Joelmedia

Joelmedia Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Joelmedia, Digital creator, Ubungo External Dar es salaam, Dar es Salaam.

Building
Empowering Youth With Practical Skills
Digital Marketing, Graphics, Video, Website, AI
Ubungo External Dar es salaam
Mawasiliano: 0745 152 680 I 0627 150 780

Kuna watu wana skills kali sana…Wanajua design.Wanajua video editing.Wanajua kutumia software nyingi.Lakini miaka inaend...
12/06/2026

Kuna watu wana skills kali sana…

Wanajua design.
Wanajua video editing.
Wanajua kutumia software nyingi.

Lakini miaka inaenda… bado hawaendi mbali.

Wakati huo huo kuna mwingine ana skill za kawaida tu, lakini opportunities zinamfuata kila siku.

Kwanini?

Kwa sababu skill inaweza kukupa nafasi.

Lakini tabia ndiyo huamua utaendelea kuwepo au utaondoka.

Mteja anaweza kuvutiwa na kazi zako leo…

Lakini ataendelea kufanya kazi na wewe kwa sababu ya:
• Mawasiliano yako
• Nidhamu yako
• Muda wako
• Heshima yako
• Namna unavyoshughulikia kazi

Watu wengi wanataka kujifunza tools mpya kila siku…

Lakini hawataki kujifunza professionalism.

Unaweza kuwa designer mzuri sana lakini:
• Unachelewa kazi
• Hujibu message
• Ukikosolewa unakasirika
• Una-disappear bila taarifa

Mwisho wa siku clients wataondoka.

Kwa sababu kwenye ulimwengu wa kazi, tabia nzuri ni asset kubwa kuliko watu wengi wanavyofikiria.

Jifunze kufinish kazi hata k**a hauna mood.

Jifunze kusema ukweli mapema k**a umechelewa.

Jifunze kupokea feedback bila ego.

Jifunze kuheshimu muda wa watu.

Wateja wengi hawatafuti perfection.

Wanatafuta mtu wanayeweza kumuamini.

Skill hufungua mlango.

Lakini tabia ndiyo huamua k**a utaendelea kukaa ndani ya chumba hicho.

Ndio maana unaweza kuona watu wawili wana skill zinazofanana…

Lakini mmoja anapanda haraka kuliko mwingine.

Mwezi huu usijifunze software tu.

Jifunze pia attitude ya kazi.

Umejifunza jambo?

Comment:
“Nitabadilika.”

Kuna sababu kwanini baadhi ya Graphic Designers wanapata clients wa kulipa vizuri… na wengine wanabaki kutengeneza poste...
12/06/2026

Kuna sababu kwanini baadhi ya Graphic Designers wanapata clients wa kulipa vizuri… na wengine wanabaki kutengeneza poster za Tsh 2,000 kila siku.

Na mara nyingi tatizo sio skill ya design.

Tatizo ni kutokuelewa marketing.

Ngoja nikuulize swali moja:

Unapomtengenezea mteja poster, flyer au social media design…

Unajiuliza tu “imependeza?”

Au unauliza pia:

“Hii design itamsaidia mteja kupata matokeo?”

Hapo ndipo tofauti inaanza.

Kwa sababu biashara nyingi hazitafuti design nzuri pekee.

Zinataka design inayouza.

Mteja hajali sana umetumia font gani au ulikaa masaa mangapi Photoshop.

Anachotaka ni kuona:

• Watu wanabofya
• Wateja wanauliza
• Mauzo yanaongezeka
• Brand inaonekana professional

Na ili uweze kufanya hilo…

Lazima ujifunze marketing.

Kwa mfano:

Ukijua target audience ni nani, utaanza kuchagua colors, font na layout kwa akili zaidi.

Ukijua psychology ya kuuza, utaelewa kwanini baadhi ya posters zinavutia attention na zingine watu wanapita tu.

Ukijua call to action, utaacha kuandika maneno ya kawaida yasiyoleta action.

Utajifunza ku-design kwa malengo.

Sio kwa kupendeza tu.

Na ukweli ni huu:

Designer anayeelewa marketing huwa anauza huduma zake kwa bei kubwa zaidi.

Kwa sababu anakuwa sio “mtu wa kubuni”.

Anakuwa sehemu ya ukuaji wa biashara ya mteja.

