Bantu Media

Bantu Media Hard News | Entertainment | Gossip | Celebrity News | Sports News
📩 For Advertisement:
📱 Whatsapp: +255 (658) 840 840
📬 Email: [email protected]

Staa mpya wa Wydad Casablanca Stephane Aziz Ki ataweka historia katika maisha yake ya soka kwa kucheza Kombe la Dunia la...
02/06/2025

Staa mpya wa Wydad Casablanca Stephane Aziz Ki ataweka historia katika maisha yake ya soka kwa kucheza Kombe la Dunia la Vilabu ambalo litaanza Juni 15 mwaka huu.

Wydad ni moja ya timu za Afrika ambazo zinashiriki michuano hiyo sambamba na Esperance,Al Ahly na Mamelodi Sundowns.

Timu hiyo kutoka Morocco itaanza kampeni ya kusaka taji hilo kwa mchezo wao wa kwanza wa Juni 18 dhidi ya Manchester City ambao utawakutanisha Stephane Aziz Ki na Erling Haaland.

Kanisa la Ufufuo na Uzima la Askofu Gwajima limefungiwa kwa kosa la kutumika Kisiasa.
02/06/2025

Kanisa la Ufufuo na Uzima la Askofu Gwajima limefungiwa kwa kosa la kutumika Kisiasa.

Golikipa wa Guinea, Moussa Camara jana alishindwa kufanya mazoezi ya mwisho kuelekea kwenye mechi ya leo ya Kufuzu Kombe...
25/03/2025

Golikipa wa Guinea, Moussa Camara jana alishindwa kufanya mazoezi ya mwisho kuelekea kwenye mechi ya leo ya Kufuzu Kombe la Dunia 2026 dhidi ya wenyeji wao Uganda.

Camara bado hajapona majeraha yake licha ya siku zilizopita kufanya mazoezi na timu hiyo.

Hii hapa orodha ya wachezaji 15 wenye majina magumu zaidi duniani 1. Sokratis Papastathopoulos(Greece)2. Jakub Błaszczyk...
22/03/2025

Hii hapa orodha ya wachezaji 15 wenye majina magumu zaidi duniani

1. Sokratis Papastathopoulos
(Greece)

2. Jakub Błaszczykowski:
(Poland)

3. Grzegorz Krychowiak:
(Poland)

4. Wojciech Szczęsny:
(Poland)

5. Yevhen Olehovych Konoplyanka:
(Ukraine)

6. Jakub Wawrzyniak:
(Poland)

7. Panagiotis Tachtsidis:
(Greece)

8. Hakan Çalhanoglu:
(Turkey)

9. Lukasz Piszczek:
(Poland)

10. Przemysław Tytoń:
(Poland)

11. Abdul-Nasir Oluwatosin Oluwadoyinsolami Tosin Adarabioyo :
( England)

12. Khvicha Kvaratskelia:
(Georgia)

13. Elijah Anuolowapo Oluwaferanmi Oluwatomi Oluwalana Ayomikulehin Adebayo
( England)

14. Vennegoor Of Hesselink:
(Netherlands)

15. Diniyar Bil Lyatedinov:
(Russian Federation)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Kinara wa Maji Afrika (The PANAF...
22/03/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Kinara wa Maji Afrika (The PANAFRICAN Water, Sanitation and Hygiene Champion Award) kutoka Taasisi ya WaterAid UK ya nchini Uingereza aliyokabidhiwa na Mkurugenzi wa WaterAid Pan Africa Dr. Tanko Yussif Azziko wakati wa hafla ya Kilele cha Wiki ya Maji na Uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Maji 2002, Toleo la 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City tarehe 22 Machi 2025, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Samia Suluhu Hassan amesema hali ya upatikanaji Wa huduma ya maji nchini ime...
22/03/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,Samia Suluhu Hassan amesema hali ya upatikanaji Wa huduma ya maji nchini imefikia asilimia 83 maeneo ya Vijijini na asilimia 95 maeneo ya mijini.

Amesema jitihada zinaendelea kuhakikisha inafikiwa asilimia 85 Kwa maeneo ya Vijijini.

Rais Samia ametoa kauli hiyo wakati wa Maadhimisho ya Kilele Cha Wiki ya Maji na Uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002 toleo la mwaka 2025 Ukumbi wa Mlimani City Dar es salaam leo Machi 22,2025.

Mwanadada maarufu  hapa nchini Queen Mlerwa anaendelea kukazia kuwa alimkataa Mwanamuziki wa Bongo Fleva  Diamond Platnu...
20/03/2025

Mwanadada maarufu hapa nchini Queen Mlerwa anaendelea kukazia kuwa alimkataa Mwanamuziki wa Bongo Fleva Diamond Platnumz akidai kuwa hana uwezo wa kumpa mahitaji yote anayoyataka.

"Mapenzi yanahitaji pesa siwezi kudate na mtu bahili ndio maana nilimkataa D, Nahitaji mwanaume mwenye uwezo wa kunipa kila kitu nitakacho kwa wakati."- Queen Mlerwa.

Toa maoni yako.

Mchungaji wa Mitume na Manabii Daudi Mashimo amehukumiwa kifungo cha miaka miwili na miezi sita Jela na Mahakama ya Wila...
18/03/2025

Mchungaji wa Mitume na Manabii Daudi Mashimo amehukumiwa kifungo cha miaka miwili na miezi sita Jela na Mahakama ya Wilaya Kinondoni baada ya kukutwa na hatia ya jinai ya kuvamia eneo la watu.

Mchungaji Mashimo alikuwa akikabiliwa na mashtaka kadhaa ya kuvamia na kuishi kwenye eneo la mlalamikaji Flora Jonasi, kuharibu mali kwa makusudi, na kufanya vurugu dhidi ya Ramsoni.

Mahakama ilimkuta na hatia katika mashtaka ya mawili, huku ikimuondolea shtaka moja ambalo wamemkuta hana hatia.

Baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mtuhumiwa ameshauri ndugu, jamaa na marafiki kukata rufaa ikiwa hawajaridhika na uamuzi huo.

Kijiji cha Mbati Wilaya ya Tunduru Ruvuma kimebarikiwa msitu wenye magogo yanayogeuka mawe, hii imesababisha kutembelewa...
10/11/2024

Kijiji cha Mbati Wilaya ya Tunduru Ruvuma kimebarikiwa msitu wenye magogo yanayogeuka mawe, hii imesababisha kutembelewa na wageni kutoka ndani na nje ya Nchi.

Mratibu wa Utalii Kanda ya Kusini ambaye pia ni Afisa Msaidizi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Tunduru Debora Mwakanosya amesema miti inayogeuka mawe (Miti mawe) ni jamii ya miti ya mitetereka ambayo Duniani inapatikana nchi mbili ambazo ni Marekani na Tanzania na ina uwezo wa kudumu zaidi ya miaka 120.

Amesema mti huo ukiuona juu unakuwa ni mti wa kawaida lakini unageuka jiwe kutokana na mfumo wa asili ambao Mungu ameuumba “hata hivyo ipo katika hatari kubwa ya kutoweka kutokana na Watu wengi kuikata kwa matumizi mbalimbali"

Address

Tabata
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bantu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share