11/01/2026
Naibu waziri wa Maji , Mhandisi Kundo Mathew amemuagiza Katibu Mkuu wizara ya Maji , kufanya tathimini ya Kukagua Miradi ya Maji inayojengwa na kusimamiwa Mkandarasi Peritus Exim Infrastructure Co. LTD na kunichukulia hatua Baada ya kubaini na kuwepo kwa Dosali katika Miradi ya Maji ambayo amekuwa akiijenga hapa nchini.
Agizo hilo amelitoa Mara Baada ya Kutembelea na Kukagua Mradi wa Maji taka unaojengwa wilayani Chato wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1, na kubaini mradi huo kutokamilika kwa wakati , Mradi kujengwa chini ya kiwango huku akisema Serikali haitofumbia Macho wala kuruhusu Baadhi ya wakandarasi kuja kuchezea Fedha za watanzania .
" Analipa Fidia ya kuchelewesha Mradi na huwa ni siku 100 Kisheria na tukishamaliza siku 100 Kisheria tunateminate Mkataba na ninazo Taarifa mkandarasi huyu huyu amekuwa kinara wa kutuchezea sekta ya Maji anao mradi uko Tabora amefanya Mchezo k**a huu anao Mradi uko Igunga amefanya Mchezo k**a huu , " Naibu Waziri wa Maji , Mathew.
Mhandisi Mathew amesema Ujenzi wa Mradi huo ulianza kujengwa June 2023 na ulitarajia kukamilika Disemba 2024 lakini Ujenzi huo umesimama na Mkandarasi huyo haonekani Eneo ambalo Ujenzi unafanyika huku akitoa Maagizo Kwa Katibu Mkuu kufanya tathimini ya Ufanyajikazi wake sambamba na kuchukua hatua .
Mathew amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Mwaka 2022 alitoa kiasi Cha Fedha Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa Mradi huo huku akisema Serikali ya Dkt. Samia imekuwa na malengo Makubwa katika kutatua changamoto za wananchi huku Baadhi ya wakandarasi wakiwa ni Sehemu ya kuharibu kazi nzuri inayofanywa na Serikali.