TZ Trends

TZ Trends Official Page for TZ Trends Media
For Reliable News, this is the perfect place

UWEKEZAJI WA NDANI NI  UTEKELEZAJI WA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050 NA ILANI YA CCM 2025-30.Kampeni ya Kitaifa ya uwez...
04/02/2026

UWEKEZAJI WA NDANI NI UTEKELEZAJI WA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050 NA ILANI YA CCM 2025-30.

Kampeni ya Kitaifa ya uwezeshaji uwekezaji wa ndani ni utekelezaji wa Vitendo wa Dira ya Taifa ya 2050 na Ilani ya CCM 2025-2030 ambayo inalenga kutekeleza adhma ya dhati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhamasisha uwekezaji wa ndani na nje ya nchi katika fursa zilizopo kwenye sekta mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Judith Kapinga wakati wa Ufunguzi wa Kongamani la Uwekezaji Kanda ya Ziwa, Februari 04,2026 Jijini Mwanza, ambapo
amebainisha kuwa Tanzania imeendelea kuimarisha imani kwa Wawekezaji wa ndani na wa Kimataifa kwa kuweza kuondoa vikwazo vya kiutawala na kuweka mazingira wezeshi yanayochochoe ustawi na ukuaji ya uchumi na maendeleo ya biashara kupitia sekta ya biashara na uwekezaji.

Kapinga amesema lengo la serikali ni kuhakikisha Tanzania inakuwa miongoni mwa nchi tatu bora barani Afrika katika kuvutia uwekezaji na kuwa na mazingira bora ya kufanya biashara ifikapo mwaka 2050.

Waziri Kapinga amebainisha kuwa Lengo la kampeni hiyo ni kubadili fikra za na Watanzania ya kuamini mwekezaji ni mgeni tu na si watanzania hivyo kutoa elimu ya uwekezaji kwa makundi mbalimbali na kuongeza hamasa itakayosaidia kuleta muamko na kuongeza idadi ya wawekezaji wa ndani kuanzia Halmashauri, Wilaya na Mikoa yote.

Waziri Kapinga amesema k**a Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Tassisi za BRELA,TBS, WMA, SIDO, TANTRADE na FCC imeendelea kuboresha na kuimarisha mazingirabya uwekezaji kwa kurahisisha mifumo ya usajili hususani kwa kanda ya ziwa mradi wa maabara za tbs umeanza ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa kandanhiyo.

Aidha ameielekeza TISEZA kuendelea na kampeni hiyo ili Watanzania waweze kuelewa dhana nzima ya uwekezaji wa ndani na kushirikiana kikamilifu na Sekretarieti za Mikoa na Sekta binafsi zote binafsi ili kufikia dhamira ya dhati ya Serikali.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema kuwa kwa sasa Mkoa huo unapokea Wafanyabiashara wengj kutoka nje ya nchi kutoka Kenya, Uganda, Congo, Burundi na Rwanda na imani kubwa ni kuwa watafanyabiashara hao wataongezeka.

04/02/2026

"Timu inapofanya vizuri Mimi sio sehemu ya mafanikio ya Timu, Wengi wanaoropoka ropoka wanapiga makelele bila kufata utaratibu sio Wanachama wa Simba na wengine Wala sio mashabiki wa Simba" Mangungu

๐ŸŽฅ

Klabu ya Raja Casablanca ya Morocco imemtangaza Moussa Balla Conte, kiungo wa ulinzi, k**a mchezaji wao mpya kwa mkopo, ...
02/02/2026

Klabu ya Raja Casablanca ya Morocco imemtangaza Moussa Balla Conte, kiungo wa ulinzi, k**a mchezaji wao mpya kwa mkopo, akitokea Yanga SC.

01/02/2026

Pamoja na yote, Mwamba anasema bado haijaisha.

