PNTV-Kiswahili

  • Home
  • PNTV-Kiswahili

PNTV-Kiswahili Pata Habari MBALI MBALI zikiwemo Michezo,BURUDANI,Biashara na Uchumi, Teknolojia nk
(1)

Mrisho mpoto alionyesha Mapenzi MAKUBWA kwa Mke wakeKwenye Moja ya mahojiano na Mrisho Mpoto(M ) yaliyofanyika miaka miw...
16/07/2025

Mrisho mpoto alionyesha Mapenzi MAKUBWA kwa Mke wake

Kwenye Moja ya mahojiano na Mrisho Mpoto(M ) yaliyofanyika miaka miwili iliyopita kwenye Tamasha la MtokoWaPasaka2023 lililofanyika MlimaniCity, Mrisho mpoto aliweka wazi kuwa yeye anaongozwa na Mke wake nyumbani na anajivunia sana kwani Bi.Mariam Ally anamuweka kuwa bora siku zote katika miaka 25 ya ndoa, Mjomba alituma salamu za mapenzi pia kwa mkewe akiwa na furaha kubwa ikionyesha ni jinsi gani anampenda Mkewe.

Leo kwa masikitiko makubwa ametangaza kifo cha mke wake, pole sana kwa mtihani huu mzito mjomba Mungu atakupitisha salama.๐Ÿ™

Follow PNTV-Kiswahili
Philemon Rwegasira Bagoka

Nyota wa Barcelona Lamine Yamal anachunguzwa kuhusiana na uwepo kwa kundi la watu wa jamii ya mbilikimo k**a watumbuizaj...
15/07/2025

Nyota wa Barcelona Lamine Yamal anachunguzwa kuhusiana na uwepo kwa kundi la watu wa jamii ya mbilikimo k**a watumbuizaji katika hafla ya kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake wikendi iliyopita ambapo alitimiza miaka 18.

Ripoti ya kuchunguzwa kwa Yamal imethibitishwa na Wizara ya haki za kijamii ya nchini Uhispania. Wizara hiyo iliiagiza Ofisi ya mwendesha mashtaka kuchunguza tukio hilo, kufuatia malalamiko kutoka kwa Chama kinachowaakilisha watu hao wanaoishi na changamoto ya kimaumbile (ADEE)

Licha ya uchunguzi kuanzishwa, mbilikimo hao wanasema hawakushurutishwa kuwepo kwenye halfa hiyo wala hawakudhalilishwa na yeyote na sio mara yao ya kwanza kuwa kwenye sherehe k**a hiyo ambapo kazi yao huwa kusakata densi na kuwasilisha vinywaji kwa wageni waalikwa.
Follow PNTV-Kiswahili

Kupitia Mradi wa kuboresha Ubora wa Elimu Sekondari (SEQUIP) wananchi mkoani Geita wamenufaika na miundombinu ya ujenzi ...
15/07/2025

Kupitia Mradi wa kuboresha Ubora wa Elimu Sekondari (SEQUIP) wananchi mkoani Geita wamenufaika na miundombinu ya ujenzi wa shule mpya mbili za sekondari zitakazorahisisha upatikanaji wa huduma za elimu mkoani humo.

Shule hizo ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Wasichana Geita ambayo imejengwa katika Manispaa ya Geita huku ikiwa imeanza kutoa huduma za elimu kwa wanafunzi.

Jumla ya Shilingi Bilioni 4.1 zimetolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika shule ya wasichana Geita ikiwemo maabara, vyumba vya madarasa na ofisi, Vyoo vya waliku na wanafunzi, mabweni, nyumba za walimu, Jengo la utawala, Bwalo, Jengo la TEHAMA, na Mashimo ya maji taka.

Pia serikali inaendelea na ujenzi wa shule mpya na ya kisasa ya Amali mkoani Geita ikiwa inajengwa katika Kijiji cha Iboya katika kata na Wilaya ya Mbogwe kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.6

Pia ukamilishaji wa Shule mpya ya Amali ambayo inajengwa ikiwa ni utekelezaji wa sera mpya ya elimu ya mafunzo ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023.

Miili ya watu wanne ikiwemo wanaume watatu na mwanamke mmoja imeokotwa ikiwa imetupwa katika vichaka maeneo tofauti ya W...
14/07/2025

Miili ya watu wanne ikiwemo wanaume watatu na mwanamke mmoja imeokotwa ikiwa imetupwa katika vichaka maeneo tofauti ya Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amesema hayo leo Jumatatu Julai 14, 2025 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kusema kuwa kati ya miili hiyo, mwili wa mwanaume mmoja, umebainika kuwa ni wa Benard Wilson Masaka (43), mfanyabiashara wa nyama (bucha) mkazi wa Manispaa ya Morogoro.

Amesema chanzo cha mauaji ya Bernard kinaelezwa kilihusishwa na wivu wa kibiashara kutokana na biashara yake ya nyama ambayo alikuwa akiifanya huko Morogoro.

Ameongeza kuwa watuhumiwa waliotajwa kuhusika katika mauaji hayo wamek**atwa na tayari wamefikishwa mahak**ani kwa ajili ya hatua nyingine za kisheria.

"Miili mingine miwili ya wanaume, ambayo bado haijatambuliwa, ilikutwa imetupwa porini katika maeneo tofauti ndani ya Wilaya ya Handeni, na inaendelea kuhifadhiwa kwa ajili ya utambuzi na uchunguzi zaidi,"amesema Kamanda Mchunguzi.

