Machinga Tv

Machinga Tv ๐—›๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ | ๐—˜๐—น๐—ถ๐—บ๐˜‚ | ๐—•๐˜‚๐—ฟ๐˜‚๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ๏ฝก
Official Machinga Tv page.

19/09/2025

Jubilee Insurance kupitia kampuni zake za Bima ya Afya na Maisha imezindua mpango maalum wa kusaidia jamii kwa kuwapatia wanafunzi 10 wa Shule ya Msingi Meru, jijini Arusha, bima ya afya. Hatua hii inalenga kusaidia familia na watoto kupata huduma bora za afya pamoja na kuimarisha ustawi wa jamii.

Kwa msaada huu, Jubilee Insurance inalenga kuhakikisha watoto wanapata huduma za afya bila mzigo wa kifedha kwa wazazi wao, sambamba na kuchangia katika maendeleo ya elimu kwa kuwa na wanafunzi wenye afya bora na uwezo wa kufuatilia masomo yao bila vikwazo vya kiafya.

19/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Zanzibar Ndugu Dkt. Hussein Ali Mwinyi pamoja na viongozi wengine wakiomba dua kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar tarehe 19 Septemba, 2025.

18/09/2025
18/09/2025

Mgombea wa Urais kutokea Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Zanzibar na RAIS wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi Amewataka wananchi wa zanzibar kuhamasisha na kudumisha Amani,Umoja na Maridhiano Katika nchi yetu
โ€Ž
โ€ŽRais Mwinyi Amesema hiyo ndo sera mama bila Amani hakuna maendeleo,"msingi wa maendeleo Katika nchi zote ni Amani"
โ€Ž
โ€ŽAidha amewaomba.wawakilishi wa wabunge,Madiwani kila mmoja Katika upande wa CCM wakizungumza Katika majukwaa,waanze kuimiza Amani, Umoja na Maridhiano Katika nchi yetu
โ€Ž

16/09/2025

DKT. SAMIA ATUMA SALAMU ZA USHINDI KWA YANGA NA SIMBA "NYOTE NINYI NI WANANGU"

Akiwa Visiwani Zanzibar leo Jumanne Septemba 16, 2025, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za Kheri kwa vilabu na Mashabiki wa Yanga Sc na Simba Sc, wanaomenyana leo kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar Es Salaam kwenye mchezo wa Ngao ya Hisani.

"Najua leo Dabi la Kariakoo linachezwa sasa mimi nipo nawaangalieni na ninachoomba kwenu wana Yanga, wana Simba ni mchezo mzuri, mchezo wa salama na mcheze mpira utakaoburudisha wananchi na utakaowapa raha, na atakayeshinda tutampongeza. Mimi nipo nawaangalieni wanangu wote wa Simba na wanangu wa Yanga." Amesema Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Vilabu vya Simba na Yanga vinacheza mchezo wao huo k**a ishara pia ya kuanza kwa ligi kuu ya Tanzania bara kwa msimu wa mwaka 2025/26, ligi ambayo inatarajiwa kuanza kesho Septemba 17, 2025 tarehe ambayo Dkt. Samia akitarajiwa pia kuendelea na kampeni zake za kusaka kura Visiwani Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti Maadili ya Bodi ya Filamu Tanzania ameongoza kikao maalum cha kujadili mwenendo wa mte...
15/09/2025

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti Maadili ya Bodi ya Filamu Tanzania ameongoza kikao maalum cha kujadili mwenendo wa mtengeneza maudhui katika mitandao ya kijamii anayejulikana k**a .

Itakumbukwa kwamba hivi karibuni mtengeneza maudhui huyo alichapisha picha jongevu ambazo zilisababisha taharuki na malalamiko kutoka kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, kutokana na maudhui hayo kuonekana kwenda kinyume na maadili, mila na utamaduni wa Kitanzania.

Mara baada ya kikao hicho, alichukuliwa na Maafisa wa Jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi, kufuatia uchunguzi ulioonyesha uwepo wa viashiria vya makosa ya jinai katika chapisho lake.