01/02/2026

"Kwa lugha nyepesi tu ambayo unaweza usiipende ni kwamba sisi msimu wetu kwenye michuano ya Kimataifa rasmi" AHMED ALLY

01/02/2026

Mwanadada Shabiki wa Klabu ya Simba baada ya Timu yake kusare Nyumbani dhidi ya Esperance de Tunis kwenye mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

29/01/2026

anaamini kutokuwa na ushirikiano wa kutosha kwa wasanii wa Tanzania ndio kikwazo kikubwa kwa wasanii na muziki wetu kushindwa kusogea kimataifa.

Jux ameyasema hayo kwenye mkutano na Waandishi wa Habari ulioandaliwa maalum kwa kutoa shukrani kwa mashabiki waliomuwezesha kushinda tuzo ya .official k**a Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki. โ€ข

๐—ง๐—ฎ๐—ป๐˜‡๐—ฎ๐—ป๐—ถ๐—ฎ ๐—ฌ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐—ถ๐—ฟ๐—ถ๐—ธ๐—ถ ๐— ๐—ท๐—ฎ๐—ฑ๐—ฎ๐—น๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—จ๐˜€๐—ฎ๐—น๐—ฎ๐—บ๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—–๐—ต๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐—น๐—ฎ ๐——๐˜‚๐—ป๐—ถ๐—ฎ๐—ป๐—ถ ๐—ž๐˜‚๐—ฝ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ฎ ๐—š๐˜‚๐—น๐—ณ๐—ผ๐—ผ๐—ฑ ๐—ช๐—ผ๐—ฟ๐—น๐—ฑ ๐—˜๐—ฐ๐—ผ๐—ป๐—ผ๐—บ๐˜† ๐—ฆ๐˜‚๐—บ๐—บ๐—ถ๐˜Tanzania imeshiriki katika ...
28/01/2026

๐—ง๐—ฎ๐—ป๐˜‡๐—ฎ๐—ป๐—ถ๐—ฎ ๐—ฌ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐—ถ๐—ฟ๐—ถ๐—ธ๐—ถ ๐— ๐—ท๐—ฎ๐—ฑ๐—ฎ๐—น๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—จ๐˜€๐—ฎ๐—น๐—ฎ๐—บ๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐—–๐—ต๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐—น๐—ฎ ๐——๐˜‚๐—ป๐—ถ๐—ฎ๐—ป๐—ถ ๐—ž๐˜‚๐—ฝ๐—ถ๐˜๐—ถ๐—ฎ ๐—š๐˜‚๐—น๐—ณ๐—ผ๐—ผ๐—ฑ ๐—ช๐—ผ๐—ฟ๐—น๐—ฑ ๐—˜๐—ฐ๐—ผ๐—ป๐—ผ๐—บ๐˜† ๐—ฆ๐˜‚๐—บ๐—บ๐—ถ๐˜
Tanzania imeshiriki katika majadiliano ya ngazi ya juu ya Gulfood World Economy Summit, k**a sehemu ya mkakati wa kuimarisha nafasi ya nchi katika biashara ya chakula na mazao ya kilimo kwenye masoko ya kimataifa.

Kupitia ushiriki wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), Bi. Irene M. Mlola, Tanzania imewasilisha mtazamo wake kuhusu umuhimu wa kujenga mifumo imara ya masoko, miundombinu ya kisasa na udhibiti madhubuti k**a nguzo muhimu za kuhimili changamoto za mabadiliko ya tabianchi, misukosuko ya minyororo ya usambazaji na mahitaji yanayoongezeka ya masoko ya kimataifa.

Ushiriki huo umeiwezesha Tanzania kushirikisha uzoefu wake katika kujenga masoko rasmi na yanayoaminika, sambamba na kujifunza mbinu bora za kimataifa zitakazosaidia kuimarisha usalama wa chakula wa ndani, kupanua masoko ya mazao ya kilimo na kuvutia wawekezaji pamoja na wanunuzi wa kimataifa.

Mjadala huo umefanyika sambamba na maonesho ya Gulfood 2026, yanayoendelea katika Dubai Exhibition Centre, Expo City โ€“ Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu. โ€ข โ€ข

Ikiwa ajenda kuu ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan leo katika kumbukizi ya kuzaliw...
28/01/2026

Ikiwa ajenda kuu ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan leo katika kumbukizi ya kuzaliwa kwake akitimiza miaka 66 ni kulinda mazingira kwa upandaji wa miti 100 kwa mkono wake, Balozi wa Mazingira ame-accept challenge ya Dkt Samia kwa kupanda miti siku ya leo.

