Breaking News Kiswahili

Breaking News Kiswahili Tunahabarisha, Tunaelimisha, Tunaburudisha

28/04/2024
29/02/2024

Jiunge hapa upate Habari kila zinapojiri

Makomandoo wa JWTZ
13/01/2024

Makomandoo wa JWTZ

Indonesia ndilo taifa ambalo linakisiwa kuwa na watu wakarimu zaidi duniani ikifuatiwa na  Ukraine na Kenya ikishika naf...
09/11/2023

Indonesia ndilo taifa ambalo linakisiwa kuwa na watu wakarimu zaidi duniani ikifuatiwa na Ukraine na Kenya ikishika nafasi ya tatu katika ngazi ya dunia.

Hii ni kwa mujibu wa wakfu wa kutoa misaada ya kibinadam wa The Charities Aid Foundation (CAF).

Je umewahi kumsaidia mgeni au kujitolea muda wako kwa ajili yake?

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limegundua eneo jipya lenye kivutio cha kipekee cha Utalii ndani ya Hifadhi ya Taif...
26/10/2023

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limegundua eneo jipya lenye kivutio cha kipekee cha Utalii ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambalo limepambwa na nguvu za asilia (Natural Pillars).

Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Ruaha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Godwell Meing’ataki amesema jitihada za kulitangaza eneo hilo zimeanza ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ili kuvutia watalii wengi zaidi na wawekezaji kutembelea na kuwekeza katika aina hiyo mpya ya Utalii.

Kamishna Meing'ataki amesema TANAPA inafanya taratibu za kuwaalika watafiti mbalimbali wa miamba, udongo na Malikale (Archiolojia) wa ndani na nje ya nchi ili kubaini na kupata taarifa sahihi za malikale zilizopo, taarifa ambazo zitalitambulisha eneo hilo kimataifa.

Eneo hilo ambalo limepewa jina la "Ruaha Magic Site", mandhari yake inafanana na masalia ya zana za Mawe mithili ya zile zilizotumika Zama za Mawe za Mwanzo.

Msanii wa muziki wa Hip-hop kutoka Nchini Marekani 🇺🇸, Lil Wayne amewajia juu viongozi wa makumbusho waliochonga sanamu ...
26/10/2023

Msanii wa muziki wa Hip-hop kutoka Nchini Marekani 🇺🇸, Lil Wayne amewajia juu viongozi wa makumbusho waliochonga sanamu lenye taswira yake. Msanii huyo amewaambia kuwa sanamu hilo wamekosea na sio yeye, wajitahidi kufanya marekebisho.

"Samahani, makumbusho ya Cire, lakini si mimi! Ila mmejaribu na ninashukuru kwa juhudi" amesema Lil Wayne.

Toa maoni yako

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria akipokea taarifa ya Kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kinacho...
26/10/2023

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria akipokea taarifa ya Kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kinachoendelea jijini Arusha katika kumbi za AICC kutoka kwa viongozi wa menejimenti ya wizara wanaosimamia kikao hicho.

Katibu wa NEC itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Paul Makonda amewataka viongozi na wanachama wa chama hicho...
26/10/2023

Katibu wa NEC itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Paul Makonda amewataka viongozi na wanachama wa chama hicho kumpa ushirikiano katika majukumu yake mapya ndani ya CCM.

Makonda aliyewahi kuwa Mkuu wa mkoa wa Dare es salaam kuanzia 2016 hadi 2021, ameyasema hayo leo Oktoba 26, 2023 katika ofisi ndogo za chama hicho zilizombo Mtaa wa Lumumba Kariakoo jijini Dar es salaam wakati wa makabidhiano ya ofisi kutoka kwa mtangulizi wake Sophia Mjema.

Katika hatua nyingine Makonda amesema yuko tayari kufundishwa, kushauriwa na kuelekezwa ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi kwa manufaa ya chama hicho na taifa zima.

