Global Publishers

Global Publishers Global Publishers & General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania

Publishers of Swahili Weekly Newspapers, namely UWAZI, IJUMAA, CHAMPIONI, SPOTI XTRA, RISASI, AMANI and IJUMAA WIKIENDA. Own Global TV Online, +255 Global Radio, Social Media and www.globalpublishers.co.tz

15/07/2026

Mwanadada Mtanzania, Rhoda Chacha Mwita aliyeondoka nchini baada ya kushawishiwa kwamba kuna kazi nzuri nchini India, amesimulia magumu aliyopitia kwa muda wa takribani miaka nane ambapo sasa anaomba msaada wa kurudi nchini.

Akihojiwa na mtangazaji Zaliam Tabuyanjaa
wa Global TV na Globalradio Tanzania, Rhoda
amesimulia alivyonyang'anywa hati ya kusafiria (passport) mara baada ya kufika India.

Video kamili ipo YouTube, Global TV.

Host: Zaliam Tabuyanjaa
šŸ”“ Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

15/07/2026

Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Serikali imefanya mambo mengi ya maendeleo katika Jimbo la Buchosa kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Shigongo alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wananchi jimboni Buchosa, wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika eneo hilo na kuwataka wawe na wivu wa maendeleo na kujitolea kwa hali na mali kuhakikisha miradi ya maendeleo inakamilika.

Shigongo amesisitiza kuwa ni lazima wananchi wawe tayari kujitolea kwa michango na nguvukazi pale wanapotakiwa kufanya hivyo kwani bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kufikia kiwango cha maendeleo kinachotarajiwa na wananchi wa Buchosa.

15/07/2026

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu leo amehudhuria kikao cha kusikiliza ushahidi katika kesi yake ya ufisadi kinachoendelea katika Mahakama ya Wilaya ya Jerusalem, hatua ambayo imevutia uangalizi mkubwa kutokana na ukweli kwamba mara chache sana amekuwa akihudhuria vikao vya aina hiyo isipokuwa alipokuwa akitoa ushahidi wake binafsi.

Leo usiku, Julai 15, ulimwengu wa soka utashuhudia mojawapo ya mikutano yenye historia nzito zaidi kwenye michuano ya Du...
15/07/2026

Leo usiku, Julai 15, ulimwengu wa soka utashuhudia mojawapo ya mikutano yenye historia nzito zaidi kwenye michuano ya Dunia England dhidi ya Argentina, wakikutana kwenye hatua ya mtoano kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2002.

Mchezo utachezwa Atlanta Stadium, ukianza saa 22:00 usiku, huku ukiwa na uzito wa ziada.Hii inaweza kuwa mechi ya mwisho ya Lionel Messi katika michuano hii ya Dunia mwaka 2026.

Timu hizi mbili zimefika hapa kwa njia inayofanana kwa namna moja zote zimepitia mafungu ya muda wa ziada. England waliifunga Norway 2-1 baada ya dakika 120, huku wakiongozwa na Jude Bellingham, ambaye amekuwa shujaa wa hatua ya mtoano akifunga jozi ya mabao dhidi ya Mexico na jozi nyingine dhidi ya Norway mafanikio ambayo hayajawahi kuonekana tangu enzi za Maradona mwaka 1986.

Argentina nao walihitaji dakika 120 kuwaangusha Switzerland 3-1, wakisaidiwa na bao zuri la JuliƔn Ɓlvarez dakika za mwisho na lile la kufunga mlango la Lautaro Martƭnez.

Historia ya timu hizi mbili imejaa chuki ya kirafiki iliyodumu miongo minne kuanzia ā€œMkono wa Munguā€ wa Maradona mwaka 1986 hadi mikutano mingine mikali iliyofuata. Sasa, miaka 40 baadaye, wanakutana tena wakiwa na viini vipya vya hadithi.

Kwa taarifa zaidi tembelea website ya Global Publishers.

Tufuatilie kupitia You Tube ya Global TV, like, comment ili kiendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

15/07/2026
15/07/2026

Mahakama ya kijeshi nchini Israel imemhukumu askari mmoja kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kutoa taarifa za siri za kijeshi kwa mtu aliyedaiwa kuwa wakala wa Iran kwa lengo la kupata malipo ya fedha.

