Manara Tv

Manara Tv For your Sports, Business, Politics, and Entertainment, with Breaking News in-depth analysis and Exclusive Interviews

Wananchi mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya huduma za afya, hatua ili...
13/08/2026

Wananchi mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya huduma za afya, hatua iliyowarahisishia upatikanaji wa huduma hizo bila kulazimika kusafiri umbali mrefu.

Hayo yamejiri Agosti 12, 2026, katika siku ya tatu ya ziara ya kikazi ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), mkoani humo, yenye lengo la kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita.

Wananchi hao wamesema wanapata huduma za afya kwa wakati na kwa urahisi, jambo walilolieleza kuwa limepunguza changamoto ya kufuata matibabu katika maeneo ya mbali.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Waziri Kapinga amesema Serikali inalenga kuboresha huduma za afya ili wananchi wapate matibabu kwa urahisi na kuendelea na shughuli zao za uzalishaji, hivyo kuimarisha uchumi wa familia na Taifa.

Amesema kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu kwa wakati.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa ushirikiano ni msingi wa maendeleo.

Ikiwa ni siku ya tatu ya ziara yake, Waziri Kapinga ametembelea miradi mbalimbali katika Majimbo ya Nanyamba, Mtwara Mjini na Mtwara Vijijini, ikiwemo kuzindua Kituo cha Afya Msangamkuu, kuzindua mabweni mawili na kutoa taulo za k**e kwa wanafunzi wa Shule ya Wasichana Mtwara, kukagua ujenzi wa Shule ya Amali Chikota, pamoja na kutembelea Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Tandahimba.

13/08/2026

MANTRA Tanzania imeadhimisha hatua nyingine muhimu katika Wilaya ya Namtumbo kwa kutoa Kadi 1,000 za Bima ya Afya ya NHIF kwa wanafunzi 1,000, ili kuwasaidia kupata huduma muhimu za afya huku wakiendelea na masomo yao.

Mkuu wa Wilaya, Ngollo Malenya, ndiye amekuwa Mgeni Rasmi, ambaye alikabidhi rasmi kadi hizo kwa wanafunzi.

Kwa upande wa MANTRA (MANTRA TANZANIA LIMITED ), kampuni iliwakilishwa na Meneja Uendelevu, Majani Moremi Wambura pamoja na Meneja Rasilimali Watu, Jerome Mashamba, wakithibitisha dhamira ya kuendelea kusaidia afya na ustawi wa jamii zinazowazunguka “Kwa sababu tunapowekeza katika afya ya vijana wetu, tunawekeza katika mustakabali wa taifa letu”

MANTRA Tanzania ni kampuni inayojishughulisha na shughuli za madini ya URANI nchini Tanzania, ikitekeleza shughuli zake katika Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma, kampuni imejikita katika uendeshaji wa shughuli zake kwa uwajibikaji sambamba na kuchangia maendeleo na ustawi wa jamii zinazozunguka maeneo yake ya kazi.

13/08/2026

Mdamo Masalu Nyalwisila mwenye miaka 40 ambae ni dereva na mkazi wa Bariadi mkoani Simiyu anashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Mwanza kwa kosa la kusababisha ajali kwa kushindwa kuchukua tahadhari katika maeneo yenye makazi ya watu na kumgonga mwanafunzi na kumsababishia kifo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Naibu kamishna Wilbrod Mutafungwa akitoa taarifa kwa waandishi wa Habari amesema tukio hilo limetokea Agosti nane mwaka huu 2026, majira ya saa tano asubuhi katika Kijiji na kata ya kisesa wilaya ya Magu, katika Barabara kuu ya Mwanza-Musoma dereva huyo akiwa na gari lenye namba za usajili T 885 ENK aina ya Scania mali ya kampuni ya Seedco Tanzania Limited likitokea Mwanza mjni kuelekea Bariadi mkoani Simiyu

Aodha kamanda Mutafungwa ameongeza kuwa gari hilo likiendesha na dereva Mdamo Masalu Nyalwisila lilimgonga mtembea kwa miguu aitwaye Prosper Yusuph Msafiri mwenye miaka saba na mwanafunzi wa darsa la kwanza aliyekuwa anavuka Barabara kutoka upande wa kulia Kwenda upande wa kushoto, baada ya kugongwa na gari hilo alifariki dunia

Jeshi la polisi limeendelea kutoa wito kwa madereva kuwa makini wanapoendesha vyombo vya moto hasa wanapopita kwenye maeneo ya makazi ya watu na kutakiwa kupunguza mwendo na kutakiwa kuzingatia alama za usalama barabarani wakati wote ili kuepuka ajali na vifo vinavyoweza kuepukika.

Mwanahabari Luqman Maloto amewaonya wasaidizi wa Rais Samia Suluhu Hassan wenye matarajio ya kuwania Urais mwaka 2030, a...
13/08/2026

Mwanahabari Luqman Maloto amewaonya wasaidizi wa Rais Samia Suluhu Hassan wenye matarajio ya kuwania Urais mwaka 2030, akiwataka kuzingatia majukumu yao ya sasa na kufanya kazi kwa uaminifu kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.

Katika makala yake, Maloto amewataja Makamu wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi na Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, akisema wanapaswa kumuunga mkono Rais Samia na kuhakikisha Serikali inatekeleza majukumu yake.

Amesema mazungumzo ya kuwahusisha viongozi hao na mbio za Urais 2030 yamekuwa yakisikika, ingawa hakuna kauli yao ya moja kwa moja kuthibitisha hilo.

