Zamaradi TV

Zamaradi TV NEWS, ENTERTAINMENT and LIFESTYLE channel that has varieties of programs including Series, Talk Shows
(2)

26/09/2025

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNGA) wameondoka ukumbini wakati Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, akihutubia jijini New York. Hatua hiyo ilikuwa ishara ya kupinga mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza.

Tukio hili si la kwanza, kwani mara kadhaa katika miaka iliyopita wajumbe wamewahi kususia hotuba za Netanyahu wakionesha kutoridhishwa na sera za Israel dhidi ya Wapalestina.

Mwaka huu Gaza na Palestina zimekuwa ajenda kuu ya mjadala wa UNGA, ambapo mataifa mengi yameunga mkono kusitishwa kwa vita na kutambuliwa rasmi kwa taifa la Palestina.

Je, unadhani misimamo k**a huu wa kususia hotuba za Israel unaweza kweli kuleta mabadiliko na nafuu kwa Wapalestina? Tuambie maoni yako.

26/09/2025

Polisi wamtafuta mwanaume kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa mwaka mmoja na nusu Arumeru

Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamsaka Daudi Sarakikya, mkazi wa Kata ya Mkwanduwa, Wilaya ya Arumeru, kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wake wa kufikia mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu.

Kwa mujibu wa maelezo ya mama wa mtoto, Prisca Elisamia Mbise, siku ya tukio mtuhumiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa mama yake mzazi (ambaye ni mama mkwe wake), baada ya Prisca kuondoka nyumbani kwenda kusuka nywele.

Prisca amedai kuwa siku hiyo Sarakikya aliaga anakwenda kazini, lakini baadaye alirudi nyumbani na kutekeleza tukio hilo la kikatili.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa linaendelea na msako wa kumtafuta mtuhumiwa huyo, na limewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha anatiwa mbaroni na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

26/09/2025

KIPI KINAKUKERA KWENYE NYUMBA ZA KUPANGA.

MAYATIMA WA MAPENZI SEMENI NA HII

Mapenzi matamu kujiachia kujibana bana hapana lakini kujiachia kuendane na mazingira ila kwenye nyumba za kupanga hapana, tashtiti zinaendana na muonekano pia.

Hii ni Moja ya kero za nyumba za kupanga je wewe kero Yako ni ipi?

26/09/2025

Zitto Kabwe apita nyumba kwa nyumba kuomba kura za Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameendelea na kampeni zake kwa staili ya kupita nyumba kwa nyumba ili kuomba kura na kusikiliza kero za wananchi.

Katika ziara yake, Zitto amewataka wananchi wa Kigoma Mjini kumpa ridhaa ya kuendelea kuwatumikia Bungeni akisisitiza kuwa kipaumbele chake ni kutatua changamoto za kiuchumi, kuboresha huduma za kijamii hususan elimu na afya, pamoja na kuimarisha miundombinu inayounganisha Kigoma na maeneo mengine nchini.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amepokea mkono wa pole kufuatia kifo cha...
26/09/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amepokea mkono wa pole kufuatia kifo cha kaka yake, Abbas Ali Mwinyi, kilichotokea jana, Septemba 25, 2025.

Katika kuonesha mshik**ano wa kitaifa, viongozi mbalimbali walifika nyumbani kwa familia huko Bweleo, Mkoa wa Mjini Magharibi, wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Viongozi wengine walioungana na Rais Samia kutoa pole ni pamoja na:

Naibu Waziri Mkuu, Dotto Mashaka Biteko

Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson Mwansasu

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla

Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zuberi Ali Maulid

Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Asha-Rose Migiro

Pamoja na viongozi wengine wa Serikali na Chama.

Kwa mujibu wa ratiba, marehemu atasaliwa Masjid Jamia Zinjibar, Mazizini baada ya Sala ya Ijumaa, na kisha kuzikwa Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja, leo Ijumaa, Septemba 26, 2025.

26/09/2025

Amchamba Mama shughuli kisa hajamualika sherehe yake. Mama viazi awapasha wanaosema kaolewa na Mzee.

Usikose kuangalia Mwambao mix Ijumaa hii saa mbili kamili usiku ndani ya kisimbuzi cha Azam pekee chaneli 413 . Marudio jumamosi saa tisa mchana na jumapili saa kumi jioni.

Host
🎥💻

Cc



26/09/2025

Mkuu wa mkoa wa Geita Martin Shigela amezipongeza taasisi za fedha kwa namna zinavyoendelea kuwawezesha wachimbaji wadogo kwa kuwapa mikopo yenye riba nafuu ili waweze kuboresha mitaji yao.

