Machinga Tv

Machinga Tv ๐—›๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ | ๐—˜๐—น๐—ถ๐—บ๐˜‚ | ๐—•๐˜‚๐—ฟ๐˜‚๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ๏ฝก
Official Machinga Tv page.

Katika kuendeleza diplomasia ya utamaduni na kuthamini kahawa k**a urithi wa pamoja, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ime...
13/06/2026

Katika kuendeleza diplomasia ya utamaduni na kuthamini kahawa k**a urithi wa pamoja, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuimarisha urafiki, maelewano na ushirikiano wa kudumu kati ya wananchi wa Tanzania na Jamhuri ya Korea, hatua inayolenga kufungua fursa zaidi za kiuchumi, utalii na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa Tamasha la Kahawa la Gongneung Forest Trail 2026 nchini Korea Kusini, Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea, Mheshimiwa Noel Kaganda, amesema kuwa tamasha hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuitangaza Tanzania kupitia kahawa yake bora pamoja na urithi wake wa kiutamaduni.

Mheshimiwa Kaganda alieleza kuwa Tanzania huzalisha takribani tani 100,000 za kahawa kila mwaka, huku sekta hiyo ikisaidia maelfu ya wakulima na kuchangia kati ya dola za Marekani milioni 200 hadi 300 katika uchumi wa taifa.

Aidha, alisisitiza kuwa kahawa si zao la biashara pekee, bali ni nyenzo muhimu ya kuimarisha uchumi, kujenga urafiki kati ya mataifa na kukuza ubadilishanaji wa tamaduni huku akiongeza kuwa kupitia zao hilo, Tanzania na Korea zinaendelea kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii.

Mbali na kuitangaza kahawa ya Tanzania, Balozi Kaganda aliwaalika washiriki wa tamasha hilo pamoja na wageni wengine kutoka Korea Kusini kutembelea vivutio vya utalii vya Tanzania, ikiwemo Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na visiwa vya Zanzibar, ambavyo vinatambulika duniani kwa uzuri wake wa kipekee na vivutio vya asili.

Alibainisha kuwa kupitia diplomasia ya utamaduni na matumizi ya kahawa k**a daraja la kuunganisha watu, Tanzania inaendelea kujenga mahusiano imara ya urafiki, maelewano na ushirikiano wa muda mrefu na Jamhuri ya Korea, huku ikifungua milango ya fursa mpya za uwekezaji, biashara na utalii kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

13/06/2026

Kocha wa Dar City ameonyesha kufurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake baada ya kuibuka na ushindi mnono wa vikapu 106 kwa 57 dhidi ya Magone katika mchezo wa Ligi ya Kikapu ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya mchezo huo, kocha huyo alisema timu yake ilicheza kwa nidhamu, ushirikiano na kufuata maelekezo ya benchi la ufundi jambo lililowezesha kupata matokeo hayo makubwa. Alisisitiza kuwa wachezaji walionyesha kujituma kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mchezo na kutumia vizuri nafasi walizozipata.

Aidha, alieleza kuwa ushindi huo unawapa morali kuelekea michezo ijayo huku akiwataka wachezaji kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kutoridhika na matokeo ya sasa. Dar City ilitawala mchezo katika robo zote na kuonyesha ubora mkubwa wa kushambulia na kujilinda, hali iliyowafanya Magone kushindwa kuhimili kasi yao.

13/06/2026

AMINI MKOSA Nahodha wa timu ya Kikapu ya DAR CITY amewapongeza wachezaji wenzake kwa ushirikiano wao mkubwa uliowapa nafasi ya kushinda vikapu 106 kwa vikapu 57 vya timu ya MAGONE katika muendelezo wa ligi ya kikapu ya Dar es Salaam inayochezwa uwanja wa DON BOSCO Upanga Jijini Dar es Salaam.

Upande wa pili Amini Mkosa amegusia ushiriki wao katika mashindano ya kimataifa kuanzia Kenya, Afrika Kusini na Nchini Rwanda katika ligi ya Kikapu Afrika hatua ya nane bora ilivyowapa uzoefu mkubwa ambao umewafanya waweze kupata ushindi katika mechi mbili mfululizo.

13/06/2026

Mjadala mkali kuhusu Kombe la Dunia uligeuka burudani baada ya gwiji wa soka Zlatan Ibrahimoviฤ‡ na staa wa mitandao IShowSpeed kukutana kwenye kipindi cha FOX Sports.

IShowSpeed alisisitiza kwa kujiamini kuwa Portugal itatwaa Kombe la Dunia kwa msaada wa Cristiano Ronaldo, lakini Zlatan hakukubaliana naye hata kidogo. Kwa utani wake wa kawaida, Zlatan alimkatisha Speed na kuzua vicheko vikubwa kwa watazamaji.