Maloto ameonya kuwa tamaa ya Urais inaweza kusababisha baadhi ya viongozi kujenga makundi, kutofanya kazi kwa uaminifu au hata kutamani Serikali iliyopo ishindwe ili kujijengea mtaji wa kisiasa.

Amesisitiza kuwa viongozi wanapaswa kufanya kazi kwa uadilifu na kuacha muda uamue kuhusu hatima ya kisiasa, akisema utendaji mzuri wa sasa unaweza kuwa msingi wa kuaminika hapo baadaye.

“Wasaidizi wa Rais wafanye kazi badala ya kuutolea macho Urais,” amesema Maloto.

13/08/2026

Msanii wa R&B kutoka nchini Marekani Trey Songz alivyofika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Magonjwa ya Moyo JKCI


13/08/2026

APP INARAHISISHA MAMBO 📱

Simba wa Bahari tunaendelea kurahisisha huduma, Sasa unaweza kupakua Application ya Silent Ocean katika simu yako ya IOS & Android (App store, Google Store) na kujipatia huduma zetu kwa urahisi zaidi, simu ikiwa kiganjani mwako.

Ni Rahisi sana.. Pakua sasa! Silent Ocean Tanzania

Maelezo zaidi, tupigie namba hii;

+255 746 813 813



13/08/2026

Utafiti wa mradi wa Mifugo na Misitu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), pamoja na Chuo Kikuu cha Copenhagen kilichopo Nchini Denmark umebaini kuwa inawezekana shughuli za ufugaji, kilimo na uhifadhi wa misitu kufanyika kwa pamoja na kupunguza migogoro, endapo jamii zitashirikishwa katika kupanga na kusimamia matumizi ya rasilimali za ardhi.

Akizungumza wakati warsha ya wasilisho ya matokeo ya utafiti huo jijini Dodoma, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt Daniel Pangalasi aliyemwakilisha Waziri wa Maliasili na Utalii, amesema utafiti huo uliofanyika katika eneo la Msitu wa Suledo, Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, una umuhimu katika kuisaidia Serikali kupata ushahidi wa kisayansi wa namna shughuli za kiuchumi zinavyoweza kuendana na uhifadhi wa misitu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mradi wa Mifugo na Misitu, Profesa Jumanne Abdallah, amesema amesema katika utafiti huo wanafunzi watatu wa shahada ya uzamivu (PhD) walifanya tafiti katika maeneo tofauti, ikiwemo kuchunguza sera, sheria na mifumo inayohusiana na mifugo na misitu; mahusiano ya wafugaji na jamii wanapoingia katika misitu ya jamii; pamoja na athari za kimazingira zinazoweza kujitokeza kutokana na mifugo kutumia maeneo ya misitu.

Akizungumza katika kikao hicho, Profesa Japhet Kashaigili, Mwakilishi wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo manufaa hayo yanahusisha pia kuboresha kipato cha wakulima na wafugaji wanaotegemea rasilimali za ardhi, huku Mbunge wa Jimbo la Kiteto, Mhe. Edward Ole Lekaita, amesema tafiti za aina hiyo ni muhimu kwa wabunge na watunga sera kwa sababu zinatoa uelewa wa kisayansi kuhusu changamoto zinazozikabili jamii.

Kwa upande wake, Dkt. Salim Nandonde, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, amesema matokeo ya utafiti huo yametoa mwanga kuhusu namna ufugaji na uhifadhi wa mazingira unavyoweza kwenda sambamba.

13/08/2026

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo, Abdul Nondo, amesema Katiba mpya itajenga taasisi imara na kuweka mifumo madhubuti ya uwajibikaji kwa viongozi na watumishi wa umma.

Nondo amesema kupitia Katiba mpya, viongozi watawajibika kwa wananchi, huku taasisi za umma zikiwa na uwezo wa kufanya kazi kwa uhuru na kulinda haki za wananchi.

Amesema hayo Agosti 12, 2026, katika Kongamano la Siku ya Vijana Duniani lililoandaliwa na Ngome ya Vijana ACT Wazalendo katika Ukumbi wa Mrina Hall, Manzese, Dar es Salaam.

13/08/2026

Kijana anayefahamika kwa jina la Sefu Musa amefariki dunia baada ya kudaiwa kupigwa na askari katika eneo la Ngorongoro, mkoani Arusha, kufuatia tuhuma za kuhusishwa na ujambazi.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa, Sefu alikuwa pamoja na Salim Hamisi maarufu Pachaa na Abdallah Nuru, wakisafiri kutoka Arusha kuelekea Babati, Manyara, kwa ajili ya mazishi ya mwenzao. Inadaiwa walipotea njia na kuishia Karatu kupitia Makuyuni.

Vijana hao walidaiwa kufika katika lango la Ngorongoro, ambako walidaiwa kuhojiwa na kutuhumiwa kuwa majangili licha ya kueleza kuwa walipotea njia. Inadaiwa walifanyiwa ukatili na baadaye kuondolewa eneo hilo.

Abdallah Nuru anadaiwa kuwapeleka wenzake hospitalini baada ya hali ya Sefu na Salim kuwa mbaya. Walipofikishwa Hospitali ya Lutheran Karatu, Sefu alikutwa tayari amefariki dunia, huku Salim akiwa katika hali mbaya na kupewa huduma ya oksijeni.

Abdallah anaendelea kupatiwa matibabu, huku mwili wa Sefu ukiwa umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.

Address

Kinondoni Biafra
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manara Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share