Kijiweni

Kijiweni Mtaa Unaongea
(1)

Baada ya Vijana wa Miguel Gamondi, Singida Black Stars kupata ushindi ugenini wa bao 1-0 katika uwanja wa Kigali Pele, l...
27/09/2025

Baada ya Vijana wa Miguel Gamondi, Singida Black Stars kupata ushindi ugenini wa bao 1-0 katika uwanja wa Kigali Pele, leo wanaikaribisha Rayon Sports kwenye Uwanja wa Azam Complex kusaka rekodi ya kufuzu hatua inayofuata.

Kutwaa Kombe la Kagame 2025, kisha kushinda mechi mbili mfululizo za kimashindano bila ya kuruhusu bao, kinaifanya Singida BS kuwa na matumaini ya kufanya vizuri leo.

Ukiachana na ushindi wa 1-0 kule Rwanda, Singida B ilikuja kupata matokeo k**a hayo mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara dhidi ya KMC, Jumanne iliyopita.

Gamondi kuna rekodi anaifukuzia, baada ya kuipeleka Yanga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara mbili mfululizo 2023-2024 ikiwa ni mara ya kwanza baada ya miaka 25 huku timu ikifika hadi robo fainali na msimu wa 2024-2025, safari hii ana kikosi cha Singida BS kinachoshiriki kimataifa kwa mara ya kwanza.

Mshindi wa jumla kati ya Singida BS dhidi ya Rayon anacheza dhidi ya mshindi kati ya Flambeau du Centre ya Burundi na Al Akhdar ya Libya katika hatua nyingine ya mtoano kuwania kufuzu makundi.

Baada ya ushindi wa mabao 3-0 ilioupata Yanga kule Angola katika mechi ya kwanza, ni mtaji mkubwa kwao kuekelea mchezo W...
27/09/2025

Baada ya ushindi wa mabao 3-0 ilioupata Yanga kule Angola katika mechi ya kwanza, ni mtaji mkubwa kwao kuekelea mchezo Wa leo wa marudiano katika uwanja wa Benjamin Mkapa huku Wananchi wakibebwa na rekodi dhidi ya Waangola.

Ukiachana na kuweka rekodi mpya ya kushinda nchini humo katika michuano ya CAF, Yanga haijawahi kutolewa na timu kutoka Angola na wala haijapata hata sare achana na kupoteza ikiwa nyumbani dhidi yao.

Rekodi zinaonesha mwaka 2007, Yanga ilicheza dhidi ya Petro De Luanda katika Ligi ya Mabingwa Afrika na kushinda kwa jumla ya mabao 3-2. Mchezo wa kwanza ugenini ilifungwa mabao 2-0, nyumbani ikashinda 3-0.

Pia mwaka 2016 Yanga ilicheza dhidi ya Sagrada Esperansa na kuitoa kwa jumla ya mabao 2-1 kwenye Kombe la Shirikisho Afrika. Mechi ya nyumbani ilishinda mabao 2-0, ugenini ikapoteza kwa bao 1-0.

Safari hii Yanga imeanza na ushindi ugenini, zimebaki dakika tisini za nyumbani kukamilisha hesabu za kwanza kuelekea makundi.

Raphinha na Joan García wa Barcelona Kukosa Mechi Dhidi ya PSG kwa Sababu ya MajeruhiKlabu ya FC Barcelona imethibitisha...
26/09/2025

Raphinha na Joan García wa Barcelona Kukosa Mechi Dhidi ya PSG kwa Sababu ya Majeruhi

Klabu ya FC Barcelona imethibitisha kuwa winga Raphinha amepata majeraha ya msuli wa paja la kulia wakati wa mchezo wa Copa del Rey dhidi ya Real Oviedo, hali itakayomfanya awe nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu.

Kwa upande mwingine, kipa Joan García alivunjika nyuzi za goti la kushoto (meniscus) katika mchezo huo huo na atafanyiwa upasuaji, huku muda wa kupona ukikadiriwa kuwa kati ya wiki nne hadi sita.

Wachezaji hao wote watakosa mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris Saint-Germain utakaopigwa Oktoba 1 katika Uwanja wa Spotify Camp Nou, jambo linaloongeza changamoto za majeruhi kwa kocha Hansi Flick.