Hata ukijua basics tu za marketing…

Target audience.
Brand positioning.
Copywriting.
Customer psychology.
Content strategy.

Tayari utakuwa hatua mbele kuliko designers wengi.

Ubunifu ni muhimu.

Lakini ubunifu unaoelewa biashara ndio unalipa zaidi.

Umejifunza jambo?

Comment: “Marketing matters” 👇

80% Ya Mafanikio Yako Ni MindsetMwaka 2018 nilihitimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Nilisoma BAED.Na jambo moja ambalo wa...
11/06/2026

80% Ya Mafanikio Yako Ni Mindset

Mwaka 2018 nilihitimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Nilisoma BAED.

Na jambo moja ambalo watu wengi hawajui ni kwamba…

Sikuwahi hata siku moja kuomba kazi ya ualimu.

Sio kwamba nilikosa nafasi.

Sio kwamba nilichukia taaluma.

Hapana.

Nilikuwa najua ninachotaka.

Na nilikuwa nimeamua mapema kwamba nataka kujenga kitu changu.

Nakumbuka kuna kipindi nilikuwa nimebakiza karibu Tsh 400,000 pekee kwenye account yangu.

Kwa watu wengi hiyo ingeonekana ni hela ya kujisitiri.

Ya kula.
Ya kupanga maisha kidogo.

Lakini nilifanya maamuzi ambayo wengi wangeona ni ya kijinga.

Niliamua kutumia pesa hiyo kujifunza skills.

Nilijua kitu kimoja:

K**a nitabadilisha maarifa yangu, maisha yangu yatabadilika.

Na ukweli ni kwamba…

Ndiyo maamuzi yaliyonifikisha hapa leo.

Sasa niseme kitu ambacho pengine hutaki kukisikia.

Baada ya kumaliza chuo au kujifunza skill yoyote…

Kuna njia mbili tu.

Ya kwanza:

Amua kujiajiri.

Ya pili:

Tafuta ajira.

Tatizo la vijana wengi ni kutokuwa clear wanataka nini.

Unakuta mtu anasema anataka biashara…

Lakini hafanyi chochote kinachomkaribisha kwenye biashara.

Hatunzi mtaji.

Hajifunzi skill.

Hajitengenezei mazingira.

Anasubiri motivation.

Ukichagua kujiajiri…

Fanya kila kinachowezesha hilo litokee.

Tumia muda wako vizuri.

Tafuta maarifa.

Nunua vifaa vinavyohitajika.

Tafuta watu sahihi wa kushirikiana nao.

Halafu anza.

Usisubiri kila kitu kikamilike.

Anza na kidogo.

Lakini anza.

Na k**a umeamua kuajiriwa…

Hakuna shida kabisa.

Hiyo pia ni njia nzuri.

Lakini fanya kila kinachotakiwa ili uajiriwe.

Jifunze skill inayotakiwa sokoni.

Tengeneza portfolio.

Fanya kazi hata za sample.

Onyesha unaweza kufanya nini.

Apply kazi online.

Tembea kutafuta opportunities physically.

Jionyeshe.

Tatizo ni kwamba watu wengi wanapenda excuses kuliko solutions.

“Mara kujiajiri ni kugumu…”

“Mara huwezi kuanza bila milioni 10…”

“Mara kodi ni nyingi…”

“Mara freelancing ukikosa kazi miezi mitatu?”

Ukikaa na hizo stori…

Utazeeka nazo.

Vile vile acha mindset ya:

“Siku hizi ajira hakuna.”

Swali ni…

Hakuna kwa nani?

Kwa sababu kila siku kuna watu wanaajiriwa.

Kuna watu wanapanda vyeo.

Kuna watu wanahama kampuni moja kwenda nyingine.

Maisha yanaendelea.

Usifanye malalamiko ya watu yawe ukweli wa maisha yako.

Amini kwamba unaweza kutoboa kwenye kile ulichochagua.

Lakini kabla ya pesa…

Kabla ya opportunity…

Kabla ya breakthrough…

Badilisha mindset.

Kwa sababu mara nyingi maisha hubadilika pale mtu anapoamua kufikiria tofauti.

Let me know kwenye comments…

Unaamini mindset inaweza kubadilisha maisha au ni hard work pekee?

