Mediawireexpress

Mediawireexpress Your News Hub for Uncovering Africa's untold narratives , one video at a time .

12/09/2025

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi nchini, ACSP Pius Lutumo, amesema hayo wakati wa mapokezi ya magari zaidi ya kumi na sita yaliyotolewa kwa ajili ya shughuli za doria na ulinzi.

Kupatikana kwa magari hayo, amesema, kutasaidia kukabiliana na uhalifu na wahalifu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Jeshi la Polisi mkoani Mara linaendelea na operesheni na doria usiku na mchana ili kuhakikisha vitendo vya uhalifu vinadhibitiwa kikamilifu katika wilaya zote.

12/09/2025

Video kutoka Nepal zimeenea kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha mawaziri na familia zao wakijaribu kuokoa maisha kwa kushikilia helikopta wakati maandamano dhidi ya serikali yakizidi kushika kasi.

Taswira hizo za taharuki zimeibua mshangao na ghadhabu miongoni mwa wananchi, huku wengi wakielezea tukio hilo k**a kielelezo cha serikali iliyoshindwa kudhibiti hasira ya umma. Katika video hiyo, maafisa wa serikali wanaonekana wakipanda helikopta kwa haraka huku wengine wakishikilia kwa hofu wakijaribu kutoroka eneo la maandamano.

Wakati picha hizo zikisambaa kwa kasi, wananchi na viongozi wa upinzani wamekuwa wakilaani hatua hiyo, wakisema ni ishara ya wazi kuwa serikali imeshindwa kuandaa mikakati ya kudhibiti maandamano na kuwalinda wananchi.

Tukio hilo limezidisha miito ya uwajibikaji kutoka kwa viongozi wa juu serikalini, huku wachambuzi wa siasa wakilitaja k**a fedheha kubwa kwa uongozi wa Nepal katika kipindi hiki kigumu cha mgogoro wa kisiasa.

Waandamanaji nchini humo wamekuwa wakionyesha hasira dhidi ya uongozi wa serikali, wakipinga ukosefu wa maandalizi, sera dhaifu na kile wanachoeleza k**a uongozi usiojali maslahi ya wananchi.

12/09/2025

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ameiagiza Wizara ya Maji kuacha kuwabambikizia wananchi bili za maji, na kuwataka wananchi kukataa kulipa bili ambazo hawajazitumia.

Aweso ametoa agizo hilo wakati akihutubia wananchi katika uzinduzi wa kampeni za mgomea udiwani Kata ya Kariakoo, Haji Manara zilizofanyika jijini Dar es Salaam, huku akisisitiza kuwa wizara hiyo itatumia mfumo mpya wa kusoma bili wa 'Pre Paid Meter' k**a TANESCO.

""Bili za maji zisiwe bambikizi, k**a mwananchi ametumia bili ya 20,000 unamwambia alipe 160,000 k**a anakiwanda 'Hapana' usikubali. Wizara ya Maji inafanya mageuzi na tumekwishaianza badala ya msoma mita kuja kusoma mita umelala na mumeo umepumzika nakuja ngo ngo ngo aah hiyo hatuwezi kukubali, tunakwenda katika mfumo wa kutumia 'Pre Paid Meter' k**a TANESCO" amesema Aweso.

12/09/2025

Watu sita wamefariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea jana katika Kijiji cha Buganjo, wilayani Rorya, mkoani Mara, baada ya gari dogo aina ya Succeed lenye namba za usajili T 625 DYV kugonga roli lenye namba T 857 BRX lililokuwa limepaki kando ya barabara.

12/09/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuboresha miundombinu ya usafiri na mwanga mkoani Tabora endapo atachaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akihutubia maelfu ya wananchi leo, Ijumaa Septemba 12, 2025, kwenye viwanja vya Ipuli, Tabora Mjini, Dkt. Samia amesema serikali yake itajenga madaraja 133 na barabara mbalimbali za kimkakati mkoani humo, sambamba na kufunga taa 2,300 ili kuruhusu shughuli za kiuchumi kufanyika muda wote.

“Tabora na wilaya zake zitapata fursa ya kufanya biashara kwa masaa 24 kwa sababu umeme ni usalama, umeme ni mwanga na unasaidia kwenye uzalishaji. Tunapoweka taa, tunatoa fursa vijana wetu wafanye kazi kwa saa 24,” amesema Dkt. Samia.

