Manara Tv

Manara Tv For your Sports, Business, Politics, and Entertainment, with Breaking News in-depth analysis and Exclusive Interviews

Habari zilizojiri kupitia kurasa za mbele za Magazeti leo Jumapili ya tarehe 14/12/2025
14/12/2025

Habari zilizojiri kupitia kurasa za mbele za Magazeti leo Jumapili ya tarehe 14/12/2025


Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa limethibitisha kumk**ata Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Mufindi, anaye...
13/12/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa limethibitisha kumk**ata Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Mufindi, anayefahamika kwa namba ya kazi WP.8402, Koplo Bikusekela, kufuatia kusambaa kwa video katika mitandao ya kijamii ikimuonesha akifanya kitendo kibaya na cha utovu wa nidhamu akiwa kazini.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Jeshi la Polisi, Askari huyo tayari amechukuliwa hatua kali za kinidhamu kutokana na tukio hilo, ambalo limekosolewa vikali na uongozi wa Jeshi hilo.

Jeshi la Polisi limesisitiza kuwa haliridhishwi kabisa na vitendo vya Askari wanaokiuka maadili, sheria na nidhamu ya kazi.

Aidha, limeonya kuwa halitasita kuchukua hatua kali za kisheria na kinidhamu dhidi ya Askari yeyote atakayebainika kufanya vitendo vinavyochafua taswira ya Jeshi la Polisi na Serikali kwa ujumla.

MWalipakodi nchini wametakiwa kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi ya mapato awamu ya nne na kuwasilisha ritani za kodi ya...
13/12/2025

MWalipakodi nchini wametakiwa kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi ya mapato awamu ya nne na kuwasilisha ritani za kodi ya ongezeko la thamani kwa wakati ili wamalize mwaka 2025 bila madeni ya kodi hali ambayo itawaepushia riba na adhabu.

Rai hiyo imetolewa Desemba 12.2025 na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Juma Mwenda alipokutana na kufanya mazungumzo na Mawakala wa Forodha na Washauri wa Kodi Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kikao hicho Kamishna Mkuu amesema kila mmoja anao wajibu wa kulipa kodi na kuisaidia nchi kujitegemea kwa mapato kwa kulipa kodi kwa wakati na kwa hiari.

Kamishna Mkuu amesema Washauri wa Kodi na Mawakala wa Forodha wanaowajibu wa kuwahimiza walipakodi wanaowahudumia kufuata sheria na kuwashauri kutokukwepa kodi kwani wakibainika watakutana na mkono wa sheria.

"Tunajua upo ukwepaji kodi unaofanyika kwa namna mbalimbali ikiwemo kufanya magendo, kutokutoa risiti za mauzo, kufanya makadirio ya uongo na njia nyingine nyingi ambazo mnazijua hivyo tunawaomba muisaidie nchi kwa kufichua ukwepaji kodi" amesema Mwenda.

Amesema vutendo vya ukwepaji kodi vinapunguza ushindani wa biashara sokoni na imani ya walipakodi wazuri hivyo hali ambayo inaendelea kupunguza wigo wa kodi.

Amesema TRA imejipanga kuongeza wigo wa kodi kwa kuongeza mapambano dhidi ya wakwepaji wa kodi na kuzuia kufanyika kwa magendo.

Kwa upande wake Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFFA) Bw. Edward Urio ametoa wito kwa walipakodi kufuata sheria za kodi kwa kutimiza wajibu wao wa kukamilisha mwaka wa kalenda bila madeni ya kodi na kuipongeza TRA kwa kuendelea kuboresha huduma kwa Walipakodi.

Urio amesema kwa Mawakala wa Forodha majukumu yao yamerahisishwa kupitia mfumo wa TANCIS ulioboreshwa ambao umekuwa ukiwarahisishia uondoshaji wa mizigo kutokana na kufanya taratibu zote kupitia mtandao.

Naye mwakilishi wa Washauri wa Kodi Bi. Victoria Soka amesema wao k**a Washauri wa Kodi watakwenda kutimiza wajibu wao kwa kuwashauri wateja wanaowahudumia watimize wajibu wao kwa wakati ili kuisaidia nchi kujitegemea.

