Kanyamala Media

Kanyamala Media HABARI | MATUKIO | LIFE STYLE | FASHION | HAPA TANZANIA NA NJE YA TANZANIA
(2)

Katika kumbukumbu za karne ya 20 barani Afrika, jina la Mobutu Sese Seko linasimama k**a kielelezo cha ukamilifu wa udik...
08/06/2026

Katika kumbukumbu za karne ya 20 barani Afrika, jina la Mobutu Sese Seko linasimama k**a kielelezo cha ukamilifu wa udikteta, ufahari uliopitiliza, na ukatili wa kisiasa.

Akiongoza nchi ya Zaire (sasa Congo DRC) kwa miaka 32, Mobutu alijenga taswira ya mtu asiyeguswa kabisa. Hata hivyo, nyuma ya kofia yake yenye ngozi ya chui na fimbo ya mamlaka, ukweli wa kihistoria unaonyesha kuwa utawala wake ulikuwa ni zao la miradi ya siri ya Shirika la Intelijensia la Marekani (CIA).

Uhusiano wao haukuwa tu wa kishirika; ulikuwa ni ushirika wa kimkakati ulioghalimu mamilioni ya dola ili kulinda maslahi ya Magharibi kipindi cha Vita vya Baridi (Cold War).

Uhusiano wa Joseph-Désiré Mobutu na CIA ulianza mwanzoni mwamiaka ya 1950, lakini ulikomaa mara dufu baada ya Congo kupata uhuru mwaka 1960. Uchaguzi wa kidemokrasia ulimuweka madarakani kijana mzalendo, Patrice Lumumba, k**a Waziri Mkuu. Lumumba alitaka nchi hiyo itumie rasilimali zake yenyewe msimamo uliotishia maslahi ya makampuni mengi ya madini ya Magharibi kwa hofu ya kuenea sera ya Ukomunisti, Marekani iliamini Patrice Lumumba angekuwa karibu na Umoja wa Kisovieti (Urusi).

Mkurugenzi wa kituo cha CIA mjini Kinshasa wakati huo, Mr. Lawrence Devlin, alimtambua Mobutu (aliyekuwa Mkuu wa Majeshi) k**a mtu sahihi wa kufanya naye kazi. Kwa msaada wa kifedha na ushauri kutoka CIA, Mobutu aliongoza mapinduzi mnamo Septemba 1960, akamwondoa Patrice Lumumba madarakani na baadaye kumkabidhi kwa maadui zake waliomuua kinyama Januari 1961. Kifo cha Patrice Lumumba kilisafisha njia kwa Mobutu kuelekea ikulu.

🗣 Mnamo Novemba 1965, Mobutu alichukua madaraka kamili ya nchi kupitia mapinduzi ya pili. Wakati huu, Shirika la kijasusi CIA haikuficha furaha yake. Ndani ya muda mfupi, Washington ilihakikisha serikali ya Mobutu inapata uhalali wa kimataifa na msaada mkubwa wa kijeshi.

Kwa Marekani, Mobutu alikuwa ni Ngome madhubuti dhidi ya Ukomunisti katika Ukanda wa Maziwa Makuu. Mamilioni ya dola taslimu yalipitishwa kupitia Shirika la CIA kwenda kwa Mobutu ili kununua uaminifu wa majenerali wa jeshi, kunyamazisha wapinzani wa kisiasa na kuimarisha vyombo vya usalama vilivyokandamiza wananchi.

🗣 Ushirikiano wa Mobutu na CIA ulivuka mipaka ya Kongo. Mobutu aligeuka kuwa mratibu mkuu wa operesheni za siri za Marekani barani Afrika k**a:

Vita vya Angola (1975): CIA ilimtumia Mobutu na ardhi ya Zaire kupitisha tani za silaha na mabilioni ya dola kwenda kwa vikundi vya waasi vya FNLA na UNITA (Jonas Savimbi) ili kupambana na serikali ya Angola iliyokuwa inasaidiwa na nchi za Urusi na Cuba.

Pia Jiji la Kinshasa likawa kituo kikuu cha ujasusi cha CIA. Mobutu alikuwa akipokea taarifa za intelijensia kutoka satelaiti za Marekani na yeye kuwapa siri za kijiografia za ukanda huo.

🗣 Wakati miundombinu ya Zaire ikizidi kuwa mibovu, shule zikikosa vitabu na mahospitali yakikosa dawa muhimu, Mobutu alijenga utawala wa Kleptocracy (utawala wa wezi). Mobutu alifanikiwa kuwa na utajiri unaokadiriwa kufikia kati ya Dola Bilioni 4 hadi Bilioni 5, Kiwango kilicholingana na deni la nchi yake kwa wakati huo. Alimiliki majumba ya kifahari huko Paris, Brussels na Uswisi na alikuwa anakodisha ndege ya kifahari ya Concorde kwenda kufanya manunuzi ya nguo Paris.

