Breaking News Kiswahili

Breaking News Kiswahili Tunahabarisha, Tunaelimisha, Tunaburudisha

28/04/2024
29/02/2024

Jiunge hapa upate Habari kila zinapojiri

Makomandoo wa JWTZ
13/01/2024

Makomandoo wa JWTZ

Indonesia ndilo taifa ambalo linakisiwa kuwa na watu wakarimu zaidi duniani ikifuatiwa na  Ukraine na Kenya ikishika naf...
09/11/2023

Indonesia ndilo taifa ambalo linakisiwa kuwa na watu wakarimu zaidi duniani ikifuatiwa na Ukraine na Kenya ikishika nafasi ya tatu katika ngazi ya dunia.

Hii ni kwa mujibu wa wakfu wa kutoa misaada ya kibinadam wa The Charities Aid Foundation (CAF).

Je umewahi kumsaidia mgeni au kujitolea muda wako kwa ajili yake?

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limegundua eneo jipya lenye kivutio cha kipekee cha Utalii ndani ya Hifadhi ya Taif...
26/10/2023

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limegundua eneo jipya lenye kivutio cha kipekee cha Utalii ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambalo limepambwa na nguvu za asilia (Natural Pillars).

Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Ruaha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Godwell Meing’ataki amesema jitihada za kulitangaza eneo hilo zimeanza ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ili kuvutia watalii wengi zaidi na wawekezaji kutembelea na kuwekeza katika aina hiyo mpya ya Utalii.

Kamishna Meing'ataki amesema TANAPA inafanya taratibu za kuwaalika watafiti mbalimbali wa miamba, udongo na Malikale (Archiolojia) wa ndani na nje ya nchi ili kubaini na kupata taarifa sahihi za malikale zilizopo, taarifa ambazo zitalitambulisha eneo hilo kimataifa.

Eneo hilo ambalo limepewa jina la "Ruaha Magic Site", mandhari yake inafanana na masalia ya zana za Mawe mithili ya zile zilizotumika Zama za Mawe za Mwanzo.

Msanii wa muziki wa Hip-hop kutoka Nchini Marekani 🇺🇸, Lil Wayne amewajia juu viongozi wa makumbusho waliochonga sanamu ...
26/10/2023

Msanii wa muziki wa Hip-hop kutoka Nchini Marekani 🇺🇸, Lil Wayne amewajia juu viongozi wa makumbusho waliochonga sanamu lenye taswira yake. Msanii huyo amewaambia kuwa sanamu hilo wamekosea na sio yeye, wajitahidi kufanya marekebisho.

"Samahani, makumbusho ya Cire, lakini si mimi! Ila mmejaribu na ninashukuru kwa juhudi" amesema Lil Wayne.

Toa maoni yako

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria akipokea taarifa ya Kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kinacho...
26/10/2023

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria akipokea taarifa ya Kikao cha 77 cha Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kinachoendelea jijini Arusha katika kumbi za AICC kutoka kwa viongozi wa menejimenti ya wizara wanaosimamia kikao hicho.

Katibu wa NEC itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Paul Makonda amewataka viongozi na wanachama wa chama hicho...
26/10/2023

Katibu wa NEC itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Paul Makonda amewataka viongozi na wanachama wa chama hicho kumpa ushirikiano katika majukumu yake mapya ndani ya CCM.

Makonda aliyewahi kuwa Mkuu wa mkoa wa Dare es salaam kuanzia 2016 hadi 2021, ameyasema hayo leo Oktoba 26, 2023 katika ofisi ndogo za chama hicho zilizombo Mtaa wa Lumumba Kariakoo jijini Dar es salaam wakati wa makabidhiano ya ofisi kutoka kwa mtangulizi wake Sophia Mjema.

Katika hatua nyingine Makonda amesema yuko tayari kufundishwa, kushauriwa na kuelekezwa ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa weledi kwa manufaa ya chama hicho na taifa zima.

MSITUMIE MATE WAKATI WA TENDO LA NDOA"Sio salama kutumia mate k**a kilainishi wakati wa tendo la ndoa kwa sababu kuna vi...
26/10/2023

MSITUMIE MATE WAKATI WA TENDO LA NDOA

"Sio salama kutumia mate k**a kilainishi wakati wa tendo la ndoa kwa sababu kuna vijidudu ambavyo vipo katika mate, kwa hiyo vinatakiwa vikae huko huko havitakiwi kuhamishwa sehemu nyingine. Ukivipeleka sehemu za siri unaweza kusababisha changamoto nyingine". Dkt. Baya Kissiwa, Mtaalamu wa Afya ya Uzazi kutoka hospitali ya Amana, Dar es Salaam

16/06/2023
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),  Mhe. Angellah Kairuki amekabidhi magari...
21/04/2023

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Angellah Kairuki amekabidhi magari 25 ikiwa ni sehemu ya Magari 200 yaliyoagizwa kupitia mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) kwa ajili ya Maafisa Elimu Sekondari wa Halmashauri zote nchini.
Pia ameahidi kujenga bweni la wanafunzi wa kiume wa shule ya sekondari Kibasila ikiwa ni ahadi kutoka kwa Mheshimiwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza mkoani Dar es Salaam katika hafla ya ugawaji wa magari hayo Mhe. Kairuki
aliwataka Wakala wa Ununuzi Serikalini (GPSA) kukakamilisha upatikanaji wa magari mengine 105 yaliyosalia kwa ajili ya mafisa elimu hao.
"Katika Halmashauri 184 zinazotakiwa kupata magari, Halmashauri 51 tayari zimepata katika awamu ya kwanza, awamu ya pili 19 na hii awamu ya tatu magari 25 hivyo bado magari 105 kwa maofisa hayo," alisema.
Aidha, ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuboresha elimu na maslahi ya walimu nchini hivyo aliwataka maofisa hao wawe wabunifu kusimamia shughuli za Kielimu na kuhakikisha kuwa Ubora wa Elimu unaimarika.
Mhe. Kairuki amesema elimu ya sekondari inahitaji uwajibikaji na huwezi kupata mafanikio pasipo kuwa na ubunifu na bidii kwa watumishi hivyo Serikali inaendelea kufanya maboresho lakini pia wasimamizi nao watekeleze wajibu wao.
Amewataka Maafisa hayo kutumia magari hayo kuongeza ufanisi wa shughuli za Kielimu na pia yatunzwe ili yaweze kudumu kwa muda mrefu.

Address

Sinza
Dar Es Salaam

Telephone

+255654429392

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Breaking News Kiswahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share