AWR Tanzania

AWR Tanzania Sikiliza Sauti ya Matumaini AWR Tanzania (Morning Star Radio zamani). ujumbe wa matumaini kwa watu wote.

Njozi za kuanzishwa kwa Radio hii, zilianza mnamo miaka ya tisini, ambapo mwaka 2000 viongozi wa makanisa ya Dar es salaam walikutana na kuweka mkakati madhubuti ya kuanzisha radio,kwa wakati huo ikijulikana k**a TAWR (Tanzania Adventist World Radio). Mwaka 2001, uchunguzi yakinifu wa kuanzishwa kwa Kituo hiki ulianza chini ya kitengo cha mawasiliano cha Makao makuu ya Kanisa Tanzania kijulikanach

o k**a TAMC (Tanzania Adventist Media Center). Baada ya mikakati madhubuti kukamilika, ujenzi wa kituo cha radio ulianza rasmi mnamo mwaka 2002, katika eneo la Mikocheni B, jijini Dar es salaam, ujenzi ambao uliendelea na kukamilika kwa sehemu kubwa mnamo mwaka 2003. Mnamo tarehe moja mwezi wa kumi mwaka 2003, kituo kilirusha matangazo yake kwa mara ya kwanza k**a
majaribio, kwa kutumia mtambo wa kurushia matangazo wenye uwezo wa watt 500, na tangu hapo safari ya
matangazo kusikika hewani iliendelea! Mwezi wa kumi na moja mwaka wa 2003, kituo kilifunguliwa rasmi na Mgeni aliyehudhuria
shughuli hiyo, Mchungaji Jan Paulsen, akija k**a Rais wa kanisa la Waadventista wasabato
Duniani, akitoea Nchini Marekani ambako ndiko makao makuu ya Kanisa Duniani, yalipo. Majuma mawili baada ya kufunguliwa rasmi kwa kituo, Mtambo wa kurushia matangazo
uliokuwa umefungwa mikocheni B mahali zilipo studio, ulishindwa kufanya kazi
kutokana na hitilafu iliyosababishwa na umeme, tatizo lililojitokeza baada ya mvua kali kunyesha. Jitihada za kujaribu kuirejesha katika hali ya kuendelea kufanya kazi zilishindikana,
jambo lililopelekea muingiliano na vyombo vingine vya habari, na kituo kufungwa kwa muda
na tume ya mawasilianona, ili kutoa nafasi ya kufanyika kwa marekebisho. Kituo kilirejea
tena katika hali yake na kuendelea na matangazo baada ya miaka miwili baadae. Mwaka 2005 mwezi wa tano,vifaa vipya vya kurushia matangazo viliagizwa ili kurejesha matangazo tena. Uagizaji huo
ulichukua muda wa miezi mitatu, na mwezi wa nane vifaa viliwasili na ufungaji ukaanza mara moja, wakati huu mtambo
ukiwa umehamishiwa eneo la kisarawe, mkoa wa Pwani. Baada ya ufungaji mtambo kukamilika, mnamo mwezi wa nane mwaka 2005, urushaji wa matangazo ya majaribio
ulianza mara moja, ambapo majaribio hayo yalichukua takribani mwezi mmoja, hadi mnamo mwezi wa tisa! Ilipofika tarehe 26, mwezi wa tano mwaka 2006, saa 11:00 jioni, kituo kilirusha
matangazo moja kwa moja kwa mara ya kwanza, baada ya matangazo ya majaribio
kukamilika! Tangu hapo, Morning Star Radio imeendelea kurusha matangazo yake hadi hivi sasa,
ambapo watu mbali mbali wamekuwa wakibarikiwa sana na matangazo haya, na kwa
hakika kituo hiki kimekuwa ni mbaraka sana kwa ma elfu ya wakaazi wa Tanzania
na dunia kwa ujumla ambapo matangazo
ya Redio hii yanasikika!

