Jax media TZ.

Jax media TZ. Kwahabari kem kem za burudani, michezo, siasa, afya, magazeti na makala mbalimbali, like page yetu.

 MKUU WA WILAYA ALAANI WANANCHI KUSHANGLIA KIFO"kitendo cha baadhi ya wananchi kushangilia kifo cha MNdugai ni kitu kwel...
07/08/2025



MKUU WA WILAYA ALAANI WANANCHI KUSHANGLIA KIFO

"kitendo cha baadhi ya wananchi kushangilia kifo cha MNdugai ni kitu kweli kimetushangaza, kwa mila za Tanzania inawezakaje mtu anashanglia kifo.

Amekuwa mwanasisa ametumika miaka mingi hawezi kukosa maadui, lakini hatukutegemea kwamba anaweza kuwa na maadui ambaye hata akifa anashangilia...

Sio ustaarabu wa Kitanzania, hili jambo wazazi wakemee vijana wanako elekea sio kuzuri, hatuna uadui wakushangilia mauti yanapomkuta mtu,

Wote ni wafu watarajiwa na tulipaswa mtu anapofariki tunatunza heshima yake" Mkuu wa wilaya ya Kongwa, ndugu Saimon Mayeka.

-----------------------------------------------RAIS SAMIA AMLILIA NDUGAI--------------,"Nimepokea kwa masikitiko taarifa...
06/08/2025

-----------------------------------------------RAIS SAMIA AMLILIA NDUGAI--------------

,"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ninatoa pole kwa familia, wanachama wote wa Chama Cha Mapinduzi, watumishi wa Bunge na Wabunge wote aliotumikia nao akiwa Spika wa Bunge letu, wananchi wa Kongwa, ndugu jamaa na marafiki.

Tuungane pamoja kumuombea kwa Mwenyezi Mungu na kuwaombea familia, ndugu, jamaa na marafiki uvumilivu, faraja na moyo wa ibada katika kipindi hiki kigumu.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Amina."


  Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Kongwa, Job Yustino Ndugai amefariki Dunia leo August 06,2025 akiwa an...
06/08/2025

Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Kongwa, Job Yustino Ndugai amefariki Dunia leo August 06,2025 akiwa anaendelea kupatiwa matibabu Hospitalini baada ya kuugua ghafla.

Ndugai aliyezaliwa January 22,1960 alishinda kura za maoni za Ubunge wa Jimbo la Kongwa.

 : AMBAKA MAMA YAKE KISHA KUMUUA--------------------------Polisi huko Molo nchini Kenya,  wamemk**ata mwanafunzi wa miak...
27/07/2025

: AMBAKA MAMA YAKE KISHA KUMUUA--------------------------

Polisi huko Molo nchini Kenya, wamemk**ata mwanafunzi wa miaka 16 wa Fomu 3 ambaye ilidaiwa alibaka mama yake na baadaye akamuua kwa kutomwonyesha baba yake halisi (wa kumzaa)

Kijana huyo baada ya mauaji alikuwa ameandaa kaburi lisilo na kina ambapo alikusudia kumzika mama yake kwa siri.

Ikiwa ni siku 3 tu tarehe 26 novemba kamphuni ya mabasi ya baraka classic bus, linalofanya safari zake Kati ya wilaya ya...
29/11/2023

Ikiwa ni siku 3 tu tarehe 26 novemba kamphuni ya mabasi ya baraka classic bus, linalofanya safari zake Kati ya wilaya ya Tandahimba Mtwara na Dar es salaam kufeli breki na kuua watu 14.

Leo 29 novemba, watu 13 wameripotiwa kufariki dunia, huku wengine 25 wakijeruhiwa katika ajali ya basi iliyohusisha basi la abiria la kampuni ya Allys Star lenye namba za usajili T 178 DVD, baada ya basi hilo kugonga kichwa cha treni, katika eneo Manyoni, mkoani Singida.

  Matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika September 2023, umetangazwa  leo Nov 23.ambapo Watahiniwa 1...
23/11/2023

Matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika September 2023, umetangazwa leo Nov 23.

ambapo Watahiniwa 1,092,960 sawa na asilimia 80.58 ya Watahiniwa 1,356,296 wenye matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2023 wamefaulu kwa kupata madaraja ya A,B na C.

Akitangaza matokeo hayo leo Jijini Dar es salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dr.Said Mohamed amesema mwaka 2022 Watahiniwa waliofaulu walikuwa ni asilimia 79.62 hivyo ufaulu mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 0.96.

Wasichana waliofaulu ni 585,040 sawa na asilimia 80.58 ambapo ubora wa ufaulu umeongezeka ikilinganishwa na asilimia 78. 91 mwaka jana huku ubora wa ufaulu kwa Wavulana ukiongozeka ambapo waliofaulu ni 507,920 sawa na asilimia 80.59 ikilinganishwa na asilimia 80.41 kwa mwaka 2022.


