AWR Tanzania

AWR Tanzania Sikiliza Sauti ya Matumaini AWR Tanzania (Morning Star Radio zamani). ujumbe wa matumaini kwa watu wote.

Njozi za kuanzishwa kwa Radio hii, zilianza mnamo miaka ya tisini, ambapo mwaka 2000 viongozi wa makanisa ya Dar es salaam walikutana na kuweka mkakati madhubuti ya kuanzisha radio,kwa wakati huo ikijulikana k**a TAWR (Tanzania Adventist World Radio). Mwaka 2001, uchunguzi yakinifu wa kuanzishwa kwa Kituo hiki ulianza chini ya kitengo cha mawasiliano cha Makao makuu ya Kanisa Tanzania kijulikanach

o k**a TAMC (Tanzania Adventist Media Center). Baada ya mikakati madhubuti kukamilika, ujenzi wa kituo cha radio ulianza rasmi mnamo mwaka 2002, katika eneo la Mikocheni B, jijini Dar es salaam, ujenzi ambao uliendelea na kukamilika kwa sehemu kubwa mnamo mwaka 2003. Mnamo tarehe moja mwezi wa kumi mwaka 2003, kituo kilirusha matangazo yake kwa mara ya kwanza k**a
majaribio, kwa kutumia mtambo wa kurushia matangazo wenye uwezo wa watt 500, na tangu hapo safari ya
matangazo kusikika hewani iliendelea! Mwezi wa kumi na moja mwaka wa 2003, kituo kilifunguliwa rasmi na Mgeni aliyehudhuria
shughuli hiyo, Mchungaji Jan Paulsen, akija k**a Rais wa kanisa la Waadventista wasabato
Duniani, akitoea Nchini Marekani ambako ndiko makao makuu ya Kanisa Duniani, yalipo. Majuma mawili baada ya kufunguliwa rasmi kwa kituo, Mtambo wa kurushia matangazo
uliokuwa umefungwa mikocheni B mahali zilipo studio, ulishindwa kufanya kazi
kutokana na hitilafu iliyosababishwa na umeme, tatizo lililojitokeza baada ya mvua kali kunyesha. Jitihada za kujaribu kuirejesha katika hali ya kuendelea kufanya kazi zilishindikana,
jambo lililopelekea muingiliano na vyombo vingine vya habari, na kituo kufungwa kwa muda
na tume ya mawasilianona, ili kutoa nafasi ya kufanyika kwa marekebisho. Kituo kilirejea
tena katika hali yake na kuendelea na matangazo baada ya miaka miwili baadae. Mwaka 2005 mwezi wa tano,vifaa vipya vya kurushia matangazo viliagizwa ili kurejesha matangazo tena. Uagizaji huo
ulichukua muda wa miezi mitatu, na mwezi wa nane vifaa viliwasili na ufungaji ukaanza mara moja, wakati huu mtambo
ukiwa umehamishiwa eneo la kisarawe, mkoa wa Pwani. Baada ya ufungaji mtambo kukamilika, mnamo mwezi wa nane mwaka 2005, urushaji wa matangazo ya majaribio
ulianza mara moja, ambapo majaribio hayo yalichukua takribani mwezi mmoja, hadi mnamo mwezi wa tisa! Ilipofika tarehe 26, mwezi wa tano mwaka 2006, saa 11:00 jioni, kituo kilirusha
matangazo moja kwa moja kwa mara ya kwanza, baada ya matangazo ya majaribio
kukamilika! Tangu hapo, Morning Star Radio imeendelea kurusha matangazo yake hadi hivi sasa,
ambapo watu mbali mbali wamekuwa wakibarikiwa sana na matangazo haya, na kwa
hakika kituo hiki kimekuwa ni mbaraka sana kwa ma elfu ya wakaazi wa Tanzania
na dunia kwa ujumla ambapo matangazo
ya Redio hii yanasikika!

Heri ya Mwaka mpya.. 2026
31/12/2025

Heri ya Mwaka mpya.. 2026

Shukrani zetu hazitokani na hali tuliyonayo, bali na tabia ya Mungu wetu. Yeye ni mwema wakati wote, na upendo wake haui...
21/12/2025

Shukrani zetu hazitokani na hali tuliyonayo, bali na tabia ya Mungu wetu. Yeye ni mwema wakati wote, na upendo wake hauishi kamwe. Leo na daima, sifa zimstahili Bwana. ๐Ÿ™โœจ

Acha shukrani ziwe sauti ya moyo wako. Kabla ya kuangalia yaliyokosekana, kumbuka uliyofanyiwa. Mungu amekufanyia mengi ...
18/12/2025

Acha shukrani ziwe sauti ya moyo wako. Kabla ya kuangalia yaliyokosekana, kumbuka uliyofanyiwa. Mungu amekufanyia mengi usiyasahau. Sifa na shukrani humfungulia Mungu milango ya baraka mpya. ๐Ÿ™Œ๐Ÿ’›

