Machinga Tv

Machinga Tv ๐—›๐—ฎ๐—ฏ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ | ๐—˜๐—น๐—ถ๐—บ๐˜‚ | ๐—•๐˜‚๐—ฟ๐˜‚๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ถ๏ฝก
Official Machinga Tv page.

11/01/2026

Naibu waziri wa Maji , Mhandisi Kundo Mathew amemuagiza Katibu Mkuu wizara ya Maji , kufanya tathimini ya Kukagua Miradi ya Maji inayojengwa na kusimamiwa Mkandarasi Peritus Exim Infrastructure Co. LTD na kunichukulia hatua Baada ya kubaini na kuwepo kwa Dosali katika Miradi ya Maji ambayo amekuwa akiijenga hapa nchini.

Agizo hilo amelitoa Mara Baada ya Kutembelea na Kukagua Mradi wa Maji taka unaojengwa wilayani Chato wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1, na kubaini mradi huo kutokamilika kwa wakati , Mradi kujengwa chini ya kiwango huku akisema Serikali haitofumbia Macho wala kuruhusu Baadhi ya wakandarasi kuja kuchezea Fedha za watanzania .

" Analipa Fidia ya kuchelewesha Mradi na huwa ni siku 100 Kisheria na tukishamaliza siku 100 Kisheria tunateminate Mkataba na ninazo Taarifa mkandarasi huyu huyu amekuwa kinara wa kutuchezea sekta ya Maji anao mradi uko Tabora amefanya Mchezo k**a huu anao Mradi uko Igunga amefanya Mchezo k**a huu , " Naibu Waziri wa Maji , Mathew.

Mhandisi Mathew amesema Ujenzi wa Mradi huo ulianza kujengwa June 2023 na ulitarajia kukamilika Disemba 2024 lakini Ujenzi huo umesimama na Mkandarasi huyo haonekani Eneo ambalo Ujenzi unafanyika huku akitoa Maagizo Kwa Katibu Mkuu kufanya tathimini ya Ufanyajikazi wake sambamba na kuchukua hatua .

Mathew amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Mwaka 2022 alitoa kiasi Cha Fedha Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa Mradi huo huku akisema Serikali ya Dkt. Samia imekuwa na malengo Makubwa katika kutatua changamoto za wananchi huku Baadhi ya wakandarasi wakiwa ni Sehemu ya kuharibu kazi nzuri inayofanywa na Serikali.

ADAI KUPEWA KIPIGO BAADA YA KUONEKANA UBALOZI WA VATICAN AKIWASHTAKI VIONGOZI WA KANISA KATOLIKI Lucy Antony Michael (35...
11/01/2026

ADAI KUPEWA KIPIGO BAADA YA KUONEKANA UBALOZI WA VATICAN AKIWASHTAKI VIONGOZI WA KANISA KATOLIKI

Lucy Antony Michael (35), Mkazi wa Yombo Dovya, Mtaa wa Makangarawe, Wilayani Temeke, Dar es Salaam amevamiwa na watu wasiojulikana akiwa anatoka nyumbani kwake, ambapo watu hao walimpiga na kumshambulia maeneo mbalimbali ya mwili wake

Lucy ambaye ni miongoni mwa watu waliojitambulisha kuwa ni Waumini wa Kanisa Katoliki walioenda kwenye Ubalozi wa Vatican, uliopo hapa nchini kwaajili ya kupeleka barua ya malalamiko juu ya mwenendo wa baadhi ya viongozi wa Kanisa hilo hivi karibuni, amesema kabla ya kuvamiwa na kushambuliwa kwake kwa siku kadhaa amekuwa kwenye misukosuko ya kupokea simu na kutumiwa sms za kejeli, matusi na wengine kumtishia maisha

Akizungumza na Waandishi wa Habari akiwa nyumbani kwake leo, Jumapili Januari 11.2026, Lucy amehusianisha kushambuliwa kwake na maoni aliyotoa mbele ya Wanahabari kuhusiana na mwenendo wa baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki, jambo ambalo ameeleza kuwa amelifanya kwa nia njema ya kujenga iliyolenga kuwarejesha viongozi hao kwenye mstari, maoni ambayo yamepokelewa kwa hisia hasi kwa baadhi watu kwenye jamii

