02/03/2022
● heshimu na thamini uumbaji wa MUNGU
● Thamini watu walio umbwa kwa sura na mfano wake, haijalishi ni mbaya au mzuri, rafiki au adui, ndugu au jirani wewe wathamini na uwapende na Yeye ata hukumu wale walio wabaya kwako.
● Mungu anaposema mpende adui yako anamaanisha ata aliye mbaya kwako usimchukie wewe jukumu lako ni kuonesha upendo tu sababu ndio roho aliyo kuumbia nayo..chochote kilicho kinyume na kusudi lake jua icho hakitokani na YEYE.
● Sasa hacha kiburi cha uzima,usidharau asiye nacho wala usinyanyue mabega kwa kupata kwako riziki...
MHUBIRI 9:11
" Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote."..
● Nawe usiye nacho usinung'unike wala kulaumu kwa kukosa kwako bali msifu YEYE aliye chanzo cha uhai wako, Mungu asikii lawama zako bali anasikiliza hoja.
ISAYA 41:21
"Haya, leteni maneno yenu, asema BWANA; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo."...
ZINGATIA,
UBARIKIWE SANA...