
13/07/2025
Klabu ya Chelsea Football Club ya nchini Uingereza imefanikiwa kutwaa taji la kombe la dunia kwa ngazi ya vilabu (FIFA CLUB WORLD CUP 2025) mara baada ya kuifunga klabu ya PSG ya nchini ufaransa kwa magoli 3-0 katika mchezo wa fainali wa mashindano hayo.
Mchezo huo uliopigwa kuanzia majira ya saa 4 kamili za usiku katika dimba la MetLife stadium,mjini New Jersey nchini Marekani umeshuhudiwa na watu mbalimbali dunia kote akiwemo rais wa Marekani Donald Trump.
Magoli ya Chelsea yaliyofungwa na Cole Palmer(alifunga mawili) na Joao Pedro yalitosha kuwapa ubingwa wababe hao wa London,na kuwa klabu ya kwanza kuwa mabingwa wa kombe hilo toka lilipobadirishwa muundo wa kiushindani.
✍️|