VIBE CODING NI NINI? NA JE, UNAWEZA KUTENGENEZA PESA KUPITIA HUU UJUZI?Kwa miaka mingi, watu wengi walikuwa wanaamini kw...
10/06/2026

VIBE CODING NI NINI? NA JE, UNAWEZA KUTENGENEZA PESA KUPITIA HUU UJUZI?

Kwa miaka mingi, watu wengi walikuwa wanaamini kwamba ili utengeneze website au app lazima ujue coding ngumu sana.

Lakini sasa kuna kitu kinaitwa:

Vibe Coding.

Kwa lugha rahisi…

Vibe Coding ni njia ya kutengeneza website, app au software kwa kutumia AI kwa kuelezea tu unachotaka kwa maandishi badala ya kuandika code nyingi mwenyewe.

Mfano:

Unaweza kuandika:

“Nitengenezee website ya hotel yenye booking system, gallery, about us na contact page.”

AI ikaandika sehemu kubwa ya code au ika-build structure ya website hiyo.

Kwa maana nyingine…

Unaelekeza idea.

AI inakusaidia kujenga.

Sasa tools gani zinatumika kwenye Vibe Coding?

Hizi ni baadhi ya tools maarufu:

• beginner-friendly kwa kutengeneza apps bila complexity kubwa ya coding
• Lovable – nzuri kwa web apps na landing pages
• Claude – kusaidia logic na coding explanation
• Bolt – kutengeneza apps kwa haraka
• Replit – coding na deployment online
• Cursor – AI code editor powerful sana
• Claude – kusaidia logic na coding explanation
• ChatGPT – kupanga structure, debugging na code generation
• v0 by Vercel – UI design kwa prompt
• Windsurf – AI coding environment

Faida za Vibe Coding:

✅ Unaweza kutengeneza project haraka sana
✅ Beginner anaweza kuanza mapema
✅ Inapunguza muda wa coding
✅ Unaweza kufanya freelancing mapema
✅ Inarahisisha kujenga MVP (prototype ya app/business idea)

Lakini kuna misconception kubwa sana:

Watu wanafikiri…

“Sasa coding imekufa.”

No.

Huo ndio ukweli ambao wengi hawataki kuusikia.

AI inaweza kusaidia coding.

Lakini bado unahitaji kufahamu:
• Logic ya website/app
• Problem solving
• Basic HTML/CSS/UX
• Jinsi ya ku-debug errors
• Jinsi ya kuelekeza AI vizuri

Ukikosa msingi…

Utakwama pale AI inapokosea.

Sasa swali kubwa:

Je programmer atapotea?

Hapana.

Lakini programmer ambaye hatumii AI anaweza kubaki nyuma.

Future inaonekana kuwa:

Developer + AI > Developer bila AI

Ukianza leo, hii inaweza kuwa roadmap yako ya siku 90:

Month 1:
Jifunze basics za websites:
HTML, CSS, structure ya websites, UI basics.

Month 2:
Anza kutumia tools k**a ChatGPT, Cursor, Lovable au Replit kujenga simple projects.

Month 3:
Jenga portfolio:
Landing pages, business websites, simple systems.

Then anza kutafuta clients.

Unaweza monetize skill hii kwa:
• Kutengeneza websites za biashara
• Landing pages
• Freelancing online
• SaaS ideas
• Selling templates
• Website maintenance

Na ukweli ni huu:

Hii inaweza kuwa moja ya high income digital skills za miaka ijayo.

Lakini usisubiri ukamilike kujifunza kila kitu.

Anza.

Jifunze kidogo kidogo.

Technology haisubiri mtu.

Niambie kwenye comments:

Je, ungependa nijieleze zaidi kuhusu roadmap ya kujifunza Vibe Coding?

Jifunze Ujuzi wa Kidigitali na Ujiongezee Fursa za KipatoHapa Joel Media tunatoa mafunzo ya vitendo yanayokusaidia kujif...
07/06/2026

Jifunze Ujuzi wa Kidigitali na Ujiongezee Fursa za Kipato

Hapa Joel Media tunatoa mafunzo ya vitendo yanayokusaidia kujifunza ujuzi wa kisasa wenye uhitaji mkubwa kwenye soko la ajira na kujiajiri.

