Sport STAR TV

Nassoro Saadun ndio ameamua mechi imalizikaje jioni ya leo kati ya Simba SC Tanzania na Azam FC . Mbio, utulivu na akili...
07/12/2025

Nassoro Saadun ndio ameamua mechi imalizikaje jioni ya leo kati ya Simba SC Tanzania na Azam FC . Mbio, utulivu na akili ya haraka ya maamuzi sahihi katika muda sahihi.

FT: Simba Sc 0-2 Azam Fc

Sport STAR TV

Azam FC imeshinda Kwa mara ya Kwanza dhidi ya Simba SC kwenye ligi kuu kutokea msimu wa 2022/23 ,Azam walikuwa wamecheza...
07/12/2025

Azam FC imeshinda Kwa mara ya Kwanza dhidi ya Simba SC kwenye ligi kuu kutokea msimu wa 2022/23 ,Azam walikuwa wamecheza michezo 6 bila ushindi wowote kwenye ligi kuu.

Seleman Matola ambaye ndiye Kaimu kocha mkuu wa klabu ya Simba SC amepoteza mchezo wake wa Kwanza kwenye ligi kuu baada ya kuiongoza Simba SC kushinda michezo 3 hapo awali

✅Simba SC 3-0 Namungo
✅Simba SC 3-0 Fountain Gate
✅Simba SC 3-0 Mbeya City
❌Simba SC 0-2 Azam FC

Sport STAR TV

CAMARA MMSAHAU KIDOGO "Camara bwana k**a inawezekana kumsahau  msahau tu bado. Amefanyiwa vipimo anachangamoto ya goti k...
06/11/2025

CAMARA MMSAHAU KIDOGO

"Camara bwana k**a inawezekana kumsahau msahau tu bado. Amefanyiwa vipimo anachangamoto ya goti kwahiyo tunasubiri maamuzi ya mwisho k**a atibiwe kawaida au upasuaji kwahiyo suala lake bado ndio maana nikasema k**a mnaweza msahau". Ahmed Ally afisa habari wa klabu ya Simba

Sport STAR TV

Takwimu za Tanzania Prisons kwenye michezo 5 ya mwisho ✅ Tanzania Prisons 1-0 KMC ❌Namungo 1-0 Tanzania Prisons ❌ Coasta...
20/10/2025

Takwimu za Tanzania Prisons kwenye michezo 5 ya mwisho

✅ Tanzania Prisons 1-0 KMC
❌Namungo 1-0 Tanzania Prisons
❌ Coastal Union 1-0 Tanzania Prisons
✅ Tanzania Prisons 3-1 Fountain Gate
🤝 Fountain Gate 1-1 Tanzania Prisons

Takwimu za Mbeya City kwenye michezo 5 ya mwisho ✅KMC 0-3 Mbeya City 🤝Mbeya City 0-0 Yanga ❌Azam FC 2-0 Mbeya City ✅ Fou...
20/10/2025

Takwimu za Mbeya City kwenye michezo 5 ya mwisho

✅KMC 0-3 Mbeya City
🤝Mbeya City 0-0 Yanga
❌Azam FC 2-0 Mbeya City
✅ Fountain Gate 0-1 Mbeya City
✅Mbeya City 5-0 Green warriors

🇸🇳 Kiungo wa kati wa Senegal Krépin Diatta: "Baada ya kusaini mkataba wangu wa kwanza, nilianza kupokea jumbe kutoka kwa...
20/10/2025

🇸🇳 Kiungo wa kati wa Senegal Krépin Diatta:

"Baada ya kusaini mkataba wangu wa kwanza, nilianza kupokea jumbe kutoka kwa wasichana ambao waliwahi kuniambia kuwa mimi ni mbaya. Walisema kuwa hali ya hewa ya Ulaya imebadilisha sura yangu sasa. Nilijitazama kwenye kioo, lakini sikuweza kuona tofauti yoyote. Hapo ndipo nilipoelewa kuwa chaguo la wanawake mara nyingi hutokana na faida ya kifedha."

