Bantu Media

Bantu Media Hard News | Entertainment | Gossip | Celebrity News | Sports News
📩 For Advertisement:
📱 Whatsapp: +255 (658) 840 840
📬 Email: [email protected]

30/09/2025

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika ujenzi wa barabara muhimu wilayani Same ili kurahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo na kufungua fursa mpya za maendeleo.

‎Akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika Septemba 30, 2025, Dkt. Samia alisema kuwa ujenzi wa barabara ya Mkomazi–Kisiwani–Same yenye urefu wa kilomita 101 tayari umeanza na kugawanywa katika vipande viwili.

‎“Kipande cha kwanza ni Mkomazi–Ndungu chenye kilomita 36 ambapo ujenzi umeanza kwa gharama ya shilingi bilioni 59, na mkandarasi ameshakamilisha kilomita 10. Aidha, kipande cha pili cha Mroyo–Same chenye kilomita 65 mkandarasi amepatikana na tumeshasaini mkataba. Tunachosubiri sasa ni malipo ya awali ili kazi ianze mara moja,” alisema Dkt. Samia.

‎Aliongeza kuwa Serikali inatambua changamoto za usafirishaji wa zao la tangawizi linalolimwa kwa wingi katika tarafa za Mamba na maeneo mengine ya milimani, na hivyo imepanga kujenga barabara hizo kwa kiwango cha zege na lami ili kurahisisha usafirishaji wa mazao.

‎“Niwaahidi barabara hizi muhimu tutazikamilisha kwa viwango bora. Mungu akituwezesha, tutaendelea kufanya kazi hii ili kila mkulima anufaike,” alisisitiza.

30/09/2025

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika kupeleka umeme vijijini na kuboresha huduma za afya nchini, huku akiahidi kuendeleza juhudi hizo ili Watanzania wote wanufaike na maendeleo.

‎Akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika Septemba 30, 2025, wilayani Same mkoani Kilimanjaro, Dkt. Samia alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM iliahidi kupeleka umeme vijijini, lakini utekelezaji wake umevuka malengo hayo na kufika hadi vitongoji.

‎“Tumemaliza zaidi ya nusu ya vitongoji vyote nchini na katika mwaka mmoja na nusu ujao tutakuwa tumemaliza vilivyobaki. Tanzania nzima itawaka umeme,” alisema Dkt. Samia.

‎Akizungumzia sekta ya afya, Dkt. Samia alikumbuka changamoto kubwa alizoziona mwaka 2015 alipokuwa mgombea mwenza, ambapo alishuhudia zahanati duni zilizoshindwa kutoa huduma bora kwa wajawazito. Alisema hali hiyo ndiyo iliyompa dhamira ya kuhakikisha kila wilaya inakuwa na hospitali na vituo vya afya vyenye vifaa kamili, dawa na watumishi.

‎“Leo namshukuru Mungu tumefanikiwa kuboresha sekta ya afya. Tutaendelea kujenga hospitali za wilaya na vituo vya afya vya kisasa ili hakuna mwanamke atakayepoteza maisha kwa sababu ya kujifungua,” alisisitiza.

‎Kwa upande wa Same, alisema tayari vituo sita vya afya vimekamilika, na sasa Serikali inakamilisha ujenzi wa vituo vingine vitatu vya afya pamoja na zahanati tano. Pia alibainisha kuwa katika kata za Zewa na Makanya miradi ya ujenzi inaendelea kwa kasi.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi k...
30/09/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo katika Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, endapo atachaguliwa kuendelea kuongoza nchi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

‎Akizungumza na wananchi wa Same, Dkt. Samia amesema CCM imeweka kipaumbele cha kuimarisha huduma za jamii, miundombinu ya barabara, elimu, afya na maji, ili kuinua maisha ya wananchi wa wilaya hiyo na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

