Mediawireexpress

Mediawireexpress Your News Hub for Uncovering Africa's untold narratives , one video at a time .

28/11/2025

M***i wa Tanzania, Sheikh Dk. Abubakar Zubeir, na Waziri wa Mambo ya Kiislamu wa Saudi Arabia, Dk. Abdullatif bin Abdulaziz Al-Sheikh, wamesaini mkataba wa ushirikiano mjini Riyadh.

Mkataba huo unalenga:

Kuimarisha elimu ya Kiislamu kupitia semina, warsha na mikutano.
Kubadilishana wataalamu wa mihadhara, waalimu wa madrasa na wasomi wa fiqhi.
Kuimarisha taasisi za Kiislamu na usimamizi wa misikiti.
Kuchapisha na kusambaza machapisho ya kielimu ili kuimarisha uelewa wa Uislamu wa wastani.

Viongozi hao wamesema ushirikiano huu utaimarisha maadili, amani, umoja na maendeleo katika jamii za nchi zote mbili.

28/11/2025

Kijana ahoji matumizi makubwa ya serikali Mbeya: apendekeza fedha zielekezwe kwa wananchi

Wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka mkoani Mbeya, kijana mmoja amehoji hadharani matumizi makubwa ya magari ya viongozi, akieleza kuwa fedha hizo zingetumika kuboresha maisha ya wananchi.

Akiwa katika viwanja vya Kabwe, Mbeya Mjini Novemba 26, 2025, kijana huyo alisema:
"Ushauri wangu binafsi, matumizi ya serikali yamekuwa makubwa sana. Kwa mfano tu Mheshimiwa Waziri, gari yako nimeiangalia haishuki chini ya milioni 500. Sasa, tafuta Cruiser ya kawaida, hizo fedha zingine ziende kwa wananchi."

28/11/2025

Vijana jijini Mbeya wametoa wito kwa serikali kuhakikisha wanashirikishwa kikamilifu katika mchakato wa kupatikana kwa Katiba Mpya, wakisema Katiba ya sasa ya mwaka 1977 haiakisi mahitaji ya kizazi cha sasa. Wamesisitiza kuwa Katiba Mpya ni hitaji muhimu kwa maendeleo ya vijana na taifa kwa ujumla, kwani itawapa nafasi ya kushiriki kikamilifu katika uamuzi wa masuala yanayowahusu.

28/11/2025

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema yupo tayari kuitwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma juu ya tuhuma dhidi yake za umiliki wa vituo vya mafuta vya Lake Oil.

Ameyasema hayo alipokuwa akiongea na watumishi wa wizara hiyo Novemba 26, 2025 akieleza kuwa ni vyema taarifa za watumishi wa umma zikawa wazi na pale panapokuwa na walakini waweze kuhojiwa na taarifa ziwekwe hadharani ili umma uwe na taarifa sahihi. "malalamiko juu ya viongozi yamekuwa mengi sana haijulikani lipi ni kweli lipi si kweli"

"Ndugu zangu kwa mfano maandamano yaliyotokea juzi hapa malalamiko yalikuwepo makubwa juu ya maadili ya viongozi ...kuna mtu mmoja anaitwa Ali Edha ana petrol station zake zinaitwa lake oil zimechomwa kwa sababu zinasemwa ni za Ridhiwani" amesema

Ridhiwani aliongeza akiitaka tume hiyo kumuita bila hofu ili kumhoji lakini pia akipendekeza wafanye uchunguzi kwanza wakikamilisha waitishe mkutano na waandishi wa habari na waombe ushahidi mwingine wa ziada kwa umma ikiwezekana.

Video Credit:

28/11/2025

Mkutano wa Mgombea Urais wa Uganda kupitia Chama cha National Unity Platform(NUP), Robert Kyagulanyi Ssentamu(Bobi Wine) uliokuwa ukifanyika eneo la Bbaale nchini humo umeshindwa kumalizika vyema baada ya askari wa Jeshi la Polisi kurusha mabomu ya machozi kitendo kilichowafanya wafuasi waliojitokeza kulazimika kuondoka.

Bobi Wine alipoona hali hiyo ya mabomu ya machozi alianza kuwaambia wananchi waondoke huku akisema yeye atabaki na kuwa wa mwisho kuondoka kwani anataka dunia ione kinachoendelea nchini humo.

Katika sehemu ya maneno yake alimrushia shutma Mkuu wa Operesheni za Polisi Uganda, Frank Mwesigwa akieleza kuwa afisa huyo akishirikiana na Rais Museveni(ambaye ni mgombea Urais pia wa Chama cha NRM) wanafanya vitendo hivyo ili kumkwamisha katika mkutano wake huo ambao alieleza kuwa ulipangwa kufanyika kihalali.