13/12/2025

Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmassy, amesema changamoto ya upatikanaji wa maji inayojitokeza Dar es Salaam inatokana na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri maeneo mbalimbali na kusababisha kupungua kwa vyanzo vya I maji.

Akizungumza kuhusu hali hiyo, Mhandisi Mmassy amesema bodi hiyo imechukua hatua mbalimbali kukabiliana na tatizo hilo, ikiwemo kusitisha utoaji wa vibali kwa watumiaji wa skimu za umwagiliaji katika Mto Ruvu wakati wa kipindi cha kiangazi.

Amesema hatua hiyo inalenga kuongeza matumizi na kulinda wingi wa maji ili kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji kwa wananchi wa Dar es Salaam na maeneo mengine yanayohudumiwa na Mto Ruvu.

13/12/2025

Mwananchi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Ally Pazuri, mkazi wa Magomeni jijini Dar es Salaam, ameeleza kufurahishwa kwake na hali ya utulivu na amani iliyoshuhudiwa nchini katika siku ya Disemba 9.

Ally Pazuri amesema ameshangazwa na kiwango cha amani na utulivu kilichokuwepo siku hiyo, akieleza kuwa hali hiyo inaakisi Tanzania ambayo wananchi wengi wanaitamani.

Aidha, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Vyombo vya Ulinzi na Usalama, kwa jitihada zao katika kulinda amani na kudumisha utulivu nchini.

Katika maoni yake, Ally ametoa wito kwa Watanzania wote kuendelea kudumisha amani, akisisitiza kuwa amani ni sehemu ya utamaduni wa Mtanzania na msingi muhimu wa maendeleo ya taifa.

Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Ado Shaibu amechangia Shilingi Milioni tatu katika harambee ya ujenzi wa Bwal...
13/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Ndugu Ado Shaibu amechangia Shilingi Milioni tatu katika harambee ya ujenzi wa Bwalo la Chakula na Ofisi ya Utawala katika Shule ya Msingi Jamhuri iliyopo Wilayani Tunduru.

Ndugu Ado ametoa mchango huo kwenye harambee ya wazazi iliyofanyika shuleni hapo leo tarehe 13 Desemba 2025 ambapo yeye alikuwa mgeni rasmi. Jumla ya Tsh. Milioni Sita na vifaa mbalimbali k**a vile Simenti, mchanga na kokoto vilichangwa.

Shule ya Jamhuri imeshika nafasi ya pili kwa ufaulu katika Wilaya ya Tunduru na ya kwanza katika Jimbo la Tunduru Kaskazini katika Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba. Ndugu Ado amekubali ombi la uongozi wa shule hiyo kuwa mlezi wake katika kukabiliana na changamoto zake ili itimize lengo lake la kuongeza ziadi ufaulu.

Katika hotuba yake, Ndugu Ado amewapongeza wazazi na wadau waliochangia kwa harambee hiyo na kuahidi kuwa harambee hiyo itakuwa endelevu ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika. Ndugu Ado ameahidi kuwashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo ndani na nje ya Tunduru ili kuichangia zaidi shule ya Jamhuri.




13/12/2025

Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, ametembelea mradi wa Umwagiliaji uliopo wilayani Masasi mkoani Mtwara ikiwa moja ya muendelezo wa ziara kwa Taasisi za Wizara ya kilimo ambapo amewahakikishia wananchi kuwa Serikali itakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima.

Serikali itahakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima hali itakayoimarisha uchumi na kuleta uhakika wa chakula.

Mhe. Chongolo amesema hayo wakati wa ziara yake katika mradi huo unaotekelezwa eneo la Ndanda, mkoani Mtwara.

Mradi huo unahusisha ujenzi wa bwawa la Umwagiliaji na uchimbaji wa mifereji mirefu, na ukikamilika unatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakulima 700 kutoka vijiji saba.

"Serikali itahakikisha miradi yote ya Umwagiliaji inakamilika na kuleta tija kwa wakulima hali itakayoimarisha uchumi na kuleta uhakika wa chakula, amesisitiza.

Amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa bwawa hilo ambalo litachochea matumaini mapya kwa wakulima wa Mtwara kwa kuwawezesha kulima mazao mbalimbali ikiwemo mboga mboga, mpunga, mahindi na mazao mengineyo.

Ameongeza kuwa ingawa Mtwara inasifika kwa kilimo cha korosho, serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imeanzisha miradi ya Umwagiliaji katika mikoa ya Lindi na Mtwara ili kuhamasisha uzalishaji wa mazao mengine ndani ya mikoa hiyo bila kutegemea mazao kutoka maeneo mengine.

Aidha, Mhe. Chongolo ameisihi Tume kusimamia kwa umakini miradi hiyo ili kuhakikisha thamani ya fedha iliyowekezwa inaonekana na wakulima wanapata uzalishaji unaoendana na viwango vinavyotakiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) Bw. Raymond Mndolwa, amesema serikali imewekeza na inaendelea kuwekeza fedha nyingi kuhakikisha wananchi wa Lindi na Mtwara wananufaika na miradi ya Umwagiliaji, hatua ambayo itawawezesha kufanya kilimo cha uhakika bila kutegemea mvua.


13/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini ameishukuru Serikali kwa ujenzi wa daraja la Nsungwe lenye thamani ya Shilingi bilioni 9.5 linalojengwa katika Kata ya Bonde la Songwe, Wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya huku akifikisha ombi la wananchi wa Jimbo hilo la kujengewa barabara muhimu kwa kiwango cha lami.

Shukrani hizo amezitoa jana Disemba 12, 2025 wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Ujenzi, Mh. Abdallah Ulega, aliyefika wilayani Mbeya kukagua na kujionea utekelezaji wa miradi ya miundombinu. Mbunge Patali amesema daraja hilo litamaliza changamoto ya mafuriko yaliyokuwa yakiwakumba wananchi nyakati za masika kutokana na kuwepo kwa daraja dogo la awali.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Patali ametumia fursa hiyo kumuomba Waziri Ulega kuanza ujenzi wa barabara mbili muhimu kwa kiwango cha lami ndani ya jimbo hilo ambazo ni barabara ya Mbalizi–Shigamba yenye urefu wa kilomita 52 na barabara ya Isyonje–Kikondo yenye urefu wa kilomita 22.

Aidha, ameongeza umuhimu wa kujengwa kwa barabara ya kilomita 35 kutoka Bonde la Songwe kwenda Isuto (Umalila), akibainisha kuwa eneo hilo ni mzalishaji mkubwa wa mazao ya kilimo na mradi huo pia umo katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030.

Kwa upande wake, Mbunge Patali pia amempongeza Waziri Ulega kwa kumleta Mkandarasi Bishanga mkoani Mbeya ambapo kwa sasa ndie Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mbeya, akisema amekuwa mstari wa mbele katika kutoa ushirikiano mzuri unaochochea kasi ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu mkoani Mbeya.

cc.

✍🏼

Kiungo wa ulinzi wa kikosi cha timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ Alphonce Mabula ameisaidia klabu yake ya Shamakhi ku...
13/12/2025

Kiungo wa ulinzi wa kikosi cha timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ Alphonce Mabula ameisaidia klabu yake ya Shamakhi kufunga bao na kutoa pasi ya bao katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Zire.

Alphonce anayechezea Ligi Kuu ya Azberjain , baada ya kumalizika mchezo huo anatarajiwa kujiunga na kambi ya kikosi cha Taifa Stars nchini Misri kwa ajili ya kujiandaa na Mashindano ya AFCON, 2025.


Chama Kikuu cha Ushirika cha MAMCU mkoani Mtwara, kinachohudumia wakulima wa Halmashauri za Manispaa ya Mtwara Mikindani...
13/12/2025

Chama Kikuu cha Ushirika cha MAMCU mkoani Mtwara, kinachohudumia wakulima wa Halmashauri za Manispaa ya Mtwara Mikindani, Mtwara Vijijini, Masasi, Nanyumbu na Namanyamba, kimefanikiwa kuuza tani 108,000 za korosho kupitia minada minne ya msimu mpya wa mauzo wa mwaka 2025.

