Machinga Tv

Machinga Tv ๐—›๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ | ๐—˜๐—น๐—ถ๐—บ๐˜‚ | ๐—•๐˜‚๐—ฟ๐˜‚๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ๏ฝก
Official Machinga Tv page.

14/05/2026

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Geita (TAKUKURU) imefanikiwa kurejesha zaidi ya shilingi milioni 3 zilizofanyiwa ubadhilifu na mhasibu wa TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2026, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Geita, James Ruge, amesema taasisi hiyo imefanya uchunguzi wa miradi yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 20

Amesema katika uchunguzi huo, TAKUKURU ilibaini kuwepo kwa mapungufu mbalimbali katika miradi 11 kati ya miradi 13 iliyokaguliwa

Aidha, amesema mbali na kurejesha fedha hizo zilizochepushwa Bukombe, TAKUKURU pia imefanikiwa kurejesha shilingi milioni moja zilizokuwa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Chato yaliyokusanywa na kutowasilishwa benki na wakusanya mapato

Takukuru imesema jumla million 15 zimereshwa katika maeneo tofauti tofauti ambazo zilikuwa zimechepushwa.

14/05/2026

Wanafunzi na Waalimu wa shule ya sekondari ya Wasichana Geita wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji wake mkubwa wa zaidi ya Shilingi Bilioni 4.6 katika shule hiyo, suala ambalo limerahisisha mazingira ya upataji na utoaji wa elimu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa maabara, maktaba na Mabweni ya kisasa pamoja na nyumba za waalimu.

Ujenzi wa shule hiyo ni utekelezaji wa mpango mkubwa wa Rais Samia wa kuimarisha elimu ya sayansi kwa wasichana Nchini, lengo likiwa ni kuongeza idadi ya wasichana wanaosoma masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati pamoja na kuwapa mazingira salama na bora ya kujifunzia ili waweze kushindana katika taaluma mbalimbali.

"Shule hii imejengwa kwa fedha za Watanzania kwa awamu mbili ambazo zilitumika kujenga madarasa 12, mabweni 8, nyumba mbili za waalimu, lakini pia ikajenga matundu 19 ya vyoo na vyote hivi vimekamilika kwa asilimia 100." Amesema Mwalimu Mwamini George, Mkuu wa Shule ya Sekondari Geita.

Mwalimu Mwamini kadhalika amemshukuru Rais Samia kwa ujenzi wa nyumba za waalimu katika shule hiyo suala ambalo limewaweka waalimu katika mazingira salama, rafiki na ya karibu, akiungana pia na Mwalimu Japhet Thobias ambaye amesema ujenzi wa shule hizo Nchi nzima zimesaidia pia katika kutoa fursa ya ajira kwa waalimu wengi.

Aidha kwa upande wao wanafunzi wa shule hiyo Lydia Hezema, Rahel Marwa na Penina Mshegoli, wamemshukuru Rais Samia kwa kuwawekea mazingira rafiki ya kusoma, wakimuahidi kusoma kwa bidii pamoja na kumtumia k**a kilelezo sahihi cha kuamini kuwa wanaweza kutimiza ndoto zao mbalimbali ikiwemo za kutamani kuwa Viongozi wakubwa wa baadae.

14/05/2026

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mkemia Mkuu wa Serikali na TRA imek**ata jumla ya lita 66,048 za kemikali bashirifu zilizoingizwa nchini kinyume cha sheria jijini Dar es Salaam.

Operesheni hiyo maalum iliyofanyika Aprili 2026 imehusisha kuk**atwa kwa watuhumiwa wawili pamoja na magari mawili yaliyokuwa yakisafirisha kemikali hizo. Uchunguzi umebaini kuwepo kwa Cyclohexanone lita 16,048 na Extra Neutral Alcohol (ENA) lita 50,000 zilizokuwa zikisafirishwa kwa vibali vya kughushi.

Aidha, DCEA imesema kemikali hizo zinaweza kutumika kutengeneza dawa za kulevya na imeteketeza pia ekari 38.5 za mashamba ya bangi katika mikoa mbalimbali, huku ikiwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa za uhalifu huo.

14/05/2026

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limethibitisha kupatikana kwa kichwa cha aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), James Temba, siku sita baada ya mwili wake kuzikwa bila kichwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 13, 2026, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema kichwa hicho kimekutwa katika eneo la Kitunda Kibeberu, Ilala, kikiwa kimefukiwa ardhini.

