RaiaPost

RaiaPost Raia wenzangu, habari ni msingi wa maendeleo na haki zetu. Tufuatilie Shughuli Zote Zenye Kuleta Maendeleo Kwa Taifa
❤️🇹🇿

Kufuatilia matukio ya nchi yetu hutuwezesha kufanya maamuzi sahihi, kushiriki kikamilifu, na kutimiza wajibu wetu wa kiraia.

01/10/2025
 : Mahak**a ya Watu ya Kati katika mji wa Changchun, Mkoa wa Jilin, imemhukumu Waziri wa zamani wa Kilimo na Masuala ya ...
29/09/2025

: Mahak**a ya Watu ya Kati katika mji wa Changchun, Mkoa wa Jilin, imemhukumu Waziri wa zamani wa Kilimo na Masuala ya Vijijini wa China, Tang Renjian, adhabu ya kifo itakayositishwa kwa miaka miwili, baada ya kupatikana na hatia ya kupokea hongo ya takribani dola milioni 38 (yuan milioni 268) sawa na Bilioni 92 za kitanzania.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Xinhua, Tang pia amepokwa haki zake zote za kisiasa milele, huku mali zake binafsi zikitaifishwa na fedha alizopata kwa njia haramu zikikabidhiwa kwa serikali.

Mahak**a ilibaini kuwa kati ya mwaka 2007 na 2024, Tang alitumia nyadhifa zake za juu katika ngazi za kitaifa na mitaa kusaidia watu wengine kupata mikataba ya biashara, kushinda zabuni za miradi na kupandishwa vyeo, na kwa malipo alipokea hongo hizo.

Credit

 : Chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ujenzi wa Jangwani Bridge, daraja jipya lenye urefu wa takribani 390 mita lik...
29/09/2025

: Chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ujenzi wa Jangwani Bridge, daraja jipya lenye urefu wa takribani 390 mita likiambatana na barabara za kuunganisha zenye jumla ya 700 mita.

Mradi huu unagharimu takribani Shilingi bilioni 97.1, na umelenga kuondoa kero za mafuriko katika bonde la Mto Msimbazi na kurahisisha usafiri wa magari na watembea kwa miguu kati ya Jangwani, Kigogo, Magomeni na katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

Ujenzi huu utapunguza athari za mvua za msimu na kuimarisha usalama wa barabara ya Morogoro, ambayo ni kiunganishi kikuu kati ya Dar es Salaam na mikoa ya nyanda za juu na magharibi mwa Tanzania.

ChanZ0

 🇹🇿
29/09/2025

🇹🇿

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, chama tawala, Stephen Wasira amesema kunung'unika na kufik...
29/09/2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, chama tawala, Stephen Wasira amesema kunung'unika na kufikisha ujumbe wa changamoto mbalimbali kwa njia ya maandamano kumepitwa na wakati kwa kusema Watanzania wanataka maendeleo ukiwemo ujenzi wa miundombinu muhimu ambayo itarahisisha shughuli za kiuchumi na ajira kwa wananchi. Kiongozi huyo wa CCM ametoa matamshi hayo jana Septemba 28, 2025 wakati alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa chama chake wa majimbo ya Vunjo na Moshi Vijijini, mjini Moshi ikiwa sehemu ya kampeni ya chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 wa Tanzania. Tujadili wazo la mbinu mbadala la kufikisha hisia za umma kwa mamlaka.

Credit
DW

Yeriko Nyerere anasema hiki Ndiyo Chama Kinachopendwa na WaTanzania Wote 🇹🇿
28/09/2025

Yeriko Nyerere anasema hiki Ndiyo Chama Kinachopendwa na WaTanzania Wote 🇹🇿

Mgombea Wa Urais Kupitia  Chauma Ameahidi kufufua Viwanda vya Chai nchini 🇹🇿
28/09/2025

Mgombea Wa Urais Kupitia Chauma
Ameahidi kufufua Viwanda vya Chai nchini 🇹🇿

Mgombea wa urais CCM Dk. Samia Suluhu Hassan ameahidi kuwa katika kipindi cha miaka mitano ijayo ikiwa wananchi watampa ...
28/09/2025

Mgombea wa urais CCM Dk. Samia Suluhu Hassan ameahidi kuwa katika kipindi cha miaka mitano ijayo ikiwa wananchi watampa ridhaa ya kuunda serikali, kutajengwa uwanja mkubwa wa michezo Msoga, Chalinze Mkoani Pwani.

"Hii ni k**a shukrani yetu kwa utumishi wa Rais wa awamu ya nne Dk. Jakaya Kikwete, mengi tumeyapa majina Kikwete lakini sio Msoga, hapa hatukufanya kitu kwahiyo uwanja ule tutauweka Msoga kuonesha shukrani yetu kwa Rais wa awamu ya nne," amesema Dk. Samia.

Dk. Samia ameyaeleza hayo leo Jumapili Septemba 28, 2025 wakati wa kampeni zake kwenye eneo la Msoga mkoani humo akiwa njiani kuelekea Mkoani Tanga.

Pia ameahidi kuendelea kusogeza huduma za kijamii karibu zaidi na wananchi pamoja na kuendelea na uhakiki wa madai ya fidia kwa baadhi ya wananchi wa Msata waliopisha miradi ya maendeleo kwenye eneo hilo.

Credit....✍️
Nipashe

Siku moja tu baada ya kuk**atwa kwa mshukiwa wa ulanguzi wa binadamu anayedaiwa kusafirisha watu hadi Urusi, timu yake y...
28/09/2025

Siku moja tu baada ya kuk**atwa kwa mshukiwa wa ulanguzi wa binadamu anayedaiwa kusafirisha watu hadi Urusi, timu yake ya wanasheria imenukuliwa na chombo cha habari cha ndani nchini Kenya akidai kuwa tayari amerahisisha safari ya zaidi ya Wakenya 1,000 hadi nchini humo bila kukumbwa na matatizo yoyote.

Kwa mujibu wa mawakili wake, Edward Gituku anadaiwa kuhusika katika kuwahamisha wanajeshi wa zamani wa Kenya ambao walisajiliwa katika vitengo vya jeshi la Urusi.

Mawakili hao wanadai zaidi kwamba wale wanaosafirishwa wana hati rasmi zinazowaidhinisha kusafiri kwa shughuli zinazohusiana na kijeshi nchini Urusi.

Mawakili hao wanadai kuwa mshtakiwa, ambaye anadaiwa kuwezesha zaidi ya Wakenya 100 kusafiri hadi Urusi katika muda wa miezi mitatu pekee, aliendesha shughuli zake bila ya udhibiti.

Zaidi ya watu 20 waliokolewa nchini Kenya kutoka kwa watuhumiwa wa ulanguzi wa binadamu ambao uliwarubuni kwa ofa za kazi nchini Urusi lakini walinuia kuwatuma kupigana nchini Ukraine, polisi walisema.

Chanzo: BBC

28/09/2025

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255658412883

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when RaiaPost posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to RaiaPost:

Share