MABAHARIA wa visiwani Zanzibar, KMKM imekuwa timu ya kwanza ya Tanzania msimu huu kutinga raundi ya pili ya michuano ya ...
26/09/2025

MABAHARIA wa visiwani Zanzibar, KMKM imekuwa timu ya kwanza ya Tanzania msimu huu kutinga raundi ya pili ya michuano ya kimataifa inayosimamiwa na CAF baada ya jioni hii kuifyatua kwa mara nyingine AS Port ya Djibouti kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa New Amaan, Unguja.

KMKM ambao ni mabingwa wa Kombe la Shirikisho Zanzibar na Ngao ya Jamii, imefuzu kwa ushindi wa jumla ya mabao 4-2 kwani katika mechi ya kwanza iliyopigwa pia uwanjani hapo wikiendi iliyopita, wenyeji wakiwa AS Port ilishinda pia 2-1.

Matokeo ya mechi ya ugenini iliwapa nguvu mabaharia hao ambao leo waliendelea kuonyesha wamepania kuweka historia ya kuwa timu ya kwanza ya visiwani hapa kufika mbali katika michuano ya CAF ikitaka kurejea rekodi zilizowahi kuwekwa na Malindi miaka ya 1990.

“Vita ya jezi feki ni vita ngumu, sio vita rahisi. Mzigo wetu wa msimu huu tulioleta umeisha lakini cha ajabu bado tunap...
26/09/2025

“Vita ya jezi feki ni vita ngumu, sio vita rahisi. Mzigo wetu wa msimu huu tulioleta umeisha lakini cha ajabu bado tunapewa taarifa kuwa mizigo mikubwa bado inaendelea kuingia nchini ya jezi za Yanga ambayo sio ya Mdhamini wetu GSM.

"Tumekuja na mpango tofauti wa kupambana na JEZI feki sana na ninaamini itakomesha hii tabia ya jezi feki. Tunazindua leo jezi toleo la pili ambayo tofauti ni mzalishaji mpya wa jezi na kitambaa pia kipo tofauti”

Tumekuwa tukiwanufaisha watu kwa kuuza jezi feki ambazo washabiki wetu huwa ni ngumu kutofautisha Kati ya jezi feki na original, tunaamini kwa toleo hili itakuwa ni solution kubwa sana kwa tatizo hili ambalo limekuwa sugu.”

Klabu haiwezi kuendelea kupoteza mapato, hii vita safari hii tumedhamiria kupambana nayo kwa akili kubwa. Niwapongeze sana Viongozi wetu kwa kuja na suluhisho hili ambalo Mwananchi ili kusapoti suluhisho hili ni wewe kununua jezi hizi mpya kwa wingi na kesho tuzivae pale kwa Mkapa. Jezi hizi zitapatikana Jangwani na maduka yote ya GSM kwa shilingi 40,000 tu.

“Jezi zote kwa bei ya jumla zitapatikana dukani kwa Sandaland The Only one”

Meneja Habari Na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga Ally Kamwe.

“Tunafahamu ya kwamba tuna mechi ya Ligi ya Mabingwa siku ya Jumapili kwenye dimba la Mkapa kuanzia saa 10 jioni na taya...
26/09/2025

“Tunafahamu ya kwamba tuna mechi ya Ligi ya Mabingwa siku ya Jumapili kwenye dimba la Mkapa kuanzia saa 10 jioni na tayari wageni wetu Gaborone United wamewasili alfajiri ya leo. Mambo yote yamekwenda vizuri na watafanya mazoezi leo na kesho.”

“Mchezo wetu wa Jumapili utachezeshwa na waamuzi kutoka nchini Niger na sasa wapo njiani. Kikosi kiliingia kambini jana baada ya mchezo dhidi ya Fountain Gate walirudi kambini na wapo timamu, hakuna mtu yeyote ambaye alipata majeraha. Watakaokosa mchezo ni Mohammed Bajaber na Abdulrazak Hamza.”

“Nipo hapa kuwathibitishia kwamba mechi yetu ya Jumapili haitakuwa na mashabiki kutumikia adhabu ya CAF. Kilichosababisha ni mchezo ni dhidi ya Al Masry, kuna shabiki aliingia uwanjani na kuna mashabiki waliwasha moto. Adhabu hiyo inakwenda pamoja na faini ya Dola 50,000 k**a Tsh. 120 milioni hivi.”

