WITO KANISA LA WAAMINI WA WITO TANZANIA (K.W.W.T)

22/11/2022

Isaya 35:1-10
[1]Nyika na mahali palipo ukiwa patafurahi; jangwa litashangilia na kuchanua maua k**a waridi.
[2]Litachanua maua mengi, na kufurahi, naam, kwa shangwe na kuimba; litapewa uzuri wa Lebanoni, utukufu wa Karmeli na Sharoni; watauona utukufu wa BWANA, ukuu wa Mungu wetu.
[3]Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu, yafanyeni imara magoti yaliyolegea.
[4]Waambieni walio na moyo wa hofu, Jipeni moyo, msiogope; tazama, Mungu wenu atakuja na kisasi, na malipo ya Mungu; atakuja na kuwaokoa ninyi.
[5]Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.
[6]Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka k**a kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba; maana katika nyika maji yatabubujika; na vijito jangwani.
[7]Na mchanga ung’aao mfano wa maji utakuwa ziwa la maji, na nchi yenye kiu itakuwa chemchemi za maji; katika makao ya mbweha, walipokuwa wamelala, patakuwa na majani, pamoja na mianzi na manyasi.
[8]Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo.
[9]Hapo hapatakuwa na simba, wala mnyama mkali hatapanda juu yake; hawataonekana hapo; bali waliokombolewa watakwenda katika njia hiyo.
[10]Na hao waliokombolewa na BWANA watarudi, watafika Sayuni wakiimba; na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao; nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia.

16/11/2022

Mathayo 8:10
[10]Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli.

alistaajabu Yesu kwa imani ya Akida yule. kwani aliogopa hata Yesu kufikia kwake kulingana na hali yake aliyowekewa na maaskari. lakini alimwomba Yesu atamke neno la uponyaji kwa yule mjakazi wake, Yesu akastaajabu imani.

Yesu anataka watu wenye imani. tena imani yenye nguvu za kuweza kuvunja ngome za Yeriko lakini kwanza umwamini yeye kuwa anaweza. na kwa IMANI yatafanyika.

Mathayo 8:26
[26]Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa IMANI haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.

Kuwa wale wanafunzi hawakuwa na imani, kwani wangeweza kutuliza dhoruba ,Yesu anaamshwa akiwa usingizini na kuanza kukemea pepo na tunaona bahari inatulia.

tuonapata picha kuwa imani ni bayana ya mambo yasiyoonekana. kiuhalisia

Waebrania 11:1
[1]Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

WAPENDWA TUISHI KWA IMANI .

KWA IMANI TUTAMSHINDA SHETANI .
KWA IMANI WAGONJWA WATAPONA
KWA IMANI VIPOFU WATAONA
KWA IMANI MAFANIKIO YATAONEKANA

NDUGU MWAMINI MUNGU KUWA YEYE PEKEE NDIYE JIBU LA MAMBO YOTE
AMEN.

16/11/2022

BWANA YESU ASIFIWE.
IMANI.
Habakuki 2:4
[4]Tazama, roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.

15/11/2022

2 Mambo ya Nyakati 1:7
[7]Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, Omba utakalo nikupe.

KANISA LA WAAMINI WA WITO TANZANIAYeremia 332 Bwana alitendaye jambo hili, Bwana aliumbaye ili alithibitishe; Bwana ndil...
01/11/2022

KANISA LA WAAMINI WA WITO TANZANIA
Yeremia 33
2 Bwana alitendaye jambo hili, Bwana aliumbaye ili alithibitishe; Bwana ndilo jina lake; asema hivi,

3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua..............

29/09/2022

2 Timotheo 2:1
[1]Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.

IBADA YA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA KANISA LA WAAMINI WA WITO ARUSHA.

26/09/2022

2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

18/09/2022

Kila pando asilo lipanda Mungu litang'olewa

19/07/2021

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when WITO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share