Mataifa ya Magharibi, IMF na Benki ya Dunia walikuwa wakifahamu vyema wizi huu wa Mobutu. Lakini kwa sababu Mobutu alikuwa "kibaraka mwaminifu," walifumba macho na kuendelea kumwongezea mikopo zaidi na zaidi.

🗣 Kosa kubwa la kimkakati alilofanya Mobutu lilikuwa kuamini kwamba uaminifu wake kwa CIA ungempa bima ya maisha ya kisiasa. Alisahau kuwa katika diplomasia ya kimataifa, Hakuna rafiki wa kudumu.

Mnamo mwaka 1989, Rasmi Vita vya Baridi vikaisha na Ghafla, Tishio la Ukomunisti likatoweka duniani na thamani ya Mobutu mbele ya macho ya Shirika la CIA ikapotea. Washington Dc ilianza kumgeuka na kumwona k**a mzigo, dikteta mlafi na nembo ya ukiukaji wa haki za binadamu.

Mwaka 1996, wakati waasi wa AFDL wakiongozwa na Laurent-Désiré Kabila (wakisaidiwa na Rwanda na Uganda) walipoanzisha vita kutoka Mashariki, Mobutu alijitahidi sana kutafuta msaada wa CIA Washington, Simu zake hazikujibiwa kabisa. Hakukuwa na silaha wala fedha zilizotumwa kumwokoa ukafuata mwisho wa madaraka yake ndani ya Congo.

Mnamo Mei 1997, huku waasi wakiwa milango ya Kinshasa, Mzee Mobutu akiwa kadhoofika sana kwa ugonjwa wa saratani aliamua alitoroka nchi na Alifariki huko nchini Morocco (Septemba 7, 1997), na kuzikwa katika makaburi madogo huko Rabat, mbali kabisa na ardhi aliyoitawala kwa dharau nyingi.

Hii ni barua yake ya kujiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi 1977.Mzee huyu tofauti na tulivyozoea mawaziri ama vion...
08/06/2026

Hii ni barua yake ya kujiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi 1977.

Mzee huyu tofauti na tulivyozoea mawaziri ama viongozi waandamizi wanapojiuzulu inakuwa ni lazima walalame kwa hili na lile,lakini kwake ilikuwa ni tofauti sana.

Ahsante mzee ruksa kwa kuweka standard katika hili.

Mapinduzi dhidi ya Waziri Mkuu wa kwanza wa Congo huru, Patrice Lumumba, mwaka 1960, yamebaki kuwa moja ya sura za giza ...
08/06/2026

Mapinduzi dhidi ya Waziri Mkuu wa kwanza wa Congo huru, Patrice Lumumba, mwaka 1960, yamebaki kuwa moja ya sura za giza katika historia ya Afrika. Ingawa Lumumba alikuwa kiongozi aliyechaguliwa kidemokrasia, Umoja wa Mataifa (UN) uliamua kumtambua Rais Joseph Kasavubu baada ya kumvua madaraka Lumumba kwa njia yenye utata mkubwa wa kikatiba. Katiba ya Congo haikutoa uwezo wa rais kumng’oa waziri mkuu bila uungwaji mkono wa bunge, jambo ambalo wataalamu wa sheria walilipinga wazi. Kutambuliwa kwa hatua hiyo na UN kulivunja uhalali wa serikali ya Lumumba na kuweka msingi wa mgogoro mkubwa wa uongozi ulioingiza Congo katika machafuko ya muda mrefu.

Katika kipindi hicho, vita baridi kati ya Marekani na Umoja wa Kisovieti vilikuwa vimefika kileleni. Lumumba, alipozuiwa na Ubelgiji na mataifa ya Magharibi kurejesha utulivu katika mikoa iliyojitenga ya Katanga na Kasai, alilazimika kuomba msaada wa kijeshi kutoka Moscow. Hatua hiyo ilitafsiriwa na mataifa ya Magharibi k**a tishio kwa maslahi yao ya kisiasa na kiuchumi, hasa kutokana na utajiri wa madini ya Congo. Kwa shinikizo la Marekani, Uingereza na Ubelgiji, UN ilichagua kumgeuka Lumumba na kumuacha bila ulinzi wala mamlaka ya utekelezaji.

