Kijiweni

Kijiweni Mtaa Unaongea
(1)

31/12/2025

Kiungo Mkabaji Mohammed Damaro Camara raia wa Tanzania 🇹🇿 ni mali ya Young Africans akitokea Singida Black Stars.

HAKUNA namna. Taifa Stars ina dakika 90 ngumu usiku wa leo mbele ya Tunisia. Ni ushindi pekee ndio unaweza kuifanya timu...
30/12/2025

HAKUNA namna. Taifa Stars ina dakika 90 ngumu usiku wa leo mbele ya Tunisia. Ni ushindi pekee ndio unaweza kuifanya timu hiyo isalie Morocco ama ifungashe virago kurudi nyumbani k**a ilivyokuwa kwa Botswana, Gabon na Guinea ya Ikweta zilizoaga mapema michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025.

Baada ya kupoteza mechi ya kwanza ya Kundi C kwa Nigeria, kisha kulazimishwa sare ya 1-1 na Uganda, Taifa Stars imeingia mtegoni, kwani inahitaji ushindi wa aina yoyote usiku wa leo ili kujiweka katika nafasi ya kusonga mbele katika fainali hizo.

Licha ya kwamba ushindi huo mbele ya Tunisia katika mechi hiyo ya mwisho ya makundi itaiweka Stars katika nafasi nzuri ya kutinga 16 Bora, pia itakuwa ni rekodi kwa timu hiyo inayoshiriki fainali hizo kwa mara ya nne tangu mwaka 1980.

Katika ushiriki wa fainali tatu za awali za mwaka 1980, 2019 na 2023, timu hiyo ya taifa ya Tanzania haijawahi kupata ushindi wowote zaidi ya kuambulia sare au vipigio kutoka kwa wapinzani.

Leo kwenye mikikimikiki ya Ligi Kuu England zitapigwa mechi ambazo huenda zikaleta mabadiliko makubwa kwenye msimamo wa ...
30/12/2025

Leo kwenye mikikimikiki ya Ligi Kuu England zitapigwa mechi ambazo huenda zikaleta mabadiliko makubwa kwenye msimamo wa ligi hiyo, huku nyingine zikitarajiwa kuchezwa Jumatano na kitu kinacholeta mvuto mkubwa katika mikikimikiki hiyo ya kibabe kabisa kwenye ligi za Ulaya.
Arsenal itahitaji ushindi ili kuendelea kung’ang’ania kileleni na kutinga Mwaka Mpya 2026 ikiwa hapo, kuchagiza harakati zake za kufukuzia ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu baada ya kukukaribia kuubeba kwa misimu mitatu mfululizo iliyopita.

Lakini, shughuli inayowakabili ni pevu, mbele yao wamesimama Aston Villa, ambao pia wapo kwenye mbio za ubingwa, huku wakiwa wameshinda mechi zao 11 mfululizo.

Kingine, Aston Villa inanolewa na kocha wa zamani wa Arsenal, Unai Emery, ambaye amekuwa na kawaida ya kukitesa kikosi hicho cha Emirates. Arsenal itahitaji kushinda ili isijali matokeo ya timu nyingine.

Rekodi zinaonyesha, mechi tano zilizopita, Aston Villa imeshinda tatu, sare moja na Arsenal imeambulia ushindi mara moja tu. Balaa hilo.
Aston Villa ikishinda, itafikia pointi za Arsenal na kwamba miamba hiyo ya Emirates itaendelea kuwa kileleni kwa tofauti ya mabao tu.

Wapinzani wengine wa Arsenal kwenye kugombania kilele cha msimamo wa Ligi Kuu England ni Manchester City, ambao wao watasubiri Jumatano, ambapo watakipiga na Sunderland ugenini.
Kwa vyovyote, Man City ya Pep Guardiola itahitaji ushindi bila ya kujali matokeo ya wapinzani wake katika mbio za ubingwa ili kuzidi kuleta presha kileleni kwenye msimamo wa ligi hiyo.

