Clouds TV

Clouds TV Kituo namba moja cha burudani kwa vijana kikisogeza kila taarifa ya entertainment mbele yako na kuhakikisha hupitwi na yanayojiri ndani na nje ya nchi.
(4)

  |  .Latifa Mohamed (A girl from Geita 🇹🇿)   tunakutakia mafanikio na baraka maishani mwako
15/06/2026

| .
Latifa Mohamed (A girl from Geita 🇹🇿) tunakutakia mafanikio na baraka maishani mwako

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ameeleza mkakati wa miaka mitatu utakaoongozwa na Rais wa Jamhuri y...
15/06/2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ameeleza mkakati wa miaka mitatu utakaoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika nafasi yake ya Bingwa wa Umoja wa Afrika wa Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto, unaolenga kusaidia nchi za Afrika kupunguza na hatimaye kutokomeza vifo vya akina mama wajawazito vinavyoweza kuzuilika.

Dkt. Shekalaghe amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa Kikao cha Kamati ya Kitaalam (TWG 5) ya Masuala ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Idara ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Ahmad Mohammed Makuwani, mafanikio ambayo Tanzania imeyapata katika kuboresha afya ya uzazi, mama na mtoto ndiyo msingi unaoiwezesha nchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kikanda za kuboresha afya ya uzazi barani Afrika.

Dkt. Makuwani amesema kuwa tangu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aanze kuongoza nchi, Serikali imeendelea kuwekeza katika afua za afya ya uzazi, mama na mtoto kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa katika Mpango Mkakati wa RMNCAH One Plan III (2021/22–2025/26). Amesema mafanikio hayo yameifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazotajwa k**a mfano wa kuigwa katika utekelezaji wa afua zinazolenga kupunguza vifo vya uzazi vinavyoweza kuzuilika.

Akifafanua mkakati huo, Dkt. Shekalaghe amesema Tanzania imeandaa andiko la dhana litakalotumika k**a mwongozo wa kushirikisha mataifa mengine ya Afrika kujifunza kutokana na mafanikio ambayo Tanzania imeyapata licha ya kuwa na rasilimali chache.

"Baada ya kufanya tathmini ya mazingira ya kila nchi, tutaandaa viashiria muhimu vya kufuatilia maendeleo pamoja na afua mahsusi zitakazotekelezwa. Mfumo wa ufuatiliaji na tathmini utawekwa ili kuhakikisha hatua zinazochukuliwa zinaleta matokeo yaliyokusudiwa," alieleza Dkt. Shekalaghe.

15/06/2026

Askofu Sylvester Gamanywa, Kiongozi Mwandamizi Mstaafu wa Baraza la Kipentekoste Tanzania (CPCT), amerejea nchini baada ya kuiwakilisha Tanzania katika Jerusalem Summit 2026 iliyofanyika Yerusalemu, Israel, mkutano mkubwa wa kimataifa uliowakutanisha viongozi waandamizi wa kiinjili, wataalamu wa maendeleo ya jamii, wanazuoni wa masuala ya kizazi na wadau mbalimbali kutoka mabara tofauti duniani.
nafasi ya kujifunza zaidi kuhusu changamoto na fursa zinazoikabili dunia katika kipindi hiki cha mabadiliko makubwa ya kijamii, kiteknolojia na kitamaduni.

Miongoni mwa ajenda kuu zilizotawala Jerusalem Summit 2026 ilikuwa ni mjadala mpana kuhusu pengo linalozidi kuongezeka kati ya kizazi cha Boomers na kizazi cha Gen Z katika karne ya ishirini na moja.

Akizungumza baada ya kurejea nchini, Askofu Gamanywa amesema kwamba ujumbe mkubwa alioubeba kutoka Yerusalemu ni wajibu wa kizazi cha sasa kuwekeza kwa makusudi katika kizazi cha Gen Z kwa kukirithisha Imani Takatifu ya Biblia na Nguvu za Roho Mtakatifu.

Amesema changamoto kubwa inayokikabili kizazi cha Gen Z leo si ukosefu wa elimu, teknolojia au fursa za kiuchumi pekee, bali ni mkengeuko mkubwa wa kimaadili unaoendelea kuongezeka duniani.

Kwa sababu hiyo, ametoa wito kwa viongozi wa dini, wazazi, taasisi za elimu, vyombo vya habari na Serikali kushirikiana katika kujenga kizazi kipya chenye maadili, uwajibikaji, uzalendo na hofu ya Mungu.

"Hata k**a mtu ana maambukizi hatumuwekei damu yenye maambukizi. Tunamuwekea damu Salama. Na damu Salama ni damu ambayo ...
15/06/2026

"Hata k**a mtu ana maambukizi hatumuwekei damu yenye maambukizi. Tunamuwekea damu Salama. Na damu Salama ni damu ambayo ni safi ambayo imeshafanyiwa uchunguzi tunaitawanya kwenye mahospitali"- Evelyn Dielly, Afisa Uhamasishaji kutoka Damu Salama Kanda ya Mashariki.


"Kauli mbiu yetu ya mwaka inasema tone la Ubinadamu, changia damu, Okoa maisha. Kila tone unalolicangia damu kuna mtu li...
15/06/2026

"Kauli mbiu yetu ya mwaka inasema tone la Ubinadamu, changia damu, Okoa maisha. Kila tone unalolicangia damu kuna mtu linampa tumaini la kuendelea kuishi. Wito wetu kwa Watanzania mtu asijione kwamba ni mwembamba hawezi kuchangia damu. Anayechangia damu ni mtu mwenye kilo kuanzia 50. Tone lako Moja la damu litamsaidia mtoto mwenye Sikoseli asiweze kupoteza maisha"- Evelyn Dielly, Afisa Uhamasishaji kutoka Damu Salama Kanda ya Mashariki.



