Nukta Fakti

Nukta Fakti NuktaFakti ni ukurasa rasmi ulioanzishwa na tovuti ya Nukta Habari kufuatilia habari za uzushi Tanzania.

Nukta Fakti is the first Swahili fact-checking initiative in Tanzania under Nukta Africa, a fast growing digital media and technology company. We debunk misinformation and disinformation to minimise more harm to our society. We believe in improving people's lives through quality content which is free from disinformation. Share with us any doubtful information for verification and we will do it for you.

Today, we join the global community in marking International Fact-Checking Day a reminder that truth is the foundation o...
02/04/2026

Today, we join the global community in marking International Fact-Checking Day a reminder that truth is the foundation of informed societies.

As a fact-checking organization, our mission goes beyond correcting misinformation. We are committed to promoting accuracy, strengthening public trust, and safeguarding the integrity of information in the digital age.

In an era where false information spreads faster than facts, verification is not optional, it is essential. Every claim must be questioned, every source examined, and every story held to the highest standard of evidence.

We reaffirm our commitment to accountability, transparency, and truth. Together, we can build a more informed and resilient society.

Verify before you share. Truth matters.

26/03/2026

MOJA KWA MOJA KUTOKA UJERUMANI
Suleiman Mwiru ( ), mwandishi wa habari wa Idhaa ya Kiswahili ya DW anaeleza umuhimu wa wahitimu wa vyuo katika fani ya habari, ubunifu na mawasiliano kupata mafunzo ya vitendo ili kuimarisha taaluma zao.

Mwiru ambaye aliwahi kufanya kazi na Nukta Africa anasema ujuzi wa kisasa k**a uandishi wa habari za takwimu, uthibitishaji habari na mawasiliano ya kimkakati unamuongezea mhitimu nafasi ya kupata ajira kwa haraka katika soko lenye ushindani mkubwa.

K**a wewe ni mhitimu wa chuo, unapenda kukuza taaluma yako ya habari na mawasiliano, changamkia fursa hii ya mafunzo maalum ya miezi 6 kutoka Nukta Africa.

Tuma maombi kwa link >>> https://shorturl.at/Pm2Ji

Mwisho wa kutuma maombi ni Machi 31, 2026.

Wakati maudhui yanayotengenezwa na AI yakiongezeka, zipo zana mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuthibitisha habari, pich...
25/03/2026

Wakati maudhui yanayotengenezwa na AI yakiongezeka, zipo zana mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuthibitisha habari, picha aua video iliyotengenezwa na akili bandia.

Miongoni mwa zana hizo ni FotoForensics ambayo huchambua picha ili kubaini k**a zimebadilishwa kwa kutafuta alama za upungufu wa faili unaotokea wakati picha inapohaririwa na kuonesha maeneo yenye mashaka.

Mbinu nyingine ni ‘Fake Image Ditector’ ni zana inayobaini picha zilizohaririwa kwa kutumia mbinu za kisasa k**a uchambuzi wa taarifa binafsi na uchambuzi wa makosa (Error Level Analysis).

Mbali na hiyo ipo Sensity AI inayootumia akili bandia kuchambua miondoko ya uso na sauti ili kubaini picha na video feki pamoja na zana ya AI or Not ambayo husaidia kutambua k**a picha ni ya kweli au imetengenezwa kwa kutumia akili bandia.

Matumizi ya akili bandia yanaendelea kushika kasi maeneo mbalimbali duniani yakiwasadia waatumiaji kufanya shughuli mbal...
25/03/2026

Matumizi ya akili bandia yanaendelea kushika kasi maeneo mbalimbali duniani yakiwasadia waatumiaji kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo za kitaaluma au kiofisi.

Kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia (WB) hadi kufikia Machi 2024 karibu watu bilioni 3 walitumia programu za akili bandia ikiwemo Chat GPT.

Programu hizo huunda maudhui kwa rangi na ubunifu wa hali ya juu zaidi ya uwezo wa binadamu suala linaloweza kuchochea kuongezeka kwa ta habari za uzushi au uchochezi katika majukwaa ya kidigitali.

Kwa mujibu wa tovuti ya NewsGuard, ambayo hufuatilia tovuti za habari za uongo, mwaka 2023 idadi ya tovuti zinazotumia AI kusambaza habari feki iliongezeka mara kumi ukilinganisha na miaka mingine.

