Mzawaonline

Mzawaonline Ukurasa Rasmi wa Mzawa Online

12/10/2025

Check out mzawaonline’s video.

06/10/2025

Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Mwanza wakiwemo mama lishe na baba lishe, wafanyabiashara ndogo ndogo pamoja na maafisa usafirishaji abiria kwa kutumia pikipiki na bajaji, wamemkaribisha jijini Mwanza mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakiahidi kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono kwenye kampeni zake na kumpa kura za kishindo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Kwa nyakati tofauti leo, Jumatatu Oktoba 6, 2025, wananchi hao wamemshukuru pia mgombea huyo kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi chake cha kwanza cha awamu ya sita, wakiitaja kwa uchache mazingira bora ya ufanyaji biashara kwa wafanyabiashara wadogo pamoja na ujenzi wa masoko na miundombinu ya usafiri na usafirishaji.

“Dkt. Samia Suluhu Hassan ni mama mwenye upendo na utu kwa wananchi wake. Tumeona hata katika mkoa wetu huu wa Mwanza ametusaidia mambo mbalimbali kwenye jamii. Hata machinga sasa hatusumbuliwi kwa kufukuzwa barabarani.”

Dkt. Samia, ambaye ameshafanya mikutano 77 katika mikoa 21 ya Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar, anatarajiwa kuanza awamu yake nyingine ya kampeni kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa kesho, Jumanne Oktoba 7, 2025, akitarajiwa kuanza kampeni zake katika mkoa wa Mwanza kabla ya baadaye kuelekea kwenye mikoa ya Geita, Shinyanga, Simiyu, Mara na Kagera, akinadi sera na ilani ya chama chake pamoja na kueleza mafanikio yaliyopatikana katika serikali yake.

06/10/2025

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Warioba Butiku, amewahimiza Watanzania kuungana na kauli rasmi iliyotolewa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) dhidi ya kulihusisha jeshi hilo na siasa, akiwaomba kusimama na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mzee Butiku ameyasema hayo leo Jumapili, Oktoba 5, 2025, mbele ya waandishi wa habari mkoani Mara, akirejea historia ya utumishi wake katika siasa, serikalini na jeshini, akimkana mwananchi aliyetumia mtandao wa kijamii kujitambulisha k**a afisa wa jeshi na kueleza kuwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania halijawahi kuwa na afisa asiyekuwa na nidhamu kwa kiwango alichoonesha mtu huyo aliyejiita Kepteni Tesha.

“Mimi nimepita jeshini, hatuna uniform ile, kwamba uwe Tanga kwenye joto halafu uvae uniform mpaka shingoni. Kwa hiyo yule si askari, na k**a ni askari, analo jeshi lake lingine, siyo Jeshi la Wananchi wa Tanzania, na sipendi kuamini wala siamini kwamba ndani ya jeshi letu tuna watu wa aina hiyo. Jeshi letu ni jeshi la Watanzania, linaongozwa na Rais wetu na Mkuu wa Majeshi, na kauli halali zinatoka kule,” amesema Mzee Butiku.

Katika hatua nyingine, Mzee Butiku amewasihi Watanzania kupuuza taarifa zisizotolewa na viongozi ama mamlaka rasmi, hususan wakati huu wa Uchaguzi Mkuu, akisisitiza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania ni suala la kikatiba, hivyo ni lazima ufanyike kwa kuzingatia sheria na katiba k**a zinavyoeleza.

Aidha, Mzee Butiku amewaeleza Watanzania kuwa ni muhimu kukubaliana kwa pamoja na kuyakataa masuala ya kulihusisha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na masuala ya siasa, kampeni na Uchaguzi Mkuu, akihimiza kila mmoja kufuata katiba na sheria k**a zinavyotaka, na kuungana pamoja kukemea jitihada za kutaka kuliingiza jeshi hilo kwenye masuala hayo, kwani si utamaduni wala desturi ya Watanzania.

05/10/2025

Mgombea ubunge wa jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Prof. Kitila Alexander Mkumbo, amewaomba wananchi wa kata ya Mburahati wampe ridhaa ya kuendelea kuongoza jimbo hilo ili aweze kuendelea kuboresha barabara na miundombinu ya kata hiyo.

Akizungumza na wakazi wa kata hiyo, Oktoba 6, 2025, Prof. Kitila alisema barabara ya Mabibo hadi Mburahati ni muhimu kwa maendeleo ya eneo hilo na ameahidi barabara hiyo kujekwa kwa kiwango cha lami, ili kurahisisha usafirishaji na maisha ya wananchi.

