04/03/2026
Je Allan Okello na Boka wanaweza kuwa na Msaada zaidi ya huu wasasa Jibu kwangu ni NDIO kubwa
Japo ukweli ni Mchungu ila inatakiwa tuseme tu ili wanaopigana wapigane wanao tulia watulie wale Nyama wanyamaze kistaarabu eeh bhanaa eeh light k**a Mimi ningelikuwa Kocha wa Yanga Sports Club leo hii ningekuwa na maamuzi magumu kutokana na situation iliopo
Kwa Sasa Timu imekumbwa na Majeraha Mengi na tena kwa wachezaji muhimu sana k**a vile Pacome,Mzize na Job japo niwengi zaidi ya hao ila Mawazo yangu ni yapi mpaka nimeandika Leo tena
Mawazo yangu ni haya Allan Okello ni Mchezaji kwanza tukubali kuwa Okello sio Mzeji anayeweza battle yani kupambana na Wachezaji wengine kuwania Mpira either kuwanyanganya au kuulinda kwa usahihi hivyo basi Okello Moja kwa Moja anapoteza Sifa ya kuwa Winga
Pili Allan Okello kwa sababu sio Mkabaji Mzuri na pia sio mchezaji anaependa kuguswa wala kukaba sana mie ningebadirishia Majukumu kwa kumchezesha namba 10 na sio Winga kwa sababu sifa ya Namba 10 wengi sio wakabaji wala wapenda kugusana ila niwazuri kumiliki Mipira kwa sababu ya uwezo wao mkubwa ya kupunguza Adui na kutoa Pasi zenye Madhara makubwa kwa Adui hivyo basi hata ukiangalia Touch nzuri alizofanya Okello utagundua kafanya akiwa anacheza eneo la namba 10 na sio Winga 7 au 11
Haya twende kwa Boka bhana Boka ni Mchezaji Mzuri sana kwenye Kupandisha Timu kutoka katika eneo lake la 3 kwenda 11 hapa huwa na Kasi sana pia ni mzuri kwenye kutengeneza Pasi za mwisho pia kufunga Sometimes napia nimefutilia uwezo wake nikaona kuwa Boka pia tukimsogeza namba 11 pale anaweza kutoa kitu kuliko hao tunaosema ni namba 11 halisia hivi sasa ukiangalia katika Timu yetu kwa Sasa hakuna Winga namba 11 anaweza kufanya k**a Boka huo ndio ukweli
Kwa hivyo basi ningempatia Boka nafasi ya Majaribio k**a Winga angalau kwa Games Mbili nione ataniofa nini
Ngoja niishie hapo kwa Sasa nitakuja na Mambo mengine baadae kuhusu Kocha wenu 🤣🤣⚠️
🏃🏃