Cheka na PNTV-Kiswahili
14/07/2025

Cheka na PNTV-Kiswahili

RASMI:Mokwena amesaini kandalasi ya kuitumikia Mc ALGER  ya Algeria Follow PNTV-Kiswahili
14/07/2025

RASMI:Mokwena amesaini kandalasi ya kuitumikia Mc ALGER ya Algeria
Follow PNTV-Kiswahili

Chama Cha Demokrasia ja Maendeleo (CHADEMA) kimetoa taarifa kwa Umma juu ya Mtaalamu wake wa Fedha na Uwekezaji, Leonard...
14/07/2025

Chama Cha Demokrasia ja Maendeleo (CHADEMA) kimetoa taarifa kwa Umma juu ya Mtaalamu wake wa Fedha na Uwekezaji, Leonard Magere kuwa amefichwa na Jeshi la Polisi.

Magere alik**atwa na Jeshi la Polisi jana Jumamosi, Julai 12, 2025 kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam alipokuwa anataka kusafiri kwenda nje ya nchi.

โ€œMpaka saa tano usiku wa jana, Polisi walisema watampeleka Kituo Kikuu cha Polisi (Central) Dar es Salaam. Lakini asubuhi ya leo viongozi wa chama walipofika Central wakaambiwa Magere hajafikishwa kituoni hapo.

Polisi wa Central waliwashauri viongozi wetu waende kituo cha Polisi cha Uwanja wa Ndege, lakini walipofika wakaambiwa Magere hayupo kituoni hapo.

Tunalitaka Jeshi la Polisi lieleze wapi walipomficha Leonard Magere na wanamshikilia kwa kosa gani.โ€ ___imeeleza taarifa hiyo ya CHADEMAโœ๏ธ

Follow PNTV-Kiswahili

Rais Paul Biya wa Cameroon 92, ametangaza kuwa atawania katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 12 nchini Cameroon.Follow
14/07/2025

Rais Paul Biya wa Cameroon 92,
ametangaza kuwa atawania katika
uchaguzi mkuu wa Oktoba 12 nchini
Cameroon.
Follow

FT  3 - 0  Club World cup Follow PNTV-Kiswahili Philemon Rwegasira Bagoka
13/07/2025

FT
3 - 0

Club World cup
Follow PNTV-Kiswahili
Philemon Rwegasira Bagoka

13/07/2025

Half Time
Chelsea 3-0 PSG
CLUB WORLD CUP

๐—›๐—”๐—ž๐—จ๐—ก๐—” ๐— ๐—ง๐—œ๐—” ๐—ก๐—œ๐—” ๐—ฌ๐—˜๐—ฌ๐—ข๐—ง๐—˜ ๐—”๐—Ÿ๐—œ๐—ฌ๐—˜๐—ž๐—”๐—ง๐—ช๐—” ๐—๐—œ๐—ก๐—” - ๐—–๐—ฃ๐—”. ๐— ๐—”๐—ž๐—”๐—Ÿ๐—Ÿ๐—”Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Itikadi, Ue...
13/07/2025

๐—›๐—”๐—ž๐—จ๐—ก๐—” ๐— ๐—ง๐—œ๐—” ๐—ก๐—œ๐—” ๐—ฌ๐—˜๐—ฌ๐—ข๐—ง๐—˜ ๐—”๐—Ÿ๐—œ๐—ฌ๐—˜๐—ž๐—”๐—ง๐—ช๐—” ๐—๐—œ๐—ก๐—” - ๐—–๐—ฃ๐—”. ๐— ๐—”๐—ž๐—”๐—Ÿ๐—Ÿ๐—”

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Itikadi, Uenezi na Mafunzo ๐—–๐—ฃ๐—”. ๐—”๐—บ๐—ผ๐˜€ ๐— ๐—ฎ๐—ธ๐—ฎ๐—น๐—น๐—ฎ akiongea na Wandishi wa Habari leo tarehe 13 Julai 2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma, amesema hakuna Mtia nia yeyote aliyeenguliwa kwenye nafasi za kuomba kugombea nafasi za Udiwani au Ubunge.

CPA. Makalla amesema mchakato bado unendelea ndani ya Chama na sasa Sekretarieti ya Chama hicho inaendelea kupokea taarifa kutoka Mikoani kisha kwenda Kamati kuu na baadae taarifa rasmi itawekwa wazi.

โ€œNaomba nisisitize, kwa utaratibu wetu wa Chama cha Mapinduzi mpaka sasa hakuna Mtu ambaye ameenguliwa au kukatwa k**a ambavyo inaripotiwa kwenye Vyombo vya Habari, nimeona ( wameandika ) huyu kapenya au huyu kafyekwa, huyu hayupo kwenye tatu bora, k**a nilivyosema mchakato huu wa uteuzi utahitimishwa na kikao cha Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi hapo ndio itakuwa mwisho wa kupata majibu ya mchakato mzima wa Wagombea wanaoteuliwa kwenda katika kura za maoniโ€

Aidha, CPA. Makalla amesisitiza kuwa mara baada ya Kamati Kuu kuketi na kujadili, CCM itatoka na kutoa taarifa rasmi ambazo ndizo za ukweli.

โ€œKamati Kuu itakapohitimisha tutatoka kuwaambia walioteuliwa kwenda katika kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi, zamani nyie mnajua ilikuwa Watu wote wakigombea wote wanakwenda kupigiwa kura za maoni kwahiyo tumesema utaratibu wa sasa watateuliwa wachache ili kwenda kupigiwa kura za maoniโ€

Follow PNTV-Kiswahili

Hili ni jiwe la Ergaki lililosimama kwa usawa kamili kwa zaidi ya miaka milioni 400.Follow PNTV-Kiswahili
13/07/2025

Hili ni jiwe la Ergaki lililosimama kwa usawa kamili
kwa zaidi ya miaka milioni 400.
Follow PNTV-Kiswahili

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when PNTV-Kiswahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to PNTV-Kiswahili:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share