Sport STAR TV

Mabeki wa Young Africans Sports club vijana Bakari Nondo Mwamnyeto na Israel Patrick Mwenda wakiwa makini kazini kwao.⚽️...
21/09/2025

Mabeki wa Young Africans Sports club vijana Bakari Nondo Mwamnyeto na Israel Patrick Mwenda wakiwa makini kazini kwao.

⚽️⚽️⚽️ kukaba ni muhimu.

26/08/2025

"Siwezi kusema jezi ya timu fulani mbaya kwa sababu jezi ni biashara za watu, Siwezi kuponda jezi ya watu kwa sababu ni maisha ya watu. Kuna mashabiki wa Simba sports club wanauza jezi hizo, Siwezi kuharibu maisha yao". Ahmed Ally afisa habari wa klabu ya Simba.

Sport STAR TV

MICHEZO KENYA 🇰🇪:' Rais wa Kenya Mh. William Ruto amewaahidi wachezaji wa timu ya taifa Harambee Stars kiasi cha shiling...
11/08/2025

MICHEZO KENYA 🇰🇪:'

Rais wa Kenya Mh. William Ruto amewaahidi wachezaji wa timu ya taifa Harambee Stars kiasi cha shilingi milioni 2.5 za KENYA kila mmoja, endapo vijana hao wataibuka na ushindi mbele ya Zambia katika mechi ya mwisho ya kundi A katika michuano ya CHAN.

Pia kiongozi huyo ameongeza kuwa endapo Kenya itatinga robo fainali, kila mchezaji atapata shilingi milioni moja pamoja na nyumba ya vyumba viwili kupitia mpango wa nyumba za gharama nafuu mahali ambapo watakapojichagulia wenyewe.

Sport STAR TV

Sasa chama cha Soka nchini Uingereza kimetangaza kupiga marufuku matumizi ya kamba za viatu za rangi ya upinde wa mvua (...
08/08/2025

Sasa chama cha Soka nchini Uingereza kimetangaza kupiga marufuku matumizi ya kamba za viatu za rangi ya upinde wa mvua (rainbow laces) na beji za unahodha za rangi hiyo kwa msimu ujao.

Kwa mjibu wa taarifa ni kuwa kampeni hiyo ilikuwa inaleta utata badala ya ujumbe chanya ambao ilikua kusudio kwao. Ikumbukwe baadhi ya wachezaji walikua hawataki matumizi hayo.

Wamezinduka eeeh...?

Sport STAR TV

06/08/2025

Hapa ndipo lilizaliwa jina la Utopolo kutoka kwa shabiki wa timu ya Young Africans sports club, Mashaka.

Acheni mashabiki wao kwa sasa watambe wamepitia magumu sana.

JKT,JKU  WAWAKILISHI WA TANZANIA CAFNa    Cosmasy William Choga Kenya inatazamiwa kuwa mwenyeji wa mechi za kufuzu kwa L...
06/08/2025

JKT,JKU WAWAKILISHI WA TANZANIA CAF

Na
Cosmasy William Choga

Kenya inatazamiwa kuwa mwenyeji wa mechi za kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa ya Wanawake ya CAF CECAFA 2025. Michuano hiyo itafanyika Septemba 4-16 jijini Nairobi, Kenya.

Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) lilituma maombi ya kuandaa mashindano ya kanda ambayo yataleta pamoja timu nane.

"Tunafuraha kwamba michuano hiyo itarejea Kenya baada ya ile ya uzinduzi kuandaliwa hapo 2021," alisema Yusuf Mossi, Mkurugenzi wa Mashindano ya CECAFA.

CECAFA iliazimia kuandaa michuano hiyo kabla ya Septemba 18, 2025, ili kuruhusu wachezaji kupatikana kwa ajili ya timu zao za taifa katika awamu ya awali ya mchujo wa kufuzu Kombe la Dunia la Wanawake U-20.

Vyama Wanachama vya Sudan, Somalia, Eritrea na Djibouti hawatatuma timu kushiriki michuano hiyo.

Mabingwa watetezi Commercial Bank of Ethiopia (CBE) FC na Yei Joint Stars ndizo timu pekee zilizojitokeza katika matoleo yote manne ya mwisho ya mchujo.

Washindi wa mchujo wa Kanda watawakilisha CECAFA kwenye Ligi ya Mabingwa ya Wanawake ya CAF 2025.

Timu nane zitakazoshiriki michuano hiyo ni pamoja na; Top Girls Academy FC (Burundi), Kenya Police Bullets (Kenya), Yei Joint Stars FC (Sudan Kusini), JKT Queens (Tanzania), Commercial Bank of Ethiopia FC (Ethiopia), Kampala Queens (Uganda), Rayon Sports Womens FC (Rwanda), JKU Princesses FC (Zanzibar)

Sport STAR TV

28/07/2025

“Kwanza tukimuuza Fei kwenda Simba tunapaswa kuilipa Yanga bilioni 1, maana yake ni kwamba tunatakiwa tupate pesa nyingi zaidi ya kubaki nayo. Haiwezekani tumuuze mchezaji kwa bei ambayo bilioni ikienda Yanga sisi tubakiwe na milioni 200 au tubaki na kiasi sawa na Yanga, haiwezekani”.

