12/06/2026
FAIDA NA MATUMIZI YA MAJINA 28
YA BARHATIH
3.TATILIYH
1.KUMUHAMISHA MTU DHWALIMU /ADUI YAKO KATIKA NYUMBA YAKO.
Liandike jina hili katika kitu kilichokigumu mfano ubao kwa idadi ya mara 13 ,kisha lisomee jina hilo hilo kwa idadi ya mara 13,kisha nenda kafukie au kuzika katika nyumba yako kwa manuizi ya kuhitaji kumuhamisha mtu dhalimu au audui yako unayehitaji aondoke katika eneo lako.Inshaallah adui huyo ataondoka yeye mwenyewe kwa idhini ya mwenyezimungu
2.KUPATA UTAJIRI WA HALALI NA MAISHA YENYE KURIDHISHA.
Mwenye kusoma jina hili kwa idadi ya mara 70 kwa muda wa siko 40 mfululizo inshaallah mwenyezimungu atamruzuku utajiri wa halali na maisha yenye kuridhisha kabla mtu huyo hajafa.
3.KUONDOA MIGOGORO NA MAGOMVI NDANI YA NYUMBA AU KATIKA NDOA.
Iwapo k**a kumekosekana maelewano au kuna ugomvi baina ya mke na mme ,basi liandike jina hili katika karatasi nyeupe kwa kutumia wino wa dhafarani iliyochanganywa na miski kwa idadi ya mara 70, kisha apewe mmojawapo wa wanandoa aibebe ile karatasi kichwani,(k**a ni mwanamme ataiweka kichwani kisha atavaa na kofia na k**a ni mwanamke ataiweka kichwani kisha atavalia na ushungi juu yake) inshaallah ugomvi huo utakwisha.
4. KUONDOA MAUZAUZA NDANI YA NYUMBA.
K**a ndani ya nyumba kuna mauzauza au vituko vya kishirikina visivyojulikana basi tamka majina haya matatu kwa idadi ya mara 100 huku ukiwa unachoma Bukhuri shari au chumvi ya mawe BARHATIH, KARIYR ,TATILIYH inshaallah mauzauza yatakwisha.
Unaweza kufatilia somo hili kwa kina zaidi katika kitabu changu cha "UTUKUFU WA MAJINA 28 YA BARHATIH" No. 1
kitabu hiki bei yake ni Tsh 15,000/=
UKikihitaji kitabu hiki wakati wowote utalipia pesa hiyo kisha utatumiwa kitabu hicho kwa njia ya whatApp au email (kitabu kipo katika mfumo wa PDF
Namba za kufanya malipo ni
+255782010104
+255764010104
+255672410104
Jina katika namba zote ni BASHIRI HUSSEN LUGAMBA.
Namba hizo zote zinapatikana whatsApp