Tanzania Editors Forum-TEF

  • Home
  • Tanzania Editors Forum-TEF

Tanzania Editors Forum-TEF We defend freedom of expression and promote editorial excellence as keystone to realization of mature democracy in Tanzania.

24/07/2025
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linampongeza ndugu Ernest Sungura, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) ...
19/07/2025

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linampongeza ndugu Ernest Sungura, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa Katibu Mkuu wa Mabaraza ya Habari Duniani (EAPC).

Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa, taifa lenye umoja, mshikamano na utulivu wa amani ndilo msingi wa mafanikio ya ma...
17/07/2025

Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa, taifa lenye umoja, mshikamano na utulivu wa amani ndilo msingi wa mafanikio ya maendeleo ya kweli.

Kauli hiyo ameitoa leo Alhamisi, wakati akizindua rasmi Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika hafla iliyofanyika jijini Dodoma, ambapo amesisitiza umuhimu wa kujenga misingi imara ya maendeleo endelevu, shindani na jumuishi kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo, huku Dira 2050 ikielezwa kuwa nyenzo muhimu ya kuielekeza Tanzania kwenye uchumi wa kisasa, unaozingatia usawa na ustawi wa jamii.

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango amesema, wakati umefika kwa wanahabari Afrika kuonesha taswira nzuri ya bara lao kwa ku...
15/07/2025

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango amesema, wakati umefika kwa wanahabari Afrika kuonesha taswira nzuri ya bara lao kwa kuandika habari chanya zenye nguvu na za kutia moyo kuhusu bara hili.

Ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua Mkutano wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika unaofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Amesema, kwa kipindi kirefu Bara la Afrika limekuwa likitegemea simulizi za vyombo vya habari vya nje ambavyo vimejikita katika habari za vita na migogoro huku vikipuuza uwezo mkubwa, uthabiti na maendeleo ya watu wa Afrika.

Lindeni tasnia ya habari kwa wivu mkubwa, uwepo wa taarifa zisizo sahihi husababisha taharuki katika jamii hivyo ni waka...
10/07/2025

Lindeni tasnia ya habari kwa wivu mkubwa, uwepo wa taarifa zisizo sahihi husababisha taharuki katika jamii hivyo ni wakati wa kuonesha utofauti kwa kuzingatia maadili ya taaluma hii - Dk. Dotto Biteko, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.

Naibu Waziri Mkuu, Dk. Dotto Biteko amesema,  tukio la Uchaguzi Mkuu ni la muda tu hivyo Watanzania wote tuvumiliane na ...
09/07/2025

Naibu Waziri Mkuu, Dk. Dotto Biteko amesema, tukio la Uchaguzi Mkuu ni la muda tu hivyo Watanzania wote tuvumiliane na kuheshimiana katika mawazo.

Dk. Biteko ambaye pia ni Waziri wa Nishati, ametoa kauli hiyo leo tarehe 9 Julai 2025 wakati akifungua Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025, jijiji Dar es Salaam.

Amesema, katika kipindi hiki ni kawaida mtoto kutofatiana mawazo na hata baba yake, na kwamba kinachopaswa ni kuvumiliana utofauti wa mawazo.

"Tuendelee kuhimiza maelewano na utamaduni wa kuheshimu tofauti za maoni.

"(Wanahabari) tutumie lugha za staha na kuripoti bila upendeleo. Watakaoshepu taifa letu liende wapi si wanasiasa bali ni nyinyi vyombo vya habari," amesema.

Serikali tunathamini uwepo wa media tena iliyo imara, serikali tunapotaka kujipima na kujitazama tunajiangalia kupitia m...
08/07/2025

Serikali tunathamini uwepo wa media tena iliyo imara, serikali tunapotaka kujipima na kujitazama tunajiangalia kupitia media.’ – Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo akizungumza na wahariri kuhusu Dira ya Maendeleo 2050 jijini Dar es Salaam.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linampongeza Dk. Kaanaeli Kaale kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabar...
29/06/2025

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linampongeza Dk. Kaanaeli Kaale kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA).

Fursa kwa Waandishi wa Habari!Je, una shauku ya kusimulia habari zenye mguso na kufichua ukweli? Usikose nafasi hii ya k...
24/06/2025

Fursa kwa Waandishi wa Habari!
Je, una shauku ya kusimulia habari zenye mguso na kufichua ukweli? Usikose nafasi hii ya kipekee ya kuboresha ujuzi wako, kupanua mtandao wako wa kitaaluma, na kuwa sehemu ya mpango wa kubadilisha tasnia ya uandishi wa habari. Omba sasa!

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Bw. Hamad Abdallah  amewaeleza wahariri wa yombo vya habari nchini ...
16/06/2025

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Bw. Hamad Abdallah amewaeleza wahariri wa yombo vya habari nchini juu ya kuendelezwa miradi ya shirika hiyo iliyosimama kwa muda mrefu kutokana na changamoto za kiutendaji.



Katika ziara hiyo iliyofanyika leo Juni 16, 2025 wahariri walizungukia miradi minne ikiwemo Moroco Square, 711, Golden Premier Residences (GPR) na Mradi wa makazi nafuu Kawe jijini Dar es Salaam.



Bw. Abdallah alibainisha kuwa baadhi ya miradi ilikwama kwa zaidi ya miaka minane sasa imefufuliwa kwa kasi kubwa kufuatia upatikanaji wa mkopo wa maendeleo ulioridhiwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hatua hii imeelezwa kuwa ni uthibitisho wa dhamira ya kweli ya serikali katika kujenga taifa kwa uwazi, ubora, na weledi.



Aidha, ziara hiyo ilikuwa na lengo la kuwapa wahariri uelewa wa kina kuhusu maendeleo ya sekta ya ujenzi wa makazi ya kisasa yanayotekelezwa kwa kasi chini ya mpango wa serikali wa kuboresha miundombinu ya makazi kwa wananchi na wawekezaji.

Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Nchemba, ametangaza bungeni kuwa serikali imefuta kodi kwenye matangazo yote ya magazeti  ya...
13/06/2025

Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Nchemba, ametangaza bungeni kuwa serikali imefuta kodi kwenye matangazo yote ya magazeti yanayozalishwa nchini.

Dk. Nchemba alitoa taarifa hiyo wakati akisoma Bajeti Kuu kwa Mwaka wa Fedha 2025 / 2026 jana.

“Hatua hii itatoa ahueni kubwa kwani kati ya chanzo cha kifo cha magazeti imekuwa hii Kodi ya VAT.

“Imekuwa kila mara unatoa risiti ya EFD kwa matangazo, halafu hiyo risiti inachelewa kulipwa, tunadaiwa VAT ambayo hatujapokea malipo,” amesema Deodatus Balile, Mwenyekiti waJukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Editors Forum-TEF posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tanzania Editors Forum-TEF:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share