Bnet Hub

Bnet Hub Shaloom! Ungana nasi kupata mafundisho na maoni huru yenye lengo la kusaidia watu katika nyanja mbalimbali za maisha kwa mtazamo wa wazi na wa kidini.

Tunampenda Yesu Kristo
Tufatilie

07/10/2025

1 Wakorintho 6:18-20
Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Jiunge na channel hii kupata mstari wa siku: πŸ‘‡
https://whatsapp.com/channel/0029VamocnxJP21D2SPnOp27

Siku yako na Ibarikiwe Mwana wa Mungu.


 Zaburi 91:55 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,___English VersionPsalm 91:5Thou shalt not be afraid fo...
29/09/2025



Zaburi 91:5
5 Hutaogopa hofu ya usiku,
Wala mshale urukao mchana,
___
English Version
Psalm 91:5
Thou shalt not be afraid for the terror by night; nor for the arrow that flieth by day;
____

Wagalatia 6: 1-51. Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu k**a huyo kw...
23/09/2025

Wagalatia 6: 1-5
1. Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu k**a huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.

2. Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.

3. Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.

4. Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.

5. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.

Siku yako na Ibarikiwe
___

1 Wakorintho 10:13Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawa...
26/08/2025

1 Wakorintho 10:13
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.




Ayubu 38:12Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza? Umeyajulisha mapambazuko mahali pake?          bibleverse
25/08/2025

Ayubu 38:12
Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza?
Umeyajulisha mapambazuko mahali pake?

bibleverse

Yakobo 4:6Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyek...
20/07/2025

Yakobo 4:6
Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.

Siku yako na Ibarikiwe
___
Jiunge na WhatsApp Channel kupata mstari wa Biblia kila siku: Click link hii: https://whatsapp.com/channel/0029VamocnxJP21D2SPnOp27

Neno la Mungu.Waefeso 4:22-24mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye...
16/07/2025

Neno la Mungu.

Waefeso 4:22-24
mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.

Siku yako na Ibarikiwe
Jiunge na WhatsApp Channel kupitia link hii ili kupata mstari wa Biblia kila siku na mafundisho ya Neno la Mungu.
https://whatsapp.com/channel/0029VamocnxJP21D2SPnOp27
____

Shaloom Mwana wa Mungu! Andiko hili linaonyesha kuwa upendo wa kweli wa mzazi kwa mtoto hujumuisha nidhamu. Kutoa maonyo...
14/07/2025

Shaloom Mwana wa Mungu! Andiko hili linaonyesha kuwa upendo wa kweli wa mzazi kwa mtoto hujumuisha nidhamu. Kutoa maonyo, kuelekeza na hata kuwa mkali inapobidi, ni dalili ya kumjali mtoto. Mzazi anayempuuza mtoto wake anamwacha katika hatari ya kulelewa bila maadili, jambo linaloweza kuathiri maisha yake ya baadaye.
Mzazi au mlezi: Kuwa tayari kuweka mipaka, kufundisha kwa upendo na kutoa nidhamu ya kujenga.

Mwalimu au kiongozi: Wajibika kwa kuwasaidia watoto kuelewa tofauti ya mema na mabaya.

Kijana au mtoto: Kubali maonyo na maelekezo k**a sehemu ya kukuza maisha bora.

Kumbuka: Nidhamu siyo chuki – ni sehemu ya malezi yenye upendo na lengo la kumjenga mtoto awe mtu bora.

πŸ“² Tufuatilie kwa mafundisho zaidi ya maisha, jamii na Neno la Mungu!
➑️ Instagram | Facebook | YouTube: Huru

Mithali 13:24
Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.

