Clouds TV

Clouds TV Kituo namba moja cha burudani kwa vijana kikisogeza kila taarifa ya entertainment mbele yako na kuhakikisha hupitwi na yanayojiri ndani na nje ya nchi.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Makunduchi kupitia tiketi ya CCM Wanu hafidhi Ameir amemhakikishia mgombea Urais wa Tanzania ...
17/09/2025

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Makunduchi kupitia tiketi ya CCM Wanu hafidhi Ameir amemhakikishia mgombea Urais wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan Kura nyingi za kishindo kutoka jimbo la Makunduchi kutokana na kazi kubwa ya kusogeza maendeleo kwenye Jimbo hilo iliyofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Akizungumza kwenye Mkutano mkubwa wa Kampeni uliofanyika kwenye Viwanja vya Skuli ya Kajengwa Wanu amemhakikishia Dkt Samia manage ni Mwenyekiti wa CCM Taifa kura nyingi kutoka Makunduchi pamoja na Kura za nyingi kwa mgombea Urais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi.


🇹🇿

17/09/2025

"Uislamu una sehemu mbili za amri zake"- Sheikh Shaaban Shunda


Hii hapa TAFU INAYOTUZUNGUKA, package unayohitaji kuifahamu kutoka timu ya taifa   ! Karibu tuijue vyema kuanzia 12:30 a...
17/09/2025

Hii hapa TAFU INAYOTUZUNGUKA, package unayohitaji kuifahamu kutoka timu ya taifa !

Karibu tuijue vyema kuanzia 12:30 asubuhi live on tv !

Usikoseee

17/09/2025

Sheikh Shaaban Shunda kutoka Jumuiya Ya Waislamu Wa Ahmadiyya akieleza kuhusu haki.


17/09/2025

Kila mwaka Jumuiya ya Ahmadiyya hufanya Mkutano Mkuu wa mwaka (Jalsa Salana) unaotoa fursa maalum ya kuwaelimisha waumini wake na jamii kwa ujumla juu ya maana ya kweli ya kumuabudu Mwenyezi Mungu na kutoa huduma kwa viumbe wake kwa kujenga amani na mahusiano mema baina ya makundi mbalimbali ya kiimani na kijamii pamoja na kuwa watiifu kwa sheria za nchi. Viongozi wa Dini, Serikali na Jamii kwa ujumla hupata nafasi ya kuhudhuria na kuwahutubia washiriki.

Jalsa Salana ya mwaka huu ni Mkutano wa 54 utakaofanyika kuanzia Ijumaa, tarehe 26 hadi Jumapili tarehe 28 Septemba 2025 katika eneo la Ahmadiyya Kitonga, Kata ya Msongola, Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na washiriki wapatao elfu tano (5000) kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani wenye kauli mbiu ya “UISLAMU NA HAKI ZA BINADAMU” na Mgeni Rasmi akitarajiwa Mhe. Abdallah Ulega.

Naungana na:-

1. Naib Amir - Sheikh Abdulrahman Ame
2. Sheikh Shaaban Shunda

Wakitueleza zaidi kwenye

17/09/2025

Sheikh Shaaban Shunda akielezea jinsi watu wote wanavyoweza kujiunga na JUMUIYA YA WAISLAMU WA AHMADIYYA.


Tabia ipi hiyo?
17/09/2025

Tabia ipi hiyo?




17/09/2025

Akiwa kwenye Kijiji cha Kajengwa, Makunduchi Unguja Visiwani Zanzibar, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan amewatoa wasiwasi Watanzania akiwahakikishia kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kikamilifu katika kuilinda Tanzania na kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na salama.

Dkt. Samia akirejea ahadi yake wakati anajitambulisha kwa Watanzania mara baada ya Chama chake kumpa ridhaa ya kuwania nafasi ya Urais, akiwa mwanamke wa kwanza kupewa nafasi hiyo katika Historia ya Chama hicho, amesema amelazimika kuyasema hayo mara baada ya Wazee wa Pemba kumuomba kusimamia amani na utulivu katika uchaguzi huo Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

“Tunakwenda kwenye uchaguzi Mkuu, ninaowaomba sana twende tudumishe amani na utulivu. Uchaguzi si vita, uchaguzi ni tendo la kidemokrasia ni watu kwenda kwenye utaratibu uliowekwa, kuweka kura zetu, rudi nyumbani katulie ili nchi ibaki salama. Si muda wote kushika silaha kunaleta suluhu ya maana, niwaombe sana ndugu zangu amani na utulivu wa nchi yetu ni jambo muhimu kuliko jambo lolote. Hutaki kishindo kapige kura rudi nyumbani tulia.” Amesema Dkt. Samia.

