22/10/2025
Mzee mmoja alichinja ng’ombe mkubwa, akawasha jiko lake la kuchomea nyama kisha akamuambia binti yake.
“Nenda uwataarifu ndugu,jamaa,marafiki na jirani zetu waje tufanye sherehe.
Lakini badala ya kutoka mualiko, binti alikimbilia barabarani na kupaza sauti.
“Tunaomba msaada, nyumba yetu inateketea kwa moto”
Baada ya muda mfupi, ni watu wachache walijitokeza huku wengine walijifanya hawakusikia chochote.
Wale wachache waliofika walikula na kunywa mpaka usiku wa Manane.
Baba akamuuliza binti yake, wako wapi ndugu jamaa marafiki na jirani zetu wengine??
Bint akamuangalia baba yake na kumuambia;
“Waliokuja wamekuja kutuokoa kwasababu (nilienda kupiga kelele kuwa nyumba yetu inateketea kwa moto) na hao ndio waliojitokeza sio kwasababu ya sherehe”
Funzo:
K**a hawajitokezi wakati wa shida zako,basi hawastahili kuwepo wakati wa furaha yako