Jax media TZ.

  • Home
  • Jax media TZ.

Jax media TZ. Kwahabari kem kem za burudani, michezo, siasa, afya, magazeti na makala mbalimbali, like page yetu.

Ikiwa ni siku 3 tu tarehe 26 novemba kamphuni ya mabasi ya baraka classic bus, linalofanya safari zake Kati ya wilaya ya...
29/11/2023

Ikiwa ni siku 3 tu tarehe 26 novemba kamphuni ya mabasi ya baraka classic bus, linalofanya safari zake Kati ya wilaya ya Tandahimba Mtwara na Dar es salaam kufeli breki na kuua watu 14.

Leo 29 novemba, watu 13 wameripotiwa kufariki dunia, huku wengine 25 wakijeruhiwa katika ajali ya basi iliyohusisha basi la abiria la kampuni ya Allys Star lenye namba za usajili T 178 DVD, baada ya basi hilo kugonga kichwa cha treni, katika eneo Manyoni, mkoani Singida.

  Matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika September 2023, umetangazwa  leo Nov 23.ambapo Watahiniwa 1...
23/11/2023

Matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika September 2023, umetangazwa leo Nov 23.

ambapo Watahiniwa 1,092,960 sawa na asilimia 80.58 ya Watahiniwa 1,356,296 wenye matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2023 wamefaulu kwa kupata madaraja ya A,B na C.

Akitangaza matokeo hayo leo Jijini Dar es salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dr.Said Mohamed amesema mwaka 2022 Watahiniwa waliofaulu walikuwa ni asilimia 79.62 hivyo ufaulu mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 0.96.

Wasichana waliofaulu ni 585,040 sawa na asilimia 80.58 ambapo ubora wa ufaulu umeongezeka ikilinganishwa na asilimia 78. 91 mwaka jana huku ubora wa ufaulu kwa Wavulana ukiongozeka ambapo waliofaulu ni 507,920 sawa na asilimia 80.59 ikilinganishwa na asilimia 80.41 kwa mwaka 2022.


MTANZANIA MATEKA ISRAEL AFARIKIWizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kifo cha Mtanzani...
17/11/2023

MTANZANIA MATEKA ISRAEL AFARIKI

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kifo cha Mtanzania Clemence Felix Mtenga ambaye ni mmoja kati ya watanzania wawili pamoja na raia wa mataifa mengine waliokuwa hawajulikani walipo tangu yaliyopotokea mapigano Oktoba 7, 2023 nchini Israel na katika maeneo ya Wapalestina hususani Gaza.

Taarifa iliyotolewa na Wizara imesema Clemence alikuwa ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania wapatao 260 waliokwenda nchini Israel kushiriki mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa vitendo chini ya Mpango wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Israel.

Tayari Wizara imechukua hatua stahiki ikiwemo kuijulisha familia na inaendelea kuwasiliana na serikali ya Israel kuhakikisha kwamba taratibu za kurejesha mwili wa marehemu nchini kwa ajili ya mazishi zinakamilika kwa wakati.

23/10/2023

MTOTO ABAKA NA KULAWITI

:Ni tukio la kustaabisha ambapo jeshi la Polisi Mkoani Mtwara linamshikilia Mtoto mwenye umri wa miaka 14 ambaye ni Mkulima na Mkazi wa Kitongoji cha Chiano Kata ya Nalingu, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara kwa tuhuma za kubaka na kulawiti Watoto wawili ambao ni Ndugu (Watoto wa Dada yake) ambao alikuwa anaachwa nao nyumbani k**a Mlezi pindi Dada yake anapokwenda kufanya shughuli zake za kila siku za kujiingizia kipato.

Mama Mzazi wa Watatoto alipomuhoji Mdogo wake amekiri kufanya hivyo ambapo amesema Mtoto wa k**e amembaka hadi akazoea na sasa anamuona k**a Mke wake huku Mtoto wa kiume akiwa amemuingilia kwa siku tatu na alikuwa anafanya hivyo Mama yao anapokuwa mbali na nyumbani huku akiwatishia kuwa wakimwambia Mama yao atawapiga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Nicodemus Katembo amesema Mtoto aliyebakwa ni wa k**e mwenye umri wa miaka saba na wa kiume wa miaka mitano amelawitiwa ambapo matukio hayo yametokea kuanzia October mosi hadi 15, mwaka huu, katika nyakati tofauti.