MSITUMIE MATE WAKATI WA TENDO LA NDOA"Sio salama kutumia mate k**a kilainishi wakati wa tendo la ndoa kwa sababu kuna vi...
26/10/2023

MSITUMIE MATE WAKATI WA TENDO LA NDOA

"Sio salama kutumia mate k**a kilainishi wakati wa tendo la ndoa kwa sababu kuna vijidudu ambavyo vipo katika mate, kwa hiyo vinatakiwa vikae huko huko havitakiwi kuhamishwa sehemu nyingine. Ukivipeleka sehemu za siri unaweza kusababisha changamoto nyingine". Dkt. Baya Kissiwa, Mtaalamu wa Afya ya Uzazi kutoka hospitali ya Amana, Dar es Salaam

16/06/2023
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),  Mhe. Angellah Kairuki amekabidhi magari...
21/04/2023

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Angellah Kairuki amekabidhi magari 25 ikiwa ni sehemu ya Magari 200 yaliyoagizwa kupitia mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) kwa ajili ya Maafisa Elimu Sekondari wa Halmashauri zote nchini.
Pia ameahidi kujenga bweni la wanafunzi wa kiume wa shule ya sekondari Kibasila ikiwa ni ahadi kutoka kwa Mheshimiwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza mkoani Dar es Salaam katika hafla ya ugawaji wa magari hayo Mhe. Kairuki
aliwataka Wakala wa Ununuzi Serikalini (GPSA) kukakamilisha upatikanaji wa magari mengine 105 yaliyosalia kwa ajili ya mafisa elimu hao.
"Katika Halmashauri 184 zinazotakiwa kupata magari, Halmashauri 51 tayari zimepata katika awamu ya kwanza, awamu ya pili 19 na hii awamu ya tatu magari 25 hivyo bado magari 105 kwa maofisa hayo," alisema.
Aidha, ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuboresha elimu na maslahi ya walimu nchini hivyo aliwataka maofisa hao wawe wabunifu kusimamia shughuli za Kielimu na kuhakikisha kuwa Ubora wa Elimu unaimarika.
Mhe. Kairuki amesema elimu ya sekondari inahitaji uwajibikaji na huwezi kupata mafanikio pasipo kuwa na ubunifu na bidii kwa watumishi hivyo Serikali inaendelea kufanya maboresho lakini pia wasimamizi nao watekeleze wajibu wao.
Amewataka Maafisa hayo kutumia magari hayo kuongeza ufanisi wa shughuli za Kielimu na pia yatunzwe ili yaweze kudumu kwa muda mrefu.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Prof. Joyce Ndalichako amekagua maandalizi y...
21/04/2023

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Prof. Joyce Ndalichako amekagua maandalizi ya sherehe za Mei Mosi na kueleza kuridhishwa na hatua zilizofikiwa.
Akipokea taarifa ya k**ati ya maandalizi walipokutana kwa lengo la kujadili na kupanga mipango mbalimbali kuelekea kilele cha sherehe hizo zinazotarajiwa kuadhimishwa katika uwanja wa Jamhuri, Mkoani Morogoro, Waziri Ndalichako amepongeza k**ati ya mkoa kwa kushirikiana na ofisi yake pamoja na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) ili kufanikisha sherehe hiyo.
“Nawapongeza kwa kazi nzuri, hakika hatua iliyofikiwa katika maandalizi inaridhisha,” amesema. Nipongeze Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) kwa namna wanavyoratibu shughuli hii na tunawaunga mkono kwa kuwa tunatambua umuhimu wa wafanyakazi katika kutekeleza malengo ya Serikali,”

ZAIDI ya viwanda vidogo vidogo 500 vya wachina vimewekezwa nchini Tanzania ambavyo vimewezesha watanzania wengi kupata a...
21/04/2023

ZAIDI ya viwanda vidogo vidogo 500 vya wachina vimewekezwa nchini Tanzania ambavyo vimewezesha watanzania wengi kupata ajira.
Hayo yamebainika wakati Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Pendo Malangwa alipofungua Mashindano ya Awali ya Siku ya Kichina Duniani yaliyoadhimishwa chuoni hapo.
Profesa Malangwa amesema asilimia kubwa ya watanzania walioajiriwa katika viwanda hivyo ni wale wanaojua lugha ya kichina kupitia elimu inayotewa na Taasisi ya Confucius iliyopo chuoni hapo.
Amesema kupitia viwanda hivyo watanzania wanaojifunza lugha ya kichina wanaweza kuajirika katika viwanda hivyo.
Amesema wachina wana mchango mkubwa katika kuunganisha nchi za kiafrika na China kupitia taasisi yake ya Confucius ambayo kazi yake kubwa ni kufundisha lugha ya kichina, utamaduni wake na michezo mbalimbali inayoendana na utamaduni wa kichina.

