Machinga Tv

Machinga Tv ๐—›๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ | ๐—˜๐—น๐—ถ๐—บ๐˜‚ | ๐—•๐˜‚๐—ฟ๐˜‚๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ๏ฝก
Official Machinga Tv page.

21/11/2025

Zaidi ya Wageni 500 kutoka kwenye Mataifa mbalimbali ya Barani Afrika na nje ya Afrika wamekutana kwa siku mbili Mkoani Arusha kwenye Kongamano la kujadili kuhusu mchango wa dini katika uchumi na maendeleo, wengi wakifurahia amani na utulivu walioushuhudia nchini tangu kuwasili kwao siku tano zilizopita.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, miongoni mwa washiriki hao kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na nchini Senegal, wameeleza kuwa Kongamano hilo lilitaka kuahirishwa kutokana na kile walichokuwa wakikiona kwenye Mitandao ya Kijamii.

"Wakati tunakuja Tanzania tulisikia vitu vingi, tukaangalia kwenye runinga na tukaona habari za uwepo wa machafuko, tukawa na wasiwasi wa Kongamano letu kiasi cha kuanza kufikiria kuahirisha lakini tunamshukuru Mungu tumefika na tumekuta amani ya kutosha na Mungu ni mwema sana kwasababu amewezesha amani Tanzania, tunamshukuru sana Mungu." Amesema Joela Athumani, Raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Bi. Joela amewataka watanzania kuishikilia kwa nguvu baraka ya amani waliyobarikiwa na Mwenyenzi Mungu, akiwataka wale wote waliokuwa wamepanga kuja nchini kutokuwa na wasiwasi wowote wa kiusalama kwani hali ni shwari na shughuli zinaendelea k**a kawaida.

Kwa upande wake Bw. Ogi Kabongo, Mkazi wa Kinshasa nchini DRC, ameeleza athari za ukosefu wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, akiwataka Watanzania kudumisha amani ya Tanzania kwa gharama yoyote ile kwani ukosefu wa amani unadhorotesha na kuua kabisa ustawi na maendeleo ya wananchi.

Aidha Bw. Fransis Owusu, Raia wa Senegal na Rais wa Full Gospel Business Men's Fellowship International ameitaka Jamii kuendelea kuiombea amani ya Tanzania, akisema amani hiyo mara zote imekuwa msingi muhimu wa maendeleo na kiwezeshi kikubwa cha mafanikio katika shughuli za kiuchumi

21/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewashukuru wananchi wa Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kwa imani kubwa waliyompatia katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akiahidi kurejea tena Mkoani Arusha kutoa shukrani zake kwa wananchi.

Dkt. Samia amebainisha hayo leo Ijumaa Novemba 21, 2025 alipotua katika Uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) na kuzungumza na mamia ya wananchi waliofika uwanjani hapo Kumpokea, akianza ziara yake ya siku mbili Mkoani Arusha.

Katika salamu zake Rais Samia amesisitiza kuhusu umuhimu wa amani kwa ustawi na maendeleo ya Watanzania, akisisitiza wananchi kutotoa fursa katika kuharibu amani na kuwasihi Wazazi na walezi kuzungumza na Vijana wao pia kuhusu umuhimu wa kutunza amani ya Tanzania.

"Niwashukuru sana kwa kuendelea kuiweka mikoa hii kuwa salama. Usalama upo, kazi zinaendelea na mambo yetu yote yanaendelea. Niwaombe sana amani pekee ndiyo tumaini letu, uhai wetu ni amani yetu sasa niwaombe sana tusitoe fursa ya kuharibu amani yetu." Amesema Rais Samia.

Rais Samia pia ametoa wito kwa wazazi na walezi kuzungumza na watoto wao kuhusu amani, akisema anafahamu kuwa matukio ya uvunjifu wa amani ya Oktoba 29, 2025 Vijana wengi walifuata mikumbo, akisema ni muhimu kuilinda amani kwani masuala ya uvunjifu wa amani si masuala ya kufanyia majaribio nchini.