Dkt. Samia yupo Visiwani Zanzibar kwenye ziara zake za Kampeni, ambapo awali pia amesisitiza kuwa ikiwa Watanzania watampa ridhaa ya kuongoza serikali atahakikisha pia analinda kwa bidii zake zote tunu za Taifa ambazo ni amani, umoja na mshik**ano k**a sehemu ya kuenzi jitihada zilizofanywa na waasisi wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Amani Abeid Karume.

17/09/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema ikiwa atachaguliwa na Watanzania katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, ameahidi kuendelea kulinda amani, uhuru, umoja na utulivu nchini k**a sehemu muhimu za kulinda na kuenzi kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Sheikh Amani Abeid Karume.

Dkt. Samia ameyaeleza hayo leo Jumatano Septemba 17, 2025, siku ya kwanza ya kampeni zake Visiwani Zanzibar kwenye Kijiji cha Kajengwa, Makunduchi, akiahidi pia kuulinda muungano na mafungamano yaliyopo Kati ya Tanzania bara na Tanzania Zanzibar.

“Naweza kusema Muungano wetu sasa umekuwa Muungano wa udugu wa damu zaidi kuliko vigezo vingine vyote. Pamoja na Muungano wetu tumeweza pia kulinda Uhuru na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na hali kadhalika kudumisha umoja, amani na utulivu nchini. Hizi ndizo tunu kuu na za msingi kwa maendeleo ya nchi yetu na hizi niwaambie tutazilinda kwa bidii zetu zote.” Amesisitiza Dkt. Samia.

Dkt. Samia amesema tunu hizo muhimu za Taifa zimeijengea Tanzania utambulisho wa pekee Kikanda na Kimataifa pamoja na kukuza mahusiano ya Kidiplomasia duniani, suala ambalo limeifanya Tanzania kuwa Mbia muhimu na wa kutegemewa Kikanda na Kimataifa pamoja na kufungua milango ya ushirikiano na fursa zaidi kwa watanzania Kimataifa

Aidha katika hatua nyingine ya kuonesha uthabiti katika kusimamia tunu hizo, Dkt. Samia ambaye ni mwanamke wa kwanza kupitishwa katika Historia ya CCM kuwania nafasi hiyo, ameahidi kuanzisha Kituo cha kumbukumbu na nyaraka za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, k**a sehemu ya kuhifadhi urithi wa Muungano na kujenga uelewa wa pamoja kwa watu kujifunza zaidi kuhusu Muungano na sababu za uwepo wake.

Mamia ya wananchi wa Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja Visiwani Zanzibar wakiwa kwenye shamra shamra za kumpokea Mgombea...
17/09/2025

Mamia ya wananchi wa Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja Visiwani Zanzibar wakiwa kwenye shamra shamra za kumpokea Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Kampeni za Uchaguzi za Chama hicho leo Jumatano tarehe 17 Septemba, 2025.

Mgombea Urais wangu Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na Mgombea Ubunge wa jimbo la Makunduchi Mh Wanu Hafidh Ameir wanat...
17/09/2025

Mgombea Urais wangu Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na Mgombea Ubunge wa jimbo la Makunduchi Mh Wanu Hafidh Ameir wanatarajia kufanya Mkutano mkubwa wa Kampeni katika Jimbo hilo kuomba ridhaa ya Wananchi kuelekea Uchaguzi mkuu wa October 29.

Dkt Samia ameanza Mikutano ya Kampeni Visiwani Zanzibar leo baada ya kumaliza kufanya Mikutano ya aina hiyo kwenye mikoa 10 ya Tanzania bara.


🇹🇿

Address

Https://www. Facebook. Com/images/places/map/red-pin. Png
Dar Es Salaam
00255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

+255222781445

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Clouds TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Clouds TV:

Share