Kijiweni

Kijiweni Mtaa Unaongea, Njoo tuzungumze kuhusu Betting, Forex, Tech na michongo ya town.
(1)

Neo Maema  amejiunga na klabu ya Simba  k**a mchezaji huru baada ya kuachana na Mamelodi Sundowns .Umeuonaje Usajili Huu...
21/08/2025

Neo Maema amejiunga na klabu ya Simba k**a mchezaji huru baada ya kuachana na Mamelodi Sundowns .

Umeuonaje Usajili Huu? Na Unadhani Utakua Msimu Wa Aina Gani Kwa Klabu Ya Simba?

Klabu ya Yanga SC imekamilisha usajili wa mkopo wa mwaka mmoja beki wa Kimataifa wa Ghana 🇬🇭,  Frank Assinki akitokea Si...
21/08/2025

Klabu ya Yanga SC imekamilisha usajili wa mkopo wa mwaka mmoja beki wa Kimataifa wa Ghana 🇬🇭, Frank Assinki akitokea Singida Black Stars.

Klabu ya Azam FC imeachana rasmi na kipa wake raia wa Sudan, Mohamed Mustafa, baada ya kufikia makubaliano ya pande zote...
21/08/2025

Klabu ya Azam FC imeachana rasmi na kipa wake raia wa Sudan, Mohamed Mustafa, baada ya kufikia makubaliano ya pande zote mbili.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Azam FC imetoa ujumbe maalumu kuthibitisha kuachana huko, ikibainisha kuwa uhusiano huo umehitimishwa kwa amani na kwa heshima baina ya pande zote.

Mustafa, ambaye alijiunga na Azam FC akitokea soka la Sudan, amehudumu klabuni hapo katika kipindi ambacho kilionekana kuwa cha mabadiliko kwenye safu ya ulinzi wa lango la timu hiyo.

Kwa sasa Azam FC inaendelea na maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa mashindano, huku safari ya Mustafa ikibakia kuwa sehemu ya historia ya klabu hiyo ya Chamazi.

Mshambuliaji wa Kibrazil, Lucas Ribeiro Costa, amewasilisha barua yake ya kuvunja mkataba kwa klabu ya Mamelodi Sundowns...
21/08/2025

Mshambuliaji wa Kibrazil, Lucas Ribeiro Costa, amewasilisha barua yake ya kuvunja mkataba kwa klabu ya Mamelodi Sundowns na kupeleka suala hilo katika Mahak**a ya Usuluhishi wa Soka ya FIFA.

Ribeiro alivutia mashabiki wengi kufuatia kiwango chake bora katika Kombe la Dunia la Klabu la FIFA 2025. Mchezaji huyo wa Kibrazil alipata sifa kubwa baada ya kufunga bao bora zaidi la mashindano hayo jambo lililoongeza hadhi yake katika soka la kimataifa.

Baada ya kuondoka ghafla katika kambi ya maandalizi ya msimu mpya ya Sundowns, Ribeiro amewasilisha suala hilo kwenye Mahak**a ya Usuluhishi wa FIFA akiomba maamuzi kuhusu athari za kuvunja mkataba huo. Anasisitiza kuwa ametenda ndani ya haki zake.

“Ninaamini nina sababu ya msingi ya kuvunja mkataba wangu na Mamelodi Sundowns FC, jambo nitakalolieleza mbele ya Mahak**a ya Usuluhishi wa FIFA,” Ribeiro alisema katika taarifa yake.

Mchezaji huyo anaendelea kuwa na matumaini kwamba maamuzi ya kisheria ya hivi karibuni, hususan kesi ya kihistoria ya Lassana Diarra iliyotolewa na Mahak**a ya Haki ya Umoja wa Ulaya (CJEU), yataimarisha msimamo wake na kumruhusu kuendeleza kazi yake ya soka bila vizuizi.

Kati ya nafasi zote za uwanjani  kipa, mabeki, viungo na washambuliaji , ni ipi unadhani huwa na mazoezi magumu zaidi na...
21/08/2025

Kati ya nafasi zote za uwanjani kipa, mabeki, viungo na washambuliaji , ni ipi unadhani huwa na mazoezi magumu zaidi na kwa nini?”

Mwamuzi wa Kimataifa wa Mauritania,Dahane Beida ndiye atakayekuwa kwenye chumba cha VAR kwenye mchezo kati Tanzania dhid...
21/08/2025

Mwamuzi wa Kimataifa wa Mauritania,Dahane Beida ndiye atakayekuwa kwenye chumba cha VAR kwenye mchezo kati Tanzania dhidi ya Morocco hapo kesho. Refa huyu ndiye aliyekataa goli la Yanga dhidi ya Mamelodi lakini pia alichezesha mchezo wa Simba dhidi ya RS Berkane.

Unadhani Utakua Mchezo Wa Aina Gani?

Baada ya hatua ya makundi ya Mashindano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) PAMOJA 2024 kukamilika, mbio za kuwania Kiatu cha Dh...
21/08/2025

Baada ya hatua ya makundi ya Mashindano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) PAMOJA 2024 kukamilika, mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu zimezidi kupamba moto wakati mashindano yakielekea robo fainali nchini Kenya, Tanzania na Uganda.