Kozi Zetu Zinazopatikana:

💻 Computer Course
Tsh 300,000 — Mwezi 1

🎨 Graphics Design
Tsh 500,000 — Miezi 3

🎥 Video Content Creation
Tsh 500,000 — Miezi 3

🌐 Website Design
Tsh 500,000 — Miezi 3

📈 Digital Marketing
Tsh 500,000 — Miezi 3

🛠 Signage Branding Course
Tsh 250,000 — Wiki 2

📍 Tunapatikana: Ubungo External, Dar es Salaam

📞 Mawasiliano:
+255 627 150 780
+255 745 152 680

Tufollow pia kwenye social media kujifunza zaidi kuhusu digital skills, technology na fursa za kujiajiri.

Joel Kadaga
Joel Media

05/06/2026

Jifunze Ujuzi wa Kidigitali na Ujiongezee Fursa za Kipato

Hapa Joel Media tunatoa mafunzo ya vitendo yanayokusaidia kujifunza ujuzi wa kisasa wenye uhitaji mkubwa kwenye soko la ajira na kujiajiri.

Kozi Zetu Zinazopatikana:

💻 Computer Course
Tsh 300,000 — Mwezi 1

🎨 Graphics Design
Tsh 500,000 — Miezi 3

🎥 Video Content Creation
Tsh 500,000 — Miezi 3

🌐 Website Design
Tsh 500,000 — Miezi 3

📈 Digital Marketing
Tsh 500,000 — Miezi 3

🛠 Signage Branding Course
Tsh 250,000 — Wiki 2

📍 Tunapatikana: Ubungo External, Dar es Salaam

📞 Mawasiliano:
+255 627 150 780
+255 745 152 680

Tufollow pia kwenye social media kujifunza zaidi kuhusu digital skills, technology na fursa za kujiajiri.

Joel Kadaga
Joel Media

Let’s Talk About Website Design Using AI ToolsKwa muda sasa, dunia ya website design imebadilika sana.Leo hii unaweza ku...
04/06/2026

Let’s Talk About Website Design Using AI Tools

Kwa muda sasa, dunia ya website design imebadilika sana.

Leo hii unaweza kubuild website au landing page nzuri kwa kutumia AI tools ndani ya muda mfupi sana kuliko zamani.

Kuna tools nyingi zinazotumika, lakini binafsi kwa sasa nimekuwa nikitumia sana:
• Stitch by Google
• Lovable

Na ukweli ni kwamba…

Matokeo yake ni mazuri sana.

Unaweza ku-build:
✅ Website pages
✅ Website copy/content
✅ Landing pages
✅ UI layout
✅ Full website ideas kuanzia mwanzo mpaka mwisho

Lakini kuna kitu muhimu nataka ujue:

AI haimaanishi umeacha kuwa website designer.

Badala yake…

Inakurahisishia kazi.

Binafsi bado natumia sana WordPress, na moja ya kitu ninachopenda kuhusu hizi AI tools ni kwamba ni very simple ku-integrate na WordPress kwa click chache sana.

Hii ina maana unaweza kutengeneza website kwa haraka zaidi, kupunguza muda wa kazi na kuongeza uwezo wa kuchukua projects nyingi zaidi.

Na k**a unapenda kuingia kwenye ulimwengu wa website design…

Hii inaweza kuwa nafasi nzuri sana kwako.

Kumbuka:

Website Design ni moja ya high income skills.

Kwa project moja tu unaweza kutengeneza kuanzia Tsh 800,000 na kuendelea kutegemea ukubwa wa kazi.

Na kwa uwepo wa AI tools hizi…

Project ambayo zamani ilichukua wiki kadhaa, leo unaweza kuikamilisha ndani ya siku 2–3 pekee.

Ukijumlisha gharama za tools na hosting, wakati mwingine unaweza kuanza kwa gharama isiyozidi Tsh 200,000.

Lakini siri kubwa si kuwa na tool.

Siri ni kujifunza:
• Structure ya website
• Layout & UX
• Copywriting basics
• WordPress
• Jinsi ya kutatua tatizo la biashara kupitia website

Tool pekee haitoshi.

Skill ndiyo inalipa.

K**a unapenda kufanya kazi online, freelancing au kujenga career kwenye digital skills…

Website Design ni moja ya skills ambazo ningependekeza uzitazame kwa umakini.

Niambie kwenye comments:

Je, ungependa kujifunza website design kwa kutumia AI + WordPress?

Andika Neno Web Design nitaandaa tutorial ya hatua kwa hatua

K**a wewe ni Graphic Designer au Content Creator, kuna kitu kimoja kitakachokufanya uaminike kwa wateja haraka sana:Port...
03/06/2026

K**a wewe ni Graphic Designer au Content Creator, kuna kitu kimoja kitakachokufanya uaminike kwa wateja haraka sana:

Portfolio.