Katibu Mkuu wa UN, Dag Hammarskjöld, alikataa kutumia vikosi vya UN kusaidia kurejesha mamlaka ya serikali halali ya Lumumba. Badala yake, UN ilimpa nafasi Kasavubu na jeshi la Mobutu kuhodhi mamlaka, hatua iliyohalalisha mapinduzi ya ndani dhidi ya Lumumba. Hatimaye Lumumba alik**atwa, akateswa, na Januari 1961 akauliwa kikatili katika tukio lililoshtua dunia nzima.

Kwa kuunga mkono kundi lililompindua, UN iliifanya Congo kuingia kwenye miongo kadhaa ya machafuko, vita vya wenyewe kwa wenyewe, uasi wa majimbo na utawala wa mabavu wa Mobutu. Congo haikupoteza tu kiongozi aliyekuwa na dira ya kitaifa, bali pia fursa ya kujenga umoja na uthabiti wa taifa changa.

Urithi wa Lumumba leo unakumbukwa k**a ishara ya mapambano dhidi ya ukoloni, usaliti wa kimataifa, na gharama kubwa ya maslahi ya kibeberu kwa bara la Afrika.

Katika simulizi hii ya kusisimua, tunaona upande wa pili wa msimamo wa Bibi T**i Mohamed wakati wa sakata la kuvunjwa kw...
07/06/2026

Katika simulizi hii ya kusisimua, tunaona upande wa pili wa msimamo wa Bibi T**i Mohamed wakati wa sakata la kuvunjwa kwa jumuiya ya East African Muslim Welfare Society (EAMWS). Bibi T**i alisimama kidete kutetea mchango wa Aga Khan katika elimu na ustawi wa Waislamu kipindi cha ukoloni.

​Hapo ndipo lugha zilipopishana kwa mara ya kwanza kati ya makomredi hawa wawili wa harakati za uhuru, huku Bibi T**i akitamka maneno mazito:

"Mimi simuogopi yeyote isipokuwa Allah Subhana wa Ta'ala."

Baada ya kauli hiyo ya Bibi T**i Mohamed kilichofuata ni Kesi ya uhaini kwake Mwezi wa 10, 1969.

​Unajifunza nini hapa kuhusu ujasiri wa viongozi wetu wa zamani? Angusha comment yako hapo chini

​ **iMohamed

Taasisi ya Usalama wa Taifa ya Tanzania (TISS) ndicho chombo chenye jukumu kubwa zaidi la kulinda usalama wa nchi yetu, ...
07/06/2026

Taasisi ya Usalama wa Taifa ya Tanzania (TISS) ndicho chombo chenye jukumu kubwa zaidi la kulinda usalama wa nchi yetu, raia wake, na rasilimali zetu dhidi ya tishio lolote la ndani au nje. Hata hivyo, ukiacha sifa zao za kiutendaji, kuna mijadala mizito inayoendelea mitaani na kwenye mitandao ya kijamii: Je, TISS inafanya kazi kiufasaha unaotakiwa katika karne hii ya 21..???

Wachambuzi wa masuala ya usalama, sheria, na siasa wanataja changamoto kuu tano (5) zinazokwaza ufanisi wa chombo hiki muhimu:

🗣 Moja ya malalamiko makubwa ni mtazamo kwamba TISS imekuwa ikitumika zaidi kulinda maslahi ya kisiasa ya chama tawala badala ya maslahi mapana ya taifa. Badala ya nguvu kubwa kuelekezwa kwenye ujasusi wa kiuchumi au uhalifu wa kimtandao, mara nyingi inaonekana ikielekezwa kudhibiti wanasiasa wa upinzani na wakosoaji wa serikali. Hali hii inashusha uaminifu wa wananchi kwa chombo hiki.

🗣 Katika nchi nyingi zilizoendelea, idara za usalama zinakuwa na K**ati Maalumu za Bunge zinazozikagua kiutendaji na kibajeti. Hapa kwetu, kwa kisingizio cha "siri za nchi," hakuna chombo huru kinachojua kwa kina kinachoendelea ndani ya TISS. Hali hii inatoa mwanya kwa baadhi ya maofisa kutumia vibaya madaraka yao bila hofu ya kuhojiwa.

🗣 Mabadiliko ya sheria ya hivi karibuni yameongeza nguvu kwa TISS, ikiwemo uwezo wa kuk**ata watu. Baadhi ya Wanasheria wanahoji: Kuwapa maofisa wa siri nguvu za kikomandoo za kuk**ata watu bila uwazi, hakuingilii kazi za Jeshi la Polisi.?? Hii inatajwa kuongeza hofu ya ukiukwaji wa haki za binadamu miongoni mwaraia.

