Pastor Elisha Tetemeko

Pastor Elisha Tetemeko Senior pastor and Truth Ministries International (GTMI) Church
Dar es salaam, Tanzania

UNAYE KATA TAMAA,  SIKIA HILI.Yakukufanya ukate tamaa ni mengi. Uache kuendelea na hilo jambo ni mengi.Umkasirikie Mungu...
10/02/2025

UNAYE KATA TAMAA, SIKIA HILI.

Yakukufanya ukate tamaa ni mengi.

Uache kuendelea na hilo jambo ni mengi.
Umkasirikie Mungu kwa kuacha au kuchelewa kukufanyia ulichokuwa umemuomba.

Yakuamua kujiua nayo yapo mengi.

LAKINI PIA
Yapo Mengi mazuri ya kukufanya Uendelee mbele.

Ambayo Mungu amekufanyia toka utoto wako mpaka hapo ulipo ni mengi.

Ambayo watu wamekufanyia toka utoto wako, hapo ulipo ni mikono ya watu wengi imehusika kufika wewe hapo.

Wala siyo mkono wa mtu moja, usijindaganye.

Kumbuka: hili kila siku.

Wewe ni mti, ulio kwenye udongo.
Mazuri yote yanayo tokea kwenye mti kuna visababisho vingi sana.
Ambavyo ni jua, maji, mbolea nk.

Vyote hivyo vinapochaganyikana ndipo mambo mazuri yanatokea kwenye huo mti.

Na mtu anapatwa na mambo mengi ya kuumiza hayo yote ni maji, jua na mbolea (takataka). -Yote yanayo kutokea ni mbolea.

KUMBUKA LINGINE HILI
Kule uliko toka siyo kwako tena, kwako ni huko mbele , lakini na hapo ulipo (kwenye hali uliyo nayo) unatakiwa kutoka maana hicho ni kituo cha wewe kufika kwenye hatma yako.

Hata k**a umebaki na fimbo tu vipige vikwazo uendelee mbele.

Hata k**a umejaa ukoma, nyanyua miguu yako piga hatua mbele.

La mwisho la Kumbuka ni hili.

Kukata tamaa, kumkasirikia Mungu, kujiua, kuacha wokovu au utumishi, kurudi nyuma kwa sababu zozote unazo ziona hakuna kitakacho badilika.

Sana sana utaangukia kwenye chuma cha moto.
Wapo watu waliwahi kufanya huo ujinga lakini waliongeza matatizo zaidi.

Soma kitabu cha Yona sura ya nne yote.

Mungu haendeshwi, hatawaliwi, wala hafanyi kila tunalo litaka anafanya matakwa yake.

Ukiweza soma Wafalme wa kwanza sura ya kumi na tisa utakutana na mtu wa Mungu Eliya naye alikutana vipindi vya kukatisha tamaa lakini Mungu alimwambia ainuke ale na safari iendelee.

Hata wewe ujue safari bado inaendelea.
Kiti chako cha ukuu bado kinakusubiri, na walioandaliwa kukushangilia nao bado wanakusubiri.

Piga hatua mwanaume, mwanamke hata k**a kwa kujivuta, kutambaa, kukimbia au kupaa cha msingi tu ufike.

Usitumie siku za wanadamu, (siku za wanadamu jumatatu mpaka jumapili yaani kuhesabu siku) utazidi kukata tamaa.

Tumia siku za Mungu haziwahi wala hazichelewi. Mungu anasiku yake aliyoiandaa kwa ajili yako.

Neema na Amani ya Yesu Kristo iwe nawe, Amina.

Shalom!!





Asante sana kwa kuja KUABUDU Nasi.Mungu akubariki sana.
09/02/2025

Asante sana kwa kuja KUABUDU Nasi.

Mungu akubariki sana.

