14/06/2026
*TANGAZO LA HIJA YA KIMATAIFA*
*MASHUHUDA WA UGANDA – NAMUGONGO & KITUO CHA HIJA KIBEHO, RWANDA*
_“Njooni, tusali pamoja mahali patakatifu”_
*Kituo cha Vijana Don Bosco Upanga, Dar es Salaam*, kupitia programu yake ya *St. Dominic Savio Pilgrimage Service*, kinawatangazia vijana na waamini wote nchini Tanzania kushiriki *Hija ya Kiroho na Kihistoria* kwenda Uganda na Rwanda.
*1. MAHALI NA TAREHE*
*Tarehe:* 10 – 20 Novemba, 2026 | Siku 11
*Nchi zitakazotembelewa:* Uganda, Rwanda na Burundi
*2. MAENEO MAKUU YA HIJA*
*A. UGANDA – NAMUGONGO*
Mahali pa ushuhuda wa damu ya Mashahidi Watakatifu wa Uganda. Wahujaji watashiriki ibada maalum na kutafakari imani yao.
*B. RWANDA – KIBEHO*
Kituo cha Hija kinachotambulika na Kanisa Katoliki Duniani, ambako Bikira Maria aliwatokea watoto mwaka 1981-1989. Tutasali kwa amani ya nchi zetu na familia zetu.
*3. ZIARA NYINGINE ZA NYONGEZA*
Ili kuongeza uzoefu wa wahujaji, ratiba inajumuisha:
*Wakiwa Uganda:*
1. Ziara ya heshima katika *Ubalozi wa Tanzania, Kampala*.
2. Kutembelea *Baraza la Maaskofu Uganda (UEC)* kwa baraka na ujumbe wa umoja.
*Wakiwa Rwanda:*
1. Ziara ya heshima katika *Ubalozi wa Tanzania, Kigali*.
2. Kujifunza historia kwa kutembelea *Kigali Genocide Memorial*.
3. Kutenda upendo kwa kutembelea *Kituo cha Watoto Yatima*.
*Fursa ya Ziada:*
K**a muda utaruhusu, tukiwa Kibeho tutapanga ziara fupi katika *Jiji la Bujumbura, Burundi* kwa ajili ya kupumzika na kuona mji.
*4. GHARAMA NA MALIPO*
*Gharama kwa Mhujaji:* *TSh 950,000/=*
*Gharama inahusisha:*
- Usafiri wa kwenda na kurudi kwa basi la hadhi ya juu
- Malazi katika vituo rasmi vilivyothibitishwa
- Chakula cha mchana na jioni katika vituo rasmi
- Kiingilio katika maeneo yote ya ziara
- Bima ya dharura ya msingi njiani
*Muhimu:* _Matumizi ya njiani yatagharamiwa na kila mhujaji mwenyewe._
*Jinsi ya Kulipa:*
Malipo yote yafanyike kupitia:
*Benki:* Mkombozi Bank
*Jina la Akaunti:* [Savio Pilgrimage Service]
*Namb