19/05/2026
MAFUNDISHO YA NJOMBE NET EVENT KUPAMBANUA IMANI YA KWELI NA KANISA LA KWELI- MH.ANTHONY MTAKA.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amesema Mafundisho ya Njombe Net Event yatapambanua ukweli na kanisa la kweli. Mheshimiwa mtaka ameyasema hayo leo May 09/05/2026 alipotembelea kituo kikuu cha mahubiri ya Njombe Net Event - Tumaini lenye Baraka unaondelea katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Njombe Mjini. Amesema kuna Mahubiri kwenye baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii yanayoendana na ramli chonganishi mahubiri hayo hayafai na siyo muhimu katika maisha ya Mwanadamu mcha Mungu.
Sambamba na hilo, Mheshimiwa mtaka amewapongeza wahudumu kwa masomo mbalimbali ya afya na familia yanayotolewa katika mkutano huo na kurushwa kote duniani, akieleza kuwa yana faida kwa jamii na maisha ya watu wengi.
Aidha ameahidi kuchangia sehemu ya mkutano huo kwa kugharimia usafiri,malazi na chakula kwaya ya Kurasini,Galilaya Central na Magomeni ili kuongeza nguvu siku ya kuhitimisha
mkutano huo.
Mkutano huo ambao Mhubiri mkuu ni Mch.Baraja Butoke,Mnenaji wa masomo ya familia ni Mch. Thomas Bihene na Masomo ya afya ni Dakitari Magomere ulianza mnamo tarehe 09/05/2026 na unaendelea hadi tarehe 30/05/2026 ukirushwa mbashari kila siku saa 11:00 jioni hadi saa 02:00 usiku kwenye vyombo mbalimbali vya habari: Hope Channel Tanzania,Awr Tanzania,Rock fm na mitandao mbalimbali ya kijamii.
Na Abel Kinyongo