RaiaPost

RaiaPost Raia wenzangu, habari ni msingi wa maendeleo na haki zetu. Tufuatilie Shughuli Zote Zenye Kuleta Maendeleo Kwa Taifa
❤️🇹🇿

Kufuatilia matukio ya nchi yetu hutuwezesha kufanya maamuzi sahihi, kushiriki kikamilifu, na kutimiza wajibu wetu wa kiraia.

‎ : Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameliagiza Jeshi la Polisi liach...
30/11/2025

‎ : Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askofu Dkt. Josephat Gwajima k**a walivyokuwa wametangaza awali ili aweze kuendelea shughuli zake.

‎Amesema baada ya kutoa msamaha kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, waumini wanahitaji wamuone kiongozi wao, hivyo anatakiwa ajitokeze hadharani aendelee na kazi yake. “Mwacheni ajitokekeze tujenge umoja wa kitaifa, tushik**ane kurudisha umoja wa kitaifa. Tumekutana na TEC, viongozi wa dini, wa mila na viongozi mbalimbali; twendeni sote kwenye jambo hili, tujitokeze tuhamasishe Tanzania yenye amani, huu ndio wito wa kiongozi wetu wa nchi”

‎Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Novemba 30, 2025) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Arumeru katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Magufuli Leganga, kata ya Usa River, wilayani Arumeru mkoani Arusha.

‎Waziri Mkuu amewataka Watanzania wakatae kushawishiwa na wanaharakati wanaochochea vurugu kwani zinarudisha nyuma maendeleo ya nchi. "Nimekuja kuwapa pole wananchi wenzangu, kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Anatambua mambo yanayoendelea. Anatambua kazi kubwa ya kujenga Taifa mnayoifanya," amesema.

‎Kabla ya mkutano huo, Waziri Mkuu alikagua uharibifu uliofanywa wakati wa vurugu za Oktoba 29, mwaka huu kwenye kituo cha polisi cha Kikatiti (mita 500 kutoka barabara kuu ya Arusha - Moshi); Mahak**a ya Mwanzo ya Maji ya Chai (km. 3 kutoka barabara hiyo kuu); kituo cha mafuta Total Energies kilichopo Maji ya Chai (kipo barabarani) ambavyo vyote vilichomwa moto ikiwemo kuiba mali kwenye supermarket na kubomoa sefu ya kutunzia fedha.

‎Waziri Mkuu amesema masuala ya maendeleo ya wilaya ya hiyo k**a vile maji na barabara yamo kwenye Ilani ya CCM na kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais lakini yatafanyika endapo tu nchi itakuwa na amani. “Tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kufukuza maendeleo, tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kuongeza umaskini kwa mtu mmoja mmoja," ameonya.

Credit

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali haitokuwa na mzaha na Watumishi wa Serikali Wazembe, Wavivu na Wala r...
25/11/2025

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali haitokuwa na mzaha na Watumishi wa Serikali Wazembe, Wavivu na Wala rushwa na kusema ikithibitika Mtumishi anafanya makosa hayo na kukwamisha utendaji asiishie kuhamishwa tu bali afukuzwe kazi.

Akiongea Jijini Dar es salaaam leo November 25,2025 kwenye mkutano wake na Wahariri wa Vyombo vya Habari, Mwigulu amesema ““Suala la nidhamu kazini hatutokuwa na mzaha nalo, uadilifu hatutokuwa na mzaha nao, bila nidhamu na uadilifu hatutotimiza malengo yaliyopo kwenye dira na Ilani, na nimewaelekeze Watendaji wa Serikali wasiwe na mzaha kwenye hili, na wale Wazembe, Wavivu, Wadokozi, Wala rushwa tutashughulika nao”

“Na nimeelekeza Mtumishi Mzembe na Mla rushwa asihamishwe akibainika na kuthibitika afukuzwe, hatuna uhaba wa Vijana wa kufanya kazi”

“Mh. Rais ameelekeza utaratibu wa kuwasikiliza Watanzania, na hili tumeshaelekeza kote kitakachofuata tutafuatiliana, ni kweli kuna baadhi ya maeneo kunakuwa na ulegevu wa utimizaji wa majukumu ya namna hii”

Credit

Rais wa Tanzania,  Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza kwam a hakutakuwa na maadhimisho ya sherehe za Uhuru December 09,...
24/11/2025

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza kwam a hakutakuwa na maadhimisho ya sherehe za Uhuru December 09,2025 na badala yake fedha ambazo zilipaswa kutumika katika sherehe hizo zitumike katika kurekebisha miundombinu iliyoharibika kutokana vurugu zilizotokea October 29, 2025.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema hayo wakati akiongea na Wakazi wa Mbezi Luis Jijini Dar es salaam leo November 24,2025.

