Infotznews

Infotznews Mbeba Majukumu Ya Duniani na Mbinguni, Rohoni na Mwilini.

WAZIRI MBARAWA AMKABIDHI OFISI WAZIRI BASHUNGWAWaziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amezungumzia umuhimu wa Wizar...
08/09/2023

WAZIRI MBARAWA AMKABIDHI OFISI WAZIRI BASHUNGWA

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amezungumzia umuhimu wa Wizara ya Ujenzi kuendeleza miradi ya kimkakakati ya ujenzi wa barabara kwa utaratibu wa uhandisi, manunuzi ujenzi na fedha (EPC+F) na ujenzi wa miradi kwa njia ya ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi (PPP) ili kufikia matarajio ya Serikali.

Akizungumza wakati akimkabidhi Ofisi Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa, jijini Dodoma, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema kazi kubwa ya kuweka misingi ya kuendeleza miradi hiyo imekamilika hivyo kazi iliyobaki ni kuendelea na kasi ya uendelezaji wa miradi hiyo.

“Mheshimiwa Waziri unayo timu nzuri ya kukusaidia kufanya kazi, hivyo itumie na kuwaongezea uzoefu wa kimataifa katika kusimamia miradi ili kuiwezesha Tanzania kuendana na kasi ya mabadiliko ya miundombinu ya kidunia”, amesisitiza Profesa Mbarawa.

Amezungumzia umuhimu wa Wizara kujenga uwezo wa kutayarisha wahandisi washauri wa miradi inayotekelezwa nchini badala ya kutumia wataalamu kutoka nje ya nchi k**a ilivyo sasa.

Aidha, Profesa Mbarawa amewashukuru wataalamu na watumishi wa Wizara ya Ujenzi kwa ushirikiano waliompa na kumsisitiza Waziri Bashungwa kuendeleza ushirikiano huo ili kufanikisha malengo ya Sekta.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa,  amemshukuru Profesa Mbarawa kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa kutekeleza miradi mikubwa ya barabara, madaraja, nyumba na ujenzi wa wa viwanja vya ndege na kuahidi kuendeleza utamaduni huo ili kuleta tija kwa wananchi.

“Tutahakikisha msingi uliojenga tunauendeleza hususan kuongeza barabara za kisasa, nyumba za viongozi na watumishi wa umma na kuhakikisha vivivuko na utengenezaji wa magari unakuwa wa uhakika”, amesema Waziri Bashungwa.

Katibu Mkuu, Mha. Balozi Aisha Amour, amemshukuru Profesa Mbarawa kwa miongozo yake na kumuahidi kumpa ushirikiano Mheshiwa Bashungwa katika usimamizi wa miradi mbalimbali ili kuweza kufikia malengo ya Serikali ya awamu ya Sita katika uendelezaji wa miundombinu nchini.

DKT. BITEKO AFUNGA KONGAMANO LA AGRFNaibu Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Doto Biteko kwa niaba ya Waziri Mkuu amefunga Rasmi Kong...
08/09/2023

DKT. BITEKO AFUNGA KONGAMANO LA AGRF

Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Doto Biteko kwa niaba ya Waziri Mkuu amefunga Rasmi Kongamano la mifumo ya Chakula lililofanyika JNICC.

Akifunga Kongamano hilo Mhe. Dkt. Naibu Waziri Biteko amesema "Kongamano hili limetaka kuwepo kwa uongozi thabiti ili kuleta mabadiliko yatakayoleta uwekezaji na limetoa jukwaa kwa viongozi na watengeneza sera likilenga vijana na wanawake kuweza kutumia vizuri rasilimali zilizopo."

Aidha amezitaka Serikali za Afrika kuweka uwiano katika sera zao ili kuwepo kwa mabadiliko katika Sera za Chakula.

Mwisho amemaliza kwa kuwakaribisha tena kufanyia Kongamano lingine Dar-es-Salaam huku akiamini jukwaa lingine mwakani litakuwa na nguvu na washiriki wengi zaidi.

