Data Sports Tv

Data Sports Tv Habari za Michezo| Uchambuzi wa Mechi.

Datasports TV Tunakuletea Uchambuzi wa kina baada ya mechi, Taarifa Sahihi na Exclusive Interviews na wadau nguli wa Michezo.

Klabu ya Yanga Imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji raia wa Uganda, Allan Okello kwa Mkataba wa miaka miwili na nusu...
12/01/2026

Klabu ya Yanga Imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji raia wa Uganda, Allan Okello kwa Mkataba wa miaka miwili na nusu akitokea Vipers FC ya nchini Uganda.

Okello amewahi kuvitumikia vilabu vya KCCA ya nchini Uganda pamoja na Padarou ya nchini Algeria.

✍️

Kocha wa Klabu ya Azam  Flotent Ibenge akizungumuza na waandishi wa habari kuelekea Mchezo wa kesho kati ya Azam FC dhid...
12/01/2026

Kocha wa Klabu ya Azam Flotent Ibenge akizungumuza na waandishi wa habari kuelekea Mchezo wa kesho kati ya Azam FC dhidi ya Yanga Amesema kuwa

"Tunajua Yanga ndiyo timu bora zaidi Tanzania kwa sasa, lakini sisi tutakuwa bora zaidi yao"

Kocha wa Azam FC, Florent Ibenge amesema wako tayari kwa fainali na wamejiandaa kuwa bora zaidi uwanjani kuliko wapinzani wao.

Ibenge amesema wachezaji wote wako tayari kwa mechi na wote anawaamini.

Nawaamini wachezaji wangu wote, Napenda kila mchezaji acheze, Sipendi kuwa na timu inayomtegemea mchezaji mmoja, kwamba asipokuwepo yeye, basi timu nzima inakufa.

Fainali ni kesho Januari 13 saa 10:30 jioni, Azam FC vs Yanga,SC, Gombani Pemba.

Young Africans  bado haijakamilisha uhamisho wa Marouf Tchakei (30)  kutoka Singida Black Stars. Tchakei alikuwa anataza...
10/01/2026

Young Africans bado haijakamilisha uhamisho wa Marouf Tchakei (30) kutoka Singida Black Stars.

Tchakei alikuwa anatazamwa na kocha Pedro Gonçalves kwenye Mapinduzi Cup .Hivi taarifa yake itatolewa na Yanga muda wowote .

✍️ Hassan Sadam

Klabu ya Azam FC imekamilisha usajili wa mshambuliaji, Aimar Hafidh Abubakar 'Halaand', akitokea klabu ya Mlandege ya Za...
10/01/2026

Klabu ya Azam FC imekamilisha usajili wa mshambuliaji, Aimar Hafidh Abubakar 'Halaand', akitokea klabu ya Mlandege ya Zanzibar.

Abubakar amesaini kandarasi ya miaka (2) kuwatumikia Azam FC hadi 2028.

✍️

Baada ya klabu ya Yanga kufanikisha usajili wa Allan Okello kutokea Vipers FC ya nchini Uganda inaelezwa kuwa nyota huyo...
10/01/2026

Baada ya klabu ya Yanga kufanikisha usajili wa Allan Okello kutokea Vipers FC ya nchini Uganda inaelezwa kuwa nyota huyo atatua nchini Tanzania siku Jumatatu, Januari 12.

Aidha, kiasi ambacho kinatajwa kutumika kumsajili Okello ni Tsh Milioni 693/= za Kitanzania.

Huku akisaini kandarasi ya miaka (2) na Miezi (6).

✍️

Taarifa zinaeleza kuwa kocha wa klabu ya  Mamelodi Sundowns chini ya miaka 19 (U19) Kristopher Bergman atajiunga na Simb...
10/01/2026

Taarifa zinaeleza kuwa kocha wa klabu ya Mamelodi Sundowns chini ya miaka 19 (U19) Kristopher Bergman atajiunga na Simba SC ili kuongeza nguvu kwenye benchi la ufundi chini ya Steve Barker.