Video ya tukio hilo imeenea kwa kasi mitandaoni, ikikusanya mamilioni ya watazamaji huku mashabiki wakibishana k**a Portugal kweli ina nafasi ya kutwaa ubingwa au Zlatan alikuwa sahihi kuipinga kauli hiyo.

๐Ÿ˜‚โšฝ Nani unaamini? Portugal kubeba Kombe la Dunia au Zlatan alikuwa anatania tu?

13/06/2026

Imamu Mkuu Masjid Mtambani Sheikh Shabani Pembe amewataka Waislamu na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kudumisha na kuilinda amani ya Tanzania, akisisitiza kuwa ikiwa serikali ingeruhusu kufanyika kwa kile kilichokuwa kimepangwa, kuratibiwa na kuhamasisha Oktoba 29, 2025 basi Tanzania isingeweza kukalika tena kutokana na uvunjifu wa amani ambao ungetokea wakati ule wa Uchaguzi.

Sheikh Shabani Pembe amebainisha hayo wakati akitoa hotuba yake kwa waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoani Dar Es Salaam na kuwataka Waislamu kuhukumu kile kilichotokea kwa uadilifu pamoja na kupima athari ambazo zingeweza kujitokeza ikiwa serikali ingewaaacha wale waliokuwa wamejitokeza barabarani kuendelea na matukio yao ya uvunjifu wa amani Nchini.

"Kituo chetu cha mwendokasi tumeshuhudia kikichomwa, Vituo vya Polisi vilichomwa, ATM pale Manyanya imechomwa na hata maduka ya watu yamechomwa na kuibiwa, hawa watu wangeachiwa wafanye wanavyotaka hii Nchi ingekuwa wapi? Ndugu zangu tunapohukumu tuhukumu kwa uadilifu, kwamba lengo lilikuwa waachiwe wafanya wanavyotaka? Au ilikuwa nini? Baadae wale wote waliowachochea wanaanza kuiona dola mbaya, Tunapohukumu mambo tuhukumu kwa uadilifu." Amesema Sheikh Pembe.

"Tunapohukumu mambo tuhukumu kwa uadilifu, amani ni tunu ndugu zangu, ikiondoka hii hata sisi hatuwezi kukusanyika. Ile Ijumaa ile kutoka Tegeta mpaka hapa nililipa Elfu sitini kwa bodaboda na nimefika hapa naambiwa M***i ametangaza hakuna ibada hapa, sasa waislamu niwaombe kuipenda Nchi yako ni katika Imani. Wale wote waliokuwa wanahamasisha yale ya Oktoba 29 hakuna hata mtoto wao aliyeguswa na kiwembe, tafsiri yake ni kuwa wao na familia zao zilibaki salama, kinyume chake familia za maskini na fukara ndio waliotolewa kafara." Ameongeza kusema.

Sheikh Pembe amewakosoa vikali pia wale wanaokosoa Tume zilizoundwa kuchukua matukio hayo ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisisisitiza kuwa Tanzania ni huru na Watanzania wanapaswa kuunga mkono busara na hekima za Viongozi wao katika kupata muafaka na suluhu ya kudumu dhidi ya kile kinachotajwa k**a sababu ya matukio ya Oktoba 29, 2025.

13/06/2026

Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imezitaka taasisi zote ambazo hazijakamilisha mchakato wa kujisajili kuhakikisha zinakamilisha ndani ya siku saba za kazi kuanzia Juni 12, 2026.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Mkurugenzi wa Tume hiyo, Dkt. Emmanuel Mkilia, amesema taasisi ambazo bado hazijaanza kabisa usajili zinapaswa kuanza mara moja na kukamilisha ndani ya muda huo uliopangwa.

Aidha, PDPC imesisitiza kuwa ukaguzi wa uzingatiaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi tayari umeanza na utaendelea kufanyika kwa ukamilifu na bila kikomo.

Dkt. Mkilia pia amewataka wananchi kulinda taarifa zao binafsi kwa kuzingatia sheria, pamoja na kutoa malalamiko kwa Tume pale wanapobaini matumizi yasiyo halali ya taarifa zao au ukiukwaji wa faragha.

Ameongeza kuwa Tume itaendelea kutoa elimu, miongozo na usimamizi ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na mfumo imara wa ulinzi wa taarifa binafsi, unaolinda haki za wananchi na kuimarisha imani katika matumizi ya teknolojia na huduma za kidijitali.