‎Dkt. Samia amebainisha kuwa tayari barabara za milimani zikiwemo Mwembe–Myamba–Ndungu, Lembeni–Kilomeni–Lomwe na Kifaru–Kirurumo–Kichwa cha Ng’ombe zimekamilika, sambamba na daraja la Hingiriri lililojengwa ili kurahisisha usafiri na shughuli za kibiashara. Aidha, amesema barabara ya Same–Kisiwani–Mkomazi nayo imefungua fursa kubwa za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

‎Katika sekta ya afya, Dkt. Samia ameahidi kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Same, huku barabara za lami zikijengwa katika mji wa Same na barabara za kiwango cha changarawe zikiboresha usafiri maeneo ya John Malecela, Makanya–Ruvu–Muungano, Same–Ruvu–Mferejini na Makuruvila.

‎Akizungumzia huduma za maji, amesema miradi ya Mroyo, Vuje, Kihurio, Msindo Awamu ya Pili na Maore–Beseline–Ihindi itakamilishwa, sambamba na ukarabati wa skimu za umwagiliaji katika maeneo ya Maore, Ngoja, Igoma, Kalemane, Bendera, Mbuyu na Yongoma, ili kuongeza uzalishaji wa kilimo.

‎Vilevile, ameeleza kuwa mradi mkubwa wa tangawizi “Mamba Myamba” wenye thamani ya Shilingi bilioni 2.5 ni kielelezo cha uwekezaji utakaosaidia wananchi kuongeza kipato, huku sekta ya elimu ikiboresha kupitia ujenzi wa shule mpya ikiwemo Sekondari ya Angellah Kairuki.

‎Katika sekta ya utalii, amesema Serikali yake itaendelea kuimarisha vivutio kwa kukamilisha jengo la kulia chakula katika Hifadhi ya Taifa Mkomazi pamoja na kuchimba visima viwili vya maji kwa ajili ya wanyamapori.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt....
29/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Muheza Ndugu Hamis Mwijuma ‘Mwana FA’ mara baada ya kuwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Muheza mkoani Tanga tarehe 29 Septemba, 2025.

Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuwasihi wananchi wa Muheza kuiami...
29/09/2025

Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuwasihi wananchi wa Muheza kuiamini CCM kwa mara nyingine, akibainisha utekelezaji mkubwa wa miradi ya maendeleo iliyofanyika wilayani humo chini ya serikali ya awamu ya sita.

‎Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni leo, Dkt. Samia amesema sekta ya afya imepewa kipaumbele, ambapo zahanati 10 zimejengwa katika vijiji mbalimbali, vituo vya afya vitatu kwenye kata za Misalai, Misozwe na Mhamba, pamoja na ujenzi na ukarabati wa Hospitali ya Wilaya. Aidha, nyumba 15 za watumishi wa afya zimejengwa huku hospitali ya wilaya ikipatiwa majengo mapya ya wagonjwa mahututi (ICU) na huduma za dharura.

‎Katika miundombinu ya barabara, amesema serikali imetekeleza ujenzi na matengenezo makubwa, ikiwemo barabara ya Muheza–Amani yenye urefu wa kilomita 40 kwa kiwango cha lami, barabara za Amani–Muheza, Pangani–Muheza na Mlingano–Kiomoni zikiwa kwenye kiwango cha changarawe, pamoja na matengenezo ya barabara ya Old Maguzoni–Old Korogwe (km 28). Pia, kilomita tatu za barabara mpya zimewekwa lami ndani ya Wilaya ya Muheza, zaidi ya kilomita 200 za changarawe zikijengwa, pamoja na madaraja matatu mapya.

‎Kwa upande wa maji, Dkt. Samia amebainisha utekelezaji wa miradi mikubwa inayogusa vijiji zaidi ya 50, vikiwemo Mikwinini, Msasa, Kwamdakeo, Kwemsala, Kisiwani, Maduma, Kwakifua, Ngarani, Mkwajuni, Gare, Kwasimba, Magomba, Misufini, Kwemwewe, Maramba A, Kwemsoso, Mwarimba, Kazita, Mgambo, Shambangeda, Zirai, Kwedunda, Mtiti na maeneo mengine mengi.