🗣 Vita vya sasa vipo kwenye teknolojia (Cybercrime), Ugaidi wa mitandaoni na Vita vya kiuchumi. Kuna hofu kuwa TISS bado inategemea mbinu za kizamani za "kuchunguza watu Mitaani" au kutumia mamluki badala ya kuwekeza kwenye mifumo mikubwa ya kisasa ya kijasusi ya kiteknolojia (Signals Intelligence na Data Analysis). K**a chombo hakiwezi kugundua mapema mikataba mibovu ya madini au utoroshaji wa rasilimali, kinakuwa kimefeli kulinda uchumi wa nchi.

🗣 Ili idara ya usalama iwe dume, inahitaji vichwa bora zaidi nchini kutoka kwa wataalamu wa IT, Wachumi, Madaktari hadi wanasheria nguli. Hata hivyo, kuna malalamiko ya chini kwa chini kuwa mfumo wa kuingia TISS wakati mwingine unagubikwa na kujuana au vigezo vya utii wa kisiasa badala ya uwezo mkubwa wa kiakili na weledi wa mtu.

Nini Kifanyike..???

Ili TISS ifanye kazi kiufasaha, ni lazima itenganishwe kabisa na siasa za vyama. Inapaswa kuwa taasisi huru inayolinda maslahi ya kila Mtanzania, iwekewe mifumo ya usimamizi bungeni na ijengewe uwezo mkubwa wa kiteknolojia ili kukabiliana na changamoto za sasa.

Nini maoni yako kuhusu utendaji wa Usalama wa Taifa wetu..?? Unafikiri wapi wanahitaji kuboresha zaidi..?? Dondosha maoni yako hapa chini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili nchini kupitia Julius Nyerere International Airpor...
06/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili nchini kupitia Julius Nyerere International Airport tarehe 06 Juni 2026, akihitimisha ziara yake ya kitaifa nchini Urusi.

Akiwasili, Rais Samia alisalimiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais Emmanuel John Nchimbi na Katibu Mkuu wa CCM Asha-Rose Migiro.

Ziara hiyo ilifanyika mjini St. Petersburg nchini Urusi, kufuatia mwaliko wa Rais wa Urusi Vladimir Putin, ambapo viongozi hao walijadili masuala ya ushirikiano wa kiuchumi na kidiplomasia.

Mnamo Septemba 15, 2007 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mwembe Yanga, Temeke, Dar es Salaam mnamo Septemba 18, Cha...
06/06/2026

Mnamo Septemba 15, 2007 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mwembe Yanga, Temeke, Dar es Salaam mnamo Septemba 18, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilisoma "Orodha ya Aibu" (List of Shame) iliyowataja viongozi na wafanyabiashara waliotuhumiwa kwa ufisadi mkubwa.

Orodha hiyo ililenga kupambana na ubadhirifu na kuamsha hisia za umma dhidi ya matumizi mabaya ya rasilimali za taifa.

Orodha hiyo iliongozwa na vigogo kadhaa waliotuhumiwa kuhusika na mikataba mibovu na kashfa za kifisadi, waliowajibika kwa nyakati tofauti:

1. Edward Lowassa (Waziri Mkuu): Alihusishwa na sakata la kampuni ya kufua umeme ya Richmond, hatua iliyomfanya ajiuzulu baadaye mnamo 2008.

2. Basil Mramba (Waziri wa Fedha): Alihusishwa na kashfa ya ukandarasi wa ukaguzi wa madini (Alex Stewart).

3. Daniel Yona (Waziri wa Nishati na Madini): Alihusishwa na mikataba ya madini na sakata la Alex Stewart.

5.Nazir Karamagi (Waziri wa Nishati na Madini): Alihusishwa na saini ya mkataba tata wa madini ya Buzwagi uliofanyika nje ya nchi.

6. Andrew Chenge (Mwanasheria Mkuu wa Serikali): Alihusishwa na kashfa ya rada na mikataba mbalimbali ya umma.

7. Rostam Azziz.
8. Ni**od Elirehema Mkono: Alikuwa ni Mbunge wa
Jimbo la Musoma Vijiji

Harakati hizo ziliongozwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa, ambaye aliwasilisha nyaraka hizo hadharani.

Kuna watu wamekuwa wananitaka nijadili ufisadi na usafi wa Edward Lowassa, katika muktadha wa orodha ya mafisadi 11 iliy...
06/06/2026

Kuna watu wamekuwa wananitaka nijadili ufisadi na usafi wa Edward Lowassa, katika muktadha wa orodha ya mafisadi 11 iliyotolewa na Chadema, Septemba 15, 2007, katika viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar es Salaam. Wanataka kujua kwanini, baada ya yote hayo, Chadema ile ile iliyojumuisha jina la Lowassa katika orodha hiyo, hatimaye ilimkaribisha na kumteua agombee urais mwaka 2015.

