13/07/2025
๐๐๐๐จ๐ก๐ ๐ ๐ง๐๐ ๐ก๐๐ ๐ฌ๐๐ฌ๐ข๐ง๐ ๐๐๐๐ฌ๐๐๐๐ง๐ช๐ ๐๐๐ก๐ - ๐๐ฃ๐. ๐ ๐๐๐๐๐๐
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Itikadi, Uenezi na Mafunzo ๐๐ฃ๐. ๐๐บ๐ผ๐ ๐ ๐ฎ๐ธ๐ฎ๐น๐น๐ฎ akiongea na Wandishi wa Habari leo tarehe 13 Julai 2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma, amesema hakuna Mtia nia yeyote aliyeenguliwa kwenye nafasi za kuomba kugombea nafasi za Udiwani au Ubunge.
CPA. Makalla amesema mchakato bado unendelea ndani ya Chama na sasa Sekretarieti ya Chama hicho inaendelea kupokea taarifa kutoka Mikoani kisha kwenda Kamati kuu na baadae taarifa rasmi itawekwa wazi.
โNaomba nisisitize, kwa utaratibu wetu wa Chama cha Mapinduzi mpaka sasa hakuna Mtu ambaye ameenguliwa au kukatwa k**a ambavyo inaripotiwa kwenye Vyombo vya Habari, nimeona ( wameandika ) huyu kapenya au huyu kafyekwa, huyu hayupo kwenye tatu bora, k**a nilivyosema mchakato huu wa uteuzi utahitimishwa na kikao cha Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi hapo ndio itakuwa mwisho wa kupata majibu ya mchakato mzima wa Wagombea wanaoteuliwa kwenda katika kura za maoniโ
Aidha, CPA. Makalla amesisitiza kuwa mara baada ya Kamati Kuu kuketi na kujadili, CCM itatoka na kutoa taarifa rasmi ambazo ndizo za ukweli.
โKamati Kuu itakapohitimisha tutatoka kuwaambia walioteuliwa kwenda katika kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi, zamani nyie mnajua ilikuwa Watu wote wakigombea wote wanakwenda kupigiwa kura za maoni kwahiyo tumesema utaratibu wa sasa watateuliwa wachache ili kwenda kupigiwa kura za maoniโ
Follow PNTV-Kiswahili