KIFUNGO CHA CHUKI >>Chuki ni shimo lefu sana kwenda chini na pia ni ukuta unaozuia watu kumfikia Mungu >>Chuki ni ukuta ...
09/02/2025

KIFUNGO CHA CHUKI

>>Chuki ni shimo lefu sana kwenda chini na pia ni ukuta unaozuia watu kumfikia Mungu
>>Chuki ni ukuta unaowazuia watu wengi washindwe kumfikia Mungu. Shimo hili la chuki linalowazuia watu wasifike kwa Mungu.Ni ukuta unaowatenganisha watu na Mungu.
*Luka 16:26

>>Chuki ni shimo linaloweka uadui kati ya watu wawili,na chuki pia hufanya tutengane na Mungu.
>>Chuki ni kifungo kizito kinachoweza kumeza hata watu wa kwenu kwasababu ya chuki
*Chukulia mfano wa Yusuph alikuwa ni mtu ambaye hakuwa na roho au kifungo cha chuki ila ndugu zake walikuwa na kifungo cha chuki juu ndugu yao.
Mwanzo 45:15

>>Ilipo chuki lazima uchungu itakuwepo na ilipo uchungu lazima chuki itakuwepo na haya huwa pamoja mda wote.
Waefeso 4:26-31

>>Ili uweze kufanikiwa inabidi ishughulikie na kifungo cha hasira,chuki,wivu,uchungu,manung'uniko hata k**a utakuwa umekwaza sana.
>>Kwenye huu dunia huwezi ishi bila kuumizwa usipoumuzwa jua hauishii duniani vizuri.
>>Lazima ufanye kuwa na upendo huwezi vikao ukuta wa kifungo cha chuki.

MADHARA YA CHUKI
1.Kuwatia watu kwenye mikono ya adui
2.Ni kupigwa kila mara
Zaburi 89:23
>>Upendo unatupatanisha,upendo unaleta baraka,upendo unaleta Neema
1 Petro 2:8-11

>>Yeyote anayetembea na chuki yupo gizani hayupo nuruni.
>>Mtu mwenye chuki ni rahisi sana kuua,ni rahisi sana kumtengenezea mwingine mabaya.jisikie vibaya kukaa na chuki duniani.

Shalom!!





SUNDAY OF MIRACLES!!Praise and Worship 🎶"It is a good thing to give Thanks unto the Lord And to sing Praises to Thy Name...
09/02/2025

SUNDAY OF MIRACLES!!

Praise and Worship 🎶
"It is a good thing to give Thanks unto the Lord And to sing Praises to Thy Name Oh Most High! " Psalm 92:1




SUNDAY OF MIRACLES !!Karibu sana kwenye Ibada ya leo bado ujachelewa na sasa ibada imefunguliwa kwa Maombi.Mahali: Mbuyu...
09/02/2025

SUNDAY OF MIRACLES !!

Karibu sana kwenye Ibada ya leo bado ujachelewa na sasa ibada imefunguliwa kwa Maombi.

Mahali: Mbuyuni-JKT

Jumapili hii Mungu ameturidhia kusogea hemani mwake kwa ajili ya kumfanyia Ibada.Ibada Itaanza saa 3 Asubuhi.Mungu amean...
07/02/2025

Jumapili hii Mungu ameturidhia kusogea hemani mwake kwa ajili ya kumfanyia Ibada.

Ibada Itaanza saa 3 Asubuhi.

Mungu ameandaa neno zuri kwa ajili yako.Utapokea muujiza utakao badilisha Maisha Yako ukiamini.

Mahali: Mbuyuni -JKT (mtaa wa kwa babayayo).

Pastor Elisha Tetemeko


KICHWA CHAKO NI UTAJIRI WAKOSulemani anatuambia tulinde sana moyo kuliko vyote.Lakini nami leo nakwambia LINDA KICHWA ch...
07/02/2025

KICHWA CHAKO NI UTAJIRI WAKO

Sulemani anatuambia tulinde sana moyo kuliko vyote.
Lakini nami leo nakwambia LINDA KICHWA chako na huo moyo ulioambiwa na Sulemani.
Narudia tena linda KICHWA chako.
kwa nini?

