06/03/2026
Ameandika Mtangazaji wa (Crown Fm)
Mwanadada โJesca Mhagamaโ Kuhusu Klabu ya Simba na Mashabiki Wake Juu ya Mchezaji wao wa Zamani โMohamed Hussein Zimbwe Jrโ ๐๐ผ
Kitu pekee nachofahamu Mohamed Hussein anatakiwa kuheshimiwa na kila aliyeshabiki wa mpira wa nchi hii.
Mohamed Hussein amekuwepo Tanzania akiitumikia timu ya Taifa lakini pia kwa mapenzi makubwa na Taaluma ya hali ya Juu ameitumikia Simba kwa zaidi ya muongo 1, akiisaidia Simba kuchukua makombe na hata kwenye nyakati ngumu pia alikuwepo,
Mkimkosoa na kumpopoa MSISAHAU kuibakiza Heshima ambayo ameitengeneza kwa miaka yote aliyoishi katika Soka,
MSISAHAU Mohamed Hussein hakukata tamaa nyakati zote hata misimu 4 ambayo Simba ilikosa Ubingwa alikuwepo hapo,
MSISAHAU kuwa wengine walionekana kuchukulia kawaida tu kila kilichokua kinatokea miaka hiyo 4 lakini Mohamed Hussein alijidhihiridha kwa namna gani anatamani mazuri kwa namna alivyojituma
MSISAHAU lile chozi aliloangusha pale Benjamin mkapa wakati Simba inachapwa goli 5 vs Yanga! Sio kwa sababu alijisikia tu! La hasha ni kwasababu alitamani mazuri zaidi kwa Club aliyokua anaitumikia ,
MSISAHAU kuwa wala hakua miongoni mwa wale mliokua mnawataja kuwa ni maduka,
MSISAHAU alivyowaongoza kunyanyua makwapa kwa jasho alilovuja uwanjani akiwa na wenziwe,
MSISAHAU kumpa heshima yake k**a Legend.
MSISAHAU kuwa Mohamed Hussein si Mtu wa maneno maneno kukaa kwake kimya bila kusema lolote mara zote mishale inaporushwa upande wake haimaanishi hakuna inayomuingia na kumuumiza k**a binadamu,
MSISAHAU kuwa Mohamed Hussein yupo kazini k**a wewe unavyoweza kuhama kituo chako cha kazi vivyo hivyo kwake.
MSISAHAU hata hivyo mnavyokubali moyoni na hamtaki kuvisema hadharani.
NB: MSISAHAU KUWA ANASIKIA, ANAAMBIWA, ANAONA NA ANAJUA KUSEMA.