Akizungumza wakati wa mnada wa tano wa korosho uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mwenyekiti wa MAMCU, Ndugu Azam Julajula, amesema mafanikio hayo yamepatikana baada ya wakulima kuridhika na bei zilizopatikana kutoka kwa wanunuzi.

Amesema katika mnada huo wa tano, bei ya juu ilikuwa shilingi 2,550 kwa kilo huku bei ya chini ikiwa shilingi 2,110 kwa kilo. Ameongeza kuwa korosho zote zilizoingizwa sokoni zilipata wanunuzi, ambapo kilo 8,064,160 zilikuwa korosho za daraja la kwanza na kilo 2,274 zilikuwa korosho za daraja la pili.

Kwa upande mwingine, wakulima wameipongeza Serikali kwa usimamizi mzuri wa mauzo ya korosho katika msimu mpya wa 2025 pamoja na kulipa malipo yao kwa wakati. Pia wameaswa kutumia fedha wanazopata kutokana na mauzo ya korosho kwa maendeleo yao binafsi, ikiwemo kuboresha mashamba na kusomesha watoto wao.

Aidha, wakulima wameendelea kutoa pongezi kwa Serikali kwa kuimarisha usimamizi wa minada ya mazao mbalimbali ikiwemo korosho, ufuta na mbaazi kupitia mfumo wa mauzo wa TMX, wakieleza kuwa mfumo huo ni wazi na unawawezesha wakulima kufuatilia mwenendo wa minada kwa karibu.


13/12/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemtaja marehemu Jenista Mhagama kuwa kiongozi jasiri, mlezi wa wengi na nguzo muhimu ya matumaini kwa wanawake na vijana, aliyetoa mchango wa kipekee katika Bunge, Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza leo Desemba 13, 2025 katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma, Rais Samia amesema ni vigumu kupata maneno ya kuelezea msiba mzito wa kiongozi aliyegusa maisha ya watu wengi k**a marehemu Mhagama, akibainisha kuwa taifa limepoteza mtumishi wa umma aliyekuwa mfano wa uadilifu, nidhamu na hofu ya Mungu.

Rais Samia amewashukuru viongozi wa dini kwa maombi na misa tangu kutokea kwa msiba huo hadi siku ya kuuaga mwili wa marehemu, pamoja na watu wote walioshiriki kwa namna mbalimbali kushughulikia msiba na kumsitiri marehemu kwa heshima kubwa.

Akizungumzia maisha ya marehemu, Rais Samia amesema Jenista Mhagama alikuwa kiongozi aliyesimama imara kutetea haki, maendeleo na usawa wa watu aliowaongoza, si tu katika jimbo lake la Peramiho bali pia katika ngazi ya taifa. Amesema uongozi wake uliwapa matumaini makubwa wanawake na vijana, huku akionesha mfano wa uongozi uliotawaliwa na misingi ya maadili na hofu ya Mungu.

Akimtaja marehemu k**a mwalimu kwa taaluma na kwa uongozi, Rais Samia amesema Jenista alitumia kipawa chake cha ualimu kulea na kusimamia wabunge na mawaziri, hususan alipokuwa akihudumu k**a Mnadhimu wa Serikali Bungeni, Katibu wa Kamati ya Wabunge wa CCM na Mwenyekiti wa Wabunge wa chama hicho.

Tukio la kuuaga mwili wa marehemu Jenista Mhagama limefanyika sambamba na Misa Takatifu, likihudhuriwa na viongozi wa Serikali, wabunge, ndugu, jamaa na waombolezaji mbalimbali waliokusanyika kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho.

13/12/2025

Taarifa kutoka nchini Congo DR zinathibitisha kuwa mchezaji Chico Ushindi ambaye alikuwa mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC amefariki dunia.

Kupitia Vyombo mbalimbali vya Habari kutoka nchini humo akiwemo Molfino Tshalumuna ambaye ni Mwanahabari vimethibitisha taarifa hii.

Mpaka umauti unamkuta Chiko alikuwa anaichezea klabu ya Bazano inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini humo.


Address

Salamanda Tower
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Manara Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share