SPARK LIGHT TV

SPARK LIGHT  TV Kwa Habari zote kali za Ndani na Nje ya Nchi,Uchumi ,Biashara ,Burudani na Michezo

29/05/2026

MICHEZO : Msemaji wa timu zote za Taifa
akieleza namna ambavyo anaichungulia kombe la Dunia kwa miaka minne ijayo.

28/05/2026

Familia ya kijana aliyejirusha chini ya lori kwenye Daraja la Kijazi, Ubungo, Mei 26, 2026, imeomba msaada wa kifedha ili kuwezesha gharama za hospitali, usafirishaji wa mwili na mazishi ya marehemu.

Akizungumza na Mwandishi wa habari Godfrey Mwita, shemeji wa marehemu,amesema familia hiyo haimudu gharama za kulipa bili ya Hospitali ya Mwananyamala, kumsafirisha mama wa kijana huyo, pamoja na gharama zote za mazishi

Familia imetoa wito kwa yeyote atakayeguswa na hali hiyo kuchangia chochote.

Fedha hizo zitatumwa kwa kaka wa marehemu kupitia :

Namba: 0799250108
Jina: BONIFACE NTABUTU

Familia imesema kila mchango utasaidia kupunguza mzigo ilionao wakati huu mgumu.

28/05/2026

Shirika la MSI Tanzania limeianzisha Tuzo ya Uandishi wa Habari za Afya ya Uzazi ndani ya Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2025, kwa lengo la kuhamasisha uandishi wa habari wenye manufaa kwa jamii.

Akizungumza Mei 28, 2026, Katibu Mtendaji wa MCT, Ernest Sungura amesema makundi mapya ya tuzo hizo yanalenga kuendana na mabadiliko ya sekta ya habari, ikiwemo habari za kidijitali na uchunguzi.

Kwa upande wake Jaji na Katibu wa jopo la majaji wa EJAT, Mwanzo Millinga amesema waandishi na vyombo vya habari vilivyoingia hatua ya mwisho vimechaguliwa kwa kuzingatia vigezo 10, ikiwemo uwezo wa habari kugusa jamii na kuleta mabadiliko chanya.

Mkurugenzi Mkazi wa MSI Tanzania, Patrick Kinemo amesema taasisi hiyo inaamini vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kutoa elimu sahihi ya afya ya uzazi kwa jamii.

Washindi wa EJAT 2025 wanatarajiwa kutangazwa Mei 29 katika hafla itakayofanyika Hoteli ya Four Points by Sheraton, Dar es Salaam.

28/05/2026

Benki ya CRDB, imesaini makubaliano ya kudhamini mashindano ya vipaji ya Bongo star Search (BSS), kwa misimu mitatu mfululilo, huku wakiahidi kutoa shilingi milioni 30, kwa washindi wa mwaka 2026.

Akiongea na waandishi wa habari Mkuu wa wateja binafsi wa Benki ya CRDB, Steven Adili amesema, wameingia makubaliano hayo ili kuunga mkono vipaji vya vijana ambavyo kupitia wao vinazalisha ajira nyingi kwenye jamii.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa mashindano ya BSS, Rita Paulsen, amesema CRDB kuingia kwenye mashindano hayo kutaongeza wigo wa kuwafikia watu wengi zaidi huenda wakaongeza na mikoa ya kufanya usaili kwenye misimu ijayo

28/05/2026

WAZIRI MAKONDA AMTEUA HAJI MANARA KUWA MSEMAJI WA TIMU ZA TAIFA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetambuliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) k**a miongoni mwa sekta wezeshi...
27/05/2026

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetambuliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) k**a miongoni mwa sekta wezeshi zinazochangia maendeleo ya elimu jumuishi na ustawi wa wanafunzi chuoni hapo.

Utambuzi huo umetolewa Mei 26, 2026, wakati wa hafla maalum ya kuwatambua na kuwapongeza wadau wa maendeleo wa chuo hicho iliyofanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, amesema mchango wa wadau mbalimbali wakiwemo TANESCO una mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na maendeleo ya kitaaluma kwa wanafunzi.

“Tunapowasaidia wanafunzi hawa, hatuwafanyii fadhila. Tunathibitisha uwezo wao, utu wao na nafasi yao halali katika elimu ya juu,” amesema Dkt. Kikwete.

Aidha, ameshukuru wadau wote wa maendeleo kwa kuendelea kushirikiana na chuo hicho katika kuhakikisha upatikanaji wa elimu jumuishi kwa wanafunzi wote, wakiwemo wenye mahitaji maalum.

Kwa upande wa TANESCO, cheti hicho cha utambuzi na pongezi kilipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Irene Gowelle, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Lazaro Twange.