15/06/2026



Kila asubuhi ya GOAT ilikuwa ni juu ya fikra ya namna atakavyoweza kuibua fursa mpya kupitia vipaji mbalimbali ikiwemo t...
14/06/2026

Kila asubuhi ya GOAT ilikuwa ni juu ya fikra ya namna atakavyoweza kuibua fursa mpya kupitia vipaji mbalimbali ikiwemo teknolojia, kilimo, masoko mtandaoni, muziki, urembo na hata kuwezesha talanta kwa wana huku akiwapiga taafu walio kwenye tasnia ya ufundi.

Lengo la kunyoosha k**a ulivyo mchongo pesa ni kuhakikisha kila Mcloudsania anapitiwa na fursa za Goat k**a ilivyo kwa serikali inafanya serikali ambapo imetangaza makadirio ya bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026.27 kuwa ni trilioni 62.33.

Ili kujua k**a kila mtu amefikiwa na ugali huo wa taifa Nura Ramadhan na Mahija Zayumba watakuja kukujuza namna mgao wa bajeti huo ulivyo kupitia Habari Clouds weekend ya Clouds TV ifikapo saa moja kamili 1:00 usiku.



..!!

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu na kuimarisha ushirikiano na taas...
14/06/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu na kuimarisha ushirikiano na taasisi za dini kwa kutambua mchango mkubwa unaotolewa na taasisi hizo katika kujenga maadili, amani, mshik**ano na maendeleo ya Taifa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, aliposhiriki Ibada katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Kiomboi Christian Centre, mjini Kiomboi, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Ibada hiyo iliongozwa na Askofu wa Jimbo la Singida Kaskazini, Dkt. Danford Obadia pamoja na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Yona Suleman Essya.

Akizungumza na waumini hao, Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua nafasi muhimu ya taasisi za dini katika malezi ya jamii na kwamba itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowezesha taasisi hizo kutekeleza majukumu yake kwa uhuru na ufanisi.

“Sisi wote tutaendelea kulinda mazingira bora ya kuendesha ibada. Serikali itaendelea kutambua na kuamini kazi inayofanywa na taasisi za dini katika kujenga Taifa letu,” amesema Dkt. Mwigulu.

Amesema taasisi za dini zimekuwa mshirika muhimu wa Serikali katika kujenga maadili mema, kuhimiza uwajibikaji, kuimarisha mshik**ano wa kijamii na kupambana na vitendo vinavyokinzana na utu na maendeleo ya wananchi.

Waziri Mkuu amesema Kanisa la TAG limekuwa na mchango mkubwa katika kuelimisha jamii, kuondoa imani potofu na kuhamasisha wananchi kuzingatia maadili na misingi sahihi ya maisha.

“TAG haikusimama kwenye ibada pekee, bali imebadilisha hata maisha ya kila siku ya wananchi. Imechangia kuondoa baadhi ya mila na imani zilizokuwa zinarudisha nyuma maendeleo ya watu wetu,” amesema.

Wakati huo huo, Dkt. Mwigulu ametoa rai kwa wananchi kuendelea kuheshimu nyumba za ibada na kuepuka kuziingiza katika shughuli zinazoweza kuvuruga dhamira na malengo yake ya msingi.

TAJI LA UBINGWA MIGUUNITaji la Ubingwa lipo miguuni katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026 ambalo linaweka historia mpya ...
13/06/2026

TAJI LA UBINGWA MIGUUNI

Taji la Ubingwa lipo miguuni katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026 ambalo linaweka historia mpya kwa kuwa mashindano makubwa zaidi kuwahi kufanyika, yakishirikisha mataifa 48 badala ya 32.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya soka tangu kuanzishwa kwa Kombe la Dunia, mashindano haya yanasimamiwa na nchi tatu ambayo yameandaliwa na Marekani, Canada, na Mexico yameshuhudia ongezeko la mechi hadi kufikia 104 zitakazochezwa katika viwanja 16 tofauti.

MWAJABU SHAFII na NURA MOHAMED wanakuletea Simulizi kwamba “taji la bingwa miguuni” si kombe tu, bali ni ndoto inayopiganiwa na kila taifa, ikibeba heshima, historia na fahari ya kuwa bora zaidi duniani katika mchezo wa soka.

🕐 Saa 1:00 jioni, kupitia
Jiunge na mjadala unaogusa historia, uhalisia wa dunia ya sasa, na mustakabali wa amani duniani.


13/06/2026

“Nimekuja leo kwa kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambua ubia huu muhimu ambao shule yenu imekuwa ikifanya katika sekta ya elimu. Hatuwezi kuyataja mafanikio katika sekta ya elimu bila kutaja mchango wa shule za sekta binafsi” - Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

Amesema hayo katika Mahafali ya 11 ya wahitimu wa Kidato cha Nne (Year 11–IGCSE) wa mwaka wa masomo 2025/2026 ya Shule ya Kimataifa ya Feza

Address

Https://www. Facebook. Com/images/places/map/red-pin. Png
Dar Es Salaam
00255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

+255222781445

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Clouds TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Clouds TV:

Share