Sport STAR TV

Klabu ya Stand United ya mkoani Shinyanga, imepoteza mchezo wake wa pili mfululizo katika ligi ya NBC Championship kwa m...
20/10/2025

Klabu ya Stand United ya mkoani Shinyanga, imepoteza mchezo wake wa pili mfululizo katika ligi ya NBC Championship kwa msimu huu mpya.

Hii imekuja baada ya leo kupigwa bao 1-0 dhidi ya Kengold kutoka jijini Mbeya katika uwanja wa Halmashauri ya Chunya jioni ya leo huku mchezo uliopita walichapwa mabao 2-1 dhidi ya Songea United yote wakiwa ugenini.

Nikizungumza na Meneja wa timu hiyo jioni ya leo Fredy Masai, amesema hana mtu yeyote wa kumlaumu lakini wanarudi kwenye uwanja wa nyumbani ili kurudisha furaha ya wanashinyanga.

Katika mchezo mwingine uliopigwa jioni ya leo Songea United wakiwa uwanja wa nyumbani Majimaji mjini Songea Mkoani Ruvuma wamelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Gunners kutoka jijini Dodoma.

Gunners inaungana na Transit Camp kuwa ni timu pekee ambazo zimetoa sare kwenye michezo yote ambayo wamecheza ugenini msimu huu.

Klabu ya Young Africans Sports Club imeondoka nchini kuelekea Tanzania baada ya kufungwa na Silver Strikers katika mchez...
20/10/2025

Klabu ya Young Africans Sports Club imeondoka nchini kuelekea Tanzania baada ya kufungwa na Silver Strikers katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Wamekuwa nchini kwa siku mbili zilizopita baada ya mchezo na walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa wa Bingu Jumatatu asubuhi.

Mchezo wa marudiano umepangwa kuchezwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Benjamin Mpaka nchini TZ.

Mabeki wa Young Africans Sports club vijana Bakari Nondo Mwamnyeto na Israel Patrick Mwenda wakiwa makini kazini kwao.⚽️...
21/09/2025

Mabeki wa Young Africans Sports club vijana Bakari Nondo Mwamnyeto na Israel Patrick Mwenda wakiwa makini kazini kwao.

⚽️⚽️⚽️ kukaba ni muhimu.

26/08/2025

"Siwezi kusema jezi ya timu fulani mbaya kwa sababu jezi ni biashara za watu, Siwezi kuponda jezi ya watu kwa sababu ni maisha ya watu. Kuna mashabiki wa Simba sports club wanauza jezi hizo, Siwezi kuharibu maisha yao". Ahmed Ally afisa habari wa klabu ya Simba.

Sport STAR TV

MICHEZO KENYA 🇰🇪:' Rais wa Kenya Mh. William Ruto amewaahidi wachezaji wa timu ya taifa Harambee Stars kiasi cha shiling...
11/08/2025

MICHEZO KENYA 🇰🇪:'

Rais wa Kenya Mh. William Ruto amewaahidi wachezaji wa timu ya taifa Harambee Stars kiasi cha shilingi milioni 2.5 za KENYA kila mmoja, endapo vijana hao wataibuka na ushindi mbele ya Zambia katika mechi ya mwisho ya kundi A katika michuano ya CHAN.

Pia kiongozi huyo ameongeza kuwa endapo Kenya itatinga robo fainali, kila mchezaji atapata shilingi milioni moja pamoja na nyumba ya vyumba viwili kupitia mpango wa nyumba za gharama nafuu mahali ambapo watakapojichagulia wenyewe.

Sport STAR TV

Sasa chama cha Soka nchini Uingereza kimetangaza kupiga marufuku matumizi ya kamba za viatu za rangi ya upinde wa mvua (...
08/08/2025

Sasa chama cha Soka nchini Uingereza kimetangaza kupiga marufuku matumizi ya kamba za viatu za rangi ya upinde wa mvua (rainbow laces) na beji za unahodha za rangi hiyo kwa msimu ujao.

Kwa mjibu wa taarifa ni kuwa kampeni hiyo ilikuwa inaleta utata badala ya ujumbe chanya ambao ilikua kusudio kwao. Ikumbukwe baadhi ya wachezaji walikua hawataki matumizi hayo.

Wamezinduka eeeh...?

Sport STAR TV

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport STAR TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport STAR TV:

Share

Category