“Niwaase mashabiki wenzangu wa Simba, uache vitendo vya vurugu uwanjani. Kwanza tuanze ulinzi wa wenyewe kwa wenyewe ukiona mtu anataka kuwasha zile fire works mzuie, ukiona mtu anataka kuingia uwanjani tushirikiane kumzuia ikiwezekana kumtoa uwanjani. Angalia mechi k**a hii tunakwenda uwanjani bila mashabiki. Hatupo hapa kulaumiana ila kukumbushana.”

“Hasara ya kwanza tunakosa mashabiki, hasara ya pili tunakosa mapato na hasara ya tatu tunalipa faini ya USD 50,000. Vilevile tumepewa adhabu kutokana na mechi ya fainaili dhidi ya RS Berkane, huku vilevile tuliwasha fireworks. Kwenye mechi ya fainali tumetozwa faini ya USD 35,000. Jumla Tumetoshwa USD 85,000 sawa na Tsh. 200 milioni.”

“Tunacheza bila mashabiki kwenye mechi dhidi ya Gaborone United pekee lakini sbaabu tumefanya makosa mfululizo CAF watakuwa makini na sisi kwelikweli sababu wanaona tunafanya vitendo ambavyo sio vya kiungwana hivyo watakuwa wanaangalia k**a Simba Sports Club tumebadilika. Ni lazima tuwe makini kwelikweli ili kuwaonyesha kwamba tumejifunza na tumebadilika. Kuanzia hivi sasa tuchukue taswira mpya kwenye eneo la ushabiki.”

“Wapo mashabiki ambao wametaka kuwa sehemu ya maumivu ambayo tunapitia Klabu ya Simba na maumivu yenyewe ni faini ya Tsh. 212,500,000 sawa na USD 85,000. Kwa mapenzi yao mashabiki wameomba kuchangia faini ili kuipunguzia klabu mzigo na sisi tumepokea na tumeridhia mashabiki wachangie hususani kwenye eneo la faini.”- Semaji Ahmed Ally.

Sergio Busquets Atangaza Kustaafu Baada ya Miaka 20 ya Kichezaji FC Barcelona na Inter Miami ⚽🇪🇸Kiungo mkongwe wa Hispan...
26/09/2025

Sergio Busquets Atangaza Kustaafu Baada ya Miaka 20 ya Kichezaji FC Barcelona na Inter Miami ⚽🇪🇸

Kiungo mkongwe wa Hispania, Sergio Busquets mwenye umri wa miaka 37, ametangaza kustaafu soka kupitia video aliyochapisha kwenye mtandao wa Instagram, akibainisha kuwa miezi yake ya mwisho ya kucheza itakuwa na klabu ya Inter Miami CF inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka Marekani (MLS).

Busquets alianza safari yake kubwa ya soka mwaka 2008 akiwa FC Barcelona, ambapo alicheza jumla ya michezo 722, akitwaa mataji 9 ya La Liga na vikombe 3 vya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Pia amechezea timu ya taifa ya Hispania michezo 143, akiwemo kwenye kikosi kilichoshinda Kombe la Dunia mwaka 2010.

Tangu ajiunge na Inter Miami mwaka 2023, Busquets amecheza zaidi ya michezo 60 na kusaidia klabu hiyo kutwaa taji la Leagues Cup mwaka 2023. Mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa hatua ya mtoano ya msimu wa 2025. 🏆✨

Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Billy Vigar, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 21 baada ya kupata jeraha kubwa l...
26/09/2025

Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Billy Vigar, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 21 baada ya kupata jeraha kubwa la ubongo wakati akiichezea Chichester City.

Vigar aliwekwa kwenye coma ya kulazimishwa baada ya kujeruhiwa katika mchezo wa Ligi ya Isthmian Premier Division dhidi ya Wingate and Finchley Jumamosi.

Taarifa kutoka kwa familia ya Vigar imesema:
"Baada ya kupata jeraha kubwa la ubongo Jumamosi iliyopita, Billy Vigar aliwekwa kwenye coma ya kulazimishwa. Jumanne alihitaji kufanyiwa upasuaji ili kusaidia nafasi yoyote ya kupona. Ingawa hatua hiyo ilisaidia, jeraha hilo lilikuwa kubwa mno kwake na alifariki Alhamisi asubuhi."

WANANCHI watacheza mchezo wa marudiano wa hatua ya awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete SC Jumamosi hii kwe...
26/09/2025

WANANCHI watacheza mchezo wa marudiano wa hatua ya awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete SC Jumamosi hii kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.