Aidha, bada ya kushambuliwa Lucy amefikisha malalamiko yake kwenye Kituo cha Polisi Makangarawe na kupewa RB No. MAR/RB/49/2026

Shuhuda wa tukio hilo Sabina Michael, Mjumbe wa Serikali ya Mtaa Ashura Salum na Daud Leonard ambaye ni mmoja wa waumini wanaosali pamoja na Lucy, kwa nyakati tofauti wameeleza kusikitishwa na tukio hilo sambamba na kuziomba mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa wote waliohusika, huku pia wakiomba kuimarishiwa zaidi usalama mtaani kwao kwani matukio ya aina hiyo yanaweza kusababisha wasiwasi kwa jamii.

11/01/2026

Lucy Antony Michael (35), Mkazi wa Yombo Dovya, Mtaa wa Makangarawe, Wilayani Temeke, Dar es Salaam amevamiwa na watu wasiojulikana akiwa anatoka nyumbani kwake, ambapo watu hao walimpiga na kumshambulia maeneo mbalimbali ya mwili wake

Lucy ambaye ni miongoni mwa watu waliojitambulisha kuwa ni Waumini wa Kanisa Katoliki walioenda kwenye Ubalozi wa Vatican, uliopo hapa nchini kwaajili ya kupeleka barua ya malalamiko juu ya mwenendo wa baadhi ya viongozi wa Kanisa hilo hivi karibuni, amesema kabla ya kuvamiwa na kushambuliwa kwake kwa siku kadhaa amekuwa kwenye misukosuko ya kupokea simu na kutumiwa sms za kejeli, matusi na wengine kumtishia maisha

Akizungumza na Waandishi wa Habari akiwa nyumbani kwake leo, Jumapili Januari 11.2026, Lucy amehusianisha kushambuliwa kwake na maoni aliyotoa mbele ya Wanahabari kuhusiana na mwenendo wa baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki, jambo ambalo ameeleza kuwa amelifanya kwa nia njema ya kujenga iliyolenga kuwarejesha viongozi hao kwenye mstari, maoni ambayo yamepokelewa kwa hisia hasi kwa baadhi watu kwenye jamii

Aidha, bada ya kushambuliwa Lucy amefikisha malalamiko yake kwenye Kituo cha Polisi Makangarawe na kupewa RB No. MAR/RB/49/2026

Shuhuda wa tukio hilo Sabina Michael, Mjumbe wa Serikali ya Mtaa Ashura Salum na Daud Leonard ambaye ni mmoja wa waumini wanaosali pamoja na Lucy, kwa nyakati tofauti wameeleza kusikitishwa na tukio hilo sambamba na kuziomba mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa wote waliohusika, huku pia wakiomba kuimarishiwa zaidi usalama mtaani kwao kwani matukio ya aina hiyo yanaweza kusababisha wasiwasi kwa jamii.

11/01/2026

Mwalimu Magoda .magodajr ameonesha kutovutiwa na mavazi yaliyovaliwa na baadhi ya wasanii walioshiriki katika tukio la Back to School lililofanyika Lamatha Village. Tukio hilo liliwakutanisha wasanii mbalimbali kwa lengo la kuchangia sekta ya elimu.

Amesema kuwa licha ya tukio hilo kutofanyika mbele ya wanafunzi, mavazi ya baadhi ya wasanii hayakuwa sahihi na yanaweza kuharibu maadili ya watoto endapo yataenezwa kupitia mitandao na vyombo vya habari. Amehimiza wasanii kuzingatia maadili katika matukio yenye muktadha wa elimu.
๐ŸŽฅ .magodajr

11/01/2026

Rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), Geofrey Kiliba, ametoa onyo kali kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza (First Years) dhidi ya tamaa za kimaisha, huku akiwataka wanafunzi wa kiume kuwa walinzi wa taaluma za wanafunzi wa k**e badala ya kuwa vyanzo vya uharibifu.

