04/02/2021
*PREPARED FOR ME* 🚗🏦🍹🥘
•1 Wakorintho.2:9
lakini, k**a ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.
- Umeshawahi kujiuliza kwanini kuna watu wengine wanaona👀 fursa lakini wewe huoni, kwanini watu wengine wanasikia👂 maelekezo ya namna ya kuenenda lakini wewe husikii.
- Katika maisha yetu kuna fursa, kuna mafanikio, kuna mambo mazuri ambayo kila mtu angependa kupata.
Lakini mambo hayo Mungu amewaandalia wale wampendao. 💕💞
- Ili tuweze kuona yale ambayo wengine hawawezi kuona na kusikia yale ambayo wengine hawawezi kusikia ni lazima tuwe miongoni mwa wale wampendao Mwokozi.💗
- Unaweza ukajiuliza mwenyewe;
• *JE UNAMPENDA MUNGU?*
- Na k**a *_NDIO_* unampenda Mungu; *Je kwanini bado unashindwa kuona na kusikia yale ambayo Mungu amekuandalia?*
- Wakati unajiuliza hilo swali nataka nikupitishe katika mifano michache katika biblia.
• Mwanzo.37:3
Basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote, maana ni mwana wa uzee wake, akamfanyia kanzu ndefu.
- Hapo tunaweza kujiuliza kwanini kanzu ndefu iliandaliwa kwa ajili ya Yusuph pekee na sio watoto wake wengine.
- Biblia inasema Israeli alimpenda Yusuph kuliko wanawe wote, sio kwamba hakuwapenda wengine lakini alimpenda Yusuph zaidi.
• Hapo tunaweza tukajifunza kitu fulani; kwamba kuna *_upendo_* alafu kuna *_upendo wa kipekee_*
• Matendo ya Mitume.13:22
Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.
- Kuna jambo la kushangaza katika huu mstari, unaweza ukajiuliza je katika Israeli yote ni Daudi pekee aliyekua anampendeza Mungu.
• Mathayo.3:17
na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
- Tuone huo mfano mwingine wakati Yesu anabatizwa 💦, Biblia inatuambia kwamba sauti ilitoka mbinguni ikisema "huyu ndie mwanangu mpendwa"
- unaweza ukajiuliza kwanini hii sauti ilisikika wakati Yesu anabatizwa na haikusikika wakati mtu mwingine yoyote anabatizwa, wakati maji ni yaleyale na mbatizaji ni yuleyule.
- Sasa unaweza ukajiuliza tena kwa mara nyingine;
• *JE UNAMPENDA MUNGU❓*
- Katika mifano yote hiyo tuliopitia unaweza ukagundua kwamba kuna *UPENDO* na kuna *UPENDO WA KIPEKEE*
- Watu wengi wanampenda Mungu lakini hawaoni na hawasikii yale mambo ambayo Mungu amewaandalia
- Tuombe Mungu🙏 ili atusaidie tuwe na Upendo wa Kipekee ili tuwe na uwezo wa kuona👀 yale ambayo wengine hawawezi kuyaona na tuweze kuyasikia👂 yale ambayo watu wengine hawawezi kuyasikia, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao❤️.
- Mungu Akubariki.