19/05/2026

MAFUNDISHO YA NJOMBE NET EVENT KUPAMBANUA IMANI YA KWELI NA KANISA LA KWELI- MH.ANTHONY MTAKA.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amesema Mafundisho ya Njombe Net Event yatapambanua ukweli na kanisa la kweli. Mheshimiwa mtaka ameyasema hayo leo May 09/05/2026 alipotembelea kituo kikuu cha mahubiri ya Njombe Net Event - Tumaini lenye Baraka unaondelea katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Njombe Mjini. Amesema kuna Mahubiri kwenye baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii yanayoendana na ramli chonganishi mahubiri hayo hayafai na siyo muhimu katika maisha ya Mwanadamu mcha Mungu.
Sambamba na hilo, Mheshimiwa mtaka amewapongeza wahudumu kwa masomo mbalimbali ya afya na familia yanayotolewa katika mkutano huo na kurushwa kote duniani, akieleza kuwa yana faida kwa jamii na maisha ya watu wengi.
Aidha ameahidi kuchangia sehemu ya mkutano huo kwa kugharimia usafiri,malazi na chakula kwaya ya Kurasini,Galilaya Central na Magomeni ili kuongeza nguvu siku ya kuhitimisha
mkutano huo.
Mkutano huo ambao Mhubiri mkuu ni Mch.Baraja Butoke,Mnenaji wa masomo ya familia ni Mch. Thomas Bihene na Masomo ya afya ni Dakitari Magomere ulianza mnamo tarehe 09/05/2026 na unaendelea hadi tarehe 30/05/2026 ukirushwa mbashari kila siku saa 11:00 jioni hadi saa 02:00 usiku kwenye vyombo mbalimbali vya habari: Hope Channel Tanzania,Awr Tanzania,Rock fm na mitandao mbalimbali ya kijamii.
Na Abel Kinyongo

Redio ya Waadventista ulimwenguni nchini Tanzania(Awr Tanzania) Adventist World Radio Tanzania tunakupongeza Elder. Revo...
18/05/2026

Redio ya Waadventista ulimwenguni nchini Tanzania(Awr Tanzania) Adventist World Radio Tanzania tunakupongeza Elder. Revocatus Julius Mange kwa kuteuliwa kuwa (Treasurer) Mhazini mkuu wa Shirika la Vyombo vya habari vya kanisa la Waadventista wa Sabato Tanzania(TAMC).Mungu amekupatia nafasi hii muhimu ya kumtumikia.
Karibu sana,Mungu akuwezeshe kuyatenda yote kwa utukufu wake.

09/05/2026

SIKU YA KWANZA - NJOMBE NET EVENT 2026

https://youtube.com/live/O_GhOs7G390

Karibu katika Mfululizo wa Mahubiri ya NJOMBE NET EVENT 2026 yanayokujia mbashara KUTOKEA NJOMBE, ungana nasi Jioni hii na kushiriki mbaraka huu kwa kushare Link hii kwa ajili ya kuwafikia wengi, Masomo ya Afya, Masomo ya Familia na Mahubiri Makuu.

Bonyeza Link Hii >> https://youtube.com/live/O_GhOs7G390
kupata mahubiri kwa LUGHA YA KISWAHILI

Welcome to the NJOMBE NET EVENT 2026 Evangelistic Series, coming to you live from Njombe. Join us this evening and share this blessing by sharing this link to reach many more people. Featuring Health Lessons, Family Lessons, and Powerful Main Sermons.

Click This Link >> https://youtube.com/live/ubzzG4fUYEY
to watch the sermon in the ENGLISH language.

مرحبًا بكم في سلسلة الكرازة NJOMBE NET EVENT 2026 القادمة إليكم مباشرةً من نجومبي.�انضموا إلينا هذا المساء وشاركوا هذه البركة من خلال مشاركة هذا الرابط للوصول إلى أكبر عدد ممكن من الناس.�تتضمن السلسلة: دروسًا صحية، ودروسًا أسرية، وعظات رئيسية قوية.
اضغط على هذا الرابط >> https://youtube.com/live/O_GhOs7G390�لمشاهدة العظة باللغة الإنجليزية.

Endelea kufatilia Hope Channel Tanzania, AWR Tanzania na Rock FM Mbeya, na kupitia katika Mitandao yetu ya Kijamii.

🌅 Fadhili zake ni mpya kila asubuhi…— Maombolezo 3:23Haijalishi jana ilikuwaje…leo ni mwanzo mpya.Mungu hajamaliza na we...
28/04/2026

🌅 Fadhili zake ni mpya kila asubuhi…
— Maombolezo 3:23

Haijalishi jana ilikuwaje…
leo ni mwanzo mpya.

Mungu hajamaliza na wewe bado.
Kila siku analeta neema mpya, nguvu mpya, na tumaini jipya.

