Bantu Media

Bantu Media Hard News | Entertainment | Gossip | Celebrity News | Sports News

Tangaza Nasi Kupitia +255658840840

30/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Kasheku Msukuma, amewataka wauguzi nchini kuzingatia ukweli na kusimamia misingi ya taaluma yao ili kujenga imani kwa wagonjwa wanaowahudumia.

Msukuma alitoa wito huo jana Mei 29, 2026 wakati akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Nzera.

Alisisitiza kuwa hatishwi na lawama za mitandaoni iwapo anasimamia ukweli na kutetea maslahi ya wananchi wa jimbo lake. Aidha, alieleza kuwa Chama Cha Mapinduzi - CCM - kinafundisha wanachama wake kuwa wakweli ili kukiimarisha chama na kuendelea kuaminiwa na wananchi, ahadi ambayo alisema ataiendeleza.

29/05/2026

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwigulu Nchemba amesema Serikali imetoa zawadi ya sh. milioni 500 kwa Timu ya Taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kwa kufanikiwa kutinga hatua ya fainali ya mashindano hayo na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo (Ijumaa, Mei 29, 2026) ofisini kwake Mlimwa, Dodoma wakati akitoa salamu za pongezi kwa timu hiyo kufuzu hatua ya fainali kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema Rais Samia amewapongeza wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wote wa timu kwa mafanikio hayo makubwa ambayo yameendelea kuandika historia mpya katika sekta ya michezo nchini.

Mwanamuziki wa Singeli  amuandikia barua ya wazi tajiri GSM akimuomba msaada wa matibabu ya kufanya surgery akidai Miguu...
29/05/2026

Mwanamuziki wa Singeli amuandikia barua ya wazi tajiri GSM akimuomba msaada wa matibabu ya kufanya surgery akidai Miguu hiyo haipo k**a binadamu wa kawaida ameweka wazi kuwa watu wanaona k**a ni trend ila kwake ni changamoto ya kweli.

29/05/2026

28/05/2026
28/05/2026

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amemteua Haji Manara kuwa msemaji wa timu zote za Taifa za Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo Mei 28, 2026, Waziri Makonda amesema Haji atafanya kazi chini ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na atazisemea timu zote za Taifa za mpira wa miguu.

26/05/2026

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, baada ya Kukemea vikali tabia zinazokiuka maadili ya Kitanzania kwa baadhi ya watengeneza maudhui mitandaoni,

alimtaka mbali na kuomba msamaha kwa kutumia video yeye anachotaka ni ajipeleke mwenyewe, ana mengi sana juu yake kabla ya kusikiliza msamaha wake aliandika Waziri Gwajima kwenye comment baada ya post ya mwanadada uyo Asnat.

Swipe kutazama video>>>

Mama Mzazi wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, Suzana Mag...
25/05/2026

Mama Mzazi wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, Suzana Magufuli amefariki dunia leo Mei 25, 2026, Chato Mkoani Geita baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akizungumza kwa njia ya simu, Mtoto wa Hayati Magufuli, Jesca Magufuli amethibitisha kutokea kwa msiba huo akieleza kuwa Bibi Suzana amefariki saa 1 usiku Nyumbani kwake Chato.

“Bibi yetu (Suzana M***a) amefariki saa moja nyumbani kwake Chato baada ya kuugua kwa muda mrefu, taratibu za msiba familia itawajulisha, Bwana ametoa na Bwana ametwaa”

🗣️Jesca.

Pumzika bibi yetu

21/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Msalala Mabula Magangila ameitaka Serikali kufikiria upya matumizi ya bandari kavu ikiwemo Bandari ya Isaka wilayani Kahama, akisema matumizi makubwa ya malori kusafirisha mizigo kwenda na kutoka nchi jirani yanaendelea kuharibu barabara huku Serikali ikitumia mabilioni ya fedha kwenye matengenezo.

‎Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/27, Magangila amesema hakuna sababu ya malori kutoka nchi za Rwanda, Burundi, Congo DRC na Uganda kufuata mizigo hadi Dar es Salaam wakati mizigo hiyo inaweza kusafirishwa kwa reli kupitia bandari kavu ya Isaka.

‎“Ni kitu gani kinatusababisha mizigo yetu yote ya transit ambayo inakwenda Rwanda, Burundi, Congo DRC na Uganda kwanini maroli yanaifuata Dar es Salaam wakati tuna bandari kavu ya Isaka na ilishawahi kuwa hivyo huko nyuma? Kwanini tunaendelea kutumia gharama kubwa ya matengenezo ya barabara kipande hiki? Reli ya kati inapita pale, SGR inapita hapo kwanini Serikali haifikirii kupunguza mzigo kwa kuanza kutumia bandari kavu ya Isaka? Hivi kweli magari kutoka Rwanda, Burundi, Congo DRC na Uganda yanafuata nini Dar es Salaam?” Mabula Magangila - Mbunge wa Jimbo la Msalala.


‎“Serikali chukueni mawazo yetu sisi vijana na sisi tuweze kuokoa hili taifa, mnufaike na wakati wetu wa sasa tukumie njia mbadala kuokoa gharama inayotumika kwenye matengenezo ya barabara zetu ili pesa tutakayo kwenda kuiokoa twende tukajenge mtandao mwingine wa lami kwenye barabara zetu nyingi ambazo sasa ni za changarawe,” amesema Magangila.

21/05/2026

Tazama Alikiba na Harmonize Walivyoshindana kupiga Push up wakiwa Gym.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255782511323

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bantu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share