Siku yako na Ibarikiwe
___

  za Tamko HuruKatika maisha, watu wenye kujiamini kweli mara nyingi hawahitaji kuonyesha au kuongea mengi kuhusu mafani...
04/06/2025

za Tamko Huru
Katika maisha, watu wenye kujiamini kweli mara nyingi hawahitaji kuonyesha au kuongea mengi kuhusu mafanikio yao au uwezo wao. Wanajua thamani yao, na hilo linaonekana kwenye matendo yao, si maneno tu. Kinyume chake, mara nyingi wale wanaojihisi kutokuwa na uhakika wana mwelekeo wa kujaribu kujionesha kwa sauti ili kujipatia uthibitisho.

Jiulize, unajitokezaje wewe katika maisha yako ya kila siku? Je, unajiamini katika hatua unazochukua, au unahisi unahitaji kuthibitishwa? Jenga imani yako ndani, na watu wataona nguvu yako bila maneno mengi.
___
Jiunge nasi Tamko Huru () kwa mafunzo, motisha, na maarifa yatakayokuwezesha kujiamini na kuishi maisha yenye maana.

πŸ“– Hekima ya Siku - Neno la MunguKatika udhaifu wetu, nguvu ya Mungu hutenda kazi kwa namna ya ajabu. Paulo alijifunza kw...
02/06/2025

πŸ“– Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Katika udhaifu wetu, nguvu ya Mungu hutenda kazi kwa namna ya ajabu. Paulo alijifunza kwamba neema ya Mungu ni ya kutosha kwa kila hali.

Usione aibu kwa udhaifu ulionao leo, kupitia udhaifu huo ndipo Mungu anapojionyesha kuwa mwenye nguvu. πŸ’ͺ

"9. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
10. Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu." (2 Wakorintho 12:9-10)

πŸ™Œ Siku yako na Ibarikiwe.
πŸ‘‰ Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

  za Tamko HuruMaisha hutupa changamoto na maumivu ambayo mara nyingi yanagusa moyo wetu kwa njia tofauti. Unapokumbwa n...
02/06/2025

za Tamko Huru
Maisha hutupa changamoto na maumivu ambayo mara nyingi yanagusa moyo wetu kwa njia tofauti. Unapokumbwa na maumivu ya zamani, una chaguo muhimu: Je, utaacha maumivu hayo yakakufanya uwe mtu mwenye chuki? Au utaamua kuyatumia magumu k**a madaraja ya kukufikisha mahali pazuri zaidi.

Kuwa mtu mwenye hekima, msikivu, na mwenye nguvu ya kusonga mbele? Uamuzi huu ni wako kila wakati β€” hakuna mtu mwingine atakayeamua badala yako. Hii ndiyo nguvu yako wewe mwenyewe β€” chagua kuwa bora zaidi kila siku.

Endelea kujifunza, kuhamasika, na kupata mwelekeo mpya ya maisha kwa kufuatilia akaunti zetu za Tamko Huru () Pamoja tunaweza kuunda maisha yenye maana na mafanikio ya kweli.

"Maumivu ya zamani yanaweza kukufanya kuwa na chuki au kukuimarisha. – Uamuzi ni wako. – John Maxwell (Mtaalamu wa Uongozi)"
___

πŸ“– Hekima ya Siku - Neno la MunguImani ya kweli huambatana na ishara na miujiza, Mungu bado anaponya, anatoa uwezo kwa wo...
01/06/2025

πŸ“– Hekima ya Siku - Neno la Mungu
Imani ya kweli huambatana na ishara na miujiza, Mungu bado anaponya, anatoa uwezo kwa wote wamwaaminio. Uwezo huu haukuishia zamaniβ€”upo hata leo!

Amini kwa moyo wote, miujiza bado inatendeka kwa jina la Yesu. Usiangalie changamoto au tatizo unalopitia, amini k**a alitenda kwa yule atatenda na kwako.

"17. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18. watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya." (Marko 16:17-18)

πŸ™Œ Siku yako na Ibarikiwe.
πŸ‘‰ Follow akaunti zetu kwa mafundisho mengine ya kiroho na ya maisha:
___

Address

Dar Es Salaam
255

Telephone

+255754060464

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bnet Hub posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Bnet Hub:

Share