Ukweli ni kwamba…

Mteja haamini maneno.

Anaamini kile anachokiona.

Unaweza kusema:
“Mimi ni designer mzuri sana.”

Lakini swali la kwanza la mteja litakuwa:

“Tuonyeshe kazi zako.”

Hapo ndipo umuhimu wa portfolio unapokuja.

Sasa tuanze na swali muhimu:

Portfolio ni nini?

Kwa lugha rahisi, portfolio ni muunganiko wa kazi zako ulizowahi kufanya.

Yaani sehemu ambayo inaonyesha uwezo wako.

Inaweza kuwa:
• Posters ulizotengeneza
• Flyers
• Banners
• Stickers
• Logo designs
• Company profiles
• Social media posts
• Branding projects

Portfolio inamsaidia mteja kuona:

“Nikimpa huyu kazi, ana uwezo wa kunipa matokeo gani?”

Na ukweli ni huu:

K**a designer huna portfolio…

Wateja wengi watakuwa wagumu kukuamini.

Sasa swali ni:

Unaweza kuonyesha portfolio yako kupitia njia gani?

Hizi ni baadhi ya njia nzuri:

✅ WhatsApp Catalog
Unaweka huduma zako pamoja na sample za kazi.

✅ Instagram Page
Page yako iwe k**a showroom ya kazi zako.

✅ PDF Document
Njia professional zaidi. Unaweka bio yako pamoja na kazi ulizofanya kisha unashare kwa client.

✅ Behance.net
Moja ya platform kubwa kwa designers kuonyesha kazi zao professionally.

✅ Website yako binafsi
Hii ndiyo level nyingine. Inaonyesha professionalism kubwa sana na huongeza credibility.

Naomba nikwambie kitu muhimu sana:

Acha tabia ya kutafuta kazi halafu unatuma screenshots random kwa mteja.

Mara nyingi hii inaonekana sio professional.

Inaonyesha hujajiandaa vizuri na hujichukulii kazi kwa seriousness.

Portfolio nzuri ina faida nyingi:

• Inakufanya uonekane mtaalamu
• Inaonyesha uko serious na kazi yako
• Inaongeza trust kwa wateja
• Inakusaidia kupata kazi hata ambazo mteja hakujua k**a unazifanya

Wakati mwingine mteja anaweza kukuuliza poster…

Lakini baada ya kuona portfolio yako anakupa:
Logo, branding, company profile au social media management.

Kwa sababu ameona uwezo wako.

Binafsi nimerekodi video nikielezea kwa ufasaha jinsi ya kutengeneza portfolio nzuri pamoja na njia hizi zote.

K**a unataka kuona video hiyo, andika:

PV (Portfolio Video)

Nitakutumia ujifunze zaidi.

Let me know k**a makala hii imekusaidia.

Joel Kadaga
Joel Media

Does Font Real  MattersTukiwa wakweli kuna wakati font pekee inaweza kuifanya design ikaanza kupop bila hata kuwa na mam...
03/06/2026

Does Font Real Matters

Tukiwa wakweli kuna wakati font pekee inaweza kuifanya design ikaanza kupop bila hata kuwa na mambo mengi

Hizi hapa leo ni font kali ambazo unaweza kuzichagua na kutumia kwenye project zako slide kulia kutazama sambamba na matumizi yake

Tuma neno FONT Ikiwa utapenda nikutumie

See What we Do More

1. Branding Services :
2. Main Account :
3. Mafunzo :
4. Production Accessories :
5. Youtube: Joel Media
5. Partner Project:
Excel Worksheets:

How to Market Yourself as a Graphic Designer (Especially K**a Una Anza)Moja ya changamoto kubwa kwa graphic designers we...
02/06/2026

How to Market Yourself as a Graphic Designer (Especially K**a Una Anza)

Moja ya changamoto kubwa kwa graphic designers wengi siyo kujua design.

Ni kujua namna ya kupata wateja.

Watu wengi wanajifunza Photoshop, Illustrator, Canva, wanajua kutengeneza poster nzuri, logo nzuri, flyer nzuri…

Lakini hawaelewi:

“Sasa watu watanijuaje?”

