Zamaradi TV

Zamaradi TV NEWS, ENTERTAINMENT and LIFESTYLE channel that has varieties of programs including Series, Talk Shows
(2)

23/05/2026

Sina Kawaida ya kuiga maisha na sitaiga.

Najikuna ninapojiweza na nina majeshi kila upande hao marafiki nn'ari hasidi wa motoni mpoooo.

23/05/2026

Kila mtu na rizki Yake hapa mjini wenye husda zao waendelee kukaa nazo.

Napendeza Sina Mume na sidangi napendeza Kwa neema ya Jaala.

Mwisho kabisa kutembea na wanaume wengi sio kupata gudubaiiii

23/05/2026

Walisema mengi Sana siku ya Leo ya kuwanyamazisha mdomo.

Wamesema mengi Sana lakini Wameumbuka maana Jibu la mjinga ni Vitendo.

Japo maskini lakini simuombi mtu. Bi Yuu k**a Bi Yuu hiyo Zanzibar mie napenda

21/05/2026

Tahaaruki imezuka eneo la Sinza jijini Dar es Salaam baada ya moto mkubwa kulipuka katika City Style Hotel usiku wa leo na kuanza kuteketeza sehemu ya jengo hilo.

Mpaka sasa chanzo cha moto huo hakijafahamika huku wananchi wengi wakikusanyika eneo la tukio kushuhudia hali ilivyo pamoja na kusaidia jitihada mbalimbali za uokoaji.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji tayari limefika katika eneo hilo na linaendelea na operesheni ya kudhibiti moto huo ili kuzuia usisambae zaidi.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa hadi sasa kuhusu madhara, majeruhi au idadi ya watu walioathirika na tukio hilo. taarifa zaidi zinatarajiwa kutolewa kadri uchunguzi utakavyoendelea

18/05/2026

Msanii mkongwe Matumaini amesema maisha yake yalijengwa katika misingi ya kujitunza na kulinda utu wake, jambo analodai huenda limechangia kuchelewa kufanikiwa kiuchumi k**a watu wengine kwenye tasnia.
Akizungumza kuhusu historia ya majina ya wasanii wa vichekesho, Matumaini amefunguka kuwa marehemu Sharo Milionea aliitwa jina la “Sharobaro” kwa mara ya kwanza na msanii Kiwewe, ingawa mwanzoni jambo hilo lilizua sintofahamu na kutokuelewana na Bob Junior.
Amesema baada ya kutoka kwa filamu ya Back From America, marehemu Sharo alianza kutumia jina la “Sharo Milionea”, hali iliyosaidia kuondoa tofauti zilizokuwepo na kufanya mambo kwenda sawa ndani ya kundi lao la burudani.
Host

18/05/2026

Mrs Captain ukimpenda muite Rais wa nyumba kubwa mwenye umri mdogo.

Anakwambia kuletewa uke wenza ndani raha unapata mapumziko na kupata muda wa kufanya biashara zako Kwa nafasi hahaha mke Mkubwa mwenye umri mdogo kachangamka vipi.

18/05/2026

Naitwa mina Dubenga nadhani hakuna asiyenijua. K**a haujaja kwenye shughuli yangu wala hujakata sare asubuhi nakuja mlangoni mwako.

Are we together? Anaitwa Minah Dubenga Madam mwenye sauti yake Wanaomjua washamjua balaa lake si kitoto

16/05/2026
15/05/2026

“Natamani kurudi kwenye game” – Matumaini awaomba producers wa Bongo wampe nafasi tena

Mwanadada Matumaini amefunguka kuhusu hamu yake ya kurejea tena kwenye game la sanaa na kazi mbalimbali za burudani, akisema bado ana ndoto kubwa ya kufanya kazi na kujikwamua kiuchumi kupitia kipaji chake.

Akizungumza kwa hisia, Matumaini amesema changamoto kubwa anayokutana nayo kwa sasa ni ukimya kutoka kwa producers wengi wa Bongo, jambo linalomfanya kujiuliza k**a wanaogopa kufanya naye kazi au la.

Amesema anatamani sana kupata nafasi nyingine ya kuonyesha uwezo wake, huku akisisitiza kuwa bado ana nguvu, uwezo na nia ya kufanya kazi kwa bidii k**a zamani.

Kupitia ujumbe wake, Matumaini amewaomba producers na wadau wa sanaa nchini wamkumbuke katika kazi zao na kumpa nafasi ya kurejea tena kwenye industry ili aweze kusimama upya kimaisha.

Address

Shabaha Street
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zamaradi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zamaradi TV:

Share

Category