29/12/2025

Ungetoboa? 😄

29/12/2025

Ungetoboa? 😂

SARE ya bao 1-1, iliyoipata Taifa Stars juzi katika Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON), dhidi ya Uganda ‘The Cranes’,...
29/12/2025

SARE ya bao 1-1, iliyoipata Taifa Stars juzi katika Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON), dhidi ya Uganda ‘The Cranes’, imeiweka timu hiyo katika mtego wa kufuzu hatua ya 16 bora, kwa sababu italazimika kuifunga Tunisia kesho, huku ikiiombea Nigeria ‘Super Eagles’, inayoongoza kundi C, ambayo tayari imeshafuzu iifunge pia Uganda.

Katika kundi hilo la C, Nigeria imefuzu hatua ya 16 bora baada ya kushinda mechi zote mbili ikianza kwa kuifunga Taifa Stars mabao 2-1, kisha kuifunga Tunisia 3-2, huku kwa upande wa kikosi hicho kinachonolewa na Muargentina Miguel Gamondi kikifungwa moja na kutoka sare pia moja hivyo, kuhitaji miujiza ya kufuzu hatua ya 16 bora.

Katika mechi hiyo ya juzi ambayo Stars ilihitaji ushindi ili kuweka matumaini hai baada ya kupoteza kwa Nigeria, ilianza kupata bao la utangulizi la Simon Msuva dakika ya 59 kwa penalti, kisha Uganda kusawazisha dakika ya 80, lililofungwa na Uche Ikpeazu, huku ikikosa pia penalti ya dakika ya 90, ya kiungo mshambuliaji, Allan Okello.

TIMU ya Kagera Sugar imeweka rekodi mpya katika Ligi ya Championship msimu huu, baada ya kikosi hicho kinachonolewa na J...
29/12/2025

TIMU ya Kagera Sugar imeweka rekodi mpya katika Ligi ya Championship msimu huu, baada ya kikosi hicho kinachonolewa na Juma Kaseja kushinda mechi tisa mfululizo, ikifuatiwa na Geita Gold na Mbeya Kwanza zilizoshinda mara nane kila mmoja.

Kagera iliyodumu katika Ligi Kuu Bara kwa miaka 20 tangu iliposhiriki 2005, ilishuka daraja msimu wa 2024-2025, baada ya kikosi hicho kushinda mechi tano, sare nane na kupoteza 17, ikishika nafasi ya 15, kufuatia kukusanya pointi 23.

Timu hiyo tangu ilipoanza ufunguzi wa Ligi ya Championship msimu huu kwa suluhu (0-0), dhidi ya maafande wa Transit Camp Oktoba 10, 2025, imeshinda mechi tisa mfululizo, ikiwa ni rekodi mpya kwa kikosi hicho kwani ilikuwa haijawahi kutokea.

Baada ya suluhu hiyo, Kagera ilizifunga Barberian mabao 2-1, (1-0) v Bigman FC, (4-1) v African Sports, (4-0) v Stand United, (2-0) v Polisi Tanzania, (1-0) v B19 FC, (3-1) v Hausung FC, (1-0) v TMA FC, kisha kuichapa Mbuni FC mabao 2-0.

Kabla ya kucheza jana, Jumapili kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mkoani Kagera dhidi ya Songea United, timu hiyo tayari imecheza mechi 11, msimu huu, ambapo kati ya hizo imeshinda tisa na kutoka sare miwili, huku ikiwa haijapoteza yoyote.

Akizungumzia mwenendo wa timu hiyo, kocha wa kikosi hicho, Juma Kaseja, amesema siri kubwa ni kila mmoja kujitambua pia malengo waliyojiwekea mwanzo mwa msimu huu, huku ushirikiano wake mzuri na wachezaji ukiwa silaha nyingine inayowabeba.

HAKUNA kingine kinachohitajika kwa Taifa Stars leo ila ni ushindi tu. Kila Mtanzania bila kujali imani yake, anapaswa ku...
27/12/2025

HAKUNA kingine kinachohitajika kwa Taifa Stars leo ila ni ushindi tu. Kila Mtanzania bila kujali imani yake, anapaswa kuomba dua njema ili Stars itoboe mbele ya Uganda The Cranes.

