FurahaFmtz

FurahaFmtz its a radio Station situated in Dar es salaam and Zanzibar
(1)

21/07/2025

Kwa kushirikiana na wanahamasisha jamii hasa watoto, vijana, na familia kutanguliza ulaji wa matunda na mbogamboga kila siku k**a sehemu muhimu ya lishe bora na afya njema.

Sikiliza FURAHA MORNING kila siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa 12:00 kamili asubuhi mpaka saa 03:00 asubuhi Kupitia masafa ya 90.9 Furaha Fm.

Cc:

21/07/2025

Umeshawahi kukutana na changamoto gani kwenye hili

Sikiliza FURAHA MORNING kila siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa 12:00 kamili asubuhi mpaka saa 03:00 asubuhi Kupitia masafa ya 90.9 Furaha Fm.

Cc:

21/07/2025

Hawa wafyekwe ni Wanafiki?

Sikiliza FURAHA MORNING kila siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa 12:00 kamili asubuhi mpaka saa 03:00 asubuhi Kupitia masafa ya 90.9 Furaha Fm.

Cc:

20/07/2025

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

Kupitia ukurasa wake rasmi, Ahmed Ally ameandika ujumbe mara baada ya barua ya kuaga na kuishukuru Simba SC kwa Aliyekuw...
20/07/2025

Kupitia ukurasa wake rasmi, Ahmed Ally ameandika ujumbe mara baada ya barua ya kuaga na kuishukuru Simba SC kwa Aliyekuwa mchezaji wa klabu hio Mohammedi Husseini Tshabalala.

"Tuna kila sababu ya kujipongeza kwa maamuzi sahihi tuliochukua kwa Nahodha wetu kipenzi

Kwanza ifahamike kuwa tunampenda, tunamheshimu na hiyo itabaki milele

Ulikua ni muda sahihi wa Tshaba kuondoka Simba na muda sahihi wa Simba kuachana na Tshaba

Kwenye hili agano sio Simba sio Tshaba ambae amepata hasara kila mmoja amenufaika na maamuzi haya

Kwa sasa wataibuka wengi kulaumu lengo lao kuonesha kuwa Simba tumekosea pili kuwapa faraja waliomchukua na tatu ni kutufinitisha sisi na Tshaba pamoja na mashabiki

Ukweli ni kwamba tumepoteza aliyewahi kuwa mchezaji wetu bora sana

Miaka mitatu nyuma mchezaji wetu mmoja ambae pia alikua Nahodha alimaliza Mkataba, Viongozi wakaona taabu kumuachia kutokana na heshima yake tukamuongezea Mkataba wa miaka miwili

Kilichofuatia miaka yote miwili alikaa Benchi na k**a haitoshi zipo nyakati alisumbuliwa na Majeraha na akaacha kucheza na akaenda kufundisha timu ya vijana akiwa bado ana mkataba wa Uchezaji

Hayo yote yalitokea kwa sababu hatukutaka kuupokea ukweli kuwa muda wake uliisha tukabaki nae kwa sababu historia na heshima

Ndugu zangu Wana Simba kwa hili tutembee kifua mbele tumefanya maamuzi kwa kuangalia Simba bora ya kesho

Wala tusiingie ubaridi kwa kua anaenda upinzani wameshaenda wengi na hakuna maajabu

Muhimu sasa ni kuwahimiza Viongozi wetu kusajili mchezaji mwingine k**a Tshabalala au zaidi ya Tshabalala

Na hapo sina shaka na viongozi wetu watafanya hilo kwa sababu maandalizi yalishafanyika muda mrefu

Kila la heri Captain Mungu akusimamie, Sisi tunakupenda sana

Wana Simba tusonge mbele mpaka tuko salama kwa sababu hakuna kinachotokea bahati mbaya!!!"

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

Muigizaji nguli wa Bollywood, Shah Rukh Khan, amepata jeraha wakati wa kurekodi   filamu yake mpya inayosubiriwa kwa ham...
19/07/2025

Muigizaji nguli wa Bollywood, Shah Rukh Khan, amepata jeraha wakati wa kurekodi filamu yake mpya inayosubiriwa kwa hamu, "King". SRK alikuwa anashiriki kwenye tukio la mapambano katika Golden To***co Studio Mumbai kwenye moja ya kipande cha filamu hiyo ndipo alipoanguka vibaya na kupata jeraha katika uti wa mgongo
baada ya tukio hilo, SRK alisafirishwa Marekani kwa ajili ya matibabu

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesogeza mbele vikao vya uchujaji wa wagombea wa ubunge kutoka Julai 19 hadi Julai 26, 2025,...
19/07/2025

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesogeza mbele vikao vya uchujaji wa wagombea wa ubunge kutoka Julai 19 hadi Julai 26, 2025, hatua iliyotangazwa leo na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, jijini Dodoma.

"Maandalizi ya mchakato wa uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi yanaendelea vizuri, na tunaendelea na maandalizi na kikao cha mwisho cha uteuzi wa wagombea kitafanyika tarehe 28 Julai, ile Kamati Kuu ambayo ilikuwa iteue leo tarehe 19 kwahiyo uteuzi wa mwisho utafanyika tarehe 28 hapahapa Dodoma.