TANGAZO LA AJIRA KUTOKA WIZARA YA AFYAWizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma n...
21/04/2023

TANGAZO LA AJIRA KUTOKA WIZARA YA AFYA
Wizara ya Afya kupitia Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/128/01/”B”/72 cha tarehe 20 Aprili, 2023; Inatangaza nafasi za kazi 247 za Kada za Afya.

WIZARAya Afya imetangaza nafasi za ajira 247 zikihusisha madakitari bingwa 30, baada ya kupata Kibali cha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Aprili 20, 2023.
1. Daktari daraja la II nafasi 15
2. Daktari wa meno daraja la II nafasi 10
3. Mfamasia daraja la II nafasi 10
4. Afisa Muuguzi daraja II nafasi 15
5. Afisa Muuguzi msaidizi daraja II nafasi 40
6. Afisa Mteknolojia daraja la II nafasi 15
7. Mteknolojia daraja la II nafasi 48
8. Mhandisi vifaa tiba daraja II nafasi 10
9. Fundi sanifu vifaa tiba daraja II nafasi 15
10. Fiziotherapia daraja la II nafasi 10
11. Afisa afya mazingira daraja II nafasi 10
12. Afisa afya mazingira msaidizi daraja II nafasi 15
13. Mtoa tiba kwa vitendo daraja II nafasi 4
Waombaji watakaochaguliwa watapangiwa hospitali za rufaa za mikoa ya Kigoma, Katavi, Sumbawanga, Songea, Njombe, Ruvuma, Mtwara, Lindi, Simiyu, Geita, Shinyanga, Ttabora, Singida, Manyara, na Mara.
Maeneo mengine ni Hospitali ya Kanda ya Chato, na Mtwara. Hospitali ya magonjwa ambukizi Kibbong’oto na vyuo vya afya.

Muda wa kutuma maombi haya ni ndani ya wiki mbili (2) tangu tarehe ya kutoka kwa Tangazo hili. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 04 Mei, 2023 saa 5:59 Usiku. Maombi yote yawasilishwe kupitia mfumo wa ajira wa Wizara unaopatikana kupitia tovuti www.ajira.moh.go.tz.
Waombaji wote mnakumbushwa kuwa makini mnapowasilisha maombi kuhakikisha umejaza vizuri vipengele vyote vinavyotakiwa kwenye mfumo ikiwa ni pamoja na kuzingatia maelekezo ya kwenye tangazo kuambatisha nyaraka zote zinazohitajika.

WAKAZI wa Mtaa wa Mkapa Kata ya Igoma wilayani Nyamagana mkoani Mwanza, wameiomba serikali kupeleka wataalamu wa miamba ...
21/04/2023

WAKAZI wa Mtaa wa Mkapa Kata ya Igoma wilayani Nyamagana mkoani Mwanza, wameiomba serikali kupeleka wataalamu wa miamba katika mtaa wao ili kupasua jiwe ambalo limezua hofu baada ya kuonekana likisogea katika makazi yao.

Mke wa Askari Polisi wilayani Kiteto Nurya Mkondya pamoja na mtoto wake Joas Oscar (2) wamefariki dunia usiku wa kuamkia...
21/04/2023

Mke wa Askari Polisi wilayani Kiteto Nurya Mkondya pamoja na mtoto wake Joas Oscar (2) wamefariki dunia usiku wa kuamkia leo Aprili 21, 2023, baada ya kutokea kwa shoti ya umeme iliyopelekea taa kudondoka kitandani na kuunguza neti na godoro wakiwa wamelala.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni imeiamrisha Hospitali ya Muhimbili kuwapima watuhumiwa watatu ambao ni Noel...
21/04/2023

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni imeiamrisha Hospitali ya Muhimbili kuwapima watuhumiwa watatu ambao ni Noel Ndale Mushi, Kelvin Maliki Ngao na David Brayan Johnson k**a wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Amri hiyo imetolewa jana Aprili 20,2023 na kusainiwa na Hakimu Mkazi J. J Rugemalila.

Address

Sinza
Dar Es Salaam

Telephone

+255654429392

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Breaking News Kiswahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share