28/11/2025
M***i wa Tanzania, Sheikh Dk. Abubakar Zubeir, na Waziri wa Mambo ya Kiislamu wa Saudi Arabia, Dk. Abdullatif bin Abdulaziz Al-Sheikh, wamesaini mkataba wa ushirikiano mjini Riyadh.
Mkataba huo unalenga:
Kuimarisha elimu ya Kiislamu kupitia semina, warsha na mikutano.
Kubadilishana wataalamu wa mihadhara, waalimu wa madrasa na wasomi wa fiqhi.
Kuimarisha taasisi za Kiislamu na usimamizi wa misikiti.
Kuchapisha na kusambaza machapisho ya kielimu ili kuimarisha uelewa wa Uislamu wa wastani.
Viongozi hao wamesema ushirikiano huu utaimarisha maadili, amani, umoja na maendeleo katika jamii za nchi zote mbili.