Ametoa pongezi hizo wakati alipotembelea katika maonesho ya 8 ya teknolojia ya madini yanayoendelea mkoani Geita katika viwanja vya Dkt Samia Suluhu Hassan.

Akiwa katika viwanja hivyo Shigela alisema kuwa hapo awali ilikuwa ni nadra kwa wachimbajji kukopesheka na mabenki lakini sasa kupitia serikali ya awamu ya sita imehakikisha wachimbaji wadogo wanaaminika na kukopesheka.

Nazo taasisi za fedha zimeendelea kuwasisitiza wachimbaji kujitokeza kuchukua mikopo hii yenye riba nafuu ili waweze kukuza mitaji

Kwa upande wake makamu rais wa kampuni ya uchimbaji ya Geita Gold Mine ambayo ni mmdhamini mkuu wa maonesho ya 8 ya teknolojia ya madini ametoa wito wa wafanya biashara na wadau mbalimbali kujitokeza kuchangamkia fursa hii adimu.

25/09/2025

Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa licha ya changamoto na makosa madogo yaliyoweza kujitokeza katika uongozi wao, hakuna chama kingine kinachoweza kulinda utu na maslahi ya Mtanzania zaidi ya CCM.

Akizungumza leo katika mkutano wa kampeni Mchinga, mkoani Lindi, Dk. Samia amewaambia wananchi kuwa safari ya miaka minne hadi mitano ya uongozi wake imejumuisha changamoto, lakini dhamira kuu ya chama imeendelea kuwa kulinda utu wa kila Mtanzania.

"Inawezekana hapa na pale katika safari yetu ya miaka minne-mitano tukawa tumekosea hapa na pale. Lakini nataka niwaambie, hakuna chama kitakachoweza kulinda na kuinua utu wa Mtanzania k**a sio Chama cha Mapinduzi (CCM)," alisema Dk. Samia huku akishangiliwa na wananchi.

25/09/2025

Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Wolfgang Pisa, ametangaza marufuku kwa watumishi wote wa kanisa kushiriki katika kampeni za kisiasa, akisisitiza kuwa hatua hiyo inalenga kulinda heshima na nafasi ya kanisa.

Akizungumza leo Septemba 25, 2025, katika misa ya kuadhimisha miaka 100 ya Seminari ya Kipalapala – Tabora, Askofu Pisa alieleza kuwa ni kosa kubwa kwa mapadri, watawa na waseminari kushiriki au kuonekana kwenye kampeni za vyama vya siasa.

"Mtawa, padri au kiongozi yeyote wa kanisa hapaswi kushiriki kwenye kampeni zozote za siasa. Wala hapaswi kutambulishwa na chama chochote kwa kuvalishwa gwanda au mavazi yenye alama za chama. Ni marufuku makubwa," amesema Askofu Pisa.

Tamko hilo limekuja siku moja baada ya picha kusambaa mitandaoni zikionyesha Masista wa Kituo cha Mtakatifu Benedicto wa Msaada wa Kikristo Afrika – Ndanda, wakihudhuria mkutano wa kampeni za CCM huko Masasi, mkoani Mtwara, wakiwa wameshikilia machapisho ya kampeni.

Askofu Pisa alionya juu ya kuvishwa mavazi ya vyama k**a kofia au fulana, na pia akatoa tahadhari kwa watu wanaodaiwa kuwarubuni watumishi wa kanisa kushiriki siasa.

"Haipaswi kumrubuni mtu asiyefahamu, iwe ni mtawa au mnovisi. Unamk**ata, unamvalisha, halafu unamfanyisha mambo ya kisiasa. Hilo ni kosa, ni dhambi na marufuku kabisa," ameongeza.

25/09/2025

Amanda arudi tena mjini kivingine ndani ya remix x Queen of dancehall
asign upya na original record label yake “Warner Records” na atarelease album yake mpya ya “Madam X” in 2026
is thinking to quit modelling for good kukimbizia ndoto zake… je unafahamu ni ndoto ipi hiyo!?
amnunulia mke wake

Host:

25/09/2025

Tangu klabu ya Simba kuachana na Fadlu Davis utani Bado unaendelea kuhusu kocha yanga Bado wanapiga kichwani kwa mtani wao.

Mdau kijiweni kinaruka Kila siku ya jumatano saa 2:00 usiku na marudio ni alhamis saa 11:00 Asubuhi Chanel namba 413
Host:

Address

Shabaha Street
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zamaradi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zamaradi TV:

Share

Category