Msasa Online

Msasa Online Matangazo Piga Simu +255758379300
(1)

MSASA ONLINE
Ni kiwanda cha habari kinacho tumia ubunifu na uvumbuzi wa teknolojia kwa kutoa habari, michezo, burudani, na elimu kidijitali kwa wafuasi wake na jamii inayozungumza kiswahili duniani kote karibu.

 Kabila Ashtakiwa Kwa Makosa Ambayo Adhabu Yake Ni Kifo…..Mahak**a Kuu ya Kijeshi mjini Kinshasa, nchini Jamhuri ya Kide...
25/07/2025


Kabila Ashtakiwa Kwa Makosa Ambayo Adhabu Yake Ni Kifo…..

Mahak**a Kuu ya Kijeshi mjini Kinshasa, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, leo inaanza kusikiliza kesi ya mashtaka ya kijeshi dhidi ya Joseph Kabila, rais wa zamani wa nchi hiyo, kwa tuhuma zinazohusiana na madai yake ya uanachama wa AFC/M23.

Haijabainika iwapo Kabila, ambaye amerejea nchini mwake katika eneo linalodhibitiwa na waasi wa M23, atafikishwa mahak**ani. Inatarajiwa kwamba anaweza kuhukumiwa bila kuwepo kwake.

Hii ilikuwa ni baada ya Bunge kumuondolea kinga, na bado hakuweza kujieleza kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Katika kesi hiyo inayoanza saa 9:00 alasiri kwa saa za Kinshasa, Kabila anatuhumiwa kwa makosa ya jinai yakiwemo kushirikiana na kundi la waasi, Usaliti, Kuhalalisha uasi, Mateso, Kuua kwa risasi, Ubakaji jijini Goma, na Kuvuruga amani.

Baadhi ya makosa haya yanaadhibiwa na kifo chini ya sheria za DRC.

 Awashtaki Waliokwisha Fariki Kwa Kumfunga Miaka 35 Kimakosa....Mwanaume mmoja kutoka Maryland nchini Marekani ambaye al...
25/07/2025


Awashtaki Waliokwisha Fariki Kwa Kumfunga Miaka 35 Kimakosa....

Mwanaume mmoja kutoka Maryland nchini Marekani ambaye alifungwa kimakosa kwa miaka 32, kwa mauaji mawili ambayo hakuyatenda, amewash*taki maafisa wa zamani wa utekelezaji wa sheria.

Hata hivyo watu wanne kati ya watano waliotajwa k**a washtakiwa tayari walishafariki.

John Huffington alitoka gerezani baada ya kupata wa Gavana wa zamani Larry Hogan Januari 2023.

Hogan alitaja ukiukaji wa maadili ya mwendesha mashtaka alipompa Huffington msamaha kamili wa kutokuwa na hatia kuhusiana na mauaji ya watu wawili yaliyotokea mwaka 1981 katika Kaunti ya Harford.

Bodi moja ya serikali ya Maryland iliidhinisha fidia ya dola milioni 2.9 kwa ajili ya Huffington.

Huffington alisema katika taarifa yake jana kwamba, ilichukua miaka mingi ya maumivu, lakini hatimaye ukweli ulidhihirika.

Alik**atwa akiwa na umri wa miaka 18, na alisema kuwa wazazi wake wote wawili hawakupata nafasi ya kuona wala kuelewa kuwa jina lake lilikuwa limesafishwa (kufutiwa hatia) na kwamba alikuwa ameachiliwa huru kwani tayari walifariki akiwa yeye bado yuko gerezani.

 Rapa Glorilla Ak**atwa Na Bangi Na Madawa Mengine Ya Kulevya.....Msanii wa muziki wa rap Bi dada maarufu nchini Marekan...
25/07/2025


Rapa Glorilla Ak**atwa Na Bangi Na Madawa Mengine Ya Kulevya.....

Msanii wa muziki wa rap Bi dada maarufu nchini Marekani, GloRilla, ambaye jina lake halisi ni Gloria Woods, amek**atwa wiki hii kwa makosa ya jinai yanayohusiana na dawa za kulevya baada ya polisi kupata kiasi kikubwa cha bangi walipokuwa wakichunguza tukio la wizi nyumbani kwake mjini Atlanta.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Sheriff wa Kaunti ya Forsyth, GloRilla alijisalimisha kwa hiari siku ya Jumanne na aliachiliwa kwa dhamana ya dola 22,260 siku hiyo hiyo.

Askari walifika nyumbani kwa msanii huyo mnamo saa 7:30 usiku wa kuamkia Jumapili baada ya kupokea taarifa za uvamizi uliotokea kwenye nyumba ya msanii huyo (nyumbani kwa GloRilla).

Woods hakuwepo nyumbani wakati huo, kwani alikuwa ametumbuiza wakati wa mapumziko ya kipindi cha kwanza cha Mchezo wa Nyota wa Ligi ya Mpira wa Vikapu kwa Wanawake (WNBA All-Star Game) siku ya Jumamosi mjini Indianapolis.

Kikosi maalum cha kupambana na dawa za kulevya kilipata hati ya upekuzi baada ya askari kunusa harufu kali inayofanana na ile ya dawa za kulevya wakati wa uchunguzi wa tukio la wizi.

Kikosi hicho kilikuta bangi ikiwa wazi ndani ya kabati la chumba kikuu cha kulala, kwa mujibu wa taarifa hiyo.

GloRilla (Gloria Woods) amefunguliwa mashtaka ya kumiliki bangi na pia kumiliki dawa nyingine za kulevya zilizodhibitiwa.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Msasa Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share