11/01/2026
Iran Yaionya Marekani Yasema Itaishambulia Israel Iwapo Marekani Itaingilia Sakata la Maandamano….
Maandamano ya kitaifa yanayopinga utawala na kupanda kwa gharama za maisha wa Iran yalishuhudia waandamanaji wakifurika mitaani katika mji mkuu wa nchi hiyo na jiji lake la pili kwa ukubwa hadi leo Jumapili, wakivuka vizingiti vya polisi na kuingia maeneo ya malengo yao.
Maandamano hayo yemeingia wiki yake ya pili huku vurugu zikiwa kubwa zaidi kuliko zile za mwanzo na kupelekea kufariki kwa watu wasiopungua 120 mpaka sasa.
Naye spika wa bunge la Iran ameonya kwamba jeshi la Marekani na Israeli watakuwa shabaha yao mashariki ya kati, ikiwa Amerika itashambulia nchi hiyo ya Kiislamu, k**a ilivyotishiwa na Rais Donald Trump.
Mamlaka ya Iran jana Jumamosi ilisema kwamba inaweza kuongeza msako wao dhidi ya wasababishi wa maandamano hayo makubwa zaidi ya kupinga serikali kuwahi kutokea kwa miaka mingi yaliyopelekea kuzimwa kwa mtandao.