Kwenye orodha ya wafungaji bora wapo Thabiso Kutumela wa Afrika Kusini, Allan Okello wa Uganda, na Oussama Lamlioui wa Morocco — kila mmoja akiwa na mabao matatu.

Uwezo wao umeisukuma mbele timu zao na pia umeangaza hatua ya makundi kwa nyakati za umaliziaji wa kiwango cha juu.
Wenye Magoli Matatu :
⚽⚽⚽Thabiso Kutumela (South Africa – eliminated)
⚽⚽⚽Allan Okello (Uganda)
⚽⚽⚽Oussama Lamlioui (Morocco)

Wenye Magoli Mawili Ambao Bado Wapo Hatua ya Robo Fainali:
⚽⚽Lalaina Rafanomezantsoa (Madagascar)
⚽⚽Mohamed Hrimat (Morocco)
⚽⚽Soufiane Bayazid (Algeria)
⚽⚽Clement Mzize (Tanzania)
⚽⚽Austine Odhiambo (Kenya)
⚽⚽Ryan Ogam (Kenya)
⚽⚽Omer Ahmed Abdelraziq (Sudan)

SIMBA SC Wanapata ushindi wao wa pili baada ya kucheza michezo mitatu ya Pre Season huko Misri. Hii leo wamecheza dhidi ...
20/08/2025

SIMBA SC Wanapata ushindi wao wa pili baada ya kucheza michezo mitatu ya Pre Season huko Misri. Hii leo wamecheza dhidi ya Al Zulfi FC inayoshiriki Ligi daraja la kwanza Nchini Saudi Arabia.

FT: SIMBA SC 🇹🇿 1-0 🇸🇦 AL ZULFI FC
23’—⚽️ Jean Charles Ahoua (Free Kick)

Ukipewa Nafasi Ya Kusajili Mmoja Kati Ya Hawa Unamsajili Nani? 😃
20/08/2025

Ukipewa Nafasi Ya Kusajili Mmoja Kati Ya Hawa Unamsajili Nani? 😃

"Jezi ya msimu huu hakuna binadamu yeyote ambaye amewahi kuona jezi nzuri k**a hii, ni jezi kali vibaya mno, Diadora wen...
20/08/2025

"Jezi ya msimu huu hakuna binadamu yeyote ambaye amewahi kuona jezi nzuri k**a hii, ni jezi kali vibaya mno, Diadora wenyewe walikuwa hawaamini k**a hiyo jezi inakuja Afrika. Wanasimba wenzangu kila mmoja aandae Tsh. 45,000 ya kununua jezi yake."

"Msimu huu tuna jezi tatu ambazo zimetengezwa na JayRutty kwa kushirikiana na Diadora. Kwenye jezi kutakuwa na nembo ya JayRutty na Diadora Msimu huu kuanzia kwenye kudesign hadi kutengenezwa kazi yote imefanyika nchini Italia na tayari zimeshaanza kuwasili nchini Tanzania na tarehe 27/08/2025 zitazinduliwa."

"Mara baada ya uzinduzi huo, jezi za Simba zitaanza kuuzwa kwenye maduka yote ambayo yameshaweka pre order na wanasubiri mzigo wao. Wakati zoezi la uzinduzi linafanyika Super Dome, kwenye maduka muda huo huo watakuwa wanachukua mizigo yao kwenda kuwauzia Wanasimba. JayRutyy ameleta jezi nyingi kwelikweli, uwe Simba, usiwe Simba zinamtosha kila Mtanzania."

"Yeyote ambaye atahitaji kuhudhuria tukio hili la uzinduzi wa jezi na kuwa mtu wa kwanza kuona jezi ya Simba msimu huu atalipa Tsh. 250,000. Akishalipa hiyo fedha yote ambayo atapata ndani ya ukumbi ni juu yetu na baada ya hapo atapewa jezi zote tatu za msimu huu. Vyote hivyo atakabidhiwa hapo hapo ukumbini."

Msemaji wa Klabu ya Simba,Ahmed Ally.

Mchezo wa Ngao ya Jamii kwaajili ya ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara utafanyika Septemba 16, 2025 kwenye Uwanja ww Ben...
20/08/2025

Mchezo wa Ngao ya Jamii kwaajili ya ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara utafanyika Septemba 16, 2025 kwenye Uwanja ww Benjamin Mkapa.
Mchezo huo utakuwa ni kati ya Yanga dhidi ya Simba.

Timu ya Taifa ya Morocco tayari imewasili jijini Dar es salaam kwaajili ya maandalizi ya mchezo wa hatua ya robo fainali...
20/08/2025

Timu ya Taifa ya Morocco tayari imewasili jijini Dar es salaam kwaajili ya maandalizi ya mchezo wa hatua ya robo fainali ya michuano ya CHAN itakayofanyika August 22 mwaka huu katika uwanja wa Benjamin Mkapa dhidi ya timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars.

Address

Rose Garden Road

00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kijiweni posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share