Vaibu TV Online

Vaibu TV Online 🌐 King Of Entertainment
(Exclusive Interviews For Sports, Musics,..)

TATHMINI YA MCHANGO WA WANAHABARI JUU KURIDHISHWA NA USAHIHI WA UTABIRI WA HALI YA HEWADar es Salaam; Tarehe 10 Septemba...
11/09/2025

TATHMINI YA MCHANGO WA WANAHABARI JUU KURIDHISHWA NA USAHIHI WA UTABIRI WA HALI YA HEWA

Dar es Salaam; Tarehe 10 Septemba, 2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekutana na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini ili kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Vuli (Oktoba – Desemba) 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Usafirishaji (NIT). Akizungumza wakati wa mkutano huo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema kupitia warsha hizi uelewa wa wanahabari kuhusu masuala ya hali ya hewa umeendelea kuimarishwa kwa kiasi kikubwa na hivyo kuwezesha taarifa zitolewazo na mamlaka kufikia jamii kwa urahisi na kwa wakati.

ā€œMnamo mwezi Julai mwaka 2025, Mamlaka iliandaa Dodoso maalumu kwa wanahabari ili kufanya tathmini ya utendaji kazi wake kwa Tasnia ya Habari, ambapo kwa taarifa niliyonayo ni kwamba tathmini hiyo imekamilika na matokeo yake yanaonesha asilimia 95 ya wanahabari waliotoa maoni yao wameridhishwa na usahihi wa utabiri wetu na asilimia 96.3 wameonesha kuzielewa taarifa hizo zinazotolewa na TMA hivyo kuzifikisha kwa jamii kwa lugha rahisiā€. Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, Dkt. Chang’a ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wadau wa Maendeleo kwa kuendelea na uwekezaji katika miundombinu ya hali ya hewa nchini na hivyo kuwezesha Mamlaka ya Hali ya Hewa kuendelea kuboresha huduma zake kwa kutoa utabiri mahususi kwa sekta mbalimbali nchini.

ā€œKwa kuzingatia umuhimu wa huduma za hali ya hewa na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuboresha miundombinu ya utoaji huduma za hali ya hewa ikiwemo ufungaji wa Rada za hali ya hewa na kuwajengea uwezo wataalam wa hali ya hewa, ambapo watumishi wapatao 97 wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania wanaendelea na masomo ya elimu ya juu ndani na nje ya nchiā€. Alisema Dkt. Chang’a

Naye, mwanahabari kutoka Harvest FM, Bw. Yonna Mgaya alitoa mrejesho wa namna taarifa za hali ya hewa zimekuwa rahisi kupatikana kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kufanikiwa kuzirusha zaidi ya mara mbili kwenye kituo chao. TMA inatarajia kutoa rasmi utabiri wa Msimu wa Mvua za Vuli 2025, tarehe 11 Septemba 2025, katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.

Watch, follow, and discover more trending content.

TATHMINI YA MCHANGO WA WANAHABARI JUU KURIDHISHWA NA USAHIHI WA UTABIRI WA HALI YA HEWADar es Salaam; Tarehe 10 Septemba...
11/09/2025

TATHMINI YA MCHANGO WA WANAHABARI JUU KURIDHISHWA NA USAHIHI WA UTABIRI WA HALI YA HEWA

Dar es Salaam; Tarehe 10 Septemba, 2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekutana na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini ili kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Vuli (Oktoba – Desemba) 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Usafirishaji (NIT). Akizungumza wakati wa mkutano huo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema kupitia warsha hizi uelewa wa wanahabari kuhusu masuala ya hali ya hewa umeendelea kuimarishwa kwa kiasi kikubwa na hivyo kuwezesha taarifa zitolewazo na mamlaka kufikia jamii kwa urahisi na kwa wakati.

ā€œMnamo mwezi Julai mwaka 2025, Mamlaka iliandaa Dodoso maalumu kwa wanahabari ili kufanya tathmini ya utendaji kazi wake kwa Tasnia ya Habari, ambapo kwa taarifa niliyonayo ni kwamba tathmini hiyo imekamilika na matokeo yake yanaonesha asilimia 95 ya wanahabari waliotoa maoni yao wameridhishwa na usahihi wa utabiri wetu na asilimia 96.3 wameonesha kuzielewa taarifa hizo zinazotolewa na TMA hivyo kuzifikisha kwa jamii kwa lugha rahisiā€. Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, Dkt. Chang’a ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wadau wa Maendeleo kwa kuendelea na uwekezaji katika miundombinu ya hali ya hewa nchini na hivyo kuwezesha Mamlaka ya Hali ya Hewa kuendelea kuboresha huduma zake kwa kutoa utabiri mahususi kwa sekta mbalimbali nchini.