AJALI MBAYA MALAWI---------------------------------------Zaidi ya abiria watatu wanahofiwa kufa kufuatia ajali ya baraba...
22/09/2023

AJALI MBAYA MALAWI
---------------------------------------

Zaidi ya abiria watatu wanahofiwa kufa kufuatia ajali ya barabarani iliyohusisha namba za usajili za Toyota Honda Freed TO 979 umbali mrefu wa barabara ya M1 huko Mzimba.

Gari hilo ambalo lilikuwa na idadi ya abiria wasiojulikana inasemekana lilikuwa likitokea Mzuzu kuelekea Mzimba Boma.

Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka Wilaya ya Mzimba wamefika eneo la tukio.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa abiria mmoja amefariki papo hapo.


Ni habari mbaya kwa mtaa wa chakula bora Manzese wilaya Ubungo, ambapo mzee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 anaye...
22/09/2023

Ni habari mbaya kwa mtaa wa chakula bora Manzese wilaya Ubungo, ambapo mzee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 anayefahamika kwa jina moja la mzee Matonya.

Amekutwa amejinyonga mpaka kufa chooni kwake usiku wa kuamkia leo Septemba 22, 2023 huku chanzo chake hakijajulikana.

Akithibitisha, mwenyekiti wa mtaa huo Oddo Ramadhani amekiri kutokea kwa tukio hilo kwenye mtaa wake na kusema amejua asubuhi ya leo baada ya mke wa marehemu kurudi kazini kukuta mlango umefungwa na baada ya kuvunja ndipo wakakuta amejinyonga chooni.

Baadhi ya majirani wamesema mzee huyo alikuwa anatumia muda mwingi kushinda ndani kutokana na matatizo yake ya kuumwa hivyo hawajui sababu iliyompelekea kujinyonga.

PROF, J AAHIDI KURUDI KWA KISHINDO"Nilitembelewa na Katibu mtendaji mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa .tanzania Dr. Kedmon M...
19/09/2023

PROF, J AAHIDI KURUDI KWA KISHINDO

"Nilitembelewa na Katibu mtendaji mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa .tanzania Dr. Kedmon Mapana Nyumbani kwangu Mbweni”

“Tuliyajenga mengi sana kuhusu sanaa yetu hasa fungia fungia ya nyimbo za wasanii maana Baraza la sanaa ni walezi na sio Polisi, pia nilimuahidi atanisikia tena hewani siku si nyingi Stay Tuned".

Professor Jay ameshea taarifa hii kupitia page yake ya Instagram akiwa na Katibu wa BASATA na kuandika


Timu zinagawana alama huko Zambia POWER D 2 - 2 SIMBA SC Magoli yote yamefungwa na Chama
16/09/2023

Timu zinagawana alama huko Zambia
POWER D 2 - 2 SIMBA SC
Magoli yote yamefungwa na Chama

Mchezo  unemalizika  Ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Al Merrikh dhidi ya  Yanga Sc zimemalizika katika dimba la P...
16/09/2023

Mchezo unemalizika Ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Al Merrikh dhidi ya Yanga Sc zimemalizika katika dimba la Pele Kigali Rwanda kwa Wananchi kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.


WATU wanne miongoni mwao wanafunzi watatu wamefariki mjini Lusaka baada ya dereva wa miaka 26 aliyedaiwa kuendesha gari ...
13/09/2023

WATU wanne miongoni mwao wanafunzi watatu wamefariki mjini Lusaka baada ya dereva wa miaka 26 aliyedaiwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi kuwagonga.

Mtu wa tano, ambaye pia ni mwanafunzi na pia aligongwa na dereva alikimbizwa katika Hospitali ya Mafunzo ya Chuo Kikuu (UTH) kwa matibabu.