Shukrani hubadilisha mtazamo wa moyo. Haijalishi unapitia nini leo, kuna sababu ya kumshukuru Mungu. Katika furaha na ch...
17/12/2025

Shukrani hubadilisha mtazamo wa moyo. Haijalishi unapitia nini leo, kuna sababu ya kumshukuru Mungu. Katika furaha na changamoto, shukrani hufungua mlango wa amani, imani, na baraka zaidi. โœจ๐Ÿ’›

Shukrani hufungua milango ya baraka na kuleta moyo karibu na Mungu. Unapoingia mbele zake kwa sifa na shukrani, unajaza ...
16/12/2025

Shukrani hufungua milango ya baraka na kuleta moyo karibu na Mungu. Unapoingia mbele zake kwa sifa na shukrani, unajaza nafsi yako furaha, amani, na uwepo Wake. Anza leo kwa kushukuruโ€”hapo ndipo ibada ya kweli huanzia. ๐Ÿ•Š๏ธ๐Ÿ’–

13/12/2025

Leo Kwenye Lulu za injili AWR Tanzania - Live na Chidach sda Choir- Dodoma
Historia ya Wimbo no 91
Abel Kinyongo
Saa 12:00 Jioni

Kila pumzi ni sababu ya kumshukuru Mungu! Wema Wake haujawahi kukoma, na fadhili Zake zinatufunika katika kila hatua ya ...
10/12/2025

Kila pumzi ni sababu ya kumshukuru Mungu! Wema Wake haujawahi kukoma, na fadhili Zake zinatufunika katika kila hatua ya safari. Leo, simama na moyo wa shukraniโ€”kwa neema iliyokuongoza, kwa rehema zilizokuokoa, na kwa upendo unaodumu milele. Mungu ni mwema, hata zaidi ya tunavyoweza kueleza! ๐Ÿ™Œ๐Ÿ’›

Usibebe mzigo peke yako! Badala ya wasiwasi kukuk**ata, peleka kila haja kwa Mungu kwa maombi, kwa kilio, kwa shukrani. ...
09/12/2025

Usibebe mzigo peke yako! Badala ya wasiwasi kukuk**ata, peleka kila haja kwa Mungu kwa maombi, kwa kilio, kwa shukrani. Kila unapotia jambo mikononi Mwake, amani Yake inaanza kutulia ndani yako. Leo, chagua kuachilia hofu na kukumbatia amani ya Mungu isiyoshindwa na chochote. ๐Ÿ™โœจ

Kila siku ni ushuhuda wa wema wa Mungu! Hata pale ambapo hatujaona majibu yote, fadhili Zake bado hazijawahi kukoma. Leo...
08/12/2025

Kila siku ni ushuhuda wa wema wa Mungu! Hata pale ambapo hatujaona majibu yote, fadhili Zake bado hazijawahi kukoma. Leo simama na moyo wa shukrani kwa neema, kwa uhai, kwa rehema zisizoisha. Mungu ni mwema, na wema wake haujawahi kupungua!

Mungu anakusimamisha juu ya msingi wa haki yake, si nguvu zako. Akikuinua, hakuna udhalimu utakaoharibu amani yako, na h...
01/12/2025

Mungu anakusimamisha juu ya msingi wa haki yake, si nguvu zako. Akikuinua, hakuna udhalimu utakaoharibu amani yako, na hakuna hofu itakayokukaribia. Wewe ni salama katika mikono ya Yule anayekulinda usiku na mchana. Tembea leo kwa ujasiri, ukijua kuwa Bwana ameweka ukuta wa amani kuizunguka maisha yako. โœจ๐Ÿ•Š๏ธ

Kuteseka kwa ajili ya kufanya lililo jema si hasara ni baraka. Wakati dunia inapoonekana kukukataa kwa sababu ya msimamo...
28/11/2025

Kuteseka kwa ajili ya kufanya lililo jema si hasara ni baraka. Wakati dunia inapoonekana kukukataa kwa sababu ya msimamo wako wa haki, Mungu anakukubali. Usiruhusu vitisho, maneno, au shinikizo za watu zikutikise.

Thamani yako imo mikononi mwa Mungu, si katika maoni ya wanadamu. Simama imara baraka zako hazitegemei watu, zinategemea Mungu anayekutetea.

Wakati moyo wako unajaribiwa na vitisho vya maisha, kumbuka hili: tumaini lako liko kwa Mungu asiyeweza kushindwa. Sauti...
25/11/2025

Wakati moyo wako unajaribiwa na vitisho vya maisha, kumbuka hili: tumaini lako liko kwa Mungu asiyeweza kushindwa. Sauti za hofu zinaweza kupaza kelele, lakini hazina nguvu juu ya mtu anayemtegemea Bwana. Ukiwa ndani ya mikono Yake, hakuna mwanadamu anayeweza kukuzuia, kukuangusha, au kukutenganisha na ushindi alioandaa kwako.

Address

P. O. BOX 77170
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AWR Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share