Marble Africa

Marble Africa We deliver timely, accurate, and engaging stories across various topics, ensuring our audience stays informed and inspired..
📌 WE ARE AFRICA

12/09/2025

DRC: Mahak**a ya Kijeshi ya DRC inatarajia kutoa hukumu ya rais wa zamani Joseph Kabila Ijumaa hii. Kabila, ambaye yuko uhamishoni kwa zaidi ya miaka miwili, anakabiliwa na tuhuma nzito za kushirikiana na waasi wa M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda.

Mashirika ya kiraia yanadai fidia ya mabilioni ya dola, huku chama chake PPRD kikiita kesi hii njama ya kisiasa. Hatima yake iko mikononi mwa mahak**a, na dunia inasubiri kuona kitakachotokea.

Bunge la Rwanda limepitisha kwa kauli moja makubaliano ya amani kati yake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Mak...
31/07/2025

Bunge la Rwanda limepitisha kwa kauli moja makubaliano ya amani kati yake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Makubaliano hayo yalisainiwa Juni 27, 2025 mjini Washington chini ya usimamizi wa Marekani, na kupitishwa rasmi na Bunge Julai 30 jijini Kigali.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, aliwaeleza wabunge kuwa Rwanda haitalegeza hatua zake za kiusalama hadi kundi la waasi la FDLR litakapoangamizwa. Pia alisisitiza umuhimu wa Kinshasa kutekeleza kikamilifu makubaliano hayo k**a ishara ya dhamira ya kweli ya kurejesha amani ya kudumu.

Baada ya kupitishwa na Bunge la Rwanda, mkataba huo sasa utapelekwa kwenye Seneti kwa hatua zaidi. Kwa upande wa DRC, bado hakuna taarifa rasmi ya kuwasilishwa kwa mkataba huo bungeni, kwani Bunge lao liko likizoni, japo baadhi ya wabunge wameomba suala hilo lijadiliwe mara moja likirejea.

Katika kuendeleza utekelezaji wa makubaliano hayo, Rwanda na DRC zinatarajiwa kukutana wiki hii mjini Washington kwa kikao cha kwanza cha Kamati ya Pamoja ya Kusimamia Makubaliano. Kamati hiyo itaangazia malalamiko, uchunguzi wa ukiukwaji, utatuzi wa migogoro, na mapendekezo ya hatua stahiki kuhakikisha amani ya kweli inafikiwa.

Klabu ya Chelsea Football Club ya nchini Uingereza imefanikiwa kutwaa taji la kombe la dunia kwa ngazi ya vilabu (FIFA C...
13/07/2025

Klabu ya Chelsea Football Club ya nchini Uingereza imefanikiwa kutwaa taji la kombe la dunia kwa ngazi ya vilabu (FIFA CLUB WORLD CUP 2025) mara baada ya kuifunga klabu ya PSG ya nchini ufaransa kwa magoli 3-0 katika mchezo wa fainali wa mashindano hayo.

Mchezo huo uliopigwa kuanzia majira ya saa 4 kamili za usiku katika dimba la MetLife stadium,mjini New Jersey nchini Marekani umeshuhudiwa na watu mbalimbali dunia kote akiwemo rais wa Marekani Donald Trump.

Magoli ya Chelsea yaliyofungwa na Cole Palmer(alifunga mawili) na Joao Pedro yalitosha kuwapa ubingwa wababe hao wa London,na kuwa klabu ya kwanza kuwa mabingwa wa kombe hilo toka lilipobadirishwa muundo wa kiushindani.

✍️|

Klabu ya Simba SC imetangaza rasmi kuachana na aliyekuwa nyota wao raia wa DR Congo,Fabrice Ngoma.Taarifa mbalimbali zin...
12/07/2025

Klabu ya Simba SC imetangaza rasmi kuachana na aliyekuwa nyota wao raia wa DR Congo,Fabrice Ngoma.Taarifa mbalimbali zinadai kuwa nyota huyo amemalizana na moya klabu kutoka katika mataifa ya kaskazini mwa Afrika.

✍️|

  Je,ni sahihi mwanadada mcheza soka kufanya mazoezi ya mpira hali ya kuwa mjamzito?.Tukutane kwenye comment..
12/07/2025

Je,ni sahihi mwanadada mcheza soka kufanya mazoezi ya mpira hali ya kuwa mjamzito?.

Tukutane kwenye comment..

