11/06/2026

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Ally Hapi, amesema ni kosa kuwapotosha wananchi kuhusu majukumu ya Mbunge, akisisitiza kuwa Mbunge ni mwakilishi wa wananchi na mdau muhimu wa maendeleo katika jimbo lake, ndani na nje ya Bunge.

Hapi ametoa kauli hiyo baada ya kuwasili katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kondoa na kuzungumza na wanachama wa CCM waliojitokeza kumpokea katika ziara yake ya kikazi. Kauli hiyo imekuja kufuatia matamshi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, ambaye alidai kuwa si wajibu wa Mbunge kupeleka maendeleo kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Hapi, kauli hiyo ni upotoshaji unaoweza kuwachanganya wananchi kuhusu nafasi na wajibu wa viongozi wanaowachagua.

Amesema Mbunge anapaswa kuwa mstari wa mbele kusimamia, kufuatilia na kutetea miradi ya maendeleo pamoja na maslahi ya wananchi anaowawakilisha.

"Mbunge ni sauti ya wananchi na kiungo muhimu katika kuharakisha maendeleo ya eneo lake.

Kauli zinazopotosha kuhusu wajibu huo hazipaswi kuachwa zipite bila kujibiwa kwa hoja na ukweli," amesema Hapi.

Aidha, amewataka wanachama wa CCM kuendelea kujibu hoja za upinzani kwa kutumia ukweli, sheria na takwimu sahihi ili wananchi waendelee kupata taarifa sahihi kuhusu maendeleo na uongozi wa nchi.

11/06/2026

"Waigizaji tuache roho mbaya mtu akifanya kitu kizuri tumpongeze siyo lazima ufanye wewe,wengi wanapenda kumsifia mtu akishakufa" Alisema muigizaji

🎤 |


11/06/2026

Wakazi wa Mitaa ya Mazengo na Fire iliyopo kata ya Upanga Magharibi wamelaani vikali hatua zilizokuwa zimechukuliwa na baadhi wa kundi la wakazi kufunga barabara za mitaa hiyo ambazo zinatumiwa na wakazi, wanafunzi na hata vyombo vya moto kuelekea maeneo mbalimbali ya Upanga na kusema kuwa tukio hilo linaleta athari kubwa hasa kwa wanafunzi na wakazi kuhatarisha usalama wao pindi wanapotumia barabara kuu kufika mashuleni.

Hivi karibuni baadhi ya wakazi wa eneo hilo waliziba barabara kadhaa kwa mageti na kuleta adha kubwa kubwa wa wanafunzi na hata wagongwa kwani barabara za mitaa hiyo ambapo nyumba zake zinamilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa zimekuwa muhimu kwa zaidi ya miaka 23, kufuatia kwa kadhia iliyokuwa imejitokeza ilipelekea sintofahamu na kuvunjwa kwa mageti hayo jambo ambalo limefika kwa kwa mkuu wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo ambapo ameahidi kwenda kukutana na wakazi ili kutatua changamoto hiyo.


11/06/2026

Lucas ambae ni kapteni wa timu ya chuo cha MUHAS amesema walipofika ni hatua kubwa sababu msimu uliopita walitoka hatua za mwanzo,wapinzani walikuwa bora kila walipopata nafasi watajipanga wakati mwingine

Kwa upande wa chuo cha takwimu amezungumza Nurudin Rashid amesema haikua rahisi kwao kufika hapo na kusonga hatua ya robo fainali walijipanga na kurekebisha makosa yao ndio sababu ya ushindi huo

✍️


11/06/2026

Mtengeneza maudhui maarufu Nchini Tanzania amesema kuwa India hakuna mtu aliyemfahamu kuwa yeye ni maarufu Tanzania hata baadhi ya wahindi waliyoonekana wakimuomba picha waliomba kupiga nae picha sababu ya weusi wake.

Full interview tumekuwekea YouTube Manara Tv


Address

Kinondoni Biafra
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manara Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share