‎“Wanamuheza wenzangu, miradi hii mnayoiona ni ushahidi kwamba CCM ikiahidi, inatekeleza. Tumeboresha afya, tumefungua barabara, tumewaletea maji. Na bado tuna mpango wa kufanya zaidi tukipata ridhaa yenu tena.

29/09/2025

Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuendeleza uwekezaji katika sekta ya uvuvi na mifugo kwa wananchi wa Wilaya ya Pangani, Mkoa wa Tanga.

‎Akihutubia mamia ya wananchi katika Viwanja vya Gombero leo Jumatatu, Septemba 29, 2025, Dkt. Samia alisema serikali imeanza mchakato wa ujenzi wa Soko la Kimataifa la Samaki katika Kata ya Kipumbwi, litakalogharimu shilingi bilioni 1.3. Soko hilo pia litahusisha miundombinu ya kukaushia dagaa ili kuongeza thamani ya bidhaa na kipato cha wavuvi.

‎Aidha, alisisitiza umuhimu wa wafugaji kutumia fursa ya ruzuku za chanjo zinazotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita, ikiwemo chanjo za bure kwa kuku na punguzo la nusu bei kwa chanjo za mbuzi na ng’ombe. Alieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza thamani ya mazao ya mifugo na kuviwezesha kushindana katika masoko ya kimataifa.

‎Akizungumzia mafanikio yaliyopatikana ndani ya miaka minne ya uongozi wake, Dkt. Samia alibainisha kuwa Pangani imenufaika na upatikanaji wa boti 15 za kisasa za uvuvi zenye thamani ya shilingi bilioni 1.6, jambo lililoongeza eneo la uvuvi na kukuza pato la wavuvi na wilaya kwa ujumla.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi k...
29/09/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuifanya Wilaya ya Pangani kuwa kitovu cha maendeleo kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa inayogusa sekta za afya, elimu, barabara, maji, biashara na viwanda.

‎Akihutubia mamia ya wananchi wa Pangani, Dkt. Samia amesema CCM imedhamiria kujenga na kukamilisha zahanati 7, vituo vya afya 3 na kuboresha Hospitali ya Wilaya, ikiwemo ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi na huduma za dharura. Aidha, aliahidi nyumba za watumishi wa afya kujengwa ili kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi.

‎Kwa upande wa miundombinu, Dkt. Samia amesisitiza kuwa serikali yake itajenga na kukarabati zaidi ya km 400 za barabara kwa kiwango cha changarawe, km 5 kwa kiwango cha lami, taa 200 za barabarani pamoja na madaraja 10, huku akiahidi kuharakisha ujenzi wa daraja la mto Pangani lenye urefu wa mita 525 litakalounganisha wananchi na kurahisisha biashara.

‎Katika sekta ya elimu, ameeleza mpango wa kujenga madarasa 36 ya shule za msingi, shule mpya 2, sekondari ya amali, mabweni 3, mabwalo 4 ya chakula, nyumba 11 za walimu na maabara 10. Vilevile, shule kongwe zitakarabatiwa na miundombinu ya elimu ya sekondari kuimarishwa, ikiwemo kidato cha tano na sita.

‎Dkt. Samia pia ameahidi kuendeleza miradi ya maji katika vijiji vya Mtonga, Mivumoni na Buyuni, sambamba na ukarabati mkubwa wa kivuko MV Tanga – Pangani II.

‎Kwa upande wa uchumi, ameahidi kujengwa kwa soko la samaki la kisasa Kipumbwi na kuanzishwa kwa viwanda vitatu vya kuchakata mkonge katika kata za Bushiri, Mkalamo na Ubangaa ili kuongeza ajira na kuinua kipato cha wananchi.