Amesisitiza kuwa dhamira ya CCM ni kuhakikisha Tabora inakuwa kitovu cha maendeleo kupitia uboreshaji wa barabara, madaraja na miundombinu ya umeme, huku akiwataka wananchi wa mkoa huo kuendelea kuamini na kuiunga mkono serikali ya chama hicho.

Hotuba hiyo ilihitimisha ziara yake ya kampeni mkoani Tabora, ambapo k**a ilivyokuwa katika mikoa mingine, Dkt. Samia amewaeleza wananchi mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka minne na nusu ya uongozi wake, pamoja na ahadi anazokusudia kutekeleza kwa miaka mitano ijayo iwapo atachaguliwa.

12/09/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa endapo atachaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, serikali yake itaendelea kuimarisha sekta za kilimo na mifugo kupitia ruzuku na miundombinu ya kisasa.

Akizungumza leo Ijumaa, Septemba 12, 2025, mbele ya wananchi wa Ipuli, mkoani Tabora, wakati akihitimisha mikutano yake ya kampeni mkoani humo, Dkt. Samia amesema serikali ya CCM itaongeza ruzuku za mbolea, pembejeo na chanjo kwa wakulima na wafugaji, sambamba na kuboresha na kujenga minada mipya pamoja na majosho kwa ajili ya wafugaji.

Aidha, ameahidi kushughulikia changamoto ya upatikanaji wa maji mkoani Tabora, akibainisha kuwa azma yake ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya maji safi na salama bila kujali anakaa wapi.

Vilevile, amewataka vijana wa Tabora kujiandaa kutumia ipasavyo fursa za ajira zinazotokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kitaifa, ikiwemo ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda, kwenda Chongoleani, Tanga, akisisitiza miradi hiyo imekuwa chachu ya ajira nyingi kwa vijana nchini.

Timu ya kulenga shabaha ya Polisi wanawake inayoshiriki katika mashindano ya Michezo ya Majeshi (BAMMATA), Septemba 10, ...
12/09/2025

Timu ya kulenga shabaha ya Polisi wanawake inayoshiriki katika mashindano ya Michezo ya Majeshi (BAMMATA), Septemba 10, 2025 imefanikiwa kuwa mshindi wa kwanza katika mashindano hayo yaliofanyika katika kambi ya Jeshi la Wananchi Chukwani Zanzibar.

Mchezo huo wa shabaha ulikuwa wa kutumia silaha aina ya Pistol na Riffle.

Timu ya Polisi Wanawake imeweza kuibuka mshindi wa kwanza kwa kuchukua medali tatu ambazo ni fedha mbili na dhahabu moja.

Aidha, timu hiyo ya Polisi Wanawake iliyoongozwa Sajenti Irene ambaye ni Mshindi medali ya dhahabu kwa Pistol, Koplo Salvina Mshindi wa medali ya fedha kwa Pistol na Koplo Neema Mshindi mdali ya fedha Riffle.

Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanu...
12/09/2025

Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, amewasili mkoani Arusha leo Ijumaa Septemba 12,2025 na kuendelea na mikutano yake ya kampeni akitokea Mkoa wa Katavi.

Mara baada ya kuwasili jijini humo,Balozi Dkt.Nchimbi ataelekea Wilayani Longido,Jimbo la Longido ambako atawahutubia Wananchi wa jimbo hilo na kuwanadi Wagombea Ubunge wa majimbo ya Mkoa huo,akiwemo mgombea Ubunge wa jimbo la Longido ,Dkt Steven Lemomo Kiruswa pamoja na Madiwani.

Dkt. Nchimbi ameendelea kuinadi Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030,ambayo kimsingi imelenga kwenda kuboresha maisha ya wananchi na ustawi wa Maendeleo katika miaka mitano ijayo.