✨ Anza tena… kwa sababu Mungu bado yupo pamoja nawe.

🙏 Njombe NET Event 2026
📍 Njombe SDA
📅 09 Mei – 30 Mei

👉 Njoo upokee Tumaini Lenye Baraka.

Usikose mjadala huu wa kipekee kupitia Radio, AWR Tanzania,
17/03/2026

Usikose mjadala huu wa kipekee kupitia Radio, AWR Tanzania,

Thanks for being a top engager and making it on to my weekly engagement list! 🎉 Bujege Bujege, Enock Pharles, Edmin Kany...
17/03/2026

Thanks for being a top engager and making it on to my weekly engagement list! 🎉 Bujege Bujege, Enock Pharles, Edmin Kanyamile, Bihemo Mandelewa, Espelius Justine Mpongo, Tumaini Daudi, Titus Fideli Mhoza, Nehemia Leonard, Joshua Wafula, Lucas Sospeter

🌍 Injili ya Milele Iwahi kwa Ulimwengu WoteLeo tunaungana na Waadventista duniani kote katika Sabato Maalumu ya Adventis...
14/03/2026

🌍 Injili ya Milele Iwahi kwa Ulimwengu Wote

Leo tunaungana na Waadventista duniani kote katika Sabato Maalumu ya Adventist World Radio (AWR).

Kupitia redio na vyombo vya mawasiliano, injili inaendelea kufika mahali ambapo wahubiri hawawezi kufika — vijijini, milimani, jangwani, na hata katika maeneo ambayo kuhubiri hadharani ni vigumu.

✨ Watu wengi wamepata tumaini
✨ Vijiji vimebadilika
✨ Maelfu wamekubali Kristo

Na yote haya yanawezekana kwa sababu watu wa Mungu wameamua kushiriki katika utume huu.

🙏 Sadaka yako leo inaweza kusaidia mtu kusikia injili kwa mara ya kwanza.

Hebu tushiriki pamoja kupeleka tumaini kwa ulimwengu.

📻 AWR – Sauti ya Matumaini kwa Ulimwengu








13/03/2026

🌍 Injili ya Milele Iwahi kwa Ulimwengu Wote

Leo tunaungana na Waadventista duniani kote katika Sabato Maalumu ya Adventist World Radio (AWR).

Kupitia redio na vyombo vya mawasiliano, injili inaendelea kufika mahali ambapo wahubiri hawawezi kufika — vijijini, milimani, jangwani, na hata katika maeneo ambayo kuhubiri hadharani ni vigumu.

✨ Watu wengi wamepata tumaini
✨ Vijiji vimebadilika
✨ Maelfu wamekubali Kristo

Na yote haya yanawezekana kwa sababu watu wa Mungu wameamua kushiriki katika utume huu.

🙏 Sadaka yako leo inaweza kusaidia mtu kusikia injili kwa mara ya kwanza.

Hebu tushiriki pamoja kupeleka tumaini kwa ulimwengu.

📻 AWR – Sauti ya Matumaini kwa Ulimwengu








TANZIAMwenyekiti wa kanisa la Waadventista wa Sabato Nyanda za juu kusini mwa Tanzania Mch.Toto Ndege Bwire kusaga.Anata...
07/03/2026

TANZIA
Mwenyekiti wa kanisa la Waadventista wa Sabato Nyanda za juu kusini mwa Tanzania Mch.Toto Ndege Bwire kusaga.Anatangaza kifo cha Mch.Joseph T Msambwa wa Mtaa wa Malangali Wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya, kilichotokea tarehe 06/03/2026 mkoani Mbeya.
Mwenyekiti anaungana na familia,waumini na wote walioguswa na msiba huo.Mazishi yatafanyika siku ya Jumatatu tarehe 09/03/2026 Mkoani Njombe.
"Naye atafuta kila chozi katika macho yao"

Uzinduzi wa Njombe Net Event Leo tarehe 07/02/2026.NJOMBE NET EVENT 2026 - TUMAINI LENYE BARAKA.Usikose!
06/02/2026

Uzinduzi wa Njombe Net Event Leo tarehe 07/02/2026.
NJOMBE NET EVENT 2026 - TUMAINI LENYE BARAKA.
Usikose!

Address

P. O. BOX 77170
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AWR Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share