"Upole sio ujinga hata kidogo, upole sio ujinga, upole saa nyingine ndio maarifa unatulia, unafikiri jambo mara mbili ma...
03/09/2023

"Upole sio ujinga hata kidogo, upole sio ujinga, upole saa nyingine ndio maarifa unatulia, unafikiri jambo mara mbili mara tatu kabla hujatoa maamuzi, kabla haujatoa kauli."

wakati wa uapisho wa Viongozi uliofanyika Ikulu ndogo, Septemba 1, 2023 Tunguu Zanzibar.

DK. MWINYI AFURAHISHWA KUONA SIMBA NA CHUI KIZIMKAZI ZANZIBARRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. ...
27/08/2023

DK. MWINYI AFURAHISHWA KUONA SIMBA NA CHUI KIZIMKAZI ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amempongeza Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wake wa kuasisi wazo la kuwa na Tamasha la Kizimkazi kwa madhumuni ya kuimarisha umoja, mshik**ano na kudumisha mila na utamaduni ili kuchochea uzalendo na kuhamasisha shughuli za Utalii na Kuleta maendeleo ya wananchi wa Kizimkazi, Wilaya ya Kusini na Mkoa mzima wa Kusini.

Aidha, Rais Dk.Mwinyi amesema Uwepo wa Wanyamapori katika Tamasha la Kizimkazi utavutia wageni zaidi Zanzibar sambamba na dhamira ya Serikali ya kuongeza vivutio vya utalii nchini kupitia matamasha mbalimbali.

Rais Dk.Mwinyi ameyasema hayo wakati akifungua Tamasha la msimu wa nane la Kizimkazi uwanja wa Kashangae Paje, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini.

26/08/2023
MAENDELEO YOTE NCHINI NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM - COMRADE SOPHIA MJEMA"Maendeleo yote ni utekelezaji wa Ilani ya Ch...
15/06/2023

MAENDELEO YOTE NCHINI NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM - COMRADE SOPHIA MJEMA

"Maendeleo yote ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, ilani inatekelezwa na Serikali inayoongozwa na Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tusibabaishwe tuendelee kumpongeza na kuunga mkono juhudi zake katika kuwatumikia Watanzania na Taifa kwa ujumla."

Akizungumza kwenye Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM na Sekretarieti ya CCM, leo tarehe 15 Juni, 2023 Wilayani Mpwapwa Jijini Dodoma.


"Niendelee kuwaomba Wananchi kote nchini kuwa macho wakati wote na endapo kutatokea tetesi za mhisiwa au mtu mwenye dali...
02/06/2023

"Niendelee kuwaomba Wananchi kote nchini kuwa macho wakati wote na endapo kutatokea tetesi za mhisiwa au mtu mwenye dalili za ugonjwa wowote usio wa kawaida au unaotia mashaka ni vyema kutoa taarifa kwa viongozi wa Serikali katika ngazi uliopo mara moja.

Aidha, vifo vyovyote visivyo vya kawaida vinapotokea katika jamii tuvitolee taarifa mapema ili uchunguzi ufanyike na k**a kuna wagonjwa basi wafanyiwe uchunguzi na kupata tiba stahiki mapema.

Kwa upande wetu Serikali, tutaendelea kuweka mifumo madhubuti wa kufuatilia tetesi, kufanya uchunguzi na kugundua na pia kudhibiti kwa haraka, magonjwa haya ya milipuko na mengine yanayowasumbua wananchi wetu." - Waziri wa Afya alipokuwa akizungumza leo baada ya kusomwa Taarifa rasmi ya kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg.

"Hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2023 jumla ya watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Marburg walikuwa watu ni tisa (9), ka...
02/06/2023

"Hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2023 jumla ya watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Marburg walikuwa watu ni tisa (9), kati ya hao wagonjwa watatu (3) wamepona akiwemo daktari wa kituo cha Afya Maruku aliyewahudumia wagonjwa wa mwanzo. Aidha, wagonjwa sita (6) walipoteza maisha akiwemo mtaalamu wa maabara kutoka Kituo cha Afya Maruku na mtoto mwenye umri wa miezi 18 ambaye mama yake ni miongoni mwa wagonjwa waliopona.