Utambuzi huo umetolewa ikiwa ni ishara ya kuthamini mchango wa TANESCO katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kujisomea kwa wanafunzi pamoja na wakufunzi wenye changamoto mbalimbali za ulemavu na mahitaji maalumu chuoni hapo.

27/05/2026

Familia ya aliyekuwa Mkurugenzi wa kiwanda cha kurejesha bidhaa za plastiki cha Xin Lin, Baozhang Ge (50), mke, mtoto, kaka pamoja na Mjomba tayari imesafiri kuelekea nchini China kwa ajili ya Mazishi ya ndugu yao aliyeuawa Mei 16,2026 na watu wanaodaiwa kuwa ni walinzi wa kiwanda chake Mabibo jijini Dar es salaam

Akiongea na Spark Light tv, mdogo wa marehemu Denis Jerry, anasema Leo wanasafiri kuelekea China kwa ajili ya maziko ya majivu ya mwili wa kaka yake yaliyochomwa Mei 24,202

Jerry amesema wakimaliza maziko atarejea Tanzania kwa ajili ya kufatilia Kesi ya kaka yake ili haki iweze kupatikana.

27/05/2026

Dereva wa gari kubwa Alexa jinsi amnavyo ajali ilitokea juu ya daraja la KIJAZI Ubungo ,boda adaiwa kukanyagwa
kichwani na kufariki.

26/05/2026

HABARI: Mtu mmoja anayedaiwa kuwa dereva wa bodaboda, amefariki dunia baada ya kujirusha kwenye lori lililokuwa kwenye mwendo kasi katika eneo la Daraja la Kijazi, Ubungo jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, kijana huyo alionekana akiwa anazungumza kwenye simu kabla ya ghafla kuivunja simu hiyo na kujitupa mbele ya lori lililokuwa likipita eneo hilo.

Tukio hilo limesababisha taharuki na huzuni kwa wananchi waliokuwepo eneo la tukio huku chanzo cha hatua hiyo kikibaki hakijafahamika mara moja.

Jitihada za kulipata Jeshi la Polisi zinaendelea ili kuthibitisha tukio hilo na kutoa taarifa rasmi kuhusu kilichotokea.

Kijana mmoja ambaye alivutia hisia za Wakenya wengi baada ya kupita ulinzi na kumkumbatia Rais William Ruto akiwa ameshi...
26/05/2026

Kijana mmoja ambaye alivutia hisia za Wakenya wengi baada ya kupita ulinzi na kumkumbatia Rais William Ruto akiwa ameshika Biblia, sasa amepewa kazi katika Kenya Ports Authority (KPA).

Tukio hilo lilitokea katika kaunti ya Kilifi wakati Rais Ruto alipokuwa akihudhuria sherehe ya kumshukuru Principal Secretary wa Wizara ya Vijana, Fikirini Jacobs. Kijana huyo aliyekuwa amebeba Biblia yenye CV yake ndani, alifanikiwa kumfikia Rais na kueleza kuwa alikuwa ametafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio.

“Niliamua kufanya hivi ili Rais anisikilize na anisaidie kupata kazi,” alisema kijana huyo baada ya tukio hilo.

Rais Ruto aliwaagiza walinzi wake wasimdhuru kijana huyo na kusikiliza ombi lake, huku akisema, “Huyu kijana ana ujasiri, tutamsaidia.”

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyanzo vya serikali pamoja na picha zilizosambazwa mtandaoni, kijana huyo sasa amepewa nafasi ya kazi katika Kenya Ports Authority (KPA), hatua iliyowafurahisha wengi mitandaoni waliokuwa wakifuatilia simulizi yake.

Wakenya wengi sasa wanamuita “Kijana wa Biblia” kutokana na tukio hilo lililogusa hisia za wengi.

26/05/2026

HABARI, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad M***a Salum, amekosoa vikali muswada uliowasilishwa na Maseneta wawili wa Marekani, akidai kuwa hatua hiyo huenda ikachochewa na wivu dhidi ya Tanzania kufuatia namna nchi ilivyoweza kuvuka salama kipindi cha matukio ya Oktoba 29, 2025.

Kauli hiyo imekuja baada ya Maseneta wa Marekani, Jeanne Shaheen na Ted Cruz, kuwasilisha muswada katika Baraza la Seneti la Marekani wakitaka kupitia upya uhusiano kati ya Marekani na Tanzania. Katika muswada huo, wameeleza wasiwasi wao kuhusu hali ya demokrasia, haki za binadamu pamoja na madai ya ukandamizaji wa kisiasa na kidini nchini Tanzania.

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
45180

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SPARK LIGHT TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SPARK LIGHT TV:

Share