14/05/2026
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Geita (TAKUKURU) imefanikiwa kurejesha zaidi ya shilingi milioni 3 zilizofanyiwa ubadhilifu na mhasibu wa TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2026, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Geita, James Ruge, amesema taasisi hiyo imefanya uchunguzi wa miradi yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 20
Amesema katika uchunguzi huo, TAKUKURU ilibaini kuwepo kwa mapungufu mbalimbali katika miradi 11 kati ya miradi 13 iliyokaguliwa
Aidha, amesema mbali na kurejesha fedha hizo zilizochepushwa Bukombe, TAKUKURU pia imefanikiwa kurejesha shilingi milioni moja zilizokuwa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Chato yaliyokusanywa na kutowasilishwa benki na wakusanya mapato
Takukuru imesema jumla million 15 zimereshwa katika maeneo tofauti tofauti ambazo zilikuwa zimechepushwa.