AWR Tanzania

AWR Tanzania Sikiliza Sauti ya Matumaini AWR Tanzania (Morning Star Radio zamani). ujumbe wa matumaini kwa watu wote.

Njozi za kuanzishwa kwa Radio hii, zilianza mnamo miaka ya tisini, ambapo mwaka 2000 viongozi wa makanisa ya Dar es salaam walikutana na kuweka mkakati madhubuti ya kuanzisha radio,kwa wakati huo ikijulikana k**a TAWR (Tanzania Adventist World Radio). Mwaka 2001, uchunguzi yakinifu wa kuanzishwa kwa Kituo hiki ulianza chini ya kitengo cha mawasiliano cha Makao makuu ya Kanisa Tanzania kijulikanach

o k**a TAMC (Tanzania Adventist Media Center). Baada ya mikakati madhubuti kukamilika, ujenzi wa kituo cha radio ulianza rasmi mnamo mwaka 2002, katika eneo la Mikocheni B, jijini Dar es salaam, ujenzi ambao uliendelea na kukamilika kwa sehemu kubwa mnamo mwaka 2003. Mnamo tarehe moja mwezi wa kumi mwaka 2003, kituo kilirusha matangazo yake kwa mara ya kwanza k**a
majaribio, kwa kutumia mtambo wa kurushia matangazo wenye uwezo wa watt 500, na tangu hapo safari ya
matangazo kusikika hewani iliendelea! Mwezi wa kumi na moja mwaka wa 2003, kituo kilifunguliwa rasmi na Mgeni aliyehudhuria
shughuli hiyo, Mchungaji Jan Paulsen, akija k**a Rais wa kanisa la Waadventista wasabato
Duniani, akitoea Nchini Marekani ambako ndiko makao makuu ya Kanisa Duniani, yalipo. Majuma mawili baada ya kufunguliwa rasmi kwa kituo, Mtambo wa kurushia matangazo
uliokuwa umefungwa mikocheni B mahali zilipo studio, ulishindwa kufanya kazi
kutokana na hitilafu iliyosababishwa na umeme, tatizo lililojitokeza baada ya mvua kali kunyesha. Jitihada za kujaribu kuirejesha katika hali ya kuendelea kufanya kazi zilishindikana,
jambo lililopelekea muingiliano na vyombo vingine vya habari, na kituo kufungwa kwa muda
na tume ya mawasilianona, ili kutoa nafasi ya kufanyika kwa marekebisho. Kituo kilirejea
tena katika hali yake na kuendelea na matangazo baada ya miaka miwili baadae. Mwaka 2005 mwezi wa tano,vifaa vipya vya kurushia matangazo viliagizwa ili kurejesha matangazo tena. Uagizaji huo
ulichukua muda wa miezi mitatu, na mwezi wa nane vifaa viliwasili na ufungaji ukaanza mara moja, wakati huu mtambo
ukiwa umehamishiwa eneo la kisarawe, mkoa wa Pwani. Baada ya ufungaji mtambo kukamilika, mnamo mwezi wa nane mwaka 2005, urushaji wa matangazo ya majaribio
ulianza mara moja, ambapo majaribio hayo yalichukua takribani mwezi mmoja, hadi mnamo mwezi wa tisa! Ilipofika tarehe 26, mwezi wa tano mwaka 2006, saa 11:00 jioni, kituo kilirusha
matangazo moja kwa moja kwa mara ya kwanza, baada ya matangazo ya majaribio
kukamilika! Tangu hapo, Morning Star Radio imeendelea kurusha matangazo yake hadi hivi sasa,
ambapo watu mbali mbali wamekuwa wakibarikiwa sana na matangazo haya, na kwa
hakika kituo hiki kimekuwa ni mbaraka sana kwa ma elfu ya wakaazi wa Tanzania
na dunia kwa ujumla ambapo matangazo
ya Redio hii yanasikika!

Wakati moyo wako unajaribiwa na vitisho vya maisha, kumbuka hili: tumaini lako liko kwa Mungu asiyeweza kushindwa. Sauti...
25/11/2025

Wakati moyo wako unajaribiwa na vitisho vya maisha, kumbuka hili: tumaini lako liko kwa Mungu asiyeweza kushindwa. Sauti za hofu zinaweza kupaza kelele, lakini hazina nguvu juu ya mtu anayemtegemea Bwana. Ukiwa ndani ya mikono Yake, hakuna mwanadamu anayeweza kukuzuia, kukuangusha, au kukutenganisha na ushindi alioandaa kwako.

Kutimiza yaliyo ya haki humleta Mungu karibu zaidi na maisha yako. Watu wanaweza kukupinga, mazingira yanaweza kukutia h...
24/11/2025

Kutimiza yaliyo ya haki humleta Mungu karibu zaidi na maisha yako. Watu wanaweza kukupinga, mazingira yanaweza kukutia hofu, lakini amani ya Mungu huzidi kelele zote. Simama imara kilicho cha haki kitashinda siku zote.

