12/09/2025
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi nchini, ACSP Pius Lutumo, amesema hayo wakati wa mapokezi ya magari zaidi ya kumi na sita yaliyotolewa kwa ajili ya shughuli za doria na ulinzi.
Kupatikana kwa magari hayo, amesema, kutasaidia kukabiliana na uhalifu na wahalifu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.
Jeshi la Polisi mkoani Mara linaendelea na operesheni na doria usiku na mchana ili kuhakikisha vitendo vya uhalifu vinadhibitiwa kikamilifu katika wilaya zote.