Global Publishers

Global Publishers Global Publishers & General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania

Publishers of Swahili Weekly Newspapers, namely UWAZI, IJUMAA, CHAMPIONI, SPOTI XTRA, RISASI, AMANI and IJUMAA WIKIENDA. Own Global TV Online, +255 Global Radio, Social Media and www.globalpublishers.co.tz

18/09/2025

Miili mitatu ya masista wa Kanisa Katoliki na dereva waliofariki kwenye ajali wilayani Misungwi jijini Mwanza imewasili katika Kanisa la Parokia ya Epifania Bugando kwa ajili ya ibada ya mazishi.

Miili hiyo imefikishwa kanisani hapo kwa msafara wa magari leo Alhamisi Septemba 18, 2025, saa 1:25 asubuhi na kushushwa kwa ajili ya ibada ya kuagwa.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda ni miongoni mwa waombolezaji waliofika kanisani hapo kuhudhuria ibada ya kuaga miili ya watawa hao ambao watazikwa jijini Dar es Salaam.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

18/09/2025

Miili ya Masista wa Kanisa Katoliki waliopoteza maisha katika ajali ya gari wilayani Misungwi, mkoani Mwanza, imewasili Boko kwa Masista Jijini Dar es Salaam.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

18/09/2025

Mtumishi wa Mungu Flora Agustino kutoka mkoani Morogoro amefunguka kuwa watu wa kijijini kwao walikuwa tayari wanaamini kuwa amefariki dunia.

Mtumishi huyp ametoa ushuhuda mzito kwa kile alichodai kuwa amekishuhudia. kupitia The Hard Talk inayoongozwa na , amesema kijijini kwao walikuwa wanaamini alishafariki dunia.

Usikose kufuatilia mkasa huu kupitia Global TV siku ya Jumamosi majira ya Saa 3:00 usiku.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

18/09/2025

Kijana Pius Yohana (21), mkazi wa Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam, ametoa kilio kizito kwa serikali baada ya kudai kufanyiwa ukatili na kundi la vijana waliomvamia wakijaribu kumpora pikipiki yake.

Katika harakati za kujitetea, Pius ameeleza kuwa alichomwa kisu kwenye uti wa mgongo na kupooza kuanzia kiunoni kushuka chini.

Tangu siku hiyo maisha yake yamebadilika kabisa; hawezi tena kutembea wala kufanya shughuli za kujikimu k**a awali.

Mama mzazi wa Pius ameiomba serikali kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake kwa watuhumiwa wa tukio hilo ambao tayari wamek**atwa.

Kwa sasa Pius amelala kitandani muda wote na ameanza kupata vidonda kutokana na kutogeuzwa mara kwa mara.

Anahitaji msaada wa haraka, ikiwemo kiti mwendo (wheel chair), vifaa vya matibabu na huduma za uangalizi wa kiafya.

K**a umeguswa na ungependa kusaidia kwa njia yoyote; kifedha au vifaa, tafadhali wasiliana au tuma msaada wako kupitia:

📞 0693 564 340
👤 Yohana John Mrangwa

18/09/2025

Mpiga kura wa mara ya kwanza! Anaanza safari yake ya uraia kwa uthubutu na matumaini makubwa, akiamua kutumia haki yake ya kidemokrasia kuweka tiki ya ushindi kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan — mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), chama chenye historia ndefu, nguvu thabiti na dira ya maendeleo ya taifa.

Kwa hatua hiyo ndogo lakini yenye maana kubwa, kijana huyu anajiunga na mamilioni ya Watanzania wengine wanaoamini katika urithi wa mapambano ya ukombozi, uimara wa umoja wa kitaifa na ahadi ya mustakabali bora zaidi.

Ni tiketi ya matumaini, ni kura ya uthibitisho kuwa kizazi kipya kiko tayari kusimama na kuunga mkono uongozi unaojali wananchi na kulinda amani, utulivu na mshik**ano wa taifa.

Kwa mara ya kwanza akipiga kura, anajua fika kwamba sauti yake ni sehemu ya historia inayoendelea kuandikwa — historia ya ushindi, historia ya maendeleo, na historia ya uthabiti wa CCM katika kuiongoza Tanzania kuelekea mustakabali ulio imara na wa matumaini mapya.

18/09/2025

Mwanafunzi wa shahada ya sheria Chuo Kikuu cha Mzumbe Tawi la Mbeya, Shyrose Mahande (21), ameuawa kikatili baada ya kutekwa na watu wasiojulikana.

Taarifa zinaeleza kuwa Mahande alitekwa Jumamosi na watu wasiojulikana walimtumia baba yake mzazi, Dkt. Mabula Mahande, video fupi zikimuonyesha akiteswa, huku wakidai kiasi cha fedha ili kumuachia huru.