Hukumu hiyo ni miongoni mwa kesi zinazochukuliwa kwa uzito mkubwa na vyombo vya usalama vya Israel, ambavyo vimekuwa vikionya kuhusu ongezeko la majaribio ya mataifa hasimu kuwatumia wanajeshi wa Israel kukusanya taarifa za kijeshi.

15/07/2026

Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwibare, Akinyi Misana, anayesoma darasa la saba, amemshangaza Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, baada ya kumuuliza swali kuhusu siri ya mafanikio yake.

Mwanafunzi huyo alimuuliza swali hilo wakati Shigongo alipokuwa akitembelea na kukagua ujenzi wa shule mpya ya Msingi Mwibare, iliyojengwa kwa fedha za Serikali.

Shigongo alimpongeza mwanafunzi huyo kwa ujasiri wake wa kuuliza swali hilo, huku akieleza kuwa siri ya mafanikio ya mtu yeyote duniani ni kuwa na juhudi, maarifa na bahati.

Aidha, aliwataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto zao na kufikia mafanikio katika maisha yao.

15/07/2026

Ripoti kutoka nchini Hispania zinasema kuwa kikundi cha wezi kimejaribu kuvunja na kuingia kwenye nyumba ya nyota mdogo wa klabu ya Barcelona na Timu ya Taifa ya Hispania, Lamine Yamal, iliyopo jijini Barcelona.

Tukio hilo la kushtusha lilifanyika wakati mchezaji huyo akiwa uwanjani akiiwakilisha nchi yake katika mchezo mkali na wenye ushindani mkubwa dhidi ya timu ya taifa ya Ufaransa.

Wezi hao walitaka kutumia mwanya wa mchezaji huyo kutokuwepo nyumbani ili kutekeleza azma yao ya kupora mali.

15/07/2026

Watu watatu wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa kufuatia ajali ya barabarani iliyohusisha magari mawili kugongana uso kwa uso katika barabara ya Handeni-Korogwe, eneo la Kata ya Sindeni, Tarafa ya Mzundu, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Ajali hiyo ilitokea usiku wa Julai 14, 2026 majira ya saa 4:30 usiku, kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga.

Kwa mujibu wa Polisi, ajali hiyo ilihusisha gari lenye namba za usajili T.712 ABH aina ya Mitsubishi Fuso lililokuwa likitoka Handeni kuelekea Korogwe na gari lenye namba za usajili T.519 EMM aina ya Eicher lililokuwa likitoka Korogwe kuelekea Handeni.

Waliopoteza maisha ni madereva wa magari hayo mawili ambao ni Yahaya Miraji (28), mkazi wa Handeni, na Japhary Ramadhan maarufu Ally (47), mkazi wa Tanga, pamoja na mwanaume mwingine mwenye umri unaokadiriwa kuwa kati ya miaka 46 na 50 ambaye bado hajafahamika.

Aidha, watu wawili ambao ni Chenga Herbet (55) na Salama Ally (56), wote wakazi wa Muheza, walijeruhiwa katika ajali hiyo na wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni wakipatiwa matibabu.

Uchunguzi wa awali wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi uliosababisha madereva kushindwa kuyamudu magari yao na hatimaye kugongana uso kwa uso, huku miili ya marehemu ikihifadhiwa hospitalini kwa ajili ya uchunguzi na taratibu nyingine za kisheria.

15/07/2026

Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo ameshiriki katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la AICT Nyehunge, iliyofanyika katika Kata ya Nyehunge, Jimbo la Buchosa.

Katika harambee hiyo, Shigongo alifanikiwa kuchangisha zaidi ya shilingi milioni 31, huku yeye mwenyewe akichangia shilingi milioni 15 kuunga mkono juhudi za waumini wa kanisa hilo katika ujenzi wa nyumba ya ibada.

Aidha, Diwani wa Viti Maalumu, Grace Wabanu, pamoja na Kalunde Masanja, walichangia kiasi cha shilingi 500,000 kila mmoja, huku Diwani wa Kata ya Nyehunge, Kura Shindika, akichangia shilingi milioni 2.5.

Shigongo aliwataka waumini wa kanisa hilo kuendelea kumtumaini Mungu na kushiriki katika shughuli za maendeleo ya kanisa.

Address

P. O. Box 7534
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 19:00

Telephone

+255719401968

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Global Publishers posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Global Publishers:

Shortcuts

Share