Rais Samia yupo Mkoani kwa ziara ya siku mbili ambapo kesho Jumamosi Novemba 22, 2025 anatarajiwa kutunuku Kamisheni na Shahada ya Sayansi ya Kijeshi kwa Maafisa wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani Arusha.

21/11/2025

Vijana wamehamasishwa kuwa mstari wa mbele katika kukemea maovu na kulinda amani na utulivu uliopo nchini pamoja na kujiepusha na makundi yenye kutenda Vitendo visivyokubalika kisheria na vyenye kuhatarisha amani ya Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa kufuatia matukio ya uvunjifu wa amani yaliyojitokeza kwenye Miji mbalimbali ya Tanzania wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, suala ambalo limemlazimu Rais Samia Suluhu Hassan kuunda Tume maalum kufuatilia chanzo cha vurugu kutokana na kuwa tukio lililowagharimu wengi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Bw. Hamis Jumanne, Mkazi wa Kichangani, Temeke amewaomba Vijana kuyakataa makundi yanayotishia amani ya Tanzania, akiwataka kutumia muda wao mwingi kujiendeleza kiuchumi badala ya kutumika kuharibu amani.

Jumanne amesisitiza kutafuta namna nzuri ya kushughulikia matatizo na mapungufu yaliyopo kwa namna ifaayo na isiyoharibu tunu za Taifa, akihimiza mazungumzo zaidi kati ya wananchi na Viongozi katika kutatua kero zilizopo.

21/11/2025

Bi. Zawadi Matuku, Mfanyabiashara wa Chanika kwa Ngwale Mkoani Dar Es Salaam ameishukuru serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama kwa udhibiti wa amani na utulivu nchini, akisema kilichotokea wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 hakuwahi kukizoea kwani Tanzania inasifika kwa amani na utulivu kote duniani.

Matuku ameyasema hayo wakati akieleza uzoefu wake dhidi ya uvunjifu wa amani uliojitokeza, akisema kwamba aliamini siku hiyo ya upigaji k***a ungekuwa wa amani na wafanyabiashara wangeendelea na shughuli zao k**a kawaida baada ya kupiga kura.

Ameomba suala hilo kutokujirudia tena, akiwahamasisha Vijaba kujiepusha na mikumbo na kuwataka kutumia muda wao mwingi katika kujiendeleza kiuchumi na kusimamia ustawi wa maisha yao badala ya kutumika na makundi yasiyoitakia mema Tanzania.

21/11/2025

Wito umetolewa kwa Vijana kujiepusha na makundi yasiyofaa pamoja na kutofuata kila wanachoambiwa kwenye Mitandao ya Kijamii nchini katika kuhakikisha amani na utulivu unaendelea kuwepo.

Wito huo umetolewa na Mzee Ally Bomba Omar, Mkazi wa Tandika Mabatini Mkoani Dar Es Salaam, akieleza kuwa tangu kuzaliwa kwake Mwaka 1949 hakuwa kushuhudia vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

"Tangu kipindi cha Mwalimu Nyerere tulikuwa tunaishi kwa amani, matatizo haya yaliyotokea hapa yamenishangaza na watu hawa sijui wametokea wapi. Sisi tusiokuwa nacho na tuliozoea kununua unga nusu kilo nusu kilo tuliteseka sana na bahati mbaya hata ukiwa na visenti unanunua wapi vitu? Maduka yote yalikuwa yamefungwa." Amesema Mzee Bomba.

Mzee huyo amefahamisha kuwa ana amini kwamba kila mmoja ana akili timamu, akisema makundi mabaya yatawapoteza, akisema maandamano yasiyo rasmi yanaleta matatizo mengi ikiwemo vifo, majeraha na uharibifu wa mali na maisha.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo amempongeza...
21/11/2025

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo amempongeza hadharani Bi Mary Barney Laseko, mhitimu wa Shahada ya Sheria (LLB), kwa kuvunja rekodi ya miaka 32 katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania).

