Global Publishers

Global Publishers Global Publishers & General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania

Publishers of Swahili Weekly Newspapers, namely UWAZI, IJUMAA, CHAMPIONI, SPOTI XTRA, RISASI, AMANI and IJUMAA WIKIENDA. Own Global TV Online, +255 Global Radio, Social Media and www.globalpublishers.co.tz

28/10/2025

Mwanadada Halima Kaisi, mkazi wa Tanzania anayeishinchini India, amewaomba Watanzania kumsaidia ili aweze kurejea nyumbani kutokana na hali mbaya ya kiafya anayopitia kwa sasa.

Halima ameeleza kuwa amekuwa akilazwa hospitalini kwa takriban miezi mitatu, lakini hali yake bado haiko vizuri, jambo ambalo limesababisha kushindwa kutembea na kuhitaji msaada wa dharura kwa ajili ya matibabu na usafirishaji kurudi Tanzania.

Video full ipo YouTube ya Global TV

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

Unalipa maksi ngapi goma hili la Simba?

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

Kufuatia sakata la mfanyabiashara maarufu Bongo, Jenifer Jovin almaarufu Niffer kuk**atwa na Jeshi la Polisi, mwandishi msomi, amefanya mahojiano na wakili mzoefu ambaye ameeleza ugumu wa sakata hilo.

Video kamili ipo Youtube.

28/10/2025

Mwimbaji wa Injili, Samiri, amefunguka kuhusu kumbukumbu zake na marehemu Ruge Mutahaba, akieleza kuwa aliwahi kuambiwa kuwa Ruge alimkubali na kuthamini kazi zake alipokuwa akifanya muziki wa kidunia.

Samiri amesema kuwa alikuwa na hamu kubwa ya kukutana na kuzungumza naye ana kwa ana, lakini bahati mbaya Ruge alifariki dunia kabla ndoto hiyo kutimia.

Video full ipo YouTube ya Global TV

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

Veronika Raymond, mama mwenye maumivu makubwa, anapaza sauti akiomba msaada kwa ajili ya mtoto wake aliyezaliwa bila njia ya haja ndogo. Mtoto huyo anavuja mkojo bila kudhibiti, hali inayomlazimu kuvaa pampers muda wote au kutumia mashuka matatu na kushindwa kuhudhuria shule, na kuhatarisha afya na utu wake kila siku.

Madaktari wamemshauri afanyiwe upasuaji maalum ili kurekebisha hali hiyo – lakini gharama ya matibabu ni Tsh 1,500,000 ambazo familia haina uwezo nazo.

🙌 K**a umeguswa, tuma mchango wako kupitia namba ya mama +255 62 606 0722(Elizabeth Moshi)

Tusaidie kurejesha tabasamu kwa mtoto huyu. Maisha yake yanaweza kubadilika kwa msaada wako mdogo leo. ❤️

📍
📍.Mollel
📍
📍






28/10/2025

Ukraine imeendeleza mashambulizi yake ya ndege zisizo na rubani dhidi ya mji mkuu wa Urusi, Moscow, kwa usiku wa pili mfululizo, katika kile kinachoonekana kuwa sehemu ya mbinu mpya ya kijeshi ya Kiev kulenga maeneo ya ndani ya Urusi. Wizara ya Ulinzi ya Urusi imethibitisha kuwa mifumo yake ya ulinzi wa anga iliweza kuharibu jumla ya ndege 17 za kijeshi za Ukraine usiku kucha, ikiwa ni pamoja na moja iliyokuwa ikielekea moja kwa moja Moscow, 13 katika eneo la Kaluga, na tatu katika eneo la Bryansk.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, ndege hizo zilinaswa na mifumo ya ulinzi wa anga kabla ya kufikia malengo yake. Hata hivyo, Meya wa Moscow, Sergei Sobyanin, alisema kupitia mtandao wa Telegram kuwa ndege moja iliyoelekezwa kwenye mji mkuu ilianguka katika eneo la mashambani nje kidogo ya jiji, na huduma za dharura zilitumwa mara moja katika eneo hilo. Sobyanin alibainisha kuwa hakuna ripoti za majeruhi au uharibifu wa mali zilizotolewa hadi sasa, ingawa uchunguzi zaidi unaendelea.

