13/06/2026
Mwigizaji maarufu nchini, Shamsa Ford, ameungana na familia, marafiki na wadau wa tasnia ya filamu kuomboleza kifo cha mwigizaji mkongwe Issa Joseph maarufu k**a Mzee Onyango, Shamsa Ford alitoa salamu za pole zilizojaa hisia na kumuombea marehemu apumzike kwa amani, huku akieleza kuwa Mzee Onyango alikuwa nguzo muhimu katika tasnia ya sanaa na mtu aliyegusa maisha ya wengi kupitia kazi zake.
Kifo cha Mzee Onyango kimeacha pengo kubwa kwa mashabiki na wasanii wengi waliopata nafasi ya kufanya kazi naye katika safari yake ya muda mrefu ya uigizaji.
Tufatilie kupitia YouTube ya FURAHA TV, upate habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika kila siku. Usisahau ku-like, ku-comment, na kusubscribe ili uweze kuendelea kuhabarika
Furaha TV channel no 419 kwenye kisimbuzi cha Azam na Startimes Channel no 118