“Ninaungana na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa pole kwa wote walioathirika na vurugu zilizotokea oktoba 29, 2025, tumuunge mkono Rais na Wajumbe wa Tume iliyoundwa kwa ajili kuchunguza kwenye undani tukio la vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025 ili tujue namna lilivyofanyika na hatua stahiki zitakazochukuliwa

“Nimepitia na kukagua uharibifu wa mali na miundombinu ya umma, huwezi kuamini k**a tukio hili limetokea Tanzania, Watanzania tunapaswa kujua miundombinu hii ni mali ya umma, tunazijenga kwa fedha zetu sisi Watanzania, si pesa za Serikali”

“Wanaoshabikia uharibifu wa miundombinu ya Umma hawapo hapa nchini, wanawaambia mkachome mali za umma, mkifanya hivi mtaishije? huko wanakoishi haya wanayowaambia mfanye huko kwao hauwezi kuyafanya.

“Wanajipa haki kwamba wao wanaipenda Tanzania, mpenda Tanzania hawezi kukwambia uichome Tanzania, msiwasikilize, mkiichoma zaidi Tanzania wao ndio wanalipwa zaidi”

Credit

Sugu...✍️
14/10/2025

Sugu...✍️

Chadema imepoteza k**anda MWINGINE.
13/10/2025

Chadema imepoteza k**anda MWINGINE.

08/10/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka W...
07/10/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuliheshimisha jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndani na nje ya nchi, kwa kulinda amani na utulivu wa nchi.

Dkt. Samia amesema kuwa Tanzania ni jina linaloheshimika sana kwa mataifa ya nje kutokana na uhusiano mzuri wa kidemokrasia ambao serikali yake imeujenga na hivyo kuwataka Watanzania kulinda heshima hiyo kwa kufuata sheria na taratibu za nchi ikiwemo kushiriki zoezi la uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 kwa amani.

Dkt. Samia ametoa wito huo leo Oktoba 7, 2025 wakati akinadi sera zake kwa wakazi wa Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza.

Amesema wapo Watanzania ambao hawapendi kuona jina la nchi yao linapata heshima kutoka kwa mataifa mengine na hivyo furaha yao ni kuchafua jina la nchi. Ni katika muktadha huo amewasisitiza Watanzania wenye nia njema na nchi yao kuwapuuza watu hao.

Kwa upande wa ahadi, amesema akipata ridhaa ya kuongoza tena nchi yetu atahakikisha serikali yake inaboresha na kuimarisha sekta zote za maendeleo ikiwemo kilimo, uvuvi, ufugaji, usafiri na usafirishaji. Amefafanua kuwa atajenga viwanda vya kuongezea thamani ya mazao na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini pamoja na kutafuta masoko ya nje ya bidhaa hizo.

Chanzo
Tbc

Mnaipeleka wapi Dunia hii 🌍😭😭😭
07/10/2025

Mnaipeleka wapi Dunia hii 🌍😭😭😭

  Mahak**a ya hakimu mkazi mkoa wa Manyara imemuhukumu Hamis Abdalah mwenye miaka 42 mkazi wa Babati Manyara miaka sita ...
07/10/2025

Mahak**a ya hakimu mkazi mkoa wa Manyara imemuhukumu Hamis Abdalah mwenye miaka 42 mkazi wa Babati Manyara miaka sita jela na faini ya milioni moja baada ya kutiwa hatiani na kosa la kujeruhi kwa kumkata masikio mtoto wa jirani yake mwenye umri wa miaka 13 aliyeelezwa kwamba alimuibia yai moja la kuku.

Hukumu hiyo imesomwa mbele ya hakimu mkazi mkoa wa Manyara Martini Masao, ambapo msh*takiwa huyo ameelezwa kutenda kosa hilo mnamo 23.08.2025.