Watu wanaweza kuahidi na kukosa, lakini Mungu hufanya na hutimiza. Ukimtegemea Bwana, moyo hupata usalama wa kweli usioy...
21/11/2025

Watu wanaweza kuahidi na kukosa, lakini Mungu hufanya na hutimiza. Ukimtegemea Bwana, moyo hupata usalama wa kweli usioyumba. Mweke Yeye kwanza hapo ndipo amani na ushindi vinapoanza.

Mungu ndiye chanzo cha nguvu zako, faraja yako, na ushindi wako. Ukimshika Yeye, hofu inanyamaza na moyo unapata amani. ...
20/11/2025

Mungu ndiye chanzo cha nguvu zako, faraja yako, na ushindi wako. Ukimshika Yeye, hofu inanyamaza na moyo unapata amani. Chochote unachopitia leo mtumainie, maana Yeye ni Nguvu zako na Wimbo wako.

Usiache hofu za watu, maneno yao, au vitisho vya mazingira zikuzuie kufanya kile Mungu amekuagiza. Yeye aliyekuita ndiye...
19/11/2025

Usiache hofu za watu, maneno yao, au vitisho vya mazingira zikuzuie kufanya kile Mungu amekuagiza. Yeye aliyekuita ndiye anayekulinda. Anatembea nawe, anakutetea, na anakutoa kwenye kila hali. Thubutu kwenda, Mungu yuko upande wako.

Kila hofu inayokukaba, kila wasiwasi unaokutia udhaifu, Bwana ana uwezo wa kukuvua navyo. Tafuta uso Wake kwa moyo wako ...
18/11/2025

Kila hofu inayokukaba, kila wasiwasi unaokutia udhaifu, Bwana ana uwezo wa kukuvua navyo. Tafuta uso Wake kwa moyo wako wote, na utashuhudia majibu, amani, na ushindi.

Usiruhusu hofu ikutawale, Mungu wako si mnyonge. Yupo njiani kuokoa, kuponya, kurejesha, na kuinua. Moyo wako uwe imara,...
17/11/2025

Usiruhusu hofu ikutawale, Mungu wako si mnyonge. Yupo njiani kuokoa, kuponya, kurejesha, na kuinua. Moyo wako uwe imara, maana msaada wako unatoka juu!

Usikose kuungana nasi kila Asubuhi katika Kipindi cha Anza na Bwana, Kuanzaia saa 11 Alfajiri hadi saa 2.00 Asubuhi, Jum...
16/11/2025

Usikose kuungana nasi kila Asubuhi katika Kipindi cha Anza na Bwana, Kuanzaia saa 11 Alfajiri hadi saa 2.00 Asubuhi, Jumatatu hadi Ijumaa

Neno La Nguvu | Nyimbo zenye Uvuvio | Habari mbalimbali | Mada za Kugusa nyanja mbalimbali za Maisha

Usikose

Hakuna adui, hali, au changamoto inayoweza kushinda wewe ambaye Mungu yupo naye. Tembea kwa imani na moyo wa ushujaa, kw...
15/11/2025

Hakuna adui, hali, au changamoto inayoweza kushinda wewe ambaye Mungu yupo naye. Tembea kwa imani na moyo wa ushujaa, kwa sababu nguvu yako imetokana na Yeye!

Mungu akiwa upande wako, giza halina nguvu, hofu haina nafasi, na adui hana neno la mwisho. Tembea kwa ujasiri, kwa maan...
14/11/2025

Mungu akiwa upande wako, giza halina nguvu, hofu haina nafasi, na adui hana neno la mwisho. Tembea kwa ujasiri, kwa maana nuru ya Bwana inaangaza mbele yako.

Mungu anakuita uinue kichwa chako. Aibu iliyopita haina mamlaka juu ya hatma yako. Yeye anayekupenda anakusimamisha tena...
13/11/2025

Mungu anakuita uinue kichwa chako. Aibu iliyopita haina mamlaka juu ya hatma yako. Yeye anayekupenda anakusimamisha tena, akikupa ujasiri wa kutembea bila hofu.

Hofu inapojaribu kuinuka, kumbuka hili: Mungu anakujua kwa jina, anakumiliki kwa upendo, na amekukomboa kwa gharama ya j...
12/11/2025

Hofu inapojaribu kuinuka, kumbuka hili: Mungu anakujua kwa jina, anakumiliki kwa upendo, na amekukomboa kwa gharama ya juu. Wewe si wa kupotea uko mikononi mwa Yeye ayezidi kila hofu.

Address

P. O. BOX 77170
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AWR Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share