"Nataka dunia ione polisi wa Uganda wametumwa na Frank Mwesigwa kuhakikisha sizungumzi na wananchi wa Uganda"

28/11/2025

Leo, Ijumaa Novemba 28.2025, Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi yaliyokuwa yamewasilishwa Mahak**ani hapo na Said Issa Mohamed (aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar) na wenzake wawili (2) dhidi ya Viongozi waandamizi na makada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake wa Tanzania Bara John Heche

Maombi hayo yaliyofunguliwa Oktoba 03 mwaka huu yalikuwa yanadai kuwa washtakiwa wamekiuka amri ya Mahak**a Kuu iliyotolewa Juni 10.2025 kupitia kesi ya madai namba 8960/2025 inayosikilizwa chini ya Jaji Hamidu Mwanga, ambapo washtakiwa wake ni Katibu Mkuu na Bodi ya Wadhamini wa CHADEMA

Pamoja na mambo mengine, katika uamuzi wake Jaji Awamu Mbagwa amesema Mahak**a imekubaliana na moja ya mapingamizi yaliyowasilishwa na upande wa utetezi ikiwemo lile lililokuwa linaeleza kuwa Mahak**a hiyo haina uwezo wa kisheria wa kusikiliza maombi hayo kutokana na kwamba yamewasilishwa nje ya muda uliotajwa kisheria

Amesema amri inayohusu marufuku kwa CHADEMA kujihusisha na shughuli zozote za kisiasa na kiutendaji imetolewa Juni 10 mwaka huu, lakini kwa mujibu wa waleta maombi wanasema mshtakiwa wa kwanza John Heche 'alihutubia' Juni 17 mwaka huu, na maombi ya kudharau amri ya Mahak**a yamewasilishwa Mahak**ani hapo Oktoba 03 mwaka huu, ambapo siku 106 baadaye suala ambalo linakinzana na matakwa ya sheria inayotaka maombi ya aina hiyo yawasilishwe ndani ya siku 60,

Akiwa Mahak**ani hapo, Wakili Hekima Mwasipu akawaeleza wanahabari kinagaubaga kuhusu undani wa maamuzi hayo ya Mahak**a

28/11/2025

Kampuni ya GSM Group imeandika historia mpya baada ya kupokea magari 100 ya kubeba mafuta (petroleum tankers) aina ya HOWO Max 400, ikiwa ni awamu ya kwanza ya mpango wao wa kuongeza uwezo wa usafirishaji nchini.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya magari hayo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa GSM, Benson Mahenya, alisema kampuni hiyo inatarajia kupokea awamu ya pili ya magari 100 ndani ya siku 21 zijazo. Hatua hiyo inalenga kutimiza lengo la kuwa na magari 200 ya mafuta kabla ya mwaka 2025 kuhitimishwa.

Mahenya alibainisha kuwa GSM ndiyo kampuni ya kwanza nchini kuingiza magari ya aina ya HOWO Max 400 yaliyotengenezwa maalum kwa ajili ya kubeba mafuta, hatua inayoongeza chachu kwenye ukuaji wa sekta ya usafirishaji Tanzania.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, TMA, inabainisha kuwa maeneo mbalimbali nchini yanatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, vip...
27/11/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, TMA, inabainisha kuwa maeneo mbalimbali nchini yanatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, vipindi vya jua, na mvua katika maeneo machache, hasa mikoa ya Kagera, Mwanza, Geita, Shinyanga, Simiyu, Mara, Kigoma na Tabora.

Mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga, Unguja na Pemba inatarajiwa kuwa na mvua nyepesi na vipindi vya jua.

Mikoa ya Morogoro, Dodoma, Singida, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Rukwa, Mbeya, Njombe, Iringa, Songwe na Lindi: Hali itakuwa ya mawingu kiasi na jua. Viwango vya joto vitakuwa kati ya 23 hadi 33°C katika miji mikuu, huku mawio na machweo yakibaki katika wastani wa saa za kawaida.

Upepo wa pwani utavuma kwa kasi ya km 20 kwa saa, kutoka Kusini Mashariki kwa Pwani ya Kaskazini na Kaskazini Mashariki kwa Pwani ya Kusini.

27/11/2025

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imefungua dirisha maalum la mwaka mmoja kwa Watanzania kufanya marekebisho ya taarifa zao za utambulisho wa taifa, ikiwa ni hatua ya kwanza kubwa ya usafi wa kumbukumbu tangu mfumo huo uanze kutumika.

Tangazo hilo limetolewa tarehe 27 Novemba 2025 na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, James Kaji, aliyeeleza kuwa kwa muda mrefu kumekuwapo maombi mengi ya mabadiliko ya taarifa ambayo hayakufanyiwa kazi kutokana na kutokidhi matakwa na taratibu zilizokuwapo awali.

