27/04/2026
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Riziki Pembe Juma, ameipongeza Timu ya Korosho Queens kwa kuibuka Mshindi wa Kombe la Muungano 2026.
Ametoa pongezi hizo, mara baada ya Timu hiyo kuwasili Ofisini kwake Migombani Wilaya ya Mjini kwa ajili ya kutoa shukrani kufuatia mashirikiano alioyatoa kwa timu hiyo.
Mhe. Warizi amesisitiza Wachezaji hao, licha ya kufanya vizuri katika michezo lakini wasisahau kuongeza bidii katika masomo ili waweze kupiga hatua zaidi.
Aidha amewataka kushiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa ndani na nje ya Nchi ili kuendeleza na kukuza vipaji vyao.
Hata hivyo Mhe. Waziri amekabidhi fedha taslim Sh. laki tano (500,000) kwa timu ya Korosho Queens kufuatiwa kupambana na kupata ushindi wa Kombe la Muungano, 2026.
Kwa upande wake Kocha Mkuu wa timu hiyo Enock Akyoo amesema wamefarajika sana kupata Kombe hilo na wachezaji wao kuonyesha umahiri mkubwa jambo ambalo limepelekea Mchezaji wao kupata Usajili kutoka Clab ya Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU).
Nae Kepten wa timu hiyo Mwasiti Abasi Kassim ametoa shukurani kwa Uongozi wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Riziki Pembe Juma kwa mashirikiano makubwa jambo ambalo limepelekea kuibuka ushindi wa Kombe hilo.
Mbali na hayo ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo waliopewa na kiongozi huyo kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla.
Jumla ya timu sita (6) zimeshiriki katika Kombe la Muungano kwa mchezo wa Wavu (Voliball) Wanawake ambapo timu nne ni kutoka Zanzibar na mbili kutoka Tanzania bara.
Imetolewa na kitengo cha Habari, Mawasiliano na Uhusiano.
WHSUM.