Kwa sababu huwezi kulinda moyo k**a kichwa chako kimekatwa, huwezi kulinda moyo k**a kichwa kimeharibiwa, huwezi kulinda moyo k**a kichwa kimechafuliwa.

Chochote huwezi kukilinda k**a KICHWA kimepatwa na shambulizi.

Mafanikio yoyote si rahisi kuyapata k**a unaruhusu KICHWA chako kukatwa, kuchafuliwa na kuharibiwa.

Ukitaka moyo wako uwe safi Linda sana KICHWA chako, uharibifu wa moyo hupitia kichwani.

Mungu alipendezwa na moyo wa Daudi, kwa maana alikuwa amempaka mafuta KICHWANI kwake.
ZABURI 23:5

Mafuta aliyo kuwa amepakwa Daudi kichwani yalimsaidia kulinda kichwa chake.
Daudi alimaliza vizuri kuliko Sulemani mwanaye.

Kwa nini Mungu alimpaka Daudi mafuta kichwani si miguuni.

ZIPO SABABU NNE.
1. Kwenye mwili kichwa kipo juu na Mungu yupo Juu.
Lengo kuu ni kuwasiliana na Mungu.

2. Uelewa wa mtu unategemea kichwa chake.

3. ⁠Kichwa ndicho kinaongoza viungo vyote vya mwili.

4. ⁠Kichwa ndicho kina macho, mdomo, masikio, ubongo uliobeba akili.

Hizo ndizo sababu za Mungu kumpaka Daudi mafuta kichwani.
Mungu amekiweka kichwa juu maana yeye yupo juu. Akili ya kuwasiliana naye ipo kichwani na moyoni.

Mungu yupo juu na kichwa kipo juu.
-Basi tafuta yaliyo juu utauokoa moyo wako.
-Basi fikiri yaliyo juu utaokoa moyo wako.

Utajiri na umaskini wa mtu unatokana na KICHWA na MOYO ulivyo ndani.

Wanaodumu katika uovu shida ipo kwenye KICHWA na MOYONI.

Huwezi kubadilisha tabia ya mtu, mpaka umbadilishe kichwani mwake na moyoni mwake na hiyo kazi mwenye uwezo wa kuifanya ni Mungu pekee yake.

Kichwa ni kitu kinacho kusanya matukio mazuri na mabaya baadaye yanapelekwa kwenye moyo.
Ili kusubiri kufanyiwa kazi.
my brethren, Protect your Head and your Heart.
Dont Joke about this.
-Your head is Your Wealth.
-Your Heart is Your Wealth

Shalom!!





05/02/2025

TAFUTA KWELI KWA GHARAMA YOYOTE....
Kataa Uongo ili usife..
Mwaka huu ishi katika kweli , Kweli ni Neno la Mungu
Biblia inasema nanyi mtaifahamu kweli na Kweli itawaweka huru.
Uwe na Siku ya Baraka.
Shalom !!




USIOGOPE !!!Umekwisha BARIKIWA na Bwana Tembea kwa Ujasiri na kwa ushindi.Siku yako IMEBARIKIWA.Shalom ! ! ..
04/02/2025

USIOGOPE !!!
Umekwisha BARIKIWA na Bwana Tembea kwa Ujasiri na kwa ushindi.
Siku yako IMEBARIKIWA.

Shalom ! !



..

....Wengi leo kinachozuia mafanikio yao ni ndani ya mioyo yao.Anayejua moyoni mwa mtu ni Mungu peke yake.Kuna vitu vinaw...
03/02/2025

....Wengi leo kinachozuia mafanikio yao ni ndani ya mioyo yao.Anayejua moyoni mwa mtu ni Mungu peke yake.