Naibu msemaji wa polisi Danny Mwale alisema kisa hicho kilitokea leo asubuhi mwendo wa saa 06:30 katika eneo la Ibex Hill huko Lusaka.

"Wanne waliothibitishwa kufariki ni James Phiri mwenye umri wa miaka 13, Felix Mwansa mwenye umri wa miaka 14 na Richard Mapulanga mwenye umri wa miaka 15 wote wakiwa katika Shule ya Family Legacy iliyopo eneo la Ibex Hill.

Marehemu wengine wa kiume bado hawajatambuliwa huku majeruhi. ametambuliwa k**a SamsoniNgoma mwenye umri wa miaka 13 pia ni mwanafunzi katika Shule ya Family Legacy,” alisema.

Bw Mwale alisema uchunguzi wa Polisi unaonyesha kuwa ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa Toyota Camry yenye namba za usajili BAL 5830 aliposhindwa kulidhibiti gari hilo kutokana na mwendo kasi na kuwagonga watembea kwa miguu watano.

“Dereva, aliyetambulika k**a Mulemwa Ak**ani mwenye umri wa miaka 26 wa Woodlands alipata majeraha madogo. Alitibiwa katika kliniki na baadaye kuruhusiwa. Amezuiliwa na polisi bado hajafunguliwa mashtaka,” alisema.


#

Mzee mmoja mwenye umri wa miaka 71 amewashangaza wengi baada ya kukiri katika simulizi yake kuwa hajawahi kuonana uso kw...
13/09/2023

Mzee mmoja mwenye umri wa miaka 71 amewashangaza wengi baada ya kukiri katika simulizi yake kuwa hajawahi kuonana uso kwa uso na mtu yeyote wa jinsia ya k**e kwa zaidi ya miaka 50.

Callixte Mzamwita kutoka Rwanda alisema alianza kujifungia ndani ya nyumba akiwa na umri wa miaka 16 na tangu wakati huo hadi sasa akiwa na umri wa miaka 77 hajawahi kukutana na mwanamke yeyote.

Mzamwita amejifungia ndani ya nyumba kwa miaka 55 sasa. Muda wote huo alijifungia ndani kwa sababu hakutaka kukutana wala kuongea na mwanamke yeyote.

"Sababu inayonifanya nijifungie ndani na kuweka uzio kuzunguka nyumba yake ni kwamba nataka kuhakikisha kwamba hakuna wanawake wanaoweza kunikaribia. Sitaki wanawake karibu nami kwa sababu wananifanya nijisikie hofu sana," mzee huyo alisema. .

Majirani walisema tangu utotoni huwa anakuwa ndani ya boma lake na anapomuona mwanamke anajaribu kuingia ndani ya nyumba yake anakimbilia ndani ya nyumba na kujifungia.

Kisayansi, hali k**a hiyo kulingana na Kliniki ya Cleveland husababishwa na hali inayojulikana k**a Gynophobia.

Hali hiyo inaweza kusababishwa na matukio mbalimbali, ikiwa ni pamoja na matukio ya awali katika utoto, au ushawishi wa kitamaduni.

Majirani hao wa k**e walisema kuwa wengi wao wamekuwa wakimsaidia ingawa hapendi mwanamke kumkaribia.

"Kila mara tunatupa chakula kwenye uzio wa boma lake, hataki tumkaribie lakini yeye huchukua kile tunachomrushia kwa mbali," alisema mmoja.

Ajabu ni kwamba mwanamume huyo hufanya kila kitu ambacho mtu wa kawaida anaweza kufanya nyumbani kwake, ikiwa ni pamoja kuoga, kujisaidia, kupika, na hata malazi.


Boss wa gari iliyoua mwanafunzi katika eneo la Spear Hotel wilayani Magu mkoani Mwanza Athuman M***a (32) amejikuta akia...
22/08/2023

Boss wa gari iliyoua mwanafunzi katika eneo la Spear Hotel wilayani Magu mkoani Mwanza Athuman M***a (32) amejikuta akiangua kilio mahak**ani baada kukosa dhamana kwa kushindwa kukidhi vigezo vya dhamana.