Wakati maudhui yanayotengenezwa na AI yakiongezeka, zipo zana mbalimbali zinazoweza kukusaidia kuthibitisha habari, picha aua video iliyotengenezwa na akili bandia.

Miongoni mwa zana hizo ni FotoForensics ambayo huchambua picha ili kubaini k**a zimebadilishwa kwa kutafuta alama za upungufu wa faili unaotokea wakati picha inapohaririwa na kuonesha maeneo yenye mashaka.

Mbinu nyingine ni ‘Fake Image Ditector’ ni zana inayobaini picha zilizohaririwa kwa kutumia mbinu za kisasa k**a uchambuzi wa taarifa binafsi na uchambuzi wa makosa (Error Level Analysis).

Mbali na hiyo ipo Sensity AI inayootumia akili bandia kuchambua miondoko ya uso na sauti ili kubaini picha na video feki pamoja na zana ya AI or Not ambayo husaidia kutambua k**a picha ni ya kweli au imetengenezwa kwa kutumia akili bandia.

Kumekuwa na video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii hususan Tiktok ikidai kuwa uchunguzi wa saratani ya mat**i kwa ...
04/03/2026

Kumekuwa na video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii hususan Tiktok ikidai kuwa uchunguzi wa saratani ya mat**i kwa kutumia biopsia husababisha saratani kuenea kwa kasi, taarifa ambayo si ya kweli.

Kupitia video aliyochapisha kwenye mtandao wa tiktok yenye jina dr_masipeti, dada huyo ambaye anajinasibu kuwa ni mtaalam wa tiba asili amewasihi watu wenye dalili ya saratani ya t**i kutokubali kufanya uchunguzi kwa kutumia njia ya kitaalam ya biopsia kwa kudai kuwa inasababisha saratani kusambaa kwa haraka.

“Usirudie tena kufanya kitu kinaitwa biopsi, saratani ukienda kufanya biopsi inasambaa kwa spidi ya hali ya juu” amepotosha dada huyo kupitia akaunti yake ya TikTok.

Taarifa ya Wizara ya Afya iliyotolewa Machi 4, 2026 imefafanua kuwa taarifa ya mwanadada huyo kuhusu biospia ni upotoshaji unaoweza kuhatarisha maisha ya wagonjwa.

Aidha, wizara imefafanua kuwa mtu anayeonekana kwenye video inayosambazwa si mtaalamu wa tiba asili na wala hatambuliwi na baraza lolote la kitaaluma nchini.

“Baada ya ufuatiliaji tumegundua muhusika anajihusisha na biashara za bidhaa za kimtandao "network marketing" na wala hatakiwi kuelimisha jamii masuala ya afya,” imesema taarifa hiyo.

Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala limewaelekeza wanataaluma wa tiba hiyo, wafanyabiashara na wajasiriamali wote wa bidhaa mbalimbali wanaotoa elimu au kutumia bidhaa hizo waondoe matangazo yote yanayopotosha jamii, kwani yanaweza kuchelewesha wagonjwa kupata matibabu kwa wakati.

Wizara imewahimiza wananchi kutotegemea taarifa zisizothibitishwa, na badala yake kufika katika vituo rasmi vya afya vinavyotambulika kwa ajili ya uchunguzi na matibabu sahihi yanayotolewa na wataalamu waliothibitishwa.

Wizara ya Afya imefafanua kuwa Biopsia ni njia salama inayotambulika duniani kote kuthibitisha aina ya saratani ili kusaidia kupanga matibabu sahihi na kwa wakati.

Katika zama za taarifa kusambaa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali, si kila unachokiona au k...
19/02/2026

Katika zama za taarifa kusambaa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali, si kila unachokiona au kusoma huwa ni kweli. Kabla ya kushare au kuamini taarifa, ni muhimu kuchukua muda kuichambua na kuithibitisha ili kuepuka kusambaza upotoshaji.

Wewe unatumia njia gani kuthibitisha taarifa?

22/10/2025

NuktaFakti imefanya uchunguzi kwenye video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha mtu anayedaiwa kuwa na mapepo akipanda ukuta kwa jinsi ambayo binadamu wa kawaida hawezi kufanya.

Kwa kutumia zana ya Invid, NuktaFakti imejiridhisha video hii imehaririwa kwa AI na sio halisi k**a watu wanavyodhani na kuisambaza kwenye mtandao.