Aidha, amebainisha kuwa barabara ya pili, ikianzia mtaa wa Barafu hadi Magomeni, tayari imeingizwa kwenye mradi wa DMDP na inatafuta wakandarasi wa ujenzi. Prof. Kitila aliongeza kuwa ofisi ya Rais, TAMISEMI, na mwandisi wa mradi wa DMDP tayari wamekubaliana kuingiza barabara hiyo kwenye mradi, huku tangazo la kupata wakandarasi limeanza.


Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Ila...
05/10/2025

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Ilani anayoinadi ya 2025/30 ameahidi kuchochea mapinduzi ya uchumi wa kisasa, fungamanishi, jumuishi na shindani utakaojengwa katika msingi wa kuongeza thamani ya rasilimali zinazozalishwa nchini.

Dkt. Samia ambaye amehitimisha kampeni zake kwenye mikoa ya Kanda ya Kaskazini, akitarajiwa kuanza kampeni Kanda ya Ziwa, akianzia na Mwanza Oktoba 07, 2025, ameeleza kuwa lengo ni kuimarisha ukuaji jumuishi wa uchumi na kukuza uchumi kwa wastani kwa mwaka kufikia asilimia 7 kutoka asilimia 5.6 iliyopo hivi sasa.

Ameahidi pia kutekeleza mpango wake wa kuanzisha mfuko maalum wa kuwezesha upatikanaji wa mitaji, hususani kwa wajasiriamali wa biashara ndogo, za kati na kampuni changa, mfuko utakaoanza na bilioni 200 ndani ya siku zake 100 za awali madarakani, kiwango ambacho kitaongezeka kadiri ya marejesho ya fedha hizo yatakavyokuwa.

“Tutaongeza pia miundombinu ya umwagiliaji itakayoongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji, kuimarisha upatikanaji wa mbegu bora na kwa bei nafuu na kuendelea kutoa ruzuku za mbolea na pembejeo, kuanzisha vituo vya ukodishaji zana za kilimo, tukitarajia pia kutoa matrekta 10,000 kwa mkopo,” amesisitiza Dkt. Samia katika mikutano yake.

Dkt. Samia pia ameahidi kuwezesha upatikanaji wa mitaji, mikopo na vifaa kwa wavuvi na wakuzaji viumbe maji, vyama vya ushirika na wawekezaji ikiwa ni sambamba na kuendeleza viwanda saba vya National Steel, Nachingwea Cashew Nuts, Mafuta Ilulu, TPL Mbeya, TPL Shinyanga, Sawmill pamoja na kiwanda cha Mwanza Tannery.

Katika sekta ya uzalishaji kuelekea mwaka 2030, Dkt. Samia ameahidi kuongeza sekta ya uzalishaji viwandani kufikia asilimia 9 kwa mwaka 2030, kufanya tafiti zaidi za maeneo yenye madini na kuongeza eneo lililopimwa ili kukuza sekta hiyo kutoka asilimia 16 ya sasa hadi kufikia asilimia 50 mwaka 2030, akiahidi pia kuifanya Tanzania kuwa kituo cha uuzaji wa madini katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati pamoja na kuimarisha masoko ya madini na vito ikiwemo Tanzanite kwa kujenga jengo la Tanzanite Exchange Centre katika eneo la Mirerani, Simanjiro.

Meneja wa TARURA Wilaya ya Rufiji, Mhandisi Nicolaus Ludigery, amesema kwamba miradi yote inayotekelezwa katika Wilaya y...
05/10/2025

Meneja wa TARURA Wilaya ya Rufiji, Mhandisi Nicolaus Ludigery, amesema kwamba miradi yote inayotekelezwa katika Wilaya ya Rufiji inaenda kuwarahisishia wananchi shughuli za kijamii na kiuchumi.

Amesema barabara nyingi zilipata athari kubwa kutokana na mafuriko na kimbunga Hidaya, hivyo wamejipanga kuhakikisha miradi yote inakamilika k**a ilivyokusudiwa.

Naye Bi. Saida Mwilu, mkazi wa Ikwiriri, amesema ujenzi wa barabara za lami katika mji wa Ikwiriri ume waletea manufaa makubwa, hususani kwa wajasiriamali ambao hutembeza bidhaa zao mitaani, kwani awali kipindi cha mvua kulikuwa na madimbwi ya maji, na kuongeza kwamba taa za barabarani zitakapowekwa zitawasaidia kufanya biashara hadi usiku kwa usalama.

Pia Bw. Malik Kitala, mwendesha bodaboda, ameishukuru Serikali kwa kuwatengenezea barabara, kwani awali kutokana na ubovu wa barabara hasa kipindi cha mvua, nauli zilikuwa juu.

Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Luteni Kanali Fredrick Komba, ameipongeza Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kw...
05/10/2025

Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Luteni Kanali Fredrick Komba, ameipongeza Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa kurejesha mawasiliano ya miundombinu ya barabara katika wilaya yake.

Amesema Wilaya ya Rufiji kwa mwaka 2023/2024 ilipata mafuriko ambayo yaliathiri sana miundombinu ya barabara katika tarafa za Mohoro, Ikwiriri pamoja na Mkongo.

“TARURA imeweza kufanya kazi nzuri kwa nafasi yake kwani kwa muda mfupi imeweza kurekebisha hitilafu zilizotokana na mafuriko.”

Akitolea mfano, Luteni Kanali Komba amesema TARURA imejenga barabara mpya za lami na daraja la Mohoro lenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 17, ambalo linaunganisha vijiji vya Ndundutawa na King’ongo, vinavyounganisha Makao Makuu ya Tarafa ya Mohoro na kijiji cha Kipoka katika Kata ya Chumbi.

“Naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutekeleza miradi mingi ya TARURA katika Wilaya ya Rufiji.”

“Mimi na wananchi tunaweza kusafiri mahali popote katika wilaya hii; ujenzi wa miundombinu umeleta matumaini makubwa kwa wananchi wa Rufiji,” ameongeza.

Amesema Serikali imeonesha dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi kwa kuhakikisha miundombinu ya barabara inakuwa thabiti na wananchi wanaweza kusafirisha mazao yao.

05/10/2025

Mgombea ubunge wa Jimbo la Kibamba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Angella Kairuki, amewahakikishia wakazi wa Kata ya Saranga kuwa kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, atatekeleza miradi zaidi ya sita ya barabara na miundombinu, inayolenga kuboresha usafirishaji na huduma za kijamii katika maeneo yao.

Akizungumza na wananchi katika mkutano uliofanyika Mtaa wa Stopover leo Oktoba 4, 2025, Kairuki alisema miradi hiyo itajumuisha ujenzi na ukarabati wa barabara za King’ong’o, Kibanda cha Mkaa, Kimara Matangini kupitia DAWASA, Vijana Ndumbi, S**a, na Ukombozi, bila kusahau barabara ya Temboni kwenda KKKT, Temboni Matosa, ambazo ni mbovu na zinahitaji barabara ya zege.

Aidha, Kairuki alisema atafuatilia utekelezaji wa mradi wa DMDP 2 unaohusisha barabara ya Temboni, Saranga, Kinyerezi, ambapo kazi ilianza na mkandarasi lakini kumekuwa na kusuasua katika utekelezaji. Pia alisisitiza umuhimu wa barabara ya kilomita sita ya S**a Golani, Saranga Upendo, kiunganishi muhimu kati ya mitaa minne ya kata hiyo na maeneo ya jirani.

04/10/2025

Mgombea ubunge wa Jimbo la Kibamba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Angella Kairuki, ameahidi kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji katika Kata ya Saranga endapo atapewa ridhaa na wananchi katika uchaguzi ujao.

Akizungumza na wakazi wa Mtaa wa Stopover leo Oktoba 4, 2025, jijini Dar es Salaam, Kairuki amesema kuwa kuna miradi takribani minne ya maji itakayotekelezwa, ikiwemo mradi wa Saranga Mkombozi Water Supply Project, unaotarajiwa kunufaisha zaidi wakazi wa maeneo ya Kwampapura kwa Mbuguli na Ukombozi.

Aidha, ametaja miradi mingine ikiwemo Kimara B (King’ong’o Zone Project), Chati King’ong’o Project, na S**a Zone Project, ambayo itanufaisha wakazi wa Stopover, Mpakani, na Mashujaa.

Kairuki amesema kazi kubwa itakayofanywa na Chama Cha Mapinduzi baada ya kupewa ridhaa ni kuimarisha mgawanyo wa maji katika mabomba makubwa na kuendelea kupanua mtandao wa usambazaji maji ili kukidhi mahitaji ya wakazi wapatao 145,974 wa Kata ya Saranga.

19/09/2025

Mgombea ubunge wa Jimbo la Kisarawe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Seleman Jafo, ameahidi kuwa endapo ataendelea kupewa ridhaa ya kuwatumikia wananchi katika kipindi cha miaka mitano ijayo, atahakikisha kunakuwepo na mikopo yenye tija kwa wanawake na vijana, pamoja na kuanzisha viwanda vidogo vidogo vitakavyoongeza ajira na thamani ya mazao.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chakenge, Kata ya Mzenga, Dkt. Jafo alisema katika kipindi kilichopita kulikuwa na changamoto katika utoaji wa mikopo, kwani baadhi ya maeneo walitumia vibaya fedha hizo, hali iliyosababisha serikali kusitisha na kuweka utaratibu mpya unaolenga kuhakikisha mikopo inaleta manufaa yaliyokusudiwa.