Vilevile, Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na timu za faragha katika taasisi mbalimbali wameshauriwa kushiriki kongamano maalum ili kuongeza uelewa na kubadilishana uzoefu na wadau wa ndani na nje ya nchi.

Dkt. Mkilia amesema Kongamano la kwanza la Faragha na Ulinzi wa Taarifa Binafsi linatarajiwa kufanyika kuanzia Juni 29 hadi Julai 1, 2026 katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

13/06/2026

Simanzi na majonzi makubwa vimetanda katika Chuo Kikuu cha St. John kilichopo Jijini Dodoma wakati wa ibada ya kuaga mwili wa mwanafunzi huyo, tukio lililohudhuriwa na wanafunzi, walimu, familia na ndugu wa karibu.

Kwa mujibu wa taarifa, Rebeca Misungwi alipata ajali ya moto usiku wa kuamkia Jumapili ya Juni 6, 2026 katika eneo walilokuwa akiishi pamoja na rafiki yake Felister Peter Francis. Ajali hiyo ilisababisha majeraha makubwa yaliyomfanya kulazwa hospitalini kwa matibabu ya dharura.

Baada ya kupatiwa matibabu kwa muda, Rebeca alifariki dunia Juni 11, 2026 akiwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, ambapo pia rafiki yake Felister alikuwa akipatiwa matibabu.

Mwili wa marehemu umefanyiwa ibada ya kuaga chuoni hapo St. John University Dodoma, kabla ya kusafirishwa kuelekea Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya mazishi.

Akizungumza kwa niaba ya familia, kaka wa marehemu, Pascal Kapote, amesema familia imepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kifo hicho na kuomba Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo halisi cha tukio hilo na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika.

Familia imethibitisha kuwa ratiba kamili ya mazishi itatolewa mara baada ya mwili kuwasili mkoani Mwanza.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

12/06/2026

Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 12 Juni 2026 amepongeza hatua kubwa iliyofikiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ya kukusanya tani 27.05 za dhahabu zenye thamani ya Shilingi trilioni 10 za Kitanzania.

Rais Samia ameyasema hayo leo Ijumaa Juni 13, 2026, aliposhiriki k**a Mgeni Rasmi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 tangu kuanzishwa kwa benki hiyo. Hafla hiyo kubwa imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam.

"Nipongeze Benki Kuu kwa mpango wa ununuzi wa dhahabu ya ndani. Hadi kufikia mwezi Mei mwaka huu, k**a alivyosema mwenyewe Gavana, akiba yetu rasilimali yetu ya dhahabu tuliyoikusanya ni tani 27.5, yenye thamani ya shilingi trilioni 10 za Kitanzania. Hapa tulipofika, si haba." Amesema Rais Samia

Katika hotuba yake, Rais Samia amesisitiza kuwa ununuzi wa dhahabu ya ndani ni mkakati imara wa kuimarisha akiba ya fedha za kigeni nchini, akisema hatua hiyo inasaidia katika kulinda thamani ya Shilingi ya Tanzania dhidi ya mtikisiko wa kiuchumi duniani.

Rais amebainisha kuwa mkakati huo unalenga pia kujenga uchumi imara na unaojitegemea kwa faida ya kizazi cha sasa na cha baadaye, akitoa wito kwa Benki Kuu kuendelea kusimamia sekta ya fedha kwa umakini mkubwa ili kudhibiti mfumuko wa bei.

Amewataka kuendeleza ubunifu katika mifumo ya kidijitali ili kurahisisha huduma za kibenki kwa wananchi wote, hasa waishio vijijini akiweka wazi kuwa ukuaji wa sekta ya fedha unapaswa kwenda sambamba na maisha halisi ya Watanzania wa kawaida.

12/06/2026

Binti mmoja mrembo kupitia ukurasa wake wa TikTok ameibua mjadala mzito kuhusu umiliki wa mali ndani ya ndoa na mahusiano.

Katika video hiyo, amesisitiza umuhimu wa wanandoa au wapenzi kujadili mada nzito mapema kwani zinaweza kufichua mitazamo muhimu kuhusu maisha ya baadaye.

Akitoa mfano wa mazungumzo yake na mpenzi wake, mrembo huyo amesema alishangazwa baada ya mpenzi wake kueleza kuwa akipata mali hataziandika kwa jina la mke wala watoto wake, bali ataandika kwa jina la mama yake.

Kwa mujibu wake, mpenzi huyo amesema amekuwa akivutiwa na baadhi ya wanamichezo wanaoweka mali zao kwa majina ya wazazi wao. Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa mitandaoni huku wengi wakitoa maoni tofauti kuhusu umiliki wa mali ndani ya familia.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Machinga Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share