Tanzania Editors Forum-TEF

Tanzania Editors Forum-TEF We defend freedom of expression and promote editorial excellence as keystone to realization of mature democracy in Tanzania.

12/01/2026
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Paul Makonda kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Awali Makonda alikuwa...
09/01/2026

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Paul Makonda kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Awali Makonda alikuwa naibu waziri wa wizara hiyo.

Wahariri nchini, wameishauri serikali kuvipa ruzuku Vyombo vya Habari ili vifanye kazi kwa ufanisi zaidi.Akizungumza kwe...
23/12/2025

Wahariri nchini, wameishauri serikali kuvipa ruzuku Vyombo vya Habari ili vifanye kazi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza kwenye semina ya siku moja iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) leo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile alitoa kauli hiyo iliyoungwa mkono na Wahariri wenzake kwa kupigiwa makofi.

“Hatuwezi kufanya kazi vizuri bila kuwezeshwa, tuachane na mawazo ya kutoka mataifa ya nje kwamba, serikali ikiwezesha Vyombo vya Habari, havitakuwa huru.

“Tunaonaje aibu kuviwezesha Vyombo vya Habari ili vijenge miundombinu ya fikra ili watu wasichome nchi yao? Mbona Vyama vya Upinzani vinapewa ruzuku na bado vinaisimamia serikali bila kuyumbishwa?” amesema Balile.

Balile alitoa kauli hiyo baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Hamis Masauni kushauri Vyombo vya Habari kuelimisha wananchi hususani vijana kuhusu faida na fursa zilizopo ndani ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Hamad Masauni amesema, vijana wengi nchini hawana uelewa kuhusu Muungan...
23/12/2025

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Hamad Masauni amesema, vijana wengi nchini hawana uelewa kuhusu Muungano na fursa zake.

Akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari jijini Dar es Salaam leo tarehe 23 Desemba, 2025 amesema, vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuwafahamisha vijana umuhimu na fursa zinazopatikana kutokana na Muungano huo.

“Rais Samia Suluhu Hassan aliagiza itolewe elimu kwa umma kwa kuwa, kuna upotoshaji mkubwa unaofanywa kuhusu Muungano, tunapaswa kuodoa chuki ambazo watu wanapandikizwa kuhusu Muungano wetu,” amesema.

Kwenye semina hiyo, Waziri Masauni amesisitiza Wahariri kuhakikisha taarifa wanazochapisha kuhusu Muungano zinatoka kwenye vyanzo sahihi, kuandandaa mijadala yenye tija na kuangazia mafanikio na sio changamoto pekee

Waziri wa Maji, Juma Awesu amesema, tatizo la maji Dar es Salaam limesababishwa na kutokuwepo mvua za kutosha hivyo kuat...
12/12/2025

Waziri wa Maji, Juma Awesu amesema, tatizo la maji Dar es Salaam limesababishwa na kutokuwepo mvua za kutosha hivyo kuathiri uzalishaji wa maji.

Akizungumza kwa simu kwenye kikao cha Wahariri na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (DAWASA), Waziri Awesu ameagiza DAWASA kuweka wazi ratiba ya ugawaji maji ili kuepuka upendeleo na malalamiko.

“Sasa hivi kuna ukamwe, mvua zimechelewa kunyesha na hili sio jambo la kuficha, niwaombe radhi Wananchi wa Dar es Salaam kutokana na upungufu huo. Niwaombe tuwe wavumilivu katika kipindi huki cha mpito.

" Nimeagiza kiwango hiki kidogo cha uzalishaji kwa sasa, DAWASA waweka wazi na usawa ratiba ya ugawaji maji ili kuepuka malalamiko,” amesema Awesu.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mk**a Bwire amesema, mtambo uliothirika zaidi ni Ruvu Chini ambapo sasa unazalisha lita 50,000,000 badala ya lita 270,000,00 kwa siku.

Amesema, hatua za haraka zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kurejesha maji ya Mto Ruvu yaliyokuwa yakipotea kwenye njia yake, kufufua visima virefu na kuchimba visima vipya, kusimamisha vibali vya matumizi mengine ya maji na kudhibiti mivujo ya maji.

Amesema, katika utatuzi wa kudumu wa tatizo la maji Dar es Salaam, tayari Serikali ya Awamu ya Sita inajenga Bwawa la Kidunda ambapo linatarajiwa kukamilika Disemba 2026.

“Lengo la Bwawa la Kidunda ni kuhifadhi maji ambapo yataweza kutumika katika kipindi k**a hiki. Tsh. 336 Bilioni zinatumika kuhakikisha bwawa hili linakamilika na mpaka sasa limefika asilimia 35 ya ujenzi wake,’ amesema Bwire.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile ameshauri kuwepo kwa taarifa za mara kwa mara kwa wananchi kuhusu huduma za maji ili wawe kwenye mazingira mazuri ya kujipanga.

05/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesisitiza umuhimu wa kuripoti habari kwa kuzingatia pande zote mbili ili kuepuka habari zinazoibua chuki.

Chalamila ametoa kauli hiyo leo tarehe 5 Desemba 2025 kwenye kikao chake na Wahariri kilicholenga kujadili hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati akizungumza na Wazee wa Dar es Salaam hivi karibuni.

“Siogopi mwandishi, naogopa upotoshaji,” amesema Chalamila.

Amesema kuwa, vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya kazi kwa weledi na kufuata miiko ya taaluma, na vitaendelea kuhakikisha wananchi wanabaki salama.

Na kwamba, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), linaendelea Kutekeleza majukumu yake kwa misingi ya sheria na taratibu zilizowekwa kwa ajili ya kulinda amani na utulivu wa nchi.

01/12/2025

Tume ya Uchunguzi wa Ghasia za Oktoba 29, ilianza kazi tarehe 20 Novemba 2025 mara baada ya kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Chande ametoa kauli hiyo leo tarehe 1 Desemba 2025 katika kikao na wahariri huku akisisitiza kwamba, tume hiyo ni huru, na imeandaa taratibu ambazo haziingiliwi na taasisi nyingine.

Amesema, wajumbe wote wamekula kiapo cha kufanya kazi kwa uadilifu na weledi.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa...
27/11/2025

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa makamu wake, Dk. Bakari Machumu.

Dk. Machumu alijiuzulu nafasi hiyo siku sita baada ya kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kushika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Dk. Machumu alikabidhi barua hiyo wakati wa mkutano wake na Wahariri, Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha k**a Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa...
27/11/2025

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akipitia barua ya kujiuzulu aliyokabidhiwa na aliyekuwa makamu wake, Dk. Bakari Machumu.

Dk. Machumu alijiuzulu nafasi hiyo siku sita baada ya kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassa kushika wadhifa wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Dk. Machumu alikabidhi barua hiyo wakati wa mkutano wake na Wahariri, Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha k**a Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Address

Mtendeni
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Editors Forum-TEF posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tanzania Editors Forum-TEF:

Share