Sport STAR TV

  • Home
  • Sport STAR TV
TETESI:- Marcio Maximo kocha wa zamani wa Taifa Stars na Young Africans sports club inaelezwa atarudi tena Tanzania awam...
22/07/2025

TETESI:-

Marcio Maximo kocha wa zamani wa Taifa Stars na Young Africans sports club inaelezwa atarudi tena Tanzania awamu hii ikiwa ni zamu ya kuionoa timu ya Kmc football club ya Kinondoni.

Vipi ataiweza ..?

Sport STAR TV

22/07/2025

Taarifa ya asubuhi hii ni kwamba mpiga siku wa Young Africans Sports club, Mudathir Yahya kaongezewa mkataba wa miaka miwili. Hivyo yupo sana Jangwani hadi 2027.

Vipi wananchi mmependa au mlitaka aondoke tu..?

Sport STAR TV

USIMWAMINI MCHEZAJI UKADHANI SHABIKI WA TIMU YENU.Na    Cosmasy William Choga Maisha yamebadilika sana. Yale ambayo tuli...
20/07/2025

USIMWAMINI MCHEZAJI UKADHANI SHABIKI WA TIMU YENU.

Na
Cosmasy William Choga

Maisha yamebadilika sana. Yale ambayo tuliyaona yanafanyika Ulaya Kwa Sasa yanafanyika Tanzania. Kwa bahati mbaya sisi mashabiki wa soka la kitanzani hatuko tayari hatuna utayari huo ambayo wenzetu wamefikia hatua wameshakomaa nao. Lakini taratibu dawa inatuingia.

Nani alikuwa Feitoto angeondoka vile Yanga. Hakuna shabiki aliamini Fei anaondoka Yanga.

Nani anaamini k**a Zimbwe kaaga Simba . Wako wanaodhani Akaunti yake ime tapeliwa na wahuni na wanaiendesha. Hawaamini watu.

Kuto kuamini Kwa mchezaji kipenzi kuondoka katika klabu yetu ni sababu tunawapa ushabiki Hawa wachezaji katika timu zetu tukasahau k**a wao wanafanya maisha kupitia soka.

Wachezaji wa Sasa hawataki kuja kuishi k**a ilivyo kuwa Kwa wale wakongwe wetu kina Mzee Jella Mtagwa na wengine.

Kila kheri Mtumishi mwadilifu wa klabu ya Simba. Licha ya kuwa shabiki wa Yanga tangu utotoni k**a ilivyokuwa Kwa Jonas lakini Utumishi wako ndani ya Simba ulikuwa mkubwa mno. K**a ambavyo Simon msiba alivyokuwa mtumishi mwadilifu Yanga lakini ni mpenzi wa Simba tangu utotoni.

Kwa hili la Fei na la Zimbwe naona Sasa tutaanza kuishi kihalisia Kwa kutambua wachezaji sio mashabiki.

"Mchezaji mwenye malengo hawezi kuingia kwenye mtego wa ushabiki katika timu. Kitu pekee Cha kuzingatia ni umeajiriwa Ili ufanye kazi" Kelvin Yondani 'Cottom juice Mweni, Injinia, Vidic".

Sport STAR TV

"Prisons niliwapa ripoti ya kuboresha timu kuelekea msimu ujao lakini hakuna mazungumzo yeyote kuhusu mkataba mpya ambac...
18/07/2025

"Prisons niliwapa ripoti ya kuboresha timu kuelekea msimu ujao lakini hakuna mazungumzo yeyote kuhusu mkataba mpya ambacho nimeweza kufanya ni kufanikisha malengo ya timu ,Mimi k**a kiongozi wa Benchi la Ufundi nasema kuwa tumefanikiwa Kwa pamoja lakini kwenye ripoti nimeeleza mahitaji ya kikosi kuelekea msimu ujao ambavyo kinapaswa kuwa

Nafasi ambayo nilipewa Tanzania Prisons ilikuwa nzuri sababu ilinitambulisha Kwa mashabiki wa Soka Tanzania kutoka kufundisha ligi ya Wilaya ,Mkoa ,Mabingwa wa mikoa ,ligi ya Daraja la Kwanza na hata ligi kuu kupitia Tanzania Prisons ilikuwa Jambo zuri kutokana na watu ambao wamenipa nafasi ya kufanya Kazi hasa kwenye Daraja la juu la Tanzania