Mashtaka matatu yamesomwa dhidi ya dereva wa gari aina ya Hiace, Malima Masota (30) ambayo ni kuendesha gari kwa mwendo wa hatari na kusababisha kifo cha mwanafunzi, Consolata Marwa kinyume na Kifungu namba 40, 63 (2) (a) na 27 (1) (a) cha Sheria ya Usalama Barabarani namba 168, marejeo ya mwaka 2002.

Mashtaka mengine dhidi ya dereva huyo wa gari iliyogonga na kusababisha kifo cha mwanafunzi na kujeruhi mwingine, ni kuendesha gari kwa mwendo wa hatari na kusababisha majeraha kwa mwanafunzi, Magreth Ntemi na kuendesha gari isiyokuwa na bima kwenye barabara kinyume na kifungu namba 4 (1) na 2 cha Sheria ya Bima ya Magari namba 169 marejeo ya 2002.


  Ni tukio la ukatili alomfanyia mwanae, mkazi wa Chamagati wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, Maneno Thomas (35)Imemgha...
18/08/2023

Ni tukio la ukatili alomfanyia mwanae, mkazi wa Chamagati wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, Maneno Thomas (35)

Imemgharimu, kifungo cha miaka mitano jela baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la ukatili dhidi ya mtoto wake kwa kumuunguza mikono yote miwili akimtuhumu kudokoa mboga aina ya chainizi.

Mneno ametiwa hatiani leo Agosti 18, 2023 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahak**a ya wilaya ya Sengerema, Evod Kisoka,

ambaye amesema mahak**a baada ya kujiridhisha na ushahidi katika shauri hilo bila shaka imemkuta na hatia ya ukatili dhidi ya mtoto wake.

Morce Mtoi, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, aliieleza mahak**a hiyo kuwa Julai 30, 2021, mshtakiwa (Thomas)

alitekeleza ukatili huo wa kummwagia maji ya moto mikononi, Daniel Maneno (8) katika kijiji cha Chamagati wilayani Sengerema mkoani Mwanza.


 : Spika Mstaafu Anne Semamba Makinda ateuliwa  kuwa Mkuu wa Chuo (Chancellor) cha Ushirika Moshi (MoCU) na Rais wa Jamh...
18/08/2023

: Spika Mstaafu Anne Semamba Makinda ateuliwa kuwa Mkuu wa Chuo (Chancellor) cha Ushirika Moshi (MoCU) na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, ambapo uteuzi huu unaanza mara moja.

Full Time : Mtibwa 2 - 4 Simba SCAnthony DK20, 22.Baleke DK5,Onana 9, Ngoma 44 na Chama 80.
17/08/2023

Full Time : Mtibwa 2 - 4 Simba SC

Anthony DK20, 22.

Baleke DK5,Onana 9, Ngoma 44 na Chama 80.


"Mie sina details za makosa yao, isipokuwa ninasimamia uhuru wa kutoa maoni ambao kwa vipimo vyote wanaokosoa Mkataba mb...
16/08/2023

"Mie sina details za makosa yao, isipokuwa ninasimamia uhuru wa kutoa maoni ambao kwa vipimo vyote wanaokosoa Mkataba mbona wako wengi sana tu na hawajak**atwa wanaendelea na mikutano tena huku wakilindwa na polisi. So this tells kwamba hoja sio kukosoa" Nape Nnauye.

Ni waziri wa habari, mawasili na teknolojia ya habari, ambapo ametoa maoni kwenye ukurasa wake wa Twitter kuhusu Kuk**atwa kwa aliyewahi kuwa Mbunge wa jimbo la Karatu, na Katibu mkuu wa Chadema Dr. Willbroad Slaa kufuatia sakata la bandari.

Kuk**atwa huko kwa Dk. Slaa na wenzake wawili kumekuja ikiwa ni siku chache tangu Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura kuonya kuhusu watu aliodai wanaandaa maandamano ya kuipindua Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, akiwataka kusitisha mpango huo kwa kuwa jeshi hilo halitowafumbia macho kwa kitendo hicho.


Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jax media TZ. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jax media TZ.:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share