Aidha, NuktaFakti imebaini pia kuna video nyingi za aina hii ambazo zimetengenezwa kwa AI inayojulikana kwa jina la Sora na kusambazwa mtandaoni.




Na Nukta Fakti

22/10/2025

NuktaFakti imefanya uchunguzi kwenye video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mgombea Mwenza wa Urais kupitia chama hicho, Dk Emmanuel Nchimbi akitamka maneno "Samia must GO" na kujiridhisha kuwa video hiyo imehaririwa kwa lengo la kupotosha uhalisia.

Tukio linaloonekana kwenye video ni tukio la Septemba 13, 2024, ambapo Balozi Emmanuel Nchimbi (alipokuwa katibu mkuu wa CCM) alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya usalama wa nchi baada ya tukio la kutekwa kwa aliyekuwa mwanachama wa Chadema, Ali Kibao.




Na Nukta Fakti

Kumekuwa na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinazosema kuwa mtengeneza maudhui maarufu wa Marekani, Khab...
22/10/2025

Kumekuwa na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinazosema kuwa mtengeneza maudhui maarufu wa Marekani, Khaby Lame amefariki dunia.

NuktaFakti imejiridhisha kuwa taarifa hizo si za kweli na zina lengo la kupotosha kwani Khaby Lame anaonekana akiendelea na kufanya shughuli zake za utengenezaji wa maudhu mitandaoni. Aidha, hakuna chombo chochote cha habari wala familia yake ilichothibitisha taarifa za kupoteza kwake maisha.




Na Nukta Fakti

Nukta Fakti imefanya uchunguzi kwenye chapisho linalosambaa kwenye mitandao ya kijamii linaloonekana k**a chapisho la mt...
22/10/2025

Nukta Fakti imefanya uchunguzi kwenye chapisho linalosambaa kwenye mitandao ya kijamii linaloonekana k**a chapisho la mtandao wa X (zamani Twitter) lenye majibizano kati ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na Masanja na kubaini kuwa chapisho hilo ni feki, limetengenezwa kwa lengo la kupotosha.

Nukta Fakti imejiridhisha kuwa chapisho hilo halijachapishwa halijachapishwa na Masanja Mkandamizaji wala Rais Samia, halipo kwenye kurasa zao rasmi za mtandao wa X. Aidha, aina ya mwandiko (fonts) na mpangilio (theme) unaoonekana kwenye chapisho hili, si rasmi unaotumika katika machapisho halisi ya mtandao wa X.




Na Nukta Fakti

"Wananchi wana nafasi kubwa sana katika uhakiki wa taarifa,’ amesema Elizabeth Orembo, Mtafiti katika Shirika la Tafiti ...
20/10/2025

"Wananchi wana nafasi kubwa sana katika uhakiki wa taarifa,’ amesema Elizabeth Orembo, Mtafiti katika Shirika la Tafiti la Research ICT Africa, wakati wa kikao cha wadau wa uhakiki wa taarifa kuhusu uzoefu wa mtandaoni katika kukabiliana na taarifa potofu kilichoratibiwa na Nukta Africa.

Amesisitiza kuwa wananchi ndio walengwa wakuu na watumiaji wakubwa wa taarifa, hivyo ni muhimu wawe mstari wa mbele katika uthibitishaji wa taarifa.




Na Nukta Fakti

"Taarifa potofu hazichagui chaneli” amesema Nuzulack Dausen, Mkurugenzi Mtendaji wa Nukta Africa, wakati wa kikao cha wa...
20/10/2025

"Taarifa potofu hazichagui chaneli” amesema Nuzulack Dausen, Mkurugenzi Mtendaji wa Nukta Africa, wakati wa kikao cha wadau wa uhakiki wa taarifa kuhusu uzoefu wa mtandaoni katika kukabiliana na upotoshaji.

Ameeleza kuwa taasisi yoyote iwe serikali, binafsi au ya kijamii inaweza kushambuliwa na taarifa potofu.

Ni wajibu wa kila mmoja kuthibitisha kabla ya kusambaza.

Address

1st Floor, 12 Mwinjuma Road, (Msolomi Street), Kinondoni Studio
Dar Es Salaam
76762

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nukta Fakti posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nukta Fakti:

Share

Category