Malengo ya klabu ndio huamua Hatma ya mwalimu wanayemtaka ,Malengo yalikuwa ni kubakiza timu ligi kuu kwenye hilo nilifanikiwa lakini malengo ya klabu na project Yao imebadilika wanaona ni Bora kuwa na Mwalimu ambaye anaweza kuwafikisha kwenye malengo husika,Malengo ndio huamua Aina ya mwalimu ambaye anahitajika na klabu

Nimepokea ofa kadhaa kutoka vilabu vya ligi kuu na vile vya championship,Nasubiri Tu commitment kuona mambo yatakuendaje ,Lakini Kwa sasa sina makubaliano yeyote ya kuwa na Tanzania Prisons Kwa msimu ujao miezi 6 yangu imeisha"

Amani Josiah aliyekuwa kocha wa Tanzania Prisons

K**a utahitaji huduma ya Moussa Balla Conte itabidi usubiri baada ya miaka mitatu📃✍🏽Verrati Conte k**a anavyojiita yeye ...
18/07/2025

K**a utahitaji huduma ya Moussa Balla Conte itabidi usubiri baada ya miaka mitatu📃✍🏽

Verrati Conte k**a anavyojiita yeye akiwa na jezi ya Young Africans Sports Club , Je unadhani atawapa matunda mazuri ..?

Sport STAR TV


KEMPES VS CRUYFF Na    Honorius Mpangala Kwanza kabisa happy birthday Fundi wa klabu ya Valencia na timu ya taifa ya Arg...
17/07/2025

KEMPES VS CRUYFF

Na
Honorius Mpangala

Kwanza kabisa happy birthday Fundi wa klabu ya Valencia na timu ya taifa ya Argentina Mario KEMPES.

Huyu fundi wa mpira Mido Sankala haswa Inside ten ya maana Kempes. Akiwa anaitumikia Valencia pale Spain kulikuwa na fundi mwingine aliyeitwa Yohan Cruyff. Cruyff alikuwa fundi Toka Uholanzi aliitumikia Fc Barcelona.

Namna ambavyo Messi alioneokana na FC Barcelona ndivyo ilivyokuwa Kwa Cruyff baba wa la masia. Baba wa Fc Barcelona.

Kempes kwake yeye na Valencia yake ilikuwa k**a unavyoona Nico Williams na Athletic club de Bilbao yake.

KOMBE LA DUNIA 1974 UJERUMANI MAGHARIBI.

Mario Kempes akiwa ni kinda kabisa ndiye aliyekuwa na umri mdogo katika kikosi Cha Argentina. Alikuwa na umri wa miaka 19. Alikuwa katika kikosi Cha Kombe la Dunia pale ujerumani Magharibi. Bingwa alikuwa ujerumani Magharibi akiicharaza Uholanzi ya Yohan Cruyff Kwa bao 2-1. Hapa Kempes alikuwa mchezaji wa klabu ya Rosario Central.

Mwaka huo ndio ulikuwa mwaka ambao Uholanzi walitambulisha mtindo wao wa Total football.

KOMBE LA DUNIA 1978 ARGENTINA

Ilikuwa ni fainali za pili mfululizo Kwa Uholanzi . Macho ya wengi yalikuwa kuwaona mafundi wawili katika fainali hii. Ni Mario Kempes akiwa ndo Nahodha wa Argentina na Yohan Cruyff akiwa ndiye Nahodha wa Uholanzi. Wawili Hawa walikuwa ni Mafundi wa vilabu vyao yaani Fc Barcelona na Valencia CF.

MECHI YA FAINALI WC 1978

Ilikuwa ni Argentina mwenyeji vs Uholanzi aliyeingia mara mbili mfululizo. Ilikuwa mechi ya Kempes vs Cruyff.

Mashabiki jukwaani walianikiza Kwa kuyaimba majina yao. Yaani wakati Uholanzi wakimwimba gwiji wao Cruyff Kwa nguvu jukwaani kwamba ndiye mwenye ufunguo wa kuwapa taji sambamba na ufundi wake.

Lakini mashabiki wa Argentina waliimba jina la Kempes wakiamini yeye ndiye Nahodha wa timu na ndiye fundi tegemeo wa kuwapa taji wakiwa Ardhi ya nyumbani.

