18/09/2025
Miili mitatu ya masista wa Kanisa Katoliki na dereva waliofariki kwenye ajali wilayani Misungwi jijini Mwanza imewasili katika Kanisa la Parokia ya Epifania Bugando kwa ajili ya ibada ya mazishi.
Miili hiyo imefikishwa kanisani hapo kwa msafara wa magari leo Alhamisi Septemba 18, 2025, saa 1:25 asubuhi na kushushwa kwa ajili ya ibada ya kuagwa.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda ni miongoni mwa waombolezaji waliofika kanisani hapo kuhudhuria ibada ya kuaga miili ya watawa hao ambao watazikwa jijini Dar es Salaam.
🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.