Tanzania Editors Forum-TEF

Tanzania Editors Forum-TEF We defend freedom of expression and promote editorial excellence as keystone to realization of mature democracy in Tanzania.

05/09/2025
Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
01/09/2025

Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025

Ile faida unayoingiza kwa kukwepa kutumia nishati safi, utakuja kuitumia kutibu madhara yatokanayo na matumizi ya nishat...
22/08/2025

Ile faida unayoingiza kwa kukwepa kutumia nishati safi, utakuja kuitumia kutibu madhara yatokanayo na matumizi ya nishati chafu hapo baadaye.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akizungumza kwenye Kongamano la Matumizi ya Nishati Safi na Salama 'Pika Kijanja 2025' lililofanyika leo tarehe 22 Agosti 2025, jijini Da es Salaam.

Kwenye kongamano hilo, wadau mbalimbali walishiriki ikiwemo mamalishe, babalishe, taasisi za serikali na za binafsi.

Tutatumia vyombo vyetu vya habari kuhakikisha tunapeleka elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi n...
22/08/2025

Tutatumia vyombo vyetu vya habari kuhakikisha tunapeleka elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi na salama katika jamii yetu ili kufikia malengo ya serikali.

Ni kauli ya Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Stella Aron aliyoitoa kwenye Kongamano la Pika Kijana 2025.

Kongamano hilo limefanyika leo tarehe 22 Agosti 2025, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila.

Mwanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMW...
22/08/2025

Mwanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Dk. Rose Reuben akizungumza wakati wa mada ya 'Tunawezaje kubadili dhana na mtazamo juu ya nishati safi ya kupikia' katika Kongamano la Pika Kijanja 2025, jijini Dar es Salam.

Kongamano hilo limelisisitiza matumzi ya nishati safi kwa maendeleo endelevu kwani matumizi ya nishati huyo hupungu gharama kwa kiwango kikubwa.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake (WPL), Neema Lugangira akikabidhi nakala za Mwongozo wa Uchaguz...
19/08/2025

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake (WPL), Neema Lugangira akikabidhi nakala za Mwongozo wa Uchaguzi Afrika wa Digital na Mitandao ya Kijamii kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania Deodatus Balile, katikati ni mwenyekiti wa jukwaa hilo Dk. Bakari Machumu.

Meneja Kanda ya Kinondoni kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii - PSSSF, Haji Moshi amekumbusha waajiri kuwasilisha michango ...
18/08/2025

Meneja Kanda ya Kinondoni kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii - PSSSF, Haji Moshi amekumbusha waajiri kuwasilisha michango ya waajiriwa wao kwa wakati.

Akizungumza kwenye mkutano wa kawaida wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) leo tarehe 18 Agosti 2025, akiwa mgeni mwalikwa, Haji amewaomba wahariri kuwakumbusha waajiriwa hao kutekeleza wajibu wao.

"Naomba kupitia jukwaa hili (la wahariri) kuwakumbusha waajiri kupeleka michango ya uanachama wao," amesema Haji.

Katibu wa Jumuiya ya Viongozi Wanawake duniani (WPL), Neema Lugangira ameshauri wahariri kuhakikisha wanatumia kwa usahi...
18/08/2025

Katibu wa Jumuiya ya Viongozi Wanawake duniani (WPL), Neema Lugangira ameshauri wahariri kuhakikisha wanatumia kwa usahihi teknolojia ya Akili Unde (AI) wakati wa Uchaguzi Mkuu kuepusha madhara katika vyombo vya habari.

Akitoa mada ya 'Uchaguzi Mkuu na Matumizi ya AI' kwenye mkutano wa kawaida wa TEF, jijini Dar es Salaam leo tarehe 18 Agosti 2025 amesema, katika uchaguzi kuna taatifa nyingi potofu hivyo AI inaweza kutumika vizuri kuhakiki usahihi wa taarifa.

"Kuna faida nyingi za kutumia AI ikiwemo kusaidia kuhakiki taarifa kwa haraka, kufuatilia kauli za uchochezi hata uchambuzi wa data," amesema.

Neema amesema, licha ya AI kuwa na matumizi makubwa kwenye dunia ya sasa, pia hutumika kupotosha jamii sambamba na kuharibu heshima ya mtu / mgombea katika jamii.

Amesisitiza kwamba, vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda maadili katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limetambulisha majina manane ya wanachama wapya wa jukwaa hilo wakati wa mkutano wa ka...
18/08/2025

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limetambulisha majina manane ya wanachama wapya wa jukwaa hilo wakati wa mkutano wa kawaida uliofanyika leo tarehe 18 Agosti 2025 jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa jukwaa hilo Deodatus Balile ametaja majina ya wanachama hao kuwa ni Innocent Mungy, Rodney Mbuya, Angetila Ossiah, Penzi Nyamungumi, Edda Sanga, Dk. Cosmas Mwaisombwa, Tutus Kaguo na David Rwenyagira.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Salim Said Salim ameshauri Mamlaka ya Mapato Tanzania...
11/08/2025

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Salim Said Salim ameshauri Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa karibu na wahariri katika kipindi chote cha Kampeni ya Elimu ya Kodi kwa Biashara za Mtandaoni.

Salim alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha TRA na wahariri kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.

“Ni wajibu wetu wanahabari kupokea elimu na kuifanyia kazi. Nikuombe Kamisha, wasaididzi wako wawe karibu na vyombo vya habari kwa ajili ya kutoa elimu, miongoni mwa kazi ya vyombo vya habari ni kujenga jamii kwa elimu k**a hizi,” alisema Salim.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda alisema, wanaolengwa katika usajili huo ni wafanyabiashara wenye kipato cha zaidi ya Tsh. 4 Milioni kwa mwaka ambao kodi yao itakuwa Tsh. 100,000 na kila mmoja atalipa kulingana na kipato chake.

Heri ya Nanenane kwa Watanzania wote
08/08/2025

Heri ya Nanenane kwa Watanzania wote

Address

Mtendeni
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Editors Forum-TEF posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tanzania Editors Forum-TEF:

Share