13/12/2025
Daktari ashtakiwa kwa kufanya Upasuaji akiwa amelewa huku akiangalia Youtube Video….
Mwanamke mmoja katika eneo la Barabanki huko Uttar Pradesh nchini India amefariki baada ya daktari bandia kumfanyia upasuaji wa mawe ya figo kwa kutazama video ya YouTube(Tutorial) .
Daktari huyo, akiwa amelewa, alishindwa kuondoa mawe hayo kwenye figo yake na badala yake akakata mishipa mingi tumboni, utumbo mdogo, na umio(oesophagus), jambo lililosababisha kifo chake.
Mwasiliwa huyo, aliyetambuliwa k**a Munishra Rawat, alipata maumivu makali ya tumbo mnamo Desemba 5 ndipo Mumewe, Fateh Bahadur, alimpeleka Shri Damodar Aushadhalaya, kliniki isiyotambulika kisheria huko Barabanki.
Daktari mmiliki es kliniki Gyan Prakash Mishra nawasaidizi Vivek Mishra na Gyan Prakash waligundua kuwa maumivu ya mwanamke huyo yalisababishwa na mawe ya figo na walipendekeza upasuaji ili na uliogharimu Rupia 25,000, ambayo baadaye ililipwa Rupia 20,000.
Siku iliyofuata, Prakash alianza upasuaji huku akitazama video ya YouTube akiwa amelewa, na matokeo yake, alikata mishipa kadhaa ya damu, na ndipo Siku iliyofuata, Munishra alifariki, kwa maumivu makali.
Fateh Bahadur mume wa mwanamke huyo aliwasilisha malalamiko katika kituo cha polisi cha eneo hilo, na baada ya kupata habari za tukio hilo, polisi walikimbilia eneo hilo na kukagua eneo la tukio lakini watuhumiwa hao wamekimbia na bado hawajak**atwa.