Aidha, Dkt. Jafo alieleza kuwa tayari wamefanikiwa kujenga kiwanda cha korosho, ambacho kinatarajiwa kutoa ajira kwa vijana na kuongeza thamani ya zao hilo muhimu katika wilaya ya Kisarawe.

17/09/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan amewatoa wasiwasi Watanzania akiwahakikishia kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kikamilifu katika kuilinda Tanzania na kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na salama.

Dkt. Samia akirejea ahadi yake wakati anajitambulisha kwa Watanzania mara baada ya Chama chake kumpa ridhaa ya kuwania nafasi ya Urais, akiwa mwanamke wa kwanza kupewa nafasi hiyo katika Historia ya Chama hicho, amesema amelazimika kuyasema hayo mara baada ya Wazee wa Pemba kumuomba kusimamia amani na utulivu katika uchaguzi huo Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

"Tunakwenda kwenye uchaguzi Mkuu, ninaowaomba sana twende tudumishe amani na utulivu. Uchaguzi si vita, uchaguzi ni tendo la kidemokrasia ni watu kwenda kwenye utaratibu uliowekwa, kuweka kura zetu, rudi nyumbani katulie ili nchi ibaki salama. Si muda wote kushika silaha kunaleta suluhu ya maana, niwaombe sana ndugu zangu amani na utulivu wa nchi yetu ni jambo muhimu kuliko jambo lolote. Hutaki kishindo kapige kura rudi nyumbani tulia." Amesema Dkt. Samia.

Dkt. Samia yupo Visiwani Zanzibar kwenye ziara zake za Kampeni, ambapo awali pia amesisitiza kuwa ikiwa Watanzania watampa ridhaa ya kuongoza serikali atahakikisha pia analinda kwa bidii zake zote tunu za Taifa ambazo ni amani, umoja na mshik**ano k**a sehemu ya kuenzi jitihada zilizofanywa na waasisi wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Amani Abeid Karume.

04/09/2025

Wakazi wa Kigoma waaswa kuunga mkono jitihada za Serikali katika utunzaji wa mazingira kwa kutumia nishati safi na salama ya kupikia

Wito huo umetolewa leo Septemba 04, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Simon Nyakoro Sirro wakati akipokea mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu unaosimamiwa na kuratibiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) .

"Kinachofanyika leo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za matumizi ya nishati safi na salama katika kutunza mazingira na kuboresha Afya za wananchi" amesema Mkuu wa mkoa Mhe. Sirro, alipokuwa akipokea mradi huo.

Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa mkuu wa mkoa, Mhandisi wa Miradi kutoka wakala wa Nishati Vijijini (REA), Raya Majallah amesema,

“Mradi huu unalenga kusambaza majiko banifu ili kukuza upatikanaji wa Nishati safi na endelevu, kupanua usambazaji wa Nishati mbadala katika maeneo ya vijijini na hivyo kuhamasisha matumizi ya teknolojia safi kupitia teknolojia za kisasa na bora za kupikia.

Katika kufanikisha hilo, Wakala wa Nishati Vijijini umekuja na mpango wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku.

Mradi huu unagharimu kiasi cha zaidi ya TZS 429.5 ambapo serikali itatoa ruzuku ya TZS 365.1 na kufanikisha usambazaji na uuzaji wa majiko 8,424.

Uuzaji na usambazaji wa majiko banifu utafanyika katika wilaya Sita (6) za mkoa wa Kigoma ambazo ni wilaya ya Buhingwe, Kakonko, Kasulu, Kibondo, Kigoma Vijijini na wilaya ya Uvinza na kila wilaya kupata majiko 1,404.

Mikataba ya mradi huu ilisainiwa tarehe 09 Mei, 2025 kati ya REA na mtoa huduma kampuni ya Envotec Services Limited. Mtoa huduma atazambaza na kuuza majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika wilaya zote Sita.

Gharama ya jiko moja ni TZS 50,990 lakini serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85 sawa na TZS 43,341.50 na hivyo mwananchi atanunua jiko kwa kiasi cha TZS 7,649 tu.

Kwa upande wake Afisa masoko wa Kampuni ya Envotec Services Limited, Bi Kisa Sefa Mwamwaja amesema, majiko haya banifu yametengenezwa kwa kutumia Teknolojia za kisasa ambazo hazihitaji matumizi makubwa ya kuni na mkaa wakati wa kupika na hivyo kusaidia katika utunzaji wa mazingira.

Address

Kimara S**a
Dar Es Salaam
1615

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mzawaonline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share