Kwanza kabisa, unatakiwa ujue kwamba kwenye industry ya Graphics Design kuna niche nyingi sana.

Usifanye kosa la kutaka kufanya kila kitu ukiwa unaanza.

Unaweza kufanya:
* Branding & Promotion Design
* Social Media Design
* Logo & Brand Identity
* Packaging Design
* Printing Design
* UI/Web Design
* Motion Graphics
* Signage & Large Format Design

Sasa kosa ambalo wengi wanafanya ni hili:

Wanataka kuwa kila kitu kwa wakati mmoja.

Leo anapost logo.
Kesho wedding card.
Kesho kutwa website.
Baadae motion graphics.

Mteja anashindwa kukuelewa.

Wateja wanapaswa wakujue k**a nani?

Jiulize:

“Nataka watu wanikumbuke kwa kazi gani?”

Kwa mfano ukichagua niche ya Branding & Promotion Design, basi jenga identity yako hapo.

Post:
✅ Stickers
✅ Banners
✅ Flyers
✅ Posters
✅ Shop branding

Hii inarahisisha sana kujiposition k**a brand.

Baada ya kuchagua niche…

Hatua inayofuata ni portfolio.

Na hapa wengi wanakosea.

Usisubiri mteja kwanza ndipo uwe na kazi za kuonyesha.

Tengeneza kazi hata k**a ni sample projects.

K**a niche yako ni branding:

Tengeneza:

Sticker design za biashara tofauti
Banners
Product labels
Promotional graphics

Halafu anza kuzipost.

Lakini kuna trick muhimu sana:

Don’t only post work. Post WORKING.

Watu wanataka kuona process.

Piga picha au video:

Ukiwa unaedit
Ukiwa printer
Ukiwa una-install branding
Ukiwa na client meeting
Ukiwa unapima banner

Hii hujenga trust kubwa sana.

Kwa sababu ukweli ni huu:

Watu hawaamini kazi pekee. Wanaamini process.

Baada ya hapo…

Sasa ni muda wa kutafuta wateja.

Bahati nzuri leo kuna njia mbili kubwa:

1. Social Media Marketing

Instagram
Facebook
TikTok
WhatsApp Status

Lakini ukiwa unaanza…

Mimi ningependekeza direct sales (physical marketing).

Kwa nini?

Kwa sababu inajenga trust haraka.

Andaa vipeperushi vizuri vinavyoonyesha:

Huduma zako
Portfolio yako
Mawasiliano yako

Then tembelea biashara.

Target:
* Salons
* Maduka ya simu
* Maduka ya kutoa na kuweka pesa
* Clinics & Pharmacies
* Restaurants
* Boutique
* Hardware
* SMEs nyingi ndogo ndogo

Biashara nyingi zina branding mbovu.

Na hiyo ndiyo opportunity yako.

Usiende kuuza tu.

Nenda kutatua tatizo.

Mwambie:

“Nimeona branding yenu inaweza kuboreshwa ili muonekane professional zaidi.”

Hapo tayari unafungua mazungumzo.

Sasa hapa ndipo watu wengi wanafeli…

Wanafanya marketing kwa wiki moja wakikosa wateja wanakata tamaa.

No.

Tenga muda wa angalau miezi 3 mfululizo.

Amua kufanya marketing:
Siku 3–4 kwa wiki.

Ukifanya hivyo consistently…

Kwa hesabu ya kawaida, utawafikia watu wengi sana.

Na kuna uwezekano mkubwa ukawa busy kiasi cha kushindwa kuhudumia clients wote.

…kwahiyo utaamua kufunga biashara.

Kidding 😄

Lakini serious consistency ndiyo kila kitu.

Na k**a unatamani kuingia kwenye dunia ya Graphics Design kwa njia sahihi, tuna darasa jipya la Graphics Design linaloanza June 08.

Utajifunza:
✅ Design Fundamentals
✅ Adobe Photoshop
✅ Adobe Illustrator
✅ Portfolio Building
✅ Jinsi ya kupata wateja

📍 Ubungo External – Dar es Salaam
🗓️ Kwa miezi 3

K**a utapenda kujiunga, unaweza kujisajili kabla nafasi hazijajaa.

Niambie kwenye comments, unadhani changamoto kubwa ya graphic designers wengi ni nini — kupata wateja au kujua kazi?

Address

Ubungo External Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 06:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Joelmedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share