Kwa masikitiko makubwa, Mahande amepatikana akiwa ameuawa kwa kuchomwa moto kwenye vibanda vya biashara eneo la Nane Nane mkoani Mbeya.

Vyombo vya usalama vinaendelea na uchunguzi wa kina kubaini waliotekeleza tukio hilo na hatua za kisheria kuchukuliwa.

Video full ipo YouTube ya Global TV

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

18/09/2025
18/09/2025

‎Mtumishi Wa Mungu Wa kimataifa kutoka Nchini Kenya Pastor Ezekiel anatarajia Kufanya Mkutano Wa Siku Tano Tanzania Mkoani Mbeya kwanzia Tarehe 24 Hadi tarehe 28 Mwezi Wa 9/2025 katika viwanja vya Chuo Cha Kilimo Uyole Zambia Road,Wagonjwa wataombewa na Watu kufunguliwa na kuombewa Baraka.

‎Kwa mawasiliano zaidi
‎0774781537
‎0689822510

18/09/2025

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linaendelea kuendeleza miradi mbalimbali ya makazi na biashara nchini, ikiwa ni pamoja na mradi wa Morocco Square uliopo jijini Dar es Salaam.

Morocco Square ni sehemu ya kisasa inayotoa huduma nyingi kwa wateja, ikijumuisha maduka, ofisi, sehemu za vyakula, na huduma zingine nyingi zinazokidhi mahitaji mbalimbali ya kijamii na kibiashara.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

18/09/2025

Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, pamoja na mkewe, Brigitte Macron, wanapanga kuwasilisha ushahidi wa picha na kisayansi mahak**ani Marekani ili kuthibitisha kwamba Bi Macron ni mwanamke halali. Hii ni sehemu ya kesi ya kumharibia sifa inayowakabili mfuasi wa mrengo wa kulia, Candace Owens, ambaye ameendeleza madai ya uwongo kwamba Brigitte Macron alizaliwa k**a mwanaume.

Wakili wa familia ya Macron, Tom Clare, amethibitisha kuwa nyaraka hizo zitatolewa mahak**ani k**a sehemu ya ulinzi wa heshima na hadhi ya familia hiyo. Wakili Clare alisema katika mahojiano na podikasti ya ‘BBC Fame Under Fire’ kuwa madai hayo yamekuwa chanzo kikubwa cha huzuni kwa Bi Macron na pia yamesababisha usumbufu mkubwa kwa Rais Emmanuel Macron.

“Bi Macron amechukulia madai haya kuwa ya kuhuzunisha sana,” alisema Clare, akiongeza kuwa familia ya Macron inachukua hatua zote muhimu kuhakikisha haki zao zinaheshimiwa.

Kwa upande mwingine, mawakili wa Candace Owens wamepinga madai ya familia ya Macron na kusema kwamba hoja hizo ni za uongo na haziendani na ukweli. Wanaamini kuwa madai haya ni sehemu ya kampeni ya kudhalilisha na kueneza uvumi dhidi ya Bw. na Bi Macron.

Kesi hii inachukua nafasi muhimu katika mjadala mkubwa wa ulinzi wa heshima, taarifa potofu na athari zake kwenye watu maarufu duniani. Familia ya Macron imeonyesha nia yao ya kutumia ushahidi wa kisayansi na picha ili kuondoa shaka na kuthibitisha ukweli wa jinsia ya Bi Macron, huku wakitafuta haki dhidi ya ueneaji wa madai ya uongo yanayoweza kuathiri sifa yao na maisha yao ya kibinafsi.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

Timiza ndoto zako na UEFA leo hapa Meridianbet kwani ODDS za kibabe na machaguo zaidi ya 1000 yapo hivyo bashiri sasa, k...
18/09/2025

Timiza ndoto zako na UEFA leo hapa Meridianbet kwani ODDS za kibabe na machaguo zaidi ya 1000 yapo hivyo bashiri sasa, kwa wale wa USSD na vitochi piga *149*10 #

18/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wananchi kudumisha amani na utulivu wakati wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.Akizungumza Septemba 17,

Address

P. O. Box 7534
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 19:00

Telephone

+255719401968

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Global Publishers posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Global Publishers:

Share

HAKUNA KILICHO BORA K**A KUNYWA MAZIWA NIYAPENDAYO

Ongeza cowbell, punguza matatizo, watoto uwa na furaha zaidi baada ya kunywa maziwa Bora ya cowbell. Maziwa Bora yenye mafuta yatokanayo na mimea. Sisitiza Cowbell 1kg , kwa matumizi ya familia yako. Ni wajibu wetu kukupatia ufahamu katika maswala mbalimbali, tuunge mkono kwa kunywa maziwa Bora ya @cowbelltanzania.