Bi Laseko ameweka historia kwa kupata Daraja la Kwanza, rekodi ambayo ilishikiliwa kwa muda mrefu na Profesa wa Sheria UDSM, Prof. Hamudi Majamba.

Tukio hilo limejiri wakati wa Mahafali ya 55 (Duru la Tatu) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa mahafali hayo, Dkt. Kikwete amesema mafanikio ya Bi Laseko ni ushahidi wa juhudi, nidhamu na uwezo mkubwa wa vijana wa Tanzania. Ameongeza kuwa matokeo hayo yanatoa matumaini mapya katika sekta ya sheria na elimu kwa ujumla.

Bi Mary Laseko pia ameweka historia nyingine muhimu kwa kuwa mwanamke wa pili nchini kupata Daraja la Kwanza kutoka Law School of Tanzania. Mwanamke wa kwanza kutimiza rekodi hiyo ni Dkt. Asha-Rose Migiro, ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mwanadiplomasia mashuhuri.

Katika mahafali hayo, Dkt. Kikwete ametunuku shahada na stashahada kwa jumla ya wahitimu 2,452, ambapo 1,386 sawa na asilimia 56.6 walikuwa wanawakeโ€”takwimu zinazoonyesha mwamko mkubwa wa wanawake katika elimu ya juu nchini.

Mafanikio ya Bi Laseko yameendelea kupongezwa na wadau mbalimbali wa sekta ya sheria, elimu na maendeleo ya vijana, wakisema kuwa yametoa hamasa kwa wanafunzi wengine na kuimarisha taswira ya elimu ya sheria nchini.

20/11/2025

"Tunashukuru sana kwa hii Wizara ya Vijana iliyoundwa tunaona hata sisi sasa tutafikiwa kwasababu kuna wakati mawazo yetu tulikosa hata pa kuyapeleka kwahiyo kwa ujio wa Wizara hii ya Maendeleo ya Vijana naamini tutaitumia kuwasilisha mawazo na maoni yetu."- Denis Faustine, Mkazi wa Ilala Mkoani Dar Es Salaam akizungumza leo Alhamisi Novemba 20, 2025.

20/11/2025

"Mimi k**a Kijana natarajia mambo mema sana kwa huu usawa aliokuwa nao Mama Samia Suluhu Hassan kwasababu tunaenda sehemu sahihi zaidi kuliko kule tulikotoka kwasababu naamini Mama Samia atafanya mambo mazuri kwa Vijana, akinamama na dada zetu na ndugu zetu wengine.

"Kikubwa niendelee kuwaomba Vijana tuendelee kupambana na tuepuke vishawishi mbalimbali na zaidi tuendelee kumuombea Rais Samia na kumsaidia katika masuala mbalimbali."- Hamza Rufeni, Mkazi wa Dar Es Salaam akitoa maoni yake kuhusu Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan ya ufunguzi wa Bunge na hotuba yake alipokuwa akiwaapisha Mawaziri na Manaibu Mawaziri Jumanne Novemba 18, 2025.

20/11/2025

Wananchi wa Kibaha Mkoani Pwani wamehimizwa kutunza amani katika maeneo yao ili waweze kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii hivyo kuwezesha ustawi na maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Mkaguzi wa Polisi, Elieza Hokororo kutoka Kitengo cha Polisi Jamii Mkoa wa Pwani alipokua akizungumza na maafisa usafirishaji kwa njia ya Pikipiki maarufu k**a Bodaboda, bajaji na wafanyabiashara wa kituo cha Mabasi Kibaha kuhusu ulinzi na usalama katika maeneo yao.

Mkaguzi Hokororo amewaeleza wafanyabiashara hao kuwa inapokosekana amani, wao k**a maafisa usafirishaji hawawezi kutoka kufanya kazi za kupakia abiria au mizigo kutoka sehemu moja kwenda nyingine, hawawezi kupata chakula wala matibabu na huduma nyingine muhimu za kijamii.

