Sport STAR TV

Matokeo ya Namungo FC kwenye michezo 16 ya karibuni chini ya Kocha Juma Ramadhan Mgunda ,Hawajashinda mchezo wowote 3-1 ...
26/05/2026

Matokeo ya Namungo FC kwenye michezo 16 ya karibuni chini ya Kocha Juma Ramadhan Mgunda ,Hawajashinda mchezo wowote

3-1 Yanga ❌
1-1 V Mbeya City 🀝
0-1 V Singida Black Stars ❌
0-0 V Mashujaa FC ❌
0-1 V Azam FC ❌
0-0 V Dodoma Jiji 🀝
1-3 V Simba SC ❌
0-2 V TRA United ❌
2-2 V JKT Tanzania 🀝
2-0 V TRA United
1-1 V Singida Black Stars 🀝
0-1 V Yanga SC ❌
3-2 V Tanzania Prisons ❌
0-1 V Pamba Jiji ❌
1-1 V Mtibwa Sugar 🀝
1-1 V Fountain Gate 🀝

πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„

09/05/2026

"Sibadilishi kauli kwa nini nilisema Eng Hersi Saidi arudi kusajili". Ally Kamwe

NOTE

Ally Kamwe akiwa anasimama kuzungumza uhalisia wa mpira hapo akiwa kavua nguo ya usemaji wa timu kila mmoja huwa anatamani kipindi kisimalizike.

Ukisikiliza kwa umakini mahojiano yake ya jana akiwa Bongo FM hapo ndio utaelewa kuwa Young Africans sports club walituibia huyu mtu kwenye uchambuzi, hapo hapo Young Africans Sports Club walipata mtu ambae akikaa na viongozi wake anaweza kuwa mshauri wa usajili wa timu yake.

Ally ana madini ya soka kichwani mwake sio tu msemaji, ukitaka kupata hayo madini kwanza ambae unamfanyia mahojiano andaa maswali ya hoja sio uamke tu na mawazo yako ya kitandani usiku ukafanya mahojiano.

Kingine ukiwa unaenda kumfanyia mahojiano kwanza ujue vizuri umejiandaaje na kupokea majibu yake.

Cosmasy William Choga

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Riziki Pembe Juma, ameipongeza Timu ya Korosho Queens kwa kuibuka...
27/04/2026

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Riziki Pembe Juma, ameipongeza Timu ya Korosho Queens kwa kuibuka Mshindi wa Kombe la Muungano 2026.

Ametoa pongezi hizo, mara baada ya Timu hiyo kuwasili Ofisini kwake Migombani Wilaya ya Mjini kwa ajili ya kutoa shukrani kufuatia mashirikiano alioyatoa kwa timu hiyo.

Mhe. Warizi amesisitiza Wachezaji hao, licha ya kufanya vizuri katika michezo lakini wasisahau kuongeza bidii katika masomo ili waweze kupiga hatua zaidi.

Aidha amewataka kushiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa ndani na nje ya Nchi ili kuendeleza na kukuza vipaji vyao.

Hata hivyo Mhe. Waziri amekabidhi fedha taslim Sh. laki tano (500,000) kwa timu ya Korosho Queens kufuatiwa kupambana na kupata ushindi wa Kombe la Muungano, 2026.

Kwa upande wake Kocha Mkuu wa timu hiyo Enock Akyoo amesema wamefarajika sana kupata Kombe hilo na wachezaji wao kuonyesha umahiri mkubwa jambo ambalo limepelekea Mchezaji wao kupata Usajili kutoka Clab ya Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU).

Nae Kepten wa timu hiyo Mwasiti Abasi Kassim ametoa shukurani kwa Uongozi wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Riziki Pembe Juma kwa mashirikiano makubwa jambo ambalo limepelekea kuibuka ushindi wa Kombe hilo.

Mbali na hayo ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo waliopewa na kiongozi huyo kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla.

Jumla ya timu sita (6) zimeshiriki katika Kombe la Muungano kwa mchezo wa Wavu (Voliball) Wanawake ambapo timu nne ni kutoka Zanzibar na mbili kutoka Tanzania bara.

Imetolewa na kitengo cha Habari, Mawasiliano na Uhusiano.

WHSUM.

Mavazi ya Alliance Girls walipowasili uwanjani kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake dhidi ya Yanga Princess dondosha ma...
26/04/2026

Mavazi ya Alliance Girls walipowasili uwanjani kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake dhidi ya Yanga Princess dondosha maoni yako juu ya muonekano wao.

Tia neno.

Sport STAR TV

25/04/2026

KUMBUKUMBU KUELEKEA MEI 3

"Ni Young Africans sports club pekee Afrika hii ambayo ikipangiwa mechi na Simba sports club inakua haina wasiwasi". Ahmed Ally afisa habari wa klabu ya Simba.

Follow

23/04/2026

Wilson Oruma amekataa kuomba msamaha kwa Young Africans Sports Club .