Kamanda Muliro amesema jumla ya watuhumiwa watano wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo, akiwemo mganga wa kienyeji anayefahamika kwa jina la Side.

Mwili wa James Temba ulizikwa Mei 7, 2026 katika kijiji cha Mande, Old Moshi Magharibi mkoani Kilimanjaro ukiwa hauna kichwa.

12/05/2026

Halmashauri ya Manispaa ya Geita , tayari imenza Kujenga Jengo la Kitega Uchumi maarufu k**a GEDECO TOWER , Jengo refu zaidi ndani ya Mkoa wa Geita lenye thamani ya Shilingi Bilioni 13 , Fedha ambazo ni Makusanyo ya Mapato ya ndani ambapo awamu ya kwanza Tayari kiasi cha shilingi Bilioni 7 kimetolewa kwa ajili ya kuanza Ujenzi huo.

Akizungumza Mara Baada ya Kufika katika Eneo linalojengwa Jengo hilo Mkuu wa wilaya ya Geita , Hashim Komba akiambatana na Wakuu wa Vitengo kutoka Idara mbalimbali ndani ya Manispaa ya Geita , ameipongeza Manispaa ya Geita kwa kuandika historia ya kutumia Fedha za Mapato ya ndani katika kujenga Mradi mkubwa wa Kimkakati .

"Lakini leo Halmashauri ya Manispaa ya Geita inaandika Histori kwa kutumia Fedha za Mapato ya Ndani zaidi ya Bilioni 13 wanakwenda kuwa na mradi Mkubwa mradi wa kimkakati , mradi wa kimageuzi kwenye Mji wetu na Mradi mkubwa wa Kiuchumi Hongereni sana Halmashauri ya Manispaa ya Geita , " DC. Komba.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita , Yefred Myenzi amesema kupitia mradi huo Halmashauri imetoa fursa za Ajira kwa ajili ya wananchi wanaopatikana ndani ya Manispaa ya Geita kwa lengo la wananchi kujikwamua kiuchumi.

12/05/2026

Wakulima wa Kata ya Nyida, Wilaya ya Shinyanga, Mkoani Shinyanga wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fursa mpya ya kuimarisha kilimo chao kupitia mradi wa umwagiliaji wa Nyida, skimu inayotajwa kuongeza uzalishaji wa mazao hususan mpunga na kuboresha maisha ya Kaya zaidi ya 1,000 katika awamu yake ya kwanza.

Rais Samia katika utekelezaji wa ujenzi wa Skimu hiyo ya Nyida, aliidhinisha jumla ya Shilingi Bilioni 14.6 kutekeleza mradi huo, ambapo kufikia sasa jumla ya Hekta 421 zinanufaika na maji ya uhakika, matarajio yakiwa ni kufikia Hekta 800 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga huku pia mradi huo ukitarajiwa kujengwa mpaka Wilayani Nzega, ukitarajiwa kuhudumia hekta 2,000.

"Zamani tulikuwa tunalima kwa zamu, maji yalikuwa kidogo sana, tulikuwa tunagombana sana wakulima na mimea ilikuwa inakauka na hata uzalishaji wetu ulikuwa chini sana lakini baada ya ujio wa Skimu hii tumenufaika sana sisi k**a wakulima. Sasa hivi maji ni ya uhakika na uzalishaji mashambani umeongezeka kutoka gunia nane kwa ekari hadi gunia 15." Amesema Bw. Michael Paul, Mkulima wa Kata ya Nyida.

Wakulima hao wakizungumza na Mwandishi wetu wa habari leo Jumamosi Mei 09, 2026, wamebainisha kuwa kilimo chao kwasasa kimepata msukumo mpya huku pia wakipiga hatua kubwa za maendeleo kutokana na kuwa na uwezo wa kulima mara mbili kwa mwaka tofauti na awali ambapo walilazimika kusubiri msimu wa mvua pekee ambao huwa ni mara moja kwa mwaka, suala ambalo lilikuwa likiwakosesha faida.

Kwa upande wake Sylvester Kabati, amemshukuru Rais Samia kwa kutekeleza mradi huo katika eneo lao, akisema utekelezaji wake ulitoa fursa za ajira kwa Vijana, ujuzi pamoja na kuongeza mzunguko wa fedha kutokana na ugeni wa watu na wataalamu waliokuwa wanautekeleza mradi huo katika eneo lao.