Kwa baadhi yao, nimekuwa natoa majibu mafupi. Kwanza, nawashauri wapitie upya orodha ya mafisadi, wasome na kujikumbusha tuhuma za Chadema kwa kila mtuhumiwa. Lowassa aliwekwa katika orodha hiyo kwa sababu alivunja mkataba wa kampuni ya City Water ya Dar es Salaam. Kampuni ilipeleka shauri mahak**ani kudai fidia.

Chadema ilimshutumu Lowassa kwa uamuzi huo ambao, kwa macho yetu wakati ule, ulikuwa wa kibabe, na ungesababishia taifa hasara iwapo serikali ingeshindwa mahak**ani. Lowassa ana bahati. Serikali ilishinda shauri hilo. Kwa mantiki hiyo, ufisadi aliotuhumiwa Mwembeyanga ulifutika wenyewe mahak**ani.

Lakini alikuwa na bahati mbaya, kwamba nguvu iliyokuwa imetumika kutangaza “ufisadi” huo mwaka 2007, haikutumika tena kutangaza “ushindi wake” mahak**ani. Akiwa ndani ya kikao kimojawapo cha Halmashauri Kuu ya CCM mwaka 2012, Lowassa alitumia ushindi wake huu kumkabili Rais Kikwete alipoleta hoja ya mafisadi mbele ya wajumbe.

Kwa mara ya kwanza, baada ya kukaa kimya kwa miaka minne, Lowassa alipata ujasiri wa kumweleza rais kuwa miongoni mwa waliotajwa kwa ufisadi katika orodha ile, na Kikwete alikuwemo, lakini alikuwa hajasafishwa na kikao chochote au mahak**a yoyote. Ni jambo la bahati mbaya kwamba wananchi wengi wanaojadili orodha ya mafisadi, wanakosea kudhani na kusema kwamba Chadema ilimtuhumu Lowassa kwa ufisadi wa Richmond. Hapana! Ufisadi wake wa Mwembeyanga ulitokana na yeye kuvunja mkataba wa City Water.

Hata sakata la Richmond lilipoibuka mwaka 2008, likamuumiza Lowassa kisiasa na kijamii, Rais Kikwete, kwa kuwa alijua ukweli halisi, alimfariji Lowassa kuwa ile ilikuwa “ajali ya kisiasa.” Baadhi yetu tulikuwa hatujajua vema undani wa sakata la Richmond. Nasi tuliingizwa katika mkumbo ambao nitaujadili baadaye kidogo. Hata leo, wapo watu wanaodhani kwamba Richmond ilikuwa mali ya Lowassa.

Mwaka 2009, niliporejea nyumbani kutoka masomoni Uingereza, miongoni mwa watu wa kwanza niliokutana nao ni Dk. Harrison Mwakyembe, mbunge wa Kyela, ambaye pia ndiye alikuwa ameongoza k**ati teule ya Bunge iliyochunguza sakata la Richmond. Katika ushirika wetu wa kupambana na ufisadi, Dk. Mwakyembe alikuwa rafiki yangu. Jioni moja, tukiwa nyumbani kwake Kunduchi, Dar es Salaam, tulizungumza mambo mengi ya kitaifa.

Dk. Mwakyembe aliniambia kuwa kilichomponza Lowassa katika Richmond si umiliki, bali akiwa waziri mkuu alishiriki katika kusimamia mchakato wa kampuni hiyo kupewa tenda. Aliniambia pia kwamba k**ati teule ilipoanza uchunguzi, katika siku za awali kabisa, iligundua kuwa rais alikuwa anahusika, lakini iliogopa kumhusisha au kumtaja rais kwa kuwa wajumbe walihofia “kuuawa.”

Aliongeza pia kuwa walikwepa kumhoji waziri mkuu Lowassa makusudi, kwani walitambua kuwa kwa cheo chake na utendaji wake, angeweza kuathiri matokeo ya kazi ya k**ati kabla haijawasilishwa bungeni. Lengo lao lilikuwa kumwadhibu waziri mkuu, kwa kuwa waliona “mkono” wake, hata k**a hakuwa mmiliki.

Jambo jingine aliloniambia ni kwamba siku chache kabla ya kwenda Bungeni, rais alimwomba Dk. Mwakyembe ampelekee nakala ya ripoti ya k**ati teule aipitie. Akasema kuwa baada ya rais kugundua kuwa jina lake halikuwa miongoni mwa watuhumiwa, alimwambia, “haya endelea.” Naye alishangaa kwamba rais alikuwa anajua, na alibariki kilichokuwa kinaendelea bungeni dhidi ya Lowassa.