Yanga SC itaingia uwanjani ikiwa na faida ya ushindi wa mabao 3-0 waliyopata katika mchezo wa ugenini mabao yakifungwa na Aziz Andambwile aliyefungua ukurasa katika anga la kimataifa, Edmund John na Prince Dube.

Ali Kamwe ambae ni Afisa Habari wa klabu ya Yanga ameweka wazi kuwa mwisho wa mchezo wa ugenini ni mwanzo wa maandalizi kuelekea katika mchezo ujao wa kimataifa hivyo wapo tayari.

“Ushindi wetu ugenini haina maana kwamba kazi imekwisha bado tutaendelea kufanya maandalizi na malengo ni kuona kwamba tunavuka hii hatua tupo tayari na mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi.”
Yanga SC imetoka kucheza mchezo wa ufunguzi wa ligi dhidi ya Pamba Jiji ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 Septemba 24 2025, Septemba 27 2025 itakuwa kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

MEDALI YA MBIO ZA DUNIA YAMPANDISHA CHEO SIMBU JESHINI BINGWA wa Dunia wa Mbio Ndefu, Alphonce Felix Simbu amepandishwa ...
26/09/2025

MEDALI YA MBIO ZA DUNIA YAMPANDISHA CHEO SIMBU JESHINI

BINGWA wa Dunia wa Mbio Ndefu, Alphonce Felix Simbu amepandishwa cheo Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kutoka Sajini (Sargeant) hadi Sajini Taji (Staff Sargeant).

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini, Jenerali Jacob John Mkunda amempandisha cheo Simbu leo baada ya kumaliza nafasi ya kwanza kwenye Mashindano ya Dunia ya Riadha Septemba 15 Jijini Tokyo nchini Japan — na kuweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kushinda Medali ya Dhahabu katika Marathon kwenye mashindano hayo.

Simbu alimaliza nafasi ya kwanza kishujaa akitumia muda wa Saa 2:09:48 na kumshinda mpinzani wake, Amanol Petros wa Ujerumani kwa tofauti ya sekunde 0.03.
Iliass Aouani wa Italia aliambulia Medali ya Shaba baada ya kumaliza nafasi ya tatu akitumia muda wa Saa 2:09:53 katika Mbio iliyohusisha wakimbiaji wengine nyota duniani k**a Haimro Alame wa Israel aliyemaliza nafasi ya nne akitumia Saa 2:10:03 na Abel Chelangat wa Uganda nafasi ya tano Saa 2:10:11 na Emile Cairess wa Uingereza.

Simbu anaongeza Medali hiyo ya Dhahabu kwenye Shaba aliyoshinda London mwaka 2017 na pia huu ukiwa mwaka mzuri kwake baada ya kumaliza nafasi ya pili pia katika mbio za Boston Marathon 2025 mwezi Aprili.

Kufuatia Uwanja wa Manungu Complex uliopo Morogoro kutokukidhi vigezo vinavyotakiwa ili utumike kwenye michezo ya Ligi K...
26/09/2025

Kufuatia Uwanja wa Manungu Complex uliopo Morogoro kutokukidhi vigezo vinavyotakiwa ili utumike kwenye michezo ya Ligi Kuu Bara, Mtibwa Sugar imeuchagua Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kwa mechi za nyumbani za Ligi Kuu Bara.

Mtibwa Sugar iliyorejea Ligi Kuu Bara msimu huu, imeanza kwa kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Mashujaa ikiwa ugenini.

Timu hiyo baada ya kupoteza mechi ya kwanza, sasa itaikaribisha Fountain Gate, Septemba 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Taarifa ya Mtibwa Sugar imesema: "Mchezo wetu unaofuata wa Ligi Kuu tunacheza dhidi ya Fountain Gate. Mchezo utachezwa Jumapili ya tarehe 28 saa 10:00 jioni uwanja wa Jamhuri Dodoma.

"Huu mchezo sisi ndio wenyeji na tumelazimika kupeleka Dodoma sababu ya marekebisho ya Uwanja wa Manungu ambao utakamilika hivi karibuni."

NBCPL 25/26➡️ Mchezo Umemalizika Simba SC 3⃣Fountain Gate FC 0⃣ ⚽ De Reuck⚽ Ahoua⚽ Sowah
25/09/2025

NBCPL 25/26

➡️ Mchezo Umemalizika

Simba SC 3⃣
Fountain Gate FC 0⃣

⚽ De Reuck
⚽ Ahoua
⚽ Sowah

Address

Rose Garden Road
Dar Es Salaam
00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kijiweni posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share