Bnet Hub

Bnet Hub Shaloom! Ungana nasi kupata mafundisho na maoni huru yenye lengo la kusaidia watu katika nyanja mbalimbali za maisha kwa mtazamo wa wazi na wa kidini.

Tunampenda Yesu Kristo
Tufatilie

Yakobo 4:6Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyek...
20/07/2025

Yakobo 4:6
Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.

Siku yako na Ibarikiwe
___
Jiunge na WhatsApp Channel kupata mstari wa Biblia kila siku: Click link hii: https://whatsapp.com/channel/0029VamocnxJP21D2SPnOp27

Neno la Mungu.Waefeso 4:22-24mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye...
16/07/2025

Neno la Mungu.

Waefeso 4:22-24
mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.

Siku yako na Ibarikiwe
Jiunge na WhatsApp Channel kupitia link hii ili kupata mstari wa Biblia kila siku na mafundisho ya Neno la Mungu.
https://whatsapp.com/channel/0029VamocnxJP21D2SPnOp27
____

Shaloom Mwana wa Mungu! Andiko hili linaonyesha kuwa upendo wa kweli wa mzazi kwa mtoto hujumuisha nidhamu. Kutoa maonyo...
14/07/2025

Shaloom Mwana wa Mungu! Andiko hili linaonyesha kuwa upendo wa kweli wa mzazi kwa mtoto hujumuisha nidhamu. Kutoa maonyo, kuelekeza na hata kuwa mkali inapobidi, ni dalili ya kumjali mtoto. Mzazi anayempuuza mtoto wake anamwacha katika hatari ya kulelewa bila maadili, jambo linaloweza kuathiri maisha yake ya baadaye.
Mzazi au mlezi: Kuwa tayari kuweka mipaka, kufundisha kwa upendo na kutoa nidhamu ya kujenga.

Mwalimu au kiongozi: Wajibika kwa kuwasaidia watoto kuelewa tofauti ya mema na mabaya.

Kijana au mtoto: Kubali maonyo na maelekezo k**a sehemu ya kukuza maisha bora.

Kumbuka: Nidhamu siyo chuki – ni sehemu ya malezi yenye upendo na lengo la kumjenga mtoto awe mtu bora.

📲 Tufuatilie kwa mafundisho zaidi ya maisha, jamii na Neno la Mungu!
➡️ Instagram | Facebook | YouTube: Huru

Mithali 13:24
Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.

Siku yako na Ibarikiwe
___

  za Tamko HuruKatika maisha, watu wenye kujiamini kweli mara nyingi hawahitaji kuonyesha au kuongea mengi kuhusu mafani...
04/06/2025

za Tamko Huru
Katika maisha, watu wenye kujiamini kweli mara nyingi hawahitaji kuonyesha au kuongea mengi kuhusu mafanikio yao au uwezo wao. Wanajua thamani yao, na hilo linaonekana kwenye matendo yao, si maneno tu. Kinyume chake, mara nyingi wale wanaojihisi kutokuwa na uhakika wana mwelekeo wa kujaribu kujionesha kwa sauti ili kujipatia uthibitisho.

Jiulize, unajitokezaje wewe katika maisha yako ya kila siku? Je, unajiamini katika hatua unazochukua, au unahisi unahitaji kuthibitishwa? Jenga imani yako ndani, na watu wataona nguvu yako bila maneno mengi.
___
Jiunge nasi Tamko Huru () kwa mafunzo, motisha, na maarifa yatakayokuwezesha kujiamini na kuishi maisha yenye maana.

📖 Hekima ya Siku - Neno la MunguKatika udhaifu wetu, nguvu ya Mungu hutenda kazi kwa namna ya ajabu. Paulo alijifunza kw...
02/06/2025

📖 Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Katika udhaifu wetu, nguvu ya Mungu hutenda kazi kwa namna ya ajabu. Paulo alijifunza kwamba neema ya Mungu ni ya kutosha kwa kila hali.

Usione aibu kwa udhaifu ulionao leo, kupitia udhaifu huo ndipo Mungu anapojionyesha kuwa mwenye nguvu. 💪

"9. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
10. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu." (2 Wakorintho 12:9-10)

🙌 Siku yako na Ibarikiwe.
👉 Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

  za Tamko HuruMaisha hutupa changamoto na maumivu ambayo mara nyingi yanagusa moyo wetu kwa njia tofauti. Unapokumbwa n...
02/06/2025

za Tamko Huru
Maisha hutupa changamoto na maumivu ambayo mara nyingi yanagusa moyo wetu kwa njia tofauti. Unapokumbwa na maumivu ya zamani, una chaguo muhimu: Je, utaacha maumivu hayo yakakufanya uwe mtu mwenye chuki? Au utaamua kuyatumia magumu k**a madaraja ya kukufikisha mahali pazuri zaidi.

Kuwa mtu mwenye hekima, msikivu, na mwenye nguvu ya kusonga mbele? Uamuzi huu ni wako kila wakati — hakuna mtu mwingine atakayeamua badala yako. Hii ndiyo nguvu yako wewe mwenyewe — chagua kuwa bora zaidi kila siku.