Sababu kuu ya Dk. Mwakyembe na wenzake kumwadhibu waziri mkuu ni ugomvi wa madaraka bungeni kati ya Lowassa (waziri mkuu na kiongozi wa shughuli za serikali bungeni) na Samuel Sitta (spika). Nimewahi kueleza kuwa “ugomvi” wao ulisababishwa na ahadi ya Kikwete wakati anagombea urais. Aliahidi kumpa Sitta uwaziri mkuu. Vile vile, aliahidi kuwapa wengine, akiwemo Lowassa.

Baada ya uchaguzi, wakati anaanza kuunda serikali, huku Pius Msekwa akiwa ameshajiandaa kugombea uspika, Rais Kikwete alituma ujumbe wa kushtukiza kwa Sitta kumwomba agombee uspika! Maelezo ya Rais Kikwete kwa Sitta ni kwamba, kwa kuwa walikuwa wamefanikiwa kuk**ata serikali, lakini hawakuwa na uhakika na bunge, alihitajika mtu wanayemwamini, awasaidie kuk**ata bunge, ili mambo yao yaende sawa sawa.

Kikwete alimwaminisha Sitta kwamba hakukuwa na mtu mwingine aliyeaminiwa kuk**ata bunge. Kwa ujumbe huo pekee, Sitta alijua kuwa hakuwa tena chaguo la Kikwete katika uwaziri mkuu. Zilianza kampeni kali kumsaidia Sitta, wakisaidiwa mno na vyombo vya habari. Msekwa aliitwa “agano la kale.” Naye kwa kutojua, alimuuliza Rais Kikwete, “nasikia hunitaki?” Rais Kikwete alikanusha kuhusika na njama hizo.

Matokeo ya uchaguzi wa spika yalimpa ushindi Sitta. Lakini katika moyo na akili zake, hakuwahi kudhani kwamba Lowassa ndiye angeteuliwa kuwa waziri mkuu. Licha ya kwamba Sitta na Lowassa walikuwa kwenye kambi moja wakati wa kampeni, yeye na baadhi ya wenzake walikuwa wameanza kumzunguka Lowassa, kwa propaganda za mwaka 1995, kwamba “alikataliwa na Mwalimu Nyerere.”
Kwa hiyo, hata alipopokea barua ya uteuzi wa waziri mkuu kutoka Ikulu, Sitta alipatwa na mshtuko alipoona jina la Lowassa na kulisoma kwa wabunge ili wapige kura ya kumthibitisha.

Muda mfupi kabla ya hapo, mbunge mmoja mpya, aliyekuwa katika kambi ya Sitta, ambaye hakupenda Lowassa awe waziri mkuu, baada ya kupata tetesi kuwa Lowassa ndiye alikuwa chaguo la Kikwete, alikimbilia kwa Mzee Samwel Malecela kumwomba asaidie kuzuia uwaziri mkuu wa Lowassa.

Akamwambia Malecela: “Nasikia atamteua Lowassa. Wewe uliondolewa kwenye kinyang’anyiro cha urais kwa sababu walisema Nyerere alikukataa. Nyerere huyo huyo si alimkataa na Lowassa? Tunataka utusaidie kufanya kampeni ya kupiga kura ya hapana, iwapo Lowassa atateuliwa.”

Mzee Malecela alimtazama mbunge huyo, akatabasamu, halafu akamwambia: “Sikiliza. Namjua Lowassa. Alipoteuliwa kuwa waziri kwa mara ya kwanza, aliletwa ofisini kwangu, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, akawa waziri wa nchi. Mimi ndiye nilikuwa waziri mkuu. Najua utendaji wa Lowassa. Ni mtu ambaye akiamua kufanya jambo, hataki kulala mpaka jambo hilo litekelezwe. Ni mchapakazi.

“Yote yatasemwa juu yake, lakini natambua kuwa akiwa waziri mkuu, atachapa kazi bila kupumzika. Pili, wewe naona ni mbunge mpya. Hujui watu hawa. Wameshashinda, na wameshika serikali. Utawapinga, lakini hutafaulu kuwazuia. Na ukishashindwa, ujue kuwa ubunge wako utakuwa wa tabu, kwa sababu watakuandama. Waache. Hutaweza kuzuia Lowassa kuwa waziri mkuu.”

Mbunge huyo aliondoka akiwa ameinamisha kichwa. Mbunge huyo, akiwa swahiba wa Sitta, alikuwa miongoni mwa wabunge machachari waliokuwa wanasumbua serikali bungeni. Zaidi ya hayo, alishiriki hata kuandika upya kanuni za bunge ili kuwezesha bunge libane serikali.

