Tanzania Editors Forum-TEF

Tanzania Editors Forum-TEF We defend freedom of expression and promote editorial excellence as keystone to realization of mature democracy in Tanzania.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa...
27/11/2025

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa makamu wake, Dk. Bakari Machumu.

Dk. Machumu alijiuzulu nafasi hiyo siku sita baada ya kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kushika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Dk. Machumu alikabidhi barua hiyo wakati wa mkutano wake na Wahariri, Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha k**a Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa...
27/11/2025

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa makamu wake, Dk. Bakari Machumu.

Dk. Machumu alijiuzulu nafasi hiyo siku sita baada ya kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassa kushika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Dk. Machumu alikabidhi barua hiyo wakati wa mkutano wake na Wahariri, Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha k**a Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Dk. Bakari Machumu amekabidhi barua ya kujiuzulu nafasi ya umakamu mwenyekiti wa Jukwaa...
26/11/2025

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Dk. Bakari Machumu amekabidhi barua ya kujiuzulu nafasi ya umakamu mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Dk. Machumu amekabidhi barua yake ya kujiuzulu kwa mwenyekiti wa jukwaa hilo Deodatus Balile, wakati wa kikao cha Wahariri na Idara ya Mawasiliano Ikulu, leo tarehe 26 Novemba 2025, jijini Dar es Salaam.

Akipokea barua hiyo, Balile amesema itafikishwa na kujadiliwa kwenye Kikao cha K**ati ya Utendaji ya jukwaa hilo.

Kikao hicho kimejadili mambo mbalimbali ya kitaaluma kwa maslahi ya wanahabari na Taifa kwa ujumla.

Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Machumu kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu tarehe 19 Novemba 2025.

26/11/2025
Serikali imejipanga kutoa mafunzo muhimu na endelevu kwa wanahabari, ikiwemo mafunzo ya usalama, kupitia Bodi ya Ithibat...
26/11/2025

Serikali imejipanga kutoa mafunzo muhimu na endelevu kwa wanahabari, ikiwemo mafunzo ya usalama, kupitia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari - Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi akitoa salamu za shukrani katika Mkutano wa Waziri Mkuu na Wahariri jijini Dar es Salaam, tarehe 25 Novemba 2025.

K**a maovu yote yaliyopangwa kutokea (tarehe 29 Oktoba 2025) yangetimia, gharama za maisha zingekuwa juu kabisa.Ni kauli...
25/11/2025

K**a maovu yote yaliyopangwa kutokea (tarehe 29 Oktoba 2025) yangetimia, gharama za maisha zingekuwa juu kabisa.

Ni kauli ya Waziri Mkuu wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba akizungumzia vurugu zilizotokea wakati na baada ya Uchgazi Mkuu 2025 kwenye mkutano wake na wahariri jijiji Dar es Salaam leo tarehe 25 Novemba 2025.

"Ombi langu, sote tunuie jambo la namna hii lisitokee tena kwenye nchi yetu. Linatutengenezea makovu yasiyopona," amesema Dk. Mwigulu.

Waziri huyo amesema, mpaka sasa watu wengi hawajui undani wa namna mpango ulivyopangwa huku akisisitiza Watanzania kuwa pamoja na kujadili mambo yao bila kuingiliwa.

"Tunatumwa uovu dhidi ya maisha yetu. Fuatilieni wenzetu walioharibikiwa, walifanya mdhaha, wengine hawakujua na walikuja kujua kwenye majuto.

"Wale wanaomezea mate na kutumwa kutugawa, niwahakikishie tutailinda Tanzania kwa gharama yoyote ile. Watameza mate mpaka yaishe na wala Tanzania haitaendshwa kwa remote," amesema.

Katika mkutano huo Dk. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuwa makini na makundi ya watu wenye nia ya kuichafua na kuiharibu Tanzania

Jukwaa la Wahariri Tanzania  (TEF) limempongeza Makamu Mwenyekiti wake Dk. Bakari Machumu kwa kuteuliwa kuwa Mkurugenzi ...
20/11/2025

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limempongeza Makamu Mwenyekiti wake Dk. Bakari Machumu kwa kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu na mwanahabari nguli Tido Mhando kwa kuwa mshauri wa Rais, Habari na Mawasiliano.

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bakari Machumu kuwa Mkurugenzi...
19/11/2025

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bakari Machumu kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Jukwaa la Wahariri Tanzania ( TEF)  limewahaikishia ushirikiano Manaibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na ...
18/11/2025

Jukwaa la Wahariri Tanzania ( TEF) limewahaikishia ushirikiano Manaibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndg. Paul Makonda na Hamis Mwinjuma.

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Mwanahabari na Mwanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Daniel Chongolo kuwa W...
17/11/2025

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Mwanahabari na Mwanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Daniel Chongolo kuwa Waziri wa Kilimo.

Rais Samia Suluhu Hassan katika baraza lake la mawaziri leo tarehe 17 Novemba 2025,  amemteua Prof. Palamagamba Kabudi k...
17/11/2025

Rais Samia Suluhu Hassan katika baraza lake la mawaziri leo tarehe 17 Novemba 2025, amemteua Prof. Palamagamba Kabudi kuongoza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo huku Hamis Mwinyijuma na Paul Makondo wakiteuliwa kuwa Manaibu Waziri.

Tutaendelea kulinda Uhuru wa Habari ili Watanzania waendelee kupata taarifa za ndani ya nchi na nje ya nchi - Rais Samia...
14/11/2025

Tutaendelea kulinda Uhuru wa Habari ili Watanzania waendelee kupata taarifa za ndani ya nchi na nje ya nchi - Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa Ufunguzi wa Bunge la 13, tarehe 14 Novemba 2025.

Address

Mtendeni
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Editors Forum-TEF posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tanzania Editors Forum-TEF:

Share