‎“Wananchi wa Pangani, naomba muendelee kutuamini. CCM haiahidi hewa, bali utekelezaji. Tulichokianza tutakimalizia na kitakachoahidiwa, kitafanyika. Maendeleo yenu ndio ajenda yetu kuu,” alisema Dkt.Samia

Maelfu ya wananchi na wapiga kura wa Pangani, Mkoani Tanga, wakiendelea kuwasili kwenye Viwanja vya Kwa Temba leo Jumata...
29/09/2025

Maelfu ya wananchi na wapiga kura wa Pangani, Mkoani Tanga, wakiendelea kuwasili kwenye Viwanja vya Kwa Temba leo Jumatatu, Septemba 29, 2025, tayari kwaajili ya kumlaki na kumsikiliza Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mgombea huyo anaanza rasmi Mikutano yake ya Kampeni Mkoani Tanga, akitarajiwa kufanikisha mikutano mitatu katika Wilaya za Pangani, Muheza, na Tanga Mjini.

Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassa...
28/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kushirikiana na sekta binafsi katika ujenzi wa barabara ya haraka (expressway) itakayounganisha Kibaha, Chalinze na Morogoro.

‎Akihutubia mkutano wa kampeni katika viwanja vya Polisi wilayani Chalinze mkoani Pwani, Septemba 28, 2025, Dkt. Samia amesema barabara hiyo itajengwa kwa awamu na itaongeza tija kiuchumi kwa Taifa kwa kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo.

‎“Kwa upande wa miundombinu tutashirikiana na sekta binafsi katika ujenzi wa Barabara ya haraka ya Kibaha–Chalinze–Morogoro ambayo itajengwa kwa awamu. Hii ni barabara yenye tija kiuchumi hivyo tutashirikiana na sekta binafsi ili wao watoe fedha sisi tufanye mambo mengine,” amesema Dkt. Samia.

‎Aidha, katika sekta ya afya, Dkt. Samia amewapongeza wananchi wa Chalinze kwa mafanikio ya kutokuwa na vifo vya mama na mtoto, akibainisha kuwa ni kielelezo cha dhamira ya serikali kuboresha huduma za afya nchini.

‎Amesema kuwa serikali yake itaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kudumisha upatikanaji wa dawa na utekelezaji wa programu ya bima ya afya ambao utakuwa mpango wa kitaifa miongoni mwa mambo mengine.

Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan, ...
26/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Ijumaa Septemba 26, 2025 anatarajiwa kuwa na Mkutano mkubwa wa Kampeni Mtwara Mjini, Mkoani Mtwara, akitarajiwa kueleza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita pamoja na yale ambayo Chama Cha Mapinduzi wamepanga kuyafanya ikiwa watepewa ridhaa kupitia uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

‎Jana Alhamisi akiwa Lindi Mjini kwenye Viwanja vya Ilulu, Dkt. Samia pamoja na kuahidi kuendelea kutoa huduma muhimu za kijamii kwa wananchi, amewahakikishia pia Watanzania kuwa mradi mkubwa wa kuchakata na kusindika gesi asilia kuwa kimiminika (LNG) umekaribia kuanza utekelezaji wake, akisema mradi huo ni mkubwa ukiwa na thamani ya Dola za Marekani Bilioni 40 sawa na Shilingi trilioni 100 na hivyo serikali ilitaka kuwa na uhakika wa manufaa kabla ya kuanza utekelezaji wake.

‎Kuhusu Uvuvi Mkoa wa Lindi, Dkt. Samia amebainisha kuwa ujenzi wa bandari ya Uvuvi Kilwa unaoendelea, utakapokamilika utatoa ajira 30,000 na kufungua fursa za Viwanda vya kuchakata samaki lakini pia serikali ina mpango wa kujenga kiwanda cha kusindika samaki kando ya ujenzi wa Kongani za Viwanda kila Wilaya ambazo zitakuwa zinaongeza thamani ya mazao ya kilimo, misitu na uvuvi.

