Simba SC Footbal

Simba SC Footbal •Akaunti rasmi ya Simba SC Football kwa habari za michezo.
•Fans
•Kwa matangazo ya biashara tutafute WhatsApp 0712 125 518

Mchezaji wa Klabu ya Liverpool, Diogo Jota amefariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea kwenye Jimbo la Zamora ...
03/07/2025

Mchezaji wa Klabu ya Liverpool, Diogo Jota amefariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea kwenye Jimbo la Zamora nchini Hispania.

Taarifa zinasema ajali hiyo imetokea baada ya gari walilokuwa wakisafiria Jota na kaka yake André (26) ambaye naye ni mchezaji wa soka wa kulipwa kuacha njia na kuwaka moto.







Bodi ya Wakurugenzi ya Simba imekutana na Bodi ya Washauri ya kujadili mambo mbalimbali ya klabu ikiwemo tathmini ya msi...
02/07/2025

Bodi ya Wakurugenzi ya Simba imekutana na Bodi ya Washauri ya kujadili mambo mbalimbali ya klabu ikiwemo tathmini ya msimu uliopita na mipango ya msimu ujao ikiwemo usajili.







𝐀𝐘𝐎𝐔𝐁 𝐋𝐀𝐊𝐑𝐄𝐃 𝐌𝐁𝐈𝐎𝐍𝐈 𝐊𝐔𝐑𝐔𝐃𝐈 𝐌𝐎𝐑𝐎𝐂𝐂𝐎, 𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐈 𝐘𝐀𝐊𝐄 𝐍𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐁𝐀 𝐘𝐀𝐅𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐓𝐀𝐌𝐀𝐓𝐈Here We Go📍 Mlinda mlango wa Klabu ya Simba SC Ay...
01/07/2025

𝐀𝐘𝐎𝐔𝐁 𝐋𝐀𝐊𝐑𝐄𝐃 𝐌𝐁𝐈𝐎𝐍𝐈 𝐊𝐔𝐑𝐔𝐃𝐈 𝐌𝐎𝐑𝐎𝐂𝐂𝐎, 𝐒𝐀𝐅𝐀𝐑𝐈 𝐘𝐀𝐊𝐄 𝐍𝐀 𝐒𝐈𝐌𝐁𝐀 𝐘𝐀𝐅𝐈𝐊𝐈𝐀 𝐓𝐀𝐌𝐀𝐓𝐈

Here We Go📍

Mlinda mlango wa Klabu ya Simba SC Ayoub Lakred yupo mbioni kurejea kwao Morocco baada ya mkataba wake na Wekundu wa Msimbazi kumalizika rasmi huku kukiwa hakuna dalili ya kuhuishwa Kwa mkataba huo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Klabu hiyo hakuna mazungumzo yoyote kati ya Simba na Lakred kuhusu kuongeza mkataba mpya hali hiyo inaashiria kuwa safari ya kipa huyo ndani ya Klabu hiyo ya Tanzania inakaribia mwisho.

Lakred alikuwa chaguo la kwanza kwenye lango la Simba misimu miwili iliyopita lakini hali ilibadilika ghafla alipoumia wakati wa maandalizi ya msimu ulioisha Nchini Misri.

Majeraha hayo yalimsababisha kukaa nje Kwa muda mrefu hali iliyowalazimu Simba kumsajili kipa wa Kimataifa kutoka Guinea Moussa Camara ambaye amemaliza msimu akiwa na clean sheet 19 rekodi Bora kabisa Kwa msimu wa 2024/2025

©







SIMBA YATUA ASEC MIMOSA'S KUMNG'OA SALIFOU DIARRASSOUBAHere We Go📍Klabu ya Simba Ipo katika hatua za Mwisho kukamilisha ...
01/07/2025

SIMBA YATUA ASEC MIMOSA'S KUMNG'OA SALIFOU DIARRASSOUBA

Here We Go📍

Klabu ya Simba Ipo katika hatua za Mwisho kukamilisha Usajili wa Winga wa Asec Mimosas Salifou Diarrassouba mwenye Umri wa miaka 23.

Tayari Mazungumzo ya Awali yamefanyika baina ya menejimenti ya Mchezaji na Klabu ya Simba SC na mchezaji ameonesha Nia Nzuri ya Kujiunga na Wekundu wa Msimbazi.