Na vikao vyote vya Halmashauri Kuu ya Taifa, Kamati Kuu vitafanyika Dodoma. Kwahiyo leo wengi walitarajia kwamba Kamati Kuu itafanya kikao chake na kufanya uteuzi wa mwisho kwa wale waliogombea nafasi mbalimbali kwa ajili ya kwenda kwenye kura za maoni" Amesema Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, jijini Dodoma.

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesogeza mbele vikao vya uchujaji wa wagombea wa ubunge kutoka Julai 19 hadi Julai 26, 2025,...
19/07/2025

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesogeza mbele vikao vya uchujaji wa wagombea wa ubunge kutoka Julai 19 hadi Julai 26, 2025, hatua iliyotangazwa leo na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, jijini Dodoma.

"Maandalizi ya mchakato wa uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi yanaendelea vizuri, na tunaendelea na maandalizi na kikao cha mwisho cha uteuzi wa wagombea kitafanyika tarehe 28 Julai, ile Kamati Kuu ambayo ilikuwa iteue leo tarehe 19 kwahiyo uteuzi wa mwisho utafanyika tarehe 28 hapahapa Dodoma.

Na vikao vyote vya Halmashauri Kuu ya Taifa, Kamati Kuu vitafanyika Dodoma. Kwahiyo leo wengi walitarajia kwamba Kamati Kuu itafanya kikao chake na kufanya uteuzi wa mwisho kwa wale waliogombea nafasi mbalimbali kwa ajili ya kwenda kwenye kura za maoni" Amesema Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, jijini Dodoma.

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

19/07/2025

Mauzo ya jezi mpya ya Lamine Yamal kwa sasa yamefika hadi £10 milioni sawa na bilion 30 na milion 300 za kitanzania hii ni ishara tosha kuwa kijana huyu sio tu nyota wa uwanjani, bali pia mkombozi wa biashara ya klabu.

Siku ya kutambulishwa rasmi kuwa atavaa jezi namba 10 namba ya heshima iliyowahi kuvaliwa na baadhi ya wachezaji wakubwa k**a Ronaldinho Gaucho na Lionel Messi mashabiki walimiminika madukani na jezi elfu 70 ziliuzwa ndani ya saa chache. Hiyo ni takriban £7 milioni papo hapo, maana kwa kila jezi moja ni €100. sawa na laki 3 na elfu 31 za za kitanzania

Sasa vuta picha msimu haujaanza bado na tayari Lamine Yamal ni bidhaa. na je itakuaje na awamu ya pili ya mauzo ikianza sambamba na michezo ya pre-season, kampeni ya jezi mpya, na ujio wa mechi za La Liga huenda mauzo yakazidi €20 milioni kwa jezi yake pekee.

Hili ni somo kwa Barcelona na vilabu vingine: mchezaji mwenye mvuto ndani na nje ya uwanja anaweza kugeuka kuwa mradi wa kibiashara wenye faida maradufu kuliko usajili wa mamilioni. Kwa Lamine Yamal, jezi namba 10 si tu mgongo ni nembo ya biashara.

Hans Billionea og

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

18/07/2025

Tarehe 18 Julai 1918, ulimwengu ulikuwa katika giza la vita.
Vita ya Kwanza ya Dunia ilikuwa karibu kufika ukingoni…
Lakini siku hiyo hiyo — kijiji kidogo cha Mvezo, Afrika Kusini, kilishuhudia kuzaliwa kwa mtoto wa Kiafrika aliyeandikwa kwenye historia: Rolihlahla Mandela.

Mandela, ambaye baadaye alijulikana k**a Nelson Mandela, alikua katika mazingira ya ubaguzi na dhuluma.
Aliona rangi ya ngozi yake ikigeuzwa hukumu.
Alikua katika taifa ambalo Waafrika walinyimwa haki zao…
Lakini hakukubali kimya. Hakukubali uonevu.

Alichagua kupaza sauti — kwa kalamu, kwa hotuba, na baadaye kwa mapambano.
Kwa hilo, alihukumiwa kifungo cha miaka 27, kwenye gereza la Robben Island.
Lakini hata akiwa kifungoni — Mandela aliendelea kuamini katika ndoto ya Afrika yenye usawa, amani na maridhiano.

Mnamo mwaka 1990, Mandela aliachiwa huru.
Na mwaka 1994 — akawa Rais wa Kwanza Mweusi wa Afrika Kusini.
Aliongoza taifa kwa msamaha badala ya kisasi.
Alichagua umoja badala ya kugawanyika kwa chuki.

Leo hii, tarehe 18 Julai, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.
Siku ya kutafakari thamani ya haki za binadamu, usawa, na msamaha.
Siku ya kujiuliza:

Je, sisi pia tuko tayari kusamehe kwa ajili ya kesho bora?

Mandela alituonesha kuwa shujaa si yule asiyeanguka… bali yule anayesimama tena kila mara akiwa na matumaini.

Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika na taarifa za uhakika.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FurahaFmtz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to FurahaFmtz:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share