Akizungumza jana, Januari 9, 2026, katika hafla ya ukaribisho wa wanafunzi wapya katika Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU), Kiliba amewasihi wanafunzi kuishi ndani ya uwezo wao na kurahisisha mahitaji yao ili kuepuka kuingia katika vishawishi vinavyoweza kukatisha ndoto zao za kitaaluma.

"Epuka tamaa, jikadirie na ishi ndani ya uwezo wako. Tumeshuhudia vijana wenzetu wengi wakipotea kwa sababu ya kutokumbuka neno hili. K**a huna hela ya kusuka, bana nywele zako; k**a huna hela ya jeans, nyoosha suruali yako ya kitambaa. Rahisisha mahitaji yako," amesisitiza Kiliba.

Aidha, Rais huyo wa TAHLISO ametoa ujumbe mahususi kwa wanafunzi wa kiume, akiwataka kumchukulia kila mwanafunzi wa k**e k**a dada au mdogo wao. Amewakumbusha kuwa binti yeyote aliyepo chuoni ana mategemeo makubwa kutoka kwa wazazi na ndugu zake walioko mikoani, hivyo kusiwe na mwanafunzi wa kiume atakayekuwa chanzo cha machozi kwa familia hizo.

10/01/2026

Alichozungimza mfanyabiashara kuhusu kitu KINACHO wakwamisha vijana WASOMI nchini.
Video Credits:

10/01/2026

Beki wa kushoto wa Klabu ya Yanga Afrika na mchezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mohamed Hussein Zimbwe โ€˜Shabalalaโ€™ , ameonyesha upande mwingine wa maisha yake nje ya uwanja wa mpira.

Kupitia mitandao ya kijamii, Tshabalala ameshare video akiwa na Influencer maarufu wakitembelea moja ya biashara zake binafsiโ€”duka la manukato linalojulikana k**a Perfume World TZ.

Duka hilo linapatikana Kinondoni, jijini Dar es Salaam, na video hiyo imewavutia mashabiki wengi waliompongeza kwa kuwekeza nje ya soka na kuwa mfano bora kwa vijana.

Shabalala anaendelea kuthibitisha kuwa mafanikio ya mwanamichezo hayaishii uwanjani pekee, bali pia katika ujasiriamali na mipango ya maisha baada ya soka.

10/01/2026

Ndugu wa mchekeshaji King'amuzi, wamemuagiza meneja wa msanii huyo bwana KUACHA KUMSIMAMIA kijana wao.

Akizungimza kwa njia ya simu Kaka wa King'amuzi aliyetambuliwa kwa jina la Paul amesikika akimwambia Rasco aache KUMSIMAMIA mdogo wao

10/01/2026
Bondia maarufu wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ametumia ukurasa wake wa Instagram kujitangazia k**a โ€œBondia mwenye maadui ...
10/01/2026

Bondia maarufu wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ametumia ukurasa wake wa Instagram kujitangazia k**a โ€œBondia mwenye maadui wengi zaidi, nguvu ya ushawishi, mashabiki wengi, na ngumi zinazouma zaidi!โ€ ๐Ÿ’ช๐Ÿพ

Mwakinyo aliendelea kueleza ushindi wake dhidi ya promoter Mapengo wa Tanga na Promoter nakumuita Limbukeni, akisisitiza kwamba yeye ndiye bondia anayehitajika zaidi na tasnia ya mchezo wa ngumi nchini.

Katika ujumbe wake, aliandika:
"Wewe na team yako nitawafundisha kwa vitendo, ya kwamba mimi ndio bondia ambaye TASNI ina hitaji zaidi!"

10/01/2026

"Kumeanza kutokea mjadala kati ya 'amani' na 'haki'. Mimi nawaambieni ni vyote." Dr. MWIGULU Waziri mkuu wa Tanzania

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Machinga Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share