Nukta Fakti

Nukta Fakti NuktaFakti ni ukurasa rasmi ulioanzishwa na tovuti ya Nukta Habari kufuatilia habari za uzushi Tanzania.

Nukta Fakti is the first Swahili fact-checking initiative in Tanzania under Nukta Africa, a fast growing digital media and technology company. We debunk misinformation and disinformation to minimise more harm to our society. We believe in improving people's lives through quality content which is free from disinformation. Share with us any doubtful information for verification and we will do it for you.

24/09/2025

Uongo hauhitaji nia mbaya kusambaa, wakati mwingine ni kushare bila kuthibitisha. ✅ Fikiria mara mbili kabla ya kusambazia wengine.




Na Nukta Fakti

Je, wajua? 🤔 Unaweza kusambaza taarifa potofu bila hata kujua! 🔄 Kabla ya kushare, chunguza chanzo, hakikisha ukweli, ki...
24/09/2025

Je, wajua? 🤔 Unaweza kusambaza taarifa potofu bila hata kujua! 🔄 Kabla ya kushare, chunguza chanzo, hakikisha ukweli, kisha sambaza kilicho sahihi ✨




Na Nukta Fakti

Je, picha hii ni halisi au imetengenezwa kwa Akili Unde (AI) ? Kwa nini ?Ukweli ni ngao dhidi ya upotoshaji! 🔍✅   Na Nuk...
24/09/2025

Je, picha hii ni halisi au imetengenezwa kwa Akili Unde (AI) ? Kwa nini ?
Ukweli ni ngao dhidi ya upotoshaji! 🔍✅




Na Nukta Fakti

Kumekuwa na taarifa feki zinazosambaa mitandaoni hususan Facebook katika chapisho lenye mfanano na machapisho ya chombo ...
23/09/2025

Kumekuwa na taarifa feki zinazosambaa mitandaoni hususan Facebook katika chapisho lenye mfanano na machapisho ya chombo cha habari cha Jambo TV zikiwa na kichwa kinachosomeka 'Wito wa Chadema: Tudumishe amani ya tafa letu'

Taarifa hizo si za kweli, zinasambazwa kwa lengo la kupotosha. Chapisho linalosambaa halijachapishwa na Jambo TV na halipo kwenye kurasa rasmi za chombo hicho cha habari.

Aidha, chapisho la taarifa kwa umma lililotumiwa k**a chanzo cha taarifa, halijatolewa na Chadema, na halipo kwenye kurasa rasmi za mitandao ya chama hicho cha siasa.




Na Nukta Fakti

K**a bado hujui ufanye nini ukikutana na habari za uzushi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2025, basi dondoo hizi  zitakusaidia k...
18/09/2025

K**a bado hujui ufanye nini ukikutana na habari za uzushi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2025, basi dondoo hizi zitakusaidia kupata ukweli.




Na Nukta Fakti

Je, unajua kutofautisha kati ya habari ya kweli na ya uzushi?   Na Nukta Fakti
16/09/2025

Je, unajua kutofautisha kati ya habari ya kweli na ya uzushi?




Na Nukta Fakti

Nukta Fakti imefanya uchunguzi kwenye chapisho linalosambaa kwenye mitandao ya kijamii hususan Facebook linaloonekana k*...
12/09/2025

Nukta Fakti imefanya uchunguzi kwenye chapisho linalosambaa kwenye mitandao ya kijamii hususan Facebook linaloonekana k**a chapisho rasmi la Mtandao wa X (zamani Twitter) lililochapishwa akaunti yenye jina Said Mchome likisambaza taarifa za uchochezi na kubaini kuwa chapisho hilo ni feki.

Chapisho hilo halijachapishwa na Said Mchome, akaunti inayoonekana imechapisha taarifa hizo haipo kwenye mtandao wa X (zamani twitter). Aidha aina ya mwandiko (fonts) na mpangilio (theme) unaoonekana kwenye chapisho hilo, si rasmi unaotumika katika machapisho halisi ya mtandao wa X.