Msimu Uliopita Simba na yanga walishindwa Kumsajili mchezaji huyo Baada ya MC Alger Kuonesha Nia Kubwa ya kumsajili Ambapo pia Dili Hilo lilikufa Dakika za Jioni.

Follow us - Instagram

Usisahau ku - Like , comment & share zaidi , kupata updates mbalimbali kutoka kwetu.

| |

Sasa naanza kuelewa kwanini wamakonde wanakula panya 🤔🤔🤔
01/07/2025

Sasa naanza kuelewa kwanini wamakonde wanakula panya 🤔🤔🤔

PERCY TAU KUJIUNGA NA SIMBA SC MSIMU UJAOHERE WE GO🔴  Klabu ya Simba SC kutoka Tanzania ipo hatua za mwisho za kuinasa S...
01/07/2025

PERCY TAU KUJIUNGA NA SIMBA SC MSIMU UJAO

HERE WE GO🔴

Klabu ya Simba SC kutoka Tanzania ipo hatua za mwisho za kuinasa Saini ya mshambuliaji wa Zamani wa Al Ahly anayekipiga kunako klabu ya Qatar SC Percy Muzi Tau Kwa mkataba wa miaka mitatu

Simba SC wamemwekea kitita cha Dola za kimarekani USD 769,231 ni sawa na sh Bilioni 2 za kitanzania ili kuinasa Saini yake

Endapo watafanikiwa kuinasa Saini yake hakika Mnyama anaenda kuwa imara msimu ujao na sioni Timu yoyote Tanzania inatakayoweza kumzuia Mnyama kunyakua Mataji yake aliyoyakosa Kwa misimu minne mfululizo.

Pia Simba wapo mbioni kuinasa Saini ya mlinzi wa kushoto wa Al Hilal ya Sudani Khadim Diaw ili kuimarisha eneo la ulinzi wa upande wa kushoto.

Endelea kufuatilia Simba SC Football Kwa habari za michezo na Burudani.




Siku ya kwanza kwenye uwanja wa mazoezi tukiwa Ismailia.
28/03/2025

Siku ya kwanza kwenye uwanja wa mazoezi tukiwa Ismailia.

Njia pekee ya kuonyesha namna gani tumefurahishwa na maamuzi haya ni kuujaza katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Masr...
28/03/2025

Njia pekee ya kuonyesha namna gani tumefurahishwa na maamuzi haya ni kuujaza katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Masry.

Kikosi cha Simba SC kimeondoka Nchini Alfajili ya leo Ijumaa kuelekea Misri tayari kwa mchezo wa robo fainali ya kombe l...
28/03/2025

Kikosi cha Simba SC kimeondoka Nchini Alfajili ya leo Ijumaa kuelekea Misri tayari kwa mchezo wa robo fainali ya kombe la Shirikisho CAFCC dhidi ya Al Masry

Mchezo huo utapigwa April 02 katika dimba la Suez ndani ya Mji wa Suez.

Kikosi ambacho kitaondoka kesho alfajiri kwenda nchini Misri.
27/03/2025

Kikosi ambacho kitaondoka kesho alfajiri kwenda nchini Misri.

Mabao ya Joshua Mutale na Lionel Ateba aliyefunga kupitia mkwaju wa penati yametosha kuihakikishia Simba SC ushindi muhi...
27/03/2025

Mabao ya Joshua Mutale na Lionel Ateba aliyefunga kupitia mkwaju wa penati yametosha kuihakikishia Simba SC ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Bigman FC na kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB

Ulikuwa mchezo ambao Simba SC ilihitaji ushindi zaidi ili kutinga robo fainali na kuweka nguvu katika mchezo wa robo fainali ya CAFCC dhidi ya Al Masry utakaopigwa April 02 huko Misri

Simba SC iliwakosa wachezaji wake wengi muhimu wa kikosi cha kwanza ambao walikuwa katika majukumu ya Timu za Taifa

Joseph Henock alifunga bao pekee la Bigman FC ambao walionekana kuleta upinzani hasa kipindi cha pili.

FULL TIME: SIMBA SC 2️⃣🆚1️⃣ BIGMAN FC
27/03/2025

FULL TIME: SIMBA SC 2️⃣🆚1️⃣ BIGMAN FC

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simba SC Footbal posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Simba SC Footbal:

Share

Category