MTANZANIA MATEKA ISRAEL AFARIKIWizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kifo cha Mtanzani...
17/11/2023

MTANZANIA MATEKA ISRAEL AFARIKI

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kifo cha Mtanzania Clemence Felix Mtenga ambaye ni mmoja kati ya watanzania wawili pamoja na raia wa mataifa mengine waliokuwa hawajulikani walipo tangu yaliyopotokea mapigano Oktoba 7, 2023 nchini Israel na katika maeneo ya Wapalestina hususani Gaza.

Taarifa iliyotolewa na Wizara imesema Clemence alikuwa ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania wapatao 260 waliokwenda nchini Israel kushiriki mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa vitendo chini ya Mpango wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Israel.

Tayari Wizara imechukua hatua stahiki ikiwemo kuijulisha familia na inaendelea kuwasiliana na serikali ya Israel kuhakikisha kwamba taratibu za kurejesha mwili wa marehemu nchini kwa ajili ya mazishi zinakamilika kwa wakati.

23/10/2023

MTOTO ABAKA NA KULAWITI

:Ni tukio la kustaabisha ambapo jeshi la Polisi Mkoani Mtwara linamshikilia Mtoto mwenye umri wa miaka 14 ambaye ni Mkulima na Mkazi wa Kitongoji cha Chiano Kata ya Nalingu, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara kwa tuhuma za kubaka na kulawiti Watoto wawili ambao ni Ndugu (Watoto wa Dada yake) ambao alikuwa anaachwa nao nyumbani k**a Mlezi pindi Dada yake anapokwenda kufanya shughuli zake za kila siku za kujiingizia kipato.

Mama Mzazi wa Watatoto alipomuhoji Mdogo wake amekiri kufanya hivyo ambapo amesema Mtoto wa k**e amembaka hadi akazoea na sasa anamuona k**a Mke wake huku Mtoto wa kiume akiwa amemuingilia kwa siku tatu na alikuwa anafanya hivyo Mama yao anapokuwa mbali na nyumbani huku akiwatishia kuwa wakimwambia Mama yao atawapiga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Nicodemus Katembo amesema Mtoto aliyebakwa ni wa k**e mwenye umri wa miaka saba na wa kiume wa miaka mitano amelawitiwa ambapo matukio hayo yametokea kuanzia October mosi hadi 15, mwaka huu, katika nyakati tofauti.

AJALI MBAYA MALAWI---------------------------------------Zaidi ya abiria watatu wanahofiwa kufa kufuatia ajali ya baraba...
22/09/2023

AJALI MBAYA MALAWI
---------------------------------------

Zaidi ya abiria watatu wanahofiwa kufa kufuatia ajali ya barabarani iliyohusisha namba za usajili za Toyota Honda Freed TO 979 umbali mrefu wa barabara ya M1 huko Mzimba.

Gari hilo ambalo lilikuwa na idadi ya abiria wasiojulikana inasemekana lilikuwa likitokea Mzuzu kuelekea Mzimba Boma.

Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka Wilaya ya Mzimba wamefika eneo la tukio.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa abiria mmoja amefariki papo hapo.


Ni habari mbaya kwa mtaa wa chakula bora Manzese wilaya Ubungo, ambapo mzee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 anaye...
22/09/2023

Ni habari mbaya kwa mtaa wa chakula bora Manzese wilaya Ubungo, ambapo mzee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 anayefahamika kwa jina moja la mzee Matonya.

Amekutwa amejinyonga mpaka kufa chooni kwake usiku wa kuamkia leo Septemba 22, 2023 huku chanzo chake hakijajulikana.

Akithibitisha, mwenyekiti wa mtaa huo Oddo Ramadhani amekiri kutokea kwa tukio hilo kwenye mtaa wake na kusema amejua asubuhi ya leo baada ya mke wa marehemu kurudi kazini kukuta mlango umefungwa na baada ya kuvunja ndipo wakakuta amejinyonga chooni.

Baadhi ya majirani wamesema mzee huyo alikuwa anatumia muda mwingi kushinda ndani kutokana na matatizo yake ya kuumwa hivyo hawajui sababu iliyompelekea kujinyonga.

PROF, J AAHIDI KURUDI KWA KISHINDO"Nilitembelewa na Katibu mtendaji mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa .tanzania Dr. Kedmon M...
19/09/2023

PROF, J AAHIDI KURUDI KWA KISHINDO

"Nilitembelewa na Katibu mtendaji mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa .tanzania Dr. Kedmon Mapana Nyumbani kwangu Mbweni”

“Tuliyajenga mengi sana kuhusu sanaa yetu hasa fungia fungia ya nyimbo za wasanii maana Baraza la sanaa ni walezi na sio Polisi, pia nilimuahidi atanisikia tena hewani siku si nyingi Stay Tuned".

Professor Jay ameshea taarifa hii kupitia page yake ya Instagram akiwa na Katibu wa BASATA na kuandika


Address

Charambe Former Mbagala Temeke Municipal Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jax media TZ. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jax media TZ.:

Share