Kwake, serikali ilikuwa Lowassa, si Kikwete. Na lilipozuka suala la Richmond, kampuni iliyoingizwa nchini na Sitta akiwa mkurugenzi mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania, mbunge huyo aliteuliwa kuwa mjumbe katika k**ati teule ya Bunge iliyochunguza sakata hilo.
Jambo ambalo halikujulikana mapema ni kwamba Dk. Mwakyembe naye alikuwa na kampuni ya kuzalisha umeme, ikishindana na Richmond. Kwa hiyo, hakustahili kuwa mwenyekiti wa k**ati teule, kwa kuwa na maslahi ya moja kwa moja. Ilikuwa lazima Lowassa “asulibiwe.” Kwao, ilikuwa zaidi ya Richmond.

Ilijulikana baadaye kwamba Lowassa hakujua kwamba Rais Kikwete alikuwa ameamua kujivua lawama katika sakata la Richmond. Mara baada ya Bunge kuahirishwa mchana, Lowassa alikwenda moja kwa moja kwa rais. Wakateta kuhusu suala hilo, na jinsi bunge lilivyochafuka.

Rais akamshauri Lowassa ajiuzulu bungeni, lakini kwa ahadi kwamba angekataa barua yake ya kujiuzulu – ilimradi ameshaonesha moyo wa uwajibikaji. Vyanzo vya kuaminika vinasema Lowassa aliomba karatasi pale pale, akaandika na kumpa karani aichape, baadaye akaisaini na kumkabidhi rais.

Mara tu alipoondoka Ikulu kuelekea Bungeni, ujumbe wa wabunge wa CCM ukaingia Ikulu wa rais na kumweleza kuwa kwa jinsi ilivyo, rais akimng’ang’ania Lowassa naye atanguka. Muda mfupi baadaye ukaja ujumbe kutoka idara ya usalama wa taifa, ukiwa na hoja hiyo hiyo, kwamba asipoondoka Lowassa wabunge wanaweza kupoteza imani na rais. Bahati mbaya, Lowassa alipokuwa amejiuzulu, Rais Kikwete hakumwite tena kumpa mrejesho wa taarifa mpya alizonazo.

Laiti Lowassa angejua kinachoendelea, angetumia fursa hiyo kujenga hoja na kujitetea bungeni. Alipokuwa kujua, alikuwa ameshachelewa. Ndivyo alivyopatikana Mizengo Pinda, na ndivyo Rais Kikwete alivyopata ujasiri wa kumpa pole Lowassa kwa kile alichoita “ajali ya kisiasa.”

Pamoja na hayo, Lowassa aliendelea kumfichia rais siri. Aliendelea kumwamini na kumlinda kwa kukaa kimya hata aliposhambuliwa. Alivunja ukimya mwaka 2012 ndani ya kikao cha NEC alipotaka rais aeleze wajumbe ukweli kuhusu Richmond. Upepo ulichafuka kwa muda, lakini baadaye kikao kiliendelea bila rais kutoa ufafanuzi.

Kwa Lowassa, huo ulikuwa ushindi mkubwa uliompatia ushujaa wa ghafla ndani ya NEC. Waliokuwa hawajui wakapata fursa ya kujua kwamba katika sakata la Richmond, yeye alipotea ili wengine wanusurike.

Hadi sasa sakata la Richmond limebaki kuwa la kisiasa. Serikali ya awamu ya tano imeanzisha mahak**a ya mafisadi, lakini hakuna anayetaka Richmond ifikishwe mahak**ani. Kwanini? Wanaogopa kusiibuke mambo mazito ambayo yalifichwa kwa miaka mingi.

Samuel Sitta alipofariki dunia mwaka 2016, niliandika tanzia nikirejea historia ya mapambano kati ya Sitta na serikali, na matokeo mema ya ushujaa aliopata kutokana na ugomvi wake na Lowassa. Kwa ajili ya kutunza kumbukumbu, katika andiko lijalo nitaweka hapa tanzia hiyo iliyochapishwa katika gazeti Mwanahalisi.

Kitu hichooo, Unakumbuka nini?
06/06/2026

Kitu hichooo, Unakumbuka nini?

Katika ulingo wa siasa za Tanzania, mjadala kuhusu chama gani kina sifa na uwezo wa kuongoza dola umekuwa ukiendelea kwa...
05/06/2026

Katika ulingo wa siasa za Tanzania, mjadala kuhusu chama gani kina sifa na uwezo wa kuongoza dola umekuwa ukiendelea kwa miongo mingi sasa. Hata hivyo, unapoangalia uhalisia wa Kisiasa, Ukomavu wa Chama na Uwezo wa kusimamia nchi vizuri kiutawala na kiuchumi, Pia kuna hoja nzito zinazothibitisha kabisa kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bado hakijafikia sifa za kiwango cha kuaminiwa kuongoza nchi, na kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinabaki kuwa chaguo bora na salama zaidi kwa mustakabali wa taifa la Tanzania.

