21/04/2026
Habari za muda huu, wanafamilia wa SMART EDUCATION TANZANIA π€
Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba radhi kwa jambo lolote ambalo huenda niliwahi kuwakwaza kwa namna yoyote ile. π
Licha ya yote, jambo la msingi ni kuendelea kushik**ana, kuombeana, na kudumisha upendo miongoni mwetu. Ni kweli hatujuani mmoja mmoja, lakini ukweli kwamba Mungu ametukutanisha katika jukwaa hili β hiyo pekee ni neema kubwa sana. β¨
πΉ Kwa wale mlio tayari mmepangiwa vituo vya kazi
Hongereni sana π Tunawatakia kila la kheri katika majukumu yenu mapya.
πΉ Kwa wale ambao bado mnasubiri
Msikate tamaa. Hili ni suala la muda tu β upo kwenye foleni, na muda wako utafika. β³
πΉ Kwa wale ambao mmetoka k**a NOT SELECTED
Msivunjike moyo. Huu sio mwisho wa safari ya ajira. Nafasi zitaendelea kutangazwa, na fursa nyingine zitakuja. Endeleeni kujaribu β muda wenu pia utafika. πͺ
π Kumbuka:
Katika jukwaa hili la SMART EDUCATION TANZANIA, sio ajira tu β pia utapata mafunzo mbalimbali yatakayokujengea uwezo binafsi na kitaaluma. Kwa waliopata ajira, hapa pia mtajifunza mifumo muhimu ya kiutumishi k**a ESS, PEPMIS, SIS, PREM na mingineyo.
Tuendelee kuwa pamoja k**a familia moja π
Nawapenda sana. Mungu awabariki wote. π
β
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji
SMART EDUCATION TANZANIA
π§ [email protected]
π 0717173853 / 0750173853
π www.smarteducation.co.tz