Aidha,amekuwa akitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kumchagua mgombea Urais wa CCM,Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan, Wabunge na Madiwani wa Chama hicho kwa kura za kishindo ifikapo Oktoba 29,2025

Rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen, ametangaza pendekezo la kuiwekea Israel vikwazo na kusitisha sehemu ya bias...
12/09/2025

Rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen, ametangaza pendekezo la kuiwekea Israel vikwazo na kusitisha sehemu ya biashara yake na Umoja wa Ulaya. Hii imekuja wakati hasira za kimataifa zikiongezeka kuhusu mashambulizi ya Israel nchini Qatar na Yemen, pamoja na njaa inayoendelea kulazimishwa dhidi ya Wapalestina wa Gaza.
Katika hotuba yake ya kila mwaka ya Hali ya Umoja wa Ulaya mjini Strasbourg, Ufaransa, von der Leyen alisema:
“Yale yanayotokea Gaza yameutikisa moyo wa dunia. Watu wanauawa wakiwa wanabembeleza chakula. Akina mama wakiwa wanabeba watoto waliokufa. Picha hizi ni za maafa kabisa. Kwa ajili ya watoto, kwa ajili ya ubinadamu — hili lazima likome.”
Von der Leyen alisisitiza kwamba njaa haiwezi kutumika k**a “silaha ya vita”.
Mapendekezo ya Vikwazo
Kusitisha usaidizi wa moja kwa moja wa Umoja wa Ulaya kwa serikali ya Israel.
Kusimamisha ufadhili wa miradi ndani ya Israel (isipokuwa kazi zinazohusiana na asasi za kiraia na kituo cha ukumbusho wa Holocaust).
Kuwalenga mawaziri wa Israel “wanaoitwa wakali” kwa vikwazo binafsi.
Kufikiria kusimamisha sehemu ya makubaliano ya biashara ya EU na Israel.
Hata hivyo, hatua kubwa zaidi zitahitaji kura kutoka nchi wanachama wa EU, jambo linaloweza kukutana na upinzani.
Marekani
Wakati huo huo, nchini Marekani, wanasiasa wa mrengo wa kushoto na wanaharakati wanaendelea kusukuma juhudi za kufuta uuzaji wa silaha kwa Israel na kukomesha ushiriki wa Marekani katika kile wanachokiita mauaji ya halaiki ya Gaza. Lakini shinikizo hili limeendelea kugonga mwamba kutokana na upinzani wa “hali ya kawaida” ya kisiasa Washington.

12/09/2025

Wananchi wanazidi kusogea uwanja wa mkapa

12/09/2025

Wananchi wa Kijiji cha Katuma Kitongoji cha Mwikang’ombe wamelalamika kuhusu changamoto ya usafiri wa barabara ya kutoka Mnyagala- Mwikang’ombe kwenda Kayenze yenye urefu wa Km 9.86 ambapo imekuwa ni kikwazo kikubwa kwa wanaanchi ambao wanatumia barabara hiyo kila siku hali inayosababisha baadhi ya wanawake wajawazito kushindwa kupata huduma kwa wakati.

Kufuatia kero hiyo Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi Onesmo Buswelu amechukizwa na kitendo hicho cha Mkandarasi kuchelewesha ukamilishaji wa ujenzi na kumuagiza Mkandarasi huyo kukamilisha ujenzi wa kalavati na kivuko cha muda kinachotumiwa na wananchi kuvuka kwenda upande wa pili, kisha kuendelea na ujenzi wa barabara yote.

Pia ameongeza kwa kumtaka Mkandarasi mkuu mwenye mkataba kufika eneo la mradi na kusimamia mafundi, ili wafanye kazi usiku na mchana ili kukamilisha mradi huo kwa wakati.

Barabara hiyo yenye gharama ya Shilingi Milioni 602,85 itakapokamilika inatarajiwa kufungua njia ya Mnyagala kwenda kata ya Katuma hali itakayochochea kasi kubwa ya usafirishaji wa raia na mazao mbalimbali.

12/09/2025

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema halitasita kuchukua hatua kali dhidi ya mtu yeyote atakayebainika kuhusika na wizi au uharibifu wa miundombinu ya umeme, kwani vitendo hivyo ni uhujumu uchumi vinavyosababisha hasara kubwa kwa Shirika na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Usalama Mwandamizi wa TANESCO, Bw. Steven Maganga, katika zoezi la ukaguzi wa mita lililofanyika Magomeni, Mburahati jijini Dar es Salaam.

Katika ukaguzi huo, TANESCO ilibaini baadhi ya wateja kufungua mita na kuweka vifaa maalumu (Resistor) vinavyopunguza kasi ya usomaji wa matumizi halisi ya umeme.

“Tumembaini mteja ambaye ameharibu miundombinu kwa makusudi kwa kufungua mita na kuweka Resistor ili kupunguza usomaji wa matumizi tofauti na hali halisi,” alisema Bw. Maganga.

Address

Samora Avenue
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mediawireexpress posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mediawireexpress:

Share