Ufundi mwingi wa kuoneshana uwezo ulitamalaki dimbani. Waliamua kuhamishia la Liga kwenye mchezo wa Kombe la Dunia. Licha ya kwamba Kwa msimu huo pale la Liga bingwa alikuwa Real Madrid lakini haikuwanyima wao kuonesha umahiri wao mbele ya macho ya watazamaji.

Ilikuwa wengine wakiimba Marioooooo .. wengine wanaitika Kwa kutaja Kempeeeeeeees.. huku wale waholanzi nao Ilikuwa ni Yohaaaaaan Wengine wanaitika Cryuuuuuuuuff..

Hadi dakika mechi inaisha Argentina 3-1 Uholanzi.

Mfungaji bora akawa Kempes Kwa magoli 6.
Mchezaji Bora akawa Kempes pia.

Dunia ilikuwa na magwiji haswa.

Luca Modric amejiunga na Associazione Calcio Milan akitokea Real Madrid ambayo amehudumu kwa miaka 13, Luca alijiunga na...
15/07/2025

Luca Modric amejiunga na Associazione Calcio Milan akitokea Real Madrid ambayo amehudumu kwa miaka 13, Luca alijiunga na Madrid akitokea Tottenham Hotspur mwaka 2012

Sport STAR TV

“Jumla nimetumia Bilioni 87 mpaka sasa tangu 2017 hivyo kusema MO hatoi hela ni Kauli ya kupotosha yenye mwelekeo wa chu...
15/07/2025

“Jumla nimetumia Bilioni 87 mpaka sasa tangu 2017 hivyo kusema MO hatoi hela ni Kauli ya kupotosha yenye mwelekeo wa chuki” . MO Dewji

Kimsingi ni k**a bosi anajitoa katika hizi lawama, lakini pia angetueleza kuhusu matangazo yake ya biashara katika jezi za Simba sports club ambayo yamejaa vya kutosha.

Post hii ya Simba SC Tanzania kwa sasa haipo.

Sport STAR TV

Rasmi aliyekua mchezaji wa Young Africans Sports club, Kennedy Musonda raia wa Zambia 🇿🇲 amejiunga na Hapoel Ramat Gan G...
13/07/2025

Rasmi aliyekua mchezaji wa Young Africans Sports club, Kennedy Musonda raia wa Zambia 🇿🇲 amejiunga na Hapoel Ramat Gan Givatayim F.C.ya Israel 🇮🇱 .

Sport STAR TV

Aliyekua kocha  wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na Wydad Casablanca ya Morocco 🇲🇦, Rhulani Mokwena ametangazwa kuw...
13/07/2025

Aliyekua kocha wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na Wydad Casablanca ya Morocco 🇲🇦, Rhulani Mokwena ametangazwa kuwa Kocha mkuu wa klabu ya MC Alger ya nchini Algeria 🇩🇿

Sport STAR TV

UJUMBE WA MOHAMMED DEWJI KWA MASHABIKI WA SIMBA Wapenzi wa Simba,Najua mioyo yenu imebeba maswali mengi. K**a Rais wenu,...
11/07/2025

UJUMBE WA MOHAMMED DEWJI KWA MASHABIKI WA SIMBA

Wapenzi wa Simba,

Najua mioyo yenu imebeba maswali mengi. K**a Rais wenu, msione nimekaa kimya wakati tumepitia kipindi hiki kigumu. Kupambania Simba ni wajibu wangu.

Huu siyo wakati wa lawama — ni wakati wa kusimama imara, kuwa kitu kimoja, na kuchukua hatua sahihi za kuleta mabadiliko chanya.

Katika siku chache zijazo, nitazungumza na nyie moja kwa moja. Kuna kazi kubwa inaendelea, na kuna matumaini ya kweli.

Simba haijapotea. Tumekuwa kwenye kipindi cha mpito — tumejenga kikosi kipya, tumeimarisha benchi la ufundi, na tumeweka msingi wa mwelekeo mpya. Msimu huu tumefika mbali zaidi ya matarajio, na msimu ujao tunarudi kwa nguvu mpya.

Naomba tuendelee kuwa wavumilivu. Tunahitaji kufanya marekebisho makubwa. Tuendelee kusimama pamoja k**a familia moja.

Mbele yetu kuna mwanga. Na kwa pamoja, tutarudi tukiwa imara zaidi, wenye njaa zaidi, na wa kishujaa zaidi.

Sport STAR TV

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport STAR TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport STAR TV:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share