Klabu ya Liverpool imetangaza rasmi kuistaafisha jezi namba 20 kwa heshima ya aliyekuwa mchezaji wao aliyepoteza maisha ...
11/07/2025

Klabu ya Liverpool imetangaza rasmi kuistaafisha jezi namba 20 kwa heshima ya aliyekuwa mchezaji wao aliyepoteza maisha hivi karibuni,Diogo Jota mnamo tarehe 3 julai.

Source:

Klabu ya Tottenham Hotspurs imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji raia wa Ghana, Mohammed Kudus kuwa mchezaji wao mpy...
10/07/2025

Klabu ya Tottenham Hotspurs imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji raia wa Ghana, Mohammed Kudus kuwa mchezaji wao mpya akitokea West Ham United.

Kudus amesaini mkataba wa miaka sita(6) utakaomuweka kwa wababe hao wa London hadi 2031.

✍️|

Klabu ya Singida Black Stars imemtambulisha beki wa zamani wa kulia wa simba,Kelvin Kijili kuwa mchezaji wao kwa kandara...
10/07/2025

Klabu ya Singida Black Stars imemtambulisha beki wa zamani wa kulia wa simba,Kelvin Kijili kuwa mchezaji wao kwa kandarasi ya miaka miwili(2).

Source:

Klabu ya Real Madrid imesema kwa yeyote anayehitaji huduma ya kinda wao raia wa Brazil 🇧🇷 Rodrygo Goes,basi watoe kitita...
10/07/2025

Klabu ya Real Madrid imesema kwa yeyote anayehitaji huduma ya kinda wao raia wa Brazil 🇧🇷 Rodrygo Goes,basi watoe kitita cha £ 100M ili kuipata saini ya nyota huyo.

Rodrygo ambaye hivi karibuni kupitia wakala wake alisema kuwa Real Madrid wanamkosea mteja wake kwani hawatoi tamko rasmi la hatma ya nyota huyo,hali inayomfanya kukosa furaha kikosini.

Rodrygo amewakati mgumu katika kikosi cha Los brancos kilicho chini ya kocha Xabi Alonso hali inayomfanya ahitaji changamoto nyengine mara baada ya kuona ufinyu wa nafasi katika kikosi cha wababe hao wa Ulaya.

✍️|

Leo ndiyo ulikuwa mchezo wa mwisho wa kiungo mshambuliaji raia wa Crotia,Luka Modric akiwa na jezi ya Real Madrid ambapo...
09/07/2025

Leo ndiyo ulikuwa mchezo wa mwisho wa kiungo mshambuliaji raia wa Crotia,Luka Modric akiwa na jezi ya Real Madrid ambapo ameshuhudia timu yake ikipoteza kwa kipigo cha mabao 4-0 dhidi ya Paris Saint Germain,katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la dunia kwa ngazi ya vilabu duniani.

Luka Modric alijiunga na Real Madrid mnamo tarehe 27 Agosti mwaka 2012 akitokea Tottenham Hotspurs akiwa ni miongoni mwa wale nyota tishio wa ile Madrid tishio barani Ulaya.

Taarifa zinaeleza Modric anaenda kujiunga na klabu ya AC Milan ya Italy.

✍️|

Klabu ya PSG usiku wa leo wametinga hatua ya fainali ya kombe la dunia kwa ngazi ya vilabu duniani mara baada ya kuichap...
09/07/2025

Klabu ya PSG usiku wa leo wametinga hatua ya fainali ya kombe la dunia kwa ngazi ya vilabu duniani mara baada ya kuichapa mabao 4-0 klabu ya Real Madrid,hivyo wataenda kukutana na Chelsea FC ya England ambayo ilitinga fainali jana mara baada ya kuwafunga Fluminense FC ya Brazil mabao 2-0.

PSG ambaye ni mabingwa wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu uliotamatika wanaenda kukutana na mabingwa wa UEFA CONFERENCE LEAGUE msimu uliotamatika Chelsea FC.

Fainali ya FIFA CLUB WORLD CUP itapigwa siku ya jumapili ya tarehe 13 mwezi Julai 2025 katika dimba la MetLife Studium katika jiji la East Rutherford,New Jersey,Marekani.

✍️|

USA president Donald Trump calls Bolsonaro’s coup trial a “Witch Hunt” and warns tariffs will begin August 1 if it’s not...
09/07/2025

USA president Donald Trump calls Bolsonaro’s coup trial a “Witch Hunt” and warns tariffs will begin August 1 if it’s not stopped. Brazil joins 21 other nations facing tough new trade threats.

Is this trade pressure, or political interference?

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Marble Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Marble Africa:

Share