Miongoni mwa waliofariki watu watano (5) walikuwa ndugu wa ukoo na mmoja alikuwa mtumishi wa kituo cha afya Maruku. Mgonjwa wa mwisho alibainika kuwa hana maambukizi (Negative) tarehe 19 Aprili 2023" - Mganga Mkuu wa Serikali Prof Tumaini Nagu alipokuwa akiwasilisha taarifa ya kitaalam ya kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg kwenye Kilele cha Mapambano dhidi ya ugonjwa huo nchini Tanzania.

“Kwa mujibu wa miongozo ya Shirika la Afya la Duniani (WHO), tangu tulipomruhusu mgonjwa wa mwisho, tulipaswa kuendelea ...
02/06/2023

“Kwa mujibu wa miongozo ya Shirika la Afya la Duniani (WHO), tangu tulipomruhusu mgonjwa wa mwisho, tulipaswa kuendelea kuchukua hatua za udhibiti ikiwemo ufuatiliaji wa tetesi katika jamii na kuchunguza wahisiwa wote kwa siku 42 tangu mgonjwa wa mwisho alipopona Virusi vya Marburg.

Kwa hesabu hizo, ilipofika juzi tarehe 31 Mei 2023, tulifikisha siku 42 tangu mgonjwa wa mwisho kupona Virusi vya Marburg, na hivyo kukidhi vigezo vya WHO vya kutangaza mwisho wa mlipuko wa ugonjwa wa Marburg. Kwa muktadha huu, leo tarehe 02 Juni 2023 ninatamka kuwa, mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi” - Mganga Mkuu wa Serikali Prof Tumaini Nagu akiwasilisha Taarifa ya kitaalam ya kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg kwenye Kilele cha Mapambano dhidi ya ugonjwa huo nchini Tanzania.

Kikundi cha ngoma Chipukizi kutoka Ipogolo kikitumbuiza katika uwanja wa Mwenyetogwa wakati wakisubiri Mgeni Rasimi Kati...
01/06/2023

Kikundi cha ngoma Chipukizi kutoka Ipogolo kikitumbuiza katika uwanja wa Mwenyetogwa wakati wakisubiri Mgeni Rasimi Katibu Mkuu wa chama cha Mapinduzi Daniel Chongolo kuhutubia mkutano wa hadhara.

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA imehatadharisha juu ya kuanza kwa msimu wa kipupwe utakaoambatana na baridi Kali kati...
27/05/2023

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA imehatadharisha juu ya kuanza kwa msimu wa kipupwe utakaoambatana na baridi Kali katika baadhi ya mikoa nchini.

Akitangaza mwelekeo wa msimu wa kipupwe unaoanzia mwezi June, Julai hadi Agosti Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA DKt Ladislaus Chang'a amesema msimu huo utakaoambatana na upepo mkali katika baadhi ya maeneo baridi lake linaweza kuongezeka zaidi.

Dk Chang'a ameitaja mikoa itakayoathirika zaidi na msimu huu ni Njombe, Iringa, Mbeya Kusini mwa Mkoa wa Morogoro na Rukwa.

Katika Mwaka wa Fedha 2023/24, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shil...
19/05/2023

Katika Mwaka wa Fedha 2023/24, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 212,457,625,000 kwa mchanganuo ufuatao:-

i) Kiasi cha Shilingi 30,503,685,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambapo Shilingi 18,522,155,000 ni za Mishahara na Shilingi 11,981,530,000 ni za Matumizi Mengineyo

ii) Kiasi cha Shilingi 181,953,940,000 kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambapo Shilingi 146,777,440,000 ni Fedha za Ndani na Shilingi 35,176,500,000 ni Fedha za Nje.

Address

Mikocheni
Dar Es Salaam
CLOUDSFM

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Infotznews posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Infotznews:

Share