Frida anaamini kupitia Mti tunajifunza ustahmilivu, na ustahmilivu unaweza kutusaidia sote! Akieleza hayo kwenye post yake ya Instagram ambayo ame-share muda mchache uliopita! ๐Ÿ™Œ๐Ÿพ โ€ข

Baada ya kupoteza mchezo wa ugenini dhidi ya Al Ahly kule Misri, kikosi cha Yanga SC kimewasili katika Uwanja wa Ndege w...
25/01/2026

Baada ya kupoteza mchezo wa ugenini dhidi ya Al Ahly kule Misri, kikosi cha Yanga SC kimewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), tayari kuendelea na maandalizi ya mchezo unaofuata wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Yanga sasa wanajipanga kwa mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahly utakaochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar, ambao utakuwa ni mchezo wa nne wa hatua ya makundi kwa timu zote mbili.

22/01/2026

PRESS | Alexandria, Egypt
CAFCL: Al Ahly ๐Ÿ†š Young Africans SC

Kiungo wa Yanga SC, Allan Okello, amesema mchezo dhidi ya Al Ahly utakuwa mgumu kutokana na uzoefu, ubora wa wachezaji na nguvu ya benchi la ufundi la wapinzani wao, hivyo ni muhimu kwa wachezaji wa Yanga kuonyesha mshik**ano na kupambana kwa dakika zote za mchezo.

Okello ameongeza kuwa katika soka la kisasa kila timu ina wachezaji wazuri, lakini tofauti kubwa hutokana na matumizi ya nafasi na uwezo wa kupunguza makosa. Ameeleza kuwa Yanga itahitaji umakini, nidhamu na matumizi sahihi ya nafasi ili kupata matokeo chanya.

Amehitimisha kwa kusema kuwa licha ya kuheshimu Al Ahly, Yanga ina imani kubwa katika uwezo wake, akisisitiza kuwa kila mchezo ni fursa ya timu kuendelea kukua na kujijenga zaidi.

22/01/2026

PRESS | Alexandria, Egypt
CAFCL: Al Ahly ๐Ÿ†š Young Africans SC

Kocha Mkuu wa Yanga SC, Pedro Soares Gonรงalves, amesema timu yake inatambua ukubwa wa Al Ahly k**a klabu kubwa zaidi Afrika, lakini hilo halitawafanya waingie uwanjani kwa hofu bali kwa dhamira ya kucheza na kushindana. Ameeleza kuwa k**a Yanga wanataka kuwa sehemu ya historia ya soka la Afrika, lazima wajifunze kucheza dhidi ya timu kubwa na kujaribu kushinda.

Pedro ameongeza kuwa kikosi cha Yanga kina ubora, wachezaji wana kiwango na ari ya kupambana, huku benchi la ufundi likiwa na imani kubwa kwamba timu inaweza kupata matokeo mazuri kwenye mchezo huo. Ameeleza kuwa kucheza dhidi ya timu bora ni sehemu ya safari ya kufikia kiwango cha juu katika soka la Afrika.

Akizungumzia kundi la mashindano, kocha huyo amesema kundi lao ni gumu kutokana na historia kubwa ya vilabu vilivyopo, lakini Yanga pia ina mpango wa muda mrefu wa kuwa miongoni mwa timu bora barani Afrika. Amebainisha kuwa baada ya mechi mbili, Yanga ina pointi nne na bado ina nafasi nzuri ya kuvuka hatua ya makundi, huku lengo kuu likiwa ni kufuzu.

Kocha Pedro amehitimisha kwa kusema kuwa kila mechi wanaiingia kwa lengo la kushinda, huku akisisitiza umuhimu wa maendeleo ya timu kwa ujumla, mshik**ano wa wachezaji na kuweka mbele malengo ya klabu kuliko maslahi binafsi.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TZ Trends posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TZ Trends:

Share