Kwa mujibu wa Kaji, baadhi ya maombi yaliyoshindikana kuweza kushughulikiwa ni ya watu waliotumia nyaraka za kughushi pamoja na wale waliojiandikisha kwa taarifa za udanganyifu walipokuwa wakipatiwa kitambulisho cha taifa.

Kaji amesema kuwa Serikali imepitisha kibali maalum cha kushughulikia maombi hayo ya mabadiliko ya taarifa ambayo awali yalizuiwa kutokana na kukinzana na miongozo ya NIDA. Kibali hicho kimetolewa kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Oktoba 2025, na zoezi litafungwa mara muda huo utakapotimia.

Dirisha hilo maalum linahusu makundi manne yafuatayo:

Waathirika wa vyeti vya kughushi – Wale waliofukuzwa katika ajira za Serikali kwa kutumia vyeti vya shule vya kughushi, ambavyo pia walivitumia kujisajili NIDA.

Watu waliotumia majina ya watu wengine kupata vyeti vya elimu.

Watu waliotoa taarifa za uongo/udanganyifu walipojisajili NIDA.

Raia wa Tanzania waliowahi kujisajili k**a wakimbizi.

Wananchi watakiwa kujitokeza na nyaraka muhimu

Mkurugenzi huyo amewataka wananchi wote wanaohusika na makundi haya kufika katika ofisi za NIDA za wilaya wakiwa na nyaraka zinazohitajika kulingana na aina ya changamoto wanazotaka kurekebisha.

Aidha, waombaji watatakiwa kuwasilisha viambatisho vya lazima pamoja na vile vya ziada watakavyoelekezwa, ikiwemo:

Nakala ya vyeti halisi vya elimu

Cheti cha kuzaliwa kilichohakikiwa na RITA

Deed poll iliyosajiliwa katika gazeti la Serikali

Nyaraka nyingine yoyote itakayohitajika na ofisi za NIDA

Kwa mujibu wa NIDA, zoezi hili ni fursa ya kipekee kwa wananchi kusahihisha taarifa zao ili kuboresha mfumo wa utambulisho wa taifa na kuepusha usumbufu wa baadaye katika upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

27/11/2025

Tanzania is facing a quiet but intensifying campaign of external political pressure, delivered not through invasions or sanctions but through diplomats, foreign-funded NGOs, religious actors, media networks and powerful Western politicians who present their interventions as “defending human rights” and “promoting good governance.” Analysts warn that beneath the language of reform lies an attempt to steer Tanzania’s internal politics and shape its future according to outside interests, a pattern increasingly recognized across Africa.

The latest tensions follow opposition campaigns, disputes around constitutional reforms and incidents of violence in which local authorities say foreign-funded activist networks played a major role. As the government attempts to stabilize the political climate, international media outlets and Western officials have issued a stream of statements portraying Tanzania as sliding into repression. Tanzanian officials counter that the same governments now warning of instability have indirectly financed groups that contributed to the unrest.

27/11/2025

Kumekuwa na ongezeko la sauti kutoka katika nchi za Kusini mwa Dunia zikizusha maswali kuhusu uhalali wa juhudi zinazoongozwa na mataifa ya Magharibi kusukuma mbele mpango wa amani wa vita vinavyoendelea nchini Ukraine Wakosoaji wanasema mpango huu unaonesha tofauti kubwa katika namna Marekani na Ulaya zinavyoshughulikia migogoro duniani, hususan inapolinganishwa na mizozo inayohusisha washirika wao.

Wachambuzi kutoka Afrika, Asia na Amerika ya Kusini wanabainisha kuwa mpango huo hauonekani k**a jitihada huru za kusitisha vita, bali k**a mkakati wa kisiasa unaolenga kuhifadhi ushawishi wa Magharibi. Wanataja kuwa kiwango k**a hicho cha shinikizo la kidiplomasia, vikwazo na harakati za kimataifa hakikuonekana katika mizozo ya Gaza, Yemen, Libya, Iraq na eneo la Sahel.

27/11/2025

Tanzania inakabiliana na kile wachambuzi wanasema ni kampeni ya kimya lakini inayoongezeka ya shinikizo la kisiasa kutoka nje si kwa kutumia nguvu za kijeshi au vikwazo vya kiuchumi, bali kupitia wanadiplomasia, NGO zinazopokea fedha kutoka nje, taasisi za dini, mitandao ya vyombo vya habari vya kimataifa na wanasiasa wenye nguvu wa Magharibi.

Wanafanya hivyo kwa kudai kuwa wanatunza haki za binadamu na kukuza utawala bora. Hata hivyo, wataalamu wanawaonya kuwa nyuma ya lugha ya mageuzi kuna lengo la kuunda siasa za ndani za Tanzania ili ziendane na maslahi ya nje, muundo unaoonekana barani

Address

Samora Avenue
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mediawireexpress posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mediawireexpress:

Share