Tamko la Bodi ya Filamu Tanzania

Bodi ya Filamu Tanzania imeendelea kuwakumbusha na kuwasisitiza watengeneza maudhui wote nchini kuhakikisha hawakiuki maadili na utamaduni wa taifa. Pia imeeleza kwamba ni wajibu wa kila mtengeneza maudhui:

Kujisajili rasmi na Bodi ya Filamu,

Kupata vibali vya utengenezaji wa kazi zao,

Kufuata taratibu na sheria zilizowekwa.

Bodi imesisitiza kuwa haitasita kumchukulia hatua mkali mwanatasnia yeyote atakayekiuka kanuni, miongozo na sheria za nchi.

15/09/2025

Bodi ya Pamba imemuzawadia Fedha Taslimu Milioni 7 na Mtungi wa Gesi Mkulima wa zao hilo Bw. Kusekwa Matonange Mkazi wa Kijiji Cha Bukondo Halmashauri ya wilaya ya Geita Mkoani Geita kwa kuvuna Zaidi ya Tani 3, za Pamba ambazo ni sawa na kilo 3024 za zao hilo na kupelekea kuwa Mzalishaji kinara ndani ya Mkoa wa Geita.

Akizungumza na Vyombo vya Habari mara Baada ya kumtembelea nyumbani kwake Mkulima huyo wa pamba amesema wakati anaandaa shamba la kulima aliaandaa shamba lenye hekali moja ambalo amevuna Pamba yenye kilo 3024 hali ambayo imempa mafanikio mkubwa mara Baada ya kuvuna.

" Niliongeza Juhudi nikawa nimepatia kilo 2012 , Muhula uliofatia nikawa nimepata kilo 2334.4, Muhula wa Pili nilipata kilo 2345, Muhula huu nimeweza kupata eneo Hilo Hilo la Ekali moja nimeweza kupata 3024 kwa hiyo Teknolojia hii Ina manufaa mkubwa Sana kwa wakulima , " Mkulima wa Pamba , Kusekwa Matonange .

Kwa upande wake Mkaguzi wa Pamba wilaya ya Geita Filbert Matonange amesema Bodi ya Pamba imetoa hamasa ya Fedha kiasi Cha Shilingi Milioni 7 pamoja na Mtungi wa Gesi kwa Mkulima huyo katika kuendelea pia kutoa hamasa kwa wakulima wengine kuendelea kuongeza Juhudi za kulima zao Hilo la Pamba ambalo ni Mkombozi kwa Taifa .

"Kwa siku ya Leo tuko hapa kwa Mkulima Bw. Safari Matonange ambaye huyu ni Mkulima ambaye ameshika nafasi ya kwanza kimkoa Mkulima huyu akiweza kulima kwa kutumia kwa kufuata kanuni 10 za kufuata KILIMO Cha Pamba alilima hekali moja ambapo kwenye hekali moja hiyo ameweza kutoa kilo 3024 , " Mkaguzi wa Pamba wilaya ya Geita , Filbert Matonange.

Akikabidhi hundi hiyo yenye thamani ya Shilingi Milioni Saba pamoja na Mtungi wa Gesi kwa Mkulima huyo Mgeni rasmi katika Hafla hiyo Ndg. Kassim ameipongeza Bodi ya Pamba kwa kutoa hamasa kwa Mkulima huyo ambaye amekuwa mkombozi na kinala kwa wakulima wanaolima zao Hilo ndani ya Mkoa wa Geita.

15/09/2025

BABA LEVO AKIHUTUBIA

15/09/2025

Mtangazaji maarufu kutoka Malkia Choice FM, Zipporah Ernest ( ) , ambaye pia ni Mkurugenzi wa Zipporah Elite Agency, amefanikisha zoezi la kutafuta model na brand ambassador wa kampuni mbalimbali.

Zoezi hilo lilifanyika Malkia Choice FM Mbezi Beach, huku tukio hilo likiambatana na sherehe ya kuadhimisha miaka miwili ya Zipporah Elite Agency tangu ilipoanzishwa mwaka 2023.