Bergman tayari amemalizana na Mamelodi, Mazungumzo na Simba SC nayo yamekamilika.

✍️

Haya hapa timu za taifa (7) ambazo zimecheza michezo mingi zaidi pasipo kupoteza mchezo wowote.Kwenye rekodi hiyo timu y...
10/01/2026

Haya hapa timu za taifa (7) ambazo zimecheza michezo mingi zaidi pasipo kupoteza mchezo wowote.

Kwenye rekodi hiyo timu ya taifa ya Italia ndio vinara wakiwa hawajafungwa mechi (37) kuanzia 2018 hadi 2021.

Italia - Mechi 37 (2018 hadi 2021)
Argentina - Mechi 36 (2019 hadi 2022)
Algeria - Mechi 35 (2018 hadi 2021)
Hispania - Mechi 35 (2007 hadi 2009)
Brazil - Mechi 35 (1993 hadi 1996)
Morocco - Mechi 31 (2023 hadi sasa)
Ufaransa - Mechi 30 (1994 hadi 1996)

✍️

Tayari mataifa (2) yamefuzu hatua ya nusu fainali na yanasubiri wapinzani ambao watacheza nao kwenye hatua hiyo.Morocco ...
10/01/2026

Tayari mataifa (2) yamefuzu hatua ya nusu fainali na yanasubiri wapinzani ambao watacheza nao kwenye hatua hiyo.

Morocco - Wanasubiri mshindi kati ya Nigeria au Algeria.

Senegal - Wanasubiri mshindi kati ya Misri au Ivory Coast.

Michezo ya Nusu fainali itachezwa Januari 14, huku mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu unatarajiwa kufanyika Januari 17.

Na fainali ya michuano ya AFCON 2025 itafanyika Januari 18,2025 kwenye dimba la Prince Moulay Abdellah Stadium,Rabat nchini Morocco.

✍️

10/01/2026
  Taarifa zinaeleza kuwa kiungo wa klabu ya Simba Mzamiru Yassin amekamilisha uhamisho wake kujiunga na klabu ya TRA Uni...
10/01/2026

Taarifa zinaeleza kuwa kiungo wa klabu ya Simba Mzamiru Yassin amekamilisha uhamisho wake kujiunga na klabu ya TRA United.

Mzamiru amaesaini mkataba wa miaka (2) kuwatumikia "Wakusanya Mapato".

Ikumbukwe kuwa Mzamiru alijiunga na Wekundu wa Msimbazi mwaka 2016 akitokea Mtibwa Sugar na amehudumu ndani ya kikosi hicho kwa miaka (10).

✍️

Klabu ya Yanga imewaita mezani watu binafsi, mashirika na wadau wote kuwekeza katika mradi wa ujenzi wa Uwanja Jangwani....
09/01/2026

Klabu ya Yanga imewaita mezani watu binafsi, mashirika na wadau wote kuwekeza katika mradi wa ujenzi wa Uwanja Jangwani.

Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limefanya mabadiliko ya ghafla ya mwamuzi wa mchezo wa robo fainali ya AFCON kati ya Mor...
09/01/2026

Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limefanya mabadiliko ya ghafla ya mwamuzi wa mchezo wa robo fainali ya AFCON kati ya Morocco na Cameroon. Wamemuondoa Amine Omar wa Misri - aliyewahi kuchezesha Dabi ya Kariakoo - na kumteua Dehane Beida wa Mauritania baada ya Morocco kulalamika rasmi.

Uteuzi wa Beida umezua gumzo Tanzania kwa sababu ana rekodi ya "kuzichafulia" timu za Tanzania kwa maamuzi yenye utata. Alishachezesha Simba SC dhidi ya Al Ahly, Yanga dhidi ya USM Alger, na hata timu ya taifa ya Taifa Stars. Hii inamfanya kuwa mwamuzi "hatari" kwa Morocco!

Address

Mabibo External
Dar Es Salaam
NON

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Data Sports Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Data Sports Tv:

Share