Volleyball24 Tanzania

Volleyball24 Tanzania Kupitia picha na video tunakuletea taarifa mbalimbali kutoka kila pembe ya Tanzania kuhusu Volleyball

DONE DEAL: Ramadhani Masempele ajiunga na East African University VC ya Rwanda! Ni hatua kubwa kwa Ramadhani Masempele, ...
20/09/2025

DONE DEAL: Ramadhani Masempele ajiunga na East African University VC ya Rwanda!

Ni hatua kubwa kwa Ramadhani Masempele, middle blocker hatari wa Tanzania, aliyekuwa mhimili wa muda mrefu ndani ya Jeshi Stars. Baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa uhodari na nidhamu ya hali ya juu, sasa anavuka mipaka kuanza ukurasa mpya katika ligi ya Rwanda.

Masempele, anayejulikana kwa nguvu, uthabiti na ukuta imara kwenye neti, ameacha alama isiyofutika kwenye volleyball ya Tanzania. Safari yake mpya itamkutanisha na Mtanzania mwenzake, Omary Bure, ambaye tayari anang’ara ndani ya klabu hiyo.

Uhamisho huu ni zaidi ya deal la kawaida ni ishara kuwa wachezaji wa Tanzania wanatambulika kimataifa, na vipaji vyao vina nafasi ya kung’aa katika anga kubwa zaidi.

Mashabiki wa volleyball Tanzania, hii ni historia nyingine inayoandikwa. Ramadhani anapanda ngazi, na sote tupo kushuhudia safari hii.

What a deal. What a journey.



🔥

Kumekuwa na mijadala mikali kuhusu mashindano ya volleyball ndani na nje ya nchi, ambapo baadhi ya watu wanalalamika kuw...
18/09/2025

Kumekuwa na mijadala mikali kuhusu mashindano ya volleyball ndani na nje ya nchi, ambapo baadhi ya watu wanalalamika kuwa vilabu vinatumia nguvu za giza (uchawi/Kulugo) ili kupata ushindi.

Lakini swali la kujiuliza ni Je, kweli tunaamini kuna uchawi kwenye volleyball?

Tupe experience yako juu ya hili swala.

17/09/2025

BAMMATA GAMES 2025
----------------------------------
Match Highlight From Bammata games 2025🔥
SMZ vs JKT

🔥

16/09/2025

Hii ni moja ya fainali kali zaidi tuliyoshuhudia, ikiwakutanisha vijana wenye umri wa chini ya miaka 18 (U18). Ukiitazama video hii, unaweza kuona wazi viwango vya juu na ushupavu walionao vijana hawa.

Sasa swali ni, wakifika miaka 20 watakuwa vipi
Hakika hawa ndio zao la kesho, wakiwa na nafasi kubwa ya kulipeperusha taifa kwenye mashindano makubwa ya kimataifa.

Tayari tumewaona nyota waliotokea kwenye program k**a hizi, akina Abbas & Khamis, Bure & Neeke, pamoja na Ramadhani & Lameck walioshiriki kwenye World Beach Pro Tour – Bujumbura (Agosti 2025).

Tuambie mtazamo wako kwenye comment
je, unaona kizazi hiki kikiwa na nafasi kubwa ya kuandika historia mpya?

📍Beit el Raas - Zanzibar

🔥
🇹🇿

13/09/2025

BAMMATA GAMES 2025
---------------------------
Receive > Set > Spike🔥


📍Amani Stadium - Zanzibar

🔥

12/09/2025

Bukoba, Tanzania – Tarehe 9 Septemba 2025, Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chachu ya maendeleo na mshik**ano kwa Watanzania baada ya kuwasili Bukoba na kuhimiza juhudi za kukuza michezo kwa vijana kupitia mchezo wa Beach Volleyball.

Tukio hili limechangiwa kwa kiasi kikubwa na Beach Volleyball Workshop Tour 2025, ambayo imepita miji ya Bukoba, Mwanza, Simiyu, Kilimanjaro, Tanga na sasa inaendelea Zanzibar, ikilenga kukuza vipaji vya vijana na kuhamasisha michezo ya ufukweni kote nchini.

Kupitia tukio hilo, Mwenge wa Uhuru umeweka nguvu mpya katika kusaidia vijana kupata nafasi ya kukuza vipaji vyao, kuimarisha mshik**ano wa kijamii, na kuchochea ari ya kushiriki michezo ya kimataifa.

Kwa upande wao, wadau wa michezo mkoani Kagera wameeleza kuwa hamasa hii inaleta matumaini mapya ya kuona vipaji vingi vikikuzwa na kuibuliwa, jambo litakalosaidia kupeleka mkoa na taifa kwa ujumla katika anga kubwa ya michezo ya ufukweni.

📍Bukoba – Kagera, Tanzania

🔥

BEACH VOLLEYBALL WORKSHOP TOUR 2025 ---------------------------K**a sehemu ya maandalizi ya mashindano ya vijana yatakay...
11/09/2025

BEACH VOLLEYBALL WORKSHOP TOUR 2025
---------------------------
K**a sehemu ya maandalizi ya mashindano ya vijana yatakayofanyika fukwe za Beit el Raas kwa siku mbili (Jumamosi na Jumapili), tulipata nafasi ya kufanya mazoezi ya pamoja na vijana kutoka Mafunzo, waliokusanyika kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

Ilikuwa fursa ya pekee ya kuwapa mbinu na tips muhimu za mchezo, kujenga mshik**ano, na kuwaandaa kwa michezo inayofuata!

📍 Mafunzo – Zanzibar




07/09/2025

BEACH VOLLEYBALL WORKSHOP TOUR - 2025
----------------------------
Greetings from Beach Mstari - Tanga Tanzania

🔥

Habari Njema!Jackson Mmari amejiunga na  kwa msimu wa 2025/2026!Baada ya ETV Hamburg, sasa ni changamoto mpya kwa shujaa...
06/09/2025

Habari Njema!
Jackson Mmari amejiunga na kwa msimu wa 2025/2026!

Baada ya ETV Hamburg, sasa ni changamoto mpya kwa shujaa wetu wa Tanzania. Tunamtakia mafanikio makubwa!

🔥

Address

Dar Es Salaam
0000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Volleyball24 Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Volleyball24 Tanzania:

Share