12/05/2026

Mmiliki wa kampuni ya Dr Toyota, bwana Salim Mbuma, amesimulia kisa cha kijana aliyempa kazi lakini baadaye akatoroka bila taarifa yoyote.

Dr Toyota amesema tukio hilo limemsikitisha sana, akieleza kuwa baadhi ya vijana wamekuwa na tabia ya uvivu na kukosa uvumilivu katika kazi. Ameongeza kuwa mafanikio yanahitaji kujituma, nidhamu na subira badala ya kukata tamaa mapema.
Video:

โ€œVijana wengi wanataka mafanikio ya haraka bila kupitia changamoto za kazi,โ€ amesema Dr Toyota.

Kauli yake imeibua mjadala mkubwa mtandaoni ambapo baadhi ya watu wameunga mkono maoni yake huku wengine wakisema mazingira ya kazi nayo yanapaswa kuangaliwa ili kuwafanya vijana wabaki kazini.

12/05/2026

Mbunge wa Kigoma Mjini, Revocatus Chipando (Baba Levo) ameshauri Bima ya afya kuunganishwa na ambulance ili kupunguza ghalama zaidi za matibabu kwa wananchi.

12/05/2026

Mbunge wa Kigoma Mjini, Revocatus Chipando (Baba Levo) ameshauri wak**atwe wanaotoa elimu ya afya kiholela mtandaoni kwakuwa wanawachanganya wananchi.

12/05/2026

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ametangaza kuwa hatajiuzulu kufuatia uamuzi wa Mahak**a ya Katiba kufufua mchakato wa uchunguzi wa kumuondoa madarakani unaohusishwa na sakata la fedha lililoibiwa katika shamba lake la Phala Phala.

Akilihutubia taifa, Ramaphosa amesema ataipeleka ripoti ya jopo huru lililochunguza sakata hilo kwenye mapitio ya kisheria, akidai kuwa ripoti hiyo ina makosa makubwa ya kisheria, tafsiri potofu ya mamlaka pamoja na hitimisho yasiyo na msingi wa ukweli.

Mahak**a ya Katiba ya Afrika Kusini hivi karibuni ilibatilisha uamuzi wa Bunge wa mwaka 2022 uliokuwa umezuia kuanzishwa kwa mchakato wa impeachment dhidi ya rais huyo. Uamuzi huo sasa umefungua njia kwa k**ati maalum ya bunge kuanza upya uchunguzi dhidi yake.

Sakata hilo linahusiana na wizi wa zaidi ya dola 580,000 zilizokuwa zimefichwa ndani ya samani katika shamba binafsi la Ramaphosa mwaka 2020. Upinzani nchini humo umekuwa ukimtuhumu rais huyo kwa kushindwa kutoa taarifa sahihi kuhusu chanzo cha fedha hizo pamoja na namna tukio hilo lilivyoshughulikiwa.

Hata hivyo, Ramaphosa ameendelea kusisitiza kuwa hakuvunja sheria yoyote na kwamba fedha hizo zilikuwa malipo halali yaliyotokana na mauzo ya nyati katika shamba hilo.

Wachambuzi wa siasa nchini Afrika Kusini wanaeleza kuwa licha ya presha kutoka kwa vyama vya upinzani, bado Ramaphosa ana nafasi kubwa ya kuendelea kusalia madarakani kutokana na uungwaji mkono anaoupata ndani ya chama tawala cha ANC na washirika wa serikali ya muungano.

Chanzo: Reuters, AP News, Financial Times (reuters.com)

11/05/2026

Rais wa Jumuiya ya Serikali za Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), Geofrey Kiliba amewatahadharisha vijana kote Nchini kuhusu hatari ya kupuuza au kuchezea amani ya taifa, akisisitiza kuwa bila utulivu hakuna ndoto ya kijana itakayotimia.

Akizungumza na Wanafunzi wa chuo Cha Maji jijini Dar es Salaam Kiliba amewataka wasomi na vijana kote nchini kuitazama amani k**a "ajenda ya lazima" na si jambo la hiari, kwani ndiyo msingi wa mipango yote ya kimaendeleo.

Kiliba amebainisha kuwa kijana yeyote mwenye shauku ya kupiga hatua kimaisha, lazima awe mlinzi wa kwanza wa utulivu wa nchi, kwani mazingira ya vurugu hayachagui wala hayamuachi mtu salama.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Machinga Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share