Akizungumza katika tukio hilo, Zipporah alisisitiza umuhimu wa kuendeleza vipaji vya vijana na kutoa nafasi kwao kuonyesha uwezo wao katika sekta ya mitindo na masoko ya bidhaa.

14/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR utakaoishia Kigoma utaendelea hadi mataifa jirani ya Burundi na Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hatua hiyo itakaofanya mkoa wa Kigoma kuwa kitovu cha usafirishaji na biashara katika ukanda huo.

Dkt. Samia ameyasema hayo Septemba 14, 2025 akizungumza kwenye Viwanja vya Katosho, Kigoma Mjini mkoani Kigoma wakati wa muendelezo wa mikutano ya kampeni za chama hicho kwenye Mikoa ya Kanda ya Magharibi

"Kigoma hii ya sasa sio mwisho wa reli ni kitovu cha biashara na maendeleo na ili kufikia lengo hilo kwenye miundombinu ya usafiri na usafirishaji, ambao ndio muhimili mkubwa wa kukuza uchumi tumejidhatiti kuunganisha mkoa huu kwa njia zote yaani barabara, anga, reli na njia ya maji na tayari maboresho ya uwanja ndege yanaendelea, njia tayari imeanza kutumika na jengo la abiria linaendelea kujengwa." Amesema Dkt. Samia.

Dkt. Samia pia amesema kando ya ujenzi wa reli hiyo, Serikali pia itafanya maboresho ya reli ya zamani ya MGR, wakinunua pia vichwa 3 vipya vya treni, mabehewa mapya 22 ya abiria na 44 ya mizigo, huku pia ukifanyika ukarabati wa mabehewa 350 ya mizigo na 33 ya abiria sambamba na mabehewa maalumu yenye kuhifadhi baridi kwaajili ya usafirishaji wa mazao ya mbogamboga na matunda.

Dkt. Samia pia amezungumzia maboresho ya sheria na kanuni kuhusu waendeshaji wa huduma za reli kwa kuruhusu waendeshaji binafsi kutoa huduma ya usafiri na usafirishaji kwenye miundombinu ya reli iliyowekwa na serikali, k**a sehemu ya kuendelea kuongeza huduma bora kwenye usafiri wa reli nchini.

14/09/2025

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa ya kimkakati nchini na ameahidi kuusimamia k**a kitovu cha biashara na uwekezaji endapo ataaminiwa kuongoza baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza leo Jumapili Septemba 14, 2025, katika viwanja vya Katosho, Kigoma Mjini, Dkt. Samia amesema serikali ya awamu ya sita imejidhatiti kuunganisha Kigoma kwa njia zote kuu za usafirishaji- reli, anga, barabara na maji ili kuhakikisha uchumi wa mkoa huo unakua kwa kasi na kufunguka kwa fursa nyingi za uwekezaji.

โ€œKigoma hii ya sasa siyo mwisho wa reli, ni kitovu cha biashara na maendeleo. Na ili kufikia lengo hilo, kwenye miundombinu ya usafiri na usafirishaji, ambao ndio muhimili mkubwa wa kukuza uchumi, tumejidhatiti kuunganisha mkoa huu kwa njia zote. Tayari maboresho ya uwanja wa ndege yanaendelea na jengo la abiria linaendelea kujengwa,โ€ amesema Dkt. Samia.

Kuhusu sekta ya usafiri wa reli, Dkt. Samia amesema ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Tabora hadi Kigoma utaunganisha pia Tanzania na mataifa jirani ya Burundi na mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Sambamba na hilo, serikali inaendelea na maboresho ya reli ya zamani ya MGR, ikiwemo ununuzi wa vichwa vitatu vipya vya treni, mabehewa 22 ya abiria na 44 ya mizigo, pamoja na ukarabati wa mabehewa 350 ya mizigo na 33 ya abiria. Pia, mabehewa maalumu ya kuhifadhi baridi yatanunuliwa ili kuwezesha usafirishaji wa mbogamboga na matunda.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Machinga Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share