Na Nukta Fakti

Kumekuwa na taarifa feki zinazosambaa mitandaoni hususan Facebook katika chapisho lenye mfanano na machapisho ya chombo ...
12/09/2025

Kumekuwa na taarifa feki zinazosambaa mitandaoni hususan Facebook katika chapisho lenye mfanano na machapisho ya chombo cha habari cha Mwananchi zikiwa na kichwa kinachosomeka 'Chadema tulifanya wrong move mwaka huu, tuache kujifariji - SUGU'

Taarifa hizo si za kweli, zinasambazwa kwa lengo la kupotosha. Chapisho linalosambaa halijachapishwa na Mwananchi Digital na halipo kwenye kurasa rasmi za chombo hicho cha habari.

Aidha, chapisho la mtandao wa X (zamani Twitter) lililotumika k**a chanzo cha taarifa ni feki, halijachapishwa na Joseph Mbilinyi, halipo kwenye ukurasa wake rasmi wa mtandao huo. Pia aina ya mwandiko (fonts) na mpangilio (theme) unaoonekana kwenye chapisho hilo, si rasmi unaotumika katika machapisho ya mtandao wa X.




Na Nukta Fakti

Kumekuwa na taarifa feki zinazosambaa mitandaoni katika chapisho lenye mfanano na machapisho ya chombo cha habari cha Mw...
11/09/2025

Kumekuwa na taarifa feki zinazosambaa mitandaoni katika chapisho lenye mfanano na machapisho ya chombo cha habari cha Mwananchi zikiwa na kichwa kinachosomeka 'OMO kutokukidhi vigezo vya kuwa mgomea Urais Zanzibar'

Taarifa hizo si za kweli, zinasambazwa kwa lengo la kupotosha. Aidha, chapisho linalosambaa halijachapishwa na Mwananchi Digital, halipo kwenye kurasa rasmi za chombo hicho cha habari. Pia aina ya mwandiko (fonts) na mpangilio (theme) unaoonekana kwenye chapisho hili, si rasmi unaotumika katika machapisho ya chombo hicho.




Na Nukta Fakti

Mitandao ni miongoni mwa nyezo za upashanaji habari zinazotumiwa na watu wengi maeneo mbalimbali duniani ikiwemo nchini ...
11/09/2025

Mitandao ni miongoni mwa nyezo za upashanaji habari zinazotumiwa na watu wengi maeneo mbalimbali duniani ikiwemo nchini Tanzania.

Takwimu mpya za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zilizotolewa hivi karibuni zinaonesha kuwa kufikia Juni, 2025 idadi ya watumiaji wa intaneti nchini imefikia milioni 54.1 ikiongezeka kutoka milioni 49.3 mwishoni mwa mwezi Machi, 2025.

Kuongezeka kwa watumiaji hawa hufanya majukwaa ya mtandaoni kuwa katika hatari ya kupokea taarifa za uzushi kutoka makundi mbalimbali ya watu yenye nia tofauti.

Miongoni mwa maeneo unayoweza kukutana na taarifa hizi za uzushi ni pamoja na mitandao ya kijamii, vyombo vya habari visivyo rasmi au blogu zisizosajiliwa na vyanzo visivyo halali vya kisiasa au watu binafsi wanaochochea propaganda.

Kumbuka kuthibitisha kila habari unayoiona mtandaoni ili uwe salama na wale wanaokuzunguka

10/09/2025

Je, video hii ni halisi au imetengenezwa kwa Akili Unde (AI) ?
Tazama kwa makini kisha tuambie ni kwanini kulingana na jibu lako.




Na Nukta Fakti

InVID ni chombo cha kidijitali kinachotumika katika uhakiki wa taarifa mtandaoni, hasa kuthibitisha uhalisia wa video na...
10/09/2025

InVID ni chombo cha kidijitali kinachotumika katika uhakiki wa taarifa mtandaoni, hasa kuthibitisha uhalisia wa video na picha. Kinasadia kugundua ikiwa video au picha ni halisi au imeharibiwa, kuchambua frames muhimu za video ili kutumika katika utafutaji wa picha (reverse image search), na kubaini chanzo na muda halisi wa video au picha.




Na Nukta Fakti

Address

1st Floor, 12 Mwinjuma Road, (Msolomi Street), Kinondoni Studio
Dar Es Salaam
76762

Website

http://www.nuktaafrica.co.tz/

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nukta Fakti posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nukta Fakti:

Share

Category