Endelea kujifunza, kuhamasika, na kupata mwelekeo mpya ya maisha kwa kufuatilia akaunti zetu za Tamko Huru () Pamoja tunaweza kuunda maisha yenye maana na mafanikio ya kweli.

"Maumivu ya zamani yanaweza kukufanya kuwa na chuki au kukuimarisha. – Uamuzi ni wako. – John Maxwell (Mtaalamu wa Uongozi)"
___

📖 Hekima ya Siku - Neno la MunguImani ya kweli huambatana na ishara na miujiza, Mungu bado anaponya, anatoa uwezo kwa wo...
01/06/2025

📖 Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Imani ya kweli huambatana na ishara na miujiza, Mungu bado anaponya, anatoa uwezo kwa wote wamwaaminio. Uwezo huu haukuishia zamani—upo hata leo!

Amini kwa moyo wote, miujiza bado inatendeka kwa jina la Yesu. Usiangalie changamoto au tatizo unalopitia, amini k**a alitenda kwa yule atatenda na kwako.

"17. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18. watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya." (Marko 16:17-18)

🙌 Siku yako na Ibarikiwe.
👉 Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

📖 Hekima ya Siku - Neno la MunguKila tendo letu la kila siku, hata lile dogo, linapaswa kuwa kwa ajili ya kumtukuza Mung...
31/05/2025

📖 Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Kila tendo letu la kila siku, hata lile dogo, linapaswa kuwa kwa ajili ya kumtukuza Mungu. Huu ni wito wa maisha ya ibada kila siku.

Maisha yako yote yawe sadaka kwa Mungu. Tukuza Mungu kwa kila jambo unalofanya.

"Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu." (1Wakorintho10:31)

🙌 Siku yako na Ibarikiwe.
👉 Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

  za Tamko HuruMaarifa peke yake hayatoshi. Maisha hayabadilishwi kwa kusoma tu au kujua mambo mengi, bali kwa kuchukua ...
30/05/2025

za Tamko Huru
Maarifa peke yake hayatoshi. Maisha hayabadilishwi kwa kusoma tu au kujua mambo mengi, bali kwa kuchukua hatua kwa kile unachokijua.

Je, ni mara ngapi umesikia au kusoma jambo zuri, ukaona limekugusa, lakini ukaendelea k**a kawaida?

Ujumbe huu ni ukumbusho wa kwamba hatua ndogo unazochukua kila siku ndizo zitakazojenga maisha bora unayoyatamani. Anza leo, usisubiri kesho!
___
Follow kurasa zetu Tamko Huru () kwa mafunzo, motisha, na maarifa yatakayokuwezesha kujiamini na kuishi maisha yenye maana.

📖 Hekima ya Siku - Neno la MunguDhambi inaleta kifo / mauti, lakini Mungu ametupa zawadi kuu—uzima wa milele kupitia kwa...
30/05/2025

📖 Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Dhambi inaleta kifo / mauti, lakini Mungu ametupa zawadi kuu—uzima wa milele kupitia kwa mwanawe Yesu Kristo. Chagua zawadi ya uzima kwa kumwamini yeye na si mshahara wa dhambi ambao ni mauti.

Acha dhambi, pokea uzima. Neema ya Mungu inapatikana bure kwa wote wanaomwamini Kristo.

"Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." (Warumi 6:23)

🙌 Siku yako na Ibarikiwe.
👉 Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

📖 Hekima ya Siku - Neno la MunguFuraha tunayopata kwa kumjua na kumtumikia Mungu ndiyo chanzo cha nguvu zetu. Hata katik...
29/05/2025

📖 Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Furaha tunayopata kwa kumjua na kumtumikia Mungu ndiyo chanzo cha nguvu zetu. Hata katika huzuni, furaha ya Bwana hutufufua. 😊

Usikubali huzuni ikudhoofishe, tafuta furaha ya Bwana, nayo itakutia nguvu mpya.

"10. Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu." (Nehemia 8:10)

🙌 Siku yako na Ibarikiwe.
👉 Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

  za Tamko HuruKila mmoja wetu anakutana na changamoto mbalimbali; kuanguka, kukataliwa, au kuonekana k**a ameshindwa. L...
28/05/2025

za Tamko Huru
Kila mmoja wetu anakutana na changamoto mbalimbali; kuanguka, kukataliwa, au kuonekana k**a ameshindwa. Lakini je, unajua nini kinamfanya mtu awe mkubwa (strong) kweli? Sio ukamilifu wa viungo, elimu, n.k, bali ni uamuzi wa kutokata tamaa.

Ujumbe wa leo ni huu: Usiruhusu kushindwa kukufanye ujione huwezi, endelea. simama tena, kuna ukubwa ndani yako unaosubiri kuonekana kwa walimwengu. Na mara nyingi, unaonekana baada ya kushindwa mara nyingi.

Ungana nasi kwa mafundisho ya maisha, jamii, imani na hekima zitakazokujenga kila siku. Fuatilia akaunti zetu ili usikose ujumbe k**a huu unaogusa maisha yako kwa undani.

“Mwanamume ni mkubwa si kwa sababu hajawahi kushindwa, bali ni kwa sababu kushindwa hakujamzuia kusonga mbele.” — Msemo wa hekima
___

Address


Telephone

+255754060464

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bnet Hub posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Bnet Hub:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share