“Mchezaji akisema amechoka kucheza Azam football club na anataka kuondoka hakuna mtu atakayemuuliza swali lolote, ataambiwa tu soma vipengele vya mkataba, tekeleza nenda huko unakotaka kwenda”. Zaka Zakazi

TISA WAAGWA MBEYA CITY Uongozi wa klabu ya Mbeya City Fc  umetangaza kuachana na wachezaji wake tisa baada ya kumalizika...
28/07/2025

TISA WAAGWA MBEYA CITY

Uongozi wa klabu ya Mbeya City Fc umetangaza kuachana na wachezaji wake tisa baada ya kumalizika kwa mikataba yao ya kuitumikia klabu hiyo ambayo imepanda daraja.

Kupitia taarifa yake klabu hiyo imewatakia kila la kheri wachezaji hao katika maisha mengine nje ya Mbeya City Fc ambao ni Kilaza Mazoea, Pius Joseph, Jeremiah Thomas, Fred Mlelwa, Mudathir Abdalah, Andrew Kihumbi, Feisal Mganga, Medson Mwakatundu na Chesco Mwasimba

Sport STAR TV

SIMBA YAPEWA BURE JONATHAN SOWAH "Hapo awali nilisema hakuna timu Tanzania ya kumnunua Jonathan Sowah lakini baada ya ta...
27/07/2025

SIMBA YAPEWA BURE JONATHAN SOWAH

"Hapo awali nilisema hakuna timu Tanzania ya kumnunua Jonathan Sowah lakini baada ya taarifa ile nimeona watu wananishambulia. Niweke wazi hakuna pesa ambayo Simba sports club wametoa bali ni mahusiano mazuri na Rais wetu na Simba akawapa mchezaji huyo k**a mchango wake tu sio kwamba Simba wamemnunua.

Mimi ndio msemaji wa taasisi nikisema kitu nakua na uhakika na kitu ambacho nakisema , kitu pekee ambacho sisi tuliwambia Simba wakakubaliane tu na mchezaji ". Hussein Massanza afisa habari wa Singida Black Stars

Sport STAR TV

"Leo nataka niwambie ukweli sasa achana na haya yote yaliyokua yanaendelea na sisi tunacheka. Pacome ZOUZOUA alisaini mk...
25/07/2025

"Leo nataka niwambie ukweli sasa achana na haya yote yaliyokua yanaendelea na sisi tunacheka. Pacome ZOUZOUA alisaini mkataba mpya siku ya ndoa ya Aziz Ki". Ally Kamwe afisa habari wa Young Africans Sports club.

Sport STAR TV

Kocha wa Magolikipa Majdi Mnasria raia wa Tunisia 🇹🇳 amejiunga na Young Africans 🇹🇿Mnasria amewahi kupita  Sportives de ...
25/07/2025

Kocha wa Magolikipa Majdi Mnasria raia wa Tunisia 🇹🇳 amejiunga na Young Africans 🇹🇿

Mnasria amewahi kupita Sportives de Gafsa, Stade Gabsien Sports, Averine Sportif de Casserine, ES Metlaoui, Golden Arrows na Olympique Akbou.

“Huwa najutia kumpoteza Gerrard (Pique)…! Dunia itaniona kituko ila ndio ukweli unaonitesa muda mwingi…! Sikuwa mwanamke...
25/07/2025

“Huwa najutia kumpoteza Gerrard (Pique)…! Dunia itaniona kituko ila ndio ukweli unaonitesa muda mwingi…! Sikuwa mwanamke mzuri kwenye siku za karibuni…! Sikusimama kwenye nafasi ya mwanamke…! Sikuwa Mke mzuri kwa mume wangu…!”

“G ni mpole lakini alichoshwa na tabia zangu…! Tulikuwa k**a wanaume wawili…! Niliamini naweza kufanya kila kitu mwenyewe na yeye akalea tu watoto kutoka mbali…! Sio kweli…! Kuna furaha naikosa. Hakuna siku mwanaume atakuwa sawa na mimi mwanamke…!”

“Ninajikuta k**a nawaumiza watoto kwa muda fulani…! Katika hasira kubwa ya Pique nilichangia pakubwa…! Kuzingatia kazi pekee bila kumzingatia Baba wa watoto wangu, kurudi nimechoka na kujiona ninaweza kufanya majukumu mengine sikumpa utulivu G na haikuwa ngumu kwake kuniacha dunia inioneshe umuhimu wake…! Ni maumivu”

Shakira, Msanii na mtumbuizaji raia wa Colombia kuhusu maisha baada ya kuachana na Gerrard Pique

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport STAR TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport STAR TV:

Share

Category