Kikawaida uongozi wa nchi unahitaji zaidi maneno ya jukwaani, Unahitaji mfumo thabiti wa kiutawala unaoweza kushirikiana na vyombo vya dola, Watumishi wa umma na Jumuiya za kimataifa bila kutikisa amani ya nchi.

Chama cha Mapinduzi (CCM) imethibitisha kuwa ni chama chenye muundo mzuri wa Kitaasisi uliopo kuanzia ngazi ya mashina hadi Taifa. Mfumo huu unakipa chama hicho uwezo wa kujipanga, kujisahihisha na kupokezana kijiti cha uongozi wa nchi kwa amani kila baada ya miaka mitano au kumi bila kuwepo kwa mtikisiko wa kisiasa.

Chama Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa upande mwingine, bado kinaonekana kusuasua katika kujenga taasisi imara isiyotegemea haiba au majina ya viongozi wachache Wakuu mfano Heche, Tundu Lissu, Godbless Lema na Sugu. CHADEMA ni Chama kinachoongozwa kwa kufuata upepo wa matukio (Event-Based Politics) badala ya mifumo thabiti ya Chama, Hivyo basi hakina sifa za kukabidhiwa usukani wa kuongoza nchi yenye watu zaidi ya Milioni 65.

Msisahau hivi karibuni, kumekuwa na malalamiko na Shuhuda kutoka kwa wanasiasa wakongwe waliowahi kuhudumu CHADEMA na CCM, k**a vile Mchungaji Peter Msigwa. Katika maelezo yake, Msigwa aliweka wazi tofauti kubwa ya kiutendaji na kimaslahi kati ya vyama hivyo viwili. Alibainisha kuwa ndani ya CCM, kuna utaratibu rasmi na unaoeleweka wa kuwajali watendaji wake pindi wanapotumwa kwenye majukumu ya chama kupitia mfumo wa posho za kujikimu (Per Diem). Tofauti na CHADEMA ambako mifumo hiyo haipo, na watendaji au viongozi mara nyingi wanalazimika kujitegemea au kujitafutia wenyewe namna ya kuishi wakiwa kazini.

Hoja hii lina uzito mkubwa wa kiutawala; K**a chama kinashindwa kuweka mifumo rasmi na endelevu ya kuwatunza na kuwalinda watendaji wake wa ndani, kitawezaje kusimamia Maslahi, Mishahara na Ustawi wa mamilioni ya watumishi wa umma wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania..???

Ustawi wa watendaji ndani ya chama ni kiashiria tosha cha uwezo wa chama hicho kusimamia uchumi na Mgawanyo mzuri wa rasilimali kitaifa.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kina historia ya mda mrefu ya kusimamia diplomasia ya kikanda na kimataifa imejenga uhusiano imara na mataifa makubwa na majirani zetu wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Sera zake za kiuchumi, ingawa zinakosolewa mara kwa mara, zimekuwa na muendelezo (Continuity) unaoruhusu wawekezaji kuwa na imani na nchi.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bado hakijajipambanua kiitikadi kwa namna inayoeleweka na inayoweza kuwapa uhakika wawekezaji wa ndani na nje au nchi jirani. Ahadi zao nyingi za kiuchumi zimekaa kimapinduzi zaidi kuliko uhalisia wa kiuchumi (pragmatism). Katika dunia ya sasa, nchi inahitaji utulivu wa kisera ili kulinda sarafu yake, kuvutia uwekezaji na kukuza ajira mambo ambayo CCM imekuwa ikidhibiti kwa uzoefu mkubwa wa kidola.

Ni kweli Demokrasia inahitaji upinzani imara ili kuishauri na kuikosoa serikali na katika hili, CHADEMA kimefanya kazi kubwa k**a chama cha upinzani. Hata hivyo, kuwa mpinzani mzuri jukwaani hakukufanyi kuwa kiongozi mzuri pale Ikulu.

Kutokana na ukosefu wa mfumo imara ya kiutawala, kutokuwepo kwa taratibu thabiti za kiustawi kwa watendaji wao wa ndani (Uchumi) na ukosefu wa uzoefu wa kusimamia vyombo vya dola, CHADEMA bado hakina sifa stahiki za kuongoza nchi kwa sasa. Kwa muktadha wa ustawi, usalama, na maendeleo ya Tanzania, CCM inabaki kuwa chaguo bora na lenye uhakika zaidi.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kanyamala Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kanyamala Media:

Share