‎Kwa Mtwara Mjini CCM na Dkt. Samia wameahidi Kujenga meli ya mizigo kutoka Mtwara hadi Visiwa vya Comoro, Ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR kutoka bandari ya Mtwara hadi Mbambabay na Songea hadi Ludewa ili kuunganishwa na mradi wa makaa ya mawe, upanuzi wa uwanja wa ndege Mtwara kwa awamu ya pili ikijumuisha ujenzi wa jengo la abiria la kisasa, mnara wa kuongozea ndege, jengo la kituo cha zimamoto na jengo la kituo cha hali ya hewa, ukamilishaji wa jengo la utawala Halmashauri ya Mtwara.

‎Wameahidi pia Ujenzi wa maghala 7 ya kuhifadhia mazao, Ujenzi wa jengo la maonesho ya kilimo la Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, Ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Arusha chini, Uboreshaji wa miundombinu ya Maji Mji wa Mtwara, ujenzi wa kiwanda cha sukari katika bonde la Mto Kitere, ujenzi wa kiwanda cha kubangua korosho, mradi mkubwa wa kutoa maji mto Ruvuma hadi Mtwara.

‎Aidha Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM imeahidi pia Upimaji na Upangaji Mji, Ujenzi daraja la Kilambo (Tanzania- Msumbiji border), ujenzi barabara ya Mangamba- Madimba (Km 35.63) na Madimba- Tangazo (Km16.87), Ujenzi wa Machinjio 3 ya kisasa, uendelezaji wa Hospitali ya Kanda Mtwara, ukamilishaji wa majengo ya Hospitali ya Manispaa ya Mtwara, Ujenzi wa vituo vya afya Kata ya Mtawanya, Mkutimango na Ndumbwe, Namtumbuka, Mnima na Chawi na ujenzi wa Zahanati 12 Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.

Maelfu ya wananchi wa Lindi Mjini wamejitokeza kwa wingi leo Septemba 25, 2025 kushiriki katika mkutano wa kampeni za Ch...
25/09/2025

Maelfu ya wananchi wa Lindi Mjini wamejitokeza kwa wingi leo Septemba 25, 2025 kushiriki katika mkutano wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika katika uwanja wa Ilulu.
‎Wananchi hao walijitokeza kwa shauku kubwa kumsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye anaendelea na mikutano yake ya kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

‎"Kwenye upande wa afya kazi ni ileile, kasi ni ileile. Kwenye maeneo ambayo bado hayajapata vituo vya afya tutajenga vi...
25/09/2025

‎"Kwenye upande wa afya kazi ni ileile, kasi ni ileile. Kwenye maeneo ambayo bado hayajapata vituo vya afya tutajenga vituo vya afya lakini kwa Mkoa wa Lindi tumejitahidi huduma za afya karibia zote zinapatikana hapa hata zile za kibingwa kwasababu kuna hospitali kubwa ya rufaa ambayo huduma zote zitamalizika ndani ya Mkoa na yale makubwa sana ndiyo yatakayoenda Muhimbili au maeneo mengine lakini huduma za kibingwa zinapatikana hapa kwahiyo kwa ukanda huu wa kusini mambo ua afya yapo vizuri.

‎Ombi la watumishi k**a nilivyosema wakati nazindua kampeni, tutakapoingia ndani ya siku mia moja za mwanzo tutaajiri Watumishi 5,000 kwenye sekta ya afya na hao wakati wa kufanya mgao Lindi nao watafaidika. Kwenye elimu tunaendelea na kasi ileile kujenga shule za msingi na sekondari na hii ni kwasababu tuna watoto na Mungu aendelee kuwaweka kwahiyo kasi ni ileile pamoja na ombi la kujenga nyumba ya waalimu huu ndio mradi tunaoenda nao kwa awamu ijayo."- Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea wa nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM akizungumza leo Septemba 25, 2025 na wananchi wa Mchinga Mkoani Lindi.

Address

Tabata
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bantu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share