ā€œKwa kuzingatia umuhimu wa huduma za hali ya hewa na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuboresha miundombinu ya utoaji huduma za hali ya hewa ikiwemo ufungaji wa Rada za hali ya hewa na kuwajengea uwezo wataalam wa hali ya hewa, ambapo watumishi wapatao 97 wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania wanaendelea na masomo ya elimu ya juu ndani na nje ya nchiā€. Alisema Dkt. Chang’a

Naye, mwanahabari kutoka Harvest FM, Bw. Yonna Mgaya alitoa mrejesho wa namna taarifa za hali ya hewa zimekuwa rahisi kupatikana kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kufanikiwa kuzirusha zaidi ya mara mbili kwenye kituo chao. TMA inatarajia kutoa rasmi utabiri wa Msimu wa Mvua za Vuli 2025, tarehe 11 Septemba 2025, katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.

09/09/2025

Watch, follow, and discover more trending content.

Klabu ya Gor Mahia, mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu ya Kenya, imewasili nchini Tanzania kwa maandalizi ya mchezo wa k...
09/09/2025

Klabu ya Gor Mahia, mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu ya Kenya, imewasili nchini Tanzania kwa maandalizi ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya

Mchezo huu, unaotarajiwa kuwa kivutio kikubwa, utapigwa kesho Jumatano kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kilele cha Simba Day.

Kuwasili kwa Gor Mahia kunazidisha hamasa ya mashabiki wa soka kutoka pande zote mbili, huku tukio la Simba Day likiahidi kutoa burudani ya kipekee na kuashiria rasmi mwanzo wa msimu mpya wa michezo kwa wekundu wa Msimbazi.

Watch, follow, and discover more trending content.

Msanii wa Bongo Fleva   kutoka Badnation ameweka wazi msimamo wake kuhusu mjadala unaoendelea juu ya nani ni mtayarishaj...
09/09/2025

Msanii wa Bongo Fleva kutoka Badnation ameweka wazi msimamo wake kuhusu mjadala unaoendelea juu ya nani ni mtayarishaji bora kwa sasa kwenye muziki wa Bongo Fleva. Kupitia ukurasa wake wa Instastory, Marioo alimpongeza S2kizzy (Zombie) akisema kwa sasa hakuna producer anayeweza kufikia kiwango chake cha mafanikio kimataifa.

Marioo alieleza kuwa ingawa kuna maproducer wengi wenye uwezo mkubwa, jitihada na kujituma kwa S2kizzy zimechangia sana wasanii kuvunja rekodi na kutamba na nyimbo zilizopenya ndani na nje ya Tanzania. Aidha, aliongeza kuwa binafsi hupata msukumo na inspiration kubwa kutokana na bidii ya kazi ya S2kizzy.

Kwa sasa, Marioo anaamini kuwa S2kizzy ndiye producer namba moja nchini, akimtaja k**a ā€œGOATā€ kutokana na mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa Bongo Fleva na kuufanikisha kufika kimataifa

Watch, follow, and discover more trending content.

QUEEN LUGEMBE AZAMILIA KUTATUA CHANGAMOTO ZA UBUNGO.Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo Kupitia Tiketi ya Chama cha ACT Wazal...
08/09/2025

QUEEN LUGEMBE AZAMILIA KUTATUA CHANGAMOTO ZA UBUNGO.

Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo Kupitia Tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Mh. Queen Lugembe Leo Tarehe 7 Sept 2025, Amezindua kampeni Rasmi Kwa Kunadi Sera Zake.

Vipaombelee Vikubwa Ambavyo Ametaja Endapo Atachaguliwa Ataenda Kutatua Changamoto Zilizopo Kwenye Afya, Mikopo, Pamoja na Barabara.

Kwa Maoni Yake Amesema Hii Siasa Inahitaji Mabadiliko ya Kuwa na Vijana Ambao Wataweza Kutatua Changamoto Zilizopo Kwenye Jamii.

Watch, follow, and discover more trending content.

10/01/2025

Ingia Youtube Kupata Full Video ya Msanii Bilnass šŸ”„šŸ”„šŸ”„šŸ”„šŸ”„

10/01/2025

Full Video Tumekuwekea Kwenye Youtube Channel ya Kusikia Kile Alichozungumza Msanii Bilnass baada ya Kuwa Balozi Mpya wa Bidhaa ya HAFERD lubricants

Address

P. O. Box. 10288
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Vaibu TV Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Vaibu TV Online:

Share

Category