Stars inatarajiwa kushuka uwanjani usiku wa leo Jumamosi kucheza mechi ya pili ya Kundi C ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 dhidi ya Uganda huku kila moja ikitoka kupoteza mechi iliyopita mbele ya Nigeria na Tunisia.

Kila moja inahitaji ushindi, lakini kwa Tanzania ni muhimu zaidi ili kuandisha historia mpya katika michuano hiyo, kiasi hata wachezaji wa timu hiyo nao wanakiri wanahitaji dua za Watanzania.

Stars na Uganda zitakutana Uwanja wa Al-Barid, Rabat, Morocco kuanzia saa 2:30 usiku kwa saa za Tanzania, mechi hiyo imebeba maana kubwa sana kwa timu zote mbili. Mechi hiyo itatanguliwa na mechi za mapema kati ya Benin na Botswana itakayopigwa saa 9:30 alasiri na ile ya Senegal na DR Congo saa 12:00 jioni zikiwa ni mechi za Kundi D, huku Tunisia na Nigeria zitaumana saa 5:00 usiku.

Klabu ya Simba Sc imemrejesha aliyekuwa Nahodha wa Wekundu hao wa Msimbazi k**a kocha wa timu vijana akitokea JKT Tanzan...
27/12/2025

Klabu ya Simba Sc imemrejesha aliyekuwa Nahodha wa Wekundu hao wa Msimbazi k**a kocha wa timu vijana akitokea JKT Tanzania baada ya kumalizika mkataba wake k**a mchezaji.

Bocco ambaye ni Mfungaji bora wa muda wote wa Ligi Kuu Tanzania John Bocco anamiliki leseni B ya shirikisho la soka Afrika CAF, amepewa programu nzima ya maendeleo ya vijana ndani ya Simba Sports Club.

Leo si ndio Boxing Day? Basi kwenye mikikimikiki ya AFCON 2025 vigogo wanane wa soka watakuwa na kazi ya kufungua maboks...
26/12/2025

Leo si ndio Boxing Day? Basi kwenye mikikimikiki ya AFCON 2025 vigogo wanane wa soka watakuwa na kazi ya kufungua maboksi ya zawadi kwa mashabiki wao watakapoonyeshana ubabe kwenye mchakamchaka wa kusaka ubingwa wa Afrika nchini Morocco.

Nani watafungua zawadi kwa kicheko? Na nani watafungua kwa kilio na kujiweka kwenye hatari ya kufungashiwa virago vyao vya kutupwa nje kwenye Afcon 2025?

MECHI ZA BOXING DAY AFCON 2025

Angola v Zimbabwe (Saa 9:30 alasiri)
Misri v Afrika Kusini (Saa 12:00 jioni)
Zambia v Comoros (Saa 2:30 usiku)
Morocco v Mali (Saa 5:00 usiku)

Mchezo Umemalizika 🇳🇬🇹🇿Mchezo wa kusisimua umemalizika kwa Nigeria kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania.Una...
23/12/2025

Mchezo Umemalizika 🇳🇬🇹🇿

Mchezo wa kusisimua umemalizika kwa Nigeria kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania.

Una Kipi Cha Kuzungumza? Umeuonaje Mchezo Huu?

23/12/2025

Safari ya kuelekea uwanjani kwenye mchezo wetu wa kwanza wa fainali za TotalEnergies AFCON 2025

Golikipa wa Azam, Zubeir Foba (23) anatarajia kuanza kwenye kikosi cha kwanza cha timu ya Taifa ya Tanzania 🇹🇿 hii leo dhidi ya Nigeria 🇳🇬

Anaenda kucheza mechi ya kwanza ya AFCON katika maisha yake ya soka

✅Alphonce Mabula nae anatarajia kuanza First XI

Address

Rose Garden Road
Dar Es Salaam
00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kijiweni posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share