Naye Msemaji wa wafanyabiashara wa kituo cha mabasi Kibaha, Bwana Rashid Madaraka amelishukuru Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa namna wanavyoshirikiana nao k**a wafanyabiashara kwa kutoa elimu mara kwa mara kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo kutunza amani na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu.

Mkaguzi Hokororo aliambatana na Mkuu wa Polisi Jamii Wilaya ya Kibaha, Wakaguzi wa kata za Maili moja, Tangini, Kongowe, Tumbi na Boko Mnemela ili kuyafikia makundi mbalimbali ya jamii ikiwemo maafisa usafirishaji na wafanyabiashara na kuwaelimisha umuhimu wa amani kwa maendeleo ya jamii.

20/11/2025

Fedha za mkopo zinazoombwa na walengwa katika makundi ya vijana,wanawake na watu wenye ulemavu wapewe kutokana na kiwango cha fedha walichomba ili wafikie malengo waliokusudia badala ya kuwapa fedha pungufu.

Akizungumza Kabla ya kukabidhi hundi ya mkopo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya GEITA, SHILINGI BILIONI MBILI NUKTA TISA TISA kwa makundi maalum,Mkuu wa wilaya ya GEITA HASHIM KOMBA amesema kumekuwepo na malalamiko ya wanavikundi kupewa mikopo pungufu na waliyoomba na kushindwa kufikia malengo yao.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya GEITA,YEFRED MYENZI amesema mwaka wa fedha 2013/2014 hadi 2022/2023 jumla ya fedha ya SHILINGI BILIONI TANO NUKTA MBILI zimetolewa kwa makundi MIA TISA NA THELATHINI na kiasi cha fedha SHILINGI BILIONI TATU NUKTA NANE MOJA zimerejeshwa na wanaendelea na jitihada za ufuatiliaji wa urejeshaji wa SHILINGI BILIONI MOJA NUKTA NNE SABA.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uhakiki ya Makundi hayo kutoka wilaya ya GEITA ambae pia ni Katibu Tawala wa wilaya hiyo,LUCY BEDA amesema wamefanya uhakiki wa makundi hayo na wamekidhi vigezo vya mkopo.

Shughuli za kiuchumi wa makundi hayo wanayofanya ni kilimo,ufugaji,usafirishaji wa abiria,huduma za kifedha,utengenezaji wa matofali,uchenjuaji wa madini,uchomeleaji,uuzaji wa nishati za kupikia,ushonaji,biashara za uuzaji wa bidhaa za ujenzi na utengenezaji wa sabuni na batiki.

Muonekano mpya WA msanii
20/11/2025

Muonekano mpya WA msanii

19/11/2025

Wananchi katika Maeneo mbalimbali ya Jimbo la Busanda wilayani Geita Mkoani humo wamempongeza Mbunge wa Jimbo la Busanda Dkt. Jafar Seif kwa Kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI - Afya huku wakimuomba kushughulikia changamoto za Afya ndani ya Jimbo hilo.

Pongezi hizo zimetolewa Leo Novemba 19 , 2025 na Baadhi ya wakazi kutoka Katika Kata ya Nyarugusu, Kata ya Bukoli , Kata ya Nyaruyeye huku Baadhi yao pia wakimuomba kushughulikia Changamoto za Barabara ambazo imekuwa kikwazo kwa Maendeleo ya wananchi hasa katika Kata ya Bukoli.

Aidha Wananchi wamesema Imani aliyopewa na. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kubwa na kumuomba kuendelea kuchanganua changamoto mbalimbali kwa wananchi ikiwemo pia Mikopo ya Asilimia 10 ambayo imekuwa ikitolewa kwa Vijana , Wanawake , wenye Ulemavu katika Halmashauri itolewe pia kwa Wazee.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Machinga Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share