Kuna vitu vinaweza vikakaa ndani ya moyo wa mtu na ndivyo vinavyozuia upenyo wake.

Maisha makubwa yanaanzia moyoni, kuamini kunaanzia ndani moyo wa mtu. Moyoni kukishaitika kila kitu linawezekana kabisa. Moyo ukishapata ugonjwa maisha ya mtu yameharibiwa.

LINDA MOYO WAKO🫀
SIKU YAKO IMEBARIKIWA.



2 Wakorintho 5:21[21]Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katik...
02/02/2025

2 Wakorintho 5:21
[21]Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.
For he hath made him to be sin for us, who knew no sin; that we might be made the righteousness of God in him.

Mungu alimtuma mwanae aje kubeba dhambi zetu, na kutupa haki zetu.
Haki moja wapo ni kupata mema,kupona magonjwa. Magonjwa sio haki yako lakini unayo ni kwa sababu ujaamua kudai haki iyo.

Mungu ajakuumba uishi maisha hayo unayoishi leo dai leo Maisha yale Mungu aliyokusudia kuishi.
Ulikusudiwa kuishi mahali salama na sio hapo ulipo leo lakini uwezi toka hapo k**a ujachukua hatua ya kudai haki yako.

Kila haki yako huwa na mikono inazuia wewe kuonekana, usiposhughulikia unaweza usiipate haki yako.

DAI HAKI YAKO LEO..

BARIKIWA SANA.



KUSIFU NA KUABUDU🎹🎤🎶
02/02/2025

KUSIFU NA KUABUDU🎹🎤🎶



IBADA YA JUMAPILI Karibu kwenye Ibada na ibada imefunguliwa wakati huu na Mama Pastor Faith Tetemeko kwa Maombi.Na sasa ...
02/02/2025

IBADA YA JUMAPILI
Karibu kwenye Ibada na ibada imefunguliwa wakati huu na Mama Pastor Faith Tetemeko kwa Maombi.

Na sasa Tunasifu tukiongozwa na
Karibu sana.





01/02/2025

SIFA ZAKE ZIVUME.......

Karibu Tumsifu na Kumwabudu Mungu Pamoja.
Ni kesho jumapili kuanzia saa 3:00 Asubuhi..... Usije pekee ako njoo na jirani yako.
Kanisa lipo Mbuyuni-JKT (mtaa wa kwa babayayo)






AMUA KUMPENDA MUNGU !
30/01/2025

AMUA KUMPENDA MUNGU !




Ni jumapili hii🔥Usipange kukosa Mtumishi wa Mungu ataombea mikono yako, k**a kuna nira au uchawi ulifunga mikono yako in...
29/01/2025

Ni jumapili hii🔥
Usipange kukosa Mtumishi wa Mungu ataombea mikono yako, k**a kuna nira au uchawi ulifunga mikono yako inakwenda kufunguliwa kabisa.
Je! Umekua mtu wa kupoteza fedha au vitu.
Je! Pesa zimekua azikai kwako au zinaisha bila kufanya jambo la msingi.
Njoo na Mungu wa mbinguni atakuweka huru.

Kanisa lipo Mbuyuni-JKT (mtaa wa kwa babayayo)
WATU WA DINI ZOTE MNAKARIBISHWA.


Karibu sana kwenye Maombi haya ya kufunga na kuomba.Ni siku 21 za kufunga na kuomba.Njoo tumuombe Mungu pamoja Kwa Ajili...
05/01/2025

Karibu sana kwenye Maombi haya ya kufunga na kuomba.

Ni siku 21 za kufunga na kuomba.

Njoo tumuombe Mungu pamoja Kwa Ajili ya Mwaka 2025.

Mwaka wa kuhuishwa UPYA 2025.

Address

Mbuyuni Bus Station(Bagamoyo Road)
Dar Es Salaam

Telephone

+255747487759

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pastor Elisha Tetemeko posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Pastor Elisha Tetemeko:

Share