25/11/2025
K**a maovu yote yaliyopangwa kutokea (tarehe 29 Oktoba 2025) yangetimia, gharama za maisha zingekuwa juu kabisa.
Ni kauli ya Waziri Mkuu wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba akizungumzia vurugu zilizotokea wakati na baada ya Uchgazi Mkuu 2025 kwenye mkutano wake na wahariri jijiji Dar es Salaam leo tarehe 25 Novemba 2025.
"Ombi langu, sote tunuie jambo la namna hii lisitokee tena kwenye nchi yetu. Linatutengenezea makovu yasiyopona," amesema Dk. Mwigulu.
Waziri huyo amesema, mpaka sasa watu wengi hawajui undani wa namna mpango ulivyopangwa huku akisisitiza Watanzania kuwa pamoja na kujadili mambo yao bila kuingiliwa.
"Tunatumwa uovu dhidi ya maisha yetu. Fuatilieni wenzetu walioharibikiwa, walifanya mdhaha, wengine hawakujua na walikuja kujua kwenye majuto.
"Wale wanaomezea mate na kutumwa kutugawa, niwahakikishie tutailinda Tanzania kwa gharama yoyote ile. Watameza mate mpaka yaishe na wala Tanzania haitaendshwa kwa remote," amesema.
Katika mkutano huo Dk. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuwa makini na makundi ya watu wenye nia ya kuichafua na kuiharibu Tanzania