Kesi hiyo namba 23254 ya mwaka 2025 imetolewa hukumu hii leo kwenye mahak**a hii ya hakimu mkazi mkoa wa Manyara, ambapo mshtakiwa huyo Hamis Abdala alimkata masikio yote mawili kwa kutumia kiwembe, kumchanja kifuani pamoja na kumbamiza kichwa ukutani.

Mbele ya mahak**a Hakimu Martin Masao alimuuliza mshtamiwa huyo unachochote cha kuiambia Mahak**a? mshtakiwa huyo aliijibu mahak**a "SINA CHOCHOTE" cha kuiambia mahak**a.

Mara baada ya mshtakiwa huyo kudai hana chochote cha kuiambia mahak**a ndipo Hakimu Martin Masao alipotoa hukumu hiyo kwa mshtakiwa kwenda jela miaka sita na faini ya milioni moja.

Hata hivyo Hakimu Martin Masao aliiambia mahak**a kuwa kosa hilo ni kinyume na kifungu cha sheria namba 225 cha kanuni za adhabu kwa makosa ya jinai sura ya 16 marejeo 2023.

 : Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ya Awamu ya Sita imefanya mageu...
07/10/2025

: Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ya Awamu ya Sita imefanya mageuzi makubwa ya maendeleo katika Wilaya ya Nyamagana, na kwamba katika awamu ijayo itahakikisha maendeleo hayo yanazidi kuimarika katika sekta zote zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni Nyamagana jijini Mwanza, Dkt. Samia amesema Serikali imeweka mkazo mkubwa katika sekta ya afya, kwa kujenga na kukarabati vituo vya afya na zahanati katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, pamoja na kuimarisha huduma za hospitali kuu ya wilaya.

“Tumeongeza upatikanaji wa huduma bora za afya, tunajenga vituo vipya, tunaajiri watumishi wa afya, na sasa mwananchi wa Nyamagana hapaswi kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma,”amesema Dkt. Samia

Katika sekta ya elimu, Dkt. Samia ameeleza kuwa Serikali imeongeza fedha za kugharamia mpango wa elimu bila ada, sambamba na ujenzi wa shule mpya za msingi na sekondari ambazo zimepunguza msongamano wa wanafunzi.

Akizungumzia maji safi na salama, Dkt. Samia amesema miradi mikubwa ya maji imefanyika kwa mafanikio, na upatikanaji wa huduma hiyo umeimarika kwa kiwango kikubwa, jambo lililopunguza changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa vijijini na mijini.

Kuhusu miundombinu, alisema Serikali imeendelea kuboresha barabara ndani ya Jiji la Mwanza, hususani Nyamagana, ili kurahisisha usafiri na biashara.
“Tumejenga barabara za lami, tumeimarisha barabara za mitaa, na sasa tunapanua miundombinu ya mitaa kwa ajili ya kukuza uchumi wa wananchi wetu,” alisema Dkt. Samia.

Katika sekta ya uchumi na uwezeshaji wananchi, amebainisha kuwa Serikali imeongeza mikopo ya asilimia 10 kupitia halmashauri kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, hatua inayowasaidia kujiajiri na kukuza uchumi wa kaya.

Credit
Ccm Tanzania

 : Jeshi la Polisi limeanza rasmi uchunguzi wa tuhuma za kutekwa kwa Humphrey Polepole kufuatia madai yaliyotolewa na Au...
07/10/2025

: Jeshi la Polisi limeanza rasmi uchunguzi wa tuhuma za kutekwa kwa Humphrey Polepole kufuatia madai yaliyotolewa na Augustino Polepole kupitia mitandao ya kijamii, ambapo alidai kuwa ndugu yake alitekwa na Afisa wa Polisi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi hilo iliyotolewa Oktoba 6, 2025, jalada la uchunguzi lilifunguliwa mara moja siku hiyo hiyo, na hatua za awali zimejumuisha ukusanyaji wa taarifa mbalimbali zinazohusiana na tukio hilo.

Polisi wamesema wanaendelea kumtafuta Augustino Polepole ili aweze kutoa ushirikiano na kufafanua kwa kina madai yake, ikiwa ni pamoja na kutoa uthibitisho kuwa Humphrey alikuwa mkazi au mpangaji wa nyumba aliyodai kuwa tukio hilo lilifanyika.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi huu ukiendelea na limeahidi kutoa taarifa zaidi kadri hatua za kisheria zitakavyopigwa.

Credit
ITV

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255658412883

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when RaiaPost posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to RaiaPost:

Share