Mashambulizi haya yameibua taharuki kwa wakaazi wa Moscow na miji jirani, huku baadhi yao wakiripoti kusikia milipuko midogo usiku wa kuamkia Jumanne. Mamlaka za Urusi zimekuwa zikiongeza doria za anga na ulinzi wa makombora katika maeneo ya karibu na mji mkuu tangu kuanza kwa mashambulizi haya ya ndege zisizo na rubani.

Video full ipo YouTube ya Global TV

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

Msikilize mchezaji wa Klabu ya Yanga, Zimbwe JR alichokisema mara baada ya kupokea tuzo ya mchezo bora wa mchezo wa leo.

Video full ipo YouTube ya Global TV

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

Mgombea ubunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, mkoani Manyara kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emanuel Nuwas, amehitimisha kampeni zake leo kwa shamrashamra kubwa zilizoambatana na ngoma za asili, huku akicheza pamoja na wananchi waliojitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo wa kufunga kampeni.

Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Nuwas ameahidi kuimarisha sekta mbalimbali endapo atapewa ridhaa ya kuongoza, zikiwemo sekta za afya, barabara, maji, na kilimo. Ametoa msisitizo maalum kwa sekta ya kilimo cha umwagiliaji, hasa katika uzalishaji wa zao la kitunguu na mazao mengine ya biashara, akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuongeza tija, ajira kwa vijana, na upatikanaji wa malighafi kwa viwanda vitakavyoanzishwa katika kila halmashauri ikiwemo Mbulu.

Aidha, Dkt. Nuwas amesema upatikanaji wa mbolea na mbegu za ruzuku utaendelea kuimarishwa, huku serikali ikiendeleza jitihada za kuongeza uzalishaji wa mbegu ndani ya nchi ili kukuza ajira kwa vijana na kupunguza uagizaji wa bidhaa hizo kutoka nje.

Katika hatua nyingine, amewaahidi wananchi wa Mbulu Vijijini kuwa kila kitongoji kitapatiwa huduma ya umeme endapo atachaguliwa kuwa mbunge, ili kuchochea maendeleo na kuboresha maisha ya wananchi vijijini.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt....
28/10/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waandishi wa Habari mara baada ya kufunga Kampeni za CCM katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 28 Oktoba, 2025.

28/10/2025

Msanii wa filamu nchini, Aunty Ezekiel, alisherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa upekee kwa kula chakula cha mchana na watoto yatima wa Kituo cha Umrah, kilichopo Magomeni, jijini Dar es Salaam.

Baada ya hafla hiyo ya upendo, Aunty Ezekiel aliandaliwa sherehe fupi na wafanyakazi wake wa Murua katika ofisi yake iliyopo Sinza Mapambano.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

28/10/2025

Bodi ya Filamu Tanzania () imempa onyo kali msanii wa filamu Sophia Rajabu maarufu k**a kutokana na maudhui aliyowahi kuchapisha kwenye mitandao yake ya kijamii, ambayo yameelezwa kwenda kinyume na maadili na utamaduni wa Kitanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dkt. Gervas Kasiga () amesema mbali na onyo hilo, bodi imemteua afisa maalum atakayefuatilia kazi zote za msanii huyo anazochapisha mtandaoni. Dkt. Kasiga ameeleza kuwa endapo Sophia atarudia kosa hilo, hatua kali zaidi zitachukuliwa dhidi yake.

Ameongeza kuwa ni wajibu wa wasanii kuwa kioo cha jamii, kwa kuchapisha maudhui yenye kuelimisha, kuburudisha, na kuleta taswira chanya ya sanaa ya Tanzania ndani na nje ya nchi.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

Address

P. O. Box 7534
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 19:00

Telephone

+255719401968

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Global Publishers posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Global Publishers:

Share

HAKUNA KILICHO BORA K**A KUNYWA MAZIWA NIYAPENDAYO

Ongeza cowbell, punguza matatizo, watoto uwa na furaha zaidi baada ya kunywa maziwa Bora ya cowbell. Maziwa Bora yenye mafuta yatokanayo na mimea. Sisitiza Cowbell 1kg , kwa matumizi ya familia yako. Ni wajibu wetu kukupatia ufahamu katika maswala mbalimbali, tuunge mkono kwa kunywa maziwa Bora ya @cowbelltanzania.