Video πŸ“Ή Cosmasy William Choga

23/04/2026

Maneno ya Zawadi Mauya kuhusu Nasreedin Nabi

OMARY RAMADHAN ISSA : KOCHA MWENYE NDOTO YA VIJANA WENGI WA ZANZIBAR Ramadhan Omari Issa maarufu k**a kocha Pogba ni mio...
23/04/2026

OMARY RAMADHAN ISSA : KOCHA MWENYE NDOTO YA VIJANA WENGI WA ZANZIBAR

Ramadhan Omari Issa maarufu k**a kocha Pogba ni miongoni mwa makocha wanaofanya vizuri kwenye ligi na soka la vijana la Zanzibar.

Omary akiwa na leseni ya ukocha Kwa ngazi ya CAF C Diploma amebeba ndoto ya vijana wengi wa Zanzibar akiwa na matunda ya wachezaji kwenye timu za vijana za Tanzania & Zanzibar lakini kwenye vilabu k**a Azam FC na timu za madaraja ya juu ya Zanzibar.

Omary Kwa msimu wa 2025/26 amefanikiwa kuipandisha Daraja timu ya Bweleo FC ya Unguja kutoka ligi ya Mkoa na kupanda mpaka ligi Daraja la Kwanza ,ambapo amewaongoza kwenye michezo 13 akishinda michezo 9 ,Kupoteza 2 na Sare 2 huku akiwa ndiye bingwa Kwa ukanda wa mkoa wa Mjini Magharibi.

Omary amewahi kufundisha timu za Kwahani Football academy 2020-2023 ,Urafiki FC mwaka 2024 kisha Kundemba FC kabla ya kujiunga na Bweleo warriors mapema mwaka huu.

Omary Kwa sasa pia ni miongoni mwa makocha wa timu ya vijana ya Taifa ya Zanzibar ( Zanzibar Future National Team)

Mafanikio akiwa kocha

Kwahani Football academy - Kocha Mkuu
U17 πŸ† (2021
U 20 πŸ†πŸ† (2023)
U 20 πŸ†πŸ† (2024)

Urafiki FC - Kocha Mkuu
Nafasi ya Tatu πŸ₯‰ (2025)

Kundemba FC - Kocha msaidizi
Nafasi ya Tatu πŸ₯‰ (2025)

Bweleo Warriors FC - Kocha Mkuu
Mabingwa ligi ya Mkoa πŸ† (2026)

IDARA YA MAWASILIANO YA MBEYA CITY IJITATHIMINIRadio , TV ,magazeti na mitandao ya kijamii ni nyenzo sahihi ya kuwasilis...
19/04/2026

IDARA YA MAWASILIANO YA MBEYA CITY IJITATHIMINI

Radio , TV ,magazeti na mitandao ya kijamii ni nyenzo sahihi ya kuwasilisha taarifa ambayo unahusu taasis kuwafikia watu wengi Kwa gharama nyepesi zaidi na Dunia ya sasa kampuni , taasis na hata Serikali wamejikita kwenye matumizi ya nyenzo hizo kuweza kuwafikia watu wengi.

Licha ya kuwa Mbeya City FC ni timu yenye idadi kubwa ya wafuatiliaji kwenye mitandao ya kijamii , Changamoto kubwa ni kuwa Idara yao ya Habari ambayo inaongozwa na John Jerome na Lugano mwankota wwmeshindwa kutoa taarifa za mara Kwa mara kuhusu wachezaji ambao wameadhibiwa na timu Kwa utovu wa nidhamu.

Mfano k**a Umma ungekuwa na taarifa za kufungiwa Kwa wachezaji kusingekuwa na shutma ambazo Kwa sasa zimekuwa zikitolewa juu ya kocha Mecky Mexime pamoja na timu ya Mbeya City jambo ambalo linaathiri haiba ( Brand ) ya Mbeya city ,Kocha Mecky pamoja na wachezaji ambao wamehusishwa kwenye skendo tajwa.

Utoaji wa taarifa k**a hizo husaidia uwazi ,uwajibikaji na Kulinda heshima ya taasis lakini kutokana na Idara ya Habari ya Mbeya City kushindwa kutekeleza majukumu Yake Kwa wakati imeleta athari hasi kwenye timu yao.

Tumesikia upande mmoja wa kocha Mecky Mexime alieleza Changamoto kupitia mahojiano yake na kituo cha EFM sasa upande wa pili wadau wa soka wanasubiri kuona Mbeya City FC watakuwa na taarifa gani kuhusu skendo tajwa.

Idara za habari na mawasiliano za vilabu zinapaswa kuwa makini kwenye nyenzo za mawasiliano ,kujua faida ,Aina ya ujumbe ambao wanaweza kushare na jamii au Umma Kwa lengo la kuzuia taharuki ambazo zinachafua chapa ya timu k**a ambavyo Kwa sasa Mbeya City imewakuta.

30/03/2026

"Nani alitoa taarifa hiyo kwamba wanawaombea uraia kwaajili ya timu ya Taifa na klabu?. Nenda kule Sudan πŸ‡ΈπŸ‡© wale wachezaji wa Al Hilal na El Merriekh wameombewa urai FIFA?

Haya ni maoni yangu na nabaki na maoni yangu kutokana na ninavyojua mimi"

Ibrahim Masoud Maestro kuhusu Uraia wa Mohammed Damaro.